Muu health care

Muu health care Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Muu health care, Medical and health, Dar es salaam boko, Dar es Salaam.

Dady
27/01/2024

Dady

TATIZO LA NGUVU ZA KIUME :Leo katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa...
19/04/2021

TATIZO LA NGUVU ZA KIUME :

Leo katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, siyo Tanzania tu, bali duniani kote. Jambo muhimu analopaswa mwanaume yeyote kufahamu ni kwamba, kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa, ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili wake.

Kuna sababu zaidi ya 200 zinazosababisha mwanaume apungue nguvu za kiume. Mtu aweza kujiuliza kwa nini kuwe na sababu nyingi namna hiyo?

Nguvu za kiume ni nini?
Nguvu za kiume ni jina la jumla lenye vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na hamu ya mapenzi; kusimama kwa uume barabara; kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa; uwezo wa kurudia tendo la ndoa; pumzi, wepesi na uchangamfu wa mwili katika kutenda tendo la lenyewe.

Ni viungo gani vinavyohusika na nguvu za kiume?
Nguvu za kiume ni tukio pana sana lenye kuhusisha viungo na vitu vingi ndani ya mwili. Kuna zaidi ya viungo na vitu 50ndani ya mwili wa mwanaume vinavyohusika na nguvu za kiume ambapo viungo hivi pia hufanya kazi zingine za mwili. Baadhi ya viungo hivyo ni ubongo, moyo, mishipa ya neva mishipa ya ateri, mirija iliyo ndani ya uume iitwayo corpora cavernosa.

Viungo vingine ni neva maalumu za parasympathetic, tezidume (prostate gland), ini, figo, homoni ya testestorone, kemikali za acetylcholine, serotonin, na dopamine, uti wa mgongo, eneo la chini ya mgongo (kiuno), eneo la nyonga.

Viungo vingine ni misuli maalumu iitwayo pelvic floor, tezi pituitari (pituitary gland), utando maalumu wa uumeni uitwao tunica albuginea, misuli iitwayopubococcygeus [PC muscles], kemikali ya nitric oxide, kemikali ya prolactin n.k.

Nini maana ya kupungua nguvu za kiume?
Unapopungua nguvu za kiume ina maana ndani ya mwili wako kuna baadhi ya vitu katika vitu nilivyovitaja hapo juu havifanyi kazi vizuri jinsi ipasavyo na inavyotakiwa. Yawezekana ni figo ndilo halifanyi kazi vizuri, au ini, au tezi dume, au neva ya parasympathetic, au moyo una

CHANZO CHA CHUNUSI, AINA ZA CHUNUSI, MADHARA NA NJIA YA KUZIONDOA CHUNUSI NA MABAKA USONI;Chunusi ni ugonjwa wa ngozi am...
19/04/2021

CHANZO CHA CHUNUSI, AINA ZA CHUNUSI, MADHARA NA NJIA YA KUZIONDOA CHUNUSI NA MABAKA USONI;
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao hujitokeza k**a vivimbe/vipele vidogo vidogo hasa sehemu za uso,kifuani na hata mgongoni.Vipele hivi hutokea wakati vishimo vya kupitisha jasho katika ngozi vinapozibwa kwa mafuta au seli za ngozi zilizokufa au wadudu yaani Bacteria.
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi ambao humwathiri binadamu kwa kiasi kikubwa . Chunusi huweza kujitokeza katika umri wowote lakini huathiri sana vijana hasa wakati wa balehe Karibu asilimia 85 ya vijana kati ya umri wa miaka 12 hadi 25 hupata chunusi na zaidi ya asilimia 20 ya wanawake wenye umri wa zaidi ya miaka ishirini hupata chunusi wakati mwingine hata watoto wadogo pia huweza kupata chunusi hii ni tofauti na watu wengi wanavyofikiria kuwa chunusi ni dalili ya balehe.
Vipele vinaweza kuwa vidogo au vikubwa. Chunusi wakati mwingine husababisha mabaka katika ngozi hali hii hutokea pale ambapo seli za ngozi zilizoharibika huondolewa na seli mpya kutengenezwa.Ngozi mpya hutengenezwa kirahisi tu mahali palipokuwa na chunusi hali hii husababisha mlingano usiosahihi wa ngozi na hutoa kidonda ambacho baadaye hubaki k**a baka. Chunusi hutokea zaidi katika uso,kifua ,mabega na mgongoni.

Chanzo cha Chunusi

Chanzo halisi cha chunusi hakijulikani.hata hivyo baadhi ya vitu vinavyoongeza uwezekanifu wa kupata chunusi ni;
Umri
K**a nilivyosema( hormone)vikemikali hutolewa kwa wingi sana mtu anapofikia umri wa kubalehe.Kemikali hizi huongeza utengenezaji wa nta (sebum) katika ngozi ambayo huchochea kutokea kwa chunusi
Vipodozi
Baadhi ya vipodozi vya usoni(Make-up) za kina dada na Marashi(spray) za nywele zina mafuta ambayo yanaweza kusababisha chunusi kuwa nyingi zaidi.
Chakula
Chunusi hazisababishwi na chakula bali baadhi ya vyakula hufanya chunusi kuwa nyingi zaidi.Hasa vyakula vyenye mafuta.
Dawa
Chunusi zinaweza kujitokeza kutokana na kutumia dawa kadhaa k**a vile antibiotics,Vidonge vya uzazi wa mpango,Steroid ni dawa zeny

SABABU ZA UKE KUTOA HARUFU MBAYAFAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUTOA HARUFU MBAYA UKENINi matumaini nyote mnaendelea vyema,Le...
19/04/2021

SABABU ZA UKE KUTOA HARUFU MBAYA
FAHAMU SABABU ZA MWANAMKE KUTOA HARUFU MBAYA UKENI
Ni matumaini nyote mnaendelea vyema,
Leo naona ni bora tukazungumzia tatizo la kutokwa na harufu mbaya ukeni maana watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajuhi kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni,leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,
~kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo
~majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nnje ya mwili pia huvikinga viungo vya uzazi dhidi ya maaambukizi ya bacteria
~Kwa kawaida huwa hayatoi harufu na huwa hayawashi na huwa na rangi nyeupe au njano pia huwa na asidi ya LACTIN ambayo huzuia bacteria kuzaliana
~mwanamke hutoa kiasi cha grams 2 za seli zilizokufa kutoka kwenye mji wa kizazi na grams 3 za ute mwepesi kila siku, kiwango hicho kinaweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mzunguko wa hedhi pia Kuna wakati ute huwa mwepesi na unaovutika na Kuna wakati pia huwa mzito wa rangi ya njano hautoi harufu
VISABABISHI VYA TATIZO HILI
~sababu za kutokwa na uchafu ukeni una vyanzo vingi sana vifuatavyo ni vyanzo vya tatizo hili
(1)BACTERIA VAGINOSIS
~Chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijafanikiwa kuwa wazi,kinachotokea ni kuongezeka kwa ghafla kwa idadi ya ya bacteria hawa na kubadilisha uwiano wa kawaida katika mazingira ya uke, wanawake wenye wapenzi wengi na wanaofanya mapenzi kwa njia ya mdomo Wana hatari ya kupata tatizo hili

AFYA NI Tumain BORAMIMBA KUHARIBIKAMIMBA CHANGA (ndani ya miezi3) KUHARIBIKIWA, CHANZO NA SABABU, DALILI NA NINI UFANYE ...
19/04/2021

AFYA NI Tumain BORA
MIMBA KUHARIBIKA

MIMBA CHANGA (ndani ya miezi3) KUHARIBIKIWA, CHANZO NA SABABU, DALILI NA NINI UFANYE ILI KUZUIA ISITOKEE TENA

Somo hili ni refu na kwa hiyo limegawanyika sehemu kuu tatu
1- Dalili za mimba kuelekea kuharibikiwa
2- Chanzo na sababu za mimba kuharibika
3- Nini cha kufanya ikiwa huwa unapatwa na hali hiyo mara kwa mara.

SEHEMU YA KWANZA

Ni kawaida sana mimba kutoka au kuharibika bila kukusudia au bila wewe kujua k**a imetoka au inakaribia kutoka. Wakati mwingine hutoka tu bila sababu yeyote na hata k**a utapimwa na vifaa vya kisasa kabisa bado sababu za mimba kuharibika hazitajulikana. Ikiwa utajua ya kwamba mimba imetoka
CHAKWANZA ni vizuri kujua sababu ya mimba hiyo kutoka, hasa k**a imeharibika kwa mara ya pili na zaidi. Sababu zinaweza kuwa nyingi k**a vile utakavyo ona katika aya zifuatazo hapo chini, kuna sababu za kijamii na kiafya. Sababu za kijamii zitafutiwe ufumbuzi kijamii, mfano mtu amelaaniwa (hapo k**a una amini katika dini) huwezi tena kupona kwa kutumia dawa, lazima ufunguliwe na kifungo hicho kwanza.
CHA PILI kupambana na icho kisababishi, baada ya kupima na kupata ushauri basi itakufaa sasa upate dawa au kufuata ushauri uliopewa, ukimaliza dozi rudi hospitalini ili uweze kujua k**a umepona kabisa au la. Kunayo tabia ya watu wengi tu askisha maliza dozi ndio inakuwa basi anaendelea na Maisha yake, hapo unakuwa unakosea. Jitahidi kurudi hospital na kupima tena upate uhakika wa tatizo k**a limeisha au la. K**a halijaisha inakuwa rahisi kwa daktarin kuchua vipimo vingine au kukupa dawa ingine.
CHA MWISHO ni kujaribu tena kubeba mimba, baada ya kuona mambo yote yako sawa, au sasa unaamini uko vizuri basi unajaribu tena kupata mimba. Zingatia siku zako za uzazi, na zingatia kupika vyakula vizuri ili mume wako apate nguvu ya kutoa mbegu nyingi na zenye afya njema. Usafi pia wa mwili na kitanda ni muhimu. Usinuke na kutoa harufu mbaya.
Mara nyingi swala la kwanza na pili watu huruka na kuendelea nakutafuta mimba. njoo

UJUE UGONJWA WA U.T.I (URINARY TRACT INFECTION)U.T.I ni maambukizi kwa njia ya mkojo na huathiri mfumo wa mkojo na mfumo...
18/04/2021

UJUE UGONJWA WA U.T.I (URINARY TRACT INFECTION)

U.T.I ni maambukizi kwa njia ya mkojo na huathiri mfumo wa mkojo na mfumo wa uzazi, wadudu huathiri sana kibofu na urethra. Jina U.T.I ni kifupi cha URINARY TRACT INFECTION (Neno la kingereza) watu wengi huzoea kuita hivyo wakijua ni jina la kiswahili, imeshazoeleka hivyo. Jinsia ya k**e wana hatari kubwa kuliko jinsia ya kiume. Maambukizi yakwenye kibofu huleta maumivu makali, madhara makubwa hutokea maambukizi yakifika mpaka kwenye figo. U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo.

U.T.I hutibika haraka kwa mtu ambaye atatumia dawa na pia yaweza kuleta madhara makubwa isipotibika huweza kuathiri mfumo wa uzazi, kibofu, na sehemu mbalimbali, tunashauri mtu mwenye U.T.I inatakiwa awe msafi na kubadili mienendo iliyo hatarini.
CHANZO CHA MAAMBUKIZI YA U.T.I

U.T.I husababishwa na wadudu wadogo sana ambao ni bakteria waitwao Escherichia coli (E. coli), wanapoingia mwilini na kuenda kuathiri mfumo wa mkojo, vitu vifuatavyo vinaweza kukuingiza kwenye hatari ya kupata U.T.I;

Kinga ya mwili kuto kuwa imara
Kutumia Vifaa au Dawa za kuzuia mimba
Kwa wa k**e; Kupungua kwa homoni ya estrogeni
Mtu mwenye kisukari
Kutumia choo kichafu na kutumia idadi kubwa ya watu
Kuwa na tatizo la mmeng’enyo na tatizo la choo
Kukaa kwa mda mrefu bila kutembeatembea
Kujihisi mchovu na kutokujisikia vizuri
Kukojoa kwa shida na kujilazimisha
Maumivu wakati wa kukojoa
Kukojoa kiasi kidogo na mara kwa mara
Mkojo kutoa harufu kali
Mkojo kuwa na rangi tofauti zisizo za kawaida kwa mfano wekundu kiasi
Kichefuchefu au kutapika
Maumivu ya tumbo, au pande za mwili karibu na tumbo mpaka sehemu za misuli
Joto laweza kuongezeka
JINSI YA KUEPUKANA NA U.T.I

Kunywa maji mengi
Acha kutumia dawa za uzazi wa mpango
Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali
Kojoa hata kidogo baada ya kujamiiana
Punguza au acha kunywa pombe na kutumia

JWA WA FANGASI ZA UKENI/ SEHEMU ZA SIRI(VAGINAL THRUSH)Ndugu zangu naomba nielezee kuhusu mwanamke na uke,kwa maana yaUK...
18/04/2021

JWA WA FANGASI ZA UKENI/ SEHEMU ZA SIRI
(VAGINAL THRUSH)

Ndugu zangu naomba nielezee kuhusu mwanamke na uke,kwa maana ya

UKE ni kiungo cha uzazi wa mwanamke, ambamo ndani yake kuna Lactobacillus bacteria na fangasi wazuri abao wako katika kiwango kinacho lingana/a balanced mix. Bacteria hawa na fangasi hizi husaidia sana kuulinda uke na maradhi mbalimbali endapo uwiano wake hauta bughuziwa. LActobacillus bakteria hutoa acid ambazo huzuia fangasi kukuwa au kuwa wengi zaidi.

UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI ni ugonjwa anaoupata mwanamke endapo fangasi watakuwa wengi zaidi ya bacteria wazuri waliopo ukeni au k**a pH ya ukeni imezidi kiwango cha kawaida kinachopaswa(pH 3.5-4.5 ndio kiwango kizuri kiafya).

FANGASI ZA UKENI MARA NYINGI HUSABABISHWA NA FANGASI WAITWAO CANDIDA ALBICANS, LAKINI WAKATI MWINGINE NI AINA NYINGINE ZA FANGASI NA HIZI NI VIGUMU SANA KUTIBIKA

VITU VINAVYOWEZA KUSABABISHA UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI

kunasababu nyingi sana baadhi ya hizo ni;

1.MATATIZO YA HOMONI(HOMONI ZA KUBADILIKA/KUWANYINGI SANA AU KUSHUKA SANA) hii inaweza kusahabishwa na; ukomo wa hedhi,ujauzito, (MP)kuwa katika siku za mwezi, matumizi ya dawa za kuongeza kiwango cha hormon za k**e

2. MATUMIZI YA ANTIBIOTICS hizi huuwa bacteria wazuri na kubadiri ph ya uke

3.KUFANYA MAPENZI NA MTU ALIYE NA UGONJWA WA FANGASI ZA SEHEMU ZA SIRI BILA KINGA

4.KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI hii inaweza kusababishwa na magonjwa mbalimbali k**a UKIMWI, KISUKARI, UPUNGUFU WA MADINI,VITAMINI NA VIRUTUBISHI MBALIMBALI VYA MWILI.

5.ULAJI MBAYA HASA KUPENDELEA VYAKULA VYENYE SUKARI KWA WINGI (SUKARI NI CHAKULA KWA FANGAS HIVYO HUONGEZEKA).

6.KUKOSA USINGIZI NA MSONGO WA MAWAZO .

DALILI ZINAZOONESHA KUWA UNAUGONJWA WA FANGAS ZA UKENI

Kuna dalili nyingi sana k**a zifuatavyo;

~MUWASHO SEHEMU ZA SIRI

~VIPELE VIDOGO VIDOGO UKENI

~KUTOKWA UCHAFU MWEUPE AU WA RANGI YA KIJIVU UKENI WENYE HARUFU MBAYA

~VIDONDA AU MICHUBUKO UKENI

~KUYOKWA NA HARUFU MBAYA UKENI

~KUPATWA NA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA

UJUE UGONJWA WA BAWASILI, MADHARA YAKEBawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika...
18/04/2021

UJUE UGONJWA WA BAWASILI, MADHARA YAKE
Bawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba.Bawasiri husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.

A.NINI KINASABABISHA BAWASIR ?
Miongoni mwa visababishi vya bawasir ni;
-Tatizo sugu la kuharisha
-Kupata haja kubwa(kinyesi)kigumu
-Uzito kupita kiasi(OBERSITY)
-Ngono ya njia ya haja kubwa(ANAL S*X)
-Umri mkubwa na mambo yanayoongeza shinikizo katika tumbo.
B.DALILI ZA BAWASIR
-Kinyesi kuchanganyika na damu wakati wa kujisaidia
-Maumivu au usumbufu katika njia ya haja kubwa
-Kutokwa na kinyesi bila kujitambua(kuvuja kinyesi)
-Kijiuvimbe katika eneo la tundu(mlango)wa kutolea haja kubwa.
-Ngozi katika eneo la tundu la haja kubwa kuwasha.
-Bawasir kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa.
C.ATHARI ZA BAWASIR
-Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
-STRAGULATED HEMORRHOID
-Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
-Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
-Kuathirika kisaikolojia
-Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
-Kupungukiwa nguvu za kiume

UJUE UGONJWA WA BAWASILI, MADHARA YAKEBawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika...
18/04/2021

UJUE UGONJWA WA BAWASILI, MADHARA YAKE
Bawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba.Bawasiri husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.

A.NINI KINASABABISHA BAWASIR ?
Miongoni mwa visababishi vya bawasir ni;
-Tatizo sugu la kuharisha
-Kupata haja kubwa(kinyesi)kigumu
-Uzito kupita kiasi(OBERSITY)
-Ngono ya njia ya haja kubwa(ANAL S*X)
-Umri mkubwa na mambo yanayoongeza shinikizo katika tumbo.
B.DALILI ZA BAWASIR
-Kinyesi kuchanganyika na damu wakati wa kujisaidia
-Maumivu au usumbufu katika njia ya haja kubwa
-Kutokwa na kinyesi bila kujitambua(kuvuja kinyesi)
-Kijiuvimbe katika eneo la tundu(mlango)wa kutolea haja kubwa.
-Ngozi katika eneo la tundu la haja kubwa kuwasha.
-Bawasir kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa.
C.ATHARI ZA BAWASIR
-Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
-STRAGULATED HEMORRHOID
-Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
-Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
-Kuathirika kisaikolojia
-Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
-Kupungukiwa nguvu za kiume. kwa msaada

Address

Dar Es Salaam Boko
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Muu health care posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram