10/01/2026
Sukari yako Inacheka Leo lakini Kesho Itakuangamiza.
Unapoamka asubuhi, unaona mwili wako uko sawa.Una nguvu, unaendelea na maisha. Lakini ndani ya damu yako, kuna jini la kimya kimya linaloitwa Glucose.
Hili likizidi kiwango, huwa ni Muuaji wa taratibu huku liki tabasamu.
ðKisukari si ugonjwa wa matajiri.
ðSio kilio cha wazee pekee.
ðNa wala si mpaka unene upite mipaka ndio ukipate.Huu ni ugonjwa wa kila mtu asiyejiajli.Namaanisha hata wewe kijana, Mwenye mitindo mibovu ya maisha Muda wowote kinakulamba.
Hiki ndicho kinatokea mwilini mwako Bila kujua.
â³ Unapenda soda baridi kuliko maji.
â³ Kila asubuhi unakula vitumbua, chapati na chai yenye sukari maradufu.
â³ Hujawahi kupima sukari ya mwili hata mara moja kwa mwaka mzima.
â³ Hufanyi mazoezi, Mwili unashindwa kutumia sukari, inakusanyika.
Mambo hubadilika Ghafla, Ukifika Hospitali, daktari anakwambia.
âSukari yako iko 400mg/dL Unahitaji insulin haraka sana kuokoa maishaâ
Na hapo safari inaanza,Vidonge kila siku, Sindano kila siku.Kidole kupigwa sindano kila asubuhi, Na hatimaye, Upofu, Figo kushindwa, Kiharusi na Upungufu wa nguvu za kiume.
Lakini unaweza kuzuia yote haya, Leo ukiwa ndani Ya Jukwaa hili La afya.
Ni rahisi kuliko unavyodhani;
â³ Kula vyakula vya asili.
â³ Tumia maji kuliko soda.
â³ Fanya mazoezi angalau dakika 30 kwa siku.
â³ Pima sukari yako angalau mara mbili kwa mwaka.
â³ Elimisha familia yako mapema, k**a kuna historia ya Kisukari mnaweza kurithishana.
Usisubiri kuwekewa insulin ndipo uanze kusema "Laiti ningejua".
Afya yako ni mali yako, Na kisukari hakina huruma.Leo ni siku bora ya kuchukua hatua kuliko kesho yenye gharama ya Matibabu na maumivu ya ugonjwa.