Afya Zetu

Afya Zetu For reliable Information on how to treat your daily life in Healthy way Join us here..like our page

MAFUA NA DAWA ZAKE; FAIDA NA MADHARA YAKEMafua ni tatizo lenye kasi kubwa katika jamii na huambatana na dalili nyingi. K...
17/08/2025

MAFUA NA DAWA ZAKE; FAIDA NA MADHARA YAKE

Mafua ni tatizo lenye kasi kubwa katika jamii na huambatana na dalili nyingi.
Kawaida mafua ni tatizo linalokuja ghafla, lenye kutokana na maambukizi ya virusi maeneo ya mfumo wa hewa wa juu.

AINA ZA MAFUA
1. Mafua yatokanayo na virusi aina ya rhinoviruses (Common cold)
2. Mafua yatokanayo na virusi aina Influenza virus (Flu)

1. COMMON COLD (MAFUA)
Mafua haya huambatana na dalili zifuatazo ambazo ni kukohoa, pua kujaa maji maji mithili ya k**asi na huweza kuziba, homa ya kawaida na uchovu ambapo dalili hujitokeza kati ya siku 1 hadi 2 mara baada ya kukumbwa na virusi. Dalili nyingi hutoweka kati ya siku 7 hadi 10, ingawa dalili nyingine huchukua karibia wiki tatu kutoweka
Uwezekano wa kuugua mafua ya aina hii hupungua kadri umri unavozidi kuwa mkubwa. Baadhi ya tafiti zimeweza kutambua kuwa watoto huugua mara sita hadi nane kwa mwaka ikilinganishwa na wazee wenye umri chini ya miaka 60 ambao hupatwa mara tatu hadi nne kwa mwaka, wakati watu wenye umri zaidi ya 60 hupatwa mara moja kwa mwaka.
Ukiachana na sababu ya umri, sababu nyingine zinazopelekea kupatwa mafua ni kutopata muda wa kulala vya kutosha na mawazo.
Mafua ya aina hii kawaida hayawezi kusababisha madhara makubwa ila mgonjwa mwenye pumu, pneumonia na magonjwa mengine yupo hatarini zaidi
NB: Common cold (mafua) watu wengi huchanganya na aina hii nyingine ya mafua (influenza virus)

2. FLU (MAFUA)
Mafua ya aina hii husababishwa na virusi aina ya influenza, influenza virus vimegawanyika katika makundi matatu ambayo ni Influenza A, B au C. Influenza A na B huathiri zaidi wanadamu lakini Influenza A hupelekea dalili kuwa mbaya zaidi. Influenza virusi inaweza kuwa hatari zaidi kwa wazee na wenye kinga ya mwili pungufu. Kawaida wagonjwa wenye mafua yatokanayo na influenza virus huugua zaidi ya wale wenye mafua aina ya common cold. Mara nyingi dalili za mafua aina flu ni k**a zifuatazo joto la mwili kupanda, hali ya kujisikia baridi sana, maumivu ya kichwa, maumivu ya misuli, na hali ya kujisikia uchovu

MAKUNDI YA DAWA AMBAYO HUTUMIKA KATIKA MATIBABU YA DALILI ZA MAFUA (PHARMACOLOGIC AGENTS)
1. Kundi la dawa la decongestants
K**a mgonjwa ana shida ya pua kujaa maji maji na k**asi, dawa zilizopo katika kundi la decongestants husaidia zaidi kupunguza hali hio.
Decongestants ni dawa ambazo huongeza msukumo wa damu puani hivyo kupelekea kupungua kwa ujazo wa maji maji na k**asi puani
Dawa zilizopo katika kundi hili la decongestants ambazo hutumika sana ni phenylephrine na pseudoephedrine

Kundi hili la decongestant kuna dawa zipo katika mfumo wa sprei hasa zile zinazofanya kazi haraka na kwa muda mfupi dawa hizo ni ephedrine, na-phazoline, na phenylephrine, pia zipo dawa ambayo hufanya kazi kwa muda mrefu oxymetazoline.
Muunganiko wa dawa hizi za kundi la decongestants husaidia zaidi kupunguza hali hii ya tatizo la mafua.
Vidonge vya pseudoephedrine hutibu kwa haraka zaidi kuliko phenylephrine.

Dawa za kundi hili la decongestant ni salama zaidi endapo zikatumika kwa usahihi lakini matumizi yake hupelekea madhara zaidi kwa kuamsha mfumo mkuu wa fahamu. Baadhi ya madhara ni k**a yafuatayo kukosa usingizi, ongezeko la presha mwilini, kukosa utulivu, wasi wasi au hofu, mapigo ya moyo kuongezeka, na pia tatizo katika mfumo wa mkojo
Dawa hizi zinapaswa kuepukika kwa watu wenye matatizo ya moyo, shinikizo la damu, kisukari na kuvimba kwa tezi dume.
Pia dawa za kundi hili hazipaswi kutumiwa kwa pamoja na dawa za kundi la monoamine oxidase inhibitors ambazo ni rasagiline (Azilect), selegiline (Eldepryl, Zelapar), isocarboxazid (Marplan), phenelzine (Nardil), na tranylcypromine (Parnate).

2. Kundi la dawa la Antihistamines
Kundi hili la dawa linaweza kutumika Ili kupunguza hali ya pua kutokwa na maji maji au k**asi kwa wingi, macho yenye kuwasha na yenye kutoa maji maji na chafya inayoambatana na mafua aina ya common cold
Kundi la antihistamine zimegawanyika katika makundi mawili
Kundi la kwanza la dawa hizi ni brompheniramine, chlorpheniramine, na clemastine hupendelewa kutumiwa kuliko dawa za kundi la pili
Kundi la pili la dawa hizi ni cetirizine, fexofenadine, na loratadine. Dawa za kundi hili haziwezi kupenya na kuingia ndani ya ubongo

Ubora wa dawa kundi la kwanza umetokana na uwezo wa hizi dawa kufanya kazi maeneo ya histaminic na muscarinic katika ubongo (medulla).
Dawa hizi za husaidia kupunguza athari za mafua kwa haraka hata ikitumiwa aina moja ya dawa lakini imeonekana kusaidia zaidi endapo dawa za kundi hili zikatumiwa kwa pamoja na kundi la dawa la decongestant na dawa za maumivu

Kundi la kwanza la dawa za antihistamines huambatana na madhara tofauti tofauti kwasababu ya uwezo wake wa kuingilia mfumo mzima wa mfumo wa fahamu.
Dawa hizi zinapelekea kupatwa na usingizi mzito, hulevya, mwili kuchoka na pia zinapaswa kutumiwa kwa uangalifu kwa wagonjwa wenye matatizo la akili kwasababu zinaweza kupelekea upotevu wa kumbu kumbu na matatizo ya kutembea
Pia, dawa hizi za kundi la kwanza huambatana na madhara yafuatayo hupelekea macho kuwa makavu, mkojo kubaki kwenye kibofu, choo kigumu
Onyo; dawa za kundi la antihistamine zisitumike kwa wagonjwa wenye glaucoma na kuvimba kwa tezi dume

3. Kundi la dawa la Antitussives
Dawa nyingi utazozikuta kwenye maduka ya madawa kwaajili ya kutibu mafua utagundua dawa ya kundi hili ipo ndani hass dextromethorphan
Dextromethorphan ni dawa iliopo kundi la antitussive ambapo hupunguza zaidi hali ya kukohoa ambayo huambatana na mafua au magonjwa mengine ya koo.

Dextromethorphan hupatikana k**a dawa moja lakini pia unaweza kuipata katika muunganiko na dawa nyingine katika kutibu dalili zaidi ya moja ya mafua.

Endapo ikatumiwa kwa kiwango kikubwa dextromethorphan husababisha dalili za magonjwa ya akili kujitokeza ambazo hufanana na zile zitokanazo na dawa za phencyclidine na ketamine;
Pia kiwango kikubwa cha dextromethorphan hupelekea mapigo ya moyo kuongezeka, mabadiliko ya mfumo wa akili, shinikizo la damu, kifafa, coma na mapafu na moyo kufeli kufanya kazi

4. Kundi la dawa la Expectorants
Kundi hili la dawa hufanya kazi kwa kupunguza uzito na ujazo wa maji maji mithili ya k**asi puani kwa mgonjwa yeyote yule mwenye matatizo ya mfumo wa hewa.
Guaifenesin ni dawa pekee ambayo mara nyingi ndio hutumika katika kundi hili. Ijapokuwa guaifenesin imekuwepo katika muunganiko na dawa nyingine
Licha ya kukosekana kwa baadhi ya taarifa zinazohusu ubora wa dawa hii, lakini guaifenesin imeendelea kutumika k**a dawa bora katika kundi hili
Dawa hii ni salama na haijahusishwa na mwingliano na dawa nyingine. Endapo ikitumika katika kiwango sahihi, dawa hii inavumilika kwasababu mara nyingi imehusishwa kuwa na madhara katika mfumo wa tumbo

5. Dawa za kutuliza maumivu na homa (Analgesic & antipyretic)
Dawa k**a aspirin, paracetamol, ibuprofen na naproxen mara nyingi hutumika katika kupubguza maumivu mwilini, maumivu ya kichwa na homa ambayo huambatana na mafua
Dawa zote hutoa matokeo sawa kulingana na dalili za mafua, ila inabidi zitumike kwa uangalifu kwasababu zimeambatana na madhara makubwa
Mgonjwa ambae ana aleji na aspirin na yule mwenye vidonda vya tumbo hawapaswi kutumia aspirin au dawa ya maumivu

NAMNA YA KUJIKINGA MWENYEWE
Virusi wanaosababisha baridi na mafua wanaweza kuenezwa kutoka kwa mtu alieathirika kwenda kwa wengine kupitia hewa na migusano.

Pia, unaweza kupata maambukizi kupitia migusano ya kinyesi. Hii hutokea pindi unapogusana mikono na mtu mwenye maambukizi au kugusa uso wake alaf uguse tena macho, mdomo au pua yako.

Unaweza saidia kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa huu kwa kufanya yafuatayo:
* Osha mikono yako kwa sabuni na maji. Osha kwa muda wa sekunde 20, na kuwaosha watoto wadogo vivo hivo.

* Epuka kugusa macho, pua na mdomo kwa mikono kabla hujanawa baada ya kugusana na alie na mafua
* Kaa mbali na mtu alieugua ugonjwa huu. Watu waliougua ugonjwa huu wanaweza kueneza kutokana mgusano au ukaribiano
*

NINI CHA KUFANYA ILI UJISIKIE VIZURI
Hakuna matibabu sahihi ya baridi. Ili ujisikie vizuri unapaswa kupata muda mwingi wa kupumzika na unywe maji mengi.
Antibaotiki haziwezi kukupa nafuu kwasababu baridi na mafua husababishwa na virusi, hazifanyi kazi dhidi ya virusi wa koo la hewa.
-Epuka kutumia antibaotiki mara kwa mara km tiba ya baridi na mafua kwasababu antibaotiki hazifanyi kazi dhidi ya virusi bali hupelekea bakteria waliopo mwilini kuwa sugu

*HOMON IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI)*:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa n...
09/08/2025

*HOMON IMBALANCE (KUVURUGIKA KWA HOMONI)*
:Hili ni tatizo linalowakumba wakina mama(wanawake) wengi ambalo husababishwa na kiwango kidogo cha hormone ya ESTROGEN.

*VYANZO VYA KUVURUGIKA KWA HORMONE*
👉Utoaji wa mimba
👉Uwepo wa sumu mwilini.
👉kutokula mlo uliokamili au mfumo mbovu wa maisha.
👉Family history(upungufu wa ongezeko ya homoni ya progesterone
👉mabadiliko ya mazingira au hali ya hewa.
👉uzito mkubwa
👉Msongo wa mawazo.
👉Kutofanya mazoezi.
👉Matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango.
👉Kukoma kwa hedhi.

*Dalili za kuvurugika kwa homoni*
👉Maumivu wakati wa tendo LA ndoa.
👉Kutoshika mimba.
👉Mzunguko wa hedhi kubadilika.
👉Kuongezeka uzito.
👉Kupungua hamu ya tendo LA ndoa.
👉Kupoteza kumbukumbu.
👉Hasira za Mara kwa Mara.
👉Damu kutoka nyingi wakati wa hedhi au kutoa damu yenye mabongemabonge
👉Uke kuwa mkavu.
👉kutoka jasho jingi usiku.
👉maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
👉mzio wa vyakula/Allerg kuchaguachagua vyakula.

*Madhara ya kuvurugika kwa homoni*
👉kutoshika ujauzito kwa mda mrefu.
👉Mimba kuharibika

Umejifunza Kitu?
Comment na SHARE na wengine

🩺 *JE WAJUA CHANZO CHA UGONJWA WA PRESHA?* 🩺  SABABU KUBWA NI HIZI Presha ya kupanda (Hypertension) ni hali ya kimya ina...
27/05/2025

🩺 *JE WAJUA CHANZO CHA UGONJWA WA PRESHA?* 🩺 SABABU KUBWA NI HIZI

Presha ya kupanda (Hypertension) ni hali ya kimya inayoweza kusababisha matatizo makubwa k**a kiharusi, shambulio la moyo, na figo kushindwa kufanya kazi.

👉 *Visababishi vikuu ni:*
✔️ Kurithi kutoka kwa familia
✔️ Ulaji wa chumvi/mafuta kupita kiasi
✔️ Kukosa mazoezi
✔️ Msongo wa mawazo
✔️ Unywaji wa pombe na uvutaji sigara
✔️ Unene uliopitiliza
✔️ Umri mkubwa
✔️ Magonjwa ya figo au mfumo wa homoni

💡 *Kinga ni bora kuliko tiba!*
Jali afya yako mapema kwa kupima mara kwa mara, kufanya mazoezi, kula vyakula bora, na kupunguza msongo wa mawazo.

SHARE na wengine

Madhara ya kula chakula k**a hikiI. Kwa kuwa ndani yake kuna amira uwezekano wa kuwa na kitumbo cha chini ni asilimia 10...
24/04/2025

Madhara ya kula chakula k**a hiki

I. Kwa kuwa ndani yake kuna amira uwezekano wa kuwa na kitumbo cha chini ni asilimia 100%

II. Kwa kuwa kumeongezwa sukari na mafuta uwezekano wa kuwa na chelesto kwenye damu ni 100%

III. Kwa kuwa imetumika pure ngano uwezekano wa kuathiri mfumo wa chakula utumbo mdogo ni kwa 100%
. . . . . .. . . .
Badala yake, watu wale maandazi ya kuchoma au kuoka na moto kwani hayatumi mafuta wala sukari sana.

. . . . . . . . . . . . . .
Madhara yataanza kuonekana baada ya miaka 10 hadi 15 ya kutumia chakula k**a hiki. . . . . . . . .. . . . .
Magonjwa atakayopata zaidi ni kuwa na
- High blood pressure
- Kiungulia
- Utumbo mnene
- Gasi za tumboni
- Shinikizo la damu . . . . . . . . . . . . . . . . .
Comment na Share

07/04/2025

VIDONDA VYA TUMBO.
Tatizo hili husababiswa na bacteria tumboni waitwao H. Pyroli.

Kuna aina kuu tatu za vidonda vya tumbo. Nazo ni
1.Gastric Ulcers
2.Duodenal Ulcers
3.Ulcers in small intestine (Intestinal Ulcers)

1.GASTIRIC ULCERS
Aina hii ya vidonda vya tumbo hutokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo.
hii.

2.DUODENAL ULCERS:
Hii hutokea kwenye duodenum.

3.ULCERS IN SMALL INTESTINE (INTESTINAL ULCERS)
Aina hii ya vidonda vya tumbo kwenye sehemu ya utumbo mdogo(small intestine).

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
1.Tumbo kujaa gesi.
2.Kiungulia
3.Kinyesi nyenye rangi k**a kahawia
4.Maumivu makali ya tumbo k**a moto.
5.Kucheua au kutoa hewa chafu
6.Maumivu wakati wa kula au mara tu baada ya kula chakula.
7.kupata choo kigumu
8.Kukosa choo kwa mda mlefu.


MADHALA YA VIDONDA VYA TUMBO.

K**a bawasiri isipotibiwa kwa uhakika na mapema inaweza kusababisha madhala yafuatayo.Bawasiri Saratani ya utumbo.Kuathirka kwa ini Kuathiri kongosho.
Stress n.k

Kwa tiba na ushauri piga ✍️☎️+255756403981

MAGIMBI: CHAKULA CHA ASILI CHENYE LISHE NA MANUFAA MENGI Magimbi ni moja ya vyakula vya mizizi vinavyolimwa na kuliwa na...
26/02/2025

MAGIMBI: CHAKULA CHA ASILI CHENYE LISHE NA MANUFAA MENGI

Magimbi ni moja ya vyakula vya mizizi vinavyolimwa na kuliwa na jamii nyingi duniani, hasa barani Afrika, Asia, na Amerika Kusini. Ni chakula cha jadi kinachopendwa kwa sababu ya lishe yake bora na uwezo wake wa kutoa nishati nyingi.

1. Asili na Kilimo cha Magimbi
Magimbi yanatambulika kwa majina mbalimbali kulingana na maeneo tofauti, lakini kitaalamu, hutambulika kwa spishi kuu mbili:
- Colocasia esculenta (Taro) – Magimbi haya yana majani mapana k**a maboga, na mizizi yake hutumika k**a chakula kikuu katika baadhi ya maeneo.
- Dioscorea spp. (Yam) – Haya ni magimbi yenye umbo refu zaidi na ngozi ngumu yenye magamba, mara nyingi huota k**a mizizi mirefu inayotambaa ardhini.

Magimbi hustawi vizuri katika udongo wenye rutuba na unyevu wa kutosha. Hustahimili hali ya hewa ya joto na mvua nyingi, ndiyo maana hulimwa sana katika maeneo ya kitropiki k**a Tanzania (hususan Kagera, Kigoma, na Morogoro), Uganda, na Nigeria.

Katika mkoa wa Kagera, magimbi ni sehemu ya chakula cha asili, yakipikwa kwa njia mbalimbali k**a kuchemsha, kukaanga, au kuchanganywa na vyakula vingine k**a nyama, maharagwe, na mboga za majani.

2. Sifa za Magimbi
✅ Chanzo kikubwa cha wanga – Hutoa nishati ya kutosha kwa mwili, hivyo ni chakula bora kwa watu wanaofanya kazi ngumu.
✅ Nyuzinyuzi nyingi – Husaidia katika mmeng’enyo wa chakula na kupunguza matatizo ya tumbo k**a kukosa choo.
✅ Ladha laini na tamu– Magimbi yana ladha ya kipekee, hasa yakipikwa vizuri kwa kukaangwa au kuchemshwa.
✅ Rangi na muundo mbalimbali– Baadhi ya magimbi yana nyama nyeupe, ya njano au hata ya zambarau, na yote yana virutubisho vya kipekee.
✅ Yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu – Magimbi mabichi yanaweza kuhifadhiwa kwa wiki kadhaa bila kuharibika ikiwa yatahifadhiwa mahali pakavu na penye ubaridi.

3. Faida za Magimbi kwa Afya
✔ Huboresha afya ya moyo – Magimbi yana madini ya potassium ambayo husaidia kudhibiti shinikizo la damu na kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.
✔ Husaidia mmeng’enyo wa chakula – Kwa kuwa yana nyuzinyuzi nyingi (fiber), magimbi husaidia mfumo wa usagaji chakula na kuzuia matatizo k**a kuvimbiwa.
✔ Chanzo kizuri cha vitamini na madini – Yana vitamini A, C, na B-complex ambazo ni muhimu kwa afya ya ngozi, macho, na kinga ya mwili.
✔ Hupunguza hatari ya kisukari– Magimbi yana low glycemic index, hivyo husaidia kudhibiti kiwango cha sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari.
✔ Husaidia kupunguza uzito – Magimbi husaidia kushibisha haraka na kupunguza hamu ya kula vyakula vyenye mafuta mengi.
✔ Huimarisha mifupa– Yana madini k**a calcium, phosphorus, na magnesium yanayosaidia kuimarisha mifupa na meno.
4. Jinsi ya Kupika na Kula Magimbi
Magimbi yanaweza kuliwa kwa njia nyingi:
➡Kuchemsha – Hili ni njia rahisi ya kupika magimbi. Yanachemshwa hadi yalainike, kisha yanaweza kuliwa k**a yalivyo au kwa maharagwe na mboga.
➡Kukaanga – Magimbi hukatwa vipande vidogo na kukaangwa kwenye mafuta, k**a chipsi.
➡ Kupika kwa n**i – Njia hii huipa magimbi ladha tamu na laini.
➡ Kutengeneza uji au unga – Baadhi ya jamii hutengeneza unga wa magimbi na kuutumia kwa uji au vyakula vingine.
➡ Kuchanganya na nyama au maharagwe – Hii ni njia maarufu ya kula magimbi katika baadhi ya sehemu, kwani husaidia kuongeza virutubisho zaidi.

5. Umuhimu wa Magimbi Katika Utamaduni wa Kagera
Katika mkoa wa Kagera, magimbi ni sehemu ya chakula cha asili na hupewa heshima kubwa katika jamii. Mara nyingi hutumika katika kifamilia. Magimbi pia ni zao la biashara linaloweza kuingiza kipato kwa wakulima wa Kagera, endapo litapewa kipaumbele katika uzalishaji na masoko.

Magimbi ni chakula chenye faida nyingi, si tu kwa afya bali pia kwa uchumi wa wakulima. Ni wakati wa vijana wa Kagera kuwekeza katika kilimo na biashara ya magimbi kwa maendeleo ya mkoa wetu.

Jitaidi sana 👇Maji💦 → Kwa Ajili ya Figo!Mayai 🥚→ Kwa Ajili ya Ubongo 🧠!Carrots🥕 → Kwa Ajili ya Macho!Nanasi 🍍→ Kwa Ajili...
26/02/2025

Jitaidi sana 👇

Maji💦 → Kwa Ajili ya Figo!

Mayai 🥚→ Kwa Ajili ya Ubongo 🧠!

Carrots🥕 → Kwa Ajili ya Macho!

Nanasi 🍍→ Kwa Ajili ya Koo!

Cabbage 🥬 → Kwa Ajili ya Utumbo!

Tango 🥒 → Kwa Ajili ya Ngozi!

Tangawizi → Kwa Ajili ya Koo na Mapafu!

Parachichi & Nyanya 🥑 → Kwa Ajili ya Afya ya Moyo 🫀!

Mazoezi exercise🏋️ → Kwa Ajili ya Afya imara na Kinga Bora ya Mwili!

SABABU ZA MAUMIVU YA KIUNO NA MGONGO KWA WANAWAKEKUNA sababu nyingi zinazofanya wanawake wengi wasumbuliwe na maumivu ya...
27/10/2024

SABABU ZA MAUMIVU YA KIUNO NA MGONGO KWA WANAWAKE

KUNA sababu nyingi zinazofanya wanawake wengi wasumbuliwe na maumivu ya kiuno mara kwa mara hasa wakati wa hedhi na kuna wengine huugua kwa muda mrefu zaidi ya miezi mitano. Zipo sababu nyingi za kuzuka kwa maumivu haya k**a vile kuwa na matatizo kwenye via vya uzazi, kibofu cha mkojo, utumbo mkubwa au misuli ya nyonga kuwa na tatizo. Maumivu yanaweza kuwa yanaendana na mzunguko wa hedhi au la, mara nyingi hujitokeza chini ya kitovu na kiunoni.

Sababu ni nyingi ambazo zinaweza kusababisha mwanamke kupata maumivu haya ya kiuno kwa muda mrefu, k**a vile kuwa na maumbukizi ya ndani ya kiuno ya muda mrefu kitaalamu huitwa Chronic Pelvic Infection. Maambukizi haya hutokana na ugonjwa wa kifua kikuu (TB) na huweza kusababisha maumivu ya kiuno.

Sababu nyingine ni kuwa na Endometriosis, hii ni hali ambayo seli za ukuta wa uzazi huota sehemu nyingine za uzazi na itokeapo hivyo basi mwanamke hujikuta akipata maumivu makali wakati wa hedhi au tendo la ndoa. Wengine hupata maambukizi ya muda mrefu ya shingo ya uzazi au mji wa uzazi nayo husababisha maumivu ya kiuno wakati wowote na hasa wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Wanawake wengine hupata maumivu hayo kutokana na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi kitaalamu huitwa Ectopic Pregnancy. Baadhi ya wanawake hutokwa na uvimbe mdogomdogo wa kizazi ambao husababisha maumivu pale unapokua kwa haraka na kukandamiza viungo vingine. Maumivu yake huwa ya wakati, huja na kuacha.

Wengine hupata maumivu wakati wa kukojoa kutokana na kuwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo ya muda mrefu huku baadhi yao wakipata maumivu baada ya kupata maambukizi ya via vya uzazi kitaalamu huitwa Pelvic Inflammatory Disease – PID au wale wenye maambukizi ya Kibofu cha Mkojo yaani Interstitial Cystitis.

Wale wenye hali hii hupata maumivu hasa chini ya kibofu cha mkojo ambayo hupungua pale anapokojoa na hujikuta akikojoa mara kwa mara na kushindwa kubana mkojo. Lakini pia ugonjwa wa Kidole Tumbo yaani Chronic Appendicitis huleta maumivu upande wa kulia chini ya kitovu ambayo huwa hayatulii na dawa za kutuliza maumivu na wapo wanaougua kiunoni chini ya kitovu kutokana na kuwa na Saratani ya Utumbo Mpana.

Wapo wanaougua kiuno kutokana na kusagika kwa mifupa kwenye maungio yaani Degenerative Joint Disease na hali hiyo inapotokea husababisha maumivu makali maeneo ya kiunoni hasa wakati wa kutembea.

TIBA

Matibabu ya kuumwa na kiuno hutegemea na kinachosababisha k**a tulivyoeleza hapo juu. Nenda kamuone daktari na akigundua tatizo baada ya uchunguzi atakupa dawa husika wewe mgonjwa, au dawa za majira k**a tatizo linahusiana na mzunguko wa hedhi au atakufanyia upasuaji na atakupa ushauri.

UMEIPENDA??
SHARE na wengine waelimike

Namna ya kujikinga na  homa ya Nyani (M-Pox) *Tahadhari za kiafya zizingatiwe.*1. Tuepuke kusalimiana kwa mikono.2. Tuep...
20/08/2024

Namna ya kujikinga na homa ya Nyani (M-Pox)

*Tahadhari za kiafya zizingatiwe.*
1. Tuepuke kusalimiana kwa mikono.
2. Tuepuke kukumbatiana.
3. Tucheze muziki kwa kutogusana.
4. Vitakasa mikono, sabuni na maji tiririka viwepo kila mahali.
5. Tunawe kila mara.
6. Tutakase mikono kila mara.
7. Virusi vya Homa ya Nyani/tumbili (Monkeypox (Mpox)) imetangazwa na WHO kuwa janga la dunia.
8. Kujikinga ni nafuu, kujitibia ni ghali.

SHARE SHARE SHARE

ASUBUHI HII.... SUPU GANI UNAIPENDA HAPO? UNADHANI INA FAIDA GANI KIAFYA?COMMENT NA SHARE
10/07/2024

ASUBUHI HII....
SUPU GANI UNAIPENDA HAPO? UNADHANI INA FAIDA GANI KIAFYA?
COMMENT NA SHARE

UGONJWA WA    FANGASI Fangasi ni magonjwa yanayoathiri ngozi, kucha na nywele, pia huathiri mdomoni na ukeni. Magonjwa h...
07/03/2024

UGONJWA WA FANGASI

Fangasi ni magonjwa yanayoathiri ngozi, kucha na nywele, pia huathiri mdomoni na ukeni. Magonjwa haya huambukiza kwa njia ya kugusana ua kshirikiana nguo hasa za ndani na tauro.

Hapa tutaangalia fangasi katika kundi la magonjwa yanayoathiri ngozi, nywele na kucha (dermatomycosis).

Kuna aina kuu 5 za magonjwa ya fangasi wa ngozi, nywele na kucha k**a ifuatavyo;

Fangasi wa kichwani, ugonjwa huu huanza na sehemu ndogo ya ngozi ya kichwa na kukua kuwa sehemu kubwa. Huathiri nywele na kuzifanya dhaifu, laini na nyepesi kukatika au kung'oka. Huwaathiri sana watoti chini ya miaka 10 na hupotea mtu akisha barehe. Matibabu take ni splina,shake off,red bubble tea,sabuni dozi zake huanzia siku 6-14.

Fangasi wa mwili, ugonjwa huu hutokea mwilini, sehemu ya ngozi iliyoathiriwa huwa nyekundu, duara k**a shiringi na kukua huku ikiacha sehemu ya katikati kuwa na ngozi nzuri. Maduara haya yanaweza kukaa yakiwa kadhaa katika sehemu moja ya ngozi. Kwa ugonjwa uliokua sana na kwa wagonjwa wenye kinga ya mwili ndogo k**a wenye VVU, nivema wakatumia dawa ya kunywa

Fangasi wa nyayo na vidole, ugonjwa huu hutokea k**a mabaka na kuchanika katikati ya vidole na huwacha sana na kuuma pia. Matibabu yake maranyingi huwa dawa ya kupaka kwa wiki 4, kwa ugonjwa uliokua sana tumia dawa ya kunywa k**a splina, bubble tea kwa wiki 6-12.

Fangasi wa kucha, ugonjwa huu huathiri kucha na hubadilisha rangi ya kucha. Huzalishwa vitu k**a chaki na ambavyo vikisuguliwa huweza kupukutika. Kucha huweza kulika na inaweza kuisha. Ili kutibu ugonjwa huu nibora kutumia dawa za kunjwa na terbinafine na itraconazole zimeonekana dawa bora zaidi.

Pityriasis, huu ni ugonjwa wa fangasi ambao huathiri sehemu ya huu sana ya ngozi katika sehemu za usoni, shingoni na mgongoni. Hutokea k**a viduara vyenye mng'ao vinavyo washa. Huongezeka na huathiri sehemu kubwa ya ngozi visipotibiwa ingwa vinaweza kupotea vyenyewe. Maranyingi ugonjwa huu hauambukizwi Ila hutokea k**a ajari tu yaapotikea mabadiliko fulani ya mwili. Sio ugonjwa hari sana kiafya ila haukubaliki kwani huharibu mwonekano wa mtu has a unapotokea maeneo ya uso na shingoni. Matibabu yake ni sawa na yale ya fangasi wa mwili.

UFAHAMU UGONJWA WA VITILIGOVitiligo ni ugonjwa ambao unaathiri ngozi, unaotokana na kuharibiwa kwa cells za kutengeneza ...
25/02/2024

UFAHAMU UGONJWA WA VITILIGO

Vitiligo ni ugonjwa ambao unaathiri ngozi, unaotokana na kuharibiwa kwa cells za kutengeneza rangi ya ngozi zinazojulikana k**a (melanocytes). Chanzo halisi cha celi hizi kushambuliwa bado hakijajulikana kitaalam, hivyo Wataalam Wengi kupata ugumu wa kujua tiba sahihi ya ugonjwa huu.

Celi hizi zikishaharibiwa ngozi huanza kubadilika rangi kwa kuweka vidoa vyeupe, na mara nyingi huonekana zaidi kwa watu wenye ngozi nyeusi, ingawa ugonjwa huu unaathiri watu wote na wa rika zote.

Kitaalam Vitiligo hauambukizi isipokuwa unaweza kurithi kutoka kwa wazazi kutokana na genes anazobeba binadamu kutoka kwa wazazi, na hauna madhara kwa kuhatarisha maisha (kuua) zaidi ya kubadili rangi yako ya ngozi.

Watu wenye ugonjwa huu mara nyingi hutumia lotion za sun screen ili kuzuia ngozi isipate madhara yatokanayo kwa kupigwa na jua kali, hasa kwa nchi zenye jua kali.

Kwa wagonjwa wa vitiligo wanashauriwa Kuwasiliana daktari Daktari Wetu mara tu anapoona dalili zake, ili kumpa dawa za kurestore rangi ya ngozi ambayo imeanza kupotea,.

Vitiligo ni ugonjwa wa ngozi ambao unasababisha ngozi kuwa na mabaka mabaka meupe kwa sababu ya kupoteza melanin. Vitiligo inaathiri watu wa rangi yoyote ya ngozi japo kwa watu wengine huwa inaonekana zaidi kutokana na rangi yake ilivyo sanasana kwa watu wenye ngozi nyeusi. Pia inatokea katika umri wowote mara nyingi katika umri chini ya miaka 40.

Dalili zake ni zipi
Mgojwa wa vitiigo hapati dalili zozote bali mfano maumivu, kuwashwa au homa bali mwenye vitiligo huanza kuona mabaka meupe au madoa yakijitokeza katika ngozi yake

Nini kinasababisha vitiligo?
Vitiligo ni tatizo ambalo linatokana na kupungua au kupotea kwa chembechembe zinazoipa ngozi rangi yake zijulikanazo k**a melanin.
Kwa nini chembechembe hizo hupotea au kupungua?
Hutokea k**a seli zinazohusika na kuzalisha melanin zikifa au zikipungukiwa na ufanisi wa kufanya kazi. Melanin zinahusika na kuwezesha nywele, ngozi na macho kuwa na rangi yake.

kwa nini hizo seli zinafeli kuzalisha melanin
Sababu za moja kwa moja hazijulikani ila kuna mambo ambayo yanasemekana kuwa yanachangia kupata tatizo la vitiligo nayo ni k**a yafuatayo;
Madhara gani mtu mwenye vitiligo atapata?

1-Athari kisaikolojia kutokana na kufikiria namna gani watu wanaomzunguka wanavyomchukulia
2-Hatari ya kuathiriwa na jua inaongezeka kiasi kwamba hatari ya kupata hata kansa za ngozi inaongezeka
3-Pia hatari ya kupata matatizo ya macho inaongezeka

Matibabu ya vitiligo ni yapi?

Matibabu hutegemea na makubaliano ya mtu mwenye tatizo na daktari wake.
-Dawa za kupakaa ili kusaidia uzalishaji wa melanin
-Dawa ZA kuchemsha ili kuzuia muwasho
-Kupunguza melanin maeneo ambayo hayajaathiriwa ili kuleta ufanano na sehemu zilizoathiriwa (depigmentation)
-Upasuaji pia hufanyika (skin grafting)
Ukiwa na tatizo hili ni vizuri kumuona mtaalamu wa magonjwa ya ngozi (Dermatologist) ili uweze kusaidiwa pia ukiona dalili za tatizo hili inashauriwa kujilinda na jua na kutochora tattoo ambazo za kujaribu kuficha tatizo Hili la ugonjwa wa ngozi

Ugonjwa huu unatibika,Nenda hospitali mapema pindi ukiona dalali za ugonjwa huu ….

SHARE na wengine wapate elimu Hii

Address

Dar Es Salam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram