23/01/2022
VYANZO/VISABABISHI VYA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)
Linapokuja suala la nini husababisha vidonda vya tumbo unaweza ukapata stori nyingi bila idadi, lakini kwa kifupi kabisa vidonda vya tumbo ni ishara za mwili kupungukiwa maji na k**a matokeo ya asidi kuzidi mwilini kuliko alkaline. Vinaweza pia kuletwa na bakteria ajulikanaye k**a H.Pyroli.
Vitu vifuatavyo vinahusika katika kuleta vidonda vya tumbo mwilini
>>Asidi iliyozidi mwilin
Kawaida mtu anapokaribia kutaka kula chakula chochote au akiwaza kutaka kula au akiuona tu msosi kwa macho,tumboni huzalishwa haidrokloriki asidi ili kuuandaa na kuusaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula Kadri unavyoendelea kuishi haidrokloriki asidi hiyo huenda kutoboa kuta za tumbo na hatimaye taratibu baadaye husababisha mtu kupata VIDONDA VYA TUMBO
Aina zote mbili za vidonda vya tumbo hutokea kutokana na kutolingana nguvu kati ya nguvu ya mnyunyizo wa asidi ya tumbo katika kushambulia na uwezo wa kuta za tumbo katika kuzuia mashambulizi.
>>Mfadhaiko wa akili utokanao na shida za maisha
Mfadhaiko huongeza utiririkaji wa asidi ndani ya tumbo Hii asidi ya ziada ambayo hutiririka ndani ya tumbo k**a matokeo ya mfadhaiko na hakuna chakula cha kufanyiwa kazi au kumeng’enywa humomonyoa kuta za tumbo na hivyo kusababisha vidonda
DALILI ZA UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)
>>Dalili zitakazokufanya ujihisi una vidonda vya tumbo ni kuchoka choka sana bila sababu maalum, kuuma mgongo au kiuno, kupungukiwa au kupoteza kabisa nguvu za kijinsia, kizunguzungu, kukosa usingizi, usingizi wa mara kwa mara. Maumivu makali sehemu ya mwili, kifua kwa ndani kana kwamba unachomwa na kitu cha moto au chenye ncha kali.
>>Maumivu hayo wakati mwingine hutokeza mgongoni na huchoma k**a sindano yenye sumu na kuacha maumivu makali. Dalili zingine ni kichefuchefu, kiungulia, tumbo kujaa gesi, tumbo kuwaka moto, maumivu makali sehemu kilipo kidonda, kukosa choo au kupata choo kwa shida tena kikiwa kigumu na chenye kukatika k**a cha mbuzi.
>>Kutapika nyongo, kutapika damu au kuharisha, sehemu za mwili kupata ganzi n.k. Pia dalili zingine ni kukosa hamu ya kula, kula kupita kiasi, kusahahu sahau na hasira.
0782646918