24/04/2023
TEZI DUME
Tezi dume ni kiungo kidogo na ni sehemu moja ya uzazi ya wanaume. Hupatikana chini ya kibofu na mbele ya mwanzo ya njia itoayo mkojo hupitia ndani ya tezi dume. Tezi dume ndiyo hutoa maji yabebayo mbegu (manii) kwa ajili ya utungishaji mimba.
Tezi dume hutanuka, mtu mwenye tezi dume iliyotanuka anaweza kuwa na saratani pia, hii huitwa saratani ya tezi dume.
DALILI ZA TEZI DUME
-Kukojoa mara nyingi hasa nyakati za usiku.Hii ni dalili ya mapema sana.
-Kulazimika, mara nyingi hasa nyakati za usiku
-kutumia nguvu kuanzisha mkojo kutoka. Hata pale mgonjwa anahisi kibofu kimejaa. Hii ni dalili ya mapema sana.
-Mkojo kutiririka polepole, hukatika katika na hutumia nguvu kutoka.
-Mkojo kushidwa kutoka hata wakati mtu anapohisi kukojoa.
-Mkojo kuendelea kutoka kidogokidogo baada ya kukojoa, matone ya mkojo huendelea kutoka hata baada ya kukojoa hivyo nguo za ndani hulowa.
-Kibofu hakiishi mkojo.
Tezi dume ikitanuka sana huleta matatizo mengi kwa wagonjwa wengine hali hii isipotibiwa. Matatizo hayo ni k**a yafuatayo:
♤Mkojo kukosa kutoka kabisa
Wagonjwa wenye tatizo hili lazima wawekewe katheta ili kumimina mkojo.
♤Madhara kwenye kibofu na figo
Kwa sababu ya kibofu kuwa na mkojo wakati wote, ukuta na misuli yake hupanuka na mwishowe hudhoofika hivi kwamba haiwezi kuzuia mkojo.
Kwa sababu ya kibofu kujaa
mkojo hurudi kwenye figo na mwishowe huharibu figo.
Tezi dume inatibika bila upasuaji. Wasiliana nasi kwa ushauri na tiba kupitia WhatsApp number 0747 995 343