Veriafya

Veriafya Chanzo namba moja cha Taarifa, Elimu na Dondoo za Afya kwa Kiswahili

Katika tukio la kusikitisha lililotokea nchini Marekani, Jaysen Carr (12) amefariki dunia baada ya kuambukizwa na vimele...
30/07/2025

Katika tukio la kusikitisha lililotokea nchini Marekani, Jaysen Carr (12) amefariki dunia baada ya kuambukizwa na vimelea hatari vya Naegleria fowleri, vinavyojulikana k**a (Amiba mla Ubongo) baada ya kuogelea katika ziwa la 'Lake Murray', South Carolina.

Amiba (Amoeba) hawa hupatikana kwa wingi katika maji ya asili yenye joto, na hushambulia Ubongo kwa kasi kubwa na mara nyingi husababisha kifo siku chache baada ya dalili kuanza.

Amiba hawa hawawezi kuonekana kwa macho wala kugunduliwa kwa urahisi na waogeleaji. Wakati wa kiangazi ambapo joto hupanda na kiwango cha maji kinashuka, viwango vyake huongezeka, na hivyo kuongeza hatari ya maambukizi kwa watu wanaoingia majini hususan kupitia Pua.

Kwa mujibu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC), maambukizi yake ni nadra sana kutokea lakini yana kiwango cha vifo kinachofikia 97%

Kujikinga dhidi ya Amiba hii hatari inashauriwa kuepuka kuruhusu maji ya asili kuingia puani wakati wa kuogelea, kutumia 'Nose clips', au kuogelea katika maji safi ya mabwawa yanayosafishwa. Pia ni muhimu kuepuka kuruka kwa kichwa katika maji ya asili yenye Joto, na kuhakikisha kuwa maji ya kutumia kwenye matibabu ya Pua ni yaliyochemshwa au yaliyo na Chumvi maalum (Saline).

Minyoo wanaweza kuziba Utumbo, hasa ikiwa kuna maambukizi makubwa. Aina fulani za Minyoo k**a Ascaris lumbricoides (Miny...
29/07/2025

Minyoo wanaweza kuziba Utumbo, hasa ikiwa kuna maambukizi makubwa. Aina fulani za Minyoo k**a Ascaris lumbricoides (Minyoo mviringo) huweza kukua kwa wingi ndani ya Utumbo hadi kufikia Sentimita 35 na kujikusanya, hivyo kusababisha kuziba kwa utumbo, hali inayoweza kupelekea Maumivu makali ya tumbo, Kutapika, Kuvimbiwa na matatizo ya kumeng’enya chakula.

Kuziba kwa utumbo kutokana na minyoo ni hatari na inaweza kuhitaji matibabu ya dharura, ikiwemo dawa za kuua minyoo au hata Upasuaji katika visa vikubwa.

Njia bora ya kuzuia tatizo hili ni kutumia dawa za Minyoo walau mara Mbili kwa Mwaka, kudumisha usafi wa Mikono, na kula vyakula vilivyoandaliwa kwa Usafi.

Wanaume wengi hutafuta mbinu za kusaidia kuchelewa kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa. Njia moja rahisi inayotumika...
27/07/2025

Wanaume wengi hutafuta mbinu za kusaidia kuchelewa kufika kileleni wakati wa tendo la ndoa. Njia moja rahisi inayotumika ni kubana pumzi kwa makusudi wakati wa tendo. Kitendo hiki huchelewesha kufikia kileleni kwa sababu kinasaidia kudhibiti msisimko wa mwili na kupunguza kasi ya mapigo ya Moyo.

Wakati mwanaume anabana pumzi, anaupa mwili wake muda wa kutulia, jambo linalosaidia kuzuia kuamshwa haraka kwa ile hali ya mwisho (kilele). Ni k**a vile mwili unalazimishwa kupunguza kasi ya mwitikio wa hisia kali. Hii ni tofauti na kupumua haraka haraka, ambayo huongeza msisimko na kumfanya afikie kilele mapema.

Hata hivyo, kubana pumzi kupita kiasi kunaweza kuwa na madhara k**a kizunguzungu au maumivu ya kichwa. Kwa hiyo, ni muhimu kutumia mbinu hii kwa busara, ikiwezekana pamoja na mazoea mengine ya kuongeza udhibiti wa Mwili

Kuna madai yanayosambaa Mtandaoni  kwamba zile alama za rangi (Kijani, Bluu, Nyekundu au Nyeusi) chini ya kasha la dawa ...
25/07/2025

Kuna madai yanayosambaa Mtandaoni kwamba zile alama za rangi (Kijani, Bluu, Nyekundu au Nyeusi) chini ya kasha la dawa ya meno zinaonesha aina ya kemikali zilizomo kwenye dawa hiyo. Mfano, Kijani ni ya dawa ya asili, Nyeusi ni kemikali tupu nk.

Madai hayo ni ya kupotosha. Alama hizo hazihusiani kabisa na viambato vya dawa ya meno. Kitaalamu, huitwa 'Eye Marks' au 'Color Marks' na hutumika kiwandani kusaidia mashine kutambua pa kukata na kufunga kasha la dawa ya Meno wakati wa uzalishaji.

Ni k**a alama za mwongozo kwa mashine za kiwanda, sio kwa watumiaji wala hazina ujumbe wowote kuhusu viambato vya ndani ya Dawa hiyo.

Unataka kujua kilicho ndani ya dawa ya meno? Soma orodha ya viambato (ingredients) upande wa kasha, si kutegemea alama ya rangi.

Kutafuna Vitunguu vibichi k**a sehemu ya mlo huimarisha Kinga ya Mwili. Husaidia kupambana na Mafua, Kikohozi na Maambuk...
24/07/2025

Kutafuna Vitunguu vibichi k**a sehemu ya mlo huimarisha Kinga ya Mwili. Husaidia kupambana na Mafua, Kikohozi na Maambukizi kwa sababu vina kemikali za asili zinazoua Vijidudu.

Pia, vitunguu ni rafiki wa Moyo. Husaidia kupunguza shinikizo la damu na mafuta mabaya, hivyo kulinda moyo dhidi ya magonjwa hatari k**a shambulio la Moyo na Kiharusi.

Ingawa harufu yake ni kali, husaidia kuboresha afya ya kinywa na mmeng’enyo wa chakula. Huua Bakteria wabaya mdomoni na kusaidia tumbo kumeng’enya chakula vizuri. Ni tiba rahisi, ya asili, na yenye faida nyingi kwa afya.

Kope bandia na lenzi za macho za urembo zinaweza kuwa chanzo cha matatizo makubwa ya macho kwa wanawake, ikiwemo upofu. ...
24/07/2025

Kope bandia na lenzi za macho za urembo zinaweza kuwa chanzo cha matatizo makubwa ya macho kwa wanawake, ikiwemo upofu. Ingawa hutumika kuongeza mvuto, zinaweza kuharibu macho k**a hazitatumika kwa usahihi.

Lenzi bandia zisizo salama au zisizotunzwa vizuri huweza kusababisha maambukizi, kuvimba kwa macho, na hata vidonda vinavyoweza kuleta upofu. Kope bandia pia huambatana na gundi zenye kemikali kali zinazoweza kusababisha kuwasha au uharibifu wa macho.

Ili kujikinga, hakikisha unatumia lenzi bandia zilizoidhinishwa na wataalamu wa macho, usivalie lenzi za marafiki, na usitumie kope bandia mara kwa mara bila ushauri wa daktari. Uzuri wa macho yako ni muhimu, lakini afya ya macho yako ni ya thamani zaidi.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kwamba janga la Virusi vya Chikungunya linaweza kuenea kote ulimwenguni, likitaka...
23/07/2025

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kwamba janga la Virusi vya Chikungunya linaweza kuenea kote ulimwenguni, likitaka hatua za haraka zichukuliwe kuzuia.

Kwa mujibu wa WHO, Ugonjwa huu unaoenezwa na Mbu ambao husababisha Homa na maumivu makali ya viungo, ambayo mara nyingi hudhoofisha mwili na katika baadhi ya matukio inaweza kusababisha Kifo hadi sasa umegunduliwa na kuambukizwa katika nchi 119 duniani, na kuweka watu bilioni 5.6 hatarini.

Ili kujikinga na Chikungunya, hakikisha unajikinga na mbu kwa kutumia vyandarua vyenye Dawa, kuvaa nguo zinazofunika mwili hasa nyakati za Usiku, kupulizia dawa za kuua mbu ndani na nje ya nyumba, na kuondoa mazalia ya Mbu k**a maji yaliyotuama kwenye vyombo, matairi na Makazi

UTI za mara kwa mara zinaweza kuathiri figo na kusababisha kushindwa kufanya kazi. Hii hutokea hasa pale maambukizi yana...
23/07/2025

UTI za mara kwa mara zinaweza kuathiri figo na kusababisha kushindwa kufanya kazi. Hii hutokea hasa pale maambukizi yanapoenea hadi kwenye figo na kusababisha uvimbe au majeraha ya kudumu.

Kadri maambukizi yanavyojirudia bila tiba sahihi, ndivyo hatari ya kuharibika kwa figo huongezeka. Hali hii inaweza kupelekea ugonjwa wa figo sugu au kushindwa kabisa kwa figo kufanya kazi.

Ili kujikinga, ni muhimu kutibu UTI mapema, kunywa Maji ya kutosha na kudumisha Usafi wa nguo za Ndani na Vyoo. Kwa wanaopata UTI mara kwa mara, ni vyema kufanya uchunguzi wa kiafya, kupata tiba ya kudumu na kuacha Matumizi holela ya dawa hasa Azuma bila kupima wala kufuata ushauri wa Kitabibu

NIGERIA: Mwanafunzi wa Mwaka wa 2, Gloria Samuel (22), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kufuatia kuhusishwa na kifo cha M...
22/07/2025

NIGERIA: Mwanafunzi wa Mwaka wa 2, Gloria Samuel (22), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kufuatia kuhusishwa na kifo cha Mhadhiri mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Prince Abubakar Audu (PAAU), Dkt Ibikunle aliyekuwa naye hotelini.

Ripoti za awali zinadai kuwa Dkt. Ibikunle alikuwa amekunywa vinywaji vya kuongeza ili kuweka Mwili wake sawa kabla ya hali yake kubadilika ghafla, na baadaye alifariki akiwa Hospitalini.

Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ikiwa ni pamoja na kubaini k**a Marehemu alipatwa na Mshtuko wa Moyo muda mfupi kabla ya Kufariki.

Matumizi makubwa ya Energy Drinks husababisha Changamoto kubwa kwa afya, pia ni chanzo cha Magonjwa sugu ya mfumo wa Damu na Moyo.

Je, wajua?Uvaaji wa suruali za kubana sana mapaja kwa muda mrefu unaweza kukandamiza mshipa wa fahamu unaoitwa lateral f...
22/07/2025

Je, wajua?

Uvaaji wa suruali za kubana sana mapaja kwa muda mrefu unaweza kukandamiza mshipa wa fahamu unaoitwa lateral femoral cutaneous nerve unaopita kwenye paja.

Hali hii husababisha ganzi, hisia ya kuchomwa-chomwa, au kuwashwa kwenye paja,ntatizo hili linajulikana kitaalamu k**a Meralgia Paresthetica au Tingling Thigh Syndrome.

Unapolalia Kisogo au Kuinamisha Kichwa kwa Nyuma wakati damu inatoka Puani, kuna uwezekano mkubwa wa damu hiyo kurudi ny...
22/07/2025

Unapolalia Kisogo au Kuinamisha Kichwa kwa Nyuma wakati damu inatoka Puani, kuna uwezekano mkubwa wa damu hiyo kurudi nyuma na kuingia Kooni au kwenye njia ya hewa.

Hali hii inaweza kukufanya ukohoe damu, upate maumivu kooni, au hata kushindwa kupumua vizuri, jambo ambalo ni hatari.

Unashauriwa kukaa wima au ukae kwenye kiti ukiweka kichwa kikielekea mbele kidogo. Finya pua kwa dakika 10–15 na tumia kitambaa baridi kwenye paji la uso au shavuni kusaidia kuzuia damu kuendelea kutoka na utumie Mdomo kupumua.

Ukiona damu haikomi ndani ya dakika 20, au unatokwa na damu mara kwa mara bila sababu inayoeleweka, tafuta msaada wa daktari haraka.

Kuweka wallet kubwa kwenye mfuko wa nyuma wa Suruali ni tabia ambayo wengi hufanya bila kufikiria, lakini inaweza kuleta...
22/07/2025

Kuweka wallet kubwa kwenye mfuko wa nyuma wa Suruali ni tabia ambayo wengi hufanya bila kufikiria, lakini inaweza kuleta Madhara kwa afya ya Mgongo na Kiuno.

Unapoketi ukiwa na wallet kubwa mfukoni, kiuno chako hubanwa upande mmoja na kusababisha mwili kukaa vibaya bila hata wewe kujua.

Hali hii ikijirudia mara kwa mara, inaweza kusababisha maumivu ya sehemu ya chini ya mgongo, Kiuno na hata mguu mmoja kuwa na ganzi au maumivu. Hii ni kwa sababu ya kushinikiza mishipa ya fahamu inayopita eneo la nyonga.

Kwa afya njema ya mgongo wako, ni vyema kuzoea kutoa wallet mfukoni unapoketi, au kuihifadhi mbele au kwenye begi. Unaweza pia kupunguza vitu visivyo vya lazima kwenye wallet ili iwe nyepesi na ndogo zaidi.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Veriafya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share