Veriafya

Veriafya Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Veriafya, Dar es Salaam.

Si salama kwa mtoto kupigwa busu na kila Mtu hasa watu wa nje kwa sababu kuna hatari ya kuambukizwa Magonjwa yanayoenezw...
13/04/2026

Si salama kwa mtoto kupigwa busu na kila Mtu hasa watu wa nje kwa sababu kuna hatari ya kuambukizwa Magonjwa yanayoenezwa kupitia mate na ngozi. Magonjwa k**a vile mafua, virusi vya herpes (HSV-1) vinavyosababisha vidonda mdomoni, na maambukizi ya Bakteria k**a Streptococcus yanaweza kupitishwa kwa mtoto kupitia busu.

Mtoto mchanga ana kinga dhaifu, hivyo maambukizi yanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha matatizo makubwa ya kiafya. Hii ni kutokana pia na ukweli kwamba ni ngumu kufahamu anayembusu Mwanao katoka kufanya jambo gani kabla ya hapo.

Ili kumlinda mtoto, ni vyema kuwaeleza watu waepuke kumbusu na kuhakikisha mikono yao ni safi kabla ya kumshika. Pia, mzazi au mlezi anapaswa kuwa makini na dalili zozote za maambukizi kwa mtoto na kumpeleka hospitalini inapobidi.

12/04/2026

Mtoto akizaliwa na Makengeza awahishwe kwa Daktari Bingwa wa Macho kwasababu ni moja ya dalili anaweza kuwa na Saratani ya Macho

Dkt. Catherine Makunja,
Bingwa wa Magonjwa ya Macho kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Mloganzila

Video: MNH-Mlongazila TV

Kulia bila sababu, Chuki na Hasira ni hisia za kawaida wakati wa Ujauzito kutokana na mabadiliko ya homoni, hasa za Estr...
12/04/2026

Kulia bila sababu, Chuki na Hasira ni hisia za kawaida wakati wa Ujauzito kutokana na mabadiliko ya homoni, hasa za Estrogen na Progesterone ambazo huathiri hisia na mhemko wa Mjamzito.

Mabadiliko haya yanaweza kusababisha Mjamzito kuwa na hisia kali, mabadiliko ya ghafla ya mhemko na hata kuongezeka kwa mfadhaiko au wasiwasi. Pia, mambo k**a uchovu, maumivu ya mwili, wasiwasi kuhusu kujifungua, na mabadiliko ya maisha yanaweza kuchangia hisia hizi.

Ingawa ni kawaida, hisia kali za Huzuni, Hasira au Chuki zinazoendelea kwa muda mrefu zinaweza kuwa ishara ya Sonona ya Ujauzito (Prenatal Depression) au Msongo wa Mawazo, hivyo ni muhimu kupata msaada wa mtaalamu wa afya endapo zinakuwa nzito au zinaathiri maisha ya kila siku.

Wagonjwa wa Figo wanapaswa kuepuka kunywa madafu kwasababu yana kiwango kikubwa cha chumvi za Potassium ambacho kinaweza...
12/04/2026

Wagonjwa wa Figo wanapaswa kuepuka kunywa madafu kwasababu yana kiwango kikubwa cha chumvi za Potassium ambacho kinaweza kusababisha matatizo ya Moyo kwakuwa figo haziwezi kuiondoa mwilini. Pia, yana maji mengi ambayo yanaweza kuzidisha tatizo la kuvimba kwa mwili na kuongeza Shinikizo la Damu.

Zaidi ya hayo, madafu yana sukari asilia ambayo inaweza kuongeza ukubwa wa tatizo kwa wagonjwa Kisukari. Hivyo muhimu kuepuka kunywa Maji haya ili kujiweka Salama.

Asubuhi sana (Alfajiri), mwili wako huwa katika hali ya Joto la chini baada ya Usingizi.Japo si mara zote, Ukioga maji y...
11/04/2026

Asubuhi sana (Alfajiri), mwili wako huwa katika hali ya Joto la chini baada ya Usingizi.

Japo si mara zote, Ukioga maji ya baridi na kuanzia Kichwani kunaweza kusababisha kusinyaa ghafla kwa Mishipa ya Damu, jambo linaloweza kupunguza mtiririko wa damu kwenda kwenye Ubongo na kusababisha Kizunguzungu, Kudondoka au hata kupoteza fahamu kwa muda mfupi

Inashauriwa kuanza kwa kumwagia maji kwenye miguu na mikono ili mwili upate muda wa kuzoea halijoto ya maji kabla ya kulowesha Kichwa.

11/04/2026

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi aliyasema haya Machi 2, 2026 kwenye Busati la Msikiti wa Mtoro

Video: Dua TV

11/04/2026

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tohara husaidia kupunguza nafasi ya Mwanaume kupata maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) kwa 60% hivyo ni muhimu kwa Wanaume kupata huduma hii, pia kutahiri Watoto ili kuwalinda mapema dhidi ya maradhi haya pindi watakapokuwa Watu wazima.

Video hii ni kumbukumbu ya hoja ya aliyekuwa Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji, aliyoitoa Bungeni Septemba 12, 2017 akiwaomba Wabunge Wanawake kutoa ushahidi juu ya umahiri wa Wanaume waliofanyiwa Tohara.

Wazazi wengi hufikiri kuwa kulinganisha watoto wao na wengine kunawatia motisha, lakini ukweli ni kwamba hili linajenga ...
11/04/2026

Wazazi wengi hufikiri kuwa kulinganisha watoto wao na wengine kunawatia motisha, lakini ukweli ni kwamba hili linajenga shinikizo na kupunguza kujiamini kwao.

Kila mtoto ni wa kipekee na ana kasi yake ya ukuaji na maendeleo. Mathalani, si watoto wote wa umri unaofanana wataanza kutambaa, kuota meno au hata kuzungumza kwa pamoja. Hii ni kawaida kabisa, watoto hawafanani.

Badala ya kumlinganisha, mtie moyo na msapoti katika safari yake ya kujifunza na kukua. Mtoto mwenye kujiamini hujifunza kwa urahisi na hukua akiwa na mtazamo chanya maishani.

10/04/2026

Takwimu hizi zimewasilishwa leo Bungeni, Aprili 10, 2026 na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Frolence Samizi wakati wa kipindi cha Maswali na majibu huku akienda mbali zaidi kwa kutaja mikoa ya Katavi, Rukwa, Kigoma na Geita kuwa miongoni mwa vinara wa Maambukizi.

Kwa kiwango kikubwa, Ugonjwa wa Homa ya Ini hasa aina B huambukizwa kwa njia zinazofanana na zile zinazoambukiza VVU hivyo ni muhimu kuchukua tahadhari kujilinda, ikiwemo kupata Chanjo sahihi.

10/04/2026

Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku Musukuma aliyasema haya Mei 14, 2024 akichangia mojawapo ya Mijadala Bungeni ambapo alimshauri Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi aone namna njema ya kutoa mafunzo yake ya elimu ya afya kwani baadhi ya watu wanatoka vijijini ambapo kazi hazifanani na wale wanaokaa mijini, akitolea mfano wa Majiji ya Dar es Salaam na Arusha.

Nini maoni yako?

Kunyoa nywele za sehemu za siri kabla ya Hedhi ni uamuzi wa mtu binafsi, lakini kuna faida kadhaa za kiafya na za usafi ...
10/04/2026

Kunyoa nywele za sehemu za siri kabla ya Hedhi ni uamuzi wa mtu binafsi, lakini kuna faida kadhaa za kiafya na za usafi zinazoweza kuzingatiwa. Moja ya faida kuu ni kudumisha usafi kwani nywele ndefu zinaweza kushikilia damu na kuongeza hatari ya harufu mbaya. Pia, kupunguza nywele kunaweza kusaidia kupunguza unyevunyevu mwingi na kufanya mtu ajisikie safi zaidi katika kipindi hicho.

Hata hivyo, ni muhimu kuchukua tahadhari unapoamua kunyoa. Kunyoa kwa haraka au kutumia vifaa visivyo safi kunaweza kusababisha mikwaruzo au michubuko ambayo inaweza kuongeza hatari ya maambukizi.

Inashauriwa kutumia wembe safi au mashine ya umeme, na baada ya kunyoa, kupaka mafuta ya asili k**a vile mafuta ya N**i au Aloe vera ili kuzuia muwasho na kuwashwa. Ikiwa una ngozi yenye Mzio au umewahi kupata vipele baada ya kunyoa, unaweza kuzingatia kupunguza nywele kwa mkasi badala ya kunyoa kabisa.

09/04/2026

Daktari Bingwa Bobezi wa Magonjwa ya Figo kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Garvin Kweka aliyasema haya Jul 4, 2025, kwenye kilele cha Maadhimisho ya miaka 10 ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi yaliyofanyika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius K. Nyerere (JNICC)

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram