Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Timu ya watumishi ambao ni mashabiki wa Yanga ORCI, imeibuka mshindi kwa kuifunga timu ya mashabiki wa Simba ORCI 3-2 ka...
01/03/2026

Timu ya watumishi ambao ni mashabiki wa Yanga ORCI, imeibuka mshindi kwa kuifunga timu ya mashabiki wa Simba ORCI 3-2 katika mpambano mkali uliokuwa na tambo nyingi hapo awali, umefanyika mapema tarehe 27 februari 2026.

Awali Katika mchezo wa kusisimua uliojawa na msukosuko uwanjani timu ya Yanga ORCI kwenye uwanja wa Jakaya Mrisho Kikwete uliopo Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam, ilijinasibu kuwa itaendeleza ubabe wa kaka zao timu halisi ya yanga huku Simba wakisema kuwa huo ndio utakuwa mwisho wa uteja, lakini mwisho wa siku, uteja uliendelea

Ushindi huo umeamsha furaha kwa timu hiyo ya Yanga ORCI na kuacha majonzi kwa timu ya Simba ORCI, ambapo hata hivyo watumishi mashabiki wa Simba wameomba mechi ya marudiano huku wakisisitiza Refa abadilishwe ili mchezo uwe wa haki.

Taasisi ya Saratani Ocean road huwa na utaratibu wa kufanya michezo mbalimbali ili kupunguza athari za magonjwa yasiyoambukizwa na shida ya tabia bwete.

Gavana Mkuu wa Maniema nchini DRC Congo Mhe. Moise M***a Kabwankubi amesema kuwa amefurahishwa na uwekezeji wa Rais wa J...
24/02/2026

Gavana Mkuu wa Maniema nchini DRC Congo Mhe. Moise M***a Kabwankubi amesema kuwa amefurahishwa na uwekezeji wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alioufanya katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Aidha Bw. Kankwabi amesema ORCI itegemee wagonjwa wengi kutoka Congo hususani kwenye jimbo la Maniema kutokana na uhakika wa ufanyaji kazi wa mashine, ili waweze kupata matibabu ya uhakika ya Saratani.

Bw. Kankwabi amesema hayo Leo februari 24, 2026 alipofanya ziara katika Taasisi ya Saratani Ocean Road baada ya kutembelea miradi mbalimbali iliyowekezwa kwa ajili ya kutoa matibabu ya Saratani.

Mhe. Kabwankubi amesisitiza kuwa yupo tayari kwa ushirikiano hasa katika sekta ya Afya kati ya Tanzania na DRC Congo kwani hii itasaidia ORCI kupokea wagonjwa kutoka nchi mbalimbali ikiwemo DRC Congo na hasa kutoka kwenye jimbo la Maniema.

Sambamba na hayo Mhe. Kabwankubi ameiomba Taasisi iendelee kuwapokea wanafunzi wanasomea udaktari wa Saratani kutoka mataifa jirani ikiwemo Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Ili waweze kuongeza ujuzi zaidi wa matibabu ya Saratani ambapo mwisho wa siku itakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wacongo kwani madaktari wakiwa wengi itasaidia utoaji wa huduma za kidaktari kwenye changamoto za Saratani nchini humo.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Diwani Msemo ameshukuru ujio wa Gavana Kabwankubi kutoka nchini DRC, Congo pamoja na barozi wa Tanzania nchini DRC Congo kwani ujio wao umechochea ushirikiano kati ya nchi hizi mbili hususan katika jimbo la Maniema.

Dkt. Msemo ametoa shukrani za dhati kwa uongozi wa awamu ya sita wa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji katika Taasisi ya Saratani Ocean Road na kuifanya kuwa Moja ya Taasisi kubwa ya matibabu ya Saratani katika bara la Afrika.

Dkt. Msemo amesema kuwa Taasisi hiyo imekuwa kimbilio la nchi mbalimbali barani Afrika hasa kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Comoro N.k, katika matibabu ya Saratani.

Viongozi hao wameahidiana kutiliana saini za kusaidiana suala la matibabu ya Saratani ambapo makubaliano hayo yatafanyika siku za hivi karibuni.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Yaweka Jiwe la Msingi la Mageuzi ya Taasisi ya Saratani Ocean Ro...
23/02/2026

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Yaweka Jiwe la Msingi la Mageuzi ya Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)
Safari ya Mageuzi kuelekea Kituo cha Ubora Barani Afrika

Tarehe 23 Februari 2026 itaendelea kukumbukwa k**a siku ya kihistoria katika safari ya mageuzi ya Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI). Mchango wa shilingi milioni 361.5 uliotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) si tu msaada wa kifedha, bali ni uwekezaji wa kimkakati unaoashiria imani, matumaini na dira ya pamoja ya kuiwezesha ORCI kufikia hadhi ya Kituo cha Ubora (Centre of Excellence) katika huduma za saratani barani Afrika.

Kwa zaidi ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, ORCI imeendelea kupiga hatua kubwa katika utoaji wa huduma za uchunguzi, tiba ya mionzi, kemotherapi na huduma shirikishi. Hata hivyo, kukosekana kwa chumba cha upasuaji ndani ya taasisi kulibaki kuwa pengo kubwa katika mnyororo wa huduma za saratani. Wagonjwa walilazimika kufanyiwa uchunguzi ORCI, kisha kwenda hospitali nyingine kwa ajili ya upasuaji, na baadaye kurejea ORCI kuendelea na matibabu. Hali hii ilisababisha usumbufu, ucheleweshaji wa matibabu, gharama za ziada na wakati mwingine athari za kiafya kwa wagonjwa, hususan kina mama na makundi mengine yenye uhitaji mkubwa.

Ujenzi wa jengo jipya la upasuaji unaondoa changamoto hiyo ya muda mrefu na kuifanya ORCI kuwa One Stop Centre kituo jumuishi kinachotoa huduma kamili chini ya paa moja. Hii si hatua ndogo; ni mapinduzi ya kimfumo yanayoweka misingi ya huduma za kimultidisciplinary, ambapo wataalamu wa upasuaji, tiba ya mionzi, tiba ya dawa (chemotherapy), uchunguzi wa kimaabara na huduma za uangalizi wa karibu watafanya kazi kwa pamoja kwa manufaa ya mgonjwa.

Kwa mtazamo wa kitaalamu, uwepo wa huduma ya upasuaji ndani ya ORCI utaongeza ufanisi wa mipango ya matibabu (treatment planning), kuimarisha ushirikiano wa kitabibu (tumor boards) na kupunguza muda wa kusubiri huduma. Wagonjwa watanufaika na mwendelezo wa matibabu usiokatika, jambo linaloongeza nafasi ya mafanikio ya tiba na kuboresha ubora wa maisha yao.

Usikose...
22/02/2026

Usikose...

Kutana na Dkt. Mamsau Ngoma faktari bingwa wa Saratani, atakaekuelezea kwa undani kuhusu Saratani ya watoto, ni live kup...
21/02/2026

Kutana na Dkt. Mamsau Ngoma faktari bingwa wa Saratani, atakaekuelezea kwa undani kuhusu Saratani ya watoto, ni live kupitia TikTok ya elimu ya afya

Tunawatakia waislamu wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhani
19/02/2026

Tunawatakia waislamu wote mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhani

Welcome to our CME....
19/02/2026

Welcome to our CME....

Tunawatakia heri ya mfungo wa Kwaresma...
18/02/2026

Tunawatakia heri ya mfungo wa Kwaresma...

Katibu Mkuu wa wizara ya afya nchini Comoro Dkt. Soudjay Mohamed mapema leo tarehe 14/02/2026 ametembelea katika Taasisi...
14/02/2026

Katibu Mkuu wa wizara ya afya nchini Comoro Dkt. Soudjay Mohamed mapema leo tarehe 14/02/2026 ametembelea katika Taasisi ya Saratani Ocean Road leongo likiwa ni kujionea mashine ambazo zimewekwa na serikali ya awamu ya sita Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika Taasisi hiyo.

Bw. Soudjay amesema kuwa amefurahishwa sana na miundombinu hiyo na namna ambavyo utoaji wa huduma za Saratani unaendelea katika Taasisi hiyo, hivyo amempongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kuwekeza kwenye Afya za watanzania.

Bw. Soudjay amesema ORCI imekuwa zaidi na kufikia viwango vya kimataifa hivyo ameahidi kuharakisha mchakato wa kuingia makubaliano kati ya ORCI na selikari ya Comoro Ili kuhakikisha wagonjwa wa Saratani kutoka Comoro kupatiwa tiba stahiki na kwa urahisi.

Katika ziara yake hiyo ambayo aliambatana na msaidizi wake Dkt. Rahia Madi Soilihi, Bw. Soudjay ametembelea mitambo ya PET CT scan iliyozinduliwa na Waziri wa afya siku za karibuni na amefurahishwa na uwekezaji wa selikari ya Dkt. Samia Suluhu Hassan huku akishangazwa na uwezo mkubwa mashine hiyo ya kutambua Saratani katika hatua za awali kabisa

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa ORCI Dkt. Diwani Msemo amesema kuwa ujio huo ni fursa kubwa hivyo ameahidi kuitumia ipasavyo ili Taasisi hiyo iweze kutoa huduma stahiki kwa wananchi wa Tanzania na wa nchi za nje k**a Comoro ili kuitangaza nchi.

Aidha Dkt. Msemo amesema kuwa amefungua milango kwa nchi mbalimbali kuweza kushirikiana na Taasisi hiyo kwa uwezo mkubwa mashine hizo ni bora ukawanufaisha wa Afrika wengi hivyo kujenga mahusiano mema baina ya Tanzania na nchi mbalimbali za Afrika.

Ujio huo umekuja mara baada ya Taasisi ya Saratani Ocean Road kuadhimisha miaka thelatini (30) ambapo kulikuwa na kongamano kubwa la kimataifalililoshirikisha nchi zaidi ya 30 barani Afrika ambapo Bw. Soudjay Mohamed alihudhuria pia.

Leo ni siku ya pili na ya mwisho ya kongamano kubwa la kimataifa juu ya Saratani, kongamano hili limekwenda sambamba na ...
13/02/2026

Leo ni siku ya pili na ya mwisho ya kongamano kubwa la kimataifa juu ya Saratani, kongamano hili limekwenda sambamba na kusherehekea maadhimisho ya miaka 30 ya ya utoaji huduma wa Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Maadhimisho hayo yamefurahiwa na wadau mbalimbali ndani na nje ya nchi ambapo wameyasifu kwa upangiliaji wa matukio pamoja na weledi wa waongoza kongamano hilo na kusema huu ni mwanzo mzuri na mengi mazuri yanakuja.


πŸ”₯πŸ”₯πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ’ͺ🏿πŸ’ͺ🏿πŸ’ͺ🏿πŸ’ͺ🏿

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Taasisi ya Saratani Ocean R...
12/02/2026

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ameipongeza Taasisi ya Saratani Ocean Road kwa juhudi zake kubwa za kujitolea katika kutoa huduma za uchunguzi, utafiti pamoja na utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu kinga na mapambano dhidi ya ugonjwa huo pamoja na matibabu ya saratani kwa wananchi wa Tanzania.

Dkt. Nchemba ametoa pongezi hizo Leo Februari 12, 2026 kwenye maadhimisho ya miaka 30 ya Taasisi ya Saratani Ocean Road yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Nchemba ameushukuru uongozi wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia katika kutekeleza ahadi zake ndani ya Taasisi ya Saratani Ocean Road kwani imekuwa msaada kwa wagonjwa wa Saratani nchini pamoja na nje ya nchi.

Dkt. Nchemba amesema Taasisi hiyo imeendelea kuwa tegemeo muhimu kwa wagonjwa kutoka maeneo mbalimbali ya nchi, huku ikionesha maendeleo makubwa katika kuboresha miundombinu, vifaa tiba na huduma za matibabu ya kitaalamu.

Aidha, Dkt. Nchemba amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Taasisi hiyo ili kuhakikisha huduma za saratani zinakuwa bora, nafuu na zinawafikia wananchi wengi zaidi kwa wakati

Maadhimisho hayo yamekusanya pamoja viongozi wa serikali, wataalamu wa afya, wadau wa maendeleo pamoja na wananchi, kwa lengo la kuadhimisha mafanikio ya taasisi hiyo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa saratani nchini kwa kipindi cha miongo mitatu tangu kuanzishwa kwake.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo tarehe 12/02/2026 akihutubia katika maadhimisho ya miaka 30 ya utoaji wa hudu...
12/02/2026

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo tarehe 12/02/2026 akihutubia katika maadhimisho ya miaka 30 ya utoaji wa huduma za Saratani za Taasisi ya Saratani Ocean road katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, ameagiza kuwa kuanzia leo Hospitali zote ambazo zitagundua mgonjwa wa Saratani zinapaswa kumleta katika Taasisi hiyo.

Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa kwa sasa Taasisi hiyo imejitosheleza kwa kuwa na mashine za kisasa ambazo zinaweza kuhudumia wagonjwa wa ndani na wa nje hivyo kwakuwa pia ndio Taasisi maalum kwaajili ya Saratani hivyo matibabu yote ya Saratani ni vyema yakafanyika hapo.

Awali Mhe. Mchengerwa amewapongeza watumishi wa Taasisi hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Dkt Diwani Msemo kwa kuibadilisha Tasisi na kusisitiza kuwa ni vyema kwa sasa wakajikita katika utoaji wa elimu kuhusu Saratani ili wananchi wapate elimu katika hatua za awali na kuweza kupata matibabu mapema kuepusha changamoto kwa watanzania.

Aidha Mhe. Mchengerwa amemshukuru Mhe. Rais kwa kuthamini Afya za watanzania na kua.ua kuwekeza kwenye Afya kwa ndio msingi pekee wa maendeleo nchini.

Leo ni siku ambayo Taasisi ya Saratani inaadhimisha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake ambapo ilianzishwa mwaka 1996 kupitia sheria namba mbili ya bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram