
17/05/2025
Usidanganywe na Rangi: Ukweli Kuhusu matikiti yaliyotiwa Rangi Bandia
Je, umewahi kujiuliza k**a tikitimaji unalonunua sokoni ni salama kweli kuliwa? Linaonekana tamu na nyekundu, lakini je, hiyo rangi ni ya asili au imeongezwa kwa kemikali.
Uchakachuaji wa tikitimaji uhusisha vitendo vya kuongeza au kubadilisha sifa za tikitimaji ili lionekane bora zaidi sokoni. Baadhi ya wauzaji huongeza rangi, maji au kemikali za kuharakisha uivaji kwa lengo la kuvutia wanunuzi au kuongeza faida.
Erythrose (E127)
Ni rangi ya bandia ambayo huwekwa kwenye matikiti ili yaonekane na rangi nyekundu zaidi, hata k**a halijaiva vizuri. Rangi hii ni aina ya kemikali ambayo hapo kabla ilitumika kwenye baadhi ya vipodozi ,vyakula na dawa, lakini si salama kwa matumizi kwenye vyakula na matunda yakiwemo matikiti kwani ilipigwa marufiku na mamlaka ya chakula na dawa marekani ( FDA ) January 2025 . Hii ni kwasababu ilionekana kusababisha madhara k**a matatizo ya homoni ,msisimko na hata kansa iwapo itatumika kwa kiwango kikubwa.
SULUHISHO
Tumia njia hizi Mbili kujua
I)Tumia pamba au kitambaa cheupe . Kata tikitimaji na upake sehemu nyekundu kwa kutumia pamba nyeupe au kitambaa . Ikiwa pamba itapata rangi, linaweza kuwa limeongezwa kemikali.k**a rangi itaacha doa, hilo tikitimaji si salama.
II) Angalia rangi ya juisi ya tikitimaji: ikiwa ni nyekundu sana au inaacha mabaki mekundu, kuna uwezekano mkubwa wa kuwa limechakachuliwa.
# Afya yako ni muhimu usidanganywe na rangi ya tikitimaji , Chagua tikitimaji la asili #