11/09/2025
CHAMA CHA WAUGUZI TANZANIA TAWI LA MUHIMBILI-MLOGANZILA CHAPONGEZWA.
Chama Cha wauguzi Tanzania tawi la hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila, Chapongezwa kwa uanzishaji wa huduma ya Upimaji wa Afya, uchunguzi wa awali na utoaji wa Elimu pamoja na ushauri kwa wananchi wa mkoa wa Dar es salaam kuhusu magonjwa yote yasiyoambukiza k**a sukari, shinikizo la juu la damu, kiharusi, saratani na magonjwa ya moyo na figo Bure kabisa bila malipo yoyote.
Pongezi hio imetolewa na Dr. Mwanaidi Amir ambaye ni Mkurugenzi wa kitengo Cha utafiti, mafunzo na ushauri wa kitaalam akimwakilisha Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali ya Taifa Muhimbili-mloganzila Dr. Julieth Magandi katika uzinduzi wa program hio iliyoanzishwa na Chama hiko na kuwahususha wauguzi kutoka Mloganzila katika zoezi lililofanyika Jana Septemba 10, 2025 kuanzia saa 3 asubuhi Hadi saa 12 jioni maeneo ya kibamba, ambapo huduma zote za upimaji, uchunguzi na Elimu na ushauri juu ya magonjwa yasiyoambukiza zilifanyika na wananchi zaidi ya 200 kujitokeza.
Aidha, zoezi hilo liliambatana na uchangiaji wa Damu kwa ajili ya mahitaji ya kina mama wajawazito wanaohitaji Damu kwa ajili ya kujifungua kwa njia ya upasuaji na wagonjwa wa ajali ambapo chupa zaidi ya 20 zilikusanywa. Vile vile Elimu na ushauri kuhusu magonjwa ya changamoto ya afya ya akili, saikolojia na lishe bora ilitolewa na wataalamu wa saikolojia na lishe kutoka hospitali hio.
Dr. Mwanaidi Amir aliwapongeza viongozi wa Chama hiko wakiongozwa na mwenyekiti wa Chama Bwn. Amon Kaponda kwa maono makubwa na juhudi za makusudi za kuwasaidia wananchi katika kujua afya zao mapema na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Chama hiko wakati wote.
Aidha, Bwn. Amon Kaponda akiongea na wananchi katika ufunguzi huo aliwasihi kuendelea kujitokeza kwa wingi ili kujua afya zao kwa kuchukua tahadhali mapema, na kuongeza kuwa serikali na hospitali ya Taifa zimekua zikitumia pesa nyingi katika kugharamia matibabu ya wagonjwa wenye maradhi hayo kwani wengi hufika hospitalini kwa kuchelewa na kujikuta wakiwa kwenye hali mbaya.
Zoezi hilo litakua endelevu na litafanyika katika maeneo mengine ya mkoa wa Dar es salaam.
Paschalina Axwesso
Katibu Mwenezi TANNA
-Mloganzila