16/04/2026
FIGO YAKO NI UHAI WAKO, USIPUUZE DALILI!
Video hii fupi inaonyesha ukweli mchungu wa jinsi Saratani ya Figo inavyoanza k**a uvimbe mdogo (Kidney Tumor),na usipoidhibiti mapema, inakua na kuanza kusambaza sumu na seli za saratani kwenye viungo vingine k**a Ini na Mapafu,na inapofika hatua hii ambayo inakuwa vigumu zaidi kutibu.
Swali ni je, unajuaje k**a figo yako ina shida?
Watu wengi hawajui dalili, lakini angalia hizi:
1️⃣ Mkojo wenye damu (hata k**a ni mara moja).
2️⃣ Maumivu ya upande mmoja wa kiuno au mgongo wa chini yasiyoisha.
3️⃣ Uvimbe unaoonekana au kuhisi maumivu pembeni ya tumbo.
4️⃣ Kupoteza hamu ya kula na uzito kupungua bila sababu.
5️⃣ Uchovu uliokithiri kila wakati.
Nini cha kufanya?
Fanya vipimo vya figo angalau mara moja kwa mwaka.Saidia figo zako kufanya kazi vizuri kwa kunywa maji ya kutosha kuende na na mwili wako.
Punguza Chumvi na Sukari maana hivi ni maadui wakubwa wa figo.
Acha Sigara maana Uvutaji wa sigara unaongeza hatari ya kupata saratani hii.
Usisubiri mpaka uone maumivu makali. Shiriki video hii na ndugu au rafiki, unaweza kuokoa maisha ya mtu leo!
Na kwa wewe ambaye tayari una changamoto yoyote figo tuma neno AFYA leo.
JaliAfyaYako AfyaCheck KingaNiBora