Queens Beauty Tips & Health Hacks

Queens Beauty Tips & Health Hacks Pata afya, uzuri na hacks za maisha ambazo zitabadilisha maisha yako wakati huo huo kukuokoa pesa. J

Hello Guys,k**a unasumbuliwa na stomach ulcers, acids or stomach bacteria, please contact me ASAP!. Nitakusaidia. Jiskia...
24/10/2021

Hello Guys,
k**a unasumbuliwa na stomach ulcers, acids or stomach bacteria, please contact me ASAP!. Nitakusaidia. Jiskia huru kuniuliza inbox, Ama whatsapp +255679031008.

WANAUME WANATUHITAJI. SISI WALA HATUWAHITAJI.Sisi kuumbwa na uke isingekua chaajabu bila uwepo wa wanaume. Wanaume wanah...
22/10/2021

WANAUME WANATUHITAJI. SISI WALA HATUWAHITAJI.

Sisi kuumbwa na uke isingekua chaajabu bila uwepo wa wanaume. Wanaume wanahitaji kufanya mapenzi. Wanawaza juu ya kufanya mapenzi muda wowote. Wanatamani Kufanya mapenzi k**a sisi tunavyotamaani vitu vitamu. Ndo maana wako tayari kufanya chochote kupata penzi lako. Kiasi wanacho hitaji kufanya mapenzi imekua udhaifu mkubwa kwao. Jumlisha udhaifu huo na utamu wako(uke), na utakua na silaha ya ajabu sana. Usisikie vibaya.

Hua nawao wanatuchezea hisia zetu. Nasi tunapaswa kutumia uhitaji wao wakufanya mapenzi kuwamiliki. Na sio lazima tulale nao. Hakika tunapenda kufanya mapenzi pia na tunapenda kustarehe. Ila tuwe wakweli, sio jambo la lazima kwetu ulivyo kwao. Unadhani nadanganya? Mara ngapi unaona wanawake wananunua wanaume wanaojiuza? HAIJAWAI tokea.

Unafahamu kwamba mwanaume asipo kojoa ataanza kuhis hamu inaoletwa na kutofanya tendo? Lazima akojowe ili hamu hio ishe. Anaweza kujiridhisha ila hio itamusaidia kwa muda tu, ila baada ya muda tena atajiskia hamu ya ajabu tena kufanya mapenzi. Bali sisi tunaweza kujizua kwa muda wa miezi na haitotusumbua kihivyo. Hio ndo nguvu zetu. Ila chakusikitisha wanawake wengi wanakosea na wanafanya kinyume ya ninavyosema, tunashindwa kujizuia na kuachia mapenzi kirahisi. Tunajitaftia kila aina ya sababu ili kujiaminisha kwamba ni sawa kufanya mapenzi na wanaume.

Wote naamini kunakipindi umeyapitia haya. Ila simuhukumu mtu. Bahadhi ya wanawake wanahiss kufanya mapenzi na mwanaume ndo njia yakumiliki. Wengine wanatamani kufanya mapenzi na wanaume maana wanaona wanaume mapenzi yamepamba moto na huo mtu. Anajiamisha kwamba ni sawa kukimbilia kufanya mapenzi kwasababu wote ni watu wazima na mapenzi ni ya moto. Wanawake wengine wanahiss wanaweza kumteka mwanaume kwasabau ni mafundi kitandani, kwaupumbavu unaamini huo mwanaume atakata kua na wewe milele kwasababu unajua kila aina ya style ya mapenzi na nimchafu kweli kitandani(uchafu wa ubunifu wa mapenzi). Na pia kuna wengine wanasema hua wanafanya mapenzi kujifurahisha na mwanaume hawamjali, ila wanakosa amani mwanaume asipowatafuta au asipo piga sim.

Haijalishi wewe ni mwanamke wa aina gani au mawaza yako yakoje, kufanya mapenzi na mtu unayempenda ni makosa. Mtego ni kwamba usifanye naye mapenzi. Mwanaume ukimpa kidogo atatamani zaidi, wanaume wanakutaka wakiwa hawawezi kupata, ndo uhalisia. Najua unahis huu ni ujinga na umechoka kuyasoma, unawaza kwamba "k**a tunapendana kwanini nisijiachie, kuna tatizo gani?".. Kumbuka hawa ni wanaume!

JISTILI ILI UPATE THAMANI UNAOISTAHILI.....

JINS YAKUTUMIA CHUNGU KYAKO CHA ASALI KUPATA CHOCHOTE UKITAKACHO KWA MWANAUMEWanawake wanaogundua kwamba vyungu vyao vya...
18/10/2021

JINS YAKUTUMIA CHUNGU KYAKO CHA ASALI KUPATA CHOCHOTE UKITAKACHO KWA MWANAUME

Wanawake wanaogundua kwamba vyungu vyao vya asali ni vya thamani! daima watarun dunia. Unapoanza kuheshimu na kuthamini chungu chako, wanaume watakuheshimu pia. Wanapogundua wewe ni mwanamke anayejua thamani yako, watajipanga vizuri kabla hawajakutongoza na kupa thamani yako au kuachana na wewe maana hawawezi kugaramikia. Hua nacheka kila nikisikia mwanaume wakisema, "ningekuwa msichana, ningekuwa tajiri!". Wanasema hivi kwa sababu hawajui uwezo wanawake walionao juu ya wanaume. Chochote unachokitaka unaweza kukipata, iwe mapenzi ya dhati, kujitolea juu yako, nyumba au almasi yani chochote.

JE UNAHITAJI NINI KUTOKA KWA WANAUME?
Tumia fursa hii kuandika chochote ungetaka kupata kutoka kwa mwanaume. Nini ungetamani kupata kwa wanaume ambacho hujawai kupata? ni uaminifu? zawadi? kupeleka kwenye mitoko? ndoa? heshima? pesa? au vyote hivi? nini haswa ungetamani kupata? Waza vizuri juu ya hao kabla hujaandika mahali (tutarudi kwenye list hii badaye). Chochote unachokitamani, chungu chako kati kati ya miguu chaweza kutaftia. Baada ya kuyasoma haya, utakua umejifunza namna yakutumia chungu kyako vizuri (kwa ustarabu), kuweka mahitaji yako nakuyapata vile vile ulivyo yahitaji.

BIDHAA YA MOTO
Chungu chako ni bidhaa. Wanaume wasinge gharamikia ingekua haina thamani. Chungu hichi chaweza kua cha bure au thamani ya mamilioni ya pesa. Hii haihusiani na umalaya. Hapa siwambii kwenda kujiuza. Ninachokisema ni unatakiwa uamuwe nini kamili unachokihitaji kutoka kwa wanaume (vitu kwenye list yako). Hio ndo thamani yako. Namaanisha huwezi kumkubalia mtu yoyote kabla hajatimiza thamani yako. Wakikupatia unachokihitaji hapo sasa unaweza UZA. Nikisema UZA namaanisha hapo unapoamua kumpa mwanaume moyo wako pamoja na mwiri wako. Hapo unapoamua kuingia kwenye mahusiano na mwanaume. Wanawake wenye ndoa za zisiokua na usaliti wametanguliza uaminifu na ukweli k**a thamani yao, na hawauzi kabla hawadhibitisha mwanaume ni mkweli na ni mwaminifu. Na wengine amabayo wanaume wao wana pesa na vitu vya thamani, hawauzi kabla hawajapewa thamani yao. Yani kabla hujapewa thamani yako usiuze. Usiwakubalie wanaume kwasababu wanaonyesha nia yakugharamikia upendo wako na mapenzi.

JE! UNAFAA THAMANI YAKO?
Wanawake wenye wanaume bora hawajapata hao mabwana kwa bahati, walijua thamani yao kabla na hawakuuza kabla yakupewa thamani hio. Unaweza kuuza bure au kuuza kwa thamani yoyote unayoitaka....... KAZI KWAKO.

Maada ya kesho ni WANAUME WANATUHITAJI, NA SISI WALA HATUWAHITAJI...

............JAMANI NOAMBA MSAADA! Na miaka 28, nimeolewa na kwa sasa niko na mimba ya mwanaume mwingine......Wadau, Mwan...
16/10/2021

............JAMANI NOAMBA MSAADA!
Na miaka 28, nimeolewa na kwa sasa niko na mimba ya mwanaume mwingine......

Wadau, Mwanamke huyu ambaye nimependekeza kumwita LULU amenifuta whatsapp kuniomba ushauri, nimeamua niwashirikishe ili wote tumsaidie na chakufanya... Lulu mwenye umri wa miaka 28 ni mwanamke aliyeolewa na amepata ujauzito nje ya ndoa mume wake akiwa safarini kikazi. changamoto alionayo ni kwamba hajui jins yakumwambia mume yake alieishi naye kwa takribani miaka minne sasa. Story yake ndo hii......

"Nilikutana na Michael nikiwa na miaka 17. Kwa muda wote huo alionyesha kunipenda ila wakati huo nilikua kwenye mahusiano na George ambaye alikua muhuni. Wakati Michael alikuwa muungwana, nadhani mimi nlikua navutiwa na wahuni.

Baada ya miaka ya kutendewa vibaya na George nliachana naye. Hapo ndo Michael alipoingia na kufuta machozi yangu. Upendo wake ulitulia na sikuwa na hofu yoyote k**a zamani nlivyokua na George maana Michael alikuwa mwaminifu hadi leo hii. Nahiss ndo maana namdhamini sana, alinipa utulivu wa maisha na mapenzi.

Labda hio ndo ilikua chanzo cha shida. Wakati Michael ndo mtu anayenifaa, nilikua natamani msisimko ya kuishi vibaya, na Michael wangu mpendwa ni kinyume kabisa. Anaishi maisha yake kwa kuzingatia ratiba madhubuti, maisha ninayo yatamani yangekua hayanibowi kupita kiasi.

Mwezi wa tatu, Michael alipata safari ya kikazi kwenda kuwendeleza masomo, kozi ya mwaka ila anarudi week ya christmas. Sikujali kwa sababu sikua mgeni wa safari zake ndefu zakikazi ila nyingi zilikua za hapa Africa.

Baada ya Michael kusafiri, niliamua kwenda na marafiki wachache out nakujiachia kidogo Zanzibar. Rafiki yangu mmoja alikuwa akitembea na kaka yake George, kwa hivyo haikunishangaza kumkuta George kwenye kundi la watu waliejumwika nasi kwenye mtoko huu.

Nahivyo wote tulikua watu wazima wakujielewa na yaliopita yalipita tukakubali, LAKINI DAAH. Usiku huo ulikua mtamu sana na ulionekana kudumu milele maana tulikua tunaruka bar kwa bar huku tukijipatia mashoti ya tequila na kujiachia kweli kweli hadi ilifika hatua sikuweza kutembea bila msaada.

Hizi ndo zilikua siku nlizozizoea kabla sijaolewa na Michael mume wangu na kutulia, na japo nlikua napenda amani, nlitamani maisha yangu ya zamani ya mitoko. Nlivyo zinduka asubui nliamka kifuani mwa George, kwenye chumba ambacho sikumbuki kuingia. Chakushangaza kilikua nichumba cha George na tulikua tuko uchi wa myama.

Huku nikijiskia kutapika na kuyajutia yaliotokea, nlichukua vitu vyangu haraka huku naapa kutowasiliana na George tena. ili nifupishe story ndefu, baada ya week mbili, ghafla nliskia hamu yakutapika. Hapo hapo moyo wangu ulinichoma huku nawaza dalili za mimba ila nikajiaminisha kwamba sio kweli. Nlivyo zidiwa na mawazo ya kuhiss mimba, nikaamua kwenda kwa doctor wetu aliethibitisha wasi wasi yangu.

Kwa sasa niko na mimba ya mwanaume mwingine na mume wangu hayupo nchini. Ghafla nahiss yote nliojenga na Michael naenda kuyapoteza akirudi na sijui jins yakumwambia ukweli maana sitaki kumpoteza na namuhitaji sana...

Jamani nisaidie chakufanya.

Wadau ndo hali hio mwenzetu Lulu anapitia naomba tumshauri vizuri maana yupo anatasoma comment zenu.

.............JINS YAKUJUA MWANAUME ANAKUPENDA........... mwanaume akiwa anakupenda, ataanza yeye kukufuata. Asipo fanya ...
15/10/2021

.............JINS YAKUJUA MWANAUME ANAKUPENDA...........

mwanaume akiwa anakupenda, ataanza yeye kukufuata. Asipo fanya hivyo, basi hakupendi. Hakuna visingizio. Usifuate wanaume. Dhibiti hisia hizo ambazo zinakuhimiza kufuata wanaume. Ni sawa kutaniana, ila usimtongoze. Ndio, hata akiwa ana aibu, hata akiwa hajui kwamba unampenda. Akiwa anakupenda, atakupigia au atakutafuta kwa njia yoyote. Akiwa hajaweka aina yoyote ya juhudi kupata, ichukue k**a ishara kwamba havutiwi na wewe.

Kumbuka pia kuwa mvumilivu kidogo. Inaweza kumchukulia muda mrefu kidogo kukwambia hisia zake, kuliko muda ambayo wewe ungemwambia ila ilvyo, usisubutu. Wanaume hufanya kazi kwa wakati wao na hii inaweza ikawa na sababu mbali mbali ila mara nyingi ni kwa sababu wanaogopa kukataliwa. Sababu nyingine ni kwamba hawatambui kuwa tunapatikana au tuko single. Ndio maana kutaniana ni vizuri. Inampa ishara kwamba una nia na umevutiwa kwake. Sababu nyingine ni kwamba wanakuogopa. Mpe nafasi kujenga ujasiri wa kukukaribia. Usikate tamaa akiwa hajakupa ishara yoyote. Kutaniana kidogo na uvumilivu utakupa utakupa subira kuliko kumfungukia wewe.

Mbali na hayo, akiwa hajakufuata basi jua hakupendi; na utakua umegundua hii bila aibu ya kukataliwa. Wanawake hawapaswi kulazimika kuweka bidii sana kupata usikivu ya mwanaume. Akiwa hajakutafuta kwa namna yoyote basi achana naye. Hakupendi, au yeye ni shoga tu maana siku hizi ndo wenzetu hao.

Hapa ni sababu tatu kwanini ni Muhimu ku kuzuia hisia zako wakati uko na umpendaye au mwanzo wa mahusiano mapya;

Sababu # 1:
Wanaume wanachukia wakishindwa kusoma hisia zetu. Ukiwa unadhibiti hisia zako kwa mwanaume mpya, unamfanya ajiulize k**a unampenda au la. Akitatanishwa na kupata jibu hilo, itamfanya aongeze bidii juu yako. Ghafla, atakuwa yeye ndo anayepiga simu na kutuma message k**a mwehu. Yeye ndiye atakayekufuata, badala ya kinyume yake.

Sababu # 2:
Wanaume wanavutiwa na wewe tu wakijua hautaki. Wanaume wameumbwa kuwinda na sisi wanawake ni moja ya vitu wanavyopenda kuwinda. Najua utakua umesikia hili hapo awali na labda unafikiria ni michezo wa kijinga kijinga tu ila ndo walivyo. Kwetu, ni ujinga kwa sababu sisi ni wanawake, akili zetu ni tofauti. Tunafikiria, "hey, ukiwa unanipenda, basi kua nami. "Wanaume sio hivyo. Wanaume wanataka kuwinda. Raha ya uwindaji huo kunamfanya mwaname avutiwe haraka na wewe kuliko kumpigia na kuacha maoni mazuri na ma like kibao kwenye ukurasa wake wa Facebook. Ndivyo ilivyo. Ukikubali haya mapema, bora kwako. Taniana naye, lakini udhibiti hamu yako ya kumfuata maana akiwa anakupenda, hakika atakufuata.

Sababu # 3:
Ni wapumbavu tu wanaokimbilia mapenzi. K**a wanawake, tunavutiwa na vitu vidogo sana. Usiwe mwepesi sana kumpenda mtu mpya, haswa ukiwa kwenye mkutano wenu wa kwanza. Dhibiti hisia hizo za furaha zinazokuja kwa urahisi sana mwanzoni mwa mahusiano. Usiende kwenye date moja au mbili na unza kupata hisia kwake au kuanza kufikiria yeye beberu wa ndoto zako. Punguza mwendo. Kujidhibiti na ujifanye mgumu kugongwa maana ndo anachokitaka tu, kufanya mapenzi na wewe.

Mafunzo: Haijalishi ni ugumu gani mwanaume anapitia kupata asali, ugumu huo ndo humfanya kua na bidi maana anajua mwisho wake ni utamu tupu. Wanaume wanapenda vitu adimu na vitu adimu ndo hivyo vigumu kupata na moja ya hivyo vitu in sisi wanawake. Ukiwa mgumu kupatikana basi na thamani yako huongezeka.

J3 tutajifunza jinsi yakutumia Vyungu vyetu vya asali kupata chochote kwa mwanaume yoyote.

.......... FAHAMU NGUVU ZA UKE............UKIFUATILIA MAFUNZO HAYA UNAWEZA KUJUWA NA KUEPUKA MAHUSIANO YASOKUWA NA MAANA...
14/10/2021

.......... FAHAMU NGUVU ZA UKE............

UKIFUATILIA MAFUNZO HAYA UNAWEZA KUJUWA NA KUEPUKA
MAHUSIANO YASOKUWA NA MAANA KWAKO NA KUJUWA YUPI NI.
MWANAUME WA NDOTO ZAKO..YANIIIII CHAGUO LAKO SAHIHI😍😍😍💏

Kila mwanamke ana uwezo wa kufanya hili kutokea. Haijalishi uko je! bonge, mfupi,mrefu, mweusi au mweupe. Unaweza kuwa binti wa miaka 18, au mama wa 45. kwa chochote unachopitia, acha nikwambie kitu, una uwezo ndani yako kubadilisha kabisa matokeo yako na wanaume.

1........JINSI YA KUZUIYA HISIA ZAKO😂

Huu ni upungufu wa kwanza kwa sababu itakuwa ngumu kujifunza, lakini pia itakuwa moja ya masomo yako makubwa. Kujifunza kutumia nguvu ya kudhibiti hisia zako kunaweza kuwa changamoto yako kubwa kwa sababu inakulazimisha kwenda kinyume na kile unachopenda kufanya, ambacho ni cha kihemko.

Wanaume ni viumbe vya ngono kwa asili na wanawake ni viumbe vya kihemko kwa asili. Ndivyo ilivyo. Haijalishi kabila yako, tamaduni, umri, nchi ya asili, au kiwango cha elimu. Haijalishi, Mwanamke ni mwanamke. Sisi sote ni tofauti, lakini ndani tunafanya kazi sawa. Sisi ni viumbe vya kihemko na hatuwezi kukataa hiyo.

Tunafikiria na mioyo yetu na tunachukua hatua juu ya mhemko. Ni sehemu ya asili na ya kawaida kabisa kuwa ya k**e. Ni hi hufanya sisi kua akina MAMA wa nguvu. Inatuwezesha kutunza wale tunaowapenda bila juhudi. Sisi ni mafundi wa kuzaliwa wa asili. Itakuwa kazi ngumu kujaribu kudhibiti kile kinachokuja kawaida(naturally), lakini tunaweza kufuka au kujibadilisha. Lazima tubadilike tukitaka kuwapiga wanaume kwenye mchezo wao wenyewe. Lazima ujifunze kudhibiti hisia zako.

Hili ndo jambo...Hakuna kitu kibaya kabisa na kuwa mhemko au hisia. Ni kawaida. Tunahitaji tu kutambua faida kubwa ya kujua wakati wa kushikilia hisia na wakati wa kuziacha. Sio lazima kuzidisha sana na kua mtu mbaya kwa wanaume bali Ni muhimu, hata hivyo, kufahamu hisia zako na uwezo wako wa kudhibiti vitendo vyako. Mara tu tunapofahamu ukweli huu, basi tunaweza kudhibiti matendo yetu kwa kudhibiti hisia zetu.

Unapojua uwezo wa kudhibiti hisia zako, unachukua nguvu ya mwanaume juu yako. Wakati inaweza kuwa "vibaya" kitaalam kufunga na kudhibiti hisia zako kwa faida yako mwenyewe ya ubinafsi, ni lazima tu ukubali ili kushinda mchezo. Kwa maoni yangu hakuna kitu kibaya na aina hii ya mawazo ya "kuficha hisia zako", kwa sababu ukiwa unafikiria juu yake, wanaume hutufanyia wakati wote!

Tumezoea tabia zao za uwongo, za kudanganywa, za kiumbwa ambazo tumekuwa tukizijua na kuzoea. Tunadhani ni "vibaya" kwamba wanatuchezea, lakini hiyo haituzuii kutumbukizwa kwenye mitego yao mara baada ya muda. Kwa hivyo, ikiwa ni mbaya au sawa, lazima ubadilishe ubadilishaji wa kihemko au hisia zako juu ya wanaume.

MAFUNZO: Sisi wanawake ni wa thamani zaidi tukidhibiti hisia zetu haswa mbele ya wanaume unayempenda kiukweli. wanapogundua kuwa sisi ni dhaifu kihemko kwao, wanatumia hisia hizi kutudhibiti na kabla hujakaa sawa umepoteza udhibiti wa mtu wako na kutumika k**a anavyotaka. Tunayo nguvu na ipo ndani yetu, tunachohitaji kufanya ni kujifunza kudhibiti hisia zetu.

Kesho tutajifunza jins yakujua Mwanaume anakutaka au Kupenda.

Tunasuka Rasta aina zote, karibuni wateja wetu, utapata huduma nzuri %100 maana mteja kwetu ni mfalme ...Fanya booking y...
13/04/2020

Tunasuka Rasta aina zote, karibuni wateja wetu, utapata huduma nzuri %100 maana mteja kwetu ni mfalme ...
Fanya booking yako sasa kwa huduma utakayo ridhika nayo👌

Queens Beauty Spa Salasala. Makao ya urembo....
13/04/2020

Queens Beauty Spa Salasala. Makao ya urembo....

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam
0255

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Queens Beauty Tips & Health Hacks posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Queens Beauty Tips & Health Hacks:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram