Furaha kwa wote

Furaha kwa wote Mental health campaign with the message "resilience with love and kindness is mental health".

The aim is to raise awareness about realities of mental health through art. We promote resilience to improve self-esteem and challenge stigma and discrimination

07/02/2025

Ungana nasi katika kampeni ya "furaha kwa wote" tujifunze kwa pamoja maswala ya afya ya akili ili tujue mbinu za kustawisha akili zetu na kukabiliana na changamoto zake.

Kutana na wataalamu mbali mbali wa maswala ya afya ya akili.

CHANGAMOTO ZA AFYA YA AKILI  - Ni ishara za ndani za wasiwasi, msongo wa mawazo, makasiriko, huzuni au ghadhabu ambazo m...
05/02/2025

CHANGAMOTO ZA AFYA YA AKILI - Ni ishara za ndani za wasiwasi, msongo wa mawazo, makasiriko, huzuni au ghadhabu ambazo mwanadamu anazipitia katika kipindi ambacho anakabiliwa na jambo la kutatua.

You can also follow on Instagram to see more about mental health awareness..

04/02/2025

Kampeni ya "furaha kwa wote" inalenga kujenga uelewa kwa jamii juu ya maswala ya afya ya akili.

Ungana nasi kuhamasisha ustahimilivu na furaha kwa kila mmoja wetu.

Asante UTT Amis kwa kusaport kampeni hii.

UTT AMIS






21/01/2025

Ustahimilivu katika upendo ndo wema ni afya ya akili.

23/12/2024

Kuna nyakati tunapitia magumu kiasi kwamba unahitaji japo mtu wa kukupa moyo, lakini hakuna hata mmoja anayekutizama kwa namna hiyo bali anaridhishwa na tabasamu unaloonesha.

Usikate tamaa, kuwa mstahimilivu, jiamini na ujithamini kwani ndio njia pekee ya kuwa thabiti.

Dax Nation Dax




Faida za "umakini wa akili" ni pamoja na:-1. Kupunguza kuwaza kupita kiasi2. Kuimarisha kumbukumbu ya kufanya kazi.3. Ku...
07/11/2024

Faida za "umakini wa akili" ni pamoja na:-
1. Kupunguza kuwaza kupita kiasi
2. Kuimarisha kumbukumbu ya kufanya kazi.
3. Kupunguza athari za kihisia
4. Kubadilika zaidi kiakili
5. Kurudhika zaidi katika mahusiano.



TipsMental Health FoundationPositive Thoughts, Love Peace and Joy for All
03/11/2024

Tips

Mental Health Foundation

Positive Thoughts, Love Peace and Joy for All

Malezi ya mzazi mmoja yamekuwa changamoto inayoongezeka kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni, na hali hii imekuwa chan...
02/10/2024

Malezi ya mzazi mmoja yamekuwa changamoto inayoongezeka kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni, na hali hii imekuwa chanzo kikubwa cha kuchanganya na kuondoa utulivu wa akili kwa wazazi na watoto wanaohusika.

Athari za malezi ya mzazi mmoja zinajitokeza kwa pande zote mbili – mzazi na mtoto. Kwa mzazi, iwe ni mama au baba, changamoto za kubeba majukumu peke yake husababisha msongo wa mawazo na kuchoka kiakili. Kwa sasa, inadhaniwa kuwa mama ndiye anayekumbana na mzigo mkubwa zaidi kutokana na hali hii. Kwa upande wa mtoto, athari ni kubwa, kwani kukua bila mzazi mmoja kunamnyima fursa ya kupata mitazamo na ushawishi wa aina mbalimbali, hali ambayo inaweza kuathiri ustawi wake wa kiakili na kijamii.

Kulea au kulelewa na mzazi mmoja kunaweza kuhatarisha afya ya akili ya pande zote. Inahitajika juhudi ya ziada kuhakikisha kuwa jamii haijiingizi kwenye mtego huu wa kuishi bila kujali athari, hasa katika mazingira ya sasa ya utandawazi yanayowafanya watu kuchukulia mambo kwa urahisi.

Ikiwa tuna afya bora ya akili, tuna uwezo wa kuboresha mahusiano yetu, kuona umuhimu wa malezi ya pamoja, na kuchangia katika kuunda familia imara. Ni muhimu tutambue kuwa watoto wetu wanahitaji malezi kutoka kwa wazazi wote wawili ili waweze kukua katika mazingira yanayowapa usalama na usaidizi wa kiakili.

Tunapenda kusikia kutoka kwako. Tafadhali shiriki nasi katika ukurasa huu kwa kutoa maoni yako juu ya mambo unayodhani yanachangia kuvunjika kwa familia na kusababisha mzazi mmoja kubaki na jukumu la malezi. Maoni yako yatatusaidia kuelewa zaidi na kutafuta njia bora za kuboresha maisha ya familia na jamii kwa ujumla.

Kazi ni kielelezo cha mwanadamu kutimiza wajibu wake kulingana na malengo aliyojiwekea. Iwe umeajiriwa au umejiajiri, dh...
01/10/2024

Kazi ni kielelezo cha mwanadamu kutimiza wajibu wake kulingana na malengo aliyojiwekea. Iwe umeajiriwa au umejiajiri, dhamira kuu ni kujipatia mahitaji muhimu.

Mazingira ya ajira yanaweza kuleta hamasa au kukatisha tamaa ya kutimiza majukumu. Kwa hiyo, ni muhimu kuhakikisha akili inakuwa katika hali nzuri na yenye utayari muda wote.

Changamoto za kiakili zimekuwa zikiongezeka kwa kasi katika maeneo mengi ya kazi, na hii imewafanya baadhi ya watu kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo.

Sasa, tushirikiane: Ni nini hasa kinachokufanya ukose utimamu wa kiakili unaopelekea kupoteza hamasa ya kufanya kazi?

Kuna mstari mwembamba sana kati ya upendo na chuki.Upendo unapaswa kuwa wa pande zote—iwe ni kutoka kwa wazazi kwenda kw...
30/09/2024

Kuna mstari mwembamba sana kati ya upendo na chuki.

Upendo unapaswa kuwa wa pande zote—iwe ni kutoka kwa wazazi kwenda kwa mtoto, kati ya ndugu, au kati ya marafiki. Lazima kuwe na uwiano sawa ili kuepusha migongano ya kihisia.

Wakati mmoja anapoonyesha upendo, na mwingine anabaki tu kupokea bila kutoa hisia yoyote, hali hii huweza kupelekea mgogoro wa kihisia. Mgogoro huo, bila tahadhari, unaweza kusababisha chuki kubwa inayoweza kusambaratisha mahusiano.

Mgogoro wa kihisia unaweza kuathiri utulivu wa akili. Akili isipokuwa sawa, maamuzi yasiyo ya busara yanaweza kutokea na kusababisha matatizo katika jamii yetu.

Ni jukumu letu kuonyesha ustahimilivu katika mapungufu yetu, kupeana nafasi, na kudumisha upendo miongoni mwetu. Ustahimilivu katika upendo na utu ni afya ya akili.

Tuonyeshe upendo kwa kumtag rafiki, ndugu, au mwandani ambaye upendo wake juu yetu hauna shaka.

Address

House No: 1045, Makondeko Str. Luguruni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255757896622

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Furaha kwa wote posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share