ManTing'i JK Pharmacy

  • Home
  • ManTing'i JK Pharmacy

ManTing'i JK Pharmacy Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ManTing'i JK Pharmacy, Medical and health, .

ManTing'i JK Pharmacy ni Duka la Dawa lililoko Kibamba shule eneo la jirani na Kona Baa.Tuko wazi masaa 24 kwaajili ya kutoa huduma kila siku.Tunazo Dawa mbalimbali kulingana na mahitaji yako.Asante

11/06/2025

Ndugu yangu sikiliza maelekezo haya muhimu kutoka kwa Mtaalamu wa Dawa kutokea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ,Mloganzila.

Kwa niaba ya uongozi na wataalamu wetu wa ManTing'i JK Pharmacy napenda kuwashukuru wateja wetu na kuwatakia uponyaji na...
08/06/2025

Kwa niaba ya uongozi na wataalamu wetu wa ManTing'i JK Pharmacy napenda kuwashukuru wateja wetu na kuwatakia uponyaji na kheri wale wote wanaosumbuliwa na maradhi.Tunapenda kuwakumbusha kufuata maelekezo ya wataalamu na kuzingatia matumizi sahihi ya dawa..Asanteni, unaweza kupata ushauri Bure kutoka dukani kwetu masaa 24 ... ubarikiwe.Mawasiliano yetu ni

0713182392

Take care of your health,we do care too...get in touch with us , ManTing'i JK Pharmacy 0713182392
08/06/2025

Take care of your health,we do care too...get in touch with us , ManTing'i JK Pharmacy
0713182392

Je,unasumbuliwa na maumivu ya kichwa,mgongo,hedhi au mwili kwa ujumla?...Pata ushauri kutoka kwa wataalamu wetu wa Dawa ...
11/05/2025

Je,unasumbuliwa na maumivu ya kichwa,mgongo,hedhi au mwili kwa ujumla?...Pata ushauri kutoka kwa wataalamu wetu wa Dawa wenye weledi na umahiri.Tupo kwaajili ya kukuhudumia na duka letu liko wazi masaa 24 Kila siku...Asante
ManTing'i JK Pharmacy
0713182392

02/11/2024
Habari , natumaini uko poa.Leo naomba nikukumbushe wajibu wako wa msingi ukiwa k**a mzazi,mlezi au muuguzi wa mgonjwa......
28/10/2024

Habari , natumaini uko poa.Leo naomba nikukumbushe wajibu wako wa msingi ukiwa k**a mzazi,mlezi au muuguzi wa mgonjwa.... "Weka Dawa mbali na watoto". ... Asante

Nikushauri ndugu mzazi ...hasa wewe mwenye mtoto mchanga kuchukua hatua stahiki kufuatilia matibabu ya mtoto pale hali y...
16/07/2024

Nikushauri ndugu mzazi ...hasa wewe mwenye mtoto mchanga kuchukua hatua stahiki kufuatilia matibabu ya mtoto pale hali yake ya kiaafya inapokuwa isiyo ya kuridhisha... mathalani mtoto kulia sana kuliko kawaida, mtoto kutokunyonya,kukosa choo kwa muda mrefu,kuvimba au kukak**aa ngozi, kuota vipele na changamoto nyingine zinazoweza kuashiria hali ya ugonjwa.Tembelea kituo Cha matibabu kilicho jirani Yako uonane na Daktari kuliko kumwanzishia dawa bila uchunguzi wa kitabibu....Kwa ushauri wa matumizi sahihi ya dawa na vifaa tiba au usafi wa mwili kwa mwanao... wasiliana nasi ManTing'i JK Pharmacy, Kibamba shule, jirani na Kona Baar -Dar, kwa simu Namba 0713182392...Tuko wazi masaa 24 Kila siku... Asante .

Tumia dawa sahihi kwa wakati sahihi ukizingatia maelekezo ya wataalamu wetu ili kudumisha Afya na kupata manufaa yaliyok...
25/06/2024

Tumia dawa sahihi kwa wakati sahihi ukizingatia maelekezo ya wataalamu wetu ili kudumisha Afya na kupata manufaa yaliyokusudiwa na mtengenezaji kufuatia ushauri wa Daktari wako.Asante na karibu ManTing'i JK Pharmacy Kibamba shule jirani na Kona Baar -Dar kwa huduma za dawa, vifaa tiba pamoja na vipodozi masaa 24 Kila siku...tupigie 0713182392 au tuma ujumbe wako Whatsapp.. Asante

Jitahidi kufanya mazoezi,kujishughulisha na kula mlo kamili Ili kujenga mwili na kuimarisha Afya Yako k**a njia rahisi y...
01/06/2024

Jitahidi kufanya mazoezi,kujishughulisha na kula mlo kamili Ili kujenga mwili na kuimarisha Afya Yako k**a njia rahisi ya kupunguza uwezekano wa kupata maradhi yasiyoambukiza k**a vile presha,kisukari na magonjwa ya moyo... Asante

Ni mambo gani unapaswa kuzingatia unapochagua dawa kwaajili ya mteja au mgonjwa wako?...Hili swali ni kwako ndugu Mtaala...
30/05/2024

Ni mambo gani unapaswa kuzingatia unapochagua dawa kwaajili ya mteja au mgonjwa wako?...
Hili swali ni kwako ndugu Mtaalamu wa Afya hususani mfamasia au Daktari.pengine Kuna vitu mbali mbali hukufanya uchukue hatua na kumshauri mteja wako dawa au kifaa tiba Cha kutumia miongoni mwa vingi vilivyoko sokoni au katika makundi mbalimbali.

Yafuatayo ni miongoni mwa mambo ya kuzingatia:-

1.Jambo la kwanza ni uwezo wa bidhaa husika kutatua changamoto ya mteja wako.Mfano, tatizo linalomsumbua ni Malaria,basi dawa ya kutibu malaria na changamoto zinazoambatana na ugonjwa huo zitakua chaguo sahihi,lakini ziko dawa nyingi za Malaria...
2.Kuzingatia miongozo ya matibabu Ili kubaini ni dawa gani itolewe badala ya nyingine,hivyo Kuna dawa za mstari wa mbele na nyingine huweza kufuatia kulingana na hali ya ugonjwa (degree and severity of the patient).
3.Endapo dawa pendekezwa au kifaa tiba kipo Cha wazalishaji tofauti ni vema kuzingatia ufanisi,ubora, usalama,unafuu wa kutumia (friendly user product).
4.Zingatia hali ya usajili na kusudio la mtengenezaji pamoja na upatikanaji wa bidhaa na gharama (dawa au kifaa tiba kiwe ni Cha gharama anayoweza kumudu mteja).
5.Zipo sababu nyingine za kitaalamu zinazoendana na sera za ndani pamoja na vipaumbele zinazolenga kudumisha ubora wa huduma mathalani kutoa zile bidhaa zilizokaa muda mrefu,zilizo kwenye mpango wa kampeni na zinazosaidia kuongeza kipato na kuchangia upatikanaji wa huduma endelevu.
6.MUHIMU SANA zingatia usalama wa mtumiaji, bidhaa inayoweza kusababisha madhara makubwa au ulemavu ama kifo isitolewe kwa mgonjwa au mtu ambae anajulikana kuwa na shida nayo iwe mzio au muingiliano. Mteja wa namna hii mchagulie dawa isiyo na shida kutoka katika kundi tofauti na dawa zinazompa shida.Jitahidi kudodosa hili mara kwa mara unapohudumia wateja wako.

Haya ndio yangu ya Leo,ongezea mengine.nitafute kwa barua pepe jumakitenge208@gmail.com au simu +255654661842 ama tiririka hapa chini

Dawa Bora,yenye ufanisi na salama pamoja na vifaa tiba iwe kipaumbele chako mtaalamu na mwanajamii mwenzangu...Asante

Posti yangu ya Leo inawalenga wanachuo na wakufunzi wa taaluma ya ufamasia.Nimeona niwaelekeze mambo ya kuzingatia wakat...
29/05/2024

Posti yangu ya Leo inawalenga wanachuo na wakufunzi wa taaluma ya ufamasia.Nimeona niwaelekeze mambo ya kuzingatia wakati unachagua sehemu ya kufanyia mazoezi kwa vitendo (field attachment).

