Afya Zetu

Afya Zetu For reliable Information on how to treat your daily life in Healthy way Join us here..like our page

🩺 *JE WAJUA CHANZO CHA UGONJWA WA PRESHA?* 🩺  SABABU KUBWA NI HIZI Presha ya kupanda (Hypertension) ni hali ya kimya ina...
27/05/2025

🩺 *JE WAJUA CHANZO CHA UGONJWA WA PRESHA?* 🩺 SABABU KUBWA NI HIZI

Presha ya kupanda (Hypertension) ni hali ya kimya inayoweza kusababisha matatizo makubwa k**a kiharusi, shambulio la moyo, na figo kushindwa kufanya kazi.

👉 *Visababishi vikuu ni:*
✔️ Kurithi kutoka kwa familia
✔️ Ulaji wa chumvi/mafuta kupita kiasi
✔️ Kukosa mazoezi
✔️ Msongo wa mawazo
✔️ Unywaji wa pombe na uvutaji sigara
✔️ Unene uliopitiliza
✔️ Umri mkubwa
✔️ Magonjwa ya figo au mfumo wa homoni

💡 *Kinga ni bora kuliko tiba!*
Jali afya yako mapema kwa kupima mara kwa mara, kufanya mazoezi, kula vyakula bora, na kupunguza msongo wa mawazo.

SHARE na wengine

Madhara ya kula chakula k**a hikiI. Kwa kuwa ndani yake kuna amira uwezekano wa kuwa na kitumbo cha chini ni asilimia 10...
24/04/2025

Madhara ya kula chakula k**a hiki

I. Kwa kuwa ndani yake kuna amira uwezekano wa kuwa na kitumbo cha chini ni asilimia 100%

II. Kwa kuwa kumeongezwa sukari na mafuta uwezekano wa kuwa na chelesto kwenye damu ni 100%

III. Kwa kuwa imetumika pure ngano uwezekano wa kuathiri mfumo wa chakula utumbo mdogo ni kwa 100%
. . . . . .. . . .
Badala yake, watu wale maandazi ya kuchoma au kuoka na moto kwani hayatumi mafuta wala sukari sana.

. . . . . . . . . . . . . .
Madhara yataanza kuonekana baada ya miaka 10 hadi 15 ya kutumia chakula k**a hiki. . . . . . . . .. . . . .
Magonjwa atakayopata zaidi ni kuwa na
- High blood pressure
- Kiungulia
- Utumbo mnene
- Gasi za tumboni
- Shinikizo la damu . . . . . . . . . . . . . . . . .
Comment na Share

07/04/2025

VIDONDA VYA TUMBO.
Tatizo hili husababiswa na bacteria tumboni waitwao H. Pyroli.

Kuna aina kuu tatu za vidonda vya tumbo. Nazo ni
1.Gastric Ulcers
2.Duodenal Ulcers
3.Ulcers in small intestine (Intestinal Ulcers)

1.GASTIRIC ULCERS
Aina hii ya vidonda vya tumbo hutokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo.
hii.

2.DUODENAL ULCERS:
Hii hutokea kwenye duodenum.

3.ULCERS IN SMALL INTESTINE (INTESTINAL ULCERS)
Aina hii ya vidonda vya tumbo kwenye sehemu ya utumbo mdogo(small intestine).

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
1.Tumbo kujaa gesi.
2.Kiungulia
3.Kinyesi nyenye rangi k**a kahawia
4.Maumivu makali ya tumbo k**a moto.
5.Kucheua au kutoa hewa chafu
6.Maumivu wakati wa kula au mara tu baada ya kula chakula.
7.kupata choo kigumu
8.Kukosa choo kwa mda mlefu.


MADHALA YA VIDONDA VYA TUMBO.

K**a bawasiri isipotibiwa kwa uhakika na mapema inaweza kusababisha madhala yafuatayo.Bawasiri Saratani ya utumbo.Kuathirka kwa ini Kuathiri kongosho.
Stress n.k

Kwa tiba na ushauri piga ✍️☎️+255756403981

MAGIMBI: CHAKULA CHA ASILI CHENYE LISHE NA MANUFAA MENGI Magimbi ni moja ya vyakula vya mizizi vinavyolimwa na kuliwa na...
26/02/2025

MAGIMBI: CHAKULA CHA ASILI CHENYE LISHE NA MANUFAA MENGI

Magimbi ni moja ya vyakula vya mizizi vinavyolimwa na kuliwa na jamii nyingi duniani, hasa barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini. Ni chakula cha jadi kinachopendwa kwa sababu ya lishe yake bora na uwezo wake wa kutoa nishati nyingi.

1. Asili na Kilimo cha Magimbi
Magimbi yanatambulika kwa majina mbalimbali kulingana na maeneo tofauti, lakini kitaalamu, hutambulika kwa spishi kuu mbili:
- Colocasia esculenta (Taro) – Magimbi haya yana majani mapana k**a maboga, na mizizi yake hutumika k**a chakula kikuu katika baadhi ya maeneo.
- Dioscorea spp. (Yam) – Haya ni magimbi yenye umbo refu zaidi na ngozi ngumu yenye magamba, mara nyingi huota k**a mizizi mirefu inayotambaa ardhini.

Magimbi hustawi vizuri katika udongo wenye rutuba na unyevu wa kutosha. Hustahimili hali ya hewa ya joto na mvua nyingi, ndiyo maana hulimwa sana katika maeneo ya kitropiki k**a Tanzania (hususan Kagera, Kigoma, na Morogoro), Uganda, na Nigeria.

Katika mkoa wa Kagera, magimbi ni sehemu ya chakula cha asili, yakipikwa kwa njia mbalimbali k**a kuchemsha, kukaanga, au kuchanganywa na vyakula vingine k**a nyama, maharagwe, na mboga za majani.

2. Sifa za Magimbi
✅ Chanzo kikubwa cha wanga – Hutoa nishati ya kutosha kwa mwili, hivyo ni chakula bora kwa watu wanaofanya kazi ngumu.
✅ Nyuzinyuzi nyingi – Husaidia katika mmeng’enyo wa chakula na kupunguza matatizo ya tumbo k**a kukosa choo.
✅ Ladha laini na tamu– Magimbi yana ladha ya kipekee, hasa yakipikwa vizuri kwa kukaangwa au kuchemshwa.
✅ Rangi na muundo mbalimbali– Baadhi ya magimbi yana nyama nyeupe, ya njano au hata ya zambarau, na yote yana virutubisho vya kipekee.
✅ Yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu – Magimbi mabichi yanaweza kuhifadhiwa kwa wiki kadhaa bila kuharibika ikiwa yatahifadhiwa mahali pakavu na penye ubaridi.

3. Faida za Magimbi kwa Afya
✔ Huboresha afya ya moyo – Magimbi yana madini ya potassium ambayo husaidia kudhibiti shinikizo la damu na kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.
✔ Husaidia mmeng’enyo wa chakula – Kwa kuwa yana nyuzinyuzi nyingi (fiber), magimbi husaidia mfumo wa usagaji chakula na kuzuia matatizo k**a kuvimbiwa.
✔ Chanzo kizuri cha vitamini na madini – Yana vitamini A, C, na B-complex ambazo ni muhimu kwa afya ya ngozi, macho, na kinga ya mwili.
✔ Hupunguza hatari ya kisukari– Magimbi yana low glycemic index, hivyo husaidia kudhibiti kiwango cha sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari.
✔ Husaidia kupunguza uzito – Magimbi husaidia kushibisha haraka na kupunguza hamu ya kula vyakula vyenye mafuta mengi.
✔ Huimarisha mifupa– Yana madini k**a calcium, phosphorus, na magnesium yanayosaidia kuimarisha mifupa na meno.
4. Jinsi ya Kupika na Kula Magimbi
Magimbi yanaweza kuliwa kwa njia nyingi:
➡Kuchemsha – Hili ni njia rahisi ya kupika magimbi. Yanachemshwa hadi yalainike, kisha yanaweza kuliwa k**a yalivyo au kwa maharagwe na mboga.
➡Kukaanga – Magimbi hukatwa vipande vidogo na kukaangwa kwenye mafuta, k**a chipsi.
➡ Kupika kwa n**i – Njia hii huipa magimbi ladha tamu na laini.
➡ Kutengeneza uji au unga – Baadhi ya jamii hutengeneza unga wa magimbi na kuutumia kwa uji au vyakula vingine.
➡ Kuchanganya na nyama au maharagwe – Hii ni njia maarufu ya kula magimbi katika baadhi ya sehemu, kwani husaidia kuongeza virutubisho zaidi.

5. Umuhimu wa Magimbi Katika Utamaduni wa Kagera
Katika mkoa wa Kagera, magimbi ni sehemu ya chakula cha asili na hupewa heshima kubwa katika jamii. Mara nyingi hutumika katika kifamilia. Magimbi pia ni zao la biashara linaloweza kuingiza kipato kwa wakulima wa Kagera, endapo litapewa kipaumbele katika uzalishaji na masoko.

Magimbi ni chakula chenye faida nyingi, si tu kwa afya bali pia kwa uchumi wa wakulima. Ni wakati wa vijana wa Kagera kuwekeza katika kilimo na biashara ya magimbi kwa maendeleo ya mkoa wetu.

Jitaidi sana 👇Maji💦 → Kwa Ajili ya Figo!Mayai 🥚→ Kwa Ajili ya Ubongo 🧠!Carrots🥕 → Kwa Ajili ya Macho!Nanasi 🍍→ Kwa Ajili...
26/02/2025

Jitaidi sana 👇

Maji💦 → Kwa Ajili ya Figo!

Mayai 🥚→ Kwa Ajili ya Ubongo 🧠!

Carrots🥕 → Kwa Ajili ya Macho!

Nanasi 🍍→ Kwa Ajili ya Koo!

Cabbage 🥬 → Kwa Ajili ya Utumbo!

Tango 🥒 → Kwa Ajili ya Ngozi!

Tangawizi → Kwa Ajili ya Koo na Mapafu!

Parachichi & Nyanya 🥑 → Kwa Ajili ya Afya ya Moyo 🫀!

Mazoezi exercise🏋️ → Kwa Ajili ya Afya imara na Kinga Bora ya Mwili!

SABABU ZA MAUMIVU YA KIUNO NA MGONGO KWA WANAWAKEKUNA sababu nyingi zinazofanya wanawake wengi wasumbuliwe na maumivu ya...
27/10/2024

SABABU ZA MAUMIVU YA KIUNO NA MGONGO KWA WANAWAKE

KUNA sababu nyingi zinazofanya wanawake wengi wasumbuliwe na maumivu ya kiuno mara kwa mara hasa wakati wa hedhi na kuna wengine huugua kwa muda mrefu zaidi ya miezi mitano. Zipo sababu nyingi za kuzuka kwa maumivu haya k**a vile kuwa na matatizo kwenye via vya uzazi, kibofu cha mkojo, utumbo mkubwa au misuli ya nyonga kuwa na tatizo. Maumivu yanaweza kuwa yanaendana na mzunguko wa hedhi au la, mara nyingi hujitokeza chini ya kitovu na kiunoni.

Sababu ni nyingi ambazo zinaweza kusababisha mwanamke kupata maumivu haya ya kiuno kwa muda mrefu, k**a vile kuwa na maumbukizi ya ndani ya kiuno ya muda mrefu kitaalamu huitwa Chronic Pelvic Infection. Maambukizi haya hutokana na ugonjwa wa kifua kikuu (TB) na huweza kusababisha maumivu ya kiuno.

Sababu nyingine ni kuwa na Endometriosis, hii ni hali ambayo seli za ukuta wa uzazi huota sehemu nyingine za uzazi na itokeapo hivyo basi mwanamke hujikuta akipata maumivu makali wakati wa hedhi au tendo la ndoa. Wengine hupata maambukizi ya muda mrefu ya shingo ya uzazi au mji wa uzazi nayo husababisha maumivu ya kiuno wakati wowote na hasa wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Wanawake wengine hupata maumivu hayo kutokana na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi kitaalamu huitwa Ectopic Pregnancy. Baadhi ya wanawake hutokwa na uvimbe mdogomdogo wa kizazi ambao husababisha maumivu pale unapokua kwa haraka na kukandamiza viungo vingine. Maumivu yake huwa ya wakati, huja na kuacha.

Wengine hupata maumivu wakati wa kukojoa kutokana na kuwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo ya muda mrefu huku baadhi yao wakipata maumivu baada ya kupata maambukizi ya via vya uzazi kitaalamu huitwa Pelvic Inflammatory Disease – PID au wale wenye maambukizi ya Kibofu cha Mkojo yaani Interst**ial Cyst**is.

Wale wenye hali hii hupata maumivu hasa chini ya kibofu cha mkojo ambayo hupungua pale anapokojoa na hujikuta akikojoa mara kwa mara na kushindwa kubana mkojo. Lakini pia ugonjwa wa Kidole Tumbo yaani Chronic Appendicitis huleta maumivu upande wa kulia chini ya kitovu ambayo huwa hayatulii na dawa za kutuliza maumivu na wapo wanaougua kiunoni chini ya kitovu kutokana na kuwa na Saratani ya Utumbo Mpana.

Wapo wanaougua kiuno kutokana na kusagika kwa mifupa kwenye maungio yaani Degenerative Joint Disease na hali hiyo inapotokea husababisha maumivu makali maeneo ya kiunoni hasa wakati wa kutembea.

TIBA

Matibabu ya kuumwa na kiuno hutegemea na kinachosababisha k**a tulivyoeleza hapo juu. Nenda kamuone daktari na akigundua tatizo baada ya uchunguzi atakupa dawa husika wewe mgonjwa, au dawa za majira k**a tatizo linahusiana na mzunguko wa hedhi au atakufanyia upasuaji na atakupa ushauri.

UMEIPENDA??
SHARE na wengine waelimike

Namna ya kujikinga na  homa ya Nyani (M-Pox) *Tahadhari za kiafya zizingatiwe.*1. Tuepuke kusalimiana kwa mikono.2. Tuep...
20/08/2024

Namna ya kujikinga na homa ya Nyani (M-Pox)

*Tahadhari za kiafya zizingatiwe.*
1. Tuepuke kusalimiana kwa mikono.
2. Tuepuke kukumbatiana.
3. Tucheze muziki kwa kutogusana.
4. Vitakasa mikono, sabuni na maji tiririka viwepo kila mahali.
5. Tunawe kila mara.
6. Tutakase mikono kila mara.
7. Virusi vya Homa ya Nyani/tumbili (Monkeypox (Mpox)) imetangazwa na WHO kuwa janga la dunia.
8. Kujikinga ni nafuu, kujitibia ni ghali.

SHARE SHARE SHARE

ASUBUHI HII.... SUPU GANI UNAIPENDA HAPO? UNADHANI INA FAIDA GANI KIAFYA?COMMENT NA SHARE
10/07/2024

ASUBUHI HII....
SUPU GANI UNAIPENDA HAPO? UNADHANI INA FAIDA GANI KIAFYA?
COMMENT NA SHARE

UGONJWA WA    FANGASI Fangasi ni magonjwa yanayoathiri ngozi, kucha na nywele, pia huathiri mdomoni na ukeni. Magonjwa h...
07/03/2024

UGONJWA WA FANGASI

Fangasi ni magonjwa yanayoathiri ngozi, kucha na nywele, pia huathiri mdomoni na ukeni. Magonjwa haya huambukiza kwa njia ya kugusana ua kshirikiana nguo hasa za ndani na tauro.

Hapa tutaangalia fangasi katika kundi la magonjwa yanayoathiri ngozi, nywele na kucha (dermatomycosis).

Kuna aina kuu 5 za magonjwa ya fangasi wa ngozi, nywele na kucha k**a ifuatavyo;

Fangasi wa kichwani, ugonjwa huu huanza na sehemu ndogo ya ngozi ya kichwa na kukua kuwa sehemu kubwa. Huathiri nywele na kuzifanya dhaifu, laini na nyepesi kukatika au kung'oka. Huwaathiri sana watoti chini ya miaka 10 na hupotea mtu akisha barehe. Matibabu take ni splina,shake off,red bubble tea,sabuni dozi zake huanzia siku 6-14.

Fangasi wa mwili, ugonjwa huu hutokea mwilini, sehemu ya ngozi iliyoathiriwa huwa nyekundu, duara k**a shiringi na kukua huku ikiacha sehemu ya katikati kuwa na ngozi nzuri. Maduara haya yanaweza kukaa yakiwa kadhaa katika sehemu moja ya ngozi. Kwa ugonjwa uliokua sana na kwa wagonjwa wenye kinga ya mwili ndogo k**a wenye VVU, nivema wakatumia dawa ya kunywa

Fangasi wa nyayo na vidole, ugonjwa huu hutokea k**a mabaka na kuchanika katikati ya vidole na huwacha sana na kuuma pia. Matibabu yake maranyingi huwa dawa ya kupaka kwa wiki 4, kwa ugonjwa uliokua sana tumia dawa ya kunywa k**a splina, bubble tea kwa wiki 6-12.

Fangasi wa kucha, ugonjwa huu huathiri kucha na hubadilisha rangi ya kucha. Huzalishwa vitu k**a chaki na ambavyo vikisuguliwa huweza kupukutika. Kucha huweza kulika na inaweza kuisha. Ili kutibu ugonjwa huu nibora kutumia dawa za kunjwa na terbinafine na itraconazole zimeonekana dawa bora zaidi.

Pityriasis, huu ni ugonjwa wa fangasi ambao huathiri sehemu ya huu sana ya ngozi katika sehemu za usoni, shingoni na mgongoni. Hutokea k**a viduara vyenye mng'ao vinavyo washa. Huongezeka na huathiri sehemu kubwa ya ngozi visipotibiwa ingwa vinaweza kupotea vyenyewe. Maranyingi ugonjwa huu hauambukizwi Ila hutokea k**a ajari tu yaapotikea mabadiliko fulani ya mwili. Sio ugonjwa hari sana kiafya ila haukubaliki kwani huharibu mwonekano wa mtu has a unapotokea maeneo ya uso na shingoni. Matibabu yake ni sawa na yale ya fangasi wa mwili.

UFAHAMU UGONJWA WA VITILIGOVitiligo ni ugonjwa ambao unaathiri ngozi, unaotokana na kuharibiwa kwa cells za kutengeneza ...
25/02/2024

UFAHAMU UGONJWA WA VITILIGO

Vitiligo ni ugonjwa ambao unaathiri ngozi, unaotokana na kuharibiwa kwa cells za kutengeneza rangi ya ngozi zinazojulikana k**a (melanocytes). Chanzo halisi cha celi hizi kushambuliwa bado hakijajulikana kitaalam, hivyo Wataalam Wengi kupata ugumu wa kujua tiba sahihi ya ugonjwa huu.

Celi hizi zikishaharibiwa ngozi huanza kubadilika rangi kwa kuweka vidoa vyeupe, na mara nyingi huonekana zaidi kwa watu wenye ngozi nyeusi, ingawa ugonjwa huu unaathiri watu wote na wa rika zote.

Kitaalam Vitiligo hauambukizi isipokuwa unaweza kurithi kutoka kwa wazazi kutokana na genes anazobeba binadamu kutoka kwa wazazi, na hauna madhara kwa kuhatarisha maisha (kuua) zaidi ya kubadili rangi yako ya ngozi.

Watu wenye ugonjwa huu mara nyingi hutumia lotion za sun screen ili kuzuia ngozi isipate madhara yatokanayo kwa kupigwa na jua kali, hasa kwa nchi zenye jua kali.

Kwa wagonjwa wa vitiligo wanashauriwa Kuwasiliana daktari Daktari Wetu mara tu anapoona dalili zake, ili kumpa dawa za kurestore rangi ya ngozi ambayo imeanza kupotea,.

Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi ambao unasababisha ngozi kuwa na mabaka mabaka meupe kwa sababu ya kupoteza melanin. Vitiligo inaathiri watu wa rangi yoyote ya ngozi japo kwa watu wengine huwa inaonekana zaidi kutokana na rangi yake ilivyo sanasana kwa watu wenye ngozi nyeusi. Pia inatokea katika umri wowote mara nyingi katika umri chini ya miaka 40.

Dalili zake ni zipi
Mgojwa wa vitiigo hapati dalili zozote bali mfano maumivu, kuwashwa au homa bali mwenye vitiligo huanza kuona mabaka meupe au madoa yakijitokeza katika ngozi yake

Nini kinasababisha vitiligo?
Vitiligo ni tatizo ambalo linatokana na kupungua au kupotea kwa chembechembe zinazoipa ngozi rangi yake zijulikanazo k**a melanin.
Kwa nini chembechembe hizo hupotea au kupungua?
Hutokea k**a seli zinazohusika na kuzalisha melanin zikifa au zikipungukiwa na ufanisi wa kufanya kazi. Melanin zinahusika na kuwezesha nywele, ngozi na macho kuwa na rangi yake.

kwa nini hizo seli zinafeli kuzalisha melanin
Sababu za moja kwa moja hazijulikani ila kuna mambo ambayo yanasemekana kuwa yanachangia kupata tatizo la vitiligo nayo ni k**a yafuatayo;
Madhara gani mtu mwenye vitiligo atapata?

1-Athari kisaikolojia kutokana na kufikiria namna gani watu wanaomzunguka wanavyomchukulia
2-Hatari ya kuathiriwa na jua inaongezeka kiasi kwamba hatari ya kupata hata kansa za ngozi inaongezeka
3-Pia hatari ya kupata matatizo ya macho inaongezeka

Matibabu ya vitiligo ni yapi?

Matibabu hutegemea na makubaliano ya mtu mwenye tatizo na daktari wake.
-Dawa za kupakaa ili kusaidia uzalishaji wa melanin
-Dawa ZA kuchemsha ili kuzuia muwasho
-Kupunguza melanin maeneo ambayo hayajaathiriwa ili kuleta ufanano na sehemu zilizoathiriwa (depigmentation)
-Upasuaji pia hufanyika (skin grafting)
Ukiwa na tatizo hili ni vizuri kumuona mtaalamu wa magonjwa ya ngozi (Dermatologist) ili uweze kusaidiwa pia ukiona dalili za tatizo hili inashauriwa kujilinda na jua na kutochora tattoo ambazo za kujaribu kuficha tatizo Hili la ugonjwa wa ngozi

Ugonjwa huu unatibika,Nenda hospitali mapema pindi ukiona dalali za ugonjwa huu ….

SHARE na wengine wapate elimu Hii

AINA ZA MALENGELENGE NA SABABU ZAKE!Malenge ya kuungua. Aina hii ya malenge ya ngozi daraja la pili, mara nyingi huzalis...
17/01/2024

AINA ZA MALENGELENGE NA SABABU ZAKE!
Malenge ya kuungua.
Aina hii ya malenge ya ngozi daraja la pili, mara nyingi huzalisha malenge ya maji mwilini.
Mchomo huu huathiri ngozi ya juu na sehemu kidogo ya ngozi ya chini, hii hupelekea kutokea kwa malengo madogo au makubwa pamoja na dalili zingine k**a, maumivu, wekundu kwenye ngozi, na unyevuunyevu kwenye eneo lililoungua.
Malenge ya ugonjwa wa Demataitiz ya mgusomguso.
Kwa sababu ya kutokea kwa mwitikio wa kinga za mwili kwenye mzio wa ngozi, mzio huu huzalisha malengelenge madogo kwenye ngozi yaliyozungukwa na wekundu kwenye mipaka yake na uvimbe.
malenge yanaweza kupasuka na kutoa maji, kutengeneza magamba na kusababisha muwasho.
Malenge ya Erithima matifomu (Erythema multiforme).
Erithima matifomu ni michomo ya muda mfupi itonanayo na kinga za mwili kwenye ngozi inayoambatana na mabaka mekundu, upele mdogo na wakati mwingine upele malenge makubwa yaliyo na maji ndani.
Magamba ya erithima matifomu huonekana kwenye ngozi ya maeneo mikono, viganja vya mikono, miguu, uso na shingo.
Vipele huweza tokea na kupotea na kutokea tena wakati mwingine. Licha ya kuweza kutokea sehemu yoyote ya mwili, malenge madogo na makubwa huonekana sana kwenye maeneo ya ngozi laini haswa kwenye midomo na ndani ya kinywa, yanaposuka hutegeneza vidonda na kuzalisha ute mzito wenye rangi ya njano au nyeupe.
Makovu yanayotoa damu, na majimaji yanayonuka huweza ambatana na dalili ya kushindwa kutafuna au kumeza chakula pamoja na kuvimba mitoki ya maeneo ya shingo.
Malenge ya kung’atwa mdudu.
Malenge ya kung’atwa na mdudu huanza kwa kuleta wekundu kwenye ngozi kisha kuzuka kwa vipele ambavyo vinaweza kutoa damu.
Malenge ya maambukizi ya tibea pedispedis.
Tinea pedis:- Tinea pedis ni maambukizi ya fangasi kanyagio na katikati ya vidole, fangasi hawa huweza sababisha malenge kwenye maeneo tajwa na baadaye hubadilika na kuwa magamba. Maambukizi makali huambatana na michomo, muwasho na kushindwa kutembea.
Malenge ya skabi.
Huzalisha malenge madogo enye shina jekundu kwenye miishio ya shimo lililotobolewa na mdudu.
Tundu huwa na urefu wa sentimita chache na huwa na uvimbe wa sentimita moja au zaidi au upele mdogo mwekundu wenye mdudu mdogo (Sarcoptes scabiei)
Chunusi kubwa zenye usaha pamoja na magamba yanaweza kutokea.
Wadudu wanaweza kuchimba mashimo kwenye kichwa cha uume, mpini wa uume na kwenye ngozi iliyoshika korodani kwa wanaume na hujichimbia kwenye t**i la mwanamke pia.
Sarcoptes scabiei huweza kujichimbia pia katikati ya vidole, maungio ya kiganja cha mkono na mkono, maungio ya mkono wa mbele na mkono, kwapani na maeneo ya kiuno kwa jinsia yoyote ile.
Ugonjwa huu huleta dalili ya muwasho inayoongezeka zaidi kwenye kipinid cha joto na haswa wakati wa usiku.
Malenge ya Surua.
Surua kwa jina jingine la kitiba smallpox, huanza kuonekana na dalili ya homa kali, uchovu wa mwili, mwili kulegea, maumivumakali ya kichwa, maumivu ya mgongo na maumivu ya tumbo.
Harara bapa au upele mdogo huanza kutokea kwanza kwenye maeneo ya ngozi laini ya midomo, koo, uso na mkono wa mbele na baadae kusambaa kwenye kiwiliwili na miguuni.
Ndani ya siku 2 harara hubadilika na kuwa malenge na baadae kujaa usaha. Upele hutokea kwa wakati mmoja, hufanana na huonekana sana kwenye maeneo ya uso na miishio ya mwili.
Upele wenye usaha huwa na umbo duara, mgumu na shina lililozama chini ya ngozi. Baada ya siku 8 hadi 9, upele wenye usaha hutengeneza gamba, baadaye hudondoka na kuacha kovu lenye shimo.
Endapo ugonjwa ni mkali yaani umehusisha ubongo, kifo hutokea, hata hivyo madhara ya ugonjwa mkali ni pamoja na kupata maambukizi ya bakteria kwenye vidonda au kupoteza damu nyingi.
Malenge ya epidemo nekrosis ya sumu.
Epidemo nekrosis ya sumu (Toxic epidermal necrolysis) hutokana na mwitikio wa kinga za mwili kwenye dawa au sumu iliyoingia mwilini.
Mwitikio huu huzalisha malenge makubwa kwenye ngozi yanayoanza k**a mabaka yenye rangi nyekundu yakifuatiwa na kuungua , kufa kwa eneo kubwa la ngozi na kubanduka kwa ukuta wa juu ya ngozi.
Dalili zinazojitokeza ni malenge makubwa yanayopasuka na kutoa maji kwenye ngozi laini, hisia za kuungua moto kwenye konjaktiva, uchovu wa mwili, homa, na maumivu ya ngozi sehemu kubwa ya mwili. Lenge kubwa hupasuka kirahisi na kuacha ngozi wazi.
Malenge ya pofria kyutinia tadatada.
Pofria kyutinia tada (Porphyria cutanea tarda) . Tatizo hili hutokana na madhaifu ya umetabolism wa molekuli ya porphyrin mwilini.
Malenge makubwa hutokea kwenye maeneo ambayo yanapigwa na jua, yenye msuguano, majeraha au kupata joto napia husababisha dalili ya macho kuumizwa na mwanga. Machanganyiko wa Vipele vidogo vigumu au vyenye maji hubadilika kuwa vidonda na baadae makovu.
Dalili sugu zinazoweza kutokea ni k**a vile kupauka au kutengeneza baka jeusi kwenye ngozi, kuota nywele nyingi zisizotegemea umri au jinsia(haipatrikosis), ngozi ya sklerodemoidi pamoja na kukojoa mkojo wenye rangi ya pinki au kahawia.
Malenge ya ugonjwa wa PemphigoidPemphigoid.
Hutanguliwa na dalili za muwasho sehemu kubwa ya mwili, kuvimba kwa mwili na dalili za pumu ya ngozi kabla ya kupata malenge makubwa. Sifa za malenge huwa ni makubwa, yenye kuta pana, magumu na yenye mipaka isiyoeleweka na hutengenezwa kwenye eneo jekundu na huonekana sana kwenye mkono, kiwiliwili, ndani ya kinywa na maeneo mengine ya ngozi laini.
MLENGE YA DERMATITIS HERPETIFORMISHERPETIFORMIS.
Ni ugonjwa wa ngozi unaotokea sana kwa wanaume kati ya umri wa miaka 20 hadi 50.
Ugonjwa huu wakati mwingine huhusiana na ugonjwa wa celiac, saratani ya maungo ya ndani ya mwili na matibabu ya kutumia immunoglobulin A au Viini Lishe Maalumu.
Malenge yanayozaliswha kutokana na ugonjwa huu huwa sugu, huweza kuwa makubwa , yenye usaha au kuwa na ugumu k**a vilele vidogo.
Mara nyingi vipele hivi hutokea kwa mpangilio unaofanana na pande mbili za mwili mfano kwenye makalio, magoti, usoni, kichwani na shingoni. Dalili zingine ni pamoja na muwasho mkali, hisia za kuungua na kung'atwa.
Baadhi ya malenge yanaweza kutoa usaha na majimaji yenye rangi ya damu iliyooza.
MAAMBUKIZI YA MALENGE YA KIRUSI CHA HERPES SIMPLEXSIMPLEX.
Malenge ya maambukizi ya kirusi cha Herpes simplex, ni kawaida sana kusababisha malenge yaliyo kwenye mkusanyiko kwenye maeneo ya midomo na sehemu ya chini ya uso.
Asilimia 25 ya wagonjwa wa kirusi huyu, huwa na malenge pia kwenye maeneo ya siri.
Sifa ya vipele hivi huwa vinawasha, vinachomachoma, kuleta hisia za kuungua na huwa kwenye makundi au kimoja kimoja na huwa na kipenyo cha milimita 2 hadi 3 na huwa haviungani kutengeneza upele mmoja mkubwa.
Upele unapopasuka hutengeneza kidonga kinachouma na kufuatiwa na kufanyika kwa gamba gumu juu ya kidonda.

Utandu mweupe(oral thrush) unakuwa k**a maziwa kwenye kinywa cha mtoto ni infection inasababishwa na fungus wanaoitwa ca...
17/01/2024

Utandu mweupe(oral thrush) unakuwa k**a maziwa kwenye kinywa cha mtoto ni infection inasababishwa na fungus wanaoitwa candida albicans.
CandidiasisThrush
Utandu(thrush) huo unamwadhiri mtoto sehemu ya ulimi ,kuta za mashavu kwa ndani na ufizi linawapata haswa watoto wachanga waliotoka kuzaliwa mpaka miezi 2-4,pia inawapata watoto wakubwa na watu wazima pia.

Sababu ya mtoto kupata utandu kinywani ni nini?

Candida fungus wanapoongeka kuwa wengi mwilini ndio wanasababisha mtoto kupata utandu kinywaji.candida fungus nao wanasababisha na haya matatizo ndio wanakuja kuzalishwa wengi kwenye mwili wa mtoto
Hana kinga ya kutosha mwilini na bado inajitengeneza ndio hapo inakuwa rahisi kwake kupata infection.
Mama alivyokuwa mjamzito au mtoto anapotumia dawa za antibiotic anapunguza kinga ya mwili ndio mana inakuwa rahisi kushambuliwa.
Mtoto akitumia antibiotic inasababisha kupunguza kinga wa bacteria
Mama anaenyonyesha nae akitumia antibiotic inachangia mtoto kupata utando
Mtoto anaweza pata hili tatizo kipindi anapozaliwa kupitia uke wa mama
Dalili za utando (thrush)

Mtoto atalia wakati wa kunyonya au kula
Mtoto atapata vipele vidogo vidogo sehemu ya matako,mapajani (diaper rash)
Utandu mweupe usio futika hata ukifutwa sehemu za ufizi juu,kuta za mashavu na juu ya ulimi images
4.Utando unaweza ambatana na rangi nyekundu k**a damu kwa mbali
5.Kunuka mdomo wa mtoto

Tiba
Utajuaje k**a ni utando wa maziwa au infection? ,safisha mikono yako vizuri kwa maji safi na sabuni,jaribu kuifuta na kidole uone k**a inaweza toka ,iwapo ikatoa ujue hayo ni maziwa tu ndio yametengeneza utandu,isipo toka ujue ni infection.

Utandu huo unaweza mletea mtoto vidonda pia mdomo ,utajua wakati wa kunyonyesha au kumpa kuchupa ya chuchu kunyoa anashindwa na kulia kutokana na maumivu anayopata,mpeleke hospital watamwandikia dawa ya maji au gel atakayo tumia baada ya wiki 1 hapo utaona mabadiliko.Madhara ya utando wa kiunywa unaweza mletea mtoto nappy rash

Homeremedies-tiba asilia unayoweza itengeneza nyumbani tumia
Mafuta ya n**i mpake sehemu ilio adhirika na mama paka kwenye chuchu,n**i ina fatty acid inasaidia kuuwa fungus, na inauwezo wa kurudisha kinga.
Apple cider vinegar nayo unaweza mpaka haina madhara
Mama anaweza kunywa mtindi (yoghut) inasaidia ila usimpe mtoto chini ya miezi 6-7
Baking soda -chemsha maji kikombe yakishachemka kabsa,epua na kuacha ya poe kidogo yawe vugu vugu kwa mbali weka baking soda koroga chukua kitambaa safi lowesha hayo maji na mpangusie mtoto kinywani penye utando.

Ushauri

Usafi ni muhimu sana kwa mtoto,mama hakikisha mat**i yako unasafisha vizuri sehemu ya chuchu kabla ujamnyonyesha ili tatizo lisijirudie sababu infection inaweza hamia kwenye chuchu,hakikisha unaosha vizuri chupa zake au pacifier (chuchu ya plastik) k**a mnampa kuinyonya.
image

Unaweza mpa paracetamol kupunguza maumivu ili amudu kula chakula (maziwa).Mama anae nyonyesha au mjamzito acha kutumia antibiotic inapunguza kinga ya mtoto na yakwako pia, sio kila ugonjwa lazima utumie antibiotic ni kali sana...

Umeipenda?
SHARE na Wengine

Address

Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share