06/12/2022
Leo Ntashare na nyinyi kuhusu maswala Mazima ya uzazi na changamoto zake kwa ujumla.
Changamoto za uzazi zinaweza kuwa kwa mwanamke Au mwanaume lakini mara nyingi huonekana sana Kwa mwanamke kwasababu yeye ndio huwa na complications nyingi kuliko mwanaume.
♦️changamoto za uzazi Kwa mwanamke zinaweza kusababishwa na vitu vifuatavyo
-Mvurugiko wa hormone
-maambukizi kwenye via vya uzazi
-uvimbe
-mirija kuziba Au kuvimba
-makovu kwenye kizazi
-mayai kutopevuka na kuchevuka
-stress.
♦️mvurugiko wa hormones
-ili mwanamke aweze kushika ujauzito kirahisi ni lazima hormones zake Za k**e (ESTROGEN NA PROGESTERONE) ziwe kwenye uwiano
Unaotakiwa kwani hizi ndipo zinazocontroll mfumo mzima wa uzazi wa mwanamke. Swali kubwa hapa ni kujua k**a anapata Siku zake vizuri kwenye mpangilio mzuri, na damu anayoipata ipoje (iko na mabonge Au nyeusi n.k)
♦️maambukizi kwenye via vya uzazi
-haya ya husisha PID, UTI za mara Kwa mara Au Fangasi za mara Kwa mara
-iwepo wa bacteria Au Fangasi wabaya hakutengenezi mazingira rafiki kwa mbegu Za kiume kuishi Hata kwa mimba kutungwa.
♦️mirija kuziba Au kuvimba
-hali hii inakuwa inazuia mbegu Za kiume kuweza kutembea kulifikia yai na k**a zikifanikiwa kupita na kulifikia yai na kutungisha mimba basi kuna asilimia kubwa ya mimba kutungwa nje ya mfuko wa uzazi kwani mimba iliyotungwa hushindwa kujishikisha kwenye mji wa mimba na mwishie ubakia kwenye mirija (ECTOPIC PREGNANCY)
♦️makovu kwenye kizazi
-makovu haya mtu anaweza kuyapata kutokana na infection Za mara Kwa mara , k**a Alishakuwa na uvimbe halafu akafanyiwa operation Au alishawahi kutoka mimba.
-makovu haya pia huwa k**a kizuizi cha mbegu Za kiume kuflow kulifata yai
♦️mayai kutopevuka na kuchevuka
-hapa nipale ambapo yai linakuwa linatolewa ila linakuwa halijakomaa na haliwezi kutungishwa. Unaweza muuliza k**a huwa anapata ule ute wa siku Za hatari (sasa hapa alisema ndio muulize huwa anapata wa rangi gani maana wengi huwa hawajui ute wa ovulation ni upi, na akisema unarangi yoyote jua kwamba huwa Hapati ule ute kwani unatakiwa kuwa colorless Yani k**a maji na uwe unavutika)
♦️stress
-hii hupelekea hormones Za stress kuwa juu so anaweza kusema hana shida yoyote ila si kweli.