21/11/2025
Mamlaka za Afya Nchini India zimezuia matumizi ya Dawa ya Kikohozi kwa watoto aina ya Coldrif zinazozalishwa na kiwanda cha Sresan Pharmaceutical baada ya kusababisha vifo vya watoto taktiban 24.
Chanzo kikubwa cha tatizo ni kemikali muhimu iliyotumiwa kutengeneza dawa hiyo, propylene glycol ambayo malighafi yake yalinunuliwa na kusafirishwa kienyeji kutoka kwa wauzaji hivyo kuchafuliwa na sumu aina ya diethylene glycol (DEG) ambayo hushambulia figo, hasa kwa watoto.
Serikali ya India ilipokagua kiwanda, ilikuta mamia ya makosa makubwa ya usalama ikiwemo mazingira machafu, kumbukumbu zilizochezewa, na taratibu za uzalishaji zisizofuatwa hivyo kuonesha udhaifu mkubwa katika usimamizi na ukaguzi wa viwanda vya dawa, pamoja na mnyororo wa upatikanaji wa malighafi ambao unapaswa kuwa salama na unaoaminika.
Tukio hili limezua hofu kubwa kwa wazazi na wataalamu wa afya, na limekumbusha ulimwengu kwamba bidhaa rahisi k**a dawa ya kikohozi zinaweza kuua ikiwa usalama hautazingatiwa.