MTAfrica Wellness

MTAfrica Wellness Beauty from the inside out 𓍯𓂃

Njia 6 za kuondoa  maumivu kipindi Cha hedhi. " Ni rahisi mno" !!1. Tembea tembea kidogo hata ndani ya chumba chako.2. F...
23/07/2025

Njia 6 za kuondoa maumivu kipindi Cha hedhi. " Ni rahisi mno" !!

1. Tembea tembea kidogo hata ndani ya chumba chako.
2. Fanya kazi ndogo ndogo.
3. Fanya mazoezi mapesi.
4. Kunywa maji ya Moto au weka miguu ndani ya maji wa moto.
5. Usiupe mwili muda wa kulala.
6. Kula matunda, mboga mboga na vyakula visivyo na mafuta, chumvi na Sukari nyingi.

Umekuwa ukipata maumivu kwa muda gani Sasa?
Maumivu yakiwa makali zaidi wasiliana nasi

0767 536 986

Hivi Unajua Kwamba Uke Hujisafisha WENYEWE?!K**a ulikuwa hujui Hii, Soma hii Mpaka MwishoDouching yaani (Kupiga deki uke...
22/07/2025

Hivi Unajua Kwamba Uke Hujisafisha WENYEWE?!

K**a ulikuwa hujui Hii, Soma hii Mpaka Mwisho

Douching yaani (Kupiga deki uke/kusafisha uke kwa kuingiza vidole/sabuni za medicated k**a protex, family n. K)
...inaaminika kuwa inasababisha maambukizi kwasababu husumbua au kuua mazingira ya bakteria wazuri,... na walinzi katika uke wako na kukuacha katika hatari zaidi ya kupata maambukizi kirahisi kila mara
.. k**a UTI, kutoa harufu mbaya ama (P.I.D) pelvic inflamatory diseases.

👉🏽Pia Kupiga deki uke kunaongeza hatari ya kupata magonjwa ya zinaa, mimba kutunga kwenye mirija ya kizazi(ectopic pregnancy)
...na aina fulani ya kansa ya kizazi (pelvic carcinoma).

🚫Kwa wale wanaoogea sabuni zenye harufu, tafadhali acheni, ogea sabuni za kawaida ambazo ni maalumu kwa ilo mfano Deto n.k,
... au Unaweza kutumia dvaginal care ni mzuri sana kwa Afya ya uke nk,
... na ni salama zaidi na zitasaidia kwa asilimia fulani kuepuka sana na changamoto za kuvurugika kwa ph ya uke.

🚫K**a hujawahi kufanya hii tabia ya kujisafisha kwa kuingiza kidole usijaribu,
... na k**a unafanya acha mara moja vitu hivi husababisha vaginal irritation ni maumivu katika uke na michubuko ambayo itakufanya usifurahie tendo la ndoa na pia kupata madhara tajwa hapo juu.

👉🏾Hayo ni mambo ya kuzingatia na kutothubutu hata kujaribu kuyafanya kwa ajili ya kulinda afya ya uzazi na kutoharibu Uke wako.
-

K**a umejifunza kitu, Fanya kusave Elimu hii kwa faida ya Baadae,

Pia Share Na Rafiki yako tujifunze pamoja.

Una Swali lolote, Uliza kwenye Comments hapo chini, nipo kukusaidia
0767 536 986

Kutokana na wanawake wengi kutojua lini watapata ujauzito inawaweka katika hatari kubwa ya kupata mimba zisizo tarajiwa ...
20/07/2025

Kutokana na wanawake wengi kutojua lini watapata ujauzito inawaweka katika hatari kubwa ya kupata mimba zisizo tarajiwa na wengine kushindwa kushika mimba.

Kwa kawaida yai la mwanamke hupevuka siku kumi na nne (14) kabla ya mzunguko wa hedhi unaofuata.

Ili kujua ni lini yai linapevuka mwanamke anatakiwa kuhesabu siku kumi na nne (14) kutoka mzungoko unaofuata. Siku ya kumi na nne ndio siku ya (siku ambayo yai linapevuka) .

Lakini kwa sababu siku za yai kupevuka hubadilika hivyo kipindi cha hatari (fertilization period) inachukuliwa k**a siku tatu kabla ya yai kupevuka na siku tatu baada ya yai kupevuka.

Kwa mfano iwapo unaanza hedhi tarehe 20 mwezi november,unahesabu siku 14 kurudi nyuma ili kujua siku ya yai kupevuka (ovulation).Kwa mfano huu siku ya yai kupevuka ni tarehe 6 mwezi novemba (tumehesabu siku 14 kurudi nyuma). Kisha unarudi nyuma siku tatu na unaongeza mbele siku tatu ili kupata siku za hatari. Hivyo siku za hatari zitakuwa kuanzia tarehe 3 mpka tarehe 9 Novemba.

Mwanamke akikutana kimwili katika kipindi hiki anaweza kupata ujauzito. Hesabu hii inatumika kwa wanawake wenye mzunguko wa siku 28.

K**a una tatizo la uzazi nitumie Ujumbe sehemu ya Message (DM) sasa
0767 536 986

1. Kupata usingizi wa kutosha;Ukilala bila nguo kabisa mwili wako unakua huru sana, nguo hua na tabia ya kukubana sana n...
20/07/2025

1. Kupata usingizi wa kutosha;
Ukilala bila nguo kabisa mwili wako unakua huru sana, nguo hua na tabia ya kukubana sana na kukunyima usingizi wa kutosha kitu ambacho wewe k**a mlalaji unaweza usigundue...wakati mwingine huenda umeshawahi kulala umevaa shati lakini asubuhi ukajikuta huna, hii ni kwasababu ukiwa katika nje ya fahamu yaani usingizini uliamka ukavua mwenyewe bila kujua sababu usingizi ulikua haupatikani vizuri.

2. Huzuia magonjwa ya ngozi
Ukilala bila nguo, joto lako la mwili hushuka kidogo na katika hali ya kawaida wadudu nyemelezi wa mwili hutaka sehemu yenye joto au unyevunyevu ili kuweza kushambulia hivyo ukilala bila nguo wadudu hawa hawatapata nafasi ya kuushambulia mwili wako na kukuletea magonjwa, hata kipindi cha baridi ni vizuri kujifunika na blanketi nyingi kuliko kuvaa nguo.

3. Husaidia kupunguza uzito
Ukilala na nguo, sababu ya ule usumbufu mtu hupata msongo wa mawazo na hali hiyo husababisha wewe kujisikia njaa na kutaka kula zaidi wakati wa usiku lakini mtu anayelala bila nguo ana-relax sana na kusinzia bila hata kusikia dalili za njaa.

4. Hulinda sehemu za siri
Kwa mwanaume kulala bila nguo huweka korodani zako katika hali ya ubaridi na kusaidia kutengeneza mbegu nyingi za kutosha, lakini pia kwa mwanamke huupa uke hewa ya kutosha ya oksijeni na kuzuia magonjwa ya fangasi yanayopenda kushambulia uko.

5. Hunogesha tendo la ndoa na mahusiano.
Utafiti unaonyesha kwamba wanandoa wanaolala bila nguo kila siku hushiriki tendo la ndoa mara nyingi zaidi kuliko wale wanaolala na nguo na hii huongeza chachu ya mahusiano na kufanya wajione wapya kila siku sababu ya miili yao kutengeneza homoni ya oxytocin( homoni ya upendo).

6. Hupunguza kasi ya kuzeeka
Ukilala bila nguo unatengeneza mazingira mazuri sana ya homoni za mwili wako kufanya kazi sana kuliko kipindi ukilala na nguo ambapo homoni zako zinafanya kazi kwenye mazingira magumu.

7. Hukupa furaha na uhuru
Kwa hali ya kawaida tu mwanamke anapotoka kazini au mizungukoni na kufika nyumbani kitu cha kwanza kabisa kufanya ni kuvua sidiria na kuitupa huko sababu ya kubanwa sana kwa siku nzima, kuvua humpa uhuru sawa sawa na mtu ambaye analala bila nguo ambaye hupata faida hiyo.
0767 536 986

Wakati wa Ovulation, mwili wa Mwanamke hupitia mabadiliko ya homoni ambayo yanaweza kusababisha harufu yake ya mwili kub...
19/07/2025

Wakati wa Ovulation, mwili wa Mwanamke hupitia mabadiliko ya homoni ambayo yanaweza kusababisha harufu yake ya mwili kubadilika. Moja ya maeneo yanayoathiriwa ni kwapa, ambapo baadhi ya wanawake huwa na harufu nzuri zaidi au tofauti na siku za kawaida kutokana na kuongezeka kwa Homoni ya estrogen ambayo huathiri jinsi mwili unavyozalisha jasho na mafuta ya ngozi.

Pia, mwili huzalisha kemikali asili zinazojulikana k**a Pheromones, ambazo huchangia katika mvuto wa asili kati ya wanadamu. Kemikali hizi huchochewa zaidi wakati wa ovulation, na zinaweza kufanya harufu ya mwili kuwa ya kuvutia zaidi kwa wengine. Aidha, bakteria waliopo kwenye ngozi pia huathiriwa na mabadiliko haya, na hivyo kusaidia kutengeneza harufu ya kipekee wakati huu wa mzunguko wa hedhi.

Ingawa si kila mwanamke atahisi mabadiliko haya, tafiti zinaonesha kuwa harufu ya mwili inaweza kuwa moja ya ishara za asili za uzazi, ambazo huchangia katika mvuto wa kijinsia bila mtu mwenyewe kutambua moja kwa moja.

Tango ni tunda muhimu sana katika kusaidia afya na uzuri wa ngozi. Unaweza kula tunda lenyewe, kupaka juisi yake, kugand...
19/07/2025

Tango ni tunda muhimu sana katika kusaidia afya na uzuri wa ngozi. Unaweza kula tunda lenyewe, kupaka juisi yake, kugandika vipande vyake vidogo vidogo au kunywa juisi yake. Njia zote hizo zinakusaidia kupata virutubisho muhimu kwa ngozi yako.

Tango husaidia sana kulainisha ngozi na kuikaza ngozi iliyonyauka na kulegea. Yaani hufanya kazi ya Skin Tonning ya asili. Pia ukiitumia kwa muda endelevu husaidia kuondoa na kuzuia chunusi kubwa kubwa (Pimples), makovu ya chunusi, makunyanzi na ukavu wa ngozi ya usoni.

Ni moja kati ya tunda muhimu sana kwa ajili ya matundo na upendezeshaji wa ngozi yako.

JINSI YA KUANDAA NA KUTUMIA TANGO VIZURI
1. Andaa tango, maji, chombo cha kuwekea vipande vya tango na kifaa cha kukatia tango (Grater) lako katika vipande vidogo vidogo na laini
2. Osha tango lako, chombo chako na kifaa chako cha kukatia tango lako
3. Bila kumenya, anza kulikatakata tango lako katika vipande vidogo vidogo sana na laini na kuweka kwenye chombo chako
4. Ukimaliza kukata tango lako chukua vipande hivyo vidogo vidogo na laini kisha paka usoni, kuzunguka macho na shingoni pamoja na juisi yake
5. Acha ikae kwa dakika 15 – 20 na kisha nawa kwa maji na uache bila kujikausha
6. Rudia hivyo kila siku na kwa muda endelevu hadi matokeo yatakapokuwa mazuri.

FAIDA ZA NJIA HII
1. Ni rahisi sana na salama
2. Ufanisi wake ni mkubwa
4. Gharama yake ni nafuu

USHAURI
Tumia matango mazuri na kata kata vizuri vipande vyako. Hakikisha unatumia mara tu baada ya kutengeneza, usilaze wala kutumia vipande vilivyolala. Kuwa mvumilivu kidogo, utaanza kuona matokeo mazuri baada ya wiki mbili.
K**a unapenda vipodozi vya asili basi tango ni zuri sana kwako. Kula tango, kunywa juisi ya tango, paka vipande na juisi ya matango.

Anza sasa…

0767 536 986

Unaposhika maji kwa muda mrefu, ngozi ya vidole hujikunja ili kukusaidia unaposhika vitu visiteleze.0767 536 986
19/07/2025

Unaposhika maji kwa muda mrefu, ngozi ya vidole hujikunja ili kukusaidia unaposhika vitu visiteleze.
0767 536 986

Kiafya hakuna faida ya ziada kunyoa sehemu za siri. Lakini unapoamua kunyoa fanya hivi ili kupunguza uwezekano wa vipele...
19/07/2025

Kiafya hakuna faida ya ziada kunyoa sehemu za siri.

Lakini unapoamua kunyoa fanya hivi ili kupunguza uwezekano wa vipele.

1. Punguza nywele za huko kwa kutumia mkasi k**a haujanyoa kwa muda mrefu

2. Oga maji ya moto(vuguvugu)- hii itasaidia kulainisha nywele za huko kwa sababu huwa ni ngumu kuliko nywele za sehemu nyingine ya mwili

3. Osha kwa sabuni isiyokuwa na manukato wala dyes. Dove inaweza kuwa chaguo zuri. Hii inasaidia kupunguza bakteria na uchafu maeneo hayo.

4. K**a una shaving cream unaweza kupata

5. Anza kunyoa taratibu, kwa kufuata muelekeo wa nywele zilivyo ota.

-Osha wembe wako kila mara ili kuondoa nywele (wembe ukijaa nywele haukati vizuri)

- Usipitishe wembe eneo moja mara nyingi

-Nyembe zilizotengenezwa kwa ajili ya wanaume zinanyoa vizuri.
-Tumia mashine yenye wembe mmoja

6. Baada ya kunyoa usipake after shave yenye alcohol zaidi ya asilimia 14, alcohol iwe asilimia 14 kushuka chini

7. K**a huwa unasumbuliwa na vipele, baada ya kunyoa paka 1% hydrocortisone cream

-Paka kiasi kidogo sana mara 1 tu

Ikiwa Umejifunza kitu, Basi Share Na Mtu mmoja unaona Elimu Hii itamsaidia

Je Ipi kwako una zingatia Zaidi, au Wewe una zingatia hayo yote Na Bado unapata Vipele?
0767 536 986

Nini husababisha tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake-1Hamu ndio mwanzo wa kila kitu. Inaanza kwanza hamu...
19/07/2025

Nini husababisha tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake-1

Hamu ndio mwanzo wa kila kitu. Inaanza kwanza hamu, unafuata utamu na baadae kilele. Hamu ni hisia za kutaka kufanya, hii ndio kwa lugha ya kawaida wanaita nyegezi.

Kukosa hisia ni tatizo linawaathiri wanawake wengi. Wengine tatizo limekuwepo tangu ajitambue, lakini wengine tatizo hili limetokea baadae tu.

Bahati mbaya sana wanawake wengi wamekuwa wakikaa kimya na hata wale ambao wamekuwa wakitafuta tiba, wamekuwa hawapati matibabu ambayo sio sahihi kutokana na uelewe mdogo wa masuala haya miongoni mwa Jumuia ya wataalam wa afya

Nini kina sababisha tatizo hili
Hili ni tatizo mtambuka; kuna sababu nyingi sana zinazosababisha mwanamke kukosa hamu ya tendo la ndoa

▫️Mahusiano - Mbali na afya ya mwili na akili, uhusiano na mwenzi wako ni jambo la muhimu sana katika kufurahia tendo la ndoa. Iwapo uhusiano wenu una matatizo, ugomvi na kukosekana kwa uaminifu inaweza kuwa sababu. Hata kwa wana ndoa ambao hawana matatizo yoyote bado kuishi pamoja muda mrefu huwa inasababisha hisia kupungua hasa kwa wanawake.

▫️Uchovu na mafadhaiko - sababu zote zinazosababisha uchovu wa mwili na stress ikiwemo kazi za nyumbani, ofisini, magonjwa k**a upungufu wa damu, magonjwa ya moyo, ugonjwa wa mapafu au magonjwa ya akili zina athari kubwa sana katika hisia za mwanamke
Pia hali hiyo hutokea baada ya mama kujifungua, ambapo mama anachoka mara kwa mara kutokana na kukidhi mahitaji ya mtoto, hali ambayo hupunguza sana hamu ya tendo la ndoa.

Wanawake wa umri wa kati wanaathiriwa na mahitaji ya wazazi, watoto wao ambao wanakuwa katika umri wa kubalehe, changamoto kazini na mabadiliko ya wenzi wao.

▫️Umri na kukoma hedhi
Matatizo huwa yanatokea mara nyingi kwa wanawake wenye umri wa kati ya miaka 45 hadi 65, na kwa kiwango cha chini kwa umri chini ya miaka hiyo.

▫️Magonjwa ya akili na baadhi ya dawa ikiwemo sonona, hofu na dawa zinazotumika kutibu magonjwa hayo zinaweza kusababisha.

Inaendelea kwenye post inayofuata. .
-

SITZ BATH inafanyika kwa kukalia maji ya vuguvugu. Daktari anaweza kukushauri ufanye  Sitz bath  k**a una vidonda au maj...
29/06/2025

SITZ BATH inafanyika kwa kukalia maji ya vuguvugu. Daktari anaweza kukushauri ufanye Sitz bath k**a una vidonda au majereha ukeni na kwenye njia ya haja kubwa. Mwanamke au mtu mwingine anaweza kufanya Sitz bath k**a amejifungua, ameshonwa ukeni, ana haemerrhoid, au kidonda kwenye njia ya haja kubwa na kwa watoto k**a anafunga choo.

Kwa wanawake wa kawaida ambao hawana matatizo yoyote ya kiafya ukeni au kwenye njia ya haja kubwa hakuna faida yoyote ya ziada ya kufanya Sitz bath kila siku, vinginevyo uwe umeshauriwa na daktari...!na wala Sitz bath haisafishi uke, uke huwa unajisafisha wenyewe naturally..!

-
Natumaini Umejifunza kitu, Mtag rafiki yako kwenye Coment tujifunze pamoja, Na k**a una changamoto yoyote ya uzazi nitumie Ujumbe whatsapp, no:0767536986, MTAfrica Wellness kwa msaada zaidi.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255772827245

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MTAfrica Wellness posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share