30/01/2026
Bawasiri (Hemorrhoids) ni hali ya kuvimba kwa mishipa ya damu sehemu ya mkundu (a**s) au ndani ya njia ya haja kubwa (re**um).
Aina za bawasiri
1. Bawasiri ya ndani – iko ndani ya re**um, mara nyingi haina maumivu lakini husababisha damu kutoka.
2. Bawasiri ya nje – iko nje ya mkundu, inauma sana na huvimba.
Dalili za bawasiri
• Kutokwa na damu wakati wa haja kubwa
• Maumivu au kuungua sehemu ya mkundu
• Kuwashwa au kuvimba
• Uvimbe au kijitundu karibu na mkundu
• Kuhisi haja haijatoka yote
Athari za bawasiri
• Maumivu makali yanayozuia kukaa au kutembea vizuri
• Upungufu wa damu (anemia) endapo damu hutoka mara kwa mara
• Maambukizi kutokana na vidonda au mipasuko
• Kuvimba sana hadi bawasiri kushindwa kurudi ndani (pr*****ed hemorrhoids)
• Msongo wa mawazo kutokana na maumivu ya muda mrefu
Sababu kuu
• Kukaa chooni muda mrefu / kujikamua sana
• Kukosa vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber)
• Kukosa maji ya kutosha
• Kukaa muda mrefu (hasa kazi za ofisini)
• Ujauzito
• Uzito kupita kiasi
Namna ya kujikinga/kupunguza
• Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi nyingi (mboga, matunda, nafaka zisizokobolewa)
• Kunywa maji ya kutosha
• Epuka kujikamua chooni
• Fanya mazoezi
• Epuka kukaa muda mrefu bila kusimama