Tehelled Afya Kwanza 04

Tehelled Afya Kwanza 04 Tunatoa usharudi juu ya Afya ya Mwanaume

14/07/2023

Here’s what you can expect after drinking an ENERGY DRINK:

After : The caffeine first enters your bloodstream. Your heart rate and blood pressure start to rise.

In : The caffeine level peaks in your bloodstream. The stimulant starts to affect you, improving not only concentration, but also how alert you are.

In : All of the caffeine is fully absorbed by your body. Your liver also responds by absorbing more sugar.

In : Your body starts to experience a sugar crash and the effects of the caffeine begin to die down. You’ll start to feel tired and low-energy.

In : This is the half-life of the caffeine. In other words, it takes this much time for your body to reduce the content of caffeine in your bloodstream by 50 percent. Women on birth control pills require double the length for their body to reduce it.

In : The time that it takes most people to fully remove caffeine from their bloodstream, depending on their age and activity level.

In : Withdrawal symptoms kick in, including headaches, irritability, and constipation.

: Studies have shown this to be the time frame for your body to become tolerant to regular caffeine intake, making you feel the effects less.

“Energy drinks are fine in moderation and as part of a balanced diet,” the infographic concludes.

But registered -nutritionist Karen Ansel, co-author of The Calendar Diet: A Month by Month Guide to Losing Weight While Living Your Life, tells Yahoo Health that final statement is “way off target.” “My concern about energy drinks is people don’t drink them in the same way that they would drink a cup of coffee or tea,” she says.

Here’s why: Coffee and tea are both naturally bitter, so a person is more likely to sip (rather than chug) them as they might with an energy drink. That natural bitterness also tells your body when you’ve have enough, so you’re unlikely to end up in the emergency room from drinking too much coffee as compared with energy drinks.

“That doesn’t even include concerns about all the sugar and calories in energy drinks,” Ansel says. A 12-ounce can of Red Bull contains 110 calories and 27 grams of sugar, while a 16-ounce can of Monster Energy has 200 calories and 50 grams of sugar

TENDE NI NINI..? Ni tunda ambalo asili yake ni kutoka uarabuni asili ya uotaji wake ni katika Mazingira ya ukame yaani J...
12/07/2023

TENDE NI NINI..?
Ni tunda ambalo asili yake ni kutoka uarabuni asili ya uotaji wake ni katika Mazingira ya ukame yaani Jangwa.

Na izi zifuatazo ni miongoni mwa Faida za Tende Katika Miili Yetu.
1. Ukila tende mara kwa mara, mwili wako utapata aina mbalimbali za madini na vitamin za kutosha, ambazo zinapatikana kwenye tunda hili maarufu duniani. Katika tende kuna kiasi kidogo tu cha mafuta (fat) na haina lehemu (kolestrol).

2. Ukila tende, utajipatia kiasi cha kutosha cha protini na vitamin B1, B2, B3, B5, A1, na C, virutubisho ambavyo ni muhimu kwa ustawi wa afya ya mwili wako kwa ujumla.

4. Ukila tende, mwili utapata nguvu na kukuondolea uchovu ndani ya nusu saa tu, kwa sababu tende ina virutubisho vya sukari asilia k**a vile ‘glucose’, ‘sucrose’ na ‘fructose’. Ili kupata faida zaidi za tende,
changanya na maziwa fresh kisha kula.

5. Tende ina madini pia aina ya ‘potassium’ na kiasi kidogo cha chumvi (sodium). Madini haya husaidia uimarishaji wa mishipa ya fahamu. ‘potassium’ huweza kumuepusha mtu na kupatwa na kiharusi (stroke). Pia tende husaidia kupunguza lehemu (cholesterol) mwilini (LDL Cholesterol).

6. Kwa wale wenye matatizo ya ugonjwa wa kukauka damu mwilini (anemia), wanaweza kupata ahueni kwa kula tende kwa wingi ambayo ina kiwango cha kutosha cha madini ya chuma ambayo huhitajika katika utengenezaji wa damu mwilini. Wakati vitu vitamu vingine huozesha meno, utamu wa tende huzuia uozaji wa meno.

7. Kwa tatizo sugu na la muda mrefu la ukosefu wa choo, loweka tende za kutosha kwenye maji kiasi cha lita moja usiku kucha, kisha asubuhi changanya maji hayo pamoja na hizo tende ili upate juisi nzito, kunywa na choo kitafunguka na kuwa laini.

8. Kwa matatizo ya ukosefu wa nguvu za kiume, mchanganyiko maalum wa tende, maziwa, asali na unga wa hiriki vinaweza kuondoa tatizo lako. Chukua kiasi cha kiganja kimoja cha tende, loweka kwenye maziwa ya mbuzi kiasi cha lita moja na yakae usiku kucha.

Asubuhi, zisage tende hizo kwenye maziwa hayo hadi zichangayike, kisha weka asali kiasi cha vijiko vitatu au vinne vikubwa pamoja na unga wa hiriki, kiasi cha nusu kijiko kidogo. Kisha kunywa mchangayiko huo kila siku hadi utakapoona mabadiliko ya kuridhisha.

9. Tende ni dawa ya unene, kwa wale wenye matatizo ya wembamba wa kupindukia na wanataka kuongeza uzito, ulaji wa tende kila siku unaweza kuwasaidia. Lakini hii ina maana kwamba, wale wanaohitaji kupunguza uzito, ulaji wa tende kwa wingi hauwezi kuwafaa. Pia tende husaidia uondoaji wa kilevi mwilini.

10. Tende inatibu saratani ya tumbo. Habari njema kuhusu tende k**a tiba ni kwamba, haina madhara yoyote kwa sababu ni dawa asilia na inafanyakazi vizuri kuliko dawa za ‘kizungu’. Tende vile vile ina imarisha nuru ya macho na tatizo la kutokuona usiku (night blindness).

Tende ni tunda ambalo linayeyuka kirahisi tumboni na lenye faida nyingi sana ambazo hulifanya liwe tunda la kipekee. Tunda hili limezoeleka kuliwa wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ila sio mbaya ukapendelea kula wakati wote kwani linafaida nyingi katika mwili.

TENDE NI NINI..? Ni tunda ambalo asili yake ni kutoka uarabuni asili ya uotaji wake ni katika Mazingira ya ukame yaani J...
12/07/2023

TENDE NI NINI..?
Ni tunda ambalo asili yake ni kutoka uarabuni asili ya uotaji wake ni katika Mazingira ya ukame yaani Jangwa.
Katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, tende ndiyo tunda linaloliwa kwa wingi, pengine kuliko tunda lingine. Tende hutokana na Mtende yaani tende ni tunda linalopatikana katika mti uitwao mtende.

Je Ulaji wa Tende Una Faida Gani Katika Miili Yetu...?
Pamoja na kuwa ni tunda lenye ladha tamu na nzuri mdomoni, lakini kisayansi pia limethibitika kusheheni madini na vitamini lukuki, hivyo kuwa na faida nyingi kiafya

Na izi zifuatazo ni miongoni mwa Faida za Tende Katika Miili Yetu.
1. Ukila tende mara kwa mara, mwili wako utapata aina mbalimbali za madini na vitamin za kutosha, ambazo zinapatikana kwenye tunda hili maarufu duniani. Katika tende kuna kiasi kidogo tu cha mafuta (fat) na haina lehemu (kolestrol).

2. Ukila tende, utajipatia kiasi cha kutosha cha protini na vitamin B1, B2, B3, B5, A1, na C, virutubisho ambavyo ni muhimu kwa ustawi wa afya ya mwili wako kwa ujumla.

3. Ulaji wa tende huimarisha na kuboresha mfumo wa usagaji chakula tumboni, hivyo utaondokana na matatizo ya ukosefu wa choo, au matatizo ya kupata choo kigumu kinachosababisha maumivu wakati wa kujisaidia. Pia ndani ya tende kuna virutubisho vya ‘amino acids’ ambavyo ni muhimu mwilini.

4. Ukila tende, mwili utapata nguvu na kukuondolea uchovu ndani ya nusu saa tu, kwa sababu tende ina virutubisho vya sukari asilia k**a vile ‘glucose’, ‘sucrose’ na ‘fructose’. Ili kupata faida zaidi za tende,
changanya na maziwa fresh kisha kula. Unapojisikia mchovu, badala ya kunywa vinywaji baridi vinavyodai kuongeza nguvu, kula tende, hata kiasi cha punje tatu kinatosha. Kwa wafunga saumu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kufungua kwa kula tende ili kuurejeshea mwili wako nguvu iliyopotea siku nzima.

5. Tende ina madini pia aina ya ‘potassium’ na kiasi kidogo cha chumvi (sodium). Madini haya husaidia uimarishaji wa mishipa ya fahamu. Watafiti wamegundua kwamba ulaji kiasi wa ‘potassium’ huweza kumuepusha mtu na kupatwa na kiharusi (stroke). Pia tende husaidia kupunguza lehemu (cholesterol) mwilini (LDL Cholesterol).

6. Kwa wale wenye matatizo ya ugonjwa wa kukauka damu mwilini (anemia), wanaweza kupata ahueni kwa kula tende kwa wingi ambayo ina kiwango cha kutosha cha madini ya chuma ambayo huhitajika katika utengenezaji wa damu mwilini. Wakati vitu vitamu vingine huozesha meno, utamu wa tende huzuia uozaji wa meno.

7. Kwa tatizo sugu na la muda mrefu la ukosefu wa choo, loweka tende za kutosha kwenye maji kiasi cha lita moja usiku kucha, kisha asubuhi changanya maji hayo pamoja na hizo tende ili upate juisi nzito, kunywa na choo kitafunguka na kuwa laini.

8. Kwa matatizo ya ukosefu wa nguvu za kiume, mchanganyiko maalum wa tende, maziwa, asali na unga wa hiriki vinaweza kuondoa tatizo lako. Chukua kiasi cha kiganja kimoja cha tende, loweka kwenye maziwa ya mbuzi kiasi cha lita moja na yakae usiku kucha.

Asubuhi, zisage tende hizo kwenye maziwa hayo hadi zichangayike, kisha weka asali kiasi cha vijiko vitatu au vinne vikubwa pamoja na unga wa hiriki, kiasi cha nusu kijiko kidogo. Kisha kunywa mchangayiko huo kila siku hadi utakapoona mabadiliko ya kuridhisha.

9. Tende ni dawa ya unene, kwa wale wenye matatizo ya wembamba wa kupindukia na wanataka kuongeza uzito, ulaji wa tende kila siku unaweza kuwasaidia. Lakini hii ina maana kwamba, wale wanaohitaji kupunguza uzito, ulaji wa tende kwa wingi hauwezi kuwafaa. Pia tende husaidia uondoaji wa kilevi mwilini.

10. Tende inatibu saratani ya tumbo. Habari njema kuhusu tende k**a tiba ni kwamba, haina madhara yoyote kwa sababu ni dawa asilia na inafanyakazi vizuri kuliko dawa za ‘kizungu’. Tende vile vile ina imarisha nuru ya macho na tatizo la kutokuona usiku (night blindness).

Tende ni tunda ambalo linayeyuka kirahisi tumboni na lenye faida nyingi sana ambazo hulifanya liwe tunda la kipekee. Tunda hili limezoeleka kuliwa wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ila sio mbaya ukapendelea kula wakati wote kwani linafaida nyingi katika mwili.

Ugonjwa wa kisukari ni nini?Ni hali ambayo hutokea wakati sukari katika damu inapokuwa nyingi kupita kiwango cha kawaida...
30/06/2023

Ugonjwa wa kisukari ni nini?

Ni hali ambayo hutokea wakati sukari katika damu inapokuwa nyingi kupita kiwango cha kawaida kwa muda murefu.

Sukari hutumiwa na mwili ili kupata nishati-lishe. Ili mwili uweze kutumia sukari inayotokana na chakula huhitaji kichocheo (hormone) cha insulin. Kichocheo hiki hutengenezwa na kongosho (pancreas).

Kichocheo cha insulin ndicho kinachodhibiti kiwango cha sukari katika damu. Wakati kongosho linaposhindwa kutengeneza kichocheo cha insulin au insulini iliyopo katika damu inaposhindwa kufanya kazi kwa ufanisi husababisha ugonjwa wa kisukari.

Aina za Kisukari

Kuna aina mbili za kisukari:-

Kisukari kinachotegemea insulini (Type 1 diabetes): Hiki huwapata zaidi watoto. Katika aina hii ya kisukari, seli za kongosho zinazotengeneza insulin huwa zimeharibika na hivyo kusababisha upungufu au ukosefu wa insulini
Kisukari kisichotegemea insulin (Type 2 diabetes): Huwapata zaidi watu wenye umri kuanzia miaka 45 na kuendelea. Katika aina hii ya kisukari, insulini ya kutosha inaweza ikatengenezwa katika kongosho lakini haifanyi kazi na hivyo mwili kushindwa kutumia sukari kwa ufanisi.

Viashiria vya kupata ugonjwa wa kisukari

Mtu yeyote anaweza kupata kisukari, hata hivyo kuna mambo mengi yanayoweza kuongeza hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari. Haya tunaweza kuyaweka katika makundi kutegemeana na aina ya kisukari:

Kisukari kinachotegemea insulini (type 1 diabetes) sababu kubwa ni kurithi ugonjwa huo katika familia au magonjwa ya kongosho (k**a saratani-pancratic carcinoma au uambukizo-pancreatitis) ambayo huweza kuua seli zinazotengeneza kichocheo cha insulini. Kiashiria kikubwa hapa ni kuangalia historia ya familia kwa pande zote-baba na mama. K**a kuna historia hiyo basi unahitaji kuwa makini. Mambo mengine yanayoongeza hatari ya kupata aina hii ya kisukari kwa mtoto ni:
Mtoto kupewa maziwa mbadala (ya kopo au ya wanyama) au kumyonyesha mtoto kwa muda mfupi (mtoto anatakiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama mara baada ya kuzaliwa hadi miaka miwili au zaidi)
Mtoto akizaliwa na uzito mkubwa kupita kiasi (kawaida uzito wa kuzaliwa ni kilo 2.5 hadi 3.2)
Unene au uzito mkubwa utotoni
Mtoto akizaliwa na mama aliye na umri zaidi ya miaka 35

Kisukari kisichotegemea insulin (type 2 diabetes) huhusishwa kwa kiasi kikubwa na mtindo wa maisha usiofaa. Baadhi ya viashiria vya aina hii ni

Uzito uliozidi na unene uliokithiri
Shinikizo kubwa la damu
Mtindo wa maisha usiofaa husasan kutofanya mazoezi, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na uvutaji sigara na tumbaku
Umri zaidi ya miaka 45
Kuwepo kwa historia ya kisukari