Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo, (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pa...
11/05/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Diwani Msemo, (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Taasisi hiyo katika viwanja vya ukumbi wa bunge jijini Dodoma..

Aidha Dkt. Msemo amewaasa waheshimiwa wabunge kutembelea katika banda hilo na kufanya uchunguzi wa Saratani mbalimbali zikiwemo zile za Tezi Dume, Matiti na Mlango wa kizazi, kwani Saratani ikigundulika mapema inatibika.

Ndani ya bajeti ya wizara ya Afya 2026/27...
11/05/2026

Ndani ya bajeti ya wizara ya Afya 2026/27...

Ndani ya bajeti ya wizara ya Afya....
11/05/2026

Ndani ya bajeti ya wizara ya Afya....

Katibu mkuu wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe mapema leo ametembelea kwenye banda la Taasisi ya Saratani Ocean Road li...
11/05/2026

Katibu mkuu wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe mapema leo ametembelea kwenye banda la Taasisi ya Saratani Ocean Road lililopo kwenye ukumbi wa bunge jijini Dodoma.

Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Shekalaghe amesema haihitaji maelezo mengi sana kutambua ubora wa kazi za Taasisi hiyo kwani inajulikana sana kwa sasa kuwa ni Taasisi imara sana ndani na nje ya nchi.

Aidha ameomba k**a kuna jambo jipya kabisa ambali hakuwahi kulijua, ndipo alipojuzwa kuwa mtambo wa Cyclotron ni miongoni mwa mitambo mikubwa kabisa ambayo ni ya 'stage three' ambapo ina uwezo mkubwa sana wa kutoa dawa kwa haraka ambapo ina uwezo wa zaidi ya dawa Mia moja kwa lisaa limoja hivyo kwa sasa kuna uwezekano mkubwa wa kuuza dawa hiyo kwenye hospitali nyingi zitakazoamua kutumia PET CT-Scan.

Leo ni siku ya kwanza ya wizara ya Afya kupitia waziri wake Mhe. Mohammed Mchengerwa kuwasilisha bajeti kamili ya wizara hiyo hapa bungeni na Taasisi ya Saratani Ocean Road tupo hapa kwaajili ya kutoa huduma za uchunguzi wa Saratani pamoja na kutoa elimu ya saratani kwa waheshimiwa wabunge.

Taasisi ya Saratani Ocean Road, tupo tayari kwaajili ya kutoa huduma kwa waheshimiwa wabunge wa jamhuri ya muungano wa T...
10/05/2026

Taasisi ya Saratani Ocean Road, tupo tayari kwaajili ya kutoa huduma kwa waheshimiwa wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, mkoani Dodoma.

Huduma hii inatolewa ndani ya viwanja vya Bunge.

Tutakuwa bungeni tukitoa elimu juu ya Saratani pamoja na uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, Matiti pamoja na Tez...
08/05/2026

Tutakuwa bungeni tukitoa elimu juu ya Saratani pamoja na uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, Matiti pamoja na Tezi Dume....
tanzania

Tunawatakia heri ya sikukuu ya wafanyakazi Duniani....
01/05/2026

Tunawatakia heri ya sikukuu ya wafanyakazi Duniani....

Taasisi ya Saratani Ocean Road inaendelea kutoa elimu pamoja na huduma za uchunguzi wa saratani katika viwanja vya Shule...
29/04/2026

Taasisi ya Saratani Ocean Road inaendelea kutoa elimu pamoja na huduma za uchunguzi wa saratani katika viwanja vya Shule ya Sekondari Zimbwini, Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya wiki Afya Kitaifa yanayoendelea mkoani humo.

Maonesho hayo yamelenga kuhamasisha wananchi kuhusu chanjo, bima ya afya kwa wote, pamoja na usafi wa mazingira.

Mgeni rasmi katika kilele cha maonesho hayo ni Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa.

Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Huduma za Uchunguzi wa Saratani na Elimu kwa Umma, Dkt. Maguha Stephano, amesema taasisi inaendelea kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuhakikisha wananchi wanapata Elimu kuhusu saratani, huduma za uchunguzi wa saratani mbalimbali pamoja na Chanjo zinazozuia maambukizi ya virusi vinavyosababisha saratani

Amesema kuwa huduma zinazotolewa ni pamoja na uchunguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi, Saratani ya matiti pamoja na Saratani ya tezi dume (kupitia kipimo cha damu)

Aidha wananchi wa Mkoa wa Pwani, hasa Wilaya ya Kibiti, wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hii muhimu kwa afya zao.

Hongereni sana
28/04/2026

Hongereni sana

Usikose kutazama kipindi hiki ....
28/04/2026

Usikose kutazama kipindi hiki ....

28/04/2026

Diwani wa Kata ya Kivukoni mhe. Diwani Sharik Choughule, mapema leo ametembelea katika Taasisi ya Saratani Ocean Road na kujionea uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali ya awamu ya sita ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Crispin Kahesa amesema kuwa kwasasa taasisi ina miradi mitano ya Kimkakati ambayo yote imepewa nguvu kubwa na serikali ya Dkt. Samia ili kusaidia wananchi kwenye magonjwa mbalimbali hususan Saratani.

Katika ziara yake hiyo Mhe. Diwani choughule amemsifu Dkt. Samia kutokana na uwekezaji huo na kusema kuwa hakika kwa sasa sekta ya Afya imeshika hatamu kwenye maendeleo yake ukilinganisha na miaka iliyopita

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share