Afya-Dr.Abely

Afya-Dr.Abely NASAIDIA WATU WENYE SHIDA SUGU ZA AFYA
Uzito bila mazoezi| nguvu za kiume| uzazi kwa jinsia zote nk

06/05/2024
22/04/2024

*DALILI ZA P.I.D*

Je ni wewe au ndugu, jamaa au rafiki yako? Okoa maisha yako/yake sasa tiba bora ya asili ya PID,UTI na fangasi sugu imepatikana

Mwanamke akianza kuonyesha dalili za ugonjwa wa P.I.D anaweza:

1. Kuhisi maumivu ya tumbo hasa maumivu chini ya kitovu
2. Kutokewa na maumivu ya mgongo mara kwa mara
3. Kutoa uchafu sehemu za siri ambao huambatana na harufu mbaya.
4. Kupata maumivu wakati wa kukojoa
5. Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa
6. Kupata damu bila mpangilio akiwa kwenye siku zake
7. Kuwa na homa mara kwa mara
8. Kichefuchefu
9. Kutapika
10 Kuwa na msongo wa mawazo na kuumwa kichwa

Kitendo Cha Kushiriki Tendo Kipindi Cha Hedhi Kina Madhara Makubwa Kwa Wanaume Na Wanawake.🎯 Matatizo ya tezi dume " PRO...
08/04/2024

Kitendo Cha Kushiriki Tendo Kipindi Cha Hedhi Kina Madhara Makubwa Kwa Wanaume Na Wanawake.

🎯 Matatizo ya tezi dume " PROSTETITS" Ni tatizo linalo wakumba Wanaume wengi na katika mfumo wa uzazi na hata kupelekea ugumba.

🎯 Maambukizi ya PELVIC INFLAMMATORY DISEASE (PID), Saratani ya shingo ya kizazi Na Kuziba kwa mirija ya uzazi, Matatizo haya usipo wahi matibabu inapelekea kutoshika mimba kabisa.

🎯 Damu ya hedhi husababisha Kulegea kwa mishipa ya uume nakupelekea tatizo la Uume kusimama Legelege. (Erectile-dysfunction).

🎯 Mwanamke kupatwa na maumivu makali ya tumbo (DYSMENORRHEA).

🎯 Kuongezeka kutoka kwa damu nzito Nyeusii na yenye mabonge, Sio hali ya kwaida ya hedhi, Nihatari kwa afya ya Uzazi.

🎯 Harufu mbaya mazingira machafu kusababisha adhari ya (kisaikolojia) Hivyo kupelekea kutofurahia tendo na kutoka mchezoni mapema,tuache tamaa.

NB: Siku 3-4 Hizo sio nyingii heshimu hedhi ya mpenzi wako, mis**ilize anahitajinini Nasio kumlazimisha akiwa katika hali ya hedhi yake. ZINGATIA βš– By @⁨Dr EmmyπŸ‘©β€βš•οΈ

*UMUHIMU WA KUTUMIA VIRUTUBISHO LISHE*Viumbe wote hai huhitaji chakula ili kuishi. Chakula huwapa binadamu nguvu ili waw...
08/04/2024

*UMUHIMU WA KUTUMIA VIRUTUBISHO LISHE*

Viumbe wote hai huhitaji chakula ili kuishi. Chakula huwapa binadamu nguvu ili waweze kufanya shughuli zao za kila siku, huwawezesha kujenga na kuikarabati miili yao, na huwawezesha kupambana na maradhi mbalimbali. Ili mwili uweze kuyafanya yote hayo na kuwa na afya nzuri, inabidi upate chakula cha aina mbalimbali. Mada ya leo inahusu umuhimu wa virutubishi katika mwili wa binadamu ambapo tutavitaja virutubishi hivyo na kuelezea umuhimu wa kila kimoja.

Kirutubishi Cha Mwili Ni Nini?

Chakula tunachokula ndicho kinachoupatia mwili virutubishi au vitu vinavyotoa nguvu mwilini, kuusaidia mwili kukua, kupambana na maradhi n.k. Kusudi mwili upate virutubishi hivyo kutoka kwenye chakula tunachokula, chakula hicho lazima kivunjwevunjwe kwanza. Zoezi hilo linaanza kwa kukitafuna chakula mdomoni, kukimeza na kwisha kufika tumboni. Kikifika tumboni, chakula hicho huchanganyika na maji na vimimina vingine zikiwemo tindikali na kisha kitaelekea kwenye utumbo mdogo. Virutubishi hufyonzwa na kuingia kwenye mfumo wa damu kupitia kuta za utumbo mdogo na kusambazwa mwilini. Mabaki yasiyofaa mwilini huelekea kwenye utumbo mpana na kisha kutoka nje ya mwili.

Kuna virutububishi muhimu sita ambavyo mwili unahitaji kupata tutoka kwenye chakula ili kuwa ana afya nzuri. Virutubishi hivi muhimu hugawanywa katika makundi makubwa mawili: micronutrients na macronutrients.

Micronutrients ni virutubishi ambavyo mwili wa mtu unahitaji kwa kiasi kidogo. Micronutrients ni pamoja na vitamini na madini.

Pamoja na ukweli kwamba mwili unahitaji virutubishi hivi kwa kiasi kidogo, ukosefu unaweza kusababisha maradhi.

Macronutrients ni virutubishi ambavyo mwili wa mtu unahitaji kwa kiasi kikubwa. Macronutrients ni pamoja na maji, protini, wanga na mafuta.

Kwa hiyo, kuna virutubishi sita ambavyo ni muhimu kwa afya ya mwili wa binadamu, navyo ni:

1. Protini
2. Wanga
3. Mafuta (fats)
4. Madini
5. Vitamini
6. Maji

Protini: Protini ni moja ya virutubishi vitatu vinavyohitajika kwa wingi katika mwili (macronutrients ), vingine vikiwa ni wanga na mafuta. Unapokula chakula chenye protini, huvunjwavunjwa na kuwa amino acids. Amino acids hutumika katika kujenga na kukarabati misuli ya mwili. Hii ni muhimu kwa watu wale ambao huwa na shughuli nzito au wanaofanya mazoezi. Sehemu zote za mwili zina misuli hivyo ni vizuri kupata chakula chenye protini ili kuirudishia kwenye hali yake. Protini vile vile husaidia katika kujenga kinga za mwili na afya ya ubongo. Vyanzo vikuu vya protini ni nyama, samaki, maziwa, siagi na mayai. Protini pia hupatikana kutokana na mimea; maharage, njegere zilizokaushwa, mbegu n.k.
Protini ni kirutubishi kinachotakiwa kwa wingi na mwili ambacho kinatakiwa na kila seli ya mwili ili kufanya kazi vizuri.

Protini hufanya kazi nyingi mwilini, ikiwa ni pamoja na:
kuhakikisha ukuaji wa misuli, mifupa, nywele, na ngozi kutengeneza kingamwili (antibodies), homoni, na vitu vingine vya muhimu kufanya kazi k**a chanzo cha fueli cha seli na tishu inapohitajika

Binadamu anaweza kuapata protini kupitia chakula. Chakula kifuatacho ni chanzo kizuri cha protini:
nyama nyekundu (tumia kwa kiasi kidogo na chagua nyama isiyo na mafuata) nyama ya kuku na batamzinga samaki na chakula kingine cha bahari maharage mayai bidhaa zitokanazo na wanyama soya njugu baadhi ya nafaka, pamoja na quinoa

Ingawa nyama na samaki ndicho chakula chenye protini kwa wingi zaidi, watu wasiokula nyama wanaweza kupata protini kutokana na bidhaa za mimea.

Wanga: Chakula cha wanga hukupa nguvu ili mwili uweze kufanya shughuli zake za kila siku vizuri. Glycogen ndani ya misuli ndicho kitu muhimu katika kukusaidia kuweka sawa kiwango cha nishati siku nzima. Chakula chenye wanga kikiliwa kongosho hutoa homoni iitwayo insulin. Insulin husaidia wanga uweze kuhifadhiwa kwenye misuli au k**a mafuta. Wanga uliohifadhiwa ndani ya mwili huitwa glycogen. Glycogen iliyohifadhiwa ndicho chanzo cha nishati katika mwili wako. Wanga hutokana na mahindi, ngano, shayiri, mchele na pia kutoka kwenye matunda na mboga.

Wanga hugawanywa katika makundi mawili: simple na complex. Wanga kutoka kwenye sukari ni simple carbohydrates na wanga kutoka kwenye nafaka ni complex carbohydrates. Wanga hutoa karibu kalori 4 kwa gramu na ndicho chanzo cha mwanzo cha nishati kwa misuli na ubongo.
Kabohaidreti ni ya lazima kwa mwili. Kabohaidreti ni sukari au wanga vinanavyotoa nishati kwa seli na tishu zote katika mwili.

Kuna aina mbili za kabohaidreti: simple na complex. Watu wanatakiwa kuwa waangalifu na matumizi ya simple carbohydrates, k**a mikate myeupe, pasta, na wali. Lakini , mwili unahitaji complex carbohydrates kwa ajili ya kusaidia katika shughuli zifuatazo:
mfumo wa kinga za mwili ufanyaji kazi wa ubongo mfumo wa neva nishati ili kufanya kazi mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

The Dietary Guilines for America wanashauri mtu apate asilimia 45-65 ya kalori zake kutokana na complex carbohydrates.

Chakula kifuatacho kina complex carbohydrates kwa wingi:
quinoa brown rice mboga za majani nafaka nzima (pasta, mkate, na vinginevyo vya kuokwa) oatmeal matunda shayiri.

Mafuta: Mafuta ni moja ya virutubishi vitatu vinavyohitajika kwa wingi na mwili, bila mafuta mwili hauwezi kuishi. Pamoja na kutoa kalori 9 kwa kila gramu, mafuta husaidia kuupa mwili joto wakati wa baridi. Mafuta pia hulainisha maungio ya mifupa. Mafuta hutunza baadhi ya vitamini k**a A, D, E na K. Chakula cha aina ya nyama na maziwa kina uwingi wa saturated fats na mboga zina kiwango kikubwa cha unsaturated fats. Mafuta hutoa kalori mara mbili ya protini. Mafuta hutunza afya ya ngozi na nywele.

Watu wengi wanahusisha chakula chenye mafuta mengi na afya mbaya. Ukweli ni kwamba mtu anahitaji aina fulani za mafuta ili kuwa na afya njema.

Mafuta huupa mwili nishati na kuasaidia baadhi ya shughuli. Lakini, inatakiwa kula mafuta yenye afya, k**a monounsaturated na polyunsaturated fats na kupunuguza au kukwepa kabisa saturated na trans fats.

Mafuta yenye afya yanasaidia katika kazi zifuatazo:
ukuaji wa seli kuganga kwa damu ujenzi wa seli mpya kuondoa hatari ya magonjwa ya moyo na kisukari miondoko ya misuli kuweka vizuri sukari katika damu tendaji kazi wa ubongo ufyonzaji wa vitamini na madini utengenezaji wa homoni utendaji kazi wa kinga za mwili

Mtu anaweza kupata mafuta yenye afya kutokana na:
njugu samaki, k**a samoni na tuna mboga za majani mbegu.

Vitamini

Vitamini ni virutubishi vinavyohitajika kwa kiwango kidogo na mwili na hutoa faida nyingi za kiafya, ikiwa ni pamoja na:
kuimarisha kinga za mwili kusaidia kuzuia au kupunguza kansa za aina fulani, k**a saratani ya tezi dume kuimarisha mifupa na meno kusaidia ufyonzwaji wa calcium kutunza afya ya ngozi kusidia mwili kuvunja na kujenga protini na wanga kutunza afya ya damu kusaidia utendaji wa ubongo na neva.

Kuna vitamini muhimu 13 ambazo wataalamu wa lishe huzigawanya katika makundi mawili: zinazoyeyuka katika mafuta na zile zinazoyeyuka katika maji.

Vitamini Zinazoyeyuka Katika mafuta ni :
Vitamini A Vitamini D Vitamini E Vitamini K.

Vitamini Zinazoyeyuka Katika Maji ni:
Vitamini B-1 (thiamine) Vitamini B-12 (cyanocobalamin) Vitamini B-6 Vitamini B-2 (riboflavin) Vitamini B-5 (pantothenic acid) Vitamini B-3 (niacin) Vitamini B-9 (folate, folic acid) Vitamini B-7 (biotin) Vitamini C

Kwa kawaida, mtu anayekula chaukula chenye uwingi wa mboga za majani, matunda, na minofu isiyokuwa na mafuta, anaweza kuapata vitamini zote anazozihitaji kutoa kwenye chakula chake. Lakini wale wanaokula matunda na mboga za majani kidogo, na wale wenye matatizo ya kiufyonzaji kwenye matumbo yao, wanahitaji kupata supplements za vitamini ili wasipatwe na tatizo la upungufu wa vitamini.

Madini

Madini ni kirutubishi kingine cha mwili kinachotakiwa kwa kiwango kidogo (micronutrient). Kuna makundi mawili ya madini: major na trace minerals. Mwili unahitaji madini kutoka makundi yote ili kuwa na afya nzuri.

Major minerals ni pamoja na:
magnesium calcium phosphorus sulfur sodium potassium chloride

Major minerals husaidia mwili katika:
kuweka vizuri viwango vya maji kutunza afya ya ngozi, nywele, na kucha kuboresha afya ya mifupa

Trace minerals ni pamoja na:
chuma selenium zinc manganese chromium copper iodine fluoride molybdenum

Trace minerals husaidia katika:
kuimarisha mifupa kuzuia kuoza kwa meno kusaidia kuganda kwa damu kusaidia kusafirisha oksijeni kusiadia kinga za mwili kusaidia kuweka sawa pressure ya mwili

Mtu anaweza kujihakikishia kupata madini ya kutosha kwa kula chakula cha aina ifuatayo:
nyama nyekundu (kula kiasi na chagua nyama isiyo na mafuta) chakula cha bahari chumvi (iodized table salt) maziwa na bidhaa nyingine za maziwa njugu na mbegu mboga za majani matunda kuku mkate na nafaka kiini cha yai nafaka nzima maharage na njegere.

Vitamini Na Madini: Vitamini na madini ni muhimu kwa miili yetu kwani huusaidia mwili kufanya kazi zake vizuri na kuongeza kasi ya ufanyaji kazi wa kemikali ndani ya mwili. Madini ya calcium na magnesium ni muhimu kwa mifupa yetu na chuma (iron) kinahitajika katika chembechembe nyekundu za damu ili kusafirisha oksijeni.

Kuna vitamini 13, ikiwa ni pamoja na vitamin A,B complex, C, D, E na F. Kwa sababu vitamini nyingi hazitengenezwi na miili yetu, zinatakiwa zipatikane kutoka kwenye chakula.

Pamoja na kwamba ni vitu muhimu, vitamini na madini huhitajika kwa kiwango kidogo. Vitamini na madini hupatikana katika chakula tunachokula, lakini kwa kawaida mahitaji ya mwili ya vitamini na madini ili uwe na afya huwa ni makubwa kuliko kiwango kinachopatikana kwa kula chakula.

Maji

Maji hujenga asilimia 65 ya mwili wa binadamu. Ni lazima mwili uwe na maji ili mwanadamu aweze kuishi. Maji yana kazi ya kusafirisha virutubishi kwenda kwenye seli na kutoa vitu visivyohitajika kutoka kwenye seli. Inashauriwa mtu anywe glasi 8 za vimiminika kwa siku. Wakati wa kufanya mazoezi, maji hufanya kazi ya kuupoza mwili.

Maji ni dhahiri ndicho kirutubishi muhimu zaidi kinachohitajika na binadamu. Mtu anaweza kuishi siku chache sana bila maji. Hata upungufu wa maji kidogo tu unaweza kuleta maumivu ya kichwa na kuzorota kwa utendaji kazi wa mwili na akili.

Mwili wa binadamu unajengwa kwa kiasi kikubwa na maji, na kila seli inahitaji maji ili kufanya kazi. Maji yanasaidia katika shughuli kadhaa za mwili, zikiwa ni pamoja na:
kutoa sumu nje ya mwili kuzuia mishtuko (shock absorption) kusafirisha virutubishi kuzuia kufunga choo kulainisha kuupa mwili maji

Chanzo kizuri cha maji ni kunywa maji asilia, ambayo hayajaongezewa utamu kutoka kwenye bomba au yaliyosindikwa kwenye chupa. Watu wasiopenda ladha ya maji wanaweza kukamulia limau au tunda lo lote la aina ya machungwa (citrus fruit).

Mtu anaweza kupata maji ya ziada kwa kula matunda yenye maji mengi.

Inashauriwa kukwepa kupata maji kutoka kwenye vinywaji vyenye sukari. Vinywaji vyenye sukari ni k**a chai iliyoungwa sukari, kahawa, soda, lemonade na juisi za matunda.

Mlo Kamili (Balanced Diet)

Mlo kamili (balanced diet) ni mlo ulio na virutubishi vinavyohitajika na mwili ili uweze kufanya kazi ipasavyo. Ili kupata virutubishi vinavyotakiwa kutoka kwenye mlo, unahitaji upate kalori nyingi kutoka:
kwenye matunda mboga nafaka nzima jamii ya kunde njugu nyama isiyo na mafuta

Kalori Ni Nini?

Kiwango cha kalori katika chakula ni kipimo cha nishati iliyohifadhiwa ndani yake. Mwili hutumia kalori kutoka katika chakula ili kukuwezesha kutembea, kufikiri, kupumua, na kufanya shughuli nyingine muhimu. Mtu wa kawaida anahitaji kiasi cha kalori 2,000 kila siku ili kuwa na uzito wa kawaida.

Lakini kiwango cha kalori kwa siku kwa mtu kinatofautiana kulingana na umri, jinsia, na uzito wa kazi zake. Kwa kawaida, wanaume huhitaji kalori nyingi kuliko wanawake, na watu wa mazoezi huhitaji kalori nyingi kuliko wale wasiofanya mazoezi.

Chanzo cha kalori katika mlo wako ni muhimu k**a kilivyo kiwango cha kalaori. Inashauriwa kupunguza matumizi ya kalori tupu (empty calories), au zile ambazo hazina au zenye thamani ndogo ndogo ya lishe. Kalori tupu ni zile zinazotokana na sukari na mafuta ya kuganda, k**a siagi.

JINSI YA KUONDOKANA NA TEZI DUME BILA UPASUAJIK**a wewe ni Baba ambaye umesumbuka sana na changamoto ya tezi Dume basi n...
04/04/2024

JINSI YA KUONDOKANA NA TEZI DUME BILA UPASUAJI

K**a wewe ni Baba ambaye umesumbuka sana na changamoto ya tezi Dume basi nina habari nzuri mno kwako

Nimekuandalia group la BURE kwa njia ya Whatsapp ambalo tutajifunza mwanzo mpaka mwisho na suluhisho tutapata

Tuma Neno TEZI DUME BILA UPASUAJI KWENDA 0755358371

Wahi sasa kwani hatutakuwa na Group la pili kwa changamoto hii.

*MAUMIVU YA MENO*                                πŸ₯¦πŸ₯¦ Una maumivu ya kichwa, ufizi unapiga, na mdomo wako unauma. Unamaumi...
04/04/2024

*MAUMIVU YA MENO*

πŸ₯¦πŸ₯¦

Una maumivu ya kichwa, ufizi unapiga, na mdomo wako unauma. Unamaumivu ya jino. Waweza muona daktari mapema k**a sivyo basi fuatisha hapa chini katika tuba hizi rahisi..........

πŸ“ŒπŸ“Œ

*-Kuosha na maji ya chumvi:*
Kwa watu wengi,kusukutua kwa maji ya chumvi ni matibabu bora ya mstari wa kwanza. Maji ya chumvi ni dawa ya asili ya kuua vijidudu ambayo inaweza kusaidia kufungua chembe za chakula na uchafu ambao unaweza kukwama kati ya meno. Kutibu maumivu ya jino kwa maji ya chumvi pia kunaweza kusaidia kupunguza uvimbe na kuponya vidonda vya mdomo.

*Tumia: Changanya 1/2 tsp. Kijiko 1 cha chumvi kwenye glasi ya maji ya uvuguvugu na uitumie k**a suuza kinywa.*

*- Kitunguu saumu*:
Kitunguu saumu kimetumika sana kwa madhumuni ya dawa katika historia. Ina kiwanja kinachoitwa allicin, ambacho kinaelezea mali yake ya nguvu ya antibacterial.

*_Tumia: Ponda kitunguu saumu safi kisha changanya na chumvi kidogo, kisha pakaa kwenye jino lililoathirika. _*

*-Karafuu*:
Karafuu zina mali ya asili ya kutuliza maumivu na antibacterial. Wao ni sehemu ya kawaida ya dawa za asili za Kichina na Kihindi, ambapo zimetumika kwa karne nyingi kutibu kila aina ya maumivu. Karafuu inachukuliwa kuwa yenye ufanisi hasa katika matibabu ya maumivu ya jino. Matumizi na maagizo: Tumia karafuu kavu au mafuta muhimu ya karafuu. Karafuu zilizokaushwa zinaweza kuwekwa kati ya jino lililoathiriwa na shavu ili kupunguza maumivu ya jino. Unaweza pia kuzama pamba ya pamba katika mchanganyiko wa matone machache ya mafuta ya karafuu na kiasi kidogo cha mafuta. Ikiwa utaweka pamba karibu na jino lako la kidonda, maumivu yanapaswa kupunguzwa kwa muda mrefu unapoiweka. Karafuu hazina ladha nzuri zaidi, kwa hivyo epuka kupaka mafuta ya karafuu au juisi kwenye ulimi wako.



*-Majani ya Mpera*:
Kwa kiasi kikubwa kwa ajili ya mali zao za kuzuia-uchochezi, kutuliza maumivu, na antimicrobial, majani mapya ya mpera yanaweza pia kutoa ahueni kutokana na maumivu ya meno. Kutumia: Tafuna majani ya mpera moja au mawili hadi juisi ianze kufanya kazi kwenye eneo lililoathiriwa. *Unaweza pia kutafuna majani mabichi ya mchicha kwa athari sawa*. Njia nyingine ya kutibu jino linalouma ni kuchanganya baadhi ya majani ya mpera na maji yanayochemka. Acha mchanganyiko upoe na sukutua kinywa chako.

*--Pilipili hoho*:
Capsaicin, dutu inayopatikana kwenye "hoho" za pilipili ambayo hupa mwili joto, hutumiwa kwa kawaida kupunguza *maumivu ya neva.* Na hiyo inaweza kujumuisha mishipa kwenye meno. Uchomaji huu unaojulikana ambao hufanya pilipili nyekundu kuhisi kuwa mbaya sana husababishwa na capsaicin, kwani huingiliana na mishipa ya ulimi na njia za pua.

*Tumia: Jaribu kuongeza matone machache ya mafuta au ubga wa hoho kwenye mpira wa pamba na kusugua kwenye jino lako lenye shida. Vinginevyo, unaweza kujaribu kutafuna pilipili. Onywa: mara capsaicin iko kwenye ulimi wako, itawaka! Bandika.*

*-Tangawizi-Cayenne:*
Tangawizi ni dawa yenye nguvu ya kutuliza maumivu. Kuchanganya na cayenne ( pilipili kichaa) ni dawa yenye nguvu.

*_Tumia: Changanya sehemu sawa za viungo hivi viwili vya hali ya joto na maji ya kutosha kutengeneza unga. Pindua pamba ndogo katika kuweka ya kutosha ili kueneza, kisha kuiweka kwenye jino lako, kuepuka ufizi na ulimi. Iache mpaka maumivu yamepungua - au kwa muda mrefu k**a unaweza kuiacha._*

*-s**i ya apple cider:*
Apple cider s**i sio tu ina mali ya kuzuia uchochezi na antiseptic, lakini pia ni tindikali kwa sababu inaua bakteria zinazosababisha maumivu ya meno.

Tumia: Unaweza kutumia s**i ya apple cider kwa kutuliza maumivu kwa kutumbukiza pamba ndani yake na kukandamiza jino kwa upole.

*Baking soda*

Inashangaza ni wangapi hutumia baking soda ya kuoka kwa kuwa ina mali ya kuzuia uchochezi ambayo itaondoa uvimbe wowote. Asili yake ya antibacterial pia itasaidia kutibu ugonjwa wowote wa jino au ufizi ambao unaweza kusababisha maumivu.

Tumia: Loanisha pamba na maji na uifunike kwa baking soda. Weka mpira wa pamba dhidi ya jino lililoathiriwa ili kuondoa maumivu ya meno.

*-Thyme:*
Thyme pia ni mali yenye nguvu ya antibacterial na antioxidant ambayo inaweza kusaidia kutibu maumivu ya meno.
Tumia: Piga matone machache ya mafuta muhimu ya thyme na matone machache ya maji kwenye pamba ya pamba. Punguza ukali wa mafuta kwa kuweka majinkidogo. Unaweza pia kuongeza tone la mafuta kwa glasi ndogo ya maji na kufanya kunywa.

Ice Cubes Barafu inaweza kusaidia kupunguza maumivu ya meno kwa kufinya miisho ya neva.

Tumia: Funga mchemraba mdogo wa barafu kwa moja ili kusababisha maumivu zaidi.

Baraka ziwe nawe

Ndimi,
*MLINZI UKUTANI*

Ifahamu Saratani Ya Tezi Dume: Mambo 7 Usiyo yajua.↩️ Saratani ya tezi dume ni ugonjwa hatari unaoathiri maelfu ya wanau...
04/04/2024

Ifahamu Saratani Ya Tezi Dume: Mambo 7 Usiyo yajua.

↩️ Saratani ya tezi dume ni ugonjwa hatari unaoathiri maelfu ya wanaume duniani kote kila mwaka. Katika makala hii tutazungumzia mambo 7 usiyo yajua kuhusu tezi dume.

Maana Ya Tezi Dume:πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

πŸ‘‰Tezi dume ni moja ya tezi la uzazi la kiume ambalo kila mwanaume analo. Tezi dume sio ugonjwa bali ni kiungo k**a viungo vingine mwilini.

πŸ‘‰Ifahamu saratani ya tezi dume: Mambo 7 usiyo yajua
Tezi Dume Inapatikana Wapi Katika Mwili?

πŸ‘‰Tezi dume inapatikana chini ya kibofu cha mkojo na inazunguka njia ya mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume.

πŸ‘‰ Kazi Za Tezi Dume Katika Mfumo Wa Uzazi:

kutengeneza majimaji ya uzazi wa mwanaume (shahawa) ambayo husaidia kurutubisha mbegu za kiume zilizotengenezwa kutoka kwenye korodani, ambapo wakati wa tendo la ndoa, mwanaume anapofika kileleni, tezi dume hukamulia majimaji (shahawa) ndani ya mrija wa mkojo na kutolewa pamoja na mbegu za kiume k**a manii (Semen). Pia husaidia mbegu za kiume kubaki na uhai kwa muda unaostahili.

πŸ‘‰ Aina Za Magonjwa Ya Tezi Dume:

Kuna aina tatu za magonjwa ya tezi dume ambazo ni;

1) Maambukizi ya bakteria (Prostatitis).

2) Kukua kwa tezi dume ambalo sio saratani (Benign Prostate Hyperplasia-BPH)).

3) Saratani ya tezi dume.

Soma pia hizi makala:

Zijue Dalili 7 Za Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Tiba Zake.

πŸ‘‰ Maana Ya Saratani Ya Tezi Dume:

Saratani ya tezi dume maana yake ni tezi dume imepata ugonjwa wa saratani (cancer). Tatizo Linakuja kiungo hiki (tezi dume) kinapoanza kutanuka kutokana na kugawanyika Kwa chembe chembe hai zake bila kufuata utaratibu wa mfumo wa mwili.

Chembechembe hizi mwishowe hutengeneza vivimbe hatari ndani ya tezi dume na hatimaye husambaa mwilini. Takwimu zinaonesha kwamba kati ya wanaume 10, wa 5 na kuendelea wana dalili za kutanuka kwa tezi dume.

Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vitokanavyo na saratani kwa wanaume duniani. Pia ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wenye umri wa miaka 70 na kuendelea.

Address

Dodoma

Telephone

+255755358371

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya-Dr.Abely posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya-Dr.Abely:

Share