Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa Kassim, mapema leo ametembelea wagonjwa waliolazwa katika wodi mbalimbali za T...
19/11/2025

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa Kassim, mapema leo ametembelea wagonjwa waliolazwa katika wodi mbalimbali za Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) na kutoa salamu za faraja pamoja na pongezi kwa watumishi wote wanaojituma kuwahudumia wagonjwa.

Akiwa katika wodi ya wagonjwa mahututi (ICU), Mhe. Majaliwa amepongeza kazi kubwa inayofanywa na madaktari, wauguzi na wataalamu wengine kwa kujitoa kwao kila siku kuokoa maisha.

Katika ziara hiyo, Mhe. Majaliwa amesisitiza umuhimu wa kuendeleza moyo wa huruma, utu na umakini kwa wagonjwa, akisema kuwa huduma nzuri ndiyo nguzo ya matarajio ya wananchi wanaotegemea ORCI kwa matibabu ya saratani.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa ORCI, Dkt. Crispin Kahesa, amemshukuru Mhe. Majaliwa kwa kutenga muda wa kutembelea wagonjwa na watumishi, akibainisha kuwa ujio wake umeleta faraja kubwa na kuwapa hamasa wagonjwa pamoja na watumishi wanaohudumu katika mazingira yenye changamoto.

Dkt. Kahesa amesema kuwa, ziara hiyo imethibitisha kwa vitendo dhamira ya viongozi wa taifa katika kusimamia afya ya wananchi.

Katika hatua nyingine Dkt. Kahesa ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuiwezesha ORCI kupitia vifaa tiba vya kisasa, maboresho ya miundombinu na kuimarisha upatikanaji wa huduma za kisasa za matibabu ya saratani.

Dkt. Kahesa amesema mashine za kisasa zilizopatikana zimeongeza ufanisi wa matibabu na kupunguza muda wa kungojea huduma.

Kwa kumalizia, Dkt. Kahesa amesisitiza kuwa mafanikio ya ORCI yanatokana na juhudi za watumishi wanaofanya kazi kwa kujituma usiku na mchana, pamoja na serikali kuamua kuwawezesha.

Dkt. Kahesa ameahidi kuwa taasisi itaendelea kuimarisha ubora wa huduma na kushirikiana na serikali pamoja na wadau mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata matibabu bora, salama na yenye ufanisi.

Waziri wa Afya wa Mkoa wa Katanga, Bi. Mumba Kiboko Valeriene, leo ameahidi kusaini Mkataba wa Makubaliano (MOU) na Taas...
18/11/2025

Waziri wa Afya wa Mkoa wa Katanga, Bi. Mumba Kiboko Valeriene, leo ameahidi kusaini Mkataba wa Makubaliano (MOU) na Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) ili kuwawezesha wagonjwa wa saratani kutoka Katanga kupata matibabu katika Taasisi hiyo.

Ahadi hii imekuja kufuatia mazungumzo yenye tija yaliyofanyika leo baina ya waziri huyo na mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, yakilenga kuboresha upatikanaji wa huduma za matibabu ya saratani kwa wakazi wa Katanga, ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa katika kupata matibabu sahihi na ya kisasa ndani ya mkoa wao.

Bi. Valeriene amesisitiza umuhimu wa ushirikiano huu, akibainisha kuwa Saratani ni miongoni mwa matatizo makubwa ya afya ya umma nchini Kongo, na Katanga haiko salama.

Aidha bi Valeriene amesema kuwa lengo kuu la makubaliano hayo ni kuhakikisha kuwa wagonjwa wa Katanga wanapata matibabu bora zaidi yanayopatikana, bila kulazimika kusafiri umbali mrefu au kutumia gharama kubwa kutafuta huduma hizo nje ya bara la Afrika.

Nae mkurugezi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo kwa upande wake ameelezea nia yake thabiti ya kutoa msaada wa kitaalamu na rasilimali muhimu ili kufanikisha mpango huu, huku akisisitiza kuwa taasisi yake ina vifaa vya kisasa na wataalamu wenye uzoefu wa kutosha katika matibabu ya saratani, ikiwemo tiba ya mionzi na tiba ya kemikali huku kwa upande wa upasuaji ikitarajiwa kuanza mapema mwakani.

Dkt. Msemo ameongeza kuwa ORCI itajitolea kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya kutoka Katanga ili kuwajengea uwezo wa kukabiliana na saratani katika ngazi za mkoa.

18/11/2025
Tunakuponheza Mhe. Florence Samizi kwa kuteuliwa kuwa Naibu waziri wa Afya..
18/11/2025

Tunakuponheza Mhe. Florence Samizi kwa kuteuliwa kuwa Naibu waziri wa Afya..

Tunakuponheza Mhe. Mohamedi Mchengerwa kwa kuteuliwa kuwa waziri wa Afya..
18/11/2025

Tunakuponheza Mhe. Mohamedi Mchengerwa kwa kuteuliwa kuwa waziri wa Afya..

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.....
13/11/2025

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.....

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo leo tarehe 12/11/2025 ametembelea ubalozi wa ...
12/11/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Diwani Msemo leo tarehe 12/11/2025 ametembelea ubalozi wa India na kufanya mazungumzo na balozi Bishwadip Dey, kuhusu kuimarisha mahusiano baina ya Taasisi ya Saratani ya Ocean na Taasisi za saratani za India hasa zile zinazomilikiwa na Serikali ikiwemo Tata Memorial Hospital.

Dkt. Msemo amesema kuwa mazungumzo hayo yamelenga katika kuijengea Taasisi ya saratani uwezo wa rasilimali watu katika tiba za saratani pamoja na kunufaika na teknolojia za kisasa ambazo zinapatikana nchini India.
Hii itasaidia kuboresha tiba utalii pamoja na kuokoa fedha za serikali zinazotumiwa kupeleka wagonjwa India na pamoja na nchi zingine.

Aidha Dkt. Msemo amemshukuru Mheshimiwa Balozi kwa kukubali kuwa daraja la mashirikiano kati ya Taasisi ya Saratani Ocean Road na Taasisi za India kwani hili pia litajenga nguzo imara ya kidiplomasia baina ya watanzania na watu kutoka India.

Kwa upande wake Mheshimiwa Balozi Bishwadip ameipongeza Taasisi ya Saratani Ocean Road kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuokoa maisha ya watanzania.

Wakati huo huo Balozi Bishwadip ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuboresha miundombinu ya matibabu ya saratani kwa kununua mashine mpya zenye Teknolojia ya kisasa kwaajili ya kusaidia watanzania katika kipindi hiki cha awamu ya sita ya uongozi wa Dr Samia Suluhu Hassan.

Rais wa bunge la Comoro ambae pia ndie  kiongozi wa pili na msaidizi wa Rais wa nchi hiyo Bw. Moustadroine Abdou, mapema...
05/11/2025

Rais wa bunge la Comoro ambae pia ndie kiongozi wa pili na msaidizi wa Rais wa nchi hiyo Bw. Moustadroine Abdou, mapema leo amesema kuwa atahakikisha wacomoro wote wenye shida za Saratani wnaletwa nchini Tanzania na kufikishwa katika Taasisi ya Saratani ocean road na kupata tiba stahiki.

Akizungumza katika ziara fupi aliyoifanya mapema leo katika Taasisi hiyo, Bw. Abdou amesema amestaajabishwa sana kuona mashine za kisasa zilizopo hapa ORCI na kusema kuanzia sasa hakuna haja ya wacomoro kupoteza pesa za walipa kodi wao kuoeleka wagonjwa Ulaya na Asia huku akisisitiza kuwa Taasisi ya Saratani ocean road inatosha kuwa mkombozi wa wananchi hao.

Katika hatuaa nyingine Bw. Abdou amesisitiza kuwa ili kupata wateja wengi kutoka nchi mbalimbali barani Afrika na hata nje ya nchi ya Afrika ni vyema watanzania wakadumisha Amani iliyopo na kujiepusha na kila aina ya vurugu ambazo zinaweza kuleta sintofahamu.

Aidha amempongeza Dkt. Samia kwa kuwezesha Taasisi hiyo kuwa na vifaa hivyo na kuahidi nchi yake kushirikiana na Tanzania ili kusukuma mbele gurudumu la maendeleo kiafya.

Nae Balozi wa Tanzania nchini Comoro Bw. Said Yakubu amesema nchi ya Tanzania siku zote ipo tayari kwa ushirikiano waowote na Comoro hivyo amemtoa hofu Mhe. Abdou kuhusu jambo hilo, huku akisema kuwa uhusiano huu utaimarisha ushirikiano wa kidiplomasia baina ya nchi hizo mbili.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo amemshukuru Mhe. Abdou kwa ziara hiyo na kusisitiza kuwa ujio huo pia umekuwa ni wa kukuza ushirikiano zaidi, hivyo ORCI haItaacha fursa yoyote itakayotokana na wananchi wa Comoro.

Hii ni ziara ya siku moja ambapo kiongozi huyo pqmoja na ujumbe wake, wametembelea maeneo mbalimbali ya ORCI na kujionea namna uchunguzi na matibabu yanavyofanyika katika Taasisi hii.

Tunakutakia majukumu mema ya kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania..
05/11/2025

Tunakutakia majukumu mema ya kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania..

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu ya kuiongoza Tanzania...
05/11/2025

Tunakutakia kila la kheri katika majukumu ya kuiongoza Tanzania...

Mafanikio makubwa sana yaliyopatikana Taasisi ya Saratani ocean road.....
28/10/2025

Mafanikio makubwa sana yaliyopatikana Taasisi ya Saratani ocean road.....

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram