19/02/2026
Moja ya madhara ya ugonjwa wa kisukari ni kukatwa baadhi ya viungo,je nini kinapekelekea hali hiyo na je ni nini ni suluhisho??
Hii ni swali muhimu sana,sasa nitoe maelezo kwa urahisi lakini kwa kina ili upone hali yako na hofu yako;
Wagonjwa wa kisukari, hasa wale wenye sukari isiyodhibitiwa, wana hatari kubwa ya matatizo ya miguu na vidole. Hali hii hutokea kwa sababu:
Madhara ya neva (neuropathy)ambayo huathiriwa na uwepo wa sukari nyingi mwilini amabyo huharibu mishipa ya fahamu (nerves).
Hii husababisha kupoteza hisia katika miguu au viganja na vidole vya mikono au miguu. Mgonjwa anaweza kushindwa kuhisi maumivu,k**a vile ya kuumwa na majeraha madogo.
Madhara kwa mishipa ya damu (poor circulation).Kisukari kinaweza kuharibu mishipa midogo ya damu, hasa miguu na vidole.Damu haifiki vizuri sehemu hizi, hivyo majeraha hayaponi haraka.
Kuungua au kuvimba kwa vidonda
Maambukizi (infections) yanapokuwa, mwili hawezi kupambana vizuri kwa sababu kinga ya mwili imeathirika.
Hii inaweza kusababisha vidonda vikubwa vinavyoshindwa kuponywa.
Matokeo ya hali hii ni vidonda visivyopona vinaweza kuharibu tishu.
Mara nyingi, ikiwa majeraha ni makubwa au yameambukizwa vibaya, daktari anaweza kupendekeza kukatwa kidogo au kimoja cha kidole, mguu au sehemu fulani ili kuokoa maisha au kuzuia maambukizi kuenea.
Suluhisho na kinga ni udhibiti wa sukari mwilini kufuatilia sukari ili isizidi kwa kujenga kinga mwilini ,lishe bora, kudumisha uzito wa mwili, na kuzuia shinikizo la juu la damu.
Kwa maneno mengine, kukatwa viungo ni suluhisho la muda mfupi ila sio mwisho inapotokea maambukizi makubwa au tishu kuharibika shida iakuwa kubwa zaidi lakini kinga na udhibiti wa sukari inaweza kuzuia hali hiyo kabisa.