Afya Yako Point

Afya Yako Point We Care About Your Health

16/04/2026

FIGO YAKO NI UHAI WAKO, USIPUUZE DALILI!

​Video hii fupi inaonyesha ukweli mchungu wa jinsi Saratani ya Figo inavyoanza k**a uvimbe mdogo (Kidney Tumor),na usipoidhibiti mapema, inakua na kuanza kusambaza sumu na seli za saratani kwenye viungo vingine k**a Ini na Mapafu,na inapofika hatua hii ambayo inakuwa vigumu zaidi kutibu.

​Swali ni je, unajuaje k**a figo yako ina shida?
Watu wengi hawajui dalili, lakini angalia hizi:
1️⃣ Mkojo wenye damu (hata k**a ni mara moja).
2️⃣ Maumivu ya upande mmoja wa kiuno au mgongo wa chini yasiyoisha.
3️⃣ Uvimbe unaoonekana au kuhisi maumivu pembeni ya tumbo.
4️⃣ Kupoteza hamu ya kula na uzito kupungua bila sababu.
5️⃣ Uchovu uliokithiri kila wakati.

​Nini cha kufanya?

​Fanya vipimo vya figo angalau mara moja kwa mwaka.Saidia figo zako kufanya kazi vizuri kwa kunywa maji ya kutosha kuende na na mwili wako.
​Punguza Chumvi na Sukari maana hivi ni maadui wakubwa wa figo.
​Acha Sigara maana Uvutaji wa sigara unaongeza hatari ya kupata saratani hii.

​Usisubiri mpaka uone maumivu makali. Shiriki video hii na ndugu au rafiki, unaweza kuokoa maisha ya mtu leo!
Na kwa wewe ambaye tayari una changamoto yoyote figo tuma neno AFYA leo.

​ JaliAfyaYako AfyaCheck KingaNiBora

Maumivu ya kifua siyo kitu cha kupuuza…Watu wengi hudhani ni uchovu tu lakini mara nyingi ni ishara ya sumu mwilini kuan...
15/04/2026

Maumivu ya kifua siyo kitu cha kupuuza…
Watu wengi hudhani ni uchovu tu lakini mara nyingi ni ishara ya sumu mwilini kuanza kuathiri mifumo muhimu.

Unajikuta;
Unachoka haraka bila sababu.
Unapata maumivu yasiyoeleweka
Mwili unakuwa mzito au hauna nguvu

Hizi ni dalili ambazo watu wengi huzipuuza…mpaka zinakuwa kubwa zaidi.

Mwili wako unahitaji kusafishwa (Detox) ili kurudisha balance ya ndani.

Detox nzuri inasaidia:
Kusafisha sumu mwilini
Kuboresha mzunguko wa damu
Kurudisha nguvu na uhai wa mwili

Usisubiri hadi hali iwe mbaya zaidi.
📲 Wasiliana nasi sasa: 0746 334 963
Upate ushauri na kuanza safari yako ya afya leo.

Shinikizo la damu (Presha au BP) na Kisukari ndio shida  “namba moja” na muhimu sana kwa hatari ya afya ya Figo.Preqha i...
15/04/2026

Shinikizo la damu (Presha au BP) na Kisukari ndio shida “namba moja” na muhimu sana kwa hatari ya afya ya Figo.

Preqha inapokuwa juu sana au chini sana bila kudhibitiwa, inaharibu kimya kimya vichujio vidogo vidogo vya Figo (nephrons) na kupelekea matatizo makubwa k**a ugonjwa wa Figo Sugu(CKD)au hata kushindwa kwa Figo(Kidney Failure).

Ikiwa ni la juu, linazidisha uharibifu; ikiwa la chini, uchujaji wa damu unapungua na sumu zinajilimbikiza mwilini.

Kudumisha shinikizo la damu katika kiwango salama ni moja ya njia bora za kulinda figo zako kila siku!

Usiendelee kuteseka wakati suluhisho lipo,kwa wewe ambaye tayari una Changamoto ya Figo au unataka kulinda na kuzipa Figo zako ubora,wasiliana nami kupitia 0746 334 963 ili kupata suluhisho na kuondokana na changamoto hii leo.

Figo zinaweza kupona wakati mazingira sahihi yanapokuwepo na sayansi inathibitisha hilo. Figo za mtu mzima zina njia za ...
13/04/2026

Figo zinaweza kupona wakati mazingira sahihi yanapokuwepo na sayansi inathibitisha hilo.

Figo za mtu mzima zina njia za kujirekebisha zenyewe,ila zimeshindwa au zinashindwa tu kufanya kazi ndani ya mwili ulio na uchochezi sugu, sumu nyingi, na mfumonwq mmeng’enyo uliyoharibika.

Ndio maana watu wengi wanaona creatinine ikishuka na GFR ikipanda kiasili kwa sababu mara nyingi tunashughulikia yale yanayoleta mabadiliko halisi:
✅ Kupunguza uchochezi sugu wa mwili
✅ Kudhibiti sukari na shinikizo la damu
✅ Kurejesha utendaji wa detoxification na mitochondria
✅ Kufuata mpango maalum unaotegemea matokeo ya vipimo vyako.

Hauhitaji kuwa mkamilifu unachohitaji ni kuacha kuzipa figo zako sababu za kuendelea kushuka.

Jiulize swali hili; Kwa nini vituo vya dialysis vinaongezeka kwa kasi kuliko vituo vya uponyaji wa figo?

Figo zako bado zina uwezo wa kujirekebisha kiasili na kupona kabisa.

Hali inabadilika kadri unavyochelewa.
Wewe mwenye changamoto ya figo,kuna suluhisho la uhakika cha kufanya tuma neno FIGO au wasiliana nami kwa simu 0746 334 963

11/04/2026

FIGO ZAKO, UHAI WAKO USIPUUZE HIZI ISHARA!

​Ugonjwa wa figo (CKD) ni kimyakimya, lakini picha hii inaonyesha wazi hatua 5 za hatari unazopaswa kuzijua. Kutoka hatua ya 1 hadi ya 5, afya ya figo inaweza kufifia bila wewe kuhisi maumivu makali mwanzoni.

Kumbuka ​eGFR ndiyo namba inayoeleza uwezo wa figo zako. Ikiwa namba inapungua, hatari inaongezeka.Kisukari na Presha ya juu ndio maadui wakubwa wa figo.

Ishara za hatari amabzo hutakiwi kuziona k**a kitu cha kawaida ni pamoja na Kuvimba miguu, uchovu uliokithiri, na mabadiliko ya mkojo.

Usiisubiri hadi figo zifikie hatua ya kufeli kabisa. Kinga ni bora kuliko tiba dhidi ya Dialysis au Kupandikiza figo).
​✅ Pima eGFR na mkojo leo ili kujua hali yako.
✅ Dhibiti sukari na presha yako sasa.

Kwa wewe ambaye tayari unachangamoto ya figo au dalili nina suluhisho maalum kwa ajili yako ndani ya siku 30,tuma neno AFYA ili uweze kupata msaada leo.

Sambaza elimu hii! Share picha hii na ndugu au rafiki ili kuokoa maisha.

Watu wengi hufikiri presha ya damu ni lazima itokane na urithi wa familia,lakini mara nyingi si hivyo...Presha inaweza k...
10/04/2026

Watu wengi hufikiri presha ya damu ni lazima itokane na urithi wa familia,lakini mara nyingi si hivyo...Presha inaweza kuja kutokana na:

Chumvi nyingi mwilini

Madini muhimu kuwa machache

Uvimbe ndani ya mwili

Sumu zinazojilimbikiza

Msongo wa mawazo wa kila siku

Mishipa ya damu midogo,hivyo damu inapita kidogo kwa nguvu na kufanya mwili unapata shida.

Habari njema unaweza kubadilisha hali hii!

Anza kwa kusafisha mwili (detox), kisha ujenge upya kwa maji ya kutosha, vyakula vyenye madini vinavyosaidia damu kuzunguka vizuri.

Mabadiliko madogo ya kila siku yanaweza kuleta tofauti kubwa.

Unataka kupunguza au kutibu presha yako kwa njia sahihi na ya asili?
Nimeandaa programu ya siku 15 inayokufundisha hatua kwa hatua.
Andika "AFYA" hapa chini ili uipate leo,na hii ni kwa watu 15 tu

10/04/2026

JE, MIGUU YAKO INAVIMBA HIVI? USIPUZE!

​Video hii inaonyesha hali kitaalamu inaitwa Edema (kuvimba kwa miguu kutokana na maji kujaa). K**a ukibonyeza mguu wako na kuacha "shimo" ambalo halirudi haraka (Pitting Edema), huo ni ishara ya mwili wako kutoa onyo.

​Miguu kuvimba si ugonjwa wenyewe, bali ni dalili ya kitu kingine mwilini. Inaweza kusababishwa na:

​Matatizo ya Moyo: Moyo kushindwa kusukuma damu vizuri.

​Magonjwa ya Figo: Figo kushindwa kutoa maji na chumvi ya ziada.

​Ini: Matatizo ya ini yanayopunguza protini mwilini.

​Mishipa ya Damu (Venous Insufficiency): Damu kushindwa kurudi juu kuelekea moyoni.

​Mtindo wa Maisha: Kukaa au kusimama kwa muda mrefu sana na kula chumvi nyingi.

​Hali hii isipodhibitiwa mapema hupelekea kutokea kwa;

​Maumivu makali na ugumu wa kutembea.

​Ngozi kuwa ngumu, kuwasha, na kupasuka (vidonda vya miguuni).

​Hatari ya maambukizi ya ngozi (Cellulitis).

​Hatari ya damu kuganda (Blood Clots/DVT) ambayo ni hatari kwa uhai.

Sasa hali hii inapotokea,wasiliana na Daktari,ikiwa uvimbe huu ni wa kudumu, unaambatana na maumivu au unazidi kuwa mkubwa, nenda hospitali haraka kufanya vipimo vya moyo, figo na ini.

Kumbuka, kila mwili una sababu yake ya kutoa ishara hizi. K**a wewe au mpendwa wako anapitia changamoto hii na ungependa kufahamu namna ya kusaidia mfumo wako wa damu na maji mwilini kurudi katika hali ya kawaida kwa njia asilia,Nitumie ujumbe neno 'AFYA' sasa hivi. Tuangalie namna ya kukusaidia kuondoa uvimbe huu kuanzia chanzo chake.

Alipoambiwa ana Kisukari cha Aina ya 2, alikaa kimya tu.Daktari alimwambia “Utakunywa dawa maisha yako yote.” Moyo wake ...
09/04/2026

Alipoambiwa ana Kisukari cha Aina ya 2, alikaa kimya tu.
Daktari alimwambia “Utakunywa dawa maisha yako yote.” Moyo wake ulijaa butwaa.

Alikuwa na hofu pamoja na kuogopa kila siku kuamka akiwa na uchovu, kula chakula halafu ajisikie usingizi na ulegevu, na kuogopa kuwa mgonjwa wa kudumu.

Lakini siku moja aliamua,hatosubiri dawa zimuongezee miaka, na kuamua kupigana vita na kuvishinda!

Akaacha kuwa “mgonjwa wa kila siku” na akaanza kuwa Mpiganaji wa Kisukari.

Hatua kwa hatua, nilimsaidia kuacha dawa kabisa, hamu ya tendo ikarudi,akapunguza hamu ya vyakula vitamu, akaondoa mafuta ya tumbo, na sasa ana nguvu na furaha siku nzima bila kuchoka ovyo.

Kisukari si ugonjwa wa sukari tu… ni tatizo la insulini.
Na habari njema ni kwamba mwili wako una uwezo wa kuurekebisha na kuuacha kabisa!

Hizi ndiyo silaha 3 rahisi nilizotumia kumsaidia kupona kisukari;

Kuboresha mlo mmoja tu

Kutembea dakika 45 kila siku

Kufuatilia insulini (si sukari tu)

Sasa nipo hapa na kukuambia na wewe au mtu unayemjua ana kisukari, na umechoka na vidonge na uchovu wa kila siku…

Andika neno "REVERSE" kwenye comment nikupe mpango wa kuanza safari ya kurudisha afya yako bila dawa na bila stress.

Hatua ndogo unayoichukua leo inaweza kukupa na kubadili maisha yako kesho. Usikae tu… anza sasa!

KisukariAsili

Ini lenye Afya (Healthy Liver)kazi yake kubwa niKuchuja damu, inazalisha nyongo(majimaji ya kuyeyusha mafuta), inahifadh...
07/04/2026

Ini lenye Afya (Healthy Liver)kazi yake kubwa ni
Kuchuja damu, inazalisha nyongo(majimaji ya kuyeyusha mafuta), inahifadhi glycogen (hifadhi ya nishati), inatengeneza protini muhimu (k**a albumin), na inasafisha sumu mwilini.

Ini lenye afya linarekebisha na linaweza kukua tena baada ya kuumia iwapo kuna tishu zenye afya za kutosha zilizobaki.

Ini lenye Mafuta (Fatty Liver / Steatosis) hapa kinachotokea ni kuwa matone ya mafuta hujilimbikiza ndani ya seli za ini (hepatocytes)na sababu kuu ni kunenepa kupita kiasi, upinzani wa insulini, unywaji pombe mwingi, na baadhi ya dawa.

Ini lenye mafuta ni tatizo la kawaida sana ulimwenguni na ugonjwa wa ini lenye mafuta usiotokana na pombe (NAFLD) huathiri hadi 25% ya watu duniani na hali inaweza kurekebishwa kwani mabadiliko ya mapema ya mafuta kwenye ini yanaweza kurekebishwa kwa urahisi kwa kupunguza uzito, kula vizuri, kufanya mazoezi, na kupunguza unywaji wa pombe.

Fibrosis (Ini lenye Kovu) kinachotokea ni Kuumia mara kwa mara kwa ini husababisha uundaji wa tishu za kovu (fibrous tissue). Tishu hii ya kovu inachukua nafasi ya baadhi ya tishu za kawaida za ini, na hivyo kuvuruga muundo wa kawaida wa ini.

Fibrosis hugawanywa katika hatua (F0–F4) kwa kutumia vipimo visivyohitaji upasuaji (k**a FibroScan, vipimo vya damu) au biopsy,na Fibrosis ya mapema wakati mwingine inaweza kupunguzwa au kusimamishwa kabisa kwa kutibu sababu kuu inayosababisha.

Cirrhosis (Ini lililoharibika kabisa / Cirrhosis) ni kovu lililoenea sana na la hali ya juu linaharibu muundo wa ini na mtiririko wa damu. Tishu zilizobaki za ini zinashindwa kufanya kazi zake muhimu.Watu wenye cirrhosis wanaweza kujisikia vizuri kwa miaka mingi hata k**a ini limeharibika sana.Matibabu yanazingatia kutibu sababu, kufuatilia hali, na kuzuia matatizo. Katika hatua za juu sana, kupandikiza ini (liver transplant) kunaweza kufikiriwa.

Saratani ya Ini (Liver Cancer / Hepatocellular Carcinoma)seli za ini zinageuka kuwa mbaya (malignant) mara nyingi hii hutokea kwenye msingi wa cirrhosis na hivyo kuuna hivyo kuunda uvimbe (tumors) ambao huharibu kazi ya ini na unaweza kuenea sehemu nyingine za mwili.
Wasiliana nami leo kupata suluhisho kwa kuandika neno AFYA dm

Ubongo wako unakuonya kabla ya kupata kiharusi ila wewe hujui unachopaswa kusikiliza.Kila sekunde 40, mtu mmoja anapata ...
06/04/2026

Ubongo wako unakuonya kabla ya kupata kiharusi ila wewe hujui unachopaswa kusikiliza.

Kila sekunde 40, mtu mmoja anapata kiharusina wengi walikuwa na ishara za onyo ambazo walizikosa kabisa.

Hapa kuna ishara 7 ambazo mwili wako unazituma kabla ya kiharusi:
Upande mmoja wa uso unashuka ghafla au unakufa ganzi. Tabasamu linakuwa la upande mmoja tu.

Udhaifu wa mkono mmoja unakuwa dhaifu ghafla hata ukiinua mikono yote miwili mmoja utashuka chini haraka.

Mabadiliko ya maneno, sentensi hazina maana na huwezi kurudia maneno rahisi.

Kushindwa kuona ghafla na kuona ukungu au unaona vitu mara mbili katika jicho moja au yote mawili.

Maumivu ya kichwa makali zaidi na yanakuja ghafla kutoka mahali popote.

Kuchanganyikiwa ghafla na huwezi kuelewa vitu rahisi. Akili inakuwa tupu kabisa.

Kupata kizunguzungu ghafla. Huwezi kutembea moja kwa moja. Uratibu unatoweka.

Kumbuka FAST:
F — Face drooping (Uso unashuka)
A — Arms weak (Mikono inakuwa dhaifu)
S — Speech slurred (Usemi unapotea)
T — Time (Wakati)
Kila dakika kiharusi kinapoendelea seli milioni 1.9 za ubongo hufa kabisa,wakati ubongo unakuwa katika hatari kubwa zaidi k**a una:
shinikizo la damu la juu, ugonjwa wa moyo (atrial fibrillation), kisukari, cholesterol ya juu, historia ya kuvuta sigara, au maisha ya kukaa tu bila mazoezi.
80% ya viharusi vinaweza kuzuilika kwa kubadilisha mtindo wa maisha.

Share na mtu unayempenda kwani habari hii inaweza kuokoa maisha leo.

Kwa maarifa ya afya ya kila siku yanayokuweka wewe na familia yako salama endelea kufuatilia ukurasa huu,na kwa wewe mwenye presha au kisukari, Andika neno "AFYA" kwenye maoni ili upate suluhisho leo.

Heri ya Pasaka 🕊️Pasaka hii ikuletee amani ya moyo, furaha ya kweli, na mwanzo mpya wenye matumaini mapya.K**a vile ushi...
05/04/2026

Heri ya Pasaka 🕊️
Pasaka hii ikuletee amani ya moyo, furaha ya kweli, na mwanzo mpya wenye matumaini mapya.
K**a vile ushindi ulivyopatikana siku hii, na wewe ukapate ushindi katika changamoto zako zote.

Afya njema, upendo mwingi, na baraka zisizoisha ziwe sehemu ya maisha yako na familia yako.
Heri ya Pasaka 🌿

Address

Moshi, Dar Es Salaam
Dodoma
MOSHI

Telephone

+255746334963

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Yako Point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya Yako Point:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram