25/01/2025
UMUHIMU wa MAJI KIPINDI Cha UJAUZITO.
Maji ni kimiminika muhimu sana kwenye mwili wa binadamu. Kazi nyingi zinazofanyika mwilini huhitaji maji ili zikamilike Mfano; Mmeng'enyo wa chakula, usafirishaji wa chakula kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, na kazi nyingine nyingi.
Kwa kifupi tunaweza kusema bila maji, mwanadamu hana kitu (amekufa).
Ikiwa maji yana kazi nyingi hivyo kwenye mwili wa mtu asiye na UJAUZITO, vipi kwa mama mjamzito? Na kwa Nini mahitaji ya maji kwa mama mjamzito yanaongezeka?
Baki nami tulidadavue hilo swala mtambuka.
Awali ya yote tunapaswa kujua kuwa tunapata maji(maji yanaingia mwilini mwetu) kwa njia mbalimbali, k**a;
1. Vyakula Mfano, Tikiti maji, Madafu,
2. Kunywa maji
3. Vinywaji Mfano,soda, juisi, n.k
4. Kuongezewa maji ukiwa mgonjwa n.k
5. Maji ya ndani ya miili yetu
Pia maji hayo yanatoka mwilini mwetu kwa njia tofauti tofauti ikiwemo kwa njia ya mkojo, jasho, kupumua (mdomoni au puani) na njia ya haha kubwa.
Kwa kawaidi miili yetu inaweza kubalansi kiwango Cha maji kinachoingia na kinachotoka.
Kipindi cha UJAUZITO Huwa Kuna mabadiliki mengi ya kimwili. Mfano wa mabiliko hayo ni uwepo wa kondo la nyuma, kuongezewa kwa ukubwa wa mfuko wa mimba, mabadiliki ya kwenye Figo na mengine mengi.
Kiwango Cha damu (blood plasma) huongezeka taratibu kuanzia wiki ya sita Hadi ya nane na kufikia kiwango chake Cha juu kwenye wiki ya 34. Ikiwa sehemu kubwa ya damu ni maji (83%), hivyo mama mjamzito ni vyema akaongeza unywaji wa maji ili kufidia ongezeko hilo.
Vilevile kiwango Cha upumuaji huongezeka kwa 40%, kasi ya kutokwa na jasho huongezeka, urination rate pia huongezeka ; hayo oyte hupoeteza maji kwa haraka sana,basi mama mjamzito anapaswa kunywa maji ya kutosha angalau glass 6 Hadi 8 kwa siku Moja ili kufidia upotevu huu wa maji.
Pia mahitaji ya virutubisho huongezeka kipindi cha UJAUZITO. Ili kusafirisha virutubisho hivyo,maji yanahitajika.
Mabadiliko hayo yote husababisha ongezeko la mahitaji ya maji mwilini.
K**a hutopata maji ya kutosha kipindi cha UJAUZITO unaweza kusababisha mtoto kuzaliww akiwa na uzito mdogo (chini ya 2•5Kg). Pia Kuna tafiti huko California ilionesha kuwa ukinywa maji mengi unasaidia kuongeza kiwango Cha maji ya uzazi(Amniotic fluid).
American institute of medicine wanapendekeza mama mjamzito anywe angalau 2.7L kwa siku huku shirika la afya duniani linapendekeza 4.8L kwa siku.
Tuhitimishe kwa kusema, maji ni muhimu sana kwenye kipindi cha UJAUZITO . Akina mama wasizembee kunywa maji au kula vyakula vyenye maji mengi.
Sauti ya mtoto aliye tumboni: "Mama kunywa maji ya kutosha, naona kiu."
Imeandaliwa na;
Godlove Ituga
0652700929