Ocean Road Cancer Institute

Ocean Road Cancer Institute Treatment,
Palliative care,
Research,
Diagnostic,
Prevention

Mweziwa Januari ni .wezi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, je! Unqjuq nini kuhusu Saratani hii?
09/01/2026

Mweziwa Januari ni .wezi wa Saratani ya Mlango wa kizazi, je! Unqjuq nini kuhusu Saratani hii?

Taasisi ya saratani ocean road imefanya hafla fupi ya kuwaaga wajumbe wa Bodi ya wadhamini ambao wamemaliza muda wao wa ...
07/01/2026

Taasisi ya saratani ocean road imefanya hafla fupi ya kuwaaga wajumbe wa Bodi ya wadhamini ambao wamemaliza muda wao wa ujumbe katika bodi hiyo ya wadhamini.

Hafla hiyo fupi imefanyika katika hotel ya Protea iliyopo Dar es Salaam na kuhudhuriwa na menejimenti ya Taasisi ya saratani ocean road pamoja na wajumbe wapya wa Bodi ya wadhamini.

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini Prof. Ephata Kaaya amewapongeza wajumbe waliomaliza muda wao kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuijenga Taasisi ya saratani ocean road.

Aidha wajumbe hao waliomaliza muda wao wametoa shukrani kwa menejimenti kwa ushirikiano mkubwa uliokuwepo katika Kipindi chote cha majukumu ya kuitumikia Taasisi hiyo.

Wajumbe wa Bodi ya wadhamini na menejimenti ya Taasisi ya saratani ocean road wakiwa katika mafunzo ya ujuzi wa uongozi ...
06/01/2026

Wajumbe wa Bodi ya wadhamini na menejimenti ya Taasisi ya saratani ocean road wakiwa katika mafunzo ya ujuzi wa uongozi na utawala wa kimkakati na ujumuishaji.

Bodi hiyo ya wadhamini imezinduliwa rasmi tarehe 6/1/2026 na waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Mafunzo hayo ni kuijengea uwezo Bodi ya wadhamini na menejimenti kuweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kufikia malenge yaliyokusudiwa.

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo amezindua rasmi Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya saratani ocean road, katika h...
06/01/2026

Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo amezindua rasmi Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya saratani ocean road, katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Taasisi hiyo.

Akizungumza na wajumbe wa bodi hiyo, mwenyekiti pamoja na menejiment, Mhe. Mchengerwa amewataka kudumisha mshikamano baina yao katika kutekeleza majukumu ya Bodi pamoja kupeana mawazo yatakayosaidia kusukuma mbele gurudumu la Taasisi hiyo.

Mhe.Mchengerwa ameipongeza bodi iliyomaliza muda wake pamoja na menejimenti ya Taasisi hiyo kwa kutekeleza yale yaliyoazimiwa katika Kipindi kilichopita, huku akitoa pongezi za kipekee kwa Mwenyekiti wa bodi Prof. Ephata Kaaya kwa kuteuliwa tena na Raisi kuendelea kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Taasisi ya saratani ocean road.

Aidha Mhe. Mchengerwa amejionea uwekezaji uliofanyika katika Taasisi hiyo zikiwemo mashine mbalimbali zilizopo za uchunguzi na matibabu ya saratani zilizosimikwa katika kipindi kilichoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, huku akitoa pongezi za dhati za usimamizi madhubuti unaofanywa na Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Diwani Msemo katika kuboresha Taasisi ya saratani ocean road.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi Prof. Ephata Kaaya amemshukuru Mhe. Mchengerwa kwa kuja kuzindua Bodi hiyo huku akiahidi kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na waziri pamoja na kufanya ubunifu mbalimbali katika kuboresha huduma zaidi za Taasisi ili iweze kusonga mbele kwa kasi ya serikali ya awamu ya sita.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya saratani ocean road Dkt. Diwani Msemo amesema kuwa kutokana na uwekezaji uliofanywa na serikali katika ununuzi wa mashine nyingine za tiba mionzi itapelekea kupunguza muda wa kusubiri kwa matibabu hayo kutoka wiki ishirini mpaka wiki mbili, kwani kwa sasa mashine zitakuwa za kutosha, hivyo itaboresha utoaji wa huduma hiyo.

Karibu sana Taasisi ya Saratani Ocean Road...
03/01/2026

Karibu sana Taasisi ya Saratani Ocean Road...

02/01/2026
*SALAAM ZA MWAKA MPYA 2026*Taasisi ya Saratani Ocean Road, inaungana na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk...
31/12/2025

*SALAAM ZA MWAKA MPYA 2026*

Taasisi ya Saratani Ocean Road, inaungana na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwatakia Watanzania Wote Heri ya Mwaka Mpya 2026.

Taasisi inaahidi kutoa huduma bora za kiuchunguzi na kimatibabu, huduma kwa mteja pamoja na huduma nyingine zote kwa viwango vya kimataifa na sekta za kiutu kwa watanzania wote pasipo ubaguzi baina ya watu, kwa kutumia rasilimali mashine za kisasa na wataalamu wabobevu waliotokana na programu maalum pamoja na pesa zilizotolewa na serikali kuboresha miundombinu ya Taasisi hii.

Tanzania yetu ni moja; tofauti zetu ni sehemu ya demokrasia, na umoja wetu ndio msingi wa maendeleo yetu.

Tuukaribishe Mwaka 2026 kwa Amani na Mshikamano huku tukiwahakikishia kwamba kwa pamoja kesho itakuwa bora kuliko jana.




__

Tanesco Saccos leo imetoa msaada wa kuwasaidia wagonjwa wa Taasisi ya saratani ocean road gharama mbalimbali za matibabu...
31/12/2025

Tanesco Saccos leo imetoa msaada wa kuwasaidia wagonjwa wa Taasisi ya saratani ocean road gharama mbalimbali za matibabu kiasi cha shilingi milioni saba.

Mwenyekiti wa Tanesco Saccos Bw. Omari Shaaban amesema msaada huo waliotoa ni msingi wa Tanesco Saccos kurejesha kwa jamii kile kinachopatikana hususani kupitia katika sekta ya afya.

Bw. Omari Shaaban amesema kuwa kutoa msaada huo pia ni kupata baraka na kuepushwa na mabalaa mbalimbali na kuweza kufanya majukumu kwa ufanisi.

Aidha Bw. Omari ameahidi kuongeza bajeti zaidi ya kusaidia wagonjwa wengi kwa kadiri itakavyowezekana kwa mwaka ujao.

Kwa upande wake Meneja wa huduma za ustawi wa jamii wa Taasisi ya saratani ocean road Bw. Malkiory Niniko amesema msaada huo ni mkubwa na unadhihirisha ushirikiano wa kijamii kuwa ni nguzo muhimu katika kuimarisha mapambano dhidi ya saratani hapa nchini.

Bw. Niniko amewashukuru Tanesco Saccos kwa niaba ya Taasisi ya saratani ocean road na kutoa wito kwa vikundi,Taasisi na mtu mmoja mmoja kutoa misaada mbalimbali katika kupambana na maradhi haya ya saratani.

Address

Ocean Road, Luthuli Street
Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ocean Road Cancer Institute posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Ocean Road Cancer Institute:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram