ELCT/NYAKAHANGA DD.HOSPITAL KARAGWE-TANZANIA

ELCT/NYAKAHANGA DD.HOSPITAL KARAGWE-TANZANIA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ELCT/NYAKAHANGA DD.HOSPITAL KARAGWE-TANZANIA, Karagwe.

Huduma za Ambulance zilikuwa za shida hivyo watu walilazimika kutumia vitanda vya kutengenza lakini kuhakikisha wagonjwa...
24/11/2023

Huduma za Ambulance zilikuwa za shida hivyo watu walilazimika kutumia vitanda vya kutengenza lakini kuhakikisha wagonjwa wanafikishwa Hospitali. Lakini pia akina Mama waliongoza na wagonjwa kwa ajili ya kuhakikisha huduma ya chakula kila aina kinapatikana. Hapo mama akiwa kijanjabo ana andaa chakula

Elct Nyakahanga Hospital Administration block
24/11/2023

Elct Nyakahanga Hospital Administration block

Elct Nyakahanga Hospital wodi B katika ubora wake miaka ile
24/11/2023

Elct Nyakahanga Hospital wodi B katika ubora wake miaka ile

Elct Nyakahanga Hospital hatuwezi kusahahu kuwaenzi wazee wetu na viongozi wetu waliokwisha tangulia mbele ya haki na we...
24/11/2023

Elct Nyakahanga Hospital hatuwezi kusahahu kuwaenzi wazee wetu na viongozi wetu waliokwisha tangulia mbele ya haki na wengine bafo wapo lakini wanahitaji faraja yetu. Tunaendelea kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki viongozi wetu wa Hospitali na wastaafu wote.
Hapo ni jengo la kanisa yetu kabla ya kufanyiwa marekebisho. Pia picha nyingine inaonyesha siku ya maafari ya kuhitimu wanafunzi wa Pre-Nursing enzi zile

Hospitali ya Elct Nyakahanga imekuwa ikitoa huduma za kimwili na kiroho.
24/11/2023

Hospitali ya Elct Nyakahanga imekuwa ikitoa huduma za kimwili na kiroho.

Elct Nyakahanga Hospital enzi hizo wakati wa black and white dhima yetu ilikuwa ni kutoa huduma bora za afya na tiba. Tu...
24/11/2023

Elct Nyakahanga Hospital enzi hizo wakati wa black and white dhima yetu ilikuwa ni kutoa huduma bora za afya na tiba. Tumetoka mbali na bado safari ni ndefu. Mungu wetu tunakuomba uendelee kutupa moyo wa kutenda kazi yako kwa wahitaji ili wauone uwepo wako katika Hospitali yetu. Mungu utubariki na zaidi wabariki viongozi wetu wa Hospitali na Dayosisi yetu ya karagwe

Kusimikwa kwa viongozi wa Hospitali ya Nyakahanga. Tarehe 22/10/2023 ilikuwa siku ya furaha na tulivu, siku muhimu na ya...
24/10/2023

Kusimikwa kwa viongozi wa Hospitali ya Nyakahanga. Tarehe 22/10/2023 ilikuwa siku ya furaha na tulivu, siku muhimu na ya kumbukumbu kwani Viongozi wawili Dr Furaha Kahindo - Mganga Mkuu na Mr Justine Kataraia - Muuguzi MKuu walisimikwa rasmi na Baba Askofu Benson Bagonza Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Dayosisi ya Karagwe kuongoza Hospitali kwa kipindi hiki.

Akisoma Hati ya Dayosisi ya karagwe kwa ajili ya viongozi wateule wa Hospitali ambao ni Dr Furaha Mganga Mkuu na Justine Kataraia Muuguzi Mkuu, Katibu mkuu wa Dayosisi Mch Jeremiah M Rugimbana alisema, kwa mujibu wa katiba ya Dayosisi ya Karagwe, ukurasa wa 27, kifungu cha 1.14.2.i kuna kazi za Halmashauri kuu. Halmashauri kuu ya Dayosisi ya Karagwe namba 142 iliyofanyika Karagwe Hoteli kayanga tarehe 7/6/2023, katika agenda yake namba HK/142/9 ilimchagua Dr Furaha Darlene aliyekuwa akikaimu nafasi ya Mganga Mkuu kuwa Mganga mkuu kamili. Aidha Manejimenti ya Dayosisi ya Karagwe kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya KKKT Dayosisi ya karagwe ilimteua Bwana Justine Kataraia kuwa Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Nyakahanga kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Kwenye nafasi hiyo ya Uongozi.

Hivyo baada ya kusomwa kwa hati hiyo Baba Askofu aliwasimika viongozi hao kila mmoja kwa nafasi yake. Mhesh Baba Askofu waombea kwa Mungu wa Mbinguni asiwapungukie wanapoamka, wanapoingi na kutoka na kuwatakia mafanikio katika wajibu huu mpya. Aidha aliwakumbusha kwamba kuwa kiongozi kuna garama zake, na nyingi ni chungu sana. Aliendelea kusema kuwa ukiwa kuongozi unapoteza uhuru wako binafsi,hutavaa k**a unavyopenda, hutakunywa k**a unavyopenda, hutakula popote unavyopenda, hutaenda popote k**a unavyopenda, utajichunga badala ya kuchungwa, utasengenywa lakini wewe huma haki ya kusengenya wengine, utalalamikiwa lakini wewe huna haki wala mahali pa kulalamika, waliochini yako wana haki ya kuonywa lakini wewe huna hiyo haki maana kosa moja unaondoka.

Address

Karagwe

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELCT/NYAKAHANGA DD.HOSPITAL KARAGWE-TANZANIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share