Tanna Mloganzila

  • Home
  • Tanna Mloganzila

Tanna Mloganzila ofisi na shughuli zote za Chama zinafanyika MNH-MLOGANZILA.

Chama Cha Wauguzi Tanzania tawi la MNH-Mloganzila yaani TANNA MNH-MLOGANZILA ni Chama Cha kitaatuma Cha Wauguzi ambacho kwa Mloganzila tawi lilifunguliwa Mwaka 2018.

Kwanini nilichagua kuwa muuguzi? Wauguzi wote mnaotembelea huu ukurasa mtuambie kwanini mlichagua kuwa Wauguzi...?? Mimi...
02/07/2025

Kwanini nilichagua kuwa muuguzi? Wauguzi wote mnaotembelea huu ukurasa mtuambie kwanini mlichagua kuwa Wauguzi...??

Mimi nitakupa sababu 9 za kwanini niliamua kuwa muuguzi, fuatana nami..


Happy new month July 2025 to all beloved nurses in Tanzania, we appreciate your dedicated effort towards caring for all ...
01/07/2025

Happy new month July 2025 to all beloved nurses in Tanzania, we appreciate your dedicated effort towards caring for all the patients you attend in your working areas.

Amon Kaponda, K.
Chairman
TANNA MNH-MLOGANZILA

Tanna HQ Tanzania

VIONGOZI WA CHAMA CHA WAUGUZI MNH- MLOGANZILA WAPONGEZWA KWA MAFANIKIO MAKUBWA NDANI YA MUDA MFUPI TOKA KUCHAGULIWA MWEZ...
19/06/2025

VIONGOZI WA CHAMA CHA WAUGUZI MNH- MLOGANZILA WAPONGEZWA KWA MAFANIKIO MAKUBWA NDANI YA MUDA MFUPI TOKA KUCHAGULIWA MWEZI FEBRUARI, 2025.

Viongozi wa Chama Cha Wauguzi Tanzania tawi la MNH-MLOGANZILA wamepongezwa kwa mafanikio makubwa ambayo Chama kimeyapata ndani ya muda mfupi tokea kuchaguliwa kwao kuwa viongozi Mwezi February 2025. Pongezi hizo zimetolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi msaidizi wa huduma za uuguzi na ukunga MNH-MLOGANZILA Bwn. Lukasi Mwaijage akimwakilisha Dr. Deborah Bukuku na kusema kuwa, ndani ya muda mfupi Wanachama wameongezeka kutoka 72 mwezi machi 2025 na kufikia 135 mwezi Juni 2025. Vile vile wamepongezwa kwa kuongeza mapato ya Chama kwa Kasi kubwa na kuweka mipango na mikakati mizuri ya kuendelea kuongeza mapato kwa kubuni miradi mipya ya Maendeleo, kutangaza uuguzi na Wauguzi wa Mloganzila. Hayo yote yamesemwa Leo Juni 19, 2025 katika kikao Cha wanachama na Wauguzi kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano (Auditorium) na kuongozwa na viongozi wa Chama hicho.

Aidha, akitoa hali ya Chama, mwelekeo na malengo kwa miezi mingine mitatu ijayo, M/kiti wa Chama hicho Bwn. Amon Kaponda amesema Chama kimejipanga vyema katika kuhakikisha wanachama wanongezeka, mapato ya Chama yanaongezeka na kubuni miradi mipya ya Maendeleo kwa kutumika Kamati ndogo ndogo za Chama ambazo ziliundwa na kwamba zinakamilisha kukusanya maoni na mapendekezo mwezi Juni 2025 na kutakuwa na kikao Cha pamoja Cha kupitia mapendekezo hayo Juni 26, 2025 ili kuyaweka katika utekelezaji.

Vile vile mwanachama wa Chama hicho Bwn. Daniel akichangia katika kikao hicho alisisitiza Wauguzi kupendana na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufikia malengo makubwa ya Chama hicho.

Paschalina Axwesso
Katibu Mwenezi TANNA MNH-MLOGANZILA
------------------------------
Juni 19, 2025


MUHIMBILI YAPATA MKURUGENZI MPYAHospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila imepata Mkurugenzi mtendaji mpya Dr. D...
17/06/2025

MUHIMBILI YAPATA MKURUGENZI MPYA

Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga na Mloganzila imepata Mkurugenzi mtendaji mpya Dr. Delilah Charles Kimambo ambaye amechukua nafasi ya Prof. Mohamed Janabi ambaye alichaguliwa kuwa mkurugenzi mtendaji wa shirika la afya Duniani (WHO) .

Dr. Kimambo kabla ya uteuzi huo alikuwa akihudumu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya kikwete (JKCI) k**a Mkurugenzi wa huduma za matibabu katika Taasisi hio.

Aidha, Dr. Kimambo amekua mwanamke wa pili kushika nafasi hio kubwa tangu kuanzishwa kwa Taasisi hio.



PROF: JANABI AWAPONGEZA WATUMISHI WA MUHIMBILI MLOGANZILA , AWAASA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORAWatumishi wa Hospitali ya ...
13/06/2025

PROF: JANABI AWAPONGEZA WATUMISHI WA MUHIMBILI MLOGANZILA , AWAASA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA

Watumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila wametakiwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuendelea kuongoza katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi wakati akiwaaga watumishi MNH Mloganzila ambapo amesema kuwa huduma za Mloganzila zimeendelea kuwa bora zaidi kutokana na juhudi zilizofanywa na Menejimenti na watumishi kwa ujumla.

Prof. Janabi amesema huduma za Muhimbili Mloganzila zimeendelea kuboreka zaidi jambo ambalo limeongeza imani kwa wananchi juu ya huduma zinazotolewa hospitalini hapo.

“Nawashukuru sana kwa ushirikiano wenu katika kipindi chote tulichokuwa pamoja , nilipoteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji Oktoba, 2022. Amesema Prof. Janabi

Prof. Janabi amebainisha kuwa ushirikiano wao, ubunifu na kujituma kumechangia kuongezeka kwa wagonjwa kutoka 400 mwaka 2022 na kufikia 1000 kwa siku mwaka 2025 , hali iliyochangiwa pia na kuongezeka kwa imani ya wananchi kuhusu ubora huduma zinazotolewa na hospitali hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu na Utawala MNH-Mloganzila Bw. Abdallah Kiwanga akizungumza kwa niaba ya watumishi, amemshukuru na kumpongeza Prof. Janabi kwa uongozi wake imara na kuahidi kuwa watayaenzi yale yote ambayo wamejifunza kwa kipindi chote ambacho wamekuwa pamoja.



TANGAZOChama Cha Wauguzi Tanzania (TANNA) tawi la MNH-MLOGANZILA kinaungana na Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania (TNMC...
12/06/2025

TANGAZO
Chama Cha Wauguzi Tanzania (TANNA) tawi la MNH-MLOGANZILA kinaungana na Baraza la uuguzi na ukunga Tanzania (TNMC) kuwakumbusha, kuwaomba na kuwasihi Wauguzi na wakunga wote wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila na Wauguzi/wakunga nchini kote kuhuhisha leseni zao za kitaaluma, kwa wale ambao leseni zao zinamaliza muda wake Juni 30, 2025 yaani mwaka wa fedha 2024/2025.

Kwani kuchelewa kuhuhisha ndani ya muda tajwa hapo juu, itawalazimu kuhuhisha kwa gharama za penati kuanzia Julai 1, 2025 ndani ya mwaka mpya wa fedha 2025/2026. Vile vile uhuhishaji huo utaenda sambamba na ukusanyaji wa CPD point kuanzia 60 tofauti na 30 za hapo awali.

Aidha, zoezi hili halitawahusu Wauguzi na wakunga ambao leseni zao zinamaliza muda wake mwezi Desemba, 2025.

Tukiwa tunakaribia kuadhimisha siku ya Wauguzi Duniani ambayo kitaifa inaadhimishwa mkoani Iringa kuanzia tarehe 9-12, M...
02/05/2025

Tukiwa tunakaribia kuadhimisha siku ya Wauguzi Duniani ambayo kitaifa inaadhimishwa mkoani Iringa kuanzia tarehe 9-12, Mei 2025.

Chama Cha Wauguzi tawi la MNH-MLOGANZILA kupitia viongozi wake wapya ambao walichaguliwa mapema mwezi February 2025, wakiongozwa na Mwenyekiti Bw. Amon Kaponda wa Kwanza kutoka kushoto wameendelea na maandalizi ya ushiriki wa maadhimisho katika kikao kilichofanyika Aprili 17, 2025 katika viunga vya Hospitali ya Taifa Muhimbili- MLOGANZILA.

Picha na,
Paschalina Awesso
Katibu Mwenezi
TANNA Mloganzila
--------------------------------
Mei 2, 2025

Address

Mloganzila

0000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanna Mloganzila posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram