Afya Yako Point

Afya Yako Point We Care About Your Health

Sukari yako Inacheka Leo lakini Kesho Itakuangamiza.Unapoamka asubuhi, unaona mwili wako uko sawa.Una nguvu, unaendelea ...
10/01/2026

Sukari yako Inacheka Leo lakini Kesho Itakuangamiza.

Unapoamka asubuhi, unaona mwili wako uko sawa.Una nguvu, unaendelea na maisha. Lakini ndani ya damu yako, kuna jini la kimya kimya linaloitwa Glucose.

Hili likizidi kiwango, huwa ni Muuaji wa taratibu huku liki tabasamu.

📍Kisukari si ugonjwa wa matajiri.

📍Sio kilio cha wazee pekee.

📍Na wala si mpaka unene upite mipaka ndio ukipate.Huu ni ugonjwa wa kila mtu asiyejiajli.Namaanisha hata wewe kijana, Mwenye mitindo mibovu ya maisha Muda wowote kinakulamba.

Hiki ndicho kinatokea mwilini mwako Bila kujua.

↳ Unapenda soda baridi kuliko maji.

↳ Kila asubuhi unakula vitumbua, chapati na chai yenye sukari maradufu.

↳ Hujawahi kupima sukari ya mwili hata mara moja kwa mwaka mzima.

↳ Hufanyi mazoezi, Mwili unashindwa kutumia sukari, inakusanyika.

Mambo hubadilika Ghafla, Ukifika Hospitali, daktari anakwambia.

“Sukari yako iko 400mg/dL Unahitaji insulin haraka sana kuokoa maisha”

Na hapo safari inaanza,Vidonge kila siku, Sindano kila siku.Kidole kupigwa sindano kila asubuhi, Na hatimaye, Upofu, Figo kushindwa, Kiharusi na Upungufu wa nguvu za kiume.

Lakini unaweza kuzuia yote haya, Leo ukiwa ndani Ya Jukwaa hili La afya.

Ni rahisi kuliko unavyodhani;

↳ Kula vyakula vya asili.

↳ Tumia maji kuliko soda.

↳ Fanya mazoezi angalau dakika 30 kwa siku.

↳ Pima sukari yako angalau mara mbili kwa mwaka.

↳ Elimisha familia yako mapema, k**a kuna historia ya Kisukari mnaweza kurithishana.

Usisubiri kuwekewa insulin ndipo uanze kusema "Laiti ningejua".

Afya yako ni mali yako, Na kisukari hakina huruma.Leo ni siku bora ya kuchukua hatua kuliko kesho yenye gharama ya Matibabu na maumivu ya ugonjwa.

10/01/2026

Mwaka 2026 Ishi Kwa Misingi Hii ya Kiafya.

1. Fanya mazoezi ya nguvu angalau mara 3 kwa wiki.

2. Lala walau masaa 7–8 kila usiku bila kukatisha usingizi.

3. Punguza just foods kwa kiwango cha chini kabisa.

4. Acha kukaa muda mrefu bila kusogea simama kila dakika 45.

5. Kunywa maji 1.5–2L kila siku bila kusubiri kiu.

6. Fanya stress detox mara moja kwa siku breathing na meditation therapy.

7. Punguza sukari na vinywaji vyenye caffeine kupita kiasi.

8. Kula chakula chenye protini kwa wingi kwenye kila mlo.

9. Linda afya ya uzazi, epuka punyet*, video za ngon*, pombe, uvutaji sigara.

10. Fanya ukaguzi wa afya angalau mara 2 kwa mwaka.

11. Jifunze kusema hapana ili kulinda afya yako ya akili.

12. Jenga circle yenye energy safi na supportive.📌

Ukweli ambao watu hawapendi kusikia ni huu*Mwili wako haukuharibiwa kwa bahati mbaya uliharibiwa na maamuzi yako ya kila...
08/01/2026

Ukweli ambao watu hawapendi kusikia ni huu

*Mwili wako haukuharibiwa kwa bahati mbaya uliharibiwa na maamuzi yako ya kila siku.*

Hakuna aliyekulazimisha kula ovyo, kukaa bila mazoezi, kutokulala wakati wa usiku, kuishi bila nidhamu ya kisaikolojia.

