Pudencial afya point

Pudencial  afya point for better health communicate with us

15/09/2024

BEBA UJAUZITO KIRAHISI

K**a umefanya vipimo vimeonyesha kuwa mayai yako ubora wake upo chini kula hivi vyakula kuviboresha mayai
📌Mayai
📌Maini
📌Samaki
📌Supu ya mifupa(supu ya kongoro)

10/09/2024

Moja ya sababu za kuziba mirija ya uzazi ni

📌magonjwa ya zinaa
📌P.I.D
📌utoaji wa mimba kiholela
📌Ugonjwa wa TB

Ipo program maalumu kwaajili yako itakayokusaidia kuzibua mirija hata ukiwa nyumbani.
☆wasiliana nasi kupata suluhisho la kudumu 0629218863

16/06/2022

Je unapata hizi dalili?

👉miwasho kwenye njia ya haja kubwa
👉kinyama au uvimbe kwenye tundu la haja kubwa
👉kupata choo kigumu mithili ya kinyesi cha mbuzi
👉maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa

●comment namba yako kupata suluhisho👇

JE WAJUA? SABABU ZINAZOPELEKEA UKE KUWA MKAVU?UKE:- ni sehemu moja wapo ya maumbile katika mfumo wa uzazi wa mwanamke.  ...
29/03/2021

JE WAJUA? SABABU ZINAZOPELEKEA UKE KUWA MKAVU?

UKE:- ni sehemu moja wapo ya maumbile katika mfumo wa uzazi wa mwanamke.

KAZI ZA UKE
👉kupitisha damu ya uke.
👉kuruhusu uume kupita wakati wa kujamiiana
👉kupokea shahawa wakati wa kujamiiana
👉kuruhusu mtoto kupita wakati wa kujifungua (SVD)

♣️Ikumbukwe kwamba ni salama kwa uke kuwa mkavu katika mazingira yasiyo ya kujamiiana
♣️ wakati mwingine sio tatizo la kiafya uke kuwa mkavu wakati wakujamiiana
♣️wakati mwingine huwa ni tatizo la kiafya

VISABABISHI
👉manukato,lotion na sabuni zenye kemikali ukeni
👉msongo wa mawazo
👉magonjwa ya zinaa na fangasi ukeni

DALILI
👉maumivu wakati wa kujamiiana
👉kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa
👉michubuko au kuungua ukeni wakati wa kujamiiana

MADHARA
👉michubuko ukeni
👉kutokufurahia tendo
👉kutokufika kileleni
👉hatari ya maambukizi ukeni eg:-bacteria,fungus

LIPO USHAURI BURE TUPIGIE SIMU NAMBA 0629214933 #

NB:- HAKUNA KITU KILICHO CHA THAMANI K**A AFYA YAKO ITHAMINI

JE WAJUA MWANAMKE NDIO CHANZO CHA MWANAUME KUSHINDWA KUFANYA TENDO LA NDOA? Ndugu zangu naomba nielezee kuhusu mwanamke ...
19/03/2021

JE WAJUA MWANAMKE NDIO CHANZO CHA MWANAUME KUSHINDWA KUFANYA TENDO LA NDOA?

Ndugu zangu naomba nielezee kuhusu mwanamke na uke,kwa maana ya

UKE ni kiungo cha uzazi wa mwanamke na laini ambacho kinapitia changamoto nyingi sana, Endapo hakitatunzwa kwenye mazingira mazuri na salama basi mwanamke atapata magonjwa mbalimbali ukeni. Ila leo nitazungumzia UGONJWA WA FANGASI UKENI.

UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI ni ugonjwa anaoupata mwanamke endapo fangasi watakuwa wengi zaidi ya bacteria wazuri waliopo ukeni au k**a pH ya ukeni imezidi kiwango cha kawaida kinachopaswa(pH 3.5-4.5 ndio kiwango kizuri kiafya).

FANGASI ZA UKENI MARA NYINGI HUSABABISHWA NA FANGASI WAITWAO CANDIDA ALBICANS, LAKINI WAKATI MWINGINE NI AINA NYINGINE ZA FANGASI NA HIZI NI VIGUMU SANA KUTIBIKA

BAADHI YA SABABU ZINAZOPELEKEA KUPATA FUNGUS UKENI

👉MATATIZO YA HOMONI(HOMONI ZA KUBADILIKA/KUWANYINGI SANA AU KUSHUKA SANA) hii inaweza kusahabishwa na; ukomo wa hedhi,ujauzito, (MP)kuwa katika siku za mwezi, matumizi ya dawa za kuongeza kiwango cha hormon za k**e

👉 MATUMIZI YA ANTIBIOTICS hizi huuwa bacteria wazuri na kubadiri ph ya uke

👉KUFANYA MAPENZI NA MTU ALIYE NA UGONJWA WA FANGASI ZA SEHEMU ZA SIRI BILA KINGA

👉KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI hii inaweza kusababishwa na magonjwa mbalimbali k**a UKIMWI, KISUKARI, UPUNGUFU WA MADINI,VITAMINI NA VIRUTUBISHI MBALIMBALI VYA MWILI.

👉ULAJI MBAYA HASA KUPENDELEA VYAKULA VYENYE SUKARI KWA WINGI (SUKARI NI CHAKULA KWA FANGAS HIVYO HUONGEZEKA).

👉UCHAFU

DALILI ZINAZOONESHA KUWA UNAUGONJWA WA FANGAS ZA UKENI

~MUWASHO SEHEMU ZA SIRI

~VIPELE VIDOGO VIDOGO UKENI

~KUTOKWA UCHAFU MWEUPE AU WA RANGI YA KIJIVU UKENI WENYE HARUFU MBAYA

~VIDONDA AU MICHUBUKO UKENI

~KUTOKWA NA HARUFU MBAYA UKENI

~KUPATWA NA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA

~KUVIMBA NA KUWA MWEKUNDU KATIKA MDOMO WA NJE WA UKE

~KUWAKA MOTO NDANI NA NJE YA UKE

JINSI YA KUEPUKA

1.EPUKA KUSAFISHA UKE KWA KUTUMIA VITU VYENYE KEMIKALI K**A SABUNI

2.EPUKA KUTUMIA MARASHI YENYE CHEMIKALI UKENI NA KUONGIZA VITU MBÀLIMBALI UKENI K**A VIDOLE, ASALI, MGAGANI N.K

3.EPUKA KUTAWADHA KUTOKEA NYUMA KWENDA MBELE BAADA YA KUJISAIDIA HAJA KUBWA AU NDOGO

4.MTIBU MPENZI WAKO ALIE NA UGONJWA WA FANGASI

5.SAFISHA UKE KWA MAJI SAFI NA KUJIFUTA KWA KITAMBAA SAFI ILIKUUACHA MKAVU

6.HAKIKISHA KINGA YA MWILI WAKO IKO JUU

7.VAA CHUPI SAFI ZITENGENEZAVYO KWA VITU HARISI K**A PAMBA NA HARIRI

8.EPUKA ULAJI MBAYA WA CHAKULA HASA PUNGUZA VYAKULA VYENYE KUKUPAYIA SUKARI KWA WINGI MWILINI

9.TUMIA PADS ZISIZO NA KEMIKALI NA ZENYE VITU VYA KUKULINDA NA MAAMBUKIZI,KUKUFANYA UWE MKAVU NA HURU

NB:-"HAKUNA KITU KILICHO CHA THAMANI K**A MWILI WAKO"

Kwa ushauri na suluhisho piga simu namba 0629214933

Kinachosababisha Meno kutobokamashimo kwenye menoTatizo la meno kutoboka au dental cavity kwa kitaalamu ni hali ya jino ...
15/03/2021

Kinachosababisha Meno kutoboka

mashimo kwenye meno
Tatizo la meno kutoboka au dental cavity kwa kitaalamu ni hali ya jino kuwa na shimo. Shimo kwenye jino huanza taratibu na huendelea kupanuka k**a jino halitatibiwa mapema. Ni kutokana na kwamba kufanyika kwa shimo kwenye jino huwa haina maumivu kwenye kipindi cha awali inakuwa vigumu kujua k**a tatizo lipo, ndio maana tunashauri kuonana na Daktari wa meno kila baada ya miezi mtatu akufanyie vipimo.
Pamoja na kwamba tayari umepata shimo kwenye jino na jino lako linaoza, fahamu kwamba kuna hatua unaweza kuchukua kuzuia hali hii isiendelee

Dalili za Meno Kutoboka
Dalili za meno kuwa na mashimo huwa inategemea na ukubwa wa tatizo la meno kuoza. dalili hizi ni k**a

👉Meno kupata ganzi

Maumivu ya meno

Uwepo wa shimo kwenye jino

Utando mweusi kwenye meno

Nini Kinachangia Meno Kutoboka na Kuoza

Kutokana na maeleo ya Dr, Eddward Mellanby kuna vitu vinne vikuu ambavyo huchangia kwa meno kutoboka na kuoza

Upungufu wa vitamini kwenye lishe (A, D, E na hasa vitamin D)
Matumizi makubwa ta vyakula vyenye tindikali
Upungufu wa madini k**a (calcium, magnesium na phosphorus)
Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari iliyosindkwa
Kila mtu na bakteria kwenye mdomo. Bakteria hawa hubadili mabaki ya vyakula mdomono kuwa tindikali. Na tindikali hii huanza kumomonyoa jino na kuruusu bakteria kushambuliza jino.Ndio maana tunashauri kusafisha meno kila baada ya kula au walau amara mbili kwa siku ili kuondoa mazingira ya bacteria wabaya kumea.

Makundi ya Watu waliopo kwenye Hatari zaidi ya Meno Kutoboka
Watu wenye matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari na tindikali kwa wingi
Uchafu wa kinywa k**a kutopiga brush vizuri
Watu wenye kukosa hamu ya kula na
Wagonjwa wa kiungulia ambapo asidi ya tumbo hurudi mpaka mdomoni.
Meno ambayo hutoboka zaidi ni yake ya mwisho yani magego. Meno haya yana uvungu na eneo pana kiasi kwamba linak**ata kiurahisi mabaki ya vyakula.Meno haya ya magego hayasafishwi vizuri kutokana na ugumu wa kuyafikia ndio maaa yanakuwa kwenye hatari zaidi ya kuoza.

Hatua 4 za kufuata uzuia Meno kutoboka
Sasa na tuchambue zile sababu kuu nne ambazo zinachangia meno kutoboka na na hatua asili za kuchukua kulinda meno yako yasiendelee kuoza.

1.Epuka Sukari
Sukari ndio sababu namba 1 ya kutoboka kwa meno yako na pia ni chanzo cha magonjwa mengine mengi k**a uzito mkubwa, kitambi, na kuvurugika kwa homoni.
Anza na kupambana na ulevi wa sukari, kwa kukaa mbali na vitu pmoja na soda na vyakula vya ngano. Tumia majani ya stevi k**a kionjo cha kuongeza utamu kwenye kinywaji chako. Tumia pia asali mbichi kwa kiwango cha kati.

2.Tumia mazao ya maziwa na Vyakula vyenye virutubishi kwa wingi
Maziwa asili yana kiwango kikubwa cha vitamin na madini ambayo huimarisha afya ya meno. Ni muhimu kutumia maziwa asili walau mara mbili kwa week. Maziwa yana Calcium, Vitamin K2, Vitamin D3, magnesium na phosphorus. Mpangilio wa vyakula uwe k**a huu

Vyakula vya wanyama k**a supu ya mifupa, nyama na mayai
Mbogamboga k**a spinach na mboga zenye kijani kilichokolea
Matunda kipande kimoja kila sikuVitamin D kutoka kwenye jua, nusu saa kila siku.
Vyakula vyenye mafuta mazuri k**a mafuta ya n**i, n**i, parachichi, mafuta ya zeituni na samaki
Karanga, mbegu na maharage
Kutokula vyakula vilivyosindkwa, na fast food
3.Jaribu Coconut Oil Pulling
Njia hii iliyoanza kutumika kwa karne nyingi ili kusafisha kinywa na kuzuia meno kutoboka. Njia hii imekuwa ikitukuzwa sana katika uwezo wake wa kusafisha kinywa kwa kuweka mafuta mdomoni na kuyazungusha kisha kutema baada ya dakika 20.
Mafuta yana uwezo wa kuvuta na kunasa uchafu na vimelea wabaya waliopo mdomoni.
Soma vizuri hapa kuelewa kuhusu coconut oil pulling.

4. Punguza matumizi ya vyakula vinavyoongeza tindikali k**a wanga uliokobolewa na kusafishwa, soda, juusi zilizosindikwa na p**i.

Kwa ushauri zaidi wasiliana nami kwa

Simu/whatsapp: 0629214933

~ JE WAJUA?  MATATIZO YANAYOPELEKEA MAUMIVU YA VIUNGO - JOINT TEARS & WEAR°.~ARTHRITIS NI NINI ?~Matatizo ya viungo,migu...
01/01/2021

~ JE WAJUA? MATATIZO YANAYOPELEKEA MAUMIVU YA VIUNGO - JOINT TEARS & WEAR°.
~
ARTHRITIS NI NINI ?
~
Matatizo ya viungo,miguu kuwaka moto , maumivu ya kiuno na mgongo , yamekua yakiwasumbua watu wengi hasa wenye uzito mkubwa , wanaofanya mazoezi na wazee wenye umri kuanzia 55+.
~
Hii ni kwasababu umri unavyozidi kwenda mwili unashindwa kuzalisha ute ute katika viungio vya mifupa na hivyo kupelekea misuguano ya mifupa Na Kusababisha maumivu makali sana na kupelekea mtu kushindwa Kukaa , Kuinuka , Kukimbia au Hata Kutembea Kabisa!!
~
- Mara Nyingi Ugonjwa Huu Huitwa ARTHRITIS , Unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa.
~
Inaweza kuwa cartilage inalika,upungufu wa synovial fluid (Maji Maji Katika Maungio ) , maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo Mbali Mbali , Ikiwemo Uzito mkubwa.
~
Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa (joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo hilo moja.
~
Chanzo Cha Arthritis Ni Nini...?
~
Ili Upate Kuelewa Vyema Chanzo cha ugonjwa huu,hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana( Maungio).
~
Mfano Goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana:
~
Maungio ya mifupa - Ligaments;
~
-Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja , hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje , ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi.
~
Cartilage ; Huu ni utando unafunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja,Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu.
~
Capsule ; Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote , ndani ya mfuko huu wa capsule kuna synovial fluid ambayo huzalishwa na synovial membrane.
~
Synovial fluid : Huu ni ute ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule.
~
K**a nilivyoeleza hapo juu kuwa kuna aina zaidi ya 100 za ugonjwa huu wa joints au arthritis.
~
Katika mada yetu ya leo tutatazama aina k**a nne hivi za ugonjwa huu,tukielezea chanzo cha kila aina....
~
1. Osteoarthritis.
- Hii ni aina ya arthritis inayosumbua watu wengi zaidi kuliko aina nyingine zote...
~
Ugonjwa huu huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa , Osteoarthritis hutokea pale cartilage inapopoteza uwezo wake wa kubonyea na kuwa ngumu hivyo kuharibika haraka.
~
- Cartilage ni kiungo cha kuhimili migandamizo ya ghafla ( shock absorber ), Cartilage hii inapopoteza ubora wake , tendons na ligaments huvutika na kusababisha maumivu.
~
Hali ya uharibifu huu wa cartilage ikiendelea mwishowe mifupa huanza kusuguana moja kwa moja na ndipo mgonjwa atakapoanza kupata maumivu makali sana sana.
~
- Athari za ugonjwa huanza taratibu na kuongezeka zaidi na Mgonjwa ataanza kupata maumivu kwenye joint baada ya kufanya shuguli fulani au baada ya mapumziko ya muda mrefu.
~
Joints zitaanza kukaza siku hadi siku , Hasa wakati wa asubuhi unapotaka kuanza shughuli zako za kawaida.
Na siku zinavyosogea ndivyo utakavyoona ni vigumu zaidi kukitumia kiungo chako , Mara nyingine utaona uvimbe kwenye joint.
~
Osteoarthritis - Hushambulia zaidi nyonga,mikono , Magoti na Uti wa Mgongo.
~
2. Rheumatoid arthritis.- Ugonjwa huu hutokea pale mfumo wa kinga ya mwili unapopungua , viungo huanza kushambuliwa , ikiwa ni pamoja na synovial membrane (synovium) na kusababisha uvimbe na maumivu.
~
Hali hii isipodhibitiwa,huweza kusababisha ulemavu . Ugonjwa huu unaweza pia kushambulia macho , Ngozi , Mapafu , Midomo , Damu na Mishipa ya Damu.
~
Huu ni ugonjwa ambao zaidi ni wa wanawake na huwatokea zaidi wawapo kati ya umri wa miaka 40 hadi 60.
~
Mgonjwa atasikia maumivu na kuona uvimbe kwenye joints za pande zote za mwili ;
~
Yaani k**a ni magoti yote mawili yatashambuliwa na Viungo vinavyo shambuliwa zaidi ni Vidole , Viwiko vya mikono na miguu.
- Athari zake huonekana zaidi asubuhi unapoamka na maumivu yanaweza kudumu kwa muda wa hadi nusu saa.
Muathirika wa ugonjwa huu hujisikia mchovu muda wote , hukosa hamu ya kula na hupungua uzito , Ugonjwa huu huweza kukua zaidi na Kusababisha matatizo katika viungo vyote vya mwili.
~
Matatizo yanayoweza kujitokeza ugonjwa ukikua ni k**a yafuatayo:
– Macho kuwa na ukavu , maumivu , wekundu , kutopenda mwanga na kutoona vizuri.
– Midomo , Ukavu au kukauka kwa lips za midomo,maumivu na maambukizi ya fizi.
– Ngozi,Vijinundu chini ya ngozi kwenye maeneo yenye mifupa
-- Mapafu,Kushindwa kupumua vizuri.
– Mishipa Ya Damu,Uharibifu wa mishipa ya damu.
– Damu , Upungufu wa chembechembe nyekundu za damu.
3. Infectious arthritis (septic arthritic).
- Aina hii ya arthritis inatokana na maambukizi ya bacteria kwenye synovial fluid. Maambukizi haya yanaweza kuwa pia ni ya fungus au virusi.
~
Wadudu kutoka sehemu nyingine ya mwili iliyo karibu na maungio ya mifupa huweza kusambaa kupitia mfumo wa damu hadi kwenye joint na kuleta maambukizi.
~
Mara nyingi mtu mwenye aina nyingine ya arthritis ndiye anayepata maambukizi ya namna hii , Mgonjwa ataanza kwanza kupata homa , maumivu na uvimbe kwenye joint.
~
Maeneo ambayo hushambuliwa zaidi na aina hii ya arthritis ni Magoti , Mabega , Kiwiko cha mkono , Kiganja (wrist) na vidole na mara nyingi ni eneo moja tu ndilo litakaloshambuliwa.
~
4. Juvenile rheumatoid arthritis (JRA).
- Ni ugonjwa ambao huwapata zaidi vijana walio na umri ulio chini ya miaka 16 na unakuja kwa namna nyingi.
Kuna aina kuu tatu za ugonjwa huu:
~
I. Pauciarticular JRA.
- ~
~Huu ndiyo unaoonekana zaidi na hauna madhara makubwa ukilinganisha na aina nyingine,Mtoto atasikia maumivu kwenye joints zinazofikia nne.
II. Polyarticular JRA.
- Huu hushambulia joints nyingi zaidi , zaidi ya nne na maumivu yake ni makali zaidi.
Kadri siku zinavyo ongezeka, ndivyo maumivu yatakavyozidi.
III. Systemic JRA.
- Huu huonekana kwa nadra ambapo maumivu hujitokeza kwenye maeneo mengi na madhara yake kuwa makubwa zaidi,
Mtoto ataanza kusikia homa za vipindi ambapo huzidi zaidi nyakati za jioni.
~
Hali hii inaweza kumtokea mtoto kwa muda mfupi au kwa wengine kwa muda mrefu sana.
Mtoto atapata mauvimu kwenye maungio ya mifupa (joints) , uvimbe kwenye maungio hayo na kukak**aa kwa viungo.
Mtoto huyu atakosa hamu ya kula hivyo kumfanya akonde.
Ugonjwa ukizidi , mtoto anaweza kudumaa (kushindwa kukua), ukuaji wa mifupa yake kuathirika na kupata matatizo ya macho (uveitis).
Changamoto Kubwa Ya Matatizo Ya Joints Huwapata Wana Michezo , Wanyanyua Vyuma (Body Builder) ,Watu Wanaofanya Kazi Ngumu,Mafundi ,Watoto Wadogo Wenye Umri wa Kuanza Kutembea , Magari , Wabeba Mizigo Na Madereva Wa Masafa Marefu Pamoja Na Wafanyakazi Wa Mahofisini Wanao Fanya Kazi Za Kukaa Zaidi.
"Lipo Suluhisho Pekee la Kumaliza Matatizo Yote Haya Kwa Haraka Sana
~
📷 Tatizo Lako linapona kabisa. Wasiliana Nasi kwa kupiga Simu namba 0629214933

🌽"UGONJWA WA KISUKARI - 🌽DIABATES  MELLITUS🌽~ Nini Chanzo ?🥒Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) hutokea pale tezi ko...
23/12/2020

🌽"UGONJWA WA KISUKARI - 🌽DIABATES MELLITUS🌽

~ Nini Chanzo ?

🥒Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) hutokea pale tezi kongosho (pancrease) inaposhindwa kutengeneza homoni au kichocheo aina ya Insulin, au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho cha insulin na kusababisha kuongezeka kiwango cha sukari kwenye damu (hyperglycemia).

🥒Insulin ni kichocheo au homoni inayotengenezwa na kongosho ili kudhibiti kiwango cha sukari.

🥒Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababishwa kuwa na kiwango kidogo cha Insulin mwilini, mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili. Ili kuelewa vyema ugonjwa wa kisukari ni muhimu kwanza kuelewa namna chakula kinavyovunjwa vunjwa na kutumiwa na mwili ili kuzalisha nguvu.

🥒Wakati chakula kinapoyeyushwa matukio kadhaa hutokea.

1.Tukio la kwanza ni sukari inayoitwa glucose ambayo ni chanzo cha nguvu mwilini huingia katika damu.

2.Tukio la pili ni kiungo kinachoitwa kongosho (pancrease) kutengeneza kichocheo cha Insulin. Kazi ya Insulin ni kuondoa glucosei katika damu na kuingiza katika misuli, seli za mafuta na ini, ambako hutumiwa k**a nishati.

🥒Watu wenye ugonjwa wa kisukari huwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kwa sababu miili yao haiwezi kupeleka sukari kwenye seli za mafuta, ini na misuli ili ihifadhiwe kwa ajili ya kuzalisha nguvu.

🥒Hii ni kutokana sababu zifuatazo.

1.Kongosho kutokuwa na uwezo wa kutengeneza insulin ya kutosha, au--->
2.Seli za mwili haziathiriwi na insulin k**a inavyotakiwa ama sababu zote hizo mbili.

🥫AINA ZA KISUKARI🥫

1⃣ KISUKARI AINA YA KWANZA🍬 - 🥫TYPE 1 DIABETES MELLITUS🥫

🥒Hii ni aina ya kisukari inayowaathiri zaidi watoto na vijana. Aina hii hutokea iwapo seli maalumu zinazotengeneza homoni ya insulin zinapokosekana katika tezi kongosho au zinapoharibika kutokana na sababu yeyote ile, na hivyo kusababisha ukosefu kabisa au upungufu wa kichocheo hicho kwenye damu.
Mambo yanayoweza kusababisha uharibifu wa seli hizi katika tezi kongosho ni pamoja na kushambuliwa tezi kongosho kunakoweza kufanywa na magonjwa ya kinga ya mwili ya mtu mwenyewe au autoimmune diseases, au kushambuliwa na vyanzo visivyojulikana.

2⃣ KISUKARI AINA YA PILI🥫 -(TYPE 2 DIABETES MELLITUS)🥫

🥒Hii ni aina ya kisukari inayotokea zaidi ukubwani. Aina hii ya kisukari husababishwa na kupungua utendaji kazi wa homoni ya insulin, au seli kushindwa kutumia insulin ipasavyo.

🥒Hali hii mara nyingi husababishwa na unene uliopitiliza yaani obesity, au hali ya kutoushughulisha mwili kabisa (physical inactivity).
Kwa vile, katika aina hii ya kisukari, insulin huzalishwa kwa kiwango cha kutosha isipokuwa tatizo lipo kwenye ufanisi na utendaji kazi wake,

3⃣KISUKARI CHA UJAUZITO (GESTATIONAL DIABETES MELLITUS)🍖

🥒Ni aina ya kisukari kinachotokea pindi kunapokuwa na ongezeko la kiwango cha sukari katika damu (hyperglycemia) wakati wa ujauzito.

🥒Aina hii ya kisukari huathiri karibu asilimia 2 hadi 5 ya mama wajawazito wote ingawa wengi wao hupata nafuu na kupona kabisa mara tu baada ya kujifungua.

🥒Hata hivyo karibu asilimia 20 mpaka 50 ya mama wajawazito wanaopata aina hii ya kisukari huweza kuendelea kuwa na ugonjwa huo hata baada ya ujauzito na hatimaye kuwa na aina ya pili ya kisukari.

🥫SABABU ZA KISUKARI🥫

🥒Sababu za kisukari hutofautiana kulingana na aina ya ugonjwa huo.

🥒Aina ya kwanza ya kisukari ina uhusiano mkubwa sana na kurithi. Aidha aina hii pia husababishwa na maambukizi virusi k**a vile Coxsackie virus type B4.

🥒Visababishi vingine ni pamoja na sumu inayotokana na kemikali za baadhi ya vyakula (food borne chemical toxins) na kwa baadhi ya watoto wachanga maziwa ya ng'ombe yanaweza kuchochea kinga ya mwili wa mtoto uushambulie mwili wenyewe na hivyo kusababisha uharibifu katika tezi kongosho.

🥒Aina ya pili ya kisukari kwa ujumla husababishwa zaidi na jinsi mtu anavyoishi na pia matatizo ya kijeneteki. Aidha kuongezeka uzito na unene kupita kiasi (obesity).

🥒Sababu nyingine ni pamoja na kuongezeka umri, maisha ya kivivu na kutofanya mazoezi na pia ugonjwa wa tezi kongosho (pancreatitis) ambao hufanya insulin inayozalishwa kuwa na ufanisi mbovu au ya kiwango cha chini.

🥫DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI🥫

▪️Kukojoa mara kwa mara.
▪️Kuhisi kiu kali na kunywa maji kwa kiwango cha kupitiliza (polydipsia).
▪️Kuhisi njaa na kula mara kwa mara (polyphagia).
▪️Kuchoka haraka.
▪️Kupungua uzito.
▪️Vipele mwilini (diabetic dermadromes).
▪️Kutoa harufu ya acetone inayofanana na harufu ya pombe.
▪️Kuhisi maumivu ya tumbo na kupoteza fahamu.

🥒Na wagonjwa wa kisukari pia huwa katika hatari ya kupata maambukizi katika kibofu cha mkojo, ngozi na kwa wanawake sehemu za siri.

▪️Suluhisho :- Kwa yeyote anayehitaji Kuondokana na Mateso Ya Kisukari Kwa Njia Ya Virutubisho Lishe awasiliane na kampuni kwa ☎️ Namba zifuatazo 0629214933

"🍬AINA ZA UZIBAJI WA MIRIJAYA UZAZI KWA WANAWAKE🍬"🥫Katika makala iliyopita Tuliona sababu kuu tatu zinazomfanya mwanamke...
22/12/2020

"🍬AINA ZA UZIBAJI WA MIRIJAYA UZAZI KWA WANAWAKE🍬"

🥫Katika makala iliyopita Tuliona sababu kuu tatu zinazomfanya mwanamke asipate mimba. Kuziba kwa mirija ya uzazi huchukua asilimia ishirini ya tatizo la ugumba kwa mwanamke au mwanamke kupoteza uwezo wa kuzaa, pamoja na hizo sababu tatu, pia zipo sababu nyingine ndogo nyingine.

🥫Aina za uzibaji; ni mirija kuziba upande wa mwishoni karibu na vifuko vya mayai Distal Tubal Occlusions.

🥫Hali hii inahusiana kabisa na tatizo la mirija kuvimba au kujaa maji hali iitwayo kitaalam Hydrosalpinx ambapo pamoja na mwanamke kushindwa kupata mimba, pia husumbuliwa na maumivu ya tumbo chini ya kitovu mara kwa mara yanayosambaa kulia na kushoto.

🥫Hali ya kuvimba kwa mirija au mirija ya uzazi kujaa maji husababishwa na maambukizi ya vimelea vya Chlamydia Trachomatics.

🥫Katika hali hii pia huweza kutokea hali ya kizazi na viungo jirani kushik**ana hivyo mirija pia hushikwa na kuziba.

🥫Hali hii ya kuziba mirija mwishoni husababisha sehemu ya mirija iliyo k**a vidole iitwayo Fimbriae kugandamana na kusababisha kushindwa kuchukua yai lililopevuka na kuliingiza katika mirija tayari kwa kutungisha mimba.

🥫Tatizo hili linapotokea, sehemu nyingine ya mirija inakuwa wazi au nzima. Mrija unaweza kuziba katikati Midsegment ambapo sababu kubwa inaweza kuwa mrija kufungwa au kukatwa k**a njia ya kufunga uzazi.

🥫Mrija unaweza kuziba mwanzoni na sababu kubwa ni maambukizi kwenye kizazi kutokana na utoaji au kuharibika mimba na maambukizi mengine sugu ya kizazi.

🥫Toa maoni yako kuhusu ulichoelewa.

🥫"Kwa Msaada Zaidi na Ushauri Kuhusu Masuala Mbali Mbali Kiafya -

📞Mawasiliano : 0629214933

"JE' UTAJUWAJE K**A TEZI DUME YAKO IKO SAWA. ?"TEZI DUME".~(Prostate gland)". Ni Nini ?~"Tezi dume ni sehemu mojawapo ya...
08/12/2020

"JE' UTAJUWAJE K**A TEZI DUME YAKO IKO SAWA. ?
"TEZI DUME".
~
(Prostate gland)". Ni Nini ?
~
"Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume.
Inaundwa na sehemu mbili ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu.
~
Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (re**um) na na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra)~
"KAZI ZA TEZI DUME AMBAZO ULIKUWA HUZIJUI;
~
1. Tezi dume hutoa majimaji ambayo huchanganyika na mbegu za kiume na kutengeneza shahawa. Asilimia 60 ya shahawa huwa ndio hayo majimaji yaliyotengenezwa na tezi dume na asilimia 40 ndio mbegu za kiume zilizotengenezwa kwenye kiwanda cha mbegu(korodani).
~
2.Majimaji yanayotoka kwenye tezi dume huanza kutangulia mbele kusafisha njia ya mkojo ili kuondoa asidi kwenye njia hiyo na kubakia hali ya alkaline ili mbegu za kiume zisife.hivyo inaondoa asidi na pia in**ilinda zisife kuanzia kwenye njia ya mkojo ya mwanaume mpaka ukeni kwa mwanamke maana napo kuna asidi sana.
~
3. Kazi nyingine ya tezi dume ni kuchuja sumu ili zisichanganyike na mbegu za kiume hivyo hata mbegu inakuwa haina ugonjwa na salama.
~
4.Tezi dume ndio yenye kufunga njia ya mkojo na kuruhusu mbegu za kiume zitoke wakati umefika kileleni na kuziba njia ya mbegu za kiume na kufungua njia ya mkojo unapokuwa umemaliza tendo.
~
5.Wanaume tukimaliza tendo huwa shahawa zinaruka sana hiyo ni kazi ya tezi dume. K**a shahawa zako zinamwagika tu lakini haziruki zenyewe k**a mkojo nikiwa na maana kwa speed ujue tezi dume lako haliko sawa.pia ngumu mbegu zako kufikia yai la mwanamke na kumpa ujauzito.
~
6.Tezi dume inailinda njia ya mkojo isishambuliwe na vijidudu vya U.T.I.
~
7. Tezi dume ni sehemu ya kilele cha raha kwenye tendo la ndoa kwa mwanaume.
~
8.Tezi dume kupitia majimaji yake ndio inayosafirisha mbegu za kiume kutoka kwa mwanaume mpaka kwa mwanamke na kukutana na yai la mwanamke.
~
9.Majimaji yanayotoka kwenye tezi dume dio chakula cha mbegu za kiume. Kwahiyo mbegu za kiume zinapata chakula kutoka kwenye tezi dume.
~
Kuvimba Tezi Dume (BPH)".
~
Kwa kadiri mwanaume anavyozeeka, ni jambo la kawaida pia kwa tezi dume kuongezeka ukubwa na kuvimba.
~
Kuvimba kwa tezi dume husababishwa na nini ?
~
Chanzo halisi cha kuvimba kwa tezi au vihatarishi vyake (risk factors) havijulikani kwa uhakika. Kwa muda mrefu imekuwa ikichukuliwa kuwa ugonjwa huu hutokea kwa wanaume watu wazima na wazee tu lakini siku hizi hata vijana..
~
"BAADHI ZA TAFITI ZINAONYESHA KUWA HORMONES,UMRI MKUBWA NA MAMBUKIZI KATIKA NJIA YA MKOJO NI VYANZO VYA KUVIMBA KWA TEZI".
~
° DALILI ZA KUVIMBA KWA TEZI DUME:
~
-Hukojoa mkojo unaokatika katika
-Hukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
-kuchukua muda kabla ya mkojo kuanza kutoka
-Hali ya kujihisi kubanwa na mkojo kila mara
-Kushindwa kuthibiti mkojo kiasi cha mkojo kutirika wenyewe.
-Hali ya kuhisi mkojo haujaisha kwenye kibofu
-Hukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku
-Kushindwa kukojoa kabisa (urine retention) .
~
BAADHI YA MADHARA YA KUVIMBA KWA TEZI:
~
-Vijiwe kwenye kibofu cha mkojo
-Uambukizi katika njia ya mkojo (UTI)
-Madhara katika figo au kibofu
-Shinikizo la damu
-Kushindwa kutoa shahawa kwenye uume (retrograde ej*******on)
-kupungua kwa nguvu za kiume na kushindwa tendo la ndoa
-Uhanithi.
~
"Lipo Suluhisho Pekee la Kumaliza Tatizo hilo Bila Kufanyiwa Upasuaji".
~
⚠️ Tatizo Lako linapona kabisa. Wasiliana Nasi kwa kupiga Simu 0629214933 whatsapp ni hii namba pia

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengi...
07/12/2020

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)

Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengine sana na ni tatizo ambalo linakera sana kwa sababu hata unapoenda hospitali Mara nyingi hawapati tatizo lolote

NINI HASWA CHANZO CHA TATIZO HILI

1:UMRI
Kawaida mtu anapokua umri umeenda, mwili mzima uzeeka pamoja na mfumo mzima wa damu, hii husababisha mishipa midogo midogo ya damu kufa, au kuziba hii husababisha chakula na hewa ya oksijeni kutofika kwa ufasaha maeneo ya mbali k**a miguuni na vidoleni hali hii hupeleekea mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa safi hivyo ganzi hutokea

2:KISUKARI
Sukari inapokua nyingi kwenye mzunguuko wa damu hupelekea kuunguza mishipa ya damu halo hii husababisha mishipa kusinyaa ambalo hupelekea hewa ya oksijeni na chakula kutofika kwa ufadsaha maeneo ya mbali sana k**a miguuni na mikononi hali hii husababisha mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa hivyo husababisha ganzi

3:DAMU NZITO
Damu inapokua nzito pia hupelekea MTU kupata tatizo LA ganzi kwa ni husababisha kutofika kwa damu kwenye mishipa midogo midogo ya damu hii hupelekea ganzi pia

TIBA YA GANZI
-Hii ni virutubisho asili ya kupambana na tatizo hili bila madhara
-Imetengenezwa na mitishamba mitatu yenye uwezo mkubwa sana wa kufungua mishipa midogo midogo ya damu ambayo inapoziba au inapokua ndio chazo cha tatizo hili
-Huzuia damu isivilie kwenye mishipa hivyo huondoa hatari ya kiharusi
-Huiuisha mishipa midogo midogo ya damu na kuruhusu damu kupi
-Inafaa sana kuifanya damu Iwe nyepesi hivyo husaidia kuondoa tatizo la ganzi

Inasaidia wakina mama wenye tatizo la mvurugiko wa hedhi hedhi vimbe kwenye kizazi

Tiba na ushauli Tuma ujumbe neno Afya kwenda namba 0629214933

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengi...
07/12/2020

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)

Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengine sana na ni tatizo ambalo linakera sana kwa sababu hata unapoenda hospitali Mara nyingi hawapati tatizo lolote

NINI HASWA CHANZO CHA TATIZO HILI

1:UMRI
Kawaida mtu anapokua umri umeenda, mwili mzima uzeeka pamoja na mfumo mzima wa damu, hii husababisha mishipa midogo midogo ya damu kufa, au kuziba hii husababisha chakula na hewa ya oksijeni kutofika kwa ufasaha maeneo ya mbali k**a miguuni na vidoleni hali hii hupeleekea mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa safi hivyo ganzi hutokea

2:KISUKARI
Sukari inapokua nyingi kwenye mzunguuko wa damu hupelekea kuunguza mishipa ya damu halo hii husababisha mishipa kusinyaa ambalo hupelekea hewa ya oksijeni na chakula kutofika kwa ufadsaha maeneo ya mbali sana k**a miguuni na mikononi hali hii husababisha mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa hivyo husababisha ganzi

3:DAMU NZITO
Damu inapokua nzito pia hupelekea MTU kupata tatizo LA ganzi kwa ni husababisha kutofika kwa damu kwenye mishipa midogo midogo ya damu hii hupelekea ganzi pia

TIBA YA GANZI
-Hii ni virutubisho asili ya kupambana na tatizo hili bila madhara
-Imetengenezwa na mitishamba mitatu yenye uwezo mkubwa sana wa kufungua mishipa midogo midogo ya damu ambayo inapoziba au inapokua ndio chazo cha tatizo hili
-Huzuia damu isivilie kwenye mishipa hivyo huondoa hatari ya kiharusi
-Huiuisha mishipa midogo midogo ya damu na kuruhusu damu kupi
-Inafaa sana kuifanya damu Iwe nyepesi hivyo husaidia kuondoa tatizo la ganzi

Inasaidia wakina mama wenye tatizo la mvurugiko wa hedhi na vimbe kwenye kizazi

Tiba na ushauli Tuma ujumbe neno Afya kwenda namba 0629214933

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengi...
07/12/2020

TATIZO LA GANZI YA MIGUU NA MIKONO(MIGUU KUWAKA MOTO NA TIBA YAKE)

Ganzi ni moja ya tatizo/ugonjwa unaowakumba watu wengine sana na ni tatizo ambalo linakera sana kwa sababu hata unapoenda hospitali Mara nyingi hawapati tatizo lolote

NINI HASWA CHANZO CHA TATIZO HILI

1:UMRI
Kawaida mtu anapokua umri umeenda, mwili mzima uzeeka pamoja na mfumo mzima wa damu, hii husababisha mishipa midogo midogo ya damu kufa, au kuziba hii husababisha chakula na hewa ya oksijeni kutofika kwa ufasaha maeneo ya mbali k**a miguuni na vidoleni hali hii hupeleekea mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa safi hivyo ganzi hutokea

2:KISUKARI
Sukari inapokua nyingi kwenye mzunguuko wa damu hupelekea kuunguza mishipa ya damu halo hii husababisha mishipa kusinyaa ambalo hupelekea hewa ya oksijeni na chakula kutofika kwa ufadsaha maeneo ya mbali sana k**a miguuni na mikononi hali hii husababisha mishipa ya fahamu kukosa chakula na hewa hivyo husababisha ganzi

3:DAMU NZITO
Damu inapokua nzito pia hupelekea MTU kupata tatizo LA ganzi kwa ni husababisha kutofika kwa damu kwenye mishipa midogo midogo ya damu hii hupelekea ganzi pia

TIBA YA GANZI
-Hii ni virutubisho asili ya kupambana na tatizo hili bila madhara
-Imetengenezwa na mitishamba mitatu yenye uwezo mkubwa sana wa kufungua mishipa midogo midogo ya damu ambayo inapoziba au inapokua ndio chazo cha tatizo hili
-Huzuia damu isivilie kwenye mishipa hivyo huondoa hatari ya kiharusi
-Huiuisha mishipa midogo midogo ya damu na kuruhusu damu kupi
-Inafaa sana kuifanya damu Iwe nyepesi hivyo husaidia kuondoa tatizo la ganzi.
Inasaidia wakina mama wenye tatizo la mvurugiko wa hedhi na vimbe kwenye uzazi

Tiba na ushauli Tuma ujumbe neno Afya kwenda namba 0629214933

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255629218863

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pudencial afya point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share