13/04/2026
Si salama kwa mtoto kupigwa busu na kila Mtu hasa watu wa nje kwa sababu kuna hatari ya kuambukizwa Magonjwa yanayoenezwa kupitia mate na ngozi. Magonjwa k**a vile mafua, virusi vya herpes (HSV-1) vinavyosababisha vidonda mdomoni, na maambukizi ya Bakteria k**a Streptococcus yanaweza kupitishwa kwa mtoto kupitia busu.
Mtoto mchanga ana kinga dhaifu, hivyo maambukizi yanaweza kuwa hatari zaidi na kusababisha matatizo makubwa ya kiafya. Hii ni kutokana pia na ukweli kwamba ni ngumu kufahamu anayembusu Mwanao katoka kufanya jambo gani kabla ya hapo.
Ili kumlinda mtoto, ni vyema kuwaeleza watu waepuke kumbusu na kuhakikisha mikono yao ni safi kabla ya kumshika. Pia, mzazi au mlezi anapaswa kuwa makini na dalili zozote za maambukizi kwa mtoto na kumpeleka hospitalini inapobidi.