Afya Yako Raha Yako

Afya Yako Raha Yako We Care About Your Health

Wengi Wanatembea Na Kisukari bila kujua na huenda ni wewe, au mtu wa karibu yako.Na mbaya zaidi, kila kona ya dunia, Vij...
25/08/2025

Wengi Wanatembea Na Kisukari bila kujua na huenda ni wewe, au mtu wa karibu yako.

Na mbaya zaidi, kila kona ya dunia, Vijijini hadi mijini watu wanazidi kuathirika na ugonjwa huu kimya kimya k**a moto unaotafuna ndani bila moshi.

Leo nakupa ukweli mzito kuhusu ugonjwa huu wa kimya kimya lakini ni hatari.

Unakunywa Maji Lakini Kiu Haiishi?

Au unakula kila saa lakini bado una njaa isiyoisha?
Unachoka sana, hata bila kufanya kazi ngumu?

K**a jibu ni "NDIYO" Sikiliza kwa makini, Hizi ni dalili za awali kabisa za Kisukari, USIPUUZE

Ugonjwa unaohusiana na kushindwa kwa mwili kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu.

Sasa hebu twende polepole Kisukari Huanzia Wapi?

Kuna aina kuu mbili 2 (Na nusu ½) za kisukari, na zote zina tabia Tofauti Tofauti.
Tuzione hapa...

1. Type 1– Kisukari cha kurithi au cha utotoni

Hiki hutokea pale ambapo kongosho lako linashambuliwa na kinga ya mwili wako...

Matokeo yake?

Mwili kukosa kabisa uwezo wa kutengeneza Insulin, homoni inayosaidia kiwangi sahihi cha sukari kuingia ndani ya seli zako.

Kwa kifupi Sukari inazunguka kwenye damu, Lakini haiingii sehemu inayotakiwa.

2. Type 2 – Kisukari cha mtindo wa maisha.

Aina hii ya kisukari kuhua kwa kasi na kuongoza duniani kwasasa husababishwa na

Kula ovyo (vyakula vya haraka, sukari, mafuta...)

Kukosa mazoezi

Uzito kupita kiasi

Msongo wa mawazo

Na hata watoto siku hizi wanakipata kwa sababu ya kula chipsi, kunywa soda, Mitindo mibovu na malezi mabovu

3. Gestational Diabetes (Kisukari cha Mimba)

Kinatokea wakati wa ujauzito, mara nyingi hutoweka baada ya kujifungua Lakini kuna uwezekano wa kupata Type 2 baadaye.

Unataka kujua k**a kisukari kimeanza kukutembelea?

Basi chunguza mwili wako kwa makini kupitia dalili hizi.

Kukojoa mara kwa mara, hasa usiku

Kiu ya ajabu, unakunywa maji lakini haikati..

Njaa isiyoeleweka

Uchovu wa mara kwa mara

Kupungua uzito bila sababu

Vidonda visivyopona..

Miwasho isiyoisha sehemu za siri au ngozi

Ukipuuza dalili hizi, unakipa kisukari nafasi ya kujenga makazi mwilini mwako.

Sasa Swali Ni Hili, UNAWEZA KUJIKINGA na Kisukari?

Ndiyo unaweza kujikinga, hataka k**a kwenye familia yako kuna mgonjwa wa kisukari.

Kisukari Type 2 kinaweza kuzuilika, na hata kudhibitiwa kikamilifu.Lakini ni lazima ubadili maisha, Sio kwa magumashi, bali kwa maarifa sahihi.

Hebu fuata haya...

Kula kwa akili, sio kwa njaa, Mboga za majani kila siku, Matunda kwa kiasi, si ya sukari nyingi, Nafaka zisizokobolewa, Punguza mafuta mabaya na sukari ya viwandani

Anza kujutuma, mwili wako haukuzaliwa ubweteke, Tembea dakika 30 kila siku, Panda ngazi badala ya lifti, Fanya mazoezi unayoyapenda k**a jogging, hata kazi ngumu k**a kulima...

Punguza uzito, Mzigo mkubwa wa mwili ni mzigo wa kongosho pia...

Tuliza akili yako, Msongo wa mawazo ni mwuaji wa kisasa Unaharibu homoni zako...

Pima sukari mara kwa mara, Huwezi kutibu kile usichokijua, Tumia glucometer nyumbani au pima hospitali...

Ukizembea...Madhara Yake Hayana Huruma.. Kisukari hakisamehi, na hakijali una miaka mingapi.

Madhara yake ni k**a mlango wa majanga, Ukiingia utakumbana na....

Kiharusi na Presha kali

Upofu

Figo kushindwa kufanya kazi (ESRF)

Vidonda visivyopona hadi kukatwa mguu..

Kukosa nguvu za kiume au matatizo ya uzazi

Swali ni je Kisukari Kinatibika?

Wengi wanaona jibu la kwamba Hakiponi lakini wanasahau kuwa kutibu Kisukari kunaanza na Kudhibiti chanzo Na chanzo kinadhibitika vizuri, Na hilo linaweza kuleta maisha marefu, yenye afya na furaha...

Kwa Type 1:

Sindano za insulin kila siku, bila kuruka dozi

Kwa Type 2:

Badili maisha k**a nilivyoeleza

Dawa za kisukari kwa ushauri wa daktari

Ufuatiliaji wa sukari mara kwa mara..

Usikubali Kuishi Bila Kujua hali yako ya kiafya, Wengine wanakufa kwa ugonjwa, wengine kwa kutojua...

Nimekuambia yote haya kwa sababu nakujali, Na najua unaweza kubadili hali yako leo au kusaidia ndugu, rafiki, au mzazi aliyeko hatarini..

Iba Siri hii  ya Asubuhi yenye Afya na Nguvu...Usianze siku kwa kusukumwa na stress, anza kwa kutawala mwili na akili ya...
22/08/2025

Iba Siri hii ya Asubuhi yenye Afya na Nguvu...

Usianze siku kwa kusukumwa na stress, anza kwa kutawala mwili na akili yako...

Dakika chache za mazoezi basi ujue damu inasafisha mwili mzima...

Glasi moja ya tangawizi moto yenye asali mbichi na limao, Unafungua wa mishipa, Unafufua kinga ya mwili, Unanyonya sumu taratibu....

Mchanganyiko huu husaidia...

Kuchochea metabolism yako (kupunguza uzito)..

Kuimarisha kinga ya mwili dhidi ya magonjwa

Kusafisha ini na kuondoa sumu mwilini

Kukuondolea uchovu na kuupa mwili nguvu mpya

Kila asubuhi, kabla ya kushuka simu, kabla ya pilika za maisha,

Jipe zawadi ya afya yako mwenyewe...

Mazoezi + Kikombe cha Tangawizi, Asali & Limao = Siri ya kuamka ukiwa na nguvu na furaha.

Unataka kuiona nguvu mpya ndani ya siku zako?

Anza leo asubuhi .

HASIRA KALI NI SUMU TULI Inaweza kukuua kimya kimya kabla hata ya adui zako...Kitaalamu, hasira ya mara kwa mara huamsha...
21/08/2025

HASIRA KALI NI SUMU TULI Inaweza kukuua kimya kimya kabla hata ya adui zako...

Kitaalamu, hasira ya mara kwa mara huamsha mfumo wa “fight or flight,” ikisababisha mwili kutoa kemikali za stress k**a cortisol na adrenaline.

Matokeo yake...

Mapigo ya moyo kwenda mbio,

Presha ya damu kupanda,

Shinikizo kwenye mishipa ya damu,

Kukosa usingizi,

Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara,

Hatari ya kiharusi, vidonda vya tumbo, magonjwa ya moyo Figo na kisukari…

Na mbaya zaidi Hasira ikishika akili, mantiki huondoka, unabaki na maamuzi ya majuto baadaye...

Sasa, Unafanyaje kudhibiti hii silaha hatari inayoitwa HASIRA...?

Tumia mbinu ya kiakili ya "STOP" Njia bora ya kudhibiti hasira bila kuathiri afya yako...

1. S – Simama...

↳ Usichukue hatua ukiwa kwenye hasira, Simama kimya, Moyo ukipiga haraka, akili ikilipuka– Tulia kwanza.

2. T – Tafakari...

Ni nini kimekuudhi? Je, hasira yako ina uhalali? Je, unaihamishia hasira ya jana kwa mtu wa leo...?

3. O – Ondoa...

Geuza mawazo yako, Toka hapo, Tembea, Piga push-up, Sikiliza mziki wa utulivu, Fanya usafi, Usikubali hasira ikufunge kiakili...

4. P – Pumua...

Pumua polepole ndani kwa sekunde 4... shikilia kwa sekunde 4... toa polepole kwa sekunde 6... Rudia mara 5.

Kupumua (deep breathing exercise) Hurejesha usawa wa kiakili na mwili wako.....

Hasira si ujasiri ni mfumo wa tahadhari wa mwili unao kuumiza kmya kmya...

Ukiidhibiti, unaishi kwa hekima, Ukiiachia ikuumize, Unaishi kwa majuto.

Tiba ya hasira haipo kwenye kulipiza kisasi Ipo kwenye kujua na kujitambua

Ukishagundulika na ugonjwa wa kudumu k**a Shinikizo la Damu, Kisukari, Figo, Moyo au Saratani, ghafla maisha hubadilika....
20/08/2025

Ukishagundulika na ugonjwa wa kudumu k**a Shinikizo la Damu, Kisukari, Figo, Moyo au Saratani, ghafla maisha hubadilika.....
UTAONDOKANA NA...

Tamaa ya macho...
Tamaa ya mwili...
Na kiburi cha Uzima...

Automatic, Unarudi kuwa mnyenyekevu mbele ya uhai..

Utaanza kuona thamani ya maji ya uvuguvugu kuliko pombe...

Utaomba usingizi wenye utulivu kuliko starehe za usiku...

Utaona umuhimu wa lishe bora kuliko kula vyakula vya kukaanga Junk foods....

Swali ni moja tu..!?

Je, lazima usubiri hadi hali iwe mbaya ili ujifunze na kujitibu..?

Learn or Perish

“Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.” Sababu Kuu Kwa Nini Tumbo Ni Chanzo Kikuu Cha Magonjwa:1. Afya ya Utumbo (Gut Health):...
31/07/2025

“Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.”

Sababu Kuu Kwa Nini Tumbo Ni Chanzo Kikuu Cha Magonjwa:

1. Afya ya Utumbo (Gut Health):

Ndani ya utumbo kuna mamilioni ya bakteria (gut microbiome) ambao wanahusika na mmeng’enyo wa chakula, kinga ya mwili, na hata hali ya akili.

Usawa wa bakteria hawa ukivurugika, unaweza kusababisha matatizo k**a:

Kuvimbiwa, gesi, na kiungulia

Magonjwa ya autoimmune (mfano lupus, arthritis)

Allergies (aleji)

Hata msongo wa mawazo (stress) na depression

2. Sumu Zinazokusanyika Mwilini

Tumboni, hasa kwenye utumbo mpana, hufanyika usafishaji wa taka za mwili.

K**a mtu hapati choo vizuri au anakula vyakula visivyo na nyuzinyuzi, sumu hubaki tumboni na hatimaye kuingia tena kwenye damu.

Hii husababisha;

Uchovu sugu

Maumivu ya viungo

Shida za ngozi

Na hata kansa

3. Uhusiano Kati ya Tumbo na Kinga ya Mwili

Zaidi ya 70% ya kinga ya mwili inajengwa tumboni.

Ukishughulikia afya ya utumbo, unasaidia mwili wote kuwa imara dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Magonjwa Ambayo Mara Nyingi Huchochewa na Matatizo ya Tumboni k**a

Kisukari

Shinikizo la damu

Magonjwa ya moyo

Magonjwa ya ngozi (eczema, acne)

Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara

Allergies na pumu

Saratani ya utumbo mpana

Changamoto za uzazi kwa wanawake na wanaume

Nini Ufanye Kuboresha Afya ya Tumbo?

Kunywa maji mengi kila siku

Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi k**a mboga mbichi, matunda, nafaka zisizokobolewa

Epuka vyakula vya kukaanga, sukari nyingi, na vinywaji baridi

Tumia virutubisho vinavyosaidia usafishaji wa utumbo.

Punguza msongo wa mawazo kwani unahusiana moja kwa moja na utumbo

29/07/2025

UNAJUA zaidi ya asilimia 70 ya kinga ya mwili inajengwa tumboni!

Ndiyo maana tunasema “Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.”

Iwapo utumbo haupo sawa unaweza kuumwa kila mara
Ukavimbiwa, kupata Gesi au Kiungulia
Ukapata maumivu ya Kichwa au hata ngozi kupata Upele
Mwili ukachoka bila sababu ya msingi

Anza leo kusafisha Tumbo lako, lishe bora ni tiba bora.

Unahitaji ushauri?
Nitumie ujumbe, nikuelekeze njia sahihi ya kuanzia.

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupata glomerulonephritis. Mambo hayo ni pamoja na:Matati...
23/07/2025

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupata glomerulonephritis.

Mambo hayo ni pamoja na:

Matatizo katika mfumo wake wa damu au lymph

Kuwahi kutumia vimiminika vilivyotengenezwa kwa kemikali za hydrocarbon

Wenye historia ya saratani

Maambukizi ya bacteria aina ya streptococcus, virusi, majipu au maambukizi katika moyo

Mambo mengine yanayoweza kuongeza hatari ya kupatwa na glomerulonephritis ni pamoja na:
1. Magonjwa ya mishipa ya damu k**a vile vasculitis au polyarteritis
2. Matumizi yaliyopitiliza ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non steroidal anti-inflammatory drugs k**a vile aspirin
3. Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili k**a vile Anti-glomerular basement membrane antibody disease na IgA nephropathy
4. Makovu katika chujio (Focal segmental glomerulosclerosis) au hali ya chujio kuwa na kuta nene kuliko kawaida (Membranoproliferative GN)
5. Magonjwa yanayoathiri viungo mbalimbali vya mwili k**a vile Henoch-Schonlein purpura, Goodpasture’s syndrome au Lupus nephritis
6. Ugonjwa wa kimetaboliki wa Amyloidosis

Inaendelea Post Inayofuata

Kuharibika Kwa Chujio za Figo (Glomerulonephritis)   Kuharibika kwa chujio ama Glomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa ...
23/07/2025

Kuharibika Kwa Chujio za Figo (Glomerulonephritis)

Kuharibika kwa chujio ama Glomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa figo unaoathiri sehemu maalum ya figo (chujio) inayohusika na uchujaji wa maji pamoja na uchafu kutoka katika damu.

Sehemu hii huitwa glomelurus au chujio k**a tutakavyokuwa tukitumia katika mada hii.
Mara nyingi chanzo halisi cha kuharibika kwa chujio za figo (glomerulonephritis) huwa hakijulikaniata japo wakati mwingine uharibifu huu unaweza kusababishwa na kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili.
Uharibifu katika chujio husababisha damu pamoja na protini kuingia katika mkojo.Tatizo hili hukua kwa haraka na figo inaweza kupoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kwa kasi ndani ya muda mfupi wa kati wiki chache mpaka miezi kadhaa. Aina hii ya kuharibika kwa chujio za figo kwa haraka hujulikana kitalaamu k**a rapidly progressive glomerulonephritis.

Takribani robo ya watu wanaopatwa na tatizo sugu la glomerulonephritis huwa hawana historia ya kuwa na ugonjwa wowote wa figo hapo kabla.Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupata glomerulonephritis.

inaendelea post inayofuata

Ugonjwa wa saratani ya Ubongo (Brain Tumor)Saratani ya ubongo ni uvimbe uliotokana na mkusanyiko wa chembebehai za ubong...
22/07/2025

Ugonjwa wa saratani ya Ubongo (Brain Tumor)

Saratani ya ubongo ni uvimbe uliotokana na mkusanyiko wa chembebehai za ubongo zilizotengenezwa kwa wingi bila mpangilio kutokana na kubadilika kwa DNA. Ikiwa chembehai hizo ni za kawaida basi uvimbe hujulikana k**a BENIGN, na kinyume chake ni CANCER.

Saratani za ubongo ziko kwenye makundi makuu mawili; yaani PRIMARY ambayo imeanzia kwenye ubongo wenyewe au SECONDARY (METASTASIS) endapo imetokea sehemu nyingine ya mwili mbali na ubongo.

Ukweli kuhusu saratani za ubongo
• Kuna aina 120 au Zaidi za saratani ya ubongo.
• Dalili na madhara yake hutegemeana na aina, ukubwa na mahali ilipo kwenye ubongo.

Vihatarishi vyake
• Umri na jinsia ya k**e.
• Baadhi ya mionzi au mionzi tiba.
• Baadhi ya magonjwa ya kinasaba k**a vile Neurofibromatosis.
• Saratani za sehemu nyingine za mwili k**a vile tezi la thyroid, mapafu, t**i na ini.

Dalili zake
• Maumivu ya kichwa
• Kupungua nuru ya macho au upofu.
• Kupungua usikivu na kupepesuka.
• Kupoteza kumbukumbu na haiba.
• Kupooza mkono au mguu vya upande mmoja.
• Kupata degedege ama kupoteza fahamu.
• Kushindwa kumeza chakula.

Matibabu Yake

• Kufanyiwa vipimo vya damu, CT scan ama MRI ya ubongo.
• Kufanyiwa upasuaji na kupewa dawa

MatibabuShambulio la moyo ni tatizo linalohitaji matibabu ya dharua. Lisipotibiwa kwa haraka husababisha kifo katika mud...
20/07/2025

Matibabu

Shambulio la moyo ni tatizo linalohitaji matibabu ya dharua. Lisipotibiwa kwa haraka husababisha kifo katika muda mfupi sana tangu mgonjwa apatwe na tatizo.

Matibabu ya tatizo hili hujumuisha

Kumpa mgonjwa hewa ya oksijeni

Mgonjwa hupewa vidonge vya Aspirini ndogo kuzuia damu kuganda (thrombolytic) kwa ajili ya kuyeyusha damu iliyaganda na hivyo kuzibua mirija midogo ya damu katika moyo iliyozibwa na kuganda huku kwa damu.

Vile vile mgonjwa hupewa dawa za kuweka chini ya ulimi kiitwacho nitrogylycerin (glyceryl trinitrate) ambazo husaidia kutanua mishipa ya damu (vasodilation)

Dawa ya kutuliza maumivu kwa mfano morphine

Dawa ya kuyeyusha mafuta katika mishipa ya damu k**a vile clopidogrel

Kuzibua mishipa ya damu inayosambaza damu katika moyo kwa kutumia Percutaneous coronary intervention (PCI)

Upasuaji (CABG)

Njia za kuzuia shambulizi la moyo;

Kuacha kuvuta sigara

Kufanya mazoezi ya mara kwa mara

Kupunguza unywaji wa pombe

Kubadilisha aina ya mlo, Kupunguza mafuta katika mlo na chumvi.

Kutumia mafuta ya samaki (omega-3 fatty acids)

Madhara ya shambulizi la moyo

Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

Matatizo katika mfumo wa mapigo ya moyo (Atrial fibrillation) ambayo hatimaye hupelekea kifo

Shambulizi la moyo kurudia mara ya pili

Kifo cha ghafla (sudden death)

Shambulizi la moyo limehusishwa na nini?Tafiti mbalimbali zimeusisha mambo yafuatayo na shambulizi la moyoMsongo wa mawa...
20/07/2025

Shambulizi la moyo limehusishwa na nini?

Tafiti mbalimbali zimeusisha mambo yafuatayo na shambulizi la moyo

Msongo wa mawazo

Maambukizi hasa vichomi vinavyosababishwa na vimelea vya chlamydophila pneumonia.

Hutokea zaidi asubuhi hasa saa tatu (saa 3 asubuhi)

Vipimo na uchunguzi

ECG ;Kipimo hiki huonyesha ni sehemu gani ya moyo iliyoathirika

Coronary angiography ;Kinasaidia kwa kuangalia wapi ambapo mishipa ya damu imekuwa membamba sana kupita kiasi (narrowing of vessels) au imeziba.

Cardiac markers levels

X-ray ya kifua (chest X-ray)

MPI (Myocardial Perfusion Imaging) ;Kipimo hiki hufanywa kwa kutumia mashine maalum ya PET Scan ambapo kinauwezo wa kugundua tatizo la shambulizi la moyo, huchunguza kikamilifu maumivu ya kifua, huangalia mwelekeo wa tiba ya kuzuia damu kuganda, hutoa mwelekeo wa ugonjwa wa shambulizi la moyo k**a ni mzuri au mbaya, hutathmini ubora wa tiba ya shambulizi la moyo kabla na baada ya mgonjwa kupata tiba, huweza kutambua hata shambulizi la moyo ambalo si rahisi kugundulika kwa kutumia vipimo vyengine na pia hutathmini ukubwa wa tatizo la shambulizi la moyo.
Hata hivyo kwa sasa kipimo hiki kinapatikana nchini kwetu.
Ili kuweza kutambua uwepo wa tatizo hili.Mwaka 1979, shirika la Afya Duniani (WHO) liliweka vigezo vya kutambua shambulizi la moyo.

Vigezo hivyo ni;

Historia ya kuwa na maumivu ya kifua zaidi ya dakika 20

Mabadiliko katika kipimo cha ECG, na

Kupanda na kushuka kwa kipimo kiitwacho kitaalamu cardiac biomarkers hasa creatine kinase - MB na troponin

Shambulizi la Moyo (Heart Attack) Moja ya magonjwa hatari sana ambayo yanaweza kumpata mtu yoyote ni ugonjwa wa shambuli...
20/07/2025

Shambulizi la Moyo (Heart Attack)

Moja ya magonjwa hatari sana ambayo yanaweza kumpata mtu yoyote ni ugonjwa wa shambulizi la moyo. Huu ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanaume na wanawake.

Kwa kawaida, ugonjwa huu hutokea pale ambapo sehemu ya nyama ya moyo inapoharibika au kufa kutokana na kukosa damu ya kutosha.

Je tatizo hili husababishwa na nini?
Husababishwa na kuziba kwa mishipa ya damu inayosambaza damu katika moyo (coronary artery blockage) kutokana na mafuta mabaya mwilini (atherosclerotic plaque).

Watu gani wapo katika hatari ya tatizo hili?
Watu walio katika hatari ya kukumbwa na ugonjwa huu ni pamoja na;

Wenye umri mkubwa miaka 45 kwa wanaume na 55 kwa wanawake

Wavutaji wa sigara

Watu wenye mafuta ya lijamu katika damu au wale wenye mafuta mabaya aina ya triglycerides na low density lipoprotein kwa kiwango kikubwa katika damu zao

Wenye kisukari

Wenye matatizo ya shinikizo la damu

Walio na unene kupita kiasi (obesity)

Wenye matatizo sugu ya kushindwa kufanya kazi kwa figo zao (chronic renal failure)

Moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

Wanywaji wa pombe kupindukia

Watumiaji wa madawa ya kulevya hasa co***ne na methamphetamine

Watu wenye msongo wa mawazo (Chronic high stress levels)

Upungufu wa vitamin B2, B6, B12 na folic acid

Dalili za shambulizi la moyo

Maumivu makali ya ghafla kifuani ambayo husambaa kwenye taya, shingo, bega na mkono wa kushoto

Kupumua kwa shida

Kutoka jasho kwa wingi sana (diaphoresis)

Kuhisi mapigo ya moyo yanapiga haraka (palpitations)

Kichefuchefu

Kutapika

Kuchoka haraka sana

Kupoteza fahamu

Address

Moshi,Dar Es Salaam
Dodoma
MOSHI

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya Yako Raha Yako posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram