Mkijacho

Mkijacho MKIJACHO

Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.

pia taasisi inatoa elimu na kupinga ukatili wa utoaji mimba!

+255746465095

WANAUME NA MIMBA ISIYOTARAJIWA (UNPLANNED PREGNANCY)MIMBA ISIYOTARAJIWA (UNPLANNED PREGNANCY)Hii ni mimba iliyopatikana ...
20/09/2024

WANAUME NA MIMBA ISIYOTARAJIWA (UNPLANNED PREGNANCY)

MIMBA ISIYOTARAJIWA (UNPLANNED PREGNANCY)

Hii ni mimba iliyopatikana kinyume na uhitaji wa wahusika,
Inaweza kuwa mwanamke na mwanaume wakawa kwenye mahusiano ya kawaida au mahusiano ya ndoa.
Mimba aina hii hutokea wahusika wanapofanya tendo la ndoa pasipo uwepo wa kinga ya kuzuia mimba.

Taasisi ya Mkijacho ilifanya utafiti kwa kuuliza maswali kutoka kwa wanaume na wanawake kupata majibu juu ya ukweli uliopo kuhusu mapokeo ya taarifa ya mimba isiyotarajiwa kwa wanaume,
walipokeaje hilo swala na yapi yalikua majibu yao na matokeo yaliyotokea baada ya taarifa za uwepo wa mimba isiyotarajiwa.

Haya ndio baadhi ya majibu.

1)Anna Johnston,

Tulikua na uhusiano mzuri tu mpaka pale nilipojigundua mjamzito na kumpatia taarifa,
Uhusiano wetu uliishia hapo.
Alisema hayuko tayari kuitwa BABA na akaamua kuniblock.

2) Peter makaranga,

Alikua ni mwanamke mwenye kila sifa niliyoihitaji,
Ujinga wangu wa kutofikiri kabla ya kutenda ulifanya tuachane baada ya kumlazimisha kutoa mimba,nilimnunulia dawa na kumpelekea alipo.
Najutia sana nilikosa mtoto na nimemkosa yeye baada ya kumlazimisha kutoa mimba alisema hayuko tayari kuua watoto wengine zaidi,
Sahivi Ameolewa ana watoto Mimi nipo tu sina mtoto hata wa kusingiziwa ๐Ÿ˜ข๐Ÿ˜ข

3)Fatma Hassan,

Kwa miaka 9 alidai ananipenda sana na siku niliyomkubalia kuwa pamoja nae ndio siku niliyopata mimba,
Baada ya kumwambia kuhusu mimba alisema hayuko tayari kuitwa BABA.
Namshukuru Mungu nimelea mimba nimejifungua mtoto mzuri sana Sasa hivi anaishia kulike picha za mtoto humu mtandaoni kunitafuta pia anaogopa ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

4)Rajab Ally,

Ukweli nilikosea sana na ninajisikia hatia hadi muda huu.
Nilikataa ujauzito usiotarajiwa,
Familia ya Binti imemuozesha binti yao na kumpa mwanaume mwingine ujauzito wangu na mpaka sasa sina haki ya kumuona mtoto wala kumtambua k**a ni mwanangu,
Ilikua hasira tu na ujana Kwa sasa namhitaji mtoto wangu sijuhi nifanyeje,

Hayo ni baadhi ya maoni ya wadau tuliowahoji lakini pia wako waliosema wanaume zao walifurahia sana na kuwapa zawadi k**a vile magari n.k

Ukweli kuhusu wanaume na mimba isiyotarajiwa (unplanned pregnancy)

Kukabiliana na mimba isiyotarajiwa (unplanned pregnancy) ni mojawapo ya kitu kinachowapa msongo wa mawazo wanawake na wengine kimewagharimu maisha yao pale walipojaribu kutoa mimba,pia wengine imewafanya kuwa na majuto makubwa maishani mwao.

Lakini pia na wanaume mara nyingi hukabiliana na msongo wa mawazo,majuto ya baadae na mfadhaiko wa akili (depression)

Bila kujali kuwa mwanamke mwenye mimba ni mkewe wa ndoa, mchumba au mchepuko.

Wanaume wengi huchanganyikiwa na kukosa utulivu pale wanaposikia wamesababisha mimba isiyotarajiwa.
Kutokana na uwepo wa sababu mbalimbali ikiwemo hofu ya uchumi,kutokua na mahusiano ya malengo na kadhalika,

Baadhi ya wanaume hupata hisia za hasira na mshangao kwanini imetokea hivyo,
Hupata maswali mengi kuhusu ukweli wa uhusika wa ubaba wao Kwa mtoto atakayezaliwa.
Huhofu kuhusu ukurasa mpya wa majukumu ya ulezi.
Huhofu kuhusu uwajibikaji na Kila kitu kuhusu mtoto atakapozaliwa.
Hali hiyo huwapelekea kukosa majibu mazuri na maamuzi mazuri juu ya hatma ya mtoto aliye tumboni kwa wakati huo.

Katika hali hiyo ya kustaajabisha na kuleta msongo wa mawazo wa muda mfupi,hujikuta katika migogoro na mara nyingi wanawake huamua kuchukua maamuzi magumu ya utoaji mimba au kuzaa na kulea peke yao.

Ikiwa wewe ni mwanaume na uko katika kipindi cha sintofahamu kuhusu mimba.

Zifuatazo ni Njia kadhaa za kukusaidia kufanya maamuzi mazuri yatakayokusaidia wewe pamoja na mwenye mimba yako.

1)KUWA MTULIVU,USICHANGANYIKIWE

Mimba isiyopangwa huleta mshtuko na hisia tofauti k**a vile hasira, usipokua makini mvurugiko huo wa hisia utakupelekea kufanya maamuzi mabaya au kuzungumza vibaya na ikakuletea athari baadae.

Hivyo basi unatakiwa kuwa mtulivu,
Tulia ujipe nafasi ya kutafakari na kuwazua k**a mtu mzima.
Epuka mambo ya kunyoosheana vidole na kumlaumu mwenzako kwasababu swala la mimba linawahusu watu wote wawili.
Hakuna mwanamke anayeweza kujipa mimba yeye mwenyewe.
Nyote wawili mlishiriki katika kupatikana Kwa mimba hiyo.
Njia bora ya kwanza Kwa ajili ya kukabiliana na hali hii ni kuamua kuwa mtulivu na kuacha kuchanganyikiwa.

Katika kipindi cha utulivu utaweza kupata mawazo bora juu ya nini kifanyike kuhusiana na mimba isiyotarajiwa.

2)YAPIME MAAMUZI YAKO

Hata k**a umechanganyikiwa na umejaa maswali mengi kuhusu mimba isiyotarajiwa.

Unapaswa kukubaliana na ukweli kuwa mimba ni yako.
Na k**a unahisi sio ya kwako basi unapaswa kupima maamuzi yako kabla ya kufanya chochote.

Kwanini unashauriwa kupima maamuzi yako?

Kwasababu maamuzi yoyote utakayofanya huwa yana matokeo mawili.

Eidha yakawa na manufaa kwako au yakawa na hasara kwako.

Jiulize yafuatayo kabla ya kuamua.

Ni,wewe ndio unatoa ridhiki kiasi unakataa mtoto asizaliwe kwasababu hauna pesa?

Unayajua madhara anayopata mwanamke kwa utoaji mimba?

Una uhakika wa kesho yako?

Hutaki kabisa kujihusisha na mtoto wako ajaye?

Una uhakika mimba sio yako umesingiziwa?

Una uhakika hutaki mtoto?

Ni kweli huhitaji kumuoa,
Je,huwezi kushirikiana na mama mtoto katika malezi?

Maswali haya yanakusaidia kupima mawazo yako dhidi ya mimba isiyotarajiwa.

Lakini pia ni vyema kujizuia kusema maneno mabaya kipindi hiki.
Ili ujipe muda wa kutosha kupata majibu sahihi.

3)SHIRIKIANA NAE,USIKIMBIE MIMBA

Pengine mmekwishatamkiana maneno mabaya baada ya kujulikana kuwa kuna mimba isiyotarajiwa,ama pengine kabla ya kugundulika kuwa kuna mimba isiyotarajiwa mlimkwazana.

Sasa haipaswi kuendelea kuwa hivyo.
Mnapaswa kushirikiana kwa amani katika uleaji wa mimba hiyo na sio lazima muishi wote ndio mshirikiane.

Inawezakana kuwa ngumu ila jitahidi kwa ajili ya mustakabali wa afya ya mtoto.

Puuzia yaliyokwishatokea iwapo mlikwazana.

Kumbuka kuwa mimba imetengenezwa na watu wawili.
Hivyo sio busara kukimbia mimba.

Shirikianeni katika utunzaji wa mimba hadi mtoto atakapozaliwa.

Zungumzeni kuhusu mipango yenu ya sasa na baadae.

Mnajiona wapi baada ya miaka kadhaa mbele?

Kitu gani mnaweza kufanya ili kusaidiana kila mmoja?

Mtamleaje mtoto?

Mnatamani mtoto aishi katika mazingira yapi?

Mtashirikiana vipi katika malezi iwapo Kila mtu atakua na mwenza mwingine bila mtoto kuathirika?

Mnapaswa kujadili wote kwa hekima na upendo,

Kumbukeni kuzaa sio uadui hivyo haipaswi kuchukiana kipindi chote cha mimba isiyotarajiwa na hata baada ya mtoto kuzaliwa.

4) JIFUNZE KATIKA HILI.

Chochote kile kitakachotokea katika kipindi cha mimba isiyotarajiwa,

Kichukulie kwa jicho la kujifunza.
Fundisho linalopatikana katika kipindi cha mimba isiyotarajiwa ni pamoja na umakini wa kujilinda na kumlinda mwanamke kupata mimba yako,

Kulipa heshima tendo la ngono kwamba halipo tu kwa ajili ya kujifurahisha bali pia tendo hilo huweza kutoa fursa ya kiumbe kuja duniani.

Halikadhalika tukio hili linakufundisha kuhusu matumizi ya njia salama ya kondomu pamoja na Njia salama za uzazi wa mpango.

Lakini pia inakupa nafasi ya kujitambua kuhusu wewe na Yale unayotamani katika maisha yako.
Kupitia kipindi hiki unajigundua k**a kweli unahitaji kuwa baba na lini unatamani kupata mtoto.
Na mambo gani unatamani kufanikisha kabla ya kupata mtoto mwingine?

Hakikisha unajifunza ili usirudie tena kosa k**a hili.

Jukumu la kujilinda na mimba isiyotarajiwa sio la mwanamke peke yake.
-----------------

Sisi,
Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.

Tunakuambia kila mimba ina haki sawa ya kuzaliwa!
Hakuna swali lenye kukosa majibu.

Tuwasiliane Whatsapp/ujumbe iwapo unahitaji ushauri au una story ya kushea na wengine kuhusu mimba.

Tupe story yako,

Je,wewe ni mtoto uliyetokana na mimba iliyotarajiwa au isiyotarajiwa?

Je, mtoto/watoto ulionao wametokana na mimba iliyotarajiwa au isiyotarajiwa?

Je,umewahi kuwa katika hali ya kuwa na ujauzito usioutarajia?

Je,una ushauri gani Kwa mtu ambaye ana ujauzito asioutarajia?

0746465095
Mkurugenzi

๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ







Niko hapa nasoma kitabu basi nimekutana na quotes kadhaa zimenitafakarisha sana.Nikiwa k**a Mkurugenzi wa Mkijacho Ni ta...
13/09/2024

Niko hapa nasoma kitabu basi nimekutana na quotes kadhaa zimenitafakarisha sana.

Nikiwa k**a Mkurugenzi wa Mkijacho

Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.
pia taasisi inatoa elimu ya ujauzito na kupinga ukatili wa utoaji ujauzito!

Nimeona nikushirikishe baadhi ya quotes tutafakari kwa pamoja.

"Any country that accepts abortion, is not teaching its people to love, but to use any violence to get what it wants." - St. Teresa of Calcutta

Tafsiri isiyo rasmi๐Ÿ‘‡

"Nchi yoyote ambayo imeruhusu utoaji wa mimba haifundishi watu wake upendo bali inafundisha watu wake kufanya vurugu kupata chochote wanachotaka" Alisema mama teresa wa calcutaโœ…โœ…โœ…

"It is a poverty to decide that a child must die so that you may live as you wish."
St. Teresa of Calcutta

Tafsiri isiyo rasmi ๐Ÿ‘‡

"Ni umaskini wa Akili kuamua mtoto kufa ili wewe uishi namna utakavyo" Alisema mama teresa wa calcuta

โœ…โœ…โœ…โœ…

Todayโ€ฆ the greatest destroyer of peace is abortionโ€ฆ because if a mother can kill her own child, what is left but for me to kill you and you to kill me โ€“ there is nothing in between. โ€
โ€“ Mother Teresa of Calcutta

Tafsiri isiyo rasmi ๐Ÿ‘‡

Leoโ€ฆ mharibifu mkuu wa amani ni utoaji wa mimbaโ€ฆ kwa sababu ikiwa mama anaweza kumuua mtoto wake mwenyewe, kilichobakia ni Mimi kukuua wewe na wewe kuniua mimi sababu hakuna utofauti wa uuaji na kutoa mimba โ€ Alisema Mama Teresa wa Calcutta โœ…โœ…โœ…

The solution [to unplanned pregnancy] is not to kill the innocent baby but to deal with the motherโ€™s values and her attitudes toward life.โ€
โ€“ Rev. Jesse Jackson,

Tafsiri isiyo rasmi ๐Ÿ‘‡

Suluhisho [la mimba isiyotarajiwa] si kumuua mtoto asiye na hatia bali kushughulika na uwezo wa mama na mitazamo yake katika maisha.โ€
โ€“ Alisema Mchungaji Jesse Jackson โœ…โœ…โœ…

The rights of children as individuals begin while yet they remain the foetus.โ€
โ€“ Victoria Woodhull,the first female presidential candidate in the United States

Tafsiri isiyo rasmi ๐Ÿ‘‡

Haki za watoto k**a watu wengine huanzia wakati bado wakiwa tumboni mwa mama zao"
-Alisema Victoria Woodhull, mgombea urais wa kwanza mwanamke nchini Marekani,
-
Victoria alimaanisha kuwa k**a zilivyo haki za binadamu karibu ulimwengu wote kuwa ni haki ya Kila binadamu kuishi ndivyo hivyo hivyo anavyopaswa kuhesabiwa mtoto aliye tumboni.

Kauli yake inathibitisha kulaani vikali utoaji wa mimba โœ…โœ… โœ…

Ndugu yangu kuna ulichojifunza hapo?

Una mtazamo gani katika swala la mimba kutolewa?

Imewahi kukuta kuwa katika hali ya kutaka kutoa mimba?.

Umewahi kutoa mimba?

Una lolote la kutuambia la kutuhusia?

Maoni yangu;
Kwa yeyote mwenye mimba na anayetamani kutoa hiyo mimba andiko hili likupe tafakari,
Tuzalie huyo mtoto,
Iko raha kubwa sana kuitwa mama!
Iko faraja kubwa sana ulimwenguni huyo mtoto kuzaliwa k**a iliwezekana mimba yake kutungwa basi upo uwezekano wa huyo mtoto kuzaliwa na akakua na akafanyika Baraka ulimwenguni.

Nakupa uzoefu wangu na uzoefu wa watu wengine kuwa wote waliowahi kutoa mimba sahivi wana majuto mnoo pia wale waliowahi kutamani kutoa mimba ila wakaishinda sauti ya uharibifu na kuamua kuzaa leo hii wanajutia kwanini walitamani kutaka kutoa mimba kwa namna watoto wao walivyoongeza thamani katika maisha yao.

PS!
Pichani ni Mimi na mtoto niliyeshinda sauti ya uharibifu kwa kuamua kumzaa.
She adds a great value to my life ๐Ÿ’ž๐Ÿ’ž

Mkurugenzi
Dr naytham hub
07467465095

SEMINA YA MALEZI YA WATOTO WANAOKOJOA KITANDANIPURPOSEFUL PARENTING ACADEMY ikishirikiana na Taasisi ya  Tunapenda kukua...
28/08/2024

SEMINA YA MALEZI YA WATOTO WANAOKOJOA KITANDANI

PURPOSEFUL PARENTING ACADEMY ikishirikiana na Taasisi ya
Tunapenda kukualika katika semina ya watoto wanaoendelea kujikojolea kitandani licha ya kuwa na umri wa miaka 6.

Semina yetu itafanyika mtandaoni Jumapili ya tarehe 8 mwezi wa 9 mwaka 2024

Mada kuu itakayozungumzwa ni yale usiyoyafahamu,nafasi ya malezi na athari zake,Nini ufanye na kipi usifanye ndani ya
MALEZI YA WATOTO WANAOKOJOA KITANDANI.

Darasa hili limeshalipiwa HAKUNA KIINGILIO

ili kujiunga โœ๏ธ

Bonyeza link

Follow this link to join my WhatsApp group: https://chat.whatsapp.com/K2rVqZdMonc4H6Wek7s6FR

Mkufunzi ni Daktari Bingwa Gladness Temu(
)

USIPANGE KUKOSA!

Imetolewa na Mkurugenzi

Dr Naytham Masoud
0746465095





TAASISI YA MKIJACHO YAUNGA MKONO JUHUDI HARAKATI ZA HEDHI SALAMAPacify pad ni taulo za k**e zilizotengenezwa kwa pamba n...
26/08/2024

TAASISI YA MKIJACHO YAUNGA MKONO JUHUDI HARAKATI ZA HEDHI SALAMA

Pacify pad ni taulo za k**e zilizotengenezwa kwa pamba na maua asilia.
Ni pedi ya maajabu kwa mwanamke kwasababu imetengenezwa na kuwekwa Anion chip katikati ambayo ni chembe hai ambazo zinatoa hewa ya oxygen pale zinapogusana na mwili wako.

Anion hizi zina uwezo wa
Kurekebisha mzunguko wa hedhi Kwa wale wenye changamoto ya mzunguko wa hedhi usioeleweka.

Vilevile pia pedi za pacify zina sifa mujarab k**a ifuatavyo.

๐Ÿ”ฅNi kubwa Ina uwezo wa kufyonza mililita 240-280
๐Ÿ”ฅImetengenezwa kwa pamba laini na imetengenezwa kiasili
๐Ÿ”ฅHuondoa maumivu ya tumbo na kiuno kipindi cha hedhi.
๐Ÿ”ฅHukomesha miwasho,uchafu ukeni,Uti sugu na fungus.
๐Ÿ”ฅ Ina harufu nzuri ya maua hivyo humfanya mwanamke kunukia wakati wote.
๐Ÿ”ฅInamuhakikishia mwanamke uhuru wakati wote atakaokuwa katika kipindi cha hedhi.

Leo rasmi Mkijacho tunazitambulisha kwenu pedi za pacify kutokea kampuni ya PacifyPads

Kuwa ni pedi Bora na salama Kwa wanawake na watoto wa k**e.

Pedi hizi zinatoa uhakika wa uhuru katika kipindi chote cha hedhi na kumuhakikishia mwanamke na mtoto wa k**e usalama wa kisaikolojia na kumuongezea hali ya kujiamini.

Kwa kushirikiana pia na taasisi ya Marm'z Relationship Hub
ambao wana mradi wa kitabu cha SHANGWE ambacho kinatoa mafunzo mengi ya kimaisha na mafunzo juu ya umuhimu wa hedhi salama ,rika na baleghe, kutambua hedhi ni nini na namna sahihi ya kujisitiri kabla ya baleghe,uthubutu na mengine mengi mazuri.

Pamoja na Elimu ya hedhi salama wanatarajia kugawa taulo za k**e maeneo yote ambayo kitabu kitafika.
Ukinunua kitabu unakua umechangia ununuzi wa taulo za k**e.

Tarehe 30 mwezi huu watakua shule ya sekondari kibasila ambapo watagawa taulo za k**e na kitabu cha SHANGWE kwa wanafunzi 200.

Kununua kitabu unalipia 10,000/= kwenda 0653544133 tigo Mariam Mbano Ukilipia toa taarifa

Pia pacify Organic Pads zinapatikana madukani kuanzia leo kwa jumla na rejareja.

Kwa habari zaidi, maswali ya bidhaa, au maombi ya sampuli, tafadhali wasiliana na:
Paulina Biseko
Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo ya Bidhaa,
PACIFY LIMITED
paulina@pacify.co.tz
0748420000

Pichani ni mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya MKIJACHO.
Dr Naytham Masoud
0746465095

TAASISI YA MKIJACHO YAHUDHURIA UZINDUZI WA TAULO MPYA ZA K**E NCHINI TANZANIATarehe 22 mwezi 8 mwaka 2024,Taasisi ya Mki...
24/08/2024

TAASISI YA MKIJACHO YAHUDHURIA UZINDUZI WA TAULO MPYA ZA K**E NCHINI TANZANIA

Tarehe 22 mwezi 8 mwaka 2024,
Taasisi ya Mkijacho ilihudhuria mkutano wa UZINDUZI WA PADS ZA PACIFY zilizozinduliwa na Muigizaji wa Filamu Tanzania Ndugu Elizabeth Michael (Lulu)

Pia tukapata nafasi ya kujifunza machache kutoka Kwa Daktari Bingwa wa wanawake ndugu Dr Jane Muzo wa Agakhan Hospital ambaye alielezea kuhusu umuhimu wa hedhi salama kwa mtoto wa k**e na madhara ya kisaikolojia anayoweza kupata mtoto wa k**e iwapo atakosa hedhi salama.

Pamoja na hayo tulijifunza kutoka kwa katibu Mkuu wa Jukwaa la Hedhi Salama Tanzania, Ndugu Severine Sylvester alitoa elimu ya hedhi salama na mchango wa wanaume katika kufanikisha hedhi kuwa salama.

Halikadhalika katika uzinduzi huu wa taulo za k**e asilia,
Ilitokea neema ya kutambulishwa kwa
Kitabu cha SHANGWE kilichoandikwa kwa ushirikiano wa waandishi watatu, ambao ni Mohammed Hammie Rajab, Mariam Mbano na Hamisi kibari wote wakiwa washindi wa tuzo mbalimbali za kitaifa na kimataifa.

Utambulisho huo pia umeweka bayana kuhusu ushirikiano wa kitabu cha SHANGWE na PACIFY ambapo tarehe 30/08/2024 kutafanyika tukio kubwa la uzinduzi likiambatana na ugawaji wa vitabu pamoja na pedi katika shule ya sekondari ya Kibasila ya jijini Dar es Salaam.

SHANGWE ni simulizi inayomhusu msichana anayeanzisha harakati za hedhi salama shuleni baada ya kupitia magumu kadhaa ni kitabu muhimu kuwa nacho.

Taasisi iliwakilishwa na Mkurugenzi mtendaji Dr Naytham Masoud ambaye anasema amefurahia sana kuwa miongoni mwa watu wachache wa kwanza wa kukisoma kitabu cha Shangwe na kuzifaham taulo za k**e ambazo zimeleta ukombozi kwa watoto wak**e.

0746465095
Mkurugenzi

๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ









Hebu leo tupige story mbili tatu ili tupate kujifunza kitu.1.Mwanaume,Ulijisikiaje mara baada ya mwanamke wako kukuambia...
23/08/2024

Hebu leo tupige story mbili tatu ili tupate kujifunza kitu.

1.Mwanaume,
Ulijisikiaje mara baada ya mwanamke wako kukuambia ana ujauzito wako?
Ulifurahia?
Ulikasirika?
Ilikuwaje?

2.Kwako mwanamke,
Siku ulipojigundua mjamzito na kumfahamisha mwanaume wako alikujibuje?
Alifurahia?
Alikasirika?

Yangu naweka kwenye comment jamani ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚.

Sisi
Mkijacho

Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.

Tunakuambia kila mimba Ina haki sawa ya kuzaliwa!
Hakuna swali lenye kukosa majibu.

Tuwasiliane Whatsapp/ujumbe iwapo unahitaji ushauri au una story ya kushea na wengine kuhusu mimba.

0746465095
Mkurugenzi

๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ







IPO SABABU YA KILA KITUDuniani,Kila jambo unaloliona linajitokeza iwe kwa uzuri au ubaya.Fahamu kuwa ipo sababu nyuma ya...
20/08/2024

IPO SABABU YA KILA KITU

Duniani,
Kila jambo unaloliona linajitokeza iwe kwa uzuri au ubaya.

Fahamu kuwa ipo sababu nyuma yake ya kutokea kwa jambo hilo,ipo sababu ya kila kitu kinachotutokea kwenye maisha yetu.

Ijapokuwa ni ngumu kwa wengi kugundua kwa haraka kuwa ipo sababu ya kila kitu kinachotutokea ndio maana huwa tunajikuta katika msongo wa mawazo na malalamiko.

Msongo wa mawazo hutupeleka mbali katika kuwaza vitu tofautitofauti na hisia mkanganyiko.

Nazungumza na mwanamke mjamzito ambaye amepata mimba bila kutarajia,(unplanned pregnancy)
Wewe kubeba ujauzito iko sababu nyuma yake.
Lipo fundisho na somo nyuma yake.
Ipo faida mbeleni ambayo Kwa sasa huenda usiione kwasababu ya mawazo uliyonayo.

Huenda ikawa ni makosa lakini huweza kuwa pia ni sababu ya kujifunza katika njia yako mwenyewe!

Katika yote,
Hebu jiruhusu kuwa mtu wa shukrani kuanzia sasa juu ya hilo unalohofia na kukosesha raha.

Tafuta namna ya kushukuru na kufurahia juu ya huo ujauzito ulionao.

Usimkatili mtoto huyo kwa mawazo ya kutoa mimba ama kutamani iharibike.

Usimkatili mtoto huyo kwa kumnyima haki yake muhimu ya kuzaliwa na kukua hapa duniani.

Sijuhi uko wapi muda huu na unawaza kitu gani,

K**a unauona huu ujumbe,

Simamisha unachofanya mshukuru Mungu na shangilia uwepo wa hiyo Baraka.

K**a hujaoga hadi muda huu tafadhali kimbilia bafuni ukaupe mwili nguvu.

K**a una nafasi ya kununua unachotaka hebu jinunulie chipsi na tunyama choma ufurahishe tumbo ndugu yangu!

Sisi
Mkijacho

Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.

Tunakuambia kila mimba Ina haki sawa ya kuzaliwa!
Hakuna swali lenye kukosa majibu.

Tuwasiliane Whatsapp/ujumbe iwapo unahitaji ushauri au una story ya kushea na wengine kuhusu mimba.

0746465095
Mkurugenzi

๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ







MIMBA ILIYOTARAJIWA NA MIMBA ISIYOTARAJIWA(PLANNED PREGNANCY VS UNPLANNED PREGNANCY)Ijapokua binadamu wote ni sawa,tunai...
20/08/2024

MIMBA ILIYOTARAJIWA NA MIMBA ISIYOTARAJIWA
(PLANNED PREGNANCY VS UNPLANNED PREGNANCY)

Ijapokua binadamu wote ni sawa,
tunaishi na kutenda sawasawa bila kujali tumetokea katika mazingira gani.
Tumetofautiana katika upatikanaji wetu,
Kuna ambao wamezaliwa Kwakuwa baba na mama waliweka kikao kujadili uwepo wao,Kisha kuna ambao wamezaliwa kwakuwa dunia ilishaamuru wawepo duniani.

Hapa ndio tunajifunza kuhusu mimba iliyotarajiwa au kupangwa (planned pregnancy)

na mimba isiyotarajiwa au kupangwa (unplanned pregnancy)

MIMBA ILIYOTARAJIWA (PLANNED PREGNANCY)

Hii ni mimba iliyopatikana baada ya maridhiano kati ya baba na mama kwa kuamua pamoja kuwa ni muda sahihi wa wao kupata mtoto iwe wako kwenye mahusiano ya kawaida au ndani ya ndoa.

Halikadhalika huweza kuwa ni mimba iliyopatikana baada ya mama kuwa tayari kupata mtoto iwe kwa njia ya kawaida ya asili au njia za kisasa za upandikizaji wa mbegu.

Mimba hii iliyotarajiwa mara nyingi huja na hisia za shangwe kutoka kwa wahusika,huonekana k**a ni jambo la ushindi mkubwa.

Naamini unaelewa kuhusu hisia inayopatikana pale unapokua umefaulu jambo lako.

Mara nyingi baada ya kuthibitika kuwa na mimba iliyotarajiwa,
Mwanamke hujaa furaha na kuwa na muhaho mkubwa (being exited) juu ya safari yake hiyo mpya ya ujauzito.

MIMBA ISIYOTARAJIWA (UNPLANNED PREGNANCY)

Hii ni mimba iliyopatikana kinyume na uhitaji wa wahusika,
Inaweza kuwa mwanamke na mwanaume wakawa kwenye mahusiano ya kawaida au mahusiano ya ndoa.
Mimba aina hii hutokea wahusika wanapofanya tendo la ndoa pasipo uwepo wa kinga ya kuzuia mimba.

Lakini pia baadhi ya wanawake hupata mimba aina hii kutokana na sababu mbalimbali.

Baadhi ya sababu hizo ikiwa ni

Kubakwa au kulazimishwa kwasababu fulani kufanya tendo la ndoa pasipo ridhaa yao,

Mfano,
Kwa upande wa wanawake wenye waume walevi na watesaji mara nyingi hulazimishwa kufanya tendo la ndoa pasipo kinga na wengine huenda mbali kuwakataza matumizi ya vidonge au njia za uzazi wa mpango.

Mimba hii isiyotarajiwa mara nyingi huja na hisia mchanganyiko ambazo ni huzuni,hofu,hasira na mawazo.

Maswali ya nizae au nitoe Huwa mengi?

Maswali ya nitawezaje kulea iwapo baba wa mtoto akikataa?

Maswali ya uchumi wangu hauko sawa itakuwaje?

Maswali ya Mimi Bado Mwanafunzi nayo Huwa hayabakii nyuma.

Maswali ya nitazaaje tena mtoto wangu Bado mdogo.

Maswali ya jamii itamchukuliaje mwanangu baada ya kusikia nimebakwa na kupata huu ujauzito?

Kwa ufupi mimba isiyotarajiwa huja na maswali mengi pamoja na Uwepo wa presha na mara nyingi baadhi ya watu huamua kutoa mimba hizo ambapo baadae hujikuta kuwa na majuto.
Kwa kukosesha haki ya kiumbe kuzaliwa au kupata madhara yaliyotokana na utoaji wa mimba hiyo.

Sisi
Mkijacho

Ni taasisi isiyo ya kiserikali inayoelimisha,kuwezesha na kutoa usaidizi wa usimamizi kwa wajawazito pamoja na watoto chini ya umri wa miaka 5.

Tunakuambia Kila mimba Ina haki sawa ya kuzaliwa!
Hakuna swali lenye kukosa majibu.

Tuwasiliane Whatsapp/ujumbe iwapo unahitaji ushauri au una story ya kushea na wengine kuhusu mimba.

Tupe story yako,

Je,wewe ni mtoto uliyetokana na mimba iliyotarajiwa au isiyotarajiwa?

Je, mtoto/watoto ulionao wametokana na mimba iliyotarajiwa au isiyotarajiwa?

Je,umewahi kuwa katika hali ya kuwa na ujauzito usioutarajia?

Je,una ushauri gani Kwa mtu ambaye ana ujauzito asioutarajia?

0746465095
Mkurugenzi

๐Ÿ‘Œ๐Ÿ‘Œ







UMEPATA UJAUZITO BILA KUTARAJIA? TUNATOA HUDUMA ZA UJAUZITO BURE!Kuna waliozaliwa kwakuwa wazazi wao walikua wamejipanga...
19/08/2024

UMEPATA UJAUZITO BILA KUTARAJIA? TUNATOA HUDUMA ZA UJAUZITO BURE!

Kuna waliozaliwa kwakuwa wazazi wao walikua wamejipanga kuhusu ujio wao,na kuwa tayari Kwa Kila kitu kuwahusu.
Yaani wameandaliwa Kila kitu kilicho ndani ya uwezo wa wazazi(Mimba zilizopangwa/Planned pregnancy)

Kisha Kuna waliozaliwa kwakuwa Dunia ilishaamuru wawepo duniani,
na wazazi hawakuwa na uchaguzi wa kutoa mimba zaidi ya kuzaa ama walijaribu kutoa mimba kwa Njia za kienyeji ikashindikana (Mimba zisizopangwa/Unplanned pregnancy)

Ipo tofauti kubwa kwa hizi mimba na hata malezi ya hao watoto watakapozaliwa kutokana na sababu mbalimbali.

Tusome simulizi ya wakili Anneth kwanza,

Anasimulia mama yake mzazi bi Flora Michael Bashungwa!

Nilitokea nyumbani kwetu karagwe na kuja jijini Dar es salaam Kufanya Kazi za ndani.
Wakati nikiishi huko nilishawishiwa kuingia katika mahusiano nikiwa na miaka 17 tu na ndugu wa familia ninayofanyia kazi.

Wakati huo niko kwenye mahusiano ya siri nikiwa sina elimu ya kutosha kuhusu ujauzito nilifanikiwa kupata mimba bila kutarajia!

Mimba imekuja kujulikana ikiwa na umri wa miezi 5 kwakuwa sikua na asili ya tumbo na pia sikua na uelewa wowote halikadhalika nilikua nikipata hedhi k**a kawaida Kila mwezi,

Ijapokua nilikua napata vihomahoma Kila ifikapo jioni ndipo boss wangu alichukua jukumu la kunipeleka hospital na kugundulika kuwa ni mjamzito.

Taharuki ilitokea Kwa muda,
Boss alihamaki nami nilistaajabu kuhusu habari za ujauzito wangu.

Wakati Kila mmoja akiwaza kuhusu hatima ya ujauzito.

Boss aliniuliza k**a nipo tayari kutoa huo ujauzito?

Tufanye Siri tutoe!....sauti ya boss ilisikika ikiungwa mkono na Daktari wa zamu.

Nilikataa niliwaambia mimi sisomi na kwa vile imeshatokea hivyo niko tayari kulea hiyo mimba na safari ya ujauzito ilianzia hapo na hatimae nilifanikiwa kupata mtoto wa k**e mzuri sana ambaye kwa Sasa ni wakili,
Ni msaada katika Maisha yangu na ya wengine wanaomzunguka,
Aneth amejaaliwa huruma na upendo wa hali ya juu sana!....

Sijuhi ingekuwaje iwapo nisingemzaa na kukubali kutoa mimba kipindi kile.

Amemalizia kusimulia bi Flora Michael Bashungwa mwanamama wa miaka 55 sasa.

Ni kawaida kuwa na hisia za kuchanganyikiwa na kukosa uhakika wa maamuzi ya kupata mtoto mara baada ya kujigundua kuwa una ujauzito usioutarajia wala kuupanga (unplanned pregnancy)

Una mimba isiyotarajiwa(isiyopangwa)
Huelewi kipi cha kufanya kwa wakati huu?
Umechanganyikiwa na kuvurugika?
Hujuhi nini cha kufanya?

Wasiliana nasi Mkijacho
Tutakusaidia kupata maamuzi sahihi,kati ya kutoa mimba au kupata mtoto.

Tuna wataalamu waliobobea katika huduma hii ambao watajibu maswali yote kuhusu ujauzito wako.

Pia tuna huduma nyingi ambazo ni suluhisho.

Tuandikie ujumbe wa kawaida au Whatsapp,
0746465095 tuweze kukupatia huduma za ushauri bure.







MAMA AKIKOSA UTULIVU WA NAFSI, MTOTO HUONEKANA MZIGOSiku kadhaa nilicomment katika post ya msanii Faiza Ally ambaye amej...
18/08/2024

MAMA AKIKOSA UTULIVU WA NAFSI, MTOTO HUONEKANA MZIGO

Siku kadhaa nilicomment katika post ya msanii Faiza Ally ambaye amejifungua hivi karibuni watoto mapacha.

Alisema anawafurahia wanae,
Nami nilicomment kuwa k**a nafsi yake Ina utulivu wa kutosha,pesa ya kula ipo,baba yupo, biashara zinaenda!

Anaanzaje kuwachukia watoto?

Ukweli wamama wote haijalishi maskini au matajiri hupenda watoto wao,

Lakini pia ukweli ni kuwa watoto huchukiwa na kuonekana mzigo kwa mama ambaye yuko katika masumbuko ya nafsi,

Moyo wake umejaa maumivu,
Ukute pia hana kipato au ajira Kwa wakati huo.
Afya mbovu,
Hana wa kumlilia akamuelewa.
Moyo wake umechoka na unatafuta pumziko.

Akili imejaa uchungu haioni Baraka wala neema mbele yake kamwe hawezi kumfurahia mtoto.

Wakati wengine hufurahia sauti za vilio za watoto wao,

Kwa mama mwenye msongo wa mawazo au maumivu ya nafsi sauti ya kilio cha mtoto huwa ni k**a mziki mbaya unaoamsha hisia za kuchanganyikiwa na kuvurugika ndio chanzo Cha watoto kufokewa bila sababu maalumu.

Watoto hugeuka mizigo na kupitia ukatili wa aina mbalimbali kwasababu ya nafsi ya mama kuwa imechoka,Ina vinyongo na maumivu ya muda mrefu yaliyokosa suluhu.

Wote waliowahi kupitia hapa najua wanaelewa hili.

Lakini pia uwepo wa changamoto mbalimbali za magonjwa ya akili nayo huwa chanzo cha watoto kufanyiwa ukatili na mama zao.

Unakuta mama mara baada ya kujifungua amepata mfadhaiko mkali wa akili au alikua na mfadhaiko mkali wa akili kipindi mjamzito.

Kwasababu ya changamoto za hisia na magonjwa ya akili kutokuonekana Kwa macho matukio haya yamekua endelevu!

Jamii imekua ikilaani matokeo bila kujishughulisha na kulaani matendo ambayo ndio chanzo cha matokeo tunayoyaona.

Nikiwa k**a daktari na mwanzilishi wa Mkijacho ambayo ni taasisi ya wajawazito na watoto.

Nalaani vikali ukatili Kwa watoto wachanga,utoaji wa mimba pamoja na kutoa rai Kwa jamii kuhusu umuhimu wa wanawake na wanaume kupata elimu ya saikolojia,kiroho, umuhimu wa watoto katika jamii, pamoja na umuhimu wa elimu ya afya ya akili Kwa wote.

Watoto ni nuru na nguvu kazi ya taifa la kesho.
Watoto ni Baraka!
Watoto ni Tunu!
Watoto huongeza ladha katika maisha ya mwanadamu ndio maana maandiko ya dini mbalimbali yanasema tuje tuzaliane na kuongezeka hapa ulimwenguni.

Lakini yote hayo ili yawe na maana ni lazima Mama ambaye ndie mtu wa kwanza kuwa na mtoto awe salama kihisia,kiroho na kiakili ili mtoto awe salama.

Halikadhalika ni muhimu pia Kwa baba kuwa salama pia kiroho na kiakili

Matukio k**a haya yataweza kuisha.
Watoto watakua salama dhidi ya ukatili.
K**a taifa tutaepukana na hizi laana za kulazimishwa!

Hatujuhi pengine huyu mtoto angekua hai huko mbeleni angekua mtu mwenye msaada eneo fulani katika taifa letu๐Ÿ˜ฅ

Dr Naytham Masoud
Mkurugenzi
Mkijacho
18/08/2024
0746465095

DSM,

Kwa wewe ambaye ni mama/baba/mama kijacho au baba kijacho.Huenda hapo ulipo kichwa kimejaa mawazo na maswali yasiyo na m...
08/04/2024

Kwa wewe ambaye ni mama/baba/mama kijacho au baba kijacho.
Huenda hapo ulipo kichwa kimejaa mawazo na maswali yasiyo na majibu.
Mengi yamezonga akili yako.
Mambo hayaendi k**a ulivyopanga ama unavyopanga!
Mambo hayawi k**a ambavyo ulikua unaota!
Umechoka sana nafsi yako.
Una hasira
Unajichukia
Una maumivu na haufurahii kuwa na watoto ama kumpokea huyo kiumbe ajaye(kijacho)

Jambo moja unalotakiwa kujikumbusha kila siku ni kwamba,

HUYO MTOTO
HAO WATOTO
HUYO KIJACHO

Hawakuomba kuzaliwa kwako,
Hawakujiamulia tu kuwemo katika maisha yako
Hawakujichagua kuwa watoto wako bali wewe umechaguliwa katika wengi,wewe ndio unapaswa kuwa mama/baba wa huyo/hao watoto.
Ulimwengu umeamua kuwa hao watoto(mtoto) lazima wawepo katika historia ya maisha yako na lipo kusudi la wao kuwemo kwenye maisha yako.

Iwe kwa wewe kukubali au kwa wewe kuendelea kukataa na kulia,

Hao watoto ni wako na hawana kosa lolote!

Shukuru kwa kukubarikiwa hao watoto!

Muda huu unaposoma ujumbe huu,
Ikiwa utakua na uchungu.
LIA!!!
GALAGALA!!!
PIGA KELELE!!!
JISEME!!!
LALAMIKA!!!

Ukishamaliza yote hayo unaweza kuingia bafuni koga maji,kisha kunywa maji.
Ukiwa karibu na hao watoto/huyo mtoto. wakumbatie waambie kuwa unawapenda sana.
K**a ni mjamzito lishike tumbo uzungumze na mtoto tumboni.

Uzoeshe na kuulazimisha moyo wako kuwapenda hao watoto.

Niamini mimi chemichemi zingine za furaha yako zimefichwa kwa hao watoto(huyo mtoto)

Haijalishi maisha ni magumu kiasi gani.

Ruhusu moyo wako kuwapenda na kuwafurahia watoto wako.

Unapaswa kuwaomba msamaha hao watoto unaowafokea bila sababu,
Unapaswa kumuomba msamaha huyo mtoto unayemchukia hali ya kuwa yuko tumboni.
Ametenda lipi?
Kosa lake ni lipi?
Amesababishaje maisha magumu,kwani hapo mwanzo ulikua tajiri?
Je,kosa lake kuzaliwa kwako?
Kati yako na huyo mtoto nani amuombe mwenzie msamaha?
Nani anayepaswa kulaumiwa?
Nani alisababisha huyo mtoto azaliwe?

Hata ukijaribu kupindisha ukweli, majibu yatabaki kuwa huyo mtoto hana kosa,wewe ndio unatakiwa kuomba msamaha kwa kumlalamikia bila sababu.

Wao wamekwishachaguliwa wawe katika historia ya maisha yako,na ipo sababu au kusudi la wao kuwepo!

Ndani ya maisha ya kila mtu lipo kusudi,
Ndani ya maisha ya kila mtu iko sababu ya kwanini imetokea kuwa hivyo.

Ndani ya taasisi yetu ya Mkijacho
Tunaamini kuwa Kila mtoto ni baraka,na tunaamini kuwa kila mtoto ni Nyota ambapo kuzaliwa kwake ni nuru na baraka kwa wengine ulimwenguni.

Kwako,
Baba/Mama.

Tunakutumia kumbatio letu ambalo ni kwa ajili ya kukupongeza na kukufariji.

Kuwa mzazi ni tunu ijapokua si kitu rahisi.

Chambilecho wahenga KULEA MIMBA SI KAZI,KAZI KULEA MWANA!

Wakubali watoto,kisha wafurahie,nao watakufurahisha!

Tunakupenda sana โค

Dr Naytham Masoud
Mkurugenzi Dr naytham hub
0746 465 095

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mkijacho posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Mkijacho:

Share