26/02/2026
*MOLAR PREGNANCY* (Mimba Zabibu/ Mimba hewa: hii ni aina ya mimba ambayo hutokea endapo mbegu ya kiume imerutubisha yai la k**e ambalo halina kiini au hata k**a yai hilo lina kiini basi kiini ambacho hakija kamilika vizuri.
Lakini pia huweza kutokea endapo mbegu mbili za kiume kuweza kurutubisha yai moja la k**e kwa wakati mmoja. Matokeo yake kuna kuwa na mgawanyiko usio sahihi wa kondo la nyuma na kijusi pia.
Mimba zabibu ni kati ya aina ya magonjwa ya mimba yanayoweza kujitokeza wakati seli za uzazi (mbegu ya mwanaume na mwanamke) kuungana na kutengeneza mimba isiyokuwa kamilifu.Tatizo hili hujitokeza kwa nadra sana lakini linaweza kuleta changamoto kubwa sana kwa muhusika.
Yai kutokuwa na kiini hutokea hasa pale homoni za kuzalisha mayai zinaposhindwa kupevusha mayai kwa kiwango kinachotakiwa na kuruhusu yai hilo hilo ambalo halijapevuka kukutana na mbegu za kiume kurutubishwa iwe mimba.
*MATIBABU YAKE.*
Ugonjwa huu unaweza kutibika na moja kati ya tiba inayotolewa ni kusafishwa mji wa mimba. Tiba zake zinakuwa na mafanikio makubwa k**a tatizo hili litajulikana mapema. Pale tatizo linapo chelewa kujulikana, linaweza likaleta madhara makubwa kwa afya ya mama.
Tiba hii itaambatana na kufanyiwa Ultrasound na vipimo vya homoni za mimba kabla na baada ya kusafishwa.
Katika kipindi cha matibabu utashauriwa usibebe mimba kwa mda usio pungua miezi 6 mpaka mwaka mmoja ili kuhakikisha hali ya kizazi ipo salama, homoni ziko salama na utulivu wa fikra wa mama.
*NYONGEZA.*π
1. Unapojihisi umebeba mimba, fika hospitali mapema kwa ajili ya vipimo.
2. Kumbuka kwamba, sio kila mwenye tatizo hili anakuwa na dalili na sio kila dalili inaashiria tatizo, hivyo njia sahihi ni kufanya vipimo.
2. Ugonjwa huu hauna kinga na k**a ulishawahi upata upo na nafasi nyingine ya kuupata tena.
3. Tumia juisi zetu ili kusafisha kizazi, kuondoa changamoto za Uzazi na kuweka homoni sawa ili ubebe ujauzito kiurahisi na mimba iliyo salama.
4. Anza Kliniki mara baada ya kujua kuwa wewe ni Mjamzito kwani ugonjwa huu usipofanyiwa tiba sahihi unaweza ukabadilika na kuwa saratani (cancer) inayo julikana k**a choriocarcinoma.
Je, uliwahi kupata changamoto ya mimba zabibu (Molar Pregnancy)?
SEBA Herbal clinic