Ihsaan Tiba Asili

Ihsaan Tiba Asili Karibu ihsaan Tiba Asili,tunatibu magonjwa yote

karibu sana tupo kwaajiri yako

28/02/2026

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Steve Chan, Hon Ramadhan, Sande Sangoi, Ñi Çóñstañt

15/02/2026

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Prisca Lameck, Davinci Code, Abdalah Taga, Lucky John, Tonny Marsta, Jimmy Wabenga, Filmon John, Alekx Levokatusi, Samsoni Matayo, Lilian Vivy

11/02/2026
Kwa MADEBE LIDAI – Nimetambuliwa hivi sasa k**a mmoja wa mashabiki wake bora! 🎉
10/02/2026

Kwa MADEBE LIDAI – Nimetambuliwa hivi sasa k**a mmoja wa mashabiki wake bora! 🎉

28/12/2025

Inapatikana kwa gharama ya T.sh 45,000/ = wasiliana nasi kwa kupitia namba 0797 409 551

19/12/2025

INAPATIKANA KWA GHARAMA YA T.SH 45,000/=

USIPUUZE NGUVU YA ASUBUHI Ni Punje 2 za Vitunguu Swaumu Zinaweza Kubadilisha Afya Yako..🧄💪Kabla hujaanza siku, hakikisha...
19/12/2025

USIPUUZE NGUVU YA ASUBUHI Ni Punje 2 za Vitunguu Swaumu Zinaweza Kubadilisha Afya Yako..🧄💪

Kabla hujaanza siku, hakikisha unatafuna punje 2 tu za vitunguu swaumu mara baada ya kuamka.

Ni mbinu ya asili inayosaidia kuimarisha mishipa, kuongeza nguvu na kulinda afya ya uzazi wakati wote....🩺

↳ Huchangia mzunguko mzuri wa damu mwilini...
↳ Husaidia kuimarisha mishipa ya uzazi...
↳ Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa..
↳ Hupunguza mafuta mabaya(cholesterol)....
↳ Huchochea homoni na nguvu za asili za mwili...
↳ K**a uume wako hausimami asubuhi tumia hii..

NB: Ni jambo dogo sana, lakini lina mchango mkubwa kwa afya yako na uimara wa mwili kwa ujumla....

Elimu sahihi + maamuzi sahihi = Afya bora.
Anza leo, jali mwili wako wakati wowote..🩺🫡

MAJANI YA MPERA NA MAAJABU YAKEMajani ya mpera ni miongoni mwa tiba asilia zilizotumika kwa muda mrefu katika jamii zetu...
18/12/2025

MAJANI YA MPERA NA MAAJABU YAKE

Majani ya mpera ni miongoni mwa tiba asilia zilizotumika kwa muda mrefu katika jamii zetu kutokana na virutubisho na kemikali asilia zinazopatikana ndani yake. Yafuatayo ni baadhi ya matumizi na faida zake:

1. Chai inayotengenezwa kwa majani ya mpera husaidia kupunguza matatizo ya kifua pamoja na kikohozi cha mara kwa mara.

2. Majani ya mpera yakioshwa na kusagwa vizuri hutumika kupaka kwenye ngozi yenye muwasho unaosababishwa na mzio (allergy).

3. Unywaji wa chai ya majani ya mpera husaidia kudhibiti kiwango cha mafuta (cholesterol) kilichozidi mwilini.

4. Kwa watu wenye changamoto ya sukari, chai ya majani ya mpera imekuwa ikitumika kusaidia kusawazisha kiwango cha sukari kwenye damu.

5. Majani ya mpera pia yanatajwa kusaidia wanaume wanaokumbana na changamoto za nguvu za kiume.

6. Yakisagwa na kuchanganywa na maji kidogo, majani haya hutumika k**a scrub ya asili ya kusafisha uso na kuondoa uchafu uliojificha kwenye ngozi.

7. Chai ya majani ya mpera ni msaada mzuri kwa watu wanaosumbuliwa na kuhara au tumbo kujaa gesi.

8. Kwa majeraha madogo, majani ya mpera yaliyosagwa yanaweza kupakwa ili kupunguza maumivu na kusaidia kuzuia maambukizi ya bakteria.

9. Majani haya yakisagwa na kupakwa kwenye sehemu iliyoumwa na mdudu husaidia kupunguza maumivu na muwasho.

10. Chai ya majani ya mpera inaaminika kusaidia katika matatizo yanayohusiana na tezi dume.

11. Kutokana na kuwa na vitamini C kwa wingi, majani ya mpera husaidia kupunguza chunusi na kuboresha afya ya ngozi.

12. Chai ya mpera husaidia kupunguza uzito wa mwili na kuboresha matumizi ya sukari ndani ya mwili.

13. Kwa watu wenye tatizo la nywele kukatika au kupungua, majani ya mpera yakichemshwa na maji yake kupakwa kichwani husaidia kuimarisha na kurefusha nywele.

14. Tafuna majani mabichi ya mpera ikiwa unasumbuliwa na maumivu ya jino, vidonda vya ufizi au harufu mbaya mdomoni.

15. Majani ya mpera yakisagwa laini na kutumika k**a scrub husaidia kupunguza dalili za ngozi kuzeeka mapema.

16. Chai ya mpera husaidia kutuliza mvurugiko wa tumbo na maumivu ya ndani ya tumbo.

Mbali na majani, juisi ya tunda la pera imekuwa ikitumika kusaidia matatizo k**a bawasiri, afya ya figo na kupunguza mafuta kwenye moyo. Kwa ujumla, karibu kila sehemu ya mti wa mpera ina matumizi ya kitabibu, ikiwemo mizizi yake ambayo ikichemshwa husaidia wanawake wenye changamoto za hedhi au kutokwa na majimaji yenye harufu sehemu za siri.

17. Majani ya mpera husaidia kuzuia kukatika kwa nywele. Chemsha majani, acha yapoe, kisha yapake kichwani na kuyasugua taratibu kwa dakika 15. Acha kwa dakika 30 kisha osha kwa maji safi bila sabuni. Fanya mara tatu kwa wiki.

18. Kwa lengo la kupunguza uzito, kunywa chai ya majani ya mpera mara kwa mara k**a sehemu ya mtindo bora wa maisha.

NAMNA YA KUTUMIA MAJANI YA MPERA

Njia ya Kwanza

Chemsha maji glasi nne kwa dakika 15–20 mpaka yatokote. Chukua majani ya mpera 10–15, yaweke kwenye maji ya moto, funika na uache kwa dakika 10–15. Koroga, chuja, chai iko tayari.

Njia ya Pili

Weka majani ya mpera moja kwa moja kwenye maji na yachemshe kwa dakika 15–20. Yakishatokota, ondoa kwenye moto, acha kwa dakika 10–15 kisha chuja.
Unaweza pia kutumia majani yaliyokauka na kusagwa; tumia kijiko kimoja cha chakula kwenye maji ya moto.

👉 Ushauri: Changanya chai ya majani ya mpera na asali mbichi badala ya sukari ili kuongeza ufanisi wake.

Chapati sio kifungua kinywa bora.! Acha mara moja, K**a unaitaka Afya bora...🩺Kila sahani ya chapati unayoanza nayo asub...
17/12/2025

Chapati sio kifungua kinywa bora.! Acha mara moja, K**a unaitaka Afya bora...🩺

Kila sahani ya chapati unayoanza nayo asubuhi, Ni hatua moja kuelekea magonjwa yasiyoambukizwa — Kisukari, shinikizo la damu, na unene kupita kiasi....

Mwili wako hauhitaji mafuta na wanga mwingi asubuhi, unahitaji mwanga safi yenye afya....

Anza siku kwa maji ya vuguvugu, mazoezi mepesi, kisha chakula chepesi chenye protini na nyuzinyuzi....

↳ Punguza wanga iliopitiliza...
↳ Fanya mazoezi kila asubuhi...
↳ Pima afya yako mara kwa mara...

NB: Magonjwa yasiyoambukizwa hayachagui umri tena — yamehamia kwa vijana, kwa sababu ya tabia na mitindo mibovu ya maisha....

Badilisha kifungua kinywa, badilisha maisha, Siku yako njema inaanza kwenye kikombe cha maji ya vuguvugu, sio kwenye chapati yenye mafuta....

Sasa naomba nikuulize wewe k**a mdau wa afya…👇

Kwa uzoefu wako au kile unachokiona kila siku kwenye jamii....

👉 Unadhani ni tabia ipi ya kifungua kinywa ndiyo inawazamisha vijana wengi kwenye magonjwa yasiyoambukizwa— Ni hizi chapati zenye wanga nyepesi na mafuta asubuhi, au ni kutokula kabisa?

👉 Na je, unafikiri suluhisho bora kwa kizazi hiki ni nini— Elimu sahihi, kubadilisha menu za familia, au nidhamu ya kufanya mazoezi asubuhi..?

Tuambie maoni yako hapa chini, Ushiriki wako unaweza kumsaidia mtu mwingine leo kuanza safari mpya ya afya njema...

By ihsaan tiba asili | Jifunze na chukua hatu kuboresha afya yako...🩺🫡

Address

Kigamboni-mjimwema Kwa Toma
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ihsaan Tiba Asili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram