02/01/2026
Ukiona haya ujue uko rijali huna haja ya kuzini kutest
Hili somo ni kwa kijana ambaye bado hujaoa.
Sio kwa kubembeleza, bali kukuweka sawa kichwani.
Kwanza elewa hili wazi kabisa:
Huna kitu cha kuthibitisha kwa mtu yeyote.
Sasa sikiliza kwa umakini.
K**a unavutiwa na wanawake, unahisi mvuto wa kawaida, unatambua uzuri bila kulazimisha tamaa — hiyo ni ishara nzuri.
K**a unasimamisha asubuhi vizuri, mara kwa mara — hiyo ni dalili ya wazi kuwa mfumo wako wa homoni uko sawa. Testosterone ipo kazini. Mwili wako uko normal.
Hapo tayari uko sawa.
Hakuna cha kuongeza.
Hakuna cha “kutest”.
Uongo unaouzwa mitaani ni huu:
“Kijana asipojaribu mapema atakuja kushindwa.”
Huo ni upotoshaji.
Ukweli ni huu 👇
Kuzini hakuthibitishi nguvu za kiume.
Mara nyingi kunathibitisha hofu, presha ya marafiki, na kukosa mwelekeo.
Kijana mwenye akili:
• Anaondoa woga
• Anaacha kuji-compare
• Anafocus na mambo ya msingi: masomo, kazi, afya, nidhamu
Ngono ni ujuzi unaojifunza, sio mtihani wa barabarani.
Ukija kuoa;
• Utajifunza taratibu mbinu za kivita
• Utakuwa mtulivu
• Itakuwa tamu zaidi kwa sababu haijaambatana na hatia, presha, wala woga
Kumbuka hili na uliweke moyoni:
Nguvu ya mwanaume haipo kwenye haraka.
Ipo kwenye udhibiti wa tamaa, afya ya mwili, na mwelekeo wa maisha.
Ukizingatia haya leo,
kesho utanishukuru.