Ukizingatia malengo ya kufanya mazoezi kwa vitendo katika taaluma na sababu mbali mbali pamoja na manufaa yanayopatikana kwa suala hili k**a tulivyoona kwenye makala zilizopita,basi Yako mambo ya kuzingatia Ili kuamua k**a sehemu unayotaka kufanyia mazoezi kwa vitendo inafaa...

Yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayopaswa kuzingatiwa :-

1.Uwepo wa huduma za kitaalamu hususani dawa za muhimu na makundi mbalimbali hata zile za maradhi yasiyopewa kipaumbele.
2.Uwepo wa wataalamu wa fani ya ufamasia wenye weledi na umahari katika utoaji huduma za dawa na ushauri.
3.Upatikanaji wa huduma za nje na za ndani kwenye vitengo mbali mbali vya matibabu na watendaji wenye sifa ikiwemo na huduma za vipimo na utafiti wa magonjwa.
4.Uwepo wa huduma za taarifa za dawa na kitengo Cha ununuzi, uhifadhi na usambazaji au ugavi wa Dawa na vifaa tiba.
5.Uongozi imara unaojali maadili, usimamizi Bora wa rasilimali watu na nidhamu ya wafanyakazi.
6.Upatikanaji wa huduma za kijamii katika eneo la kufanyia mazoezi kwa vitendo ikiwa ni pamoja na maji,umeme,usafiri, soko na malazi.
7.Uwepo wa makubaliano na mahusiano mema baina ya chuo au taasisi ya kitaalamu na taasisi mwanafunzi anapofanyia mafunzo yake kuhusu wajibu wa pande zote mbili.
8.Uwezekano wa kufikika kirahisi na umbali unaohimilika kutoka chuoni Hadi hapo kurahisisha ufikaji wa mwanachuo na ufuatiliaji wa maendeleo yake Toka chuoni.
9.Kituo husika kiwe kinatambulika kwa wanajamii,chenye ushuhuda mzuri na kitambulike kutoa huduma zake kihalali na serikali.
10.Ukubwa wa taasisi ya matibabu na uwezo pamoja na idadi ya wanachuo inaoweza kuhimili kwa mkupuo.

Unaweza ukawa na sababu nyingine nje ya hizi lakini hizi ndio za msingi.Usisite kutujuza mambo unayozingatia unapofanya maamuzi haya.nitafute kupitia jumakitenge208@gmail.com au +255654661842, Asante

Ukiwa k**a mtaalamu wa Afya, mshauri mama mjamzito kuhudhuria kliniki na kupata matibabu mara tu anapoumwa.Zaidi mshauri...
28/05/2024

Ukiwa k**a mtaalamu wa Afya, mshauri mama mjamzito kuhudhuria kliniki na kupata matibabu mara tu anapoumwa.Zaidi mshauri kuzingatia kanuni za Afya ikiwa ni pamoja na usafi wa mwili na mazingira,kula mlo kamili, kufanya mazoezi na kupata muda wa kupumzika na kujikinda na maradhi ya kuambukiza.

Jambo kubwa ni kufuatilia maelekezo ya wataalamu wa Afya anayopewa ikiwa ni pamoja na matumizi sahihi ya dawa na maandalizi yanayompasa kabla ya kujifungua....

Tuambie ni hali gani ya hatari ambayo mama mjamzito akiiona anatakiwa kufika katika kituo Cha kutolea huduma za Afya haraka iwezekanavyo?....Tuandikie kwa barua pepe jumakitenge208@gmail.com au simu Namba +255654661842 ama weka mchango wako hapa chini... Asante

Address


Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ManTing'i JK Pharmacy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to ManTing'i JK Pharmacy:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Practice
  • Claim ownership or report listing
  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share