Hayo yote yalikuwa Maamuzi madogo madogo, yaliyofanywa mara kwa mara, hadi yakawa mtindo mbovu wa maisha.

Magonjwa mengi ya leo si ajali za kimaumbile,ni matokeo ya mwili kuchoka kubeba uzembe wa muda mrefu.

Ndiyo maana watu wengi wanatafuta dawa, si mabadiliko.

Wanataka *kurekebisha matokeo* bila kugusa chanzo.

Lakini mwili wako haujadili, Unalipa kulingana na ulivyoutumia.

Kubadili afya yako si safari ya motisha,
Ni hukumu ya nidhamu,
Ni kukubali kwamba starehe ulizopenda ndizo zilikuwa zikikuharibu taratibu.

Usipobadili mitindo yako ya maisha kwa hiari,
Maumivu yatakubadilisha kwa lazima.

Na hapo, uchaguzi hautakuwa wako tena,

Afya yako ni adhabu au thawabu, kulingana na maamuzi unayofanya leo.

Watu Wengi Hujiuliza Kwanini Ganzi Hutokea Kwenye Vidole Vya Mikono Na Miguu Na Kupelekea Mwili Kush*tuka Ghafra, Hata K...
07/01/2026

Watu Wengi Hujiuliza Kwanini Ganzi Hutokea Kwenye Vidole Vya Mikono Na Miguu Na Kupelekea Mwili Kush*tuka Ghafra, Hata Kukosa Uwezo Wa Kutembea Muda Mwingine

CHANZO KIKUU CHA GANZI KWA MGONJWA WA KISUKARI

1.Sukari kuwa juu kwa muda mrefu (Chronic hyperglycemia)Hii huharibu mishipa ya fahamu taratibu na kusababisha ganzi.

2.Uharibifu wa mishipa ya fahamu (Diabetic peripheral neuropathy)na hivyo hupoteza uwezo wa kusafirisha hisia sahihi.

3.Kuziba kwa mishipa midogo ya damu (Microvascular damage) na hii hupelekea kukosa damu na oksijeni ya kutosha.

4.Msongo wa Oxidative stress.Sukari huzalisha sumu (free radicals) zinazoangamiza seli za fahamu.

5.Upungufu wa Vitamini B (B1, B6, B12) ambazo ni Vitamini muhimu kwa afya ya fahamu hivyo upungufu wake huleta ganzi.

6.Udhibiti duni wa kisukari kwa muda mrefu.Kadri sukari inavyodhibitiwa vibaya, ndivyo uharibifu wa fahamu unavyoongezeka.

7.Kuvimba kwa mishipa ya fahamu(Inflammation)
Huongeza maumivu, kuchomachoma na ganzi kwenye vidole.

NJIA 5 ZA KUPUNGUZA AU KUONDOA GANZI
1.Kudhibiti sukari kwenye kiwango sahihi kila siku.Hii ndiyo tiba ya msingi bila hili ganzi itaendelea.

2.Kutumia virutubisho vya kuimarisha mishipa ya fahamu k**a Vitamini B-complex, Alpha Lipoic Acid, Magnesium.

3.Kufanya mazoezi mepesi ya miguu na mikono kila siku huongeza mzunguko wa damu kwenye mishipa ya fahamu.

4.Kula lishe inayolinda mishipa ya fahamu k**a mboga za majani, samaki, karanga, vyakula vyenye antioxidants.

5.Kuanza hatua mapema kabla fahamu hazijaharibika kabisa.

Ganzi ya mwanzo inaweza kurekebishika, ya muda mrefu huwa inachukua muda mrefu sana.

Ganzi kwa mgonjwa wa kisukari ni onyo la mwili, si dalili ya kupuuzwa.

Kudhibiti sukari mapema ni sawasawa na kulinda fahamu zako.

Una kisukari na bado unahisi:– Uchovu wa mara kwa mara?– Kiu kali?– Kukojoa mara kwa mara?Watu wengi wanajua “namba ya s...
05/01/2026

Una kisukari na bado unahisi:

– Uchovu wa mara kwa mara?
– Kiu kali?
– Kukojoa mara kwa mara?

Watu wengi wanajua “namba ya sukari” tu,
lakini hawajui hali ya mwili wao inavyoendelea.

Kudhibiti kisukari kunahitaji:

✔ Vipimo sahihi
✔ Ushauri wa karibu
✔ Ufuatiliaji wa mara kwa mara

Bila hivyo, madhara k**a:
– Figo
– Macho
– Presha
yanaweza kujitokeza kimya kimya.

📍 Afya Yako Point – Dodoma
Tunatoa ushauri na vipimo kwa wanaoishi na kisukari.

Pata ushauri & vipimo WhatsApp 0746334963

Dalili kuu za glomerulonephritis ni kuwa na damu katika mkojo (hali inayoufanya mkojo kuwa na rangi k**a nyeusi, kutu au...
05/01/2026

Dalili kuu za glomerulonephritis ni kuwa na damu katika mkojo (hali inayoufanya mkojo kuwa na rangi k**a nyeusi, kutu au samawati; mkojo kuwa k**a wenye povu jingi (kwa sababu ya kuwa na protini nyingi kuliko kawaida) na kuvimba uso, macho, miguu au tumbo (hali inayojulikana k**a edema)

Dalili nyingine ni pamoja na
•Maumivu ya tumbo
•Kutapika damu
•Kuharisha au kupata choo kikubwa chenye kuchanganyika na damu
•Kukohoa kupita kiasi pamoja na kupumua kwa shida
•Homa
•Maumivu ya misuli na viungo, uchovu, maumivu ya mwili mzima pamoja na kukosa hamu ya kula
•Kutokwa na damu puani.

Baada ya muda, figo hushindwa kufanya kazi na mgonjwa huanza kuwa na dalili za mtu mwenye ugonjwa sugu wa figo yaani CHRONIC KIDNEY DISEASE (CKD)

05/01/2026

Channel • 9 followers • Kujifunza Na Kuelewa Mambo Mbalimbali Yahusuyo Afya Yako Na Njia Sahihi Za Kujilinda Dhidi Ya Magonjwa Mbalimbali Yasiyoambukiza Yatokanayo Na Tabia Pamoja Na Mtindo Wa Maisha

Takribani robo ya watu wanaopatwa na tatizo sugu la glomerulonephritis huwa hawana historia ya kuwa na ugonjwa wowote wa...
05/01/2026

Takribani robo ya watu wanaopatwa na tatizo sugu la glomerulonephritis huwa hawana historia ya kuwa na ugonjwa wowote wa Figo hapo kabla.

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupata glomerulonephritis.

Mambo hayo ni pamoja na:

•Matatizo katika mfumo wake wa damu au lymph

•Kuwahi kutumia vimiminika vilivyotengenezwa kwa kemikali za hydrocarbon

•Wenye historia ya saratani

•Maambukizi ya bacteria aina ya streptococcus, virusi, majipu au maambukizi katika moyo

Mambo mengine yanayoweza kuongeza hatari ya kupatwa na glomerulonephritis ni pamoja na:

•Magonjwa ya mishipa ya damu k**a vile vasculitis au polyarteritis

•Matumizi yaliyopitiliza ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non steroidal anti-inflammatory drugs k**a vile aspirin

•Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili k**a vile Anti-glomerular basement membrane antibody disease na IgA nephropathy

•Makovu katika chujio (Focal segmental glomerulosclerosis) au hali ya chujio kuwa na kuta nene kuliko kawaida (Membranoproliferative GN)

•Magonjwa yanayoathiri viungo mbalimbali vya mwili k**a vile Henoch-Schonlein purpura, Goodpasture’s syndrome au Lupus nephritis

•Ugonjwa wa kimetaboliki wa Amyloidosis

Kuharibika Kwa Chujio za Figo (Glomerulonephritis)  Kuharibika kwa chujio au Glomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa Fi...
05/01/2026

Kuharibika Kwa Chujio za Figo (Glomerulonephritis)

Kuharibika kwa chujio au Glomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa Figo unaoathiri sehemu maalum ya Figo (chujio) inayohusika na uchujaji wa maji pamoja na uchafu kutoka katika damu.Sehemu hii huitwa glomelurus au chujio.

Mara nyingi chanzo halisi cha kuharibika kwa chujio za Figo (glomerulonephritis) kunaweza kusababishwa na kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili.

Uharibifu katika chujio husababisha Damu pamoja na Protini kuingia katika mkojo.
Tatizo hili hukua kwa haraka na Figo linaweza kupoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kwa kasi ndani ya muda mfupi au ndani ya wiki chache mpaka miezi kadhaa.
Aina hii ya kuharibika kwa chujio za Figo kwa haraka hujulikana kitalaamu k**a rapidly progressive glomerulonephritis.

JE, UNAJUA?Kisukari kinaweza kuharibu Macho, Figo, na Mishipa ya Fahamu kimyakimya bila dalili za mapema 😳Sukari inapoku...
02/01/2026

JE, UNAJUA?

Kisukari kinaweza kuharibu Macho, Figo, na Mishipa ya Fahamu kimyakimya bila dalili za mapema 😳

Sukari inapokua juu kwa muda mrefu husababisha uharibifu wa mishipa midogo ya damu kitaalamu huitwa (Microvascular damage), jambo linaloweza kupelekea afya yako kuishia kwenye

↳ Upofu (diabetic retinopathy)

↳ Kufeli kwa Figo (diabetic nephropathy)

↳ Ganzi na maumivu ya neva (diabetic neuropathy)

Changamoto kubwa ni kwamba madhara haya hujitokeza taratibu, mara nyingi bila ishara za awali, hadi pale uharibifu unapokuwa mkubwa.

Mwaka 2026, chukua tahadhari ya afya yako. Pima kiwango cha Sukari mara kwa mara, fuata lishe yenye uwiano sahihi.

Fanya mazoezi ya mwili kwa uendelevu,fanya Diabetic Checkup angalau mara mbili kwa mwaka, hata k**a hujisikii vibaya.

Kinga ni bora kuliko tiba, usisubiri dalili kujitokeza.
Linda Macho yako, Figo zako na Afya yako kwa ujumla kwa kuchukua hatua mapema.

Swali la Leo
Ni lini mara ya mwisho ulipima kiwango cha sukari kwenye damu yako?

Heri ya Mwaka Mpya 2026!Uwe mwaka wa Neema mpya, Fursa mpya na Ushindi mpya.Uwe mwaka wa Afya njema, Amani ya moyo na Ba...
01/01/2026

Heri ya Mwaka Mpya 2026!

Uwe mwaka wa Neema mpya, Fursa mpya na Ushindi mpya.

Uwe mwaka wa Afya njema, Amani ya moyo na Baraka zisizoisha.

Kila kilichokuumiza 2025 kibaki nyuma,na kila ndoto uliyoibeba iingie 2026 ikiwa na mwanga wa matumaini.

Mungu akuongoze, akulinde na akuinue zaidi.

Happy New Year 2026

Address

Moshi, Dar Es Salaam
Dodoma
MOSHI

Telephone

+255746334963

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Yako Point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya Yako Point:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram