Veriafya

Veriafya Taarifa za afya zilizothibitishwa, rahisi na zinazoeleweka

01/03/2026

Bakteria wanaotoka kwenye sehemu ya Haja Kubwa wanaweza kuwa Chanzo cha Mtu kuugua Ugonjwa wa UTI mara kwa mara.

Sikiliza ufafanuzi wa Dkt. Ikrah Abdallah, Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Hospital ya Rufaa ya Mkoa Temeke alioutoa kupitia Kituo cha Redio Clouds FM

01/03/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi alizungumza haya kupitia Upendo Media.

Ushauri huu unaweza kufaa kwa Watu wanaohangaika kufanya 'Diet' bila kuelewa njia sahihi na Muongozo wa kufuata. Msikikize akifafanua kwa undani zaidi

01/03/2026

Matumizi mabaya ya Dawa za Kutuliza Maumivu huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa Figo.

Pia, tafiti za afya zimebainisha uhusika wake katika kusababisha vidonda vya tumbo.

Tutumie dawa hizi kwa Uangalifu.

28/02/2026

Mwanamke anapofikisha miaka 35 anashauriwa kukoma kushika Ujauzito ili kumuepusha na changamoto mbalimbali za Uzazi

Fuatana na Zuhura Mbuguni, Kaimu Mratibu wa Uzazi wa Mpango Taifa, kutoka Wizara ya Afya kitengo cha Afya ya Uzazi na Mtoto akifafanua swala hili kupitia Elimu ya Afya Online TV

28/02/2026

⚠️🛑🔴⛔HATARI: AZUMA si dawa sahihi kutibu ugonjwa wa UTI na Magonjwa mengine ya Zinaa. Acha kuitumia vibaya

28/02/2026

Epuka Matumizi makubwa ya Chumvi, yanaweza kusababisha upate Shinikizo la Juu la Damu pia ni chanzo cha magonjwa mengine yasiyo ya Kuambukiza

VIDEO: Muhimbili TV

28/02/2026

Unywaji wa Maji husaidia kuondoa Vijidudu vya UTI Mwilini

Fuatana na Dkt. Ikrah Abdallah, Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Hospital ya Rufaa ya Mkoa Temeke akifafanua suala hili kwa undani kupitia Kituo cha Redio Clouds FM

28/02/2026

Watu wenye vidonda vya tumbo hawashauriwi kutumia Soda na Energy Drinks kwani huongeza ukubwa wa Tatizo

28/02/2026

Kwa siku, binadamu anashauriwa kunywa lita 2–3 za maji ili kusaidia mwili kufanya kazi vizuri. Kunywa maji ya kutosha hulinda figo kwa kusaidia kuchuja taka mwilini kwa ufanisi, kupunguza hatari ya mawe kwenye figo, na kuweka mkojo ukiwa safi ili kuzuia maambukizi ya njia ya mkojo (UTI).

Pia, maji husaidia kudhibiti joto la mwili, kuboresha mmeng’enyo wa Chakula, kulainisha ngozi, kuongeza kiwango cha nishati, na kuwezesha mzunguko mzuri wa damu.

VIDEO: Muhimbili TV

28/02/2026

Unatumia muda gani kubadili pampasi za watoto? Unajua kwamba usipobadili kwa wakati no chanzo cha wao kuugua UTI?

Sikiliza ufafanuzi huu wa kitaalamu, na share video hii kwa wazazi wengi ili waelewe!

27/02/2026

Ukifunga Chakula, Fikra zako zinakuwa bora zaidi, uwezo wako wa kufanya Mambo unaongezeka

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akizungumza kupitia Upendo Media

27/02/2026

Tabia ya kutokwenda Haja Ndogo kwa wakati, pamoja na Kutokunywa maji mengi huchangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa UTI

Fuatana na Dkt. Ikrah Abdallah, Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Hospital ya Rufaa ya Mkoa Temeke akifafanua suala hili kwa undani kupitia Kituo cha Redio Clouds FM

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram