Procy Afya Point

Procy Afya Point Karibu Procy Afya Point ,Sehemu Ya Kuaminika Kwa Elimu Ya Afya,Lishe Bora Na Suluhisho La Changamoto Za Kiafya Kwa Njia Rahisi Na Salama

Ukishagundulika na ugonjwa wa kudumu k**a Shinikizo la Damu, Kisukari, Figo, Moyo au Saratani, ghafla maisha hubadilika....
20/08/2025

Ukishagundulika na ugonjwa wa kudumu k**a Shinikizo la Damu, Kisukari, Figo, Moyo au Saratani, ghafla maisha hubadilika.....
UTAONDOKANA NA...
Tamaa ya macho...
Tamaa ya mwili...
Na kiburi cha Uzima...
Automatic, Unarudi kuwa mnyenyekevu mbele ya uhai..
Utaanza kuona thamani ya maji ya uvuguvugu kuliko pombe...
Utaomba usingizi wenye utulivu kuliko starehe za usiku...
Utaona umuhimu wa lishe bora kuliko kula vyakula vya kukaanga Junk foods....
Swali ni moja tu..!?
Je, lazima usubiri hadi hali iwe mbaya ili ujifunze na kujitibu..?
Learn or Perish

“Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.” Sababu Kuu Kwa Nini Tumbo Ni Chanzo Kikuu Cha Magonjwa?1. Afya ya Utumbo (Gut Health):...
31/07/2025

“Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.”

Sababu Kuu Kwa Nini Tumbo Ni Chanzo Kikuu Cha Magonjwa?

1. Afya ya Utumbo (Gut Health):

Ndani ya utumbo kuna mamilioni ya bakteria (gut microbiome) ambao wanahusika na mmeng’enyo wa chakula, kinga ya mwili, na hata hali ya akili.

Usawa wa bakteria hawa ukivurugika, unaweza kusababisha matatizo k**a:

Kuvimbiwa, gesi, na kiungulia

Magonjwa ya autoimmune (mfano lupus, arthritis)

Allergies (aleji)

Hata msongo wa mawazo (stress) na depression

2. Sumu Zinazokusanyika Mwilini

Tumboni, hasa kwenye utumbo mpana, hufanyika usafishaji wa taka za mwili.

K**a mtu hapati choo vizuri au anakula vyakula visivyo na nyuzinyuzi, sumu hubaki tumboni na hatimaye kuingia tena kwenye damu.

Hii husababisha;

Uchovu sugu

Maumivu ya viungo

Shida za ngozi

Na hata kansa

3. Uhusiano Kati ya Tumbo na Kinga ya Mwili

Zaidi ya 70% ya kinga ya mwili inajengwa tumboni.

Ukishughulikia afya ya utumbo, unasaidia mwili wote kuwa imara dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Magonjwa Ambayo Mara Nyingi Huchochewa na Matatizo ya Tumboni k**a;

Kisukari

Shinikizo la damu

Magonjwa ya moyo

Magonjwa ya ngozi (eczema, acne)

Maumivu ya kichwa ya mara kwa mara

Allergies na pumu

Saratani ya utumbo mpana

Changamoto za uzazi kwa wanawake na wanaume

Nini Ufanye Kuboresha Afya ya Tumbo?

Kunywa maji mengi kila siku

Kula vyakula vyenye nyuzinyuzi k**a mboga mbichi, matunda, nafaka zisizokobolewa

Epuka vyakula vya kukaanga, sukari nyingi, na vinywaji baridi

Tumia virutubisho vinavyosaidia usafishaji wa utumbo.

Punguza msongo wa mawazo kwani unahusiana moja kwa moja na utumbo

29/07/2025

UNAJUA zaidi ya asilimia 70 ya kinga ya mwili inajengwa tumboni!
Ndiyo maana tunasema “Magonjwa Mengi Huanzia Tumboni.”

Iwapo utumbo haupo sawa unaweza kuumwa kila mara

Ukavimbiwa, kupata Gesi au Kiungulia

Ukapata maumivu ya Kichwa au hata ngozi kupata Upele

Mwili ukachoka bila sababu ya msingi

Anza leo kusafisha Tumbo lako, lishe bora ni tiba bora.

Unahitaji ushauri?
Nitumie ujumbe, nikuelekeze njia sahihi ya kuzuia magonjwa yasiyoambukiza kwa kulilinda tumbo lako.

WATANZANIA wengi wana uzito uliopitiliza (mabonge) kutokana na kutozingatia ulaji unaofaa huku takwimu zikionyesha ni wa...
23/07/2025

WATANZANIA wengi wana uzito uliopitiliza (mabonge) kutokana na kutozingatia ulaji unaofaa huku takwimu zikionyesha ni watu saba pekee nchini katika 100 wanaozingatia mlo kamili.

Takwimu Aidha, Mtanzania mmoja katika watatu, ana uzito uliokithiri na watu wenye elimu na uhakika wa kipato ndio waathirika zaidi.
Katika maeneo machache ambayo tunafanya vizuri ni kwenye mazoezi kwa sababu kumekuwa kwa mfano na marathoni nyingi.
Hatufanyi vizuri kabisa katika masuala ya ulaji bado ni watu saba katika 100 ambao wanazingatia ulaji unaofaa.

Suala la uzito na unene kupita kiasi pia hali imezidi kuwa mbaya, zamani ilikuwa ni katika kila watu wanne, mmoja ana uzito uliokithiri, sasa hivi ni mtu mmoja katika kila watu watatu ana uzito au unene uliokithiri, kwa hiyo hatufanyi vizuri katika eneo hili.

Bahati mbaya kuliko zote vijana ndio wanaathirika zaidi kuliko rika lingine lolote na wanawake wanaathirika zaidi kuliko wanaume na watu wenye umri mdogo na wanawake ndio wako kwenye hatari zaidi.

Utafiti unaonesha kwamba magonjwa yasiyoambukiza k**a saratani, kisukari, figo na shinikizo la juu la damu, yanaathiri zaidi watu wenye kipato cha chini, lakini ni kinyume chake katika baadhi ya nchi k**a Tanzania ambako waathirika wakubwa ni wasomi na wenye uhakika wa kipato.

Katika jamii mfano za wafanyakazi ndio wanaotumia vyakula vya viwandani zaidi, pombe zaidi, ndio watu wenye fursa ya kununua soda na vitu vingine ambavyo vinaathiri afya,wanaathirika zaidi kutokana na mtindo wa maisha kwa kuwa hawana nafasi ya kupata chakula bora kwa kuwa wananunua vyakula wasivyojua namna vilivyoandaliwa na pia hawapati nafasi ya kufanya mazoezi.

Hali hii hupelekea ghrama kubwa kwenye vitu vikubwa vinavyouelemea mwili ikiwemo kutibu magonjwa k**a saratani, matatizo ya figo, shinikizo la juu la damu, kiharusi na kisukari.

Jitahidi upate muda wa kufanya mazoezi na upate mlo kamili unaopaswa kuzingatiwa kila siku na aina yake kwenye mabano ni wanga (ugali, wali au ndizi), mboga (kabichi, spinachi, mchicha au figiri) protini (nyama, samaki, kunde, njegere na maharage), matunda (embe, chungwa, papai au tikiti), vitamini (karanga au korosho) na maji ya kutosha

Madhara yanayoweza kuletwa na ugonjwa wa uti wa mgongoUgonjwa wa uti wa mgongo unaweza kusababisha• Kuamshwa kwa chembec...
20/07/2025

Madhara yanayoweza kuletwa na ugonjwa wa uti wa mgongo

Ugonjwa wa uti wa mgongo unaweza kusababisha
• Kuamshwa kwa chembechembe za damu zinazo sababisha damu kuganda kitaalamu – Disseminated Intravascular Coagulopathy (DIC).

• Kuvuja damu kwa katika tezi za adrenalin na kupelekea kutokea kwa ugonjwa ambao kitaalamu unaitwa – waterhouse friderichsen syndrome.

• Kwa watoto, ugonjwa huu unaweza kusababisha mtoto kuwa na kichwa kikubwa - hydrocephalus.

Matibabu ya ugonjwa wa Uti wa MgongoKwa wagonjwa waliopoteza fahamu ni vizuri kuhakikisha wanapumua vizuri, na njia za h...
20/07/2025

Matibabu ya ugonjwa wa Uti wa Mgongo

Kwa wagonjwa waliopoteza fahamu ni vizuri kuhakikisha wanapumua vizuri, na njia za hewa ziko wazi.

Halikadhalika, iwapo itathibitika kuwa bakteria ndiyo wanaosababisha ugonjwa huu, mgonjwa anaweza kupewa mojawapo ya dawa hizi za antibiotiki k**a cefotaxime au Cefriaxone.

Aidha baadhi ya madaktari hupendelea kuongeza dawa za steroids k**a dexamethasone k**a sehemu ya matibabu.

Iwapo itathibitika ugonjwa huu umesababishwa na virus, dawa k**a Acyclovir huweza kutumika.

Hali kadhalika, ikithibitika kuwa vimelea waliosababisha ugonjwa huu ni wa kundi la fungus, dawa k**a Amphotericin B au flucytosine zaweza kutumika. Mgonjwa pia hupewa Paracetamol kwa ajili ya kushusha homa na kuondoa maumivu ya kichwa.

Vipimo na uchunguziPamoja na kumchunguza mgonjwa kuhusu kuwepo kwa dalili na viashiria vya ugonjwa huu wa Uti wa mgongo,...
20/07/2025

Vipimo na uchunguzi

Pamoja na kumchunguza mgonjwa kuhusu kuwepo kwa dalili na viashiria vya ugonjwa huu wa Uti wa mgongo, daktari pia anaweza kufanya vipimo vifuatavyo;

• Kuchunguza damu ya mgonjwa kwa ajili ya kuangalia uwepo wa vimelea vinavyosababisha ugonjwa na pia kufahamu ni aina gani ya vimelea hao. Hali kadhalika, damu inaweza pia kutumika kuotesha vimelea maabara ili kugundua aina ya vimelea na dawa gani nzuri zinazofaa kwa ajili ya matibabu (culture and sensitivity).

• Kipimo kinachofanyika kwa kuchukua maji ya uti wa mgongo wa mgonjwa na kuyachunguza maabara ili kutambua uwepo wa vimelea, aina ya vimelea na dawa zinazofaa kutibu vimelea hao (Lumbar puncture).

• Kwa baadhi ya maeneo yenye vifaa k**a CT-scan na MRI, mgonjwa pia huweza kuchunguzwa kwa kutumia vifaa hivi ili kufahamu uwepo wa ugonjwa, sehemu lilipo na madhara yaliyosababishwa na ugonjwa huu wa uti wa mgongo. Hata hivyo vipimo hivi haviwezi kutambua aina wala dawa ya kutibu vimelea vinavyosababisha ugonjwa huo.

Dalili za ugonjwa wa uti wa mgongoDalili na viashiria vya uti wa mgongo ni pamoja na;• Shingo kukak**aa na kuwa ngumu is...
20/07/2025

Dalili za ugonjwa wa uti wa mgongo

Dalili na viashiria vya uti wa mgongo ni pamoja na;
• Shingo kukak**aa na kuwa ngumu isivyo kawaida
• Mgonjwa kujihisi homa kali
• Maumivu makali ya kichwa
• Mgonjwa kupoteza fahamu
• Mgonjwa kupatwa na degedege (seizures) na mwili kukak**aa
• Mgonjwa kushindwa kuvumilia mwanga (photophobia)
• Mgonjwa kutoweza kukaa sehemu yenye makelele (phonophobia)
• Kwa watoto, kuvimba utosi
Aidha, wakati wa kumfanyia mgonjwa uchunguzi, daktari anaweza kuangalia pia viashiria vingine vinavyoonesha kuwepo kwa ugonjwa wa uti wa mgongo. Ishara hizi ni k**a vile
• Mgonjwa kuhisi maumivu kwenye uti wa mgongo yanayozuia kukunjua goti wakati anapofanyiwa uchunguzi wa kukunjua goti lake (pain limits passive extension of the knee). Ishara hii huitwa ishara ya Kerning au Kerning's sign.
• Wakati mwingine mgonjwa anapoelekezwa kujitahidi kukunja shingo, miguu (yaani paja pamoja na goti) navyo hujikunja pia (flexion of the neck causes involuntary flexion of the knee and hip). Ishara hii huitwa ishara ya Brudzinski au Brudzinski’s sign.

Ugonjwa Wa Uti wa Mgongo (Meningitis)Ugonjwa wa uti wa mgongo hutokea iwapo utando unaofunika ubongo na uti wa mgongo ut...
20/07/2025

Ugonjwa Wa Uti wa Mgongo (Meningitis)

Ugonjwa wa uti wa mgongo hutokea iwapo utando unaofunika ubongo na uti wa mgongo utapatwa na maambukizi.

Ugonjwa wa Uti wa mgongo husababishwa na vimelea mbalimbali vya makundi ya bakteria, virus na hata fungus.

Tukivigawanya visababishi hivi katika makundi haya, tutaona kuwa bakteria wanaosababisha ugonjwa wa uti wa mgongo ni k**a vile; bakteria wajulikanao k**a;
Beta-streptococci,
Hemophilus influenza,
Escherichia coli,
Listeria monocytogenes,
Neisseria meningitides,
Streptococci pneumoniae pamoja na
Mycobacteria tuberculosis, ambao pia ni maarufu kwa kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu.

Aidha kutoka kundi la virus, virus wanaojulikana kwa kusababisha ugonjwa huu wa uti wa mgongo ni pamoja na Herpes simplex type 2, HIV pamoja na Varicella zoster.

Vimelea vya fungus ambavyo hujulikana kwa kusababisha ugonjwa wa uti wa mgongo ni pamoja na wale wajulikanao k**a Coccoidiodomycosis pamoja na Cryptococci meningetides.

Je, unajua afya ya mifupa ni msingi wa maisha yako ya kila siku? Mifupa yetu ni nguzo kuu inayotuwezesha kusimama, kutem...
20/07/2025

Je, unajua afya ya mifupa ni msingi wa maisha yako ya kila siku?

Mifupa yetu ni nguzo kuu inayotuwezesha kusimama, kutembea, hata kulinda viungo ndani mwetu.
Lakini, maisha ya kisasa, vyakula visivyofaa, ukosefu wa mazoezi, na umri vinaweza kuathiri afya ya mifupa yako.

Leo nawapa njia rahisi za kuimarisha mifupa yako:

✅ Kula vyakula vyenye Calcium na Vitamin D (maziwa, samaki, mboga za majani).
✅ Fanya mazoezi ya kuimarisha mifupa k**a kutembea, kuruka kamba, au yoga.
✅ Epuka uvutaji sigara na pombe kupita kiasi.
✅ Fanya vipimo vya afya ya mifupa k**a unahisi maumivu au ugumu.

Afya ya mifupa si kitu cha kuchelewa kuanzia leo!
Changanya njia hizi na maisha yako na utaona mabadiliko.

Umejaribu nini kuimarisha mifupa yako? Share nasi hapa chini na tusaidiane!

Yafahamu madhara ya ugonjwa Osteoporosis na tiba zake;Mojaya madhara ya ugonjwa huu ni Ulemavu wa kudumu kutokana na kuv...
09/07/2025

Yafahamu madhara ya ugonjwa Osteoporosis na tiba zake;

Mojaya madhara ya ugonjwa huu ni Ulemavu wa kudumu kutokana na kuvunjika kwa uti wa mgongo au paja

Maumivu sugu yanayosababisha kutotembea vizuri

Kushuka kwa ubora wa maisha (hata kufanya shughuli ndogo inakuwa ngumu)

Hatari ya kifo ndani ya mwaka 1 baada ya kuvunjika kwa paja kwa wazee

Msongo wa mawazo (depression) kwa wagonjwa waliopoteza uwezo wa kujitegemea

Matibabu ya ugonjwa huu ni pamoja na ;
A) Kubadili Mtindo wa Maisha

Kula vyakula vyenye kalsiamu & vitamin D

Kufanya mazoezi ya uzito mdogo mfano kutembea, kupanda ngazi, aerobics

Kupunguza uzito au kuongeza BMI kwa walio chini ya kawaida

Kuacha pombe na sigara

B) Dawa za Hospitali
Bisphosphonates Alendronate, Risedronate hizi hutumika Kuzuia kuvunjika kwa mfupa kwa kuimarisha density na unatakiwa kutumia asubuhi kabla ya kula, kaa wima kwa dakika 30.

Calcium carbonate / citrate yenye 500-1000 mg/siku hutumika Kuongeza akiba ya kalsiamu unatakiwa utumie pamoja na chakula.

Vitamin D3 (Cholecalciferol) 800-2,000 IU/siku hii husaidia kunyonya calcium na Hakikisha usi-overdose.

Hormone Replacement Therapy (HRT) Estrogen + Progesterone Kwa wanawake wa menopause husaidia lakini Huongezeka hatari ya saratani.

Denosumab hizi ni Sindano kila miezi 6,Huzuia kuvunjika kwa mifupa kwa wale wasiovumilia bisphosphonates.

Teriparatide (PTH analog),hii ni Sindano kila siku na Husaidia uundaji wa mfupa mpya.Ni Ghali, huhitajika kwa kesi kali

C) Lishe na Virutubisho Vinavyosaidia

Calcium hii ina 1000-1200 mg kwa siku na Hujenga na kudumisha mifupa

Vitamin D3 ina 1000–2000 IU ambayo Husaidia ngozi ya calcium kwenye utumbo.

Magnesium 250-400 mg hii Husaidia kazi ya Vitamin D na uimara wa mfupa.

Collagen type I yenye 5-10 g ni Msingi wa mfupa na cartilage

Vitamin K2 yenye 90–120 mcg hii Husaidia kuweka calcium kwenye mfupa badala ya mishipa

Zinc na Boron hii huchochea ukuaji wa mfupa mpya

Jitahidi kufanya yafuatayo kwa ajili ya afya yako;

Pima hali ya mifupa (Bone Mineral Density test) k**a una hatari kubwa.

Anza virutubisho vya Calcium + Vit D ukiwa ≥ 50 au umevunjika mfupa bila sababu.

Epuka kuvuta sigara, pombe nyingi, na epuka kukaa kitandani muda mrefu.

Tembea angalau dakika 30 kila siku mazoezi mepesi yanazuia kupoteza mfupa.

Kula vyakula k**a samaki wa kukaangwa na mifupa (dagaa), maziwa, spinach, mayai, uyoga, maharage na mbegu.

UFAHAMU UGONJWA WA OSTEOPOROSISOsteoporosis ni hali ya mifupa kupungua uzito na uimara wake, na hivyo kuwa dhaifu sana n...
08/07/2025

UFAHAMU UGONJWA WA OSTEOPOROSIS
Osteoporosis ni hali ya mifupa kupungua uzito na uimara wake, na hivyo kuwa dhaifu sana na kuvunjika kwa urahisi hata kwa mshtuko mdogo.

Duniani, mtu 1 kati ya 3 wanawake na 1 kati ya 5 wanaume walio na miaka 50+ hupata fracture (kupasuka kwa mfupa) kutokana na osteoporosis.
Inaathiri zaidi wanawake baada ya kukoma hedhi.

Sababu Kuu za ugonjwa huu ni;

Umri mkubwa (hasa 50+)

Kukosa mazoezi ya nguvu

Lishe duni (hasa upungufu wa calcium na vitamin D)

Kukoma hedhi kwa wanawake

Matumizi ya muda mrefu ya dawa za corticosteroids

Historia ya familia ya ugonjwa huu

Dalili za ugonjwa huu ni;

Maumivu ya mgongo (haswa kiuno)

Kupungua kwa urefu wa mwili

Kuinama au kujipinda mgongo

Kuvunjika kwa mifupa kirahisi (mf. nyonga, mkono, au uti wa mgongo)

Madhara yatokanayo na ugonjwa ni k**a ;

Kupoteza uhuru wa kutembea

Maumivu ya kudumu

Kupoteza urefu wa mwili

Hatari kubwa ya kuvunjika kwa mifupa mikubwa (k**a nyonga)

Matibabu pamoja na Kinga ya ugonjwa huu ni;

Tumia vyakula vyenye calcium & vitamin D (maziwa, mboga za kijani, samaki wa minofu)

Fanya mazoezi ya kubeba uzito (weight-bearing exercises)

Epuka sigara na pombe

Dawa maalum hupendekezwa na daktari (mf. bisphosphonates)

Supplement k**a OsteoProcare husaidia kujenga na kuimarisha mifupa

Usingoje kuvunjika ndipo uchukue hatua. Lisha mifupa yako leo kwa afya ya kesho!

Address

Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Procy Afya Point posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram