Afya Yako Point

Afya Yako Point We Care About Your Health

Moja ya madhara ya ugonjwa wa kisukari ni kukatwa baadhi ya viungo,je nini kinapekelekea hali hiyo na je ni nini ni sulu...
19/02/2026

Moja ya madhara ya ugonjwa wa kisukari ni kukatwa baadhi ya viungo,je nini kinapekelekea hali hiyo na je ni nini ni suluhisho??

Hii ni swali muhimu sana,sasa nitoe maelezo kwa urahisi lakini kwa kina ili upone hali yako na hofu yako;

Wagonjwa wa kisukari, hasa wale wenye sukari isiyodhibitiwa, wana hatari kubwa ya matatizo ya miguu na vidole. Hali hii hutokea kwa sababu:

Madhara ya neva (neuropathy)ambayo huathiriwa na uwepo wa sukari nyingi mwilini amabyo huharibu mishipa ya fahamu (nerves).

Hii husababisha kupoteza hisia katika miguu au viganja na vidole vya mikono au miguu. Mgonjwa anaweza kushindwa kuhisi maumivu,k**a vile ya kuumwa na majeraha madogo.

Madhara kwa mishipa ya damu (poor circulation).Kisukari kinaweza kuharibu mishipa midogo ya damu, hasa miguu na vidole.Damu haifiki vizuri sehemu hizi, hivyo majeraha hayaponi haraka.

Kuungua au kuvimba kwa vidonda
Maambukizi (infections) yanapokuwa, mwili hawezi kupambana vizuri kwa sababu kinga ya mwili imeathirika.
Hii inaweza kusababisha vidonda vikubwa vinavyoshindwa kuponywa.

Matokeo ya hali hii ni vidonda visivyopona vinaweza kuharibu tishu.
Mara nyingi, ikiwa majeraha ni makubwa au yameambukizwa vibaya, daktari anaweza kupendekeza kukatwa kidogo au kimoja cha kidole, mguu au sehemu fulani ili kuokoa maisha au kuzuia maambukizi kuenea.

Suluhisho na kinga ni udhibiti wa sukari mwilini kufuatilia sukari ili isizidi kwa kujenga kinga mwilini ,lishe bora, kudumisha uzito wa mwili, na kuzuia shinikizo la juu la damu.

Kwa maneno mengine, kukatwa viungo ni suluhisho la muda mfupi ila sio mwisho inapotokea maambukizi makubwa au tishu kuharibika shida iakuwa kubwa zaidi lakini kinga na udhibiti wa sukari inaweza kuzuia hali hiyo kabisa.

Leo ninazungumza na wewe ambaye umekuwa ukipitia changamoto za Figo, umehangaika mara nyingi bila kupata majibu sahihi, ...
11/02/2026

Leo ninazungumza na wewe ambaye umekuwa ukipitia changamoto za Figo, umehangaika mara nyingi bila kupata majibu sahihi, na labda hata hujui k**a dalili unazozipata zinatoka kwenye Figo zako.

Wewe ambaye kila siku unakojoa mara nyingi sana au mara chache kupita kiasi, na hata ukikojoa unahisi maumivu makali sehemu ya chini ya tumbo au mgongoni.

Unayehisi miguu kuvimba, uso kuvimba asubuhi, mwili kuchoka bila sababu, uchovu wa kupindukia, au shinikizo la damu kupanda mara kwa mara bila kuelewa chanzo.

Au pengine umekuwa ukipata U.T.I zinazojirudia mara nyingi kiasi kwamba zimekutesa kwa muda mrefu na hujui ni kwa nini hata ukimeza dawa, tatizo linakuja tena na tena.

Ninazungumza pia na wewe ambaye una harufu kali kwenye mkojo, mkojo wa rangi ya njano iliyokolea sana, au hata rangi ya kahawia.

Hizi zote ni ishara kwamba Figo zako zinateseka kimya kimya.

K**a umekuwa ukiamka asubuhi kichwa kinauma, miguu imejaa maji, au mwili mzima unahisi mzito basi tambua kuwa mwili wako unakuomba msaada.

Sasa suluhisho sahihi juu ya figo zako limepatikana lakini kabla ya matibabu, ni muhimu zaidi kuelewa chanzo ili tatizo lisiendelee kukurudia tena.

CHANZO CHA MATATIZO YA FIGO

Kutokunywa maji ya kutosha
Hii ndiyo sababu kubwa. Ukiwa na upungufu wa maji, figo zinahangaika kutoa taka mwilini. Ndiyo maana unapata U.T.I, maumivu ya mgongo na uchovu.

Mafuta mengi, vyakula vya chumvi na chemicals nyingi mwilini ni moja ya vitu ambavyo hupelekea
Figo kujaa taka,hivyo zinashindwa kupitisha damu vizuri. Hapa ndipo pressure inapanda na mwili unaanza kuvimba.

Matumizi ya antibiotics bila ushauri
Dawa zisipotumiwa vizuri zinaharibu figo taratibu bila wewe kuona mapema.

Kisukari na presha
Haya ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kuharibu figo kimya kimya kwa miaka mingi.

U.T.I sugu au inayojirudia bila kutibiwa ipasavyo huenda juu mpaka kwenye figo na kuanza kuharibu mfumo wa kuchuja damu.

MADHARA YA KUPUUZA DALILI ZA FIGO
– Mwili kuvimba siku hadi siku
– Maumivu makali ya mgongo na kiuno
– Kuvimba uso asubuhi
– Shinikizo la damu kupanda mara kwa mara
– Kukosa nguvu za mwili, kutozingatia kazini
– U.T.I sugu ambayo inaumiza kila mara
– Na hatari kubwa zaidi: kushindwa kwa figo
Ukishafikia hatua ya figo kushindwa kufanya kazi, gharama zake ni kubwa na huzuni yake ni kubwa zaidi na yote haya yanaweza kuzuilika leo, mapema.

CHUKUA HATUA SASA
Kwa wale wa Dodoma Tunapatikana:
📍 Ipagala – Shule ya Biblia Emmausi (maarufu k**a kanisa la Biblia Emmausi)
Na kwa gharama ndogo ya TSh 5,000 tu, unamuona daktari na kupata mwelekeo sahihi wa afya yako leo.

Usisubiri mpaka figo zikose kabisa uwezo.
Mwili wako umekuonya vya kutosha.
Sasa ni zamu yako kuusikiliza.
Kwa mawasiliano na msaada wa haraka save namba hizi:
📞 0746 334 963
Kwa wale wa mikoani tunafanya delivery mkoa wowote.

Ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini haswa?Uwepo wa Glucose nyingi inayozunguka katika mfumo wako wa damu husababish...
06/02/2026

Ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini haswa?

Uwepo wa Glucose nyingi inayozunguka katika mfumo wako wa damu husababisha ugonjwa wa kisukari, bila kujali aina.

Ingawa, sababu kwa nini viwango vya sukari kwenye damu yako ni vikubwa hutofautiana kulingana na aina ya ugonjwa wa kisukari.

Hizi hapa ni Sababu mbali mbali zinazochangia hali hiyo:

1- Tatizo la Insulin resistance:

Aina ya 2 ya kisukari hutokana hasa na ukinzani wa insulini. Ukinzani huu wa insulini hutokea wakati seli kwenye misuli, mafuta na ini hazitoi matokeo inavyopaswa dhidi ya insulini.

Sababu na baadhi ya hali huchangia viwango tofauti vya ukinzani wa insulini.

Sababu hizo ni pamoja na;

-Uzito mkubwa au kunenepa kupita kiasi,
Kutokufanya Mazoezi ya mwili.

-Mabadiliko ya Vichocheo au homoni mwilini.

-Swala la kimaumbile au Genetics factor
Matumizi ya baadhi ya dawa fulani.n.k

2-Tatizo kwenye Mfumo wa kinga
mwili(Autoimmune disease)

Kisukari aina ya kwanza(Type 1 diabetes) pamoja na Latent autoimmune diabetes in adults (LADA) ambapo nilitaja aina hii hapo awali, hutokea wakati mfumo wako wa kinga unaposhambulia seli zinazozalisha insulini kwenye kongosho lako.

3- Tatizo la Hormonal imbalances:

-Wakati wa Ujauzito, placenta huweza kutoa homoni zinazosababisha ukinzani wa insulini. Unaweza kupata kisukari wakati wa ujauzito ikiwa kongosho yako haiwezi kutoa insulini ya kutosha kushinda ukinzani wa insulini uliojitokeza.

Hali nyingine zinazohusiana na homoni k**a vile tatizo la akromegali pia zinaweza kusababisha kisukari cha Aina ya 2.

4- Uharibifu wa kongosho(Pancreatic damage):

Uharibifu wa kongosho lako kutokana na hali k**a vile ajali, upasuaji au jeraha unaweza kuathiri uwezo wake wa kutengeneza insulini, na kusababisha ugonjwa wa kisukari hasa Aina ya 3 ya kisukari(Type 3 diabetes).

5- Matatizo ya kimaumbile au kigenetic(Genetic mutations):

Mabadiliko fulani ya kijenetic yanaweza kusababisha Ugonjwa wa kisukari hasa kuanzia kwa watoto wachanga,aina hii ya kisukari hufahamika k**a neonatal diabetes.

6- Utumiaji wa muda mrefu wa baadhi ya dawa

Aina za Ugonjwa wa KisukariKuna aina kadhaa za Ugonjwa wa kisukari.1.Kisukari aina ya kwanza(Type 1 Diabetes)2.Kisukari ...
05/02/2026

Aina za Ugonjwa wa Kisukari

Kuna aina kadhaa za Ugonjwa wa kisukari.

1.Kisukari aina ya kwanza(Type 1 Diabetes)

2.Kisukari aina ya Pili(Type 2 diabetes)
Kisukari cha

2.Mimba(Gestational diabetes)

Pamoja na aina nyingine kadhaa ambazo watu wengi hawazizungumzii kabisa ila zipo,mfano kuna
Type 3 Diabetes

Latent Autoimmune Diabetes In Adults (LADA)

Maturity-onset Diabetes

Neonatal diabetes.

Sasa tuangalie aina hizi za kisukari, tukianza na ;

1. Kisukari aina ya Kwanza(Type 1 diabetes)
Aina hii ya Ugonjwa huhusisha kongosho au Pancrease kutokuzalisha na kutoa Insulin kabisa.

Hapa kongosho haitengenezi Insulini kabisa, kwa sababu mfumo wa kinga ya mwili hushambulia seli za kongosho zinazotengeneza insulini.

Aina hii ya 1 ya kisukari kwa Kawaida hugunduliwa kwa watoto na vijana, lakini inaweza kutokea katika umri wowote pia.

2. Kisukari Aina ya Pili(Type 2 diabetes)
Kwa aina hii, mwili wako hautengenezi insulini ya kutosha au seli za mwili wako hazitumii vizuri ipasavyo insulini iliyopo.

Hii ndiyo aina ya Ugonjwa wa kisukari ambao huwapata Watu Wengi Zaidi na Inaathiri zaidi watu wazima, lakini kwa sasa hata vijana na watoto wanakuwa nayo pia kutokana na ulaji na mtindo wa maisha tunayoishi kwa sasa.

Katika aina ya 2 ya kisukari, kongosho hutengeneza insulini kidogo kuliko ilivyokuwa hapo awali, na mwili wako unatengeneza ukinzani dhidi ya insulini ndogo iliyopo yaani Insulin Resistance.

3. Kisukari cha Mimba(Gestational diabetes):
Aina hii ya kisukari inatokea wakati wa ujauzito, na kawaida hupotea baada ya ujauzito au baada ya kujifungua.

Ingawa baadhi ya tafiti zinaonyesha ikiwa una kisukari wakati wa ujauzito, uko katika hatari kubwa ya kupata kisukari cha Aina ya 2 baadaye maishani.

Dalili Za Ugonjwa wa kisukari

Ukali wa dalili unaweza kutofautiana kulingana na aina ya ugonjwa wa kisukari ulionao.

Dalili hizi kawaida huwa kali zaidi katika aina ya 1 ya kisukari kuliko kisukari cha Aina ya 2.

Dalili za kisukari kwa Ujumla ni zipi?

Dalili za ugonjwa wa kisukari ni pamoja na:

1.Kuongezeka kwa kiu na kinywa kuwa kikavu zaidi.
2.Kukojoa mara kwa mara.
3.Kupata sana Uchovu wa mwili
4.Macho kutokuona vizuri au kuona marue rue
5.Kupunguza Uzito kwa kasi bila Sababu inayoeleweka, au
Mtu kukonda
6.Kupata Ganzi au hali ya kuchoma choma katika mikono au miguu yako.
7.Vidonda kupona polepole au kuchelewa zaidi kupona
8.Kuwa kwenye hatari ya kupata Maambukizi ya mara kwa mara ya ngozi,
9.Kupoteza hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa wanaume na wanawake na pia kupata maambukizi ya Fangasi ukeni n.k

Katika somo lijalo tutaona ugonjwa wa Kisukari husababishwa na nini?

Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa ambao unahusisha kuwepo kwa kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kuliko kawaida au kuwa...
04/02/2026

Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa ambao unahusisha kuwepo kwa kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kuliko kawaida au kuwa na kiwango kidogo sana cha sukari kwenye damu kuliko kawaida.

Hivo hapa tunapata aina mbili za kisukari;

(i) Kisukari cha kupanda au kwa kitaalam tunaita Hyperglycemia

(ii) Na kisukari cha kushuka au kwa kitaalam tunaita Hypoglycemia

Ila tutazungumzia zaidi kuhusu kisukari cha kupanda,hivo kila tutakapozungumzia Ugonjwa wa Kisukari ujue tunazungumzia Sukari ya kupanda.

Ugonjwa huu hutokea wakati sukari yako kwenye damu (glucose) iko juu sana.

Na mara nyingi hutokea wakati;

1.Kongosho linaposhindwa kuzalisha Insulini ya kutosha kutokana na vyakula vya kila siku.

2.Insulin Resistance, ukinzani huu unatokana na uwepo wa Cholesterol ambayo hugandisha mafuta kwenye seli za mwili na mishipa ya damu,ambapo seli ndio huzalishwa na kuwa na NAD+.

3.NAD+ kushindwa kufanya kazi vizuri.NAD+ hii ndiyo inayofanya kazi ya kuvunjavunja sukari iliyo ndani ya mwili kuwa nishati ya mwili,na hii hutokea sana kwa kadri umri wa mtu unavyozidi kuwa mkubwa kwani seli zinazidi kuchoka na kupungua.

Kwa sasa ugonjwa wa kisukari huathiri watu wa umri wowote kutokana na vyakula na mtindo wa maisha tunayoishi kwa sasa.

Ugonjwa wa kisukari kwa sasa na kwa watu wengi umekuwa ni sugu,ila muhimu ni kujua na aina mbili kati ya tatu za ugonjwa huu zinaweza kudhibitiwa na kupona kwa dawa pamoja na mabadiliko ya mtindo wa maisha.

Kwa Asilimia kubwa Glucose (sukari) hasa hutoka kwenye Wanga au Carbohydrates katika vyakula unavyokula na vinywaji unavyokunywa,na hii ndio chanzo cha nishati kwa mwili wako.

Damu yako hubeba Glucose hadi kwenye seli zote za mwili wako ili kutumia kwa ajili ya nishati.

Glucose inapokuwa kwenye mfumo wako wa damu, inahitaji usaidizi "au ufunguo" ambao ni INSULIN ili kufikia lengo la mwisho.

Sasa Ikiwa kongosho yako haitengenezi Insulini ya kutosha au mwili wako hauitumii ipasavyo, glucose hujilimbikiza kwenye damu yako, na kusababisha sukari kuwa juu kwenye damu (hyperglycemia).

Baada ya Muda wa kuuwa na kiwango cha juu cha Sukari kwenye damu mfululizo ndio kusababisha shida za kiafya, k**a vile;
-Ugonjwa wa moyo
-Shinikizo la juu la damu,
-kiharusi,
-Shambulio la moyo,
-Uharibifu wa neva,
-Ulemavu unaotokana na vidonda visivypona,
-Shida ya uzazi kwa wote wanaume na wanawake,
-Kufeli kwa Figo pamoja na
-Shida za macho.

“Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…” Hosea 4:6Na leo hii bado tunajiumiza kwa sababu hatujui mwili wetu unasem...
03/02/2026

“Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…” Hosea 4:6

Na leo hii bado tunajiumiza kwa sababu hatujui mwili wetu unasema nini.
Tunapuuzia dalili ndogo k**a Uchovu, Maumivu ya mara kwa mara, Kisukari, Presha ,Figo mpaka zinageuka kuwa matatizo makubwa.

Sio kwamba hatuna uwezo wa kujilinda ila kukosa maarifa sahihi ya afya.

Afya inapopangwa na kulindwa mapema, magonjwa yanapungua.
Lakini ukikosa maarifa, mwili ndio utakufundisha kwa maumivu.

Chagua kujua ili kuzuia kabla mambo hayajaharibika.

Ungependa kuelewa zaidi kuhusu mwili wako, dalili zako, au namna ya kujitibu mapema?
Andika “ELIMU” kwenye comment au nitumie DM.

Unazijua Faida za kunywa pombe???Leo nitazungumzia faida za pombe....Hebu tuanze na faida zake kidogo:✅ Inakufanya ujisi...
28/01/2026

Unazijua Faida za kunywa pombe???

Leo nitazungumzia faida za pombe....
Hebu tuanze na faida zake kidogo:
✅ Inakufanya ujisikie relaxed baada ya siku ndefu
✅ Huongeza ujasiri kidogo kuzungumza mbele ya watu
✅ Hufanya mazungumzo ya kirafiki yawe rahisi kwa muda mfupi
Lakini ukweli ni huu…

Faida hizi ni za muda mfupi, madhara yake ni ya muda mrefu:
Stress, afya inashuka, uhusiano unashuka chini au kuvunjika, nguvu zako kuishia polepole.

Furaha ya muda mfupi haipaswi kuharibu kesho yako.
Mtu mzima sio anayekunywa au asiye kunywa…mtu mzima ni anayejua lini aache na kujua thamani ya kila chaguo.

Je, umewahi kujisikia unafurahia pombe kwa muda kidogo kisha kesho ukaona madhara yake?
Share experience yako hapa chini ⬇️

ULAJI MBAYA SI TATIZO LA TUMBO TU… NI TATIZO LA MAISHA YAKO70% ya kinga ya mwili wako iko tumboni unapokula hovyohovyo l...
27/01/2026

ULAJI MBAYA SI TATIZO LA TUMBO TU… NI TATIZO LA MAISHA YAKO

70% ya kinga ya mwili wako iko tumboni unapokula hovyohovyo leo, mwili wako haufurahi ila unahatarisha afya yako ya kesho.Mambo k**a;
🔴 Uchovu wa kila siku
🔴 Unene au kukonda kupita kiasi
🔴 Kupoteza hamu ya tendo
🔴 Maumivu ya mgongo, viungo na kichwa
🔴 Hasira za mara kwa mara na mawazo mengi
🔴 Kushuka kwa kinga ya mwili
🔴 Magonjwa ya presha, kisukari na matatizo ya tumbo

Ni dalili za kukuonesha afya yako iko hatarini,ila cha kusikitisha zaidi dalili zote hizi zinaanza kimya kimya… halafu siku moja zinakuja kwa pamoja.

Chakula unachokula leo ndicho kitakachoamua hatua ya maisha yako kesho.

Usisubiri daktari akuambie kile mwili wako unakuomba sasa badilisha ulaji wako mapema.Chagua afya kabla haijakulazimisha.

K**a unajali afya yako na ya familia yako,
follow ukurasa huu ,niandikie “AFYA” inbox nikupe mwongozo rahisi wa kuanza leo

Kosa Kubwa Unalofanya Kila Asubuhi Ni kunywa chai na chapati,STOP.Unadhani chapati ni kifungua kinywa bora? Ipo hivi.Kil...
21/01/2026

Kosa Kubwa Unalofanya Kila Asubuhi Ni kunywa chai na chapati,STOP.

Unadhani chapati ni kifungua kinywa bora? Ipo hivi.

Kila sahani ya chapati unayoanza nayo asubuhi, ni hatua moja kuelekea magonjwa yasiyoambukizwa k**a Kisukari, shinikizo la damu, na unene kupita kiasi(Obesity)

Mwili wako hauhitaji mafuta na wanga nyingi asubuhi, unahitaji mwanga safi kidogo na yenye afya.

Anza siku kwa mazoezi mepesi, Kisha chakula chepesi chenye protini na nyuzinyuzi.

Punguza wanga iliopitiliza.
Fanya mazoezi kila asubuhi.
Pima afya yako mara kwa mara.

Magonjwa yasiyoambukizwa hayachagui umri tena yamehamia kwa vijana, kwa sababu ya tabia na mitindo mibovu ya maisha.

Badilisha kifungua kinywa, badilisha maisha, Siku yako njema inaanza kwenye kikombe cha maji ya vuguvugu, sio kwenye chapati yenye mafuta.

Jifunze na chukua hatu kuboresha afya yako.

Mambo 5 ya Kuzingatia kwa MwenyeChangamoto ya Figo1.Kunywa Maji kwa Kiasi SahihiUsinywe maji mengi kupita kiasi wala mac...
20/01/2026

Mambo 5 ya Kuzingatia kwa Mwenye
Changamoto ya Figo

1.Kunywa Maji kwa Kiasi Sahihi
Usinywe maji mengi kupita kiasi wala machache sana.
Maji mengi sana yanaweza kulemea figo, machache yanaweza kuifanya ichoke.
Fuata ushauri wa daktari au mshauri wa afya kulingana na hali yako.

2.Epuka Chumvi Nyingi.

Chumvi nyingi huongeza shinikizo la damu na kuharibu figo zaidi.
Punguza vyakula vya kusindika k**a:
– Chips
– Soseji
– Tambi za pakiti
– Vyakula vya makopo

3.Punguza Protini Nzito Kupita Kiasi
Nyama nyingi, mayai mengi na maziwa mengi vinaweza kuifanya figo ifanye kazi kupita uwezo.
Kula kwa kiasi, sio kuacha kabisa bila ushauri wa mtaalamu.

4.Epuka Dawa Bila Ushauri
Usitumie dawa ovyo, hasa;
-Dawa za maumivu (painkillers)
– Dawa za kienyeji bila uhakika
Dawa nyingi huharibu figo taratibu bila mtu kujua.

5.Fanya Vipimo na Ufuatiliaji wa Mara kwa Mara
Usisubiri uanze kuumwa sana.
Pima:
– Mkojo
– Damu
– Shinikizo la damu
Hii inasaidia kugundua tatizo mapema na kulidhibiti.

Figo ni “chujio” la mwili wako. Ukiliharibu, mwili mzima unaathirika.
Jilinde leo, usisubiri kesho.

Afya ya figo ni uhai wako.Anza kujilinda leo.

Follow ukurasa huu kwa elimu zaidi za afya

Makosa wanayoyafanya watu wenye changamoto ya kisukari 👇1. Kula bila ratiba, leo unakula sana, kesho huli2. Kula wanga m...
18/01/2026

Makosa wanayoyafanya watu wenye changamoto ya kisukari 👇

1. Kula bila ratiba, leo unakula sana, kesho huli
2. Kula wanga mwingi bila kupima kiasi (ugali, wali, viazi kwa kupitiliza)

3. Kunywa vinywaji vyenye sukari kwa kisingizio cha “ni kidogo tu”

4. Kukaa bila kusogea muda mrefu

5. Kutojali usingizi na msongo wa mawazo

6. Kuacha kufuatilia kiwango cha sukari mara kwa mara

7. Kusikiliza kila ushauri wa watu bila kuuliza mtaalamu

Kisukari sio mwisho wa maisha ni somo la kujijali zaidi.

Ukijua kula kwa mpangilio, kusogea, na kujitunza, unaishi vizuri.

Ukifollow page hii:
– Utajifunza kula kwa busara
– Namna ya kuepuka makosa haya na namna utapona kisukari bila masharti mengi.

👇 FOLLOW sasa au andika “KISUKARI ” kwenye comment tuanze safari ya afya pamoja.

Hapo ndipo Suppliments zinapoleta utofauti,haibadilishi GMO lakini:👉 Inasaidia kusafisha mwili👉 Inasaidia kurudisha viru...
15/01/2026

Hapo ndipo Suppliments zinapoleta utofauti,haibadilishi GMO lakini:
👉 Inasaidia kusafisha mwili
👉 Inasaidia kurudisha virutubisho
👉 Inasaidia kupunguza mzigo wa sumu

Zamani chakula kilitosha kujenga mwili.Leo, chakula kimebadilika lakini miili yetu haijabadilika.Ndiyo maana hatuwezi tena kutegemea chakula pekee.Lazima tusafishe mwili, tuulinde kwa kinga,na tuujenge kwa supplements.

Address

Moshi, Dar Es Salaam
Dodoma
MOSHI

Telephone

+255746334963

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Yako Point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya Yako Point:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram