29/04/2026
Taasisi ya Saratani Ocean Road inaendelea kutoa elimu pamoja na huduma za uchunguzi wa saratani katika viwanja vya Shule ya Sekondari Zimbwini, Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya Maonesho ya wiki Afya Kitaifa yanayoendelea mkoani humo.
Maonesho hayo yamelenga kuhamasisha wananchi kuhusu chanjo, bima ya afya kwa wote, pamoja na usafi wa mazingira.
Mgeni rasmi katika kilele cha maonesho hayo ni Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa.
Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Huduma za Uchunguzi wa Saratani na Elimu kwa Umma, Dkt. Maguha Stephano, amesema taasisi inaendelea kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuhakikisha wananchi wanapata Elimu kuhusu saratani, huduma za uchunguzi wa saratani mbalimbali pamoja na Chanjo zinazozuia maambukizi ya virusi vinavyosababisha saratani
Amesema kuwa huduma zinazotolewa ni pamoja na uchunguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi, Saratani ya matiti pamoja na Saratani ya tezi dume (kupitia kipimo cha damu)
Aidha wananchi wa Mkoa wa Pwani, hasa Wilaya ya Kibiti, wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hii muhimu kwa afya zao.