AFYA TIPS DAILY

  • Home
  • AFYA TIPS DAILY

AFYA TIPS DAILY Hii ni page ambayo tutajifunza mambo mbalimbali yanayohusu Afya. Karibuni nyote.

MAJI NI UHAI: LAKINI JE UNAYANYWA YA KUTOSHA🤨⁉️Maji ni sehemu ya kundi la chakula, pia yana umuhimu mkubwa kiafya katika...
18/04/2025

MAJI NI UHAI: LAKINI JE UNAYANYWA YA KUTOSHA🤨⁉️

Maji ni sehemu ya kundi la chakula, pia yana umuhimu mkubwa kiafya katika kufanikisha kazi mbalimbali mwilini.
Asilimia 60 ya mwili wa binadamu ni maji, lakini kiasi kikubwa cha maji hupotea mwilini Kila siku kupitia mkojo,kinyesi na jasho.Hivyo basi, ni muhimu kuwa na utaratibu wa kunywa Kiwango cha maji kinachohitajika ili kuuweka mwili katika afya bora.

NI ZIPI FAIDA ZA KUNYWA MAJI YA KUTOSHA❓

🔺Maji husaidia katika uyeyushwaji wa chakula, usafirishaji wa virutubishi na ufyonzaji wa virutubishi mwilini.
🔺Maji husaidia katika kutengeneza maji maji yanayopatikana katika viungo vya mwili k**a vile viwiko na magoti, hivyo husaidia viungo hivyo kufanya kazi.
🔺Maji hurekebisha joto mwilini.
🔺Maji husaidia kuondoa uchafu na mabaki ya uchafu mwilini kwa njia ya jasho na mkojo.
🔺Maji husaidia kupunguza uchovu mwilini.
🔺Maji husaidia kuzuia uwezekano wa kupata baadhi ya magonjwa k**a vile saratani ya tumbo na kibofu cha mkojo, maambukizi ya njia ya mkojo
(UTI) na mawe kwenye figo(renal calculi)
🔺Maji husaidia kuboresha Afya ya ngozi.

NI KIASI KIPI CHA MAJI AMBACHO MTU ANASHAURIWA KUNYWA KWA SIKU ❓

Kiwango cha maji kinachohitajika Kunywewa kwa siku kinatofautiana kutokana na sababu mbalimbali k**a vile umri,jinsia na uzito.

🔺Kwa watu wazima, mwanaume anashauriwa Kunywa maji takriban lita 3.6 kwa siku huku mwanamke akishauriwa Kunywa takriban lita 2.7 kwa siku.
🔺Watoto walioanza kupewa chakula( miezi 6 na kuendelea) wapewe maji kulingana na uhitaji wao.
🔺Watoto Kabla ya miezi sita hairuhusiwi kiafya kupewa chakula na kinywaji chochote zaidi ya maziwa ya mama.
🔺watu wenye uzito mkubwa wanahitaji Kiwango kikubwa zaidi cha maji ukilinganisha na watu wenye uzito mdogo.Ili kupata Kiwango sahihi cha maji (katika lita) kulingana na uzito wako, chukua uzito wako(Kg) gawa kwa 24.
🔺Uhitaji wa maji mwilini pia unaweza kuathiriwa na hali ya afya, hali ya hewa na shughuli za mwili
(Physical activity) k**a vile mazoezi n.k.

ANGALIZO‼️
Usinywe maji mengi kwa wakati mmoja utahatarisha figo zako. Jitahihidi Kunywa maji kidogokidogo.

ZINGATIA
Kunywa maji safi na Salama kulinda Afya yako. Kwani maji yasiyo safi na Salama huweza kusababisha magonjwa k**a typhoid na kipindupindu.

Marejeo:
https://www.medicalnewstoday.com/articles/290814
https://www.tfnc.go.tz/tips/umuhimu-wa-maji-mwilini
https://www.who.int/publications/i/item/9789240045064
https://wa.me/c/255656169598

Usisahau kulike, kuccoment na kushare ili elimu iwafikie watu wengi kwa ujumla.

MAGOJWA YASIYOAMBUKIZA:ADUI MKUBWA ANAYEJIFICHA KWENYE MAISHA YETU YA KILA SIKUMagonjwa yasiyoambukiza ni magonjwa ambay...
11/04/2025

MAGOJWA YASIYOAMBUKIZA:ADUI MKUBWA ANAYEJIFICHA KWENYE MAISHA YETU YA KILA SIKU

Magonjwa yasiyoambukiza ni magonjwa ambayo hayaenezwi kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine.
Aghalabu, magonjwa haya husababishwa zaidi na mtindo wa maisha(lifestyle), ulaji(dietary factors) na mazingira. Yafuatayo ni miongoni mwa magonjwa yasiyoambukiza ambayo yamekuwa ni tatizo kubwa katika jamii yetu;

🔺Magonjwa ya moyo na mishipa ya damu(cardiovascular diseases) K**a vile shinikizo la damu(hypertension),kiharusi(stroke) na ugonjwa wa moyo(coronary heart disease)

🔺Kisukari, hususani kisukari aina ya pili (Type 2 diabetes)

🔺Magonjwa ya mfumo wa hewa na upumuaji, K**a vile pumu (asthma) na ugonjwa wa mapafu (chronic obstructive pulmonary diseases-COPD)

🔺Saratani(cancers), K**a vile saratani ya mapafu,ini,utumbo mpana na saratani ya matiti.

JE MTINDO UPI WA MAISHA UNAOPELEKEA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA🤨⁉️

🔺Uchafuzi wa hali ya hewa na matumizi ya tumbaku.
Uzalishaji wa hewa chafu kutokana na shughuli zetu za Kila siku pamoja na uvutaji wa sigara na bidhaa za tumbaku huhatarisha mfumo wa upumuaji na mishipa ya damu.
Hali hii hupelekea magonjwa K**a saratani ya mapafu,magonjwa ya moyo,kisukari na magonjwa Sugu ya mfumo wa hewa.

🔺Lishe duni (unhealthy diet)
Ulaji wa vyakula vya Sukari nyingi kupitiliza,vyakula vya mafuta mengi na chumvi nyingi ni hatari kwa afya kwa sababu huweza kusababisha ugonjwa wa kisukari cha aina ya pili, shinikizo la damu, ugonjwa wa moyo na baadhi ya saratani.

🔺Kutokufanya mazoezi
Kutokufanya mazoezi pamoja na kufanya shughuli zisizotumia nguvu (sedentary behaviors) kwa muda mrefu huongeza uzito kupita kiasi na unene uliokithiri(Obesity) pamoja na kupelekea matatizo ya kisukari,shinikizo la damu na magonjwa ya moyo.

🔺Matumizi mabaya ya pombe( harmful use of alcohol)
Kunywa pombe kupita kiasi huua seli za ini na kusababisha magonjwa ya ini K**a vile ini kushindwa kufanya kazi(cirrhosis), ini kujaa mafuta(alcoholic fatty liver diseases),uvimbe wa ini(alcoholic hepatitis) na saratani ya ini.
Mbali na kuathiri Afya ya ini, ulevi wa pombe kupindukia pia hupelekea shinikizo la damu,matatizo ya figo pamoja na matatizo ya Afya ya akili.

JE TUNAWEZAJE KUJIKINGA NA HATARI KUPATA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA🤨⁉️
Njia muhimu ni kuepuka vihatarishi vyote vinavyoweza kupelekea magonjwa haya, K**a vile;

🔺Kuepuka uvutaji wa bidhaa za tumbaku pamoja na kupunguza uchafuzi wa hewa.

🔺Kuzingatia lishe bora, K**a vile kupunguza ulaji wa vyakula vya sukari,mafuta na chumvi nyingi pamoja na kuongeza ulaji wa mbogamboga na matunda.

🔺Kufanya mazoezi mara kwa mara

🔺Kuepuka ulevi wa pombe kupindukia.

CHUKUA HATUA, BORESHA MTINDO WA MAISHA.

Marejeo:
https://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/noncommunicable-diseases

https://wa.me/c/255656169598

Usisahau kulike na kucomment page yetu katika muendelezo wa mada mbalimbali za Afya.

FAHAMU MAANA YA AFYA NA VIPENGELE VYAKEKwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO) Afya inafafanuliwa k**a “Hali ya usta...
09/04/2025

FAHAMU MAANA YA AFYA NA VIPENGELE VYAKE

Kwa mujibu wa shirika la Afya duniani (WHO) Afya inafafanuliwa k**a “Hali ya ustawi wa kimwili, Kiakili na kijamii, na si tu kutokuwepo kwa magonjwa au udhaifu”.

Hata hivyo, baadhi ya wasomi wameongeza katika ufafanuzi wa Afya kwamba, Afya pia inahusiha ustawi wa kihisia(emotions), kiroho (Spirits) na masuala ya kijinsia( sexual aspects of life).

Hivyo basi,kutokana na tafsiri mbalimbali za Afya kutoka kwa wanazuoni mbalimbali pamoja na WHO Afya imegawanywa katika vipengele Vikuu vifuatavo;

🔺Afya ya mwili (physical health)
Hii hujumuisha uwezo mzima wa mwili kufanya kazi.Ili mwili ufanye kazi vizuri Unahitaji lishe bora,kufanya mazoezi, kupata mapumziko ya kutosha pamoja na kufuata kanuni mbalimbali za kiafya ili Kuepukana na magonjwa ambayo yangeweza kusababisha mwili usifanye kazi k**a inavyotakiwa.

🔺Afya ya akili (mental health)
Hii hujumuisha uwezo wa mtu kufikiri,kufanya maamuzi,kupanga mawazo pamoja na kutatua changamoto. Mfano,kujitambua,kudhibiti hisia pamoja na uwezo wa kukabiliana na changamoto na matatizo kwenye maisha. Hapa tunaangalia uwezo wa mtu wa kukabialiana na hali ya msongo wa mawazo, wasiwasi na matatizo mengine ya afya ya akili. Afya ya akili ina uhusiano mkubwa na Afya ya mwili Mfano, mtu akipata ugonjwa sugu huathiri uwezo wake wa kufanya shughuli za Kila siku na kupelekea hali ya sonona na wasiwasi kutokana na hali ya uchumi na ugonjwa.

🔺Afya ya kijamii (social health)
Hii hujumuisha uwezo wa mtu kuanzisha na kudumisha mahusiano mazuri na watu, kushiriki katika shughuli za kijamii pamoja na kujihisi kuwa sehemu ya jamii. Mfano,uwezo wa kuzungumza na watu vizuri (Communication skills), huruma(empathy) na uwezo wa kujenga mahusiano yenye tija katika jamii inayomzunguka (social support network)

🔺Afya ya hisia (Emotional health)
Hii inahusisha zaidi uwezo wa mtu kitambua, kudhibiti na kueleza hisia zake k**a vile hasira,huzuni, furaha au msongo wa mawazo kwa njia iliyo sahihi. Mfano, Kujitambua kihisia, kujijali na kuweza kukabiliana na changamoto katika njia sahihi na kuweza kuzitatua.

🔺Afya ya kiroho (spiritual health)
Ni Hali ya ustawi ambapo mtu Anapata maana, kusudi na uelekeo katika maisha yake kupitia, uhusiano wake na Mungu, Imani pamoja na maadili.Mfano wa ustawi wa Afya ya kiroho ni pamoja na Kusali,kujifunza na kufuata maandiko matakatifu, pamoja na kutenda mema na kuacha maovu.

🔺Afya ya Mazingira (Environmental health)
Inahusisha jinsi mazingira yanavyoweza kuathiri Afya zetu kwa ujumla. Kwa Mfano,upatikanaji wa hewa na maji safi, makazi bora na Salama na mazingira bora yanayotuzunguka kwa ujumla vyote vina mchongo mkubwa katika Afya zetu.

Kupitia maelezo ya hapo awali, tunapata kujifunza kwamba Afya ni neno Lenye maana pana sana. Watu wengi hufikiri Afya ni hali ya Kutokuwa na ugonjwa tu, lakini Afya ni zaidi ya maana hiyo. Mtu aweza kuwa mzima kimwili lakini akawa mgonjwa kiakili, kijamii, kihisia au kiroho.

Hitimisho:Ni juu yetu kuhakikisha tunalinda Afya zetu kwa ajili ya ustawi mzima wa maisha yetu kwa ujumla.
Pia ahsante kwa kusoma utangulizi huu mfupi katika mwendelezo wa mada zingine zinazohusiana na maswala ya Afya. Tusisahau kulike, kucomment, na kushare kwa wenzetu tuelimike sote.

Marejeo:

https://www.medicalnewstoday.com/articles/150999 -health

https://academic.oup.com/phe/article/16/3/210/7232444

https://www.who.int/about/governance/constitution

https://wa.me/c/255656169598

Address

Upanga

11103

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA TIPS DAILY posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram