Veriafya

Veriafya Taarifa za afya zilizothibitishwa, rahisi na zinazoeleweka

12/01/2026

Nursemaid’s Elbow ni jeraha dogo linalotokea mara nyingi kwa watoto wadogo (hasa chini ya miaka 5) pale mkono unapovutwa kwa nguvu ghafla. Mfano, kumvuta mtoto kwa mkono ili asidondoke, kumuinua kwa mkono mmoja, au kucheza kwa kumzungusha kwa mikono.

Hali hii husababisha mfupa mdogo wa kiwiko kutoka kidogo mahali pake, hivyo mtoto huhisi maumivu na kushindwa kuutumia mkono huo. Mtoto anaweza kuushikilia mkono chini na kulia.

Wazazi na Walezi mnashauriwa kuepuka kumbeba Mtoto kwa utaratibu huu, ni vyema kutumia Mikono yote miwili ili kumlinda.

VIDEO: Mtandao

Kula kachumbari ovyo kunaweza kusababisha Homa ya Matumbo (Typhoid). Hii ni kwa sababu Kachumbari isiyoandaliwa kwenye M...
12/01/2026

Kula kachumbari ovyo kunaweza kusababisha Homa ya Matumbo (Typhoid). Hii ni kwa sababu Kachumbari isiyoandaliwa kwenye Mazingira ya usafi inaweza kuwa na Bakteria, Virusi au vijidudu vingine vinavyosababisha Maambukizi ya tumbo.

Hatari huongezeka pale inapoliwa bila kuosha mikono, vyombo au bila kuhifadhiwa katika Mazingira safi.

Hakikisha nyanya zinazotengeneza kachumbari zimesafishwa vizuri, imeandaliwa kwa kuzingatia usafi, na mikono yako iko safi kabla ya kula. Epuka kula ovyo au kutoka kwenye chanzo kisicho salama.

Mtoto kupiga kwikwi ni jambo la kawaida na mara nyingi si hatari, hutokea kwa sababu misuli ya kupumua (Diaphragm) ya mt...
11/01/2026

Mtoto kupiga kwikwi ni jambo la kawaida na mara nyingi si hatari, hutokea kwa sababu misuli ya kupumua (Diaphragm) ya mtoto huwa bado haijakomaa vizuri, hasa katika miezi ya mwanzo ya maisha.

Mara nyingi kwikwi husababishwa na mtoto kunyonya haraka, kushiba kupita kiasi, kumeza hewa wakati wa kunyonya, au mabadiliko ya ghafla ya joto. Hali hii kwa kawaida haimsababishii maumivu wala usumbufu mkubwa.

Kwa kawaida, kwikwi huisha yenyewe bila dawa wala matibabu maalum. Mzazi anaweza kumsaidia mtoto kwa kumnyonyesha polepole, kumpa maji kidogo k**a kafikisha umri wa miezi 6, kuhakikisha anacheua baada ya kunyonya, na kumweka katika mkao wa wima kwa dakika chache.

11/01/2026

Matumizi ya Bangi na Dawa za Kulevya humpa mhusika Nguvu za Kushiriki Tendo la ndoa kwa muda mfupi na huonekana kuwa na faida lakini baada ya muda mrefu huacha madhara ya kudumu kiasi cha Kumaliza Nguvu za Kiume na kuondoa uwezo wa Mbegu za Kiume kwenye Kutungisha Ujauzito.

Dkt. Peter Mfisi
Kutoka Mamlaka ya Kudhibiti dawa za kulevya

Video: Elimu Ya Afya Online TV

Zhanna Samsonova, mshawishi wa Mitandao ya kijamii mwenye umri wa miaka 39 anayejulikana k**a Zhanna D’Art, alifariki du...
10/01/2026

Zhanna Samsonova, mshawishi wa Mitandao ya kijamii mwenye umri wa miaka 39 anayejulikana k**a Zhanna D’Art, alifariki dunia mwaka 2023 baada ya miaka kadhaa ya kufuata misimamo mikali ya lishe akiishi kwa kula vyakula vichache sana, hususan matunda, majani ya mbegu zinazoota na juisi, jambo lililozua mjadala mpana kuhusu usalama wa lishe za kupitiliza.

Kwa mujibu wa taarifa za familia na ripoti za vyombo vya habari, Zhanna alionekana kudhoofika sana kiafya kabla ya kifo chake na alifariki kwa maambukizi makali, sababu ikidaiwa kuwa ni Mwili ulipungukiwa virutubisho muhimu

Kisa hiki kinaibua mjadala mpana wa afya ya umma kuhusu hatari za lishe kali zisizo na uwiano. Kula matunda pekee hukosa virutubisho muhimu k**a Protini, Vitamin B12, Calcium na baadhi ya madini, ambavyo ni muhimu kwa misuli, kinga ya mwili na afya kwa ujumla.

Afya bora haihusiani na kula chakula “Cha asili” pekee, bali inahitaji lishe yenye mchanganyiko sahihi wa virutubisho kulingana na mahitaji ya Mwili.

10/01/2026

Vyakula vya kuepukwa kwa watu wenye Vidonda vya tumbo ni vyakula vyenye Asidi nyingi mfano Matunda k**a Machungwa Malimao, vyakula vyenye mafuta mengi au vilivyopikwa kwenye mafuta mengi, Chai ya tangawizi kali au yenye majani makali, vinywaji k**a Soda na 'Energy Drinks'.

Pia waepuke Msongo wa Mawazo, kulala tu mara baada ya kula na kutumia dawa bila ushauri wa Daktari.

Careen Mageyema
Mratibu na Msimamizi wa masuala ya lishe.
Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi

Video: Katavi RRH

Busu linaweza kuonekana k**a ishara ya upendo, lakini kwa mtoto mchanga linaweza kuwa hatari.Watoto wachanga wana kinga ...
10/01/2026

Busu linaweza kuonekana k**a ishara ya upendo, lakini kwa mtoto mchanga linaweza kuwa hatari.

Watoto wachanga wana kinga dhaifu, hivyo wanaweza kuambukizwa kwa urahisi vimelea k**a Virusi, mafua, au bakteria wengine kutoka kwa watu wazima hata k**a mtu hana dalili zozote.

Njia salama ni kuwaomba wageni wamwangalie tu mtoto, wamsalimie kwa mbali, au wamguse kwa mikono safi, bila kumbusu. Hatua hii ndogo inaweza kusaidia kumlinda mtoto dhidi ya maambukizi hatarishi katika wiki na miezi ya mwanzo ya maisha.

Mamlaka ya Dawa nchini Uganda (NDA) imethibitisha matumizi ya Lenacapavir, dawa mpya ya kuzuia Maambukizi ya Virusi vya ...
10/01/2026

Mamlaka ya Dawa nchini Uganda (NDA) imethibitisha matumizi ya Lenacapavir, dawa mpya ya kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, inayotolewa mara mbili kwa mwaka kupitia sindano, ikiwa pia na maudhi machache kuliko Vidonge.

Kwa mujibu wa Mamlaka hiyo, Dawa hii itasaidia kupunguza maambukizi mapya ya VVU, hasa kwa vijana na makundi yaliyo hatarini na taarifa za Kimaabara zinaonesha kuwa ni salama na yenye ufanisi mkubwa.

Hii ni hatua muhimu kwa Uganda katika kupambana na Maambukizi ya VVU na kuelekea malengo ya kimataifa ya kumaliza Ugonjwa wa UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

09/01/2026

Visababishi vya Saratani ya Mlango wa Kizazi ni hivi vifuatavyo; kuanza kujamiana katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi au kubadilisha wapenzi mara kwa mara, kuzaa watoto wengi na Uvutaji wa sigara

Rehema Eliraha
Mtoa Huduma, Marie Stopes

VIDEO: Afya Talk TV

Kitaalamu, inashauriwa Mtoto Mchanga alazwe Chali (Kwa Mgongo) ili kuepusha asipatwe na Kifo cha Ghalfa.Wazazi wengi huw...
09/01/2026

Kitaalamu, inashauriwa Mtoto Mchanga alazwe Chali (Kwa Mgongo) ili kuepusha asipatwe na Kifo cha Ghalfa.

Wazazi wengi huwa na wasiwasi kuwa kumlaza mtoto chali kunaweza kusababisha apaliwe kwa kumeza makohozi au mabaki ya vitu anavyo cheua. Kisayansi, jambo hili ni gumu kutokea kwani mfumo wa mwili umetengenezwa kwa namna inayoruhusu Mtoto kumeza kila anachotoa kirahisi pasipo Kumpalia au Kumdhuru.

Kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika kwa miaka mingi, Mtoto aliyelalia mgongo huwa na uwezo mkubwa zaidi wa kuepuka hatari ya kupaliwa kuliko yule aliyelalia tumbo kwakuwa mlango wa njia ya hewa (Trachea) hulalia juu ya Koo tofauti na pale anapolalia tumbo ambapo mlango huo huwa upo chini, kiasi cha kurahisisha zoezi la kupaliwa na kuingia kwa vimimika kwenye Koo la hewa.

Marekani imetangaza rasmi Miongozo mipya ya Lishe ya Kitaifa kwa mwaka 2025–2030, ikilenga kubadili mwelekeo wa ulaji kw...
09/01/2026

Marekani imetangaza rasmi Miongozo mipya ya Lishe ya Kitaifa kwa mwaka 2025–2030, ikilenga kubadili mwelekeo wa ulaji kwa wananchi wake kwa kusisitiza ulaji wa chakula halisi chenye Virutubisho badala ya vyakula vya Kisasa vilivyotengenezwa viwandani.

Miongozo hiyo, iliyotolewa Januari 8, 2026 inalenga kukabiliana na ongezeko la Magonjwa yasiyoambukiza k**a Kisukari, Presha, Magonjwa ya Moyo, Saratani na Unene kupita kiasi.

Kwa mujibu wa miongozo hiyo, Wananchi wanahimizwa kula Protini ya ubora wa juu katika kila mlo, ikiwemo Samaki, Nyama, Mayai, Maharage na Karanga, pamoja na mboga mboga, Matunda, nafaka zisizokobolewa, Mafuta mazuri na maziwa yasiyo na sukari za Nyongeza.

Miongozo hiyo pia inashauri kupunguza matumizi ya sukari za Viwandani na Pombe, ikieleza kuwa hakuna kiwango cha sukari kinachochukuliwa kuwa salama kiafya, na kwamba Pombe inapaswa kuepukwa au kutumiwa kwa kiwango kidogo sana.

08/01/2026

Mwanamke ukiona usiku unaanza kukabwa na kukosa pumzi usikimbilie kwa waganga ukadhani ni jinamizia bali nenda hospitalini pengine Hedhi yako imeanza kukoma.

Dkt. Lilian Mnabwiru
Daktari Bingwa wa Magonjwa Uzazi

VIDEO: Elimu ya Afya Online TV

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram