Brightfuture center

Brightfuture center Na wasaidia watu wenye changamoto za kiafya kwa tiba mbadala

10/09/2024

K**a unaaangalia post hii unatamani uitwe mama. Zamu yako imekalbia Mungu wetu sote🙏

09/09/2024

Sababu za kuziba kwa mirija ya uzazi

Kuziba kwa mirija ya uzazi ni tatizo linaloweza kuathiri uwezo wa mwanamke kupata mimba. Kuna sababu mbalimbali zinazochangia kuziba kwa mirija hii, na zifuatazo ni baadhi ya hizo:

Maambukizi: Maambukizi ya bakteria katika viungo vya uzazi, k**a vile nyumba ya uzazi, yanaweza kusababisha makovu ndani ya mirija ya uzazi. Haya makovu yanaweza kuzuia mchakato wa usafirishaji wa kijiyai na mbegu za kiume.

Endometriosis: Hali hii inahusisha ukuaji wa tishu za endometrial (tishu zinazofunika ndani ya nyumba ya uzazi) mahali pengine nje ya nyumba ya uzazi. Tishu hizi zinaweza kujipachika kwenye mirija ya uzazi na kusababisha kuziba.

Magonjwa yanayoenea kwa njia ya kujamiiana: Magonjwa k**a kisonono (Gonorrhea) na klamidia yanaweza kushambulia maeneo ya viungo vya uzazi, hivyo kuchangia kuziba kwa mirija.

Upasuaji: Kuwahi kufanyiwa upasuaji katika eneo la kiuno au nyumba ya uzazi kunaweza kuacha makovu ambayo yanashik**ana na mirija, hivyo kusababisha kuziba.

Uvimbe wa Fibroid: Uvimbe huu unaweza kukua na kuzuia njia za mirija, hasa pale unapojichimbia karibu na maeneo hayo.

Ectopic Pregnancy: Mimba inayokua katika mirija badala ya nyumba ya uzazi inaweza kusababisha uharibifu wa tishu na makovu baada ya upasuaji.

Vifaa visivyo safi: Matumizi ya vifaa visivyo safi wakati wa kusafisha nyumba ya uzazi au kufanya upasuaji kunaweza kuleta maambukizi ambayo yanachangia kuziba.

Mambo mengine hatarishi: Haya ni pamoja na uvamizi wa maambukizi mwilini, kupasuka kwa kidole tumbo, au ajali ambazo zinaweza kuathiri maeneo haya.

Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango: Ingawa siyo sababu kubwa sana, matumizi haya yanaweza kuchangia matatizo fulani yanayohusiana na mfumo wa uzazi.

Kujifungulia maeneo yasiyo salama: Hii inaweza kusababisha majeraha au maambukizi ambayo yanachangia kuziba kwa mirija.

Kwa ujumla, tatizo la kuziba kwa mirija ya uzazi linaweza kuwa na madhara makubwa ikiwa ni pamoja na ugumba kwa wanawake kutokana na kushindwa kwa mbegu za kiume kurutubisha kijiyai cha kike.

Madhara yanayo sababishwa na kisukari
09/09/2024

Madhara yanayo sababishwa na kisukari

17/09/2023

TIBA YA MIFUPA NA MAUNGIO YA MIFUPA MGONGO KIUNO

Watu wengi wenye umri wa miaka 30 na kuendelea hupata matatizo ya maungio ya mifupa. Hii husababishwa na jinsi tunavyoishi,
▪️ kutopata lishe bora,
▪️ kufanya mazoezi bila kuzingatia namna ya kulinda maungio,
▪️ kufanya kazi nzito,
▪️ kuwa na uzito mkubwa wa mwili,
▪️mwilli kupoteza uwezo wake wa kutengeneza ute kwenye maungio ambayo inatokana na umri na sababu zingine za kiafya.

Hii hupelekea kuwa na maumivu makali mpaka kushindwa kutembea au kusogeza baadhi ya viungo.

Inawezekana hata wewe umeshaanza kuzisikia athari za haya matatizo ila wengi hua wanagundua kwa kuchelewa sana sababu hatuna desturi ya kukagua afya zetu mara kwa mara. Ila pia inawezekana kuna mtu unamfahamu ambaye tayari ameanza kupata athari zake.

Usikae kimya suluhisho lipo,Tuna tiba asili kabisa na maalumu kwa ajili ya kuondoa maumivu ya viungo na mifupa, kuzuia kulika kwa mifupa na viungo.
1.Huongeza ute ute kwenye maungio.
2.Huondoa changamoto ya Arthritis.
3.Huzuia kulika na kusagana kwa maelezo zaidi kuhusu Afya yako wasiliana nami kwa What'sApp no 0623928663

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Brightfuture center posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram