Afya yako na dr alexander

  • Home
  • Afya yako na dr alexander

Afya yako na dr alexander karibuni

Homa ya ini (Hepatitis) husababishwa na sababu mbalimbali, na hizi ni baadhi za sababu kuu:1. Maambukizi ya Virusi: Hii ...
14/01/2025

Homa ya ini (Hepatitis) husababishwa na sababu mbalimbali, na hizi ni baadhi za sababu kuu:

1. Maambukizi ya Virusi: Hii ni sababu kuu ya homa ya ini. Virusi vinavyosababisha homa ya ini ni:

Hepatitis A: Hutokana na kula au kunywa chakula au maji yaliyochafuliwa na virusi.

Hepatitis B: Husambazwa kupitia damu, mbegu za kiume, au mawasiliano ya karibu ya kijinsia. Pia inaweza kutokea kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Hepatitis C: Hutokea hasa kupitia kugusana na damu iliyo na virusi, k**a vile kupitia matumizi ya sindano za pamoja au matibabu ya madaktari/au wauguzi wasioweza kudumisha usafi wa vifaa.

Hepatitis D: Hii inahitaji virusi vya Hepatitis B ili kuweza kuishi, na husambazwa kupitia damu au mawasiliano ya kijinsia.

Hepatitis E: Hutokea hasa kutokana na kunywa maji machafu yaliyochafuliwa na virusi.

2. Matumizi ya Pombe Kupita Kiasi: Matumizi ya pombe kwa kiwango kikubwa na kwa muda mrefu yanaweza kusababisha uharibifu wa ini na homa ya ini (Alcoholic Hepatitis).

3. Madawa: Baadhi ya dawa, ikiwa ni pamoja na zile zinazotumika kwa matibabu ya magonjwa mengine, zinaweza kusababisha homa ya ini k**a madhara ya dawa. Hali hii inaitwa "drug-induced hepatitis."

4. Magonjwa ya Kinga ya Mwili (Autoimmune Diseases): Katika baadhi ya hali, mfumo wa kinga ya mwili unaweza kushambulia ini kwa makosa, hali hii inaitwa "autoimmune hepatitis."

5. Homa ya Ini ya Kiasi (Non-Alcoholic Fatty Liver Disease - NAFLD): Hii inatokea wakati mafuta yanapokusanyika kwenye ini, mara nyingi kutokana na unene kupita kiasi, kisukari, au matatizo mengine ya metaboli.

6. Maambukizi ya Bakteria au Parasitic: Ingawa ni nadra, baadhi ya maambukizi ya bakteria au vimelea vya minyoo vinaweza kusababisha homa ya ini, hasa katika maeneo ya joto na maji machafu.

7. Kufanya Maisha ya Hatari: Tabia za kijinsia zisizo salama na kushiriki kwa karibu na watu wenye hatari ya maambukizi (k**a vile kutumia dawa kwa sindano) kunaongeza hatari ya kupata homa ya ini, hasa aina za B, C, na D.

Kuelewa sababu hizi kunaweza kusaidia katika kuchukua hatua za kujikinga, k**a vile kujizuia na maambukizi, kupokea chanjo kwa aina fulani za homa ya ini, na kubadili tabia hatarishi.

06/12/2024

Mtu kupata uvimbe kwenye mkono na kutoa usahau (au puru) kunaweza kuwa ni dalili ya matatizo mbalimbali, na inategemea na hali ya uvimbe na dalili nyingine zinazojitokeza. Baadhi ya matatizo ambayo yanaweza kusababisha hali hii ni:

1. Infection (Maambukizi): Maambukizi ya bakteria, virusi, au fangasi yanaweza kusababisha uvimbe na kutoa usaha. Maambukizi haya yanaweza kutokea baada ya jeraha au vidonda kwenye ngozi. Baadhi ya maambukizi maarufu ni k**a vile cellulitis, ambapo ngozi na misuli chini yake huvimba.

2. Abscess (Puru): Hii ni hali ambapo maambukizi ya bakteria husababisha uvimbe wenye usaha ndani yake. Abscess hujulikana k**a puru, na inaweza kutokea baada ya majeraha au kutokana na maambukizi ya bakteria kwenye follicles za nywele au tezi za mafuta.

3. Lymphadenopathy (Uvimbaji wa tezi za lymph): Tezi za lymph kwenye sehemu mbalimbali za mwili zinaweza kuvimba k**a njia ya mwili kupambana na maambukizi. Hii inaweza kuhusisha uvimbe kwenye mkono na kutoa usaha ikiwa maambukizi ni ya bakteria.

4. Cyst (Kisukari): Cyst ni mfuko wenye majimaji au umajimaji unaoweza kuonekana k**a uvimbe. Katika baadhi ya matukio, cyst inaweza kujaa pus (usaha) ikiwa kuna maambukizi.

5. Hali ya ngozi (K**a Acne au Folliculitis): Acne au folliculitis inaweza kusababisha uvimbe na kutoa usaha kwenye maeneo k**a mikono, hasa k**a kuna maambukizi kwenye follicle za nywele.

6. Hali ya autoimmune: Magonjwa ya autoimmune k**a vile lupus au rheumatoid arthritis yanaweza kusababisha uvimbe na maumivu, ingawa haya siyo mara nyingi husababisha usaha.

Hali hii ni ya muhimu kutibiwa na mtaalamu wa afya, kwa sababu maambukizi au matatizo mengine yanaweza kuwa na madhara makubwa. Ikiwa uvimbe unasisitiza, kuna joto, maumivu au homa, ni muhimu kutafuta huduma ya matibabu haraka.

๐“๐Ž๐Š๐Ž๐Œ๐„๐™๐€ ๐‡๐Ž๐Œ๐€ ๐˜๐€ ๐ˆ๐๐ˆ [ ๐—›๐—˜๐—ฃ๐—”๐—ง๐—œ๐—ง๐—œ๐—ฆ ๐] ๐๐ƒ๐€๐๐ˆ ๐˜๐€ ๐–๐ˆ๐Š๐ˆ  ๐Ÿ๐Ÿ:Rejesha afya na tumaini jema la maisha yako:HOMA YA INI INATIBIKA:...
27/11/2024

๐“๐Ž๐Š๐Ž๐Œ๐„๐™๐€ ๐‡๐Ž๐Œ๐€ ๐˜๐€ ๐ˆ๐๐ˆ [ ๐—›๐—˜๐—ฃ๐—”๐—ง๐—œ๐—ง๐—œ๐—ฆ ๐] ๐๐ƒ๐€๐๐ˆ ๐˜๐€ ๐–๐ˆ๐Š๐ˆ ๐Ÿ๐Ÿ:

Rejesha afya na tumaini jema la maisha yako:
HOMA YA INI INATIBIKA:

HEPATITIS B :- Ni homa ya INI inayosababishwa na kirus wa Hepatitis B.

Virusi ivyo vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza watu mara 100 zaidi ya virusi vya ukimwi.

Zifuatazo ni baadhi ya njia za usambaaji wa virusi vya homa ya ini ambazo ni pamoja na:-

[1] Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

[2 ] Kufanya mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini.

[3 ] Kuchangia vifaa vyenye ncha kali k**a sindano hasa kwa watumiaji wa madawa ya kulevya au wachora tattoo, miswaki.

[4 ] Kuongezewa damu ambayo ina maambukizi ya virus vya homa ya INI aina ya Hepatitis.

[5 ] Kunyonyana Ndimi Dendaโ€™ na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini.

[6 ] Kuchangia taulo na mtu mwenye ugonjwa huu.

[7 ] Kubadilishana nguo na mtu mwenye huu ugonjwa au kukumbatiana wakati mkiwa mnavuja jasho.

Tafiti za kitaalamu zinaonesha kuwa virusi hivyo ni hatari kuliko virus vya ukimwi kwa sababu vinaweza kuishi nje ya mwili wa binadamu (yaani nje ya mfumo wa damu) kwa siku saba 7 hadi nane 8.

Virusi vya ukimwi (VVU) havina uwezo wa kuishi nje ya mfumo wa damu hata kwa dakika moja.

Mtu mwenye homa ya ini ana wastani mdogo wa kuishi kuliko mwenye ukimwi.

Kwa maana hiyo, mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini hufariki dunia haraka sana k**a hatopatiwa matibabu mapema basi huishi muda mfupi sana kuliko mwenye VVU.

๐๐€๐€๐ƒ๐‡๐ˆ ๐˜๐€ ๐ƒ๐€๐‹๐ˆ๐‹๐ˆ ๐™๐ˆ๐“๐Ž๐Š๐€๐๐€๐™๐Ž ๐๐€ ๐‡๐Ž๐Œ๐€ ๐˜๐€ ๐ˆ๐๐ˆ:

[1 ] Uchovu wa mara kwa mara

[2 ] Kichefuchefu.

[3 ] Mwili kuwa dhaifu na Kukosa nguvu.

[4 ] Homa kali.

[5 ] Kupoteza hamu ya kula.

[6 ] Kupungua uzito.

[7 ] Maumivu makali ya tumbo upande wa ini.

[8 ] Macho na ngozi kuwa vya njano.

[7 ] Mkojo mweusi/mkojo kuwa na rangi iliyokolea k**a coca-cola.

Kuna baadhi ya wagonjwa wa homa ya ini hukaa muda mlefu [Miaka mingi] pasipo kuona dalili yoyote za homa ya ini, kwa kipindi iki ini likiendelea kuharibika hatimae huja kupata ugonjwa mkali wa ini na kusababisha ini kushindwa kabisa kufanya kazi pia huweza kusababisha kifo asipopata matibabu sahihi na mapema.
Hii hatua huitwa โ€œ๐—™๐˜‚๐—น๐—บ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐—ป๐˜ ๐—น๐—ถ๐˜ƒ๐—ฒ๐—ฟ ๐—ณ๐—ฎ๐—ถ๐—น๐˜‚๐—ฟ๐—ฒโ€.

Dalili huja kuonekana waziwazi miaka mingi baada ya mtu kuambukizwa.

Kwa wenye maambukizi ya virusi aina C matibabu ya Dawa kwa wiki 8 humaliza tatizo [Kupona kabisa] .

Na kwa wenye Virus aina ya B matibabu ya Dawa ni kwa wiki 12 adi 16 humaliza virus wote. [Kupona kabisa]

๐—•๐—”๐—”๐——๐—›๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐— ๐—”๐——๐—›๐—”๐—ฅ๐—” ๐—ฌ๐—”๐—ง๐—ข๐—ž๐—”๐—ก๐—”๐—ฌ๐—ข ๐—ก๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ ๐—œ๐—ฆ๐—œ๐—ฃ๐—ข ๐—ง๐—œ๐—•๐—œ๐—ช๐—” ๐— ๐—”๐—ฃ๐—˜๐— ๐—”:

[1 ] INI kushindwa kabisa kufanya kazi (liver failure).

[2 ] Saratani ya ini (hepatoma).

[3 ] Figo kuferi na kujaa maji

[4 ] Maumivu ya tumbo yasiyo isha

[5 ]Tumbo, Sura na miguu kuvimba.

[6 ] Njaa ya mara kwa mara na kali.

[7 ] Manjano ya macho na ngozi yasiyo isha

[8 ] Mgonjwa Kupoteza maisha

๐—จ๐—ฆ๐—›๐—”๐—จ๐—ฅ๐—œ ๐—ก๐—” ๐—ž๐—จ๐— ๐—จ๐—ข๐—ก๐—” ๐——๐—”๐—ž๐—ง๐—”๐—ฅ๐—œ ๐—›๐—จ๐—ง๐—ข๐—Ÿ๐—˜๐—ช๐—” ๐—•๐—จ๐—ฅ๐—˜...

Bonyeza namba hii kuwasiliana nasi kupitia WhatsApp au kupiga simu

๐Ÿ“ž 0692094104

๐—ช๐—”๐—ž๐—”๐—ง๐—œ ๐—จ๐—ก๐—”๐—ฃ๐—ข ๐—˜๐—ก๐——๐—˜๐—Ÿ๐—˜๐—” ๐—ž๐—จ๐—ง๐—จ๐— ๐—œ๐—” ๐——๐—ข๐—ญ๐—œ ๐—จ๐—ง๐—”๐—ฃ๐—˜๐—ช๐—” ๐—จ๐—ง๐—”๐—ฅ๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—จ ๐—ช๐—” ๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ๐—ก๐—š๐—”๐—ง๐—œ๐—” ๐—Ÿ๐—œ๐—ฆ๐—›๐—˜ ๐—•๐—ข๐—ฅ๐—” ๐—ฆ๐—”๐— ๐—•๐—”๐— ๐—•๐—” ๐—ž๐—ช๐—” ๐—–๐—›๐—”๐—ก๐—š๐—”๐— ๐—ข๐—ง๐—ข ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ, ๐—œ๐—Ÿ๐—œ ๐—ž๐—จ๐—ฃ๐—”๐—ง๐—” ๐— ๐—”๐—ง๐—ข๐—ž๐—˜๐—ข ๐—–๐—›๐—”๐—ก๐—ฌ๐—” ๐—ก๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—”๐—ฅ๐—”๐—ž๐—” ๐—ญ๐—”๐—œ๐——๐—œ ๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—ž๐—” ๐—ž๐—จ๐—ง๐—ข๐—ž๐—ข๐— ๐—˜๐—ญ๐—” ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ:

๐“๐”๐๐€๐๐€๐“๐ˆ๐Š๐€๐๐€ ๐ƒ๐€๐‘ ๐„๐’ ๐’๐€๐‹๐€๐€๐Œ - ๐Š๐ˆ๐Œ๐€๐‘๐€ - ๐’๐“๐Ž๐ ๐Ž๐•๐„๐‘:

- ๐—ž๐—”๐—ฅ๐—œ๐—•๐—จ ๐—ง๐—จ๐—ž๐—จ๐—›๐—จ๐——๐—จ๐— ๐—œ๐—˜ -

๐—™๐—”๐—›๐—”๐— ๐—จ  ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ฉ๐—œ๐—ฅ๐—จ๐—ฆ๐—œ ๐—ฉ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ, ๐——๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—Ÿ๐—œ ๐—ก๐—” ๐— ๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—”๐—•๐—จ:Homa ya ini hujulikana kwa kitaalamu k**a Hepatitis.Hep...
24/11/2024

๐—™๐—”๐—›๐—”๐— ๐—จ ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ฉ๐—œ๐—ฅ๐—จ๐—ฆ๐—œ ๐—ฉ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ, ๐——๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—Ÿ๐—œ ๐—ก๐—” ๐— ๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—”๐—•๐—จ:

Homa ya ini hujulikana kwa kitaalamu k**a Hepatitis.

Hepatitis ni kirusi kinacho sababisha saratani ya ini baada ya kuishi na maambukizi ya muda mrefu pasipo kutibia.

Katika maeneo yetu, bara la afrika maambukizi ya virusi vya homa ya ini ndio sababu kuu ya shida kwenye ini.

Virusi vya homa ya ini vipo vya aina 5 (A,B,C,D,E) ambapo aina mbili za virusi (B na C ) ndio sababu kuu za ugonjwa wa homa ya ini na husambaa kupitia damu na majimaji ya mwili.

Homa ya ini ni sawa janga linaloua kimya kimya kulingana na takwimu za vifo vya dunia inakadiriwa kirusi cha homa ya ini aina ya B pekee huua watu 600,000 hivi kila mwaka.

Kwa wastani zaidi ya watu bilioni mbili, yaani, asilimia 33 hivi ya watu wote ulimwenguni, wameambukizwa virusi vya HBV (Hepatitis B Virus), na wengi wao hupona baada ya miezi michache kupitia kinga zao za mwili au kupitia medications ya dozi za Ant-hepatitis B Virus.

Watu milioni 350 hivi huendelea kuwa na virusi hivyo mwilini, wengi huishi bila dalili na kuendelea kuambukiza watu wengine.

๐—•๐—”๐—”๐——๐—›๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ก๐—๐—œ๐—” ๐—ญ๐—” ๐—ž๐—จ๐—ฆ๐—”๐— ๐—•๐—”๐—ญ๐—” ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ฉ๐—œ๐—ฅ๐—จ๐—ฆ ๐—ฉ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ:

โ–ช๏ธKushiliki ngono isiyo salama na mtu mwenye kuishi na maambukizi ya virus vya Hepatitis.

โ–ช๏ธKuchangia vitu vyenye ncha kali k**a vile sindano, kisu NK.

โ–ช๏ธKuvaliana na nguo na mtu mwenye maambukizi ya virus vya Hepatitis.

โ–ช๏ธKushika maji maji yatokayo mwilini mwa mtu alie na maambukizi ya virus vya homa ya ini Hepatitis.

โ–ช๏ธKuchangia damu au kutumia vifaa vya kusafishia damu k**a ilivyo kwa Dialysis ya figo.

๐—•๐—”๐—”๐——๐—›๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐——๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—Ÿ๐—œ ๐—ญ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ:

Kwa kawaida dalili za mwanzo za homa ya ini hutokea ndani ya miezi 6 baada kuambukizwa,na hutokea kwa baadhi ya watu hazitokei kwa kila mtu.

Mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini hupata dalili zifuatazo;

[ 1 ] Tumbo kujaa Gesi, vidonda vya tumbo, uchovu na kuishiwa nguvu.

[ 2 ] Kichefuchefu na kutapika.

[ 3 ] Miwasho ya ngozi na majipu.

[ 4 ] Homa kali na za mara kwa mara.

[ 5 ] Kupoteza hamu ya kula, kuharisha.

[ 6 ] Kupungua uzito kupita kiasi.

[ 7 ] Maumivu makali ya tumbo upande wa ini upande wa kulia.

[ 8 ] Macho na ngozi kuwa vya njano.

[ 9 ] Mkojo mweusi/mkojo kuwa na rangi iliyokolea k**a coca-cola.

๐— ๐—”๐——๐—›๐—”๐—ฅ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—ž๐—จ๐—œ๐—ฆ๐—›๐—œ ๐—ก๐—” ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ฉ๐—œ๐—ฅ๐—จ๐—ฆ๐—œ ๐—ฉ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—ข๐— ๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—œ๐—ก๐—œ ๐—ž๐—ช๐—” ๐— ๐—จ๐——๐—” ๐— ๐—Ÿ๐—˜๐—™๐—จ ๐—ฃ๐—”๐—ฆ๐—œ๐—ฃ๐—ข ๐—ž๐—จ๐—ง๐—œ๐—•๐—œ๐—ช๐—”:

Kuna kundi dogo la wagonjwa wa homa ya ini hupata ugonjwa mkali wa ini na kusababisha ini kushindwa kabisa kufanya kazi pia huweza kusababisha kifo. Hii hatua huitwa โ€œ๐—ณ๐˜‚๐—น๐—บ๐—ถ๐—ป๐—ฎ๐—ป๐˜ ๐—น๐—ถ๐˜ƒ๐—ฒ๐—ฟ ๐—ณ๐—ฎ๐—ถ๐—น๐˜‚๐—ฟ๐—ฒโ€.

Watu wenye maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini mara nyingi huwa hawana dalili kwa miaka mingi, kadri muda unavyoenda virusi vya hepatitis husababisha ini kusinyaa hatua hii ya ini kusinyaa huitwa (๐—น๐—ถ๐˜ƒ๐—ฒ๐—ฟ ๐—ฐ๐—ถ๐—ฟ๐—ฟ๐—ต๐—ผ๐˜€๐—ถ๐˜€) hupelekea ini kushindwa kabisa kufanya kazi vyema.

Pia maambukizi ya virusi vya homa ya ini huchangia kupata saratani ya ini ambayo hujulikana kwa kitaalamu k**a ๐—ต๐—ฎ๐—ฝ๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ฐ๐—ฒ๐—น๐—น๐˜‚๐—น๐—ฎ๐—ฟ ๐—ฐ๐—ฎ๐—ฟ๐—ฐ๐—ถ๐—ป๐—ผ๐—บ๐—ฎ.

๐—ž๐—จ๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—”: Watu wengi wameangaika katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili, ili kunusuru maisha kwa ghalama mbali mbali na hatimae kukosa kutimiza lengo la matibabu katika kumaliza tatizo hili na mwisho huishi na fikra potofu au tofauti ya kuamini kwamba ugonjwa huu hauna tiba na hivyo hupoteza matumaini ya kuendelea kuishi.

Ugonjwa huu unatibika kupitia dozi sahihi ya Hepatitis Ant-Viral uku ukizingatia lishe yenye manufaa kwa afya ya INI pamoja na seli zake, mazoezi na utumiaji wa matunda kwa wingi pamoja na mboga za majani.

Matibabu ya tatizo hili yanategemea pia na hatua ya tatizo lilipo fikia katika upande wa afya ya ini [Liver Demage] pamoja na wingi wa maambukizi, tatizo linaweza kuisha mapema na kupata chanjo ya kuzuiya kupata tena maambukizi ya virusi vya homa ya ini endapo utawai matibabu ya mapema kabla ya ini kufikia hatua mbaya ya kovu.

Sikuzote kovu la ini halitibiki na hii ndio sababu ya kwamba homa ya ini haina tiba unaweza ukatokomeza maambukizi na kupata chanjo lakini k**a ini tayari limesha kuwa na kovu inakuwa bado ni changamoto kwasababu kovu la ini ndio chanzo cha saratani ya ini:

๐—ž๐—ช๐—”๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ๐—ก๐—š๐—”๐—ง๐—œ๐—” ๐— ๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—”๐—•๐—จ ๐—ก๐—” ๐—Ÿ๐—œ๐—ฆ๐—›๐—˜ ๐—•๐—ข๐—ฅ๐—” ๐—ก๐—œ ๐—›๐—”๐—ง๐—จ๐—” ๐—ญ๐—” ๐— ๐—ฆ๐—œ๐—ก๐—š๐—œ - ๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—ž๐—” ๐—ž๐—จ๐—ง๐—ข๐—ž๐—ข๐— ๐—˜๐—ญ๐—” ๐— ๐—”๐—”๐— ๐—•๐—จ๐—ž๐—œ๐—ญ๐—œ ๐—ก๐—” ๐—ž๐—จ๐—˜๐—ฃ๐—จ๐—ฆ๐—›๐—” ๐—›๐—”๐—ง๐—”๐—ฅ๐—œ ๐—ญ๐—” ๐—ฆ๐—œ๐—ž๐—จ ๐—ญ๐—œ๐—๐—”๐—ญ๐—ข:

๐—ž๐—ฎ๐—ฟ๐—ถ๐—ฏ๐˜‚ ๐˜๐˜‚๐—ธ๐˜‚๐—ต๐˜‚๐—ฑ๐˜‚๐—บ๐—ถ๐—ฒ ๐—ธ๐˜„๐—ฎ ๐—ฐ๐—ต๐—ฎ๐—ป๐—ด๐—ฎ๐—บ๐—ผ๐˜๐—ผ ๐˜‡๐—ฎ ๐—ฎ๐—ณ๐˜†๐—ฎ ๐˜๐˜‚๐—ป๐—ฎ๐˜๐—ผ๐—ฎ ๐—จ๐—ฆ๐—›๐—”๐—จ๐—ฅ๐—œ ๐—ฉ๐—œ๐—ฃ๐—œ๐— ๐—ข ๐—ก๐—” ๐— ๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—”๐—•๐—จ *NAMBA 0692094104

24/11/2024

*VITAMIN C CHEWABLE TABLETS.*

๐ŸฅฐHii ni bidhaa mpya kabsa yenye radha ya chungwa na ni nzuri sana na mahususi kwa watoto, wajawazito, wamama wanaonyonyesha na watu wazima.

๐ŸฅฐIna vidonge 120 na 100mg, unaweza kutumia pamoja na chakula au bila chakula.

Idadi ya vidonge kwa siku;
๐Ÿ–๏ธMiaka 4-13 atumie 1.
๐Ÿ–๏ธMiaka 14-17 na mjawazito atumie 1-2.
๐Ÿ–๏ธAnayenyonyesha atumie 1-3.
๐Ÿ–๏ธMtu mzima atumie 1-5.
๐ŸฅฐNi bidhaa nzuri na tamu sana hata mtoto asiyependa kutumia vidonge ataipenda sana.

*FAIDA ZA KUTUMIA VITAMIN C CHEWABLE TABLETS KUTOKA BF SUMA*
๐Ÿ‘‰Inazuia na kutibu anemia.
๐Ÿ‘‰Inaongeza kinga ya mwili kwa kuziwezesha chembe cells nyeupe kufanya kazi yake kwa ufanisi wa hali ya juu.
๐Ÿ‘‰Inazuia kukak**a kwa cell za ateri.
๐Ÿ‘‰Ina antioxidant za kutosha kwa ajiri ukuimalisha cells na kuzuia cells zisiharibike.
๐Ÿ‘‰Inasaidia kuponesha vidonda haraka.
๐Ÿ‘‰Inazalisha collagen za kutosha ambazo ni proteins zinazoimalisha ngozi, mishipa ya damu na damu yenyewe, mifupa na cartilage.
๐Ÿ‘‰Inasaidia uchukuliwaji wa madini chuma mwilini(Iron absorption) a

Gout (au gouty arthritis) ni aina ya ugonjwa wa viungo unaosababishwa na kiwango kikubwa cha asidi ya uric mwilini, amba...
24/11/2024

Gout (au gouty arthritis) ni aina ya ugonjwa wa viungo unaosababishwa na kiwango kikubwa cha asidi ya uric mwilini, ambayo inajikusanya na kutengeneza madini ya urate kwenye viungo, hasa kwenye vidole vya miguu, magoti, au goti, na kusababisha maumivu makali, uvimbe, na joto kwenye eneo lililoathirika.

Sababu za Gout:

1. Kiwango cha Juu cha Asidi ya Uric: Asidi ya uric ni bidhaa ya kuvunjika kwa purine, ambayo ni dutu inayopatikana kwenye vyakula vya wanyama (k**a nyama nyekundu, samaki, na dagaa) na baadhi ya vinywaji (k**a pombe, hasa bia). Wakati asidi hii inavyozidi mwilini, inawezekana kutengeneza vidonda vya madini ya urate kwenye viungo, na kusababisha gout.

2. Uharibifu wa Uondoaji wa Asidi ya Uric: Wakati mwingine, mwili unakuwa na shida ya kutoa asidi ya uric, kutokana na matatizo ya figo au matatizo mengine ya kimetaboliki.

3. Magonjwa ya Msingi: Gout inahusiana sana na magonjwa k**a kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya moyo, na fetma, ambapo mtu ana kiwango cha juu cha asidi ya uric kwa sababu ya metabolic disorders.

4. Matumizi ya Vinywaji vya Pombe na Chakula: Vinywaji vya pombe, hasa bia, na vyakula vyenye purine nyingi k**a nyama nyekundu, samaki wa mafuta, na vyakula vya baharini, vinaweza kuongeza kiwango cha asidi ya uric mwilini.

5. Kujitahidi Kupunguza Uzito Haraka: Kupunguza uzito haraka au kufunga mlo kwa njia isiyo ya kawaida kunaweza kuongeza kiwango cha asidi ya uric kwa sababu ya kubomoa mafuta mwilini.

6. Vitu vya Kijeredi (Genetics): Gout inaweza kuwa ya kurithi, na watu wenye historia ya familia ya gout wana hatari kubwa zaidi ya kupata ugonjwa huu.

Dalili za Gout:

Maumivu Makali na Haraka: Gout kawaida huanza ghafla, na maumivu yanaweza kuwa makali sana, mara nyingi huanza usiku. Maumivu haya ni makali sana kwenye viungo, hasa kwenye vidole vya miguu (pamoja na sehemu ya goti).

Uvimbe na Joto: Sehemu iliyoathirika itakuwa na uvimbe mkubwa, na itakuwa na joto na ngozi nyekundu au yenye kung'aa.

Hali ya Kuumwa kwa Vidole au Viungo: Gout inaweza kuathiri vidole vya miguu, magoti, viwiko, au hata vidole vya mikono. Hali hii inaweza kubadilika na kutokea tena mara kwa mara.

Hisia za Uchovu na Maumivu ya Kudumu: Baada ya kushambuliwa na gout, mtu anaweza kujisikia uchovu na maumivu kidogo ya kudumu kwenye viungo.

Matibabu ya Gout:

1. Dawa za Kupunguza Maumivu na Uchochezi:

Nonsteroidal Anti-inflammatory Drugs (NSAIDs): Dawa k**a ibuprofen, naproxen, au diclofenac hutumika kupunguza maumivu na uchochezi wa gout.

Colchicine: Dawa hii husaidia kupunguza uchochezi wa gout na ina athari nzuri katika kutibu maumivu ya ghafla ya gout.

Corticosteroids: Dawa hizi zinaweza kutumika inapohitajika, hasa kwa watu ambao hawawezi kutumia NSAIDs au colchicine.

2. Dawa za Kupunguza Kiwango cha Asidi ya Uric:

Allopurinol: Hii ni dawa inayozuia mwili kuzalisha asidi ya uric. Inasaidia kupunguza maumivu ya gout na kuepuka madoa ya ugonjwa huu.

Febuxostat: K**a allopurinol, hii ni dawa inayosaidia kupunguza kiwango cha asidi ya uric kwenye mwili.

3. Badiliko la Lishe na Maisha:

Kupunguza Vyakula Vyenye Purine: Epuka vyakula vya wanyama vyenye purine nyingi (k**a nyama nyekundu, samaki wa mafuta, na mkaa wa baharini). Pia, epuka pombe, hasa bia.

Kunywa Maji Kwa Wingi: Kunywa maji mengi kusaidia mwili kutoa asidi ya uric kwa njia ya mkojo.

Kudhibiti Uzito: Kupunguza uzito wa mwili unaweza kusaidia kupunguza kiwango cha asidi ya uric mwilini na kupunguza shinikizo kwenye viungo.

4. Mazoezi na Matibabu ya Kudhibiti Magonjwa Msingi:

Kudhibiti Kisukari, Shinikizo la Damu, na Cholesterol: Hali hizi zinaweza kuchangia ongezeko la asidi ya uric, hivyo ni muhimu kudhibiti na kutibu magonjwa haya ili kupunguza hatari ya gout.

5. Kuepuka Kufunga au Kupunguza Uzito kwa Haraka: Jaribu kupunguza uzito kwa taratibu ili kuepuka kuongeza asidi ya uric mwilini kwa njia ya kubomoa mafuta haraka.

Vidokezo:

Matibabu ya mapema: Gout inaweza kuwa na madhara makubwa ikiwa haitatibiwa mapema. K**a mtu ana dalili za gout, ni muhimu kumwona daktari kwa uchunguzi na matibabu.

Kudhibiti Maumivu: Dawa za maumivu k**a ibuprofen na colchicine zinaweza kusaidia kupunguza maumivu ya haraka wakati wa mashambulizi ya gout.

Gout ni ugonjwa ambao unaweza kudhibitiwa kwa kubadilisha mtindo wa maisha na kwa matibabu ya dawa. Ikiwa ugonjwa huo unarudiarudia, daktari anaweza kupendekeza matibabu ya kudumu ili kuzuia mashambulizi ya baadaye.

Karibu afya njematz 0692094104 #

Mtu mwenye tatizo la kisukari (diabetes) ni mtu ambaye ana shida na usawa wa sukari (glucose) kwenye damu yake. Kisukari...
21/11/2024

Mtu mwenye tatizo la kisukari (diabetes) ni mtu ambaye ana shida na usawa wa sukari (glucose) kwenye damu yake. Kisukari ni ugonjwa unaotokea wakati mwili hauwezi kuzalisha insulini ya kutosha au hauwezi kuitumia ipasavyo. Insulini ni homoni inayosaidia sukari kuingia kwenye seli na kutumika k**a nishati.

Aina kuu za kisukari ni:

1. Kisukari cha aina ya 1: Hapa, mwili hawezi kuzalisha insulini kabisa, na hivyo mgonjwa lazima apokee insulini kila siku.

2. Kisukari cha aina ya 2: Hii ni aina ya kisukari ambapo mwili bado unaweza kuzalisha insulini, lakini seli za mwili hazitambui insulini vizuri (insulin resistance). Hii inaweza kusababisha kiwango cha sukari kwenye damu kuongezeka.

3. Kisukari cha ujauzito: Hii hutokea wakati wa ujauzito, ambapo mwili wa mjamzito hauwezi kuzalisha insulini ya kutosha.

Matatizo ya kisukari ni pamoja na:

Kupungua kwa uwezo wa mwili kuponya vidonda

Kuona kwa shida (mtazamo wa blurred)

Uchovu

Kikohozi kisichotibika

Mabadiliko kwenye uzito

Kudhibiti kisukari kunaweza kufanyika kwa mabadiliko ya mtindo wa maisha k**a vile kula chakula bora, kufanya mazoezi ya kawaida, na kutumia dawa au insulini kulingana na aina ya kisukari.

21/11/2024

Super discount

Maumivu ya mgongo yanaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, ikiwemo:1. Maumivu ya misuli: Kuinua vitu vizito au kufanya...
05/11/2024

Maumivu ya mgongo yanaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, ikiwemo:

1. Maumivu ya misuli: Kuinua vitu vizito au kufanya kazi kwa muda mrefu bila mapumziko.

2. Mjeredi: Ajali au kuanguka kunaweza kusababisha majeraha kwenye mgongo.

3. Matatizo ya diski: Kutoboka au kuharibika kwa diski za mgongo.

4. Arthritis: Uvimbe katika viungo unaoweza kuathiri mgongo.

5. Magonjwa ya mifupa: K**a vile osteoporosis.

6. Miondoko duni: Kuweka mwili katika mkao mbaya au kukosekana kwa mazoezi.

K**a una maumivu ya kudumu, ni vyema kutafuta ushauri wa kitaalamu.

โ€œKUNA UTOFAUTI GANI KATI YA KISUKARI AINA YA 1 NA AINA YA 02โ€.โ‡๏ธโ€Katika uainishaji wa ugonjwa wa kisukari kuna aina 4, l...
27/08/2024

โ€œKUNA UTOFAUTI GANI KATI YA KISUKARI AINA YA 1 NA AINA YA 02โ€.

โ‡๏ธโ€Katika uainishaji wa ugonjwa wa kisukari kuna aina 4, lakini kwa mazoezi inaelezwa k**a aina ya 1 au 2. Aina ya 1 kawaida hutokea kwa vijana chini ya umri wa miaka 30, ambao hawana historia ya kurithi ya ugonjwa wa kisukari.โ€Kwa kawaida hutokea kwa dalili kali.

โ‡๏ธโ€Aina ya kisukari cha 2 kawaida hutokea kwa watu wazima wenye umri wa zaidi ya miaka 40, kuhusiana na uzito mkubwa na ukubwa wa tumbo uliopimwa sentimita 80 kwa wanawake na sentimita 90 kwa wanaume.

โœ… Sukari wakati mwingine huhusishwa na shinikizo la damu na ini lenye mafutaโ€ kulingana na Josรฉ Agustรญn Mesa Pรฉrez, rais wa Chama cha Kisukari cha Amerika ya Kusini.

NI VYAKULA GANI VINAVYOSABABISHA UGONJWA WA KISUKARI!?

โ‡๏ธโ€Hapana. Hakuna chakula ambacho kinaweza kusababisha kisukari peke yake. Mkanganyiko huo unatokana na ukweli kwamba mtu wa kale alihitaji kuweka akiba ya nishati ili kuweza kuishi na alifanikisha hili kupitia njia za kuokoa insulini.โ€ Lakini kwa sasa nishati hiyo hiyo haitumiki na badala yake inaleta athari za kiafya baada ya kulimbikizwa kwa kutotumiwa.

โ‡๏ธโ€Kula mboga za kijani kibichi na matunda ya rangi tofauti inaweza kusaidia kusawazisha lishe na kuongeza kinga ya mwili ya asili ambayo husaidia kuzuia ugonjwa wa kisukari.โ€

โŒโ€kiwango cha juu cha mafuta, hasa k**a ya asili ya wanyama, pamoja na wanga rahisi na vyakula vya viwandani vinahusishwa na hatari kubwa ya kupata aina ya kisukari cha 2.โ€

SARATANI NI NINIโ‡๏ธ Miili yetu ina chembechembe hai nyingi ambazo huzaliana, hukua, na kufa kwa mpangalio maalumChembeche...
27/08/2024

SARATANI NI NINI
โ‡๏ธ Miili yetu ina chembechembe hai nyingi ambazo huzaliana, hukua, na kufa kwa mpangalio maalum
Chembechembe hizi zinapobadirika na kuanza kuzaliana na kukua katika utaratibu ambao sio wa kawaida ndio zinasababisha saratani.

โœ… Chembe chembe za Saratani hufuata mfumo huo usio wa kawaida โ€“ zinazaliana haraka zaidi bila mpangilio na kukua kwa haraka zaidi na wakati mwingine kuwa na umbile kubwa zaidi.
Chembechembe hizi za saratani zisipodhibitiwa/zisipotibiwa mapema zina uwezo wa kusambaa na kuota sehemu nyingine ya mwili wa mhusika โ€“

AINA ZA SARATANI
Saratani ni uvimbe unaojitiokeza mahala popote katika mwili wa binadamu, uvimbe huu hauna maumivu yoyote mwanzoni

โœ…Saratani zipo za aina nyingi sana na majina yake hutegemea kiungo kilichougua na aina ya chembechembe hai zilizoshambuliwa

Kiungo chochote chaweza shambuliwa, mfano
1.Shingo ya mfuko wa kizazi
2.Matiti
3.Ngozi
4.Koo na njia ya chakula Tumbo, utumbo, kongosho, ini
5.Kibofu cha mkojo na tezi dume
6.Mapafu ,ubongo,macho, mifupa,misuli
7.Matezi hasa kwa watoto
8.Damu
N.K.

NINI KINASABAISHA SARATANI / VIASHIRIA HATARISHI
โ‡๏ธHakuna sababu moja pekee ambayo husababisa saratani, bali ni mchanganyiko wa vitu vingi vinavyotuzunguka ikiwemo Viumbe hai, Kemikali, na aina ya maisha tunaishi kila siku.

โฉSaratani tofauti zina vyanzo vyake tofauti
Mfano:-

VISIVYOZUILIKA
Jinsia, umri, uwezekano wa kurithi mionzi ya jua??

VINAVYOZUILIKA
โ–ถ๏ธMatumizi ya kemikali au Mionzi
โ–ถ๏ธUvutaji wa sigara
โ–ถ๏ธMaambukizi ya baadhi ya vimelea :virus , bacteria, fangasi
โ–ถ๏ธMatumizi Makubwa ya pombe
โ–ถ๏ธMatumizi ya kemikali na mionzi
โ–ถ๏ธUlaji mbovu: mafuta mengi, nyama nyekundu kwa wingi n.k
โ–ถ๏ธKutofanya mazoezi
โ–ถ๏ธUnene uliokithiri
โ–ถ๏ธ*Madawa,sumu ya kuulia wadudu*
โ–ถ๏ธWasichana kuanza ngono katika umri mdogo

*KUSAFISHA MWILI KWA PROGRAM MAALUM MARA KWA MARA KUTASAIDIA SANA KUKUKINGA NA HII CHANGAMOTO

WAGONJWA WA KISUKARI WAPO KATIKA HATARI YA KUPATA SHAMBULIO LA MOYO.Takwimu zinaonyesha  Watu milioni 18 hufariki kutoka...
26/08/2024

WAGONJWA WA KISUKARI WAPO KATIKA HATARI YA KUPATA SHAMBULIO LA MOYO.

Takwimu zinaonyesha Watu milioni 18 hufariki kutokana na magonjwa ya moyo duniani.

Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababisha Ugonjwa wa moyo kwa kusababisha mkusanyiko wa utando wa lehemu kwenye mishipa ya damu.

Utando wa lehemu husababisha mishipa kuwa membamba na kupunguza mtiririko wa damu hali iitwayo Atherosclerosis au ugumu wa mishipa.

Kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye moyo kunaweza kusababisha msh*tuko wa moyo.

Na Ugumu wa mishipa unaweza kutokea katika sehemu nyingine za mwili pia.

Vilevile madhara yote haya yanayotokea kwenye moyo yanaweza yasiwe na dalili yoyote.

Lakini madhara yote haya yanaweza kugundulika na kupunguza hatari ya ugonjwa wa moyo k**a utafanya vipimo sahihi kwa wakati sahihi na kuchukua hatua stahiki.

Ukigundulika na ugonjwa wa kisukari ni vyema ukapata suluhisho la ugonjwa mapema kabla haujafikia kwenye madhara makubwa k**a haya.

Kwa ushauri na Tiba wasiliana nasi 0692094104

Address

Kigamboni

Telephone

+255692094104

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya yako na dr alexander posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya yako na dr alexander:

  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram