04/10/2022
*HORMONE IMBALANCE, HEDHI NA UZAZI WA MPANGO*
Ni kitendo cha kuongezeka au kupungua kwa vichochezi katika mwili wa mwanamke pale anapo pata hedhi, hivyo kufanya mwili kubadilika.
*DALILI ZA MVURUGIKO WA HOMONI*
⚫️Ukavu ukeni
⚫️Maumivu wakati wa tendo la ndoa
⚫️Kutoa jasho usiku
⚫️Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
⚫️Upungufu wa hamu ya tendo la ndoa
⚫️Mabadiliko ya siku za hedhi na kupata hedhi kwa muda mrefu unaozidi siku 7. (heavy bleeding, au kujaza pedi moja kwa saa moja)
⚫️Kukosa hedhi kwa muda mrefu, na kutoa damu yenye mabonge mabonge wakati wa hedhi
⚫️Uchovu wa mara kwa mara
⚫️Hasira za mara kwa mara⚫️Kukosa usingizi
⚫️Homa za usiku na Kizunguzungu cha mara kwa mara
⚫️Mzio wa vyakula (Allergie), kuchaguachagua vyakula
⚫️Ongezeko ya tumbo na nyama uzembe
⚫️Kuharibika kwa ngozi (chunusi, vipele… n.k)
⚫️Maumivu ya viungo
⚫️Upungufu wa nywele kichwani.
⚫️Kusahau sana (kukosa kumbukumbu)
⚫️Kuwa na hamu ya kula vyakula au vinywaji vya viwandani.
⚫️Kupata hedhi wakati wa ujauzito (progesterone ikiwa imezidi)
⚫️Kutokupata hedhi (balehe) adi umri wa miaka 20 na kuendelea
⚫️Mwili kutokukua, kuonekana k**a binti mdogo, na kutokukua kwa via vya uzazi
⚫️Msongo wa mawazo na kukosa kujiamini
⚫️Kusinyaa na kupauka kwa
ngozi wakati wa siku za hedhi na wakati wa utumiaji wa njia za uzazi wa mpango
⚫️Maumivu ya kichwa mara kwa mara
⚫️Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)
⚫️Kutokupata choo kwa wakati
⚫️Misuli hudondoka
*MADHARA YA MVURUGIKO WA HOMONI*
👉Kutoshika ujauzito kwa muda mrefu
👉Mimba kuharibika mara kwa mara
👉Kukosa mtoto au Ugumba
👉Maumivu wakati wa tendo la ndoa
👉Kuwa na tabia na maumbile ya kiume
👉UTI (Urinary Tract Infection)
👉Kuzeeka mapema
👉Kuziba kwa mirija ya uzazi
👉Uvimbe (Fibroids and Cysts).