Imara psychology and therapy services.IPTS

Imara psychology and therapy services.IPTS Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Imara psychology and therapy services.IPTS, Psychologist, 61usa River, Arusha.

KUNA UKUU(UMALKIA/UFALME) UTAUKOSA KWA SABABU  TU YA KIBURI CHAKO.Kuna watu wengi wamekosa kuwa wakuu kwa sababu tu ya  ...
21/07/2025

KUNA UKUU(UMALKIA/UFALME) UTAUKOSA KWA SABABU TU YA KIBURI CHAKO.

Kuna watu wengi wamekosa kuwa wakuu kwa sababu tu ya viburi walivyonavyo yaani kuwa Waziri mkuu,Rais ,wabunge,mawakili Wa kimataifa, wasimamizi Wa makampuni makubwa,wakuu Wa mikoa na ukuu Wa aina yoyote wa kifalme.

Tukirejea katika biblia Vashti aliukosa UMALKIA kwa sababu tu ya kiburi chake alipoitwa na mfalme Ahasuero alikataa kwenda.

ESTA 1:11-12

Ukuu wako unaweza ukaondolewa kwako kwa sababu ya kiburi chako,Kuna nafasi ulistahili ukae wewe k**a mtawala ila umezikosa kutokana TU na kiburi chako

Kuna kibali Cha sauti Yako umekikosa kwa sababu tu ya kiburi chako,Kuna mtu ana mawazo mazuri,hoja nzuri, ila yameshindwa kufika kwa mfalme kutokana TU na kiburi chake.

Kuna nafasi ya utawala ambayo ulistahili wewe ila imeondolewa TU kwako kwa sababu ya kiburi chako.tukirejea TU kwenye hii habari ya Vashti aliukosa UMALKIA kwa sababu ya kiburi chake na kupewa ESTA kuwa malkia



ESTA 2:17

Uzuri wako Wa sura usikufanye uwe na kiburi, maana Mungu atainua wazuri kuliko wewe kuishika nafasi Yako(UMALKIA/UFALME) Wako.Uzuri Wa Vashti haukuonekana kwa mfalme baada ya yeye kukataa amri ya mfalme Ahasuero.Mungu akamuinua ESTA mzuri zaidi na aliyejawa hekima.

Tuache kiburi maana Kuna ukuu tuliyoubeba ila tumebakia kwenye ngazi za kuwa mabalozi Wa nyumba kumi,wenyeviti Wa vitongoji, na wenyeviti Wa vijiji wakati kiuhalisia sisi ni mawaziri wakuu na wafalme.

fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko

JAMII,TAIFA VIFANYE NINI ILI KUONDOKANA NA MATATIZO YA WATU KUJIONDOA UHAI(KUJINYONGA,KUNYWA SUMU,KUJIRUSHA KWENYE MAJEN...
20/07/2025

JAMII,TAIFA VIFANYE NINI ILI KUONDOKANA NA MATATIZO YA WATU KUJIONDOA UHAI(KUJINYONGA,KUNYWA SUMU,KUJIRUSHA KWENYE MAJENGO MAREFU)

1. Elimu kuhusu afya ya akili

Kuelimisha jamii kuhusu matatizo ya afya ya akili hasa kupitia Shule, makanisa, misikiti, na vyombo vya habari Ili kufundisha watu kutambua dalili za msongo wa mawazo, huzuni kali (depression), au hali zingine za kiakili.

2.Kumshirikisha rafiki Yako Wa karibu pale unapokuwa na changamoto,watu wengi huwa wanakosa rafiki Yao Wa karibu kumshirikisha mambo Yao mazito ya moyoni,ninaposema rafiki Wa karibu ni yule rafiki Yako Wa shida na Raha unapomwelezea matatizo Yako anaweza akakupa msaada WA kutatua changamoto inayokukumba.

3.Kutoa Ajira na kuwapa watu matumaini Ukosefu wa ajira, umasikini, madeni, au kukata tamaa,Serikali inapaswa kuweka sera za kusaidia vijana na watu wanaopitia hali ngumu za kiuchumi—k**a kutoa Ajira ,mikopo midogo, mafunzo ya kazi na kutoa msaada WA kisaikolojia wale waliokosa matumaini.

4.Kuepuka ulevi au matumizi ya madawa ya kulevya,mara matumizi ya vileo huwa yanamzuia mtu kufikiri na kufanya maamuzi sahihi,unapoona una msongo Wa mawazo unatakiwa ujiepushe na matumizi ya madawa ya kulevya .

5. Mazingira salama ya kijamii na kifamilia,Familia na jamii zinapaswa kujenga mahusiano ya karibu, yenye upendo na msaada.Hali za ukatili, manyanyaso, unyanyapaa, au kutengwa zinachangia matatizo ya afya ya akili. Hivyo kuwa karibu na jamii kutasaidia na kutatua matatizo.

6.Kuepuka kukaa mwenyewe unapokuwa na msongo wa mawazo,upweke wa kukaa mwenyewe unaweza kuchangia kujiondoa uhai hivyo unapokuwa na msongo wa mawazo au changamoto yoyote unatakiwa uwe unakaa na watu sahihi kwenye maisha yako.

7.Kufanya ibada na kusali,Mungu hurejesha vyote vilivyopotea hivyo unapokuwa na msongo wa mawazo ni muhimu kufanya ibada kwa uaminifu na kusali kwa kuwa Mungu huwa anasikia haha za miyoyo yetu pale tunapomuomba kwa uaminifu na kwa kumaanisha.

8.kuonana Wataalamu Wa saikolojia na washauri na saa, un

NI KWANINI WATU HUJIONDOA UHAI(KUJINYONGA,KUNYWA SUMU AU KUJIRUSHA KWENYE MAJENGO MAREFU)Siku hizi ukiingia kwenye mitan...
17/07/2025

NI KWANINI WATU HUJIONDOA UHAI(KUJINYONGA,KUNYWA SUMU AU KUJIRUSHA KWENYE MAJENGO MAREFU)

Siku hizi ukiingia kwenye mitandao ya kijamii,kwenye vyombo vya habari unakutana na taarifa zinazoumiza sana za watu kujiondoa uhai.

Jamii huwa inapitia wakati mgumu sana pale ambapo mwanafamilia anajiondoa uhai wake,kwa sababu maswali huwa ni mengi sana kuhusu huyo aliyejiondoa uhai.Nipende nikuletee makala yenye kuonesha sababu za watu kujiondoa uhai na namna ya kusaidia kizazi Ili kiepukane na mawazo ya kujiondoa uhai k**a suluisho la matatizo yanayowakumba.Somo hili nitatoa sababu na nini kifanyike Ili kuokoa kizazi kilichokosa matumaini ya kuishi.

SABABU ZINAZOFANYA WATU KUJIONDOA UHAI.

1 MAGONJWA YA AKILI.magonjwa ya akili k**a vile sonona,hisia mseto, na wasiwasi humfanya mtu ashindwe kufikiri na kuanza kukosa matumaini na kuona k**a yeye ni mzigo kwa jamii.

2.KUKOSA MATUMAINI,mtu akikosa matumaini huona k**a hakuna kitu ambacho kinaweza kukaa sawa,hivyo huchangia kuona k**a kujiondoa uhai ndiyo utatuzi WA jambo wakati siyo kweli.

3.TRAUMA( KIWEWE),maumivu ya mda mrefu,kufanyiwa vitendo viovu k**a vile ubakaji, kuumizwa kihisia huwa kunamfanya mtu ajisikie vibaya mda wote kutokana na hisia kuathiriwa.

4.KUMPOTEZA MTU UNAYEMPENDA,Kufiwa na mtu wakaribu, kuvunjika kwa mahusiano hii husababisha kuona kuwa hakuna mtu atakayeweza kuziba pengo la huyo mtu Wa karibu na kufanya mtu alone TU Hana msaada mwingine kwenye hii dunia

5.MASUALA YA KIUCHUMI,Kuwa na madeni mengi,kukosa Hela ,kukosa kazi,huwa zinapelekea sana mtu kuwa na mawazo mabaya ambayo hupelekea yeye kuona hakuna Tena tumaini la kuishi na kuanza kujionea aibu .

6.MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA,Utumiaji wa madawa ya kulevya k**a vile pombe,bangi,huwa vinasababisha mtu kushindwa kufikiri sahihi na kufanya maamuzi mabaya .

7.UPWEKE NA KUTENGWA ,upweke WA mda mrefu na kukosa mahusiano mazuri na watu huwa kunapelekea mtu kuwa na mawazo mengi ya kujiondoa uhai.

K**a una ndugu Yako unamuona hayuko sawa

SIFA SABA ZA  KUZINGATIA MWÀNAUME  UNAPOTAKA KUOA MWANAMKE.Wanawake huwa wanavutiwa na maneno mazuri yanayotoka kinywani...
02/05/2025

SIFA SABA ZA KUZINGATIA MWÀNAUME UNAPOTAKA KUOA MWANAMKE.

Wanawake huwa wanavutiwa na maneno mazuri yanayotoka kinywani mwa mwanaume ndo maana unaweza ukakuta mwanamke mzuri na mrembo ameolewa na mwanaume mwenye sura personal,Maskini,mlevi na hata ambaye Hana mwelekeo wa maisha ,hiyo basi wanawake huvutiwa na kile wanachokisikia Kwa mwanaume na wanaume huwa wanavutiwa zaidi na kile wanachokiona yaani uzuri na urembo wa mwanamke, hivyo mwanamke usisahau kujipamba na kujiremba haya yote yamethibitishwa na KINGSLEY OKONKWO kwenye kitabu chake kinachoitwa 7QUALITIES WISE MEN WANT.

SIFA SABA ZA KUZINGATIA MWÀNAUME UNAPOTAKA KUOA MWANAMKE.

1.MWANAMKE MWENYE HOFU YA MUNGU.
Ninaposema HOFU ya Mungu siyo tu kwenda kwenye nyumba za ibada au msikitini.
Tukirejea kwenye biblia unaona mwanamke aliyekubali mtoto asikatwe katwe mfalme SULEMAN alipotaka kusuluisha ugomvi wa wanawake wawili kuhusu mtoto aliye kufa.

1 wafalme3:25-26
2.MKE MWEMA ,mke mwema ni WA thamani sana maana anakuwa na mawazo mema na mwenye kuwa na miradi na kuisimamia,mke mwema amesifiwa sana katika kitabu Cha mithali 31:10 kuwa uzuri wake ulipita madini ya rubi.
3.AWE MPOLE NA MWENYE UTULIVU.Asiwe mtu wa kuvutana na mwanaume Kwa maneno, Wanaume wengi tumekimbilia Kwa kuchagua maumbile makubwa yaani hips badala ya kuangalia upole na utulivu.Mungu anasema kuwa upole na roho ya utulivu ni vitu vya thamani sana Kwa mwanamke.

4.MWANAMKE AWE NA HEKIMA, mwanamke awe anajua kweli na kutenda Yale mazuri.
Mithali 14:1 anasema kuwa mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake Kwa mikono yake mwenyewe.

5.AWE MWANAMKE MKARIMU,wanaume wengi huwa wanapenda wanawake wakarimu mwenye mahusiano mazuri na watu wengine hasa ndugu,na pia huwa anapenda zaidi kuona mwanamke anayemuoa anawajali na kuwahudumia vizuri marafiki zake wanapokuja kumtembelea

6.AWE NA AFYA NJEMA NA ROHO NZURI, asiwe mtu wa kuathiriwa na MABAYA aliyowahi kutendewa ,ajue kusamehe na kusahau.

7.AWE MWAMINIFU,mwanamke unayetaka kuwa naye kwenye maisha

30/04/2025

UBAYA ULIOSHINDWA KUUCHA NDO UMEKWAMISHA MAFANIKIO YAKO(KUPIGA HATUA YAKO KUFIKA MBELE ZAIDI).

Kuna watu wengi wanalalamika hawafanikiwi kimaisha na wengine wanajiona k**a wamelogwa kumbe hawajalogwa kinachowakwamisha tu ni ubaya walioshindwa kuucha,

Tukirejea kwenye biblia takatifu inakuambia ujitenge na ubaya wa Kila namna.

1 Wathesalonike 5:22

[22]jitengeni na ubaya wa kila namna

Napenda nikuoneshe ubaya ulioshindwa kuucha na unasababisha wewe kutokufanikiwa au kupiga HATUA ya mafanikio

HAYA NDIYO MABAYA YANAYOKWAMISHA MAFANIKIO YAKO

1.KIBURI,Kiburi kimekuwa kikiwakwamisha wengi na wameshindwa kufika mbali maana eneo lake la kazi k**a ni ofsini Kila mtu anajua wewe una Kiburi .

2.ULEVI,Kuna wengi wamekwamisha kimaendeleo na ulevi maana Kila pesa anayoipata yote tu huwa inaenda kwenye ulevi.

3.USINZI NA UASHERATI,Kuna ambaye amekuwa Kila anachopata anakitumia Kwa kujua Kila mtaa wenye mwanamke mzuri wa sura na umbo na kutumia nao kwa kuendekeza zinaa.

4.CHUKI,Kuna watu wenye chuki Hadi wanajichukia wenyewe,ukishakuwa na chuki ni vigumu sana kufanikiwa ,maana unakosa uhuru wa kifikira na kimawazo.

5.WIZI NA UDOKOZI ,Kuna mtu ambaye ni mwizi Hadi ofsini huwa huwa aachwi mwenye Kwa sababu anaweza akaondoka hata na kijiko au kitu Chochote tu ofsini.

6.UGOMVI ,Kuna mtu ambaye Kila saa huwa anakuwa tu na ugomvi na kila mtu,na mtu huyu hawezi kukaa na mtu yoyote pasipo kugombana.

7.WIVU,Kuna mwingine anaona wivu wa mafanikio ya mwingine ,kumbe hajui kuwa kufanikiwa Kwa mwenzako ndo mafanikio yako

Hayo ni baadhi tu ya MABAYA ambayo yanakuwa yanakukwamisha usifanikiwe.

Nikuàmbie tu wewe unayesoma huu ujumbe umwombe Mungu sana ili akutenge na haya MABAYA niliyokuorodheshea.

fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia

MADHARA MAKUU MATANO YA KUTOKUFANYA KAZI.Bwana Mungu aliwapa wanadamu agizo la kufanya kazi lakini Leo hii watu wengi ha...
28/04/2025

MADHARA MAKUU MATANO YA KUTOKUFANYA KAZI.

Bwana Mungu aliwapa wanadamu agizo la kufanya kazi lakini Leo hii watu wengi hawataki kufanya kazi.

Turejeekitabu Cha 2wathesalonike 3:6-15

Nipende kuanzia ule mstari wa 8.

2 Wathesalonike 3:8

[8]wala hatukula chakula kwa mtu ye yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote.

HAYA NDO MADHARA MAKUU MATANO YA KUTOKUFANYA KAZI.

1.KUWALEMEA WATU(KUWA MZIGO ),usipofanya kazi utalemea watu maana watu watakuwa wanatenda majukumu Yako uliyoshindwa kutekeleza


2.KUWA MTU USIYEKUWA NA MWELEKEO,Hii itakufanya tu ufanye vitu bila utaratibu,mfano unakuwa na mda wa kupoteza Hadi marafiki wanakuwa wanakuchukua kuwasindikiza Kila mahali.maana wewe unakuwa unapatikana tu mda wote k**a ardhi.

3.KUUA MAONO NA KILE KIPAWA KILICHO NDANI YAKO,anaposema asiye Fanya kazi na asile.hii inamaanisha kwamba usipofanya kazi hutokula ,na ukikataa kula utakufa,hivyo ukikaataa kufanya kazi utaua Yale MAONO yaliyondani Yako.

4.KUTENGWA NA JAMII,Maneno ya Mungu yanasema mjitenge na wasiofanya kazi,usipofanya kazi lazima utengwe na jamii maana unakuwa mtu asiyekuwa na mchango kwenye jamii.

5.KUSENGENYA,Ukikataa kufanya kazi utapata mda mwingi wa kushulika na mambo ya watu wengine

Nipende kusema tufanye kazi ili tule vitu vya jasho letu wenyewe na tupunguze kuwa mizigo Kwa wengine.

fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko.

*MAZUNGUMZO YA KARIBU(INTIMATE CONVERSATION)* Haya ni mazungumzo ambayo tunaweza kuyatazama k**a dira ya maisha ya mahus...
03/10/2024

*MAZUNGUMZO YA KARIBU(INTIMATE CONVERSATION)*

Haya ni mazungumzo ambayo tunaweza kuyatazama k**a dira ya maisha ya mahusiano hasa ya ndoa ,Mazungumzo haya ya karibu huwa ni mazungumzo ambayo unatakiwa uwe karibu na mwezi wako au mpenzi wako huku mkiongea Kwa furaha na na kujadili mambo ambayo yanaibua hisia na uthamani wenu. Dhana hii imeibuliwa na mtaalam WILLARD F.HARLEY kwenye kitabu chake kiitwacho _His _Needs Her Needs_

Mfano wa maneno yatakayoibua hisia Kwa mwezi wako ni kumwambia maneno k**a haya Nakupenda sana, wewe ni kitu pekee ambacho nina hapa duniani naye akujibu hivi Na mimi pia nakupenda sana, wewe ni mwanga wangu katika giza.

*KUNA MAMBO AMBAYO HUWEZA KUHARIBU MAZUNGUMZO YA KARIBU.*

Mambo ya kuepuka katika mazungumzo yenu ya karibu ni haya hapa

*1. *KUTOKUONESHA HESHIMA** ,Unapokuwa na mwezi wako hasa kwenye haya mazungumzo ya karibu hutakiwi ufanye vitendo vtakavyomkwaza mwezi wako epuka kufyonza ,kupepesa pepesa macho ,kupandisha mabega na hata kusonya.

2 *.MSIZUNGUMZIE MAKOSA YALIYOKWISHA TENDEKA AU KUJADILI MAMBO YALIYO PITA*
Kwenye familia au mahusiano ya ndoa huwa MAKOSA hayaepukiki k**a ushajua ulishamkosea mwezi/ mpenzi wako au kutokufurahisha mpenzi wako epuka sana kuishi katika MAKOSA yaliyokwisha pita Bali mnatakiwa muwe na mawazo chanya yanayoibua hisia na mikakati mnayotarajia kuifanya.

*3.EPUKA KUONESHA HASIRA,* mazungumzo ya Hasira huibua kashifa matukano na masimango ,hivyo siku zote unaooona una Hasira usiongee kitu au kufanya Chochote maana mtaishia kwenye mabishano.

Nikukumbushe kuwa familia Bora haujengwi Kwa kuwa na Mali nyingi bali Kwa mazungumzo ya karibu na yanayoibua hisia na fikra chanya katika maisha. Kuishi maisha ya furaha ni kuwa na mazungumzo ya karibu na mwezi wako.

* fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko*

BENKI YA UPENDO(LOVE BANK)Unaweza ukashangaa na kustaajabu kusikia  upendo una benki.Ni kweli benki ya upendo ipo na dha...
26/09/2024

BENKI YA UPENDO(LOVE BANK)

Unaweza ukashangaa na kustaajabu kusikia upendo una benki.Ni kweli benki ya upendo ipo na dhana hii imeibuliwa na mtaalam Willard F.Harley kwenye kitabu chake kiitwacho His Needs Her Needs ,NIKUOMBE msomaji wa makala hii ukaribie uone na kujifunza mengi kuhusu benki ya upendo.

Kila mwanadamu huwa ana benki ya upendo.

Benki ya upendo Iko hivi unapokutana na mtu na akawa na mazungumzo yanayojenga huwa unakuwa umeweka kitu kwenye benki ya upendo kwa unayeongea naye na endapo utakuwa na mazungumzo mabaya au yanayokera Kwa unayezungumza naye unakuwa umetoa kitu kwenye benki ya upendo Kwa unayezungumza naye.

Benki ya upendo Ina sehemu mbili ambazo ni depost(kuweka) na withdraw (kutoa)

Kwa upande wa wanandoa au wapenzi hii benki ya upendo inatakiwa idumishwe sana tena Kwa upande wa kuweka( deposit)

Unapomfanyia mwenzi wako au mpenzi wako mambo mazuri na ya kumfurahisha k**a vile kununulia Zawadi,kumjali, kumsikiliza na kumheshimu huwa unaweka kitu Cha dhamani kubwa sana kwenye benki ya upendo umpendaye

lakini unapokuwa unatenda mambo mabaya k**a vile usaliti,kujibu kwa jasba, kutokumsikiliza mwezi au mpenzi wako huwa unato Ile dhamani iliyoko ndani benki ya upendo wa mahusiano yenu.

Ili kujenga familia Bora lazima benki ya upendo kwako iwe unaiwekea mambo mazuri.

fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko.

FAHAMU ADUI MKUBWA WA MAFANIKIO YAKOunaweza ukajiona haufanikiwi kwenye maisha Yako na kuanza kuona umelogwa wakati hauj...
04/09/2024

FAHAMU ADUI MKUBWA WA MAFANIKIO YAKO
unaweza ukajiona haufanikiwi kwenye maisha Yako na kuanza kuona umelogwa wakati haujalogwa

ADUI MKUBWA WA MAFANIKIO YAKO NI KUWA NA HISIA HASI.(Negative emotions)

Hizi hapa ndo HISIA HASI zinazokuzuia usipate mafanikio Yako

1. Hofu
2. chuki
3. Hasira
4. huzuni
5. aibu
6. wivu
7. husuda
8.kukata tamaa
9.Kujihurumia

K**a unataka kuwa mtu mwenye mafanikio na furaha katika maisha Yako unachotakiwa ni kuondokana na HISIA HASI.

fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko

*FAHAMU NAMNA YA KUKABILIANA NA KUSHINDA  MSONGO WA MAWAZO.* Msongo wa mawazo umeweza kudhoofisha afya ya akili ya watu ...
22/08/2024

*FAHAMU NAMNA YA KUKABILIANA NA KUSHINDA MSONGO WA MAWAZO.*

Msongo wa mawazo umeweza kudhoofisha afya ya akili ya watu wengi hivyo basi napenda nikupe njia kuu za kushindamsongo wa mawazo

*1. Unatakiwa ujue ni Nini chanzo Cha wewe kuwa na msongo wa mawazo* ,unaweza ukakuta chanzo kikuu labda kwako ni kukosa pesa, mahusiano,au kazi unayoifanya.Nipende kukumjulisha kuwa ukishajua ni kipi kinakupa msongo utaweza kujua namna ya kuepuka na hicho kinachokupa wewe msongo.

*2. Mshirikishe mtu wako wa karibu(yaani yule mtu ambaye ni msiri wako na rafiki mliyeshibana).* Kuna watu wanaokufa kutokana na kubaki na mambo moyoni bila kuwashirikisha watu wao wa karibu ambao wangeweza kuwasaidia kufumbua tatizo au changamoto wanazopitia.

*3. Kuvuta punzi ndani au kufanya tafakuri* .unapokuwa na msongo wa mawàzo jitahidi ukae sehemu palipotulia unavuta punzi ndani Kwa dakika Moja au dakika mbili na kuiachia Fanya hivyo mara kadhaaa hiyo itakusaidia sana.

4. *Jitahidi kufanya Yale mambo yanayokupa furaha k**a vile kusikiliza mziki,* Mziki huwa unampa mtu uponyaji hasa unapokuwa na msongo wa mawazo,mfano mzuri kutoka biblia takatifu ni Sauli alipoingiwa na roho mchafu alimtafuta Daudi ampigie mziki mzuri na WENYE ustadi Ile roho chafu ikamtoka Sauli

1Samweli 16:23
[23]Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha.

*5.Tembelea mazingira yenye kijani kibichi* ,tembelea maeneo yenye mazingira ya kijani kibichi yatakusaidia kuondoa msongo wa mawazo.

*6.Tafuta wataalam wa saikolojia waliobobea kwenye taaluma hiyo watakusaidia.*

Hizo ni namna za Kukabiliana na msongo wa mawazo ila Kuna njia Moja ambayo ni kuu zaidi utafute USO wa Mungu na kumweleza yote yanayokusibu.

Asante kwa kufuatilia somo la msongo wa mawazo.

* fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko.*

**Je kuna MADHARA yoyote mtu anapopatwa na Msongo wa MAWAZO?* Jibu ni ndiyo huwa Kuna MADHARA tena makubwa sana,hebu tua...
09/08/2024

**Je kuna MADHARA yoyote mtu anapopatwa na Msongo wa MAWAZO?*

Jibu ni ndiyo huwa Kuna MADHARA tena makubwa sana,hebu tuangalie haya MADHARA ya msongo wa a MAWAZO.Kuna MADHARA hasa sehemu kuu nne ambazo ni kimwili,kiafya, KIAKILI na katika mahusiano lakini nitaweka MADHARA haya kiujumla .

1 **.msongo wa mawazo husababisha presure (shinikizo la damu),Magonjwa ya moyo ,maumivu ya tumbo na kuhara.
*
2 **.msongo wa mawazo huathiri mfumo wa ubongo Kwa asilimia kubwa na kuanza kuwa na wasiwasi,huzuni,kukereka hata kwa jambo lisilo la msingi,kupoteza kumbukumbu,na Kukosa umakini Kwa kitu unachokifanya* .
*
3. *msongo wa mawazo husababisha watu kuwa walevi waliopindukia,matumizi ya madawa ya kulevya,kula kupita kiasi au kushindwa kula kabisa, na wengine kujitenga na watu na kutaka kuwa wenyewe tu.*

4 *.Migogoro katika katika mahusiano n Kukosa utulivu,pia Kukosa hamu ya tendo la ndoa.*

Hayo ni baadhi tu ya MADHARA ambayo huwa yanajitokeza pale ambapo unapatwa na Msongo wa mawazo.

Usikose MWENDELEZO wa darasa lijalo ili ujifunze namna ya kuepuka na Msongo wa mawazo,na usisahau kunifuata kwenye ukurasa wangu wa facebook Kwa hiyo link https://www.facebook.com/profile.php?id=61560564674499

* fikra, ishi kwa raha, mwanasaikoloji tva Elia Nnko* .

*

*Ushawahi kujua kuwa sehemu ulipoajiriwa au kujiajiri panaweza kukusababisha wewe* kuwa na MSONGO wa MAWAZO (stress) Heb...
06/08/2024

*Ushawahi kujua kuwa sehemu ulipoajiriwa au kujiajiri panaweza kukusababisha wewe* kuwa na MSONGO wa MAWAZO (stress)
Hebu Leo tuangalie Vyanzo vya MSONGO wa MAWAZO Kwa kuanza kuangalia eneo la kazi /sehemu ulipoajiriwa

1 *Msongo wa mawazo kazini ,* mara nyingi kuwa na Mzigo mkubwa wa kazi, kuwa na bosi mkorofi au wenzako kuwa na maneno maneno kazini, kutokuwa na uhakika wa kazi, Kunaweza kusababisha msongo wa mawazo.

2 *.migogoro ya ndoa (mahusiano) na migogoro ya kifamilia,* ninaposema matatizo katika mahusiano najumuisha talaka,mwanaume kumpa Binti ujauzito na kukataa ujauzito.Pia kutokuwepo na maelewano na wanafamilia au kumtunza mwanafamilia mgonjwa, vinaweza vyote kuchangia mtu kupata msongo wa mawazo.

3. *Matatizo ya kifedha,(mikopo isiyokuwa ya ulazima k**a vile kausha damu) vikoba,* mtu anapokuwa na Matatizo ya pesa hupelekea kuwa na madeni mengi ambayo yanakuwa hayajashirikishwa pañde zote mbili yaani unakuta mtu amekopa Hela kwenye vikundi bila kumshirikisha mwezi wake hivyo basi kupelekea mtu kuwa na MSONGO wa mawazo anapoanza kudaiwa na watu na taasisi mbalimbali alizokopa.

4. *Mabadiliko ya maisha,* Matukio makubwa katika maisha k**a vile kuhamia, kufunga ndoa, kupata mtoto, kupatiwa talaka, au kupoteza mpendwa wanaweza kusababisha msongo wa mawazo.

5. *ukosefu wa ajira* ,kutokuwa na ajira Kwa mda mrefu kumechangia sana watu wengi kupata Msongo wa mawazo hasa pale unapokuta aliyesoma amesoma Kwa shida na ameshatumia Hela nyingi akiamini kuwa elimu itamkomboa kimaisha.

6. *trauma au kiwewe* ,kushuhidia matukio k**a vile ajali au kupata majeraha na Magonjwa ya muda mrefu, yanaweza kuleta msongo wa mawazo na kuchosha kiakili.
7 *.michezo ya kubashiri* ,hiki ni chanzo kikubwa sana hasa Kwa vijana Kwa Msongo wa MAWAZO pale ambapo unakuta mtu anamatarajio ya kushinda kitita Cha Hela na anapokoseshwa na timu Moja au mbili alizozipa ushindi na kushindwa kupata kiasi alichotegemea kukipata.
fikra, ishi kwa raha, mwanasaikolojia Elia Nnko

Address

61usa River
Arusha

Telephone

+255759766430

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Imara psychology and therapy services.IPTS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Imara psychology and therapy services.IPTS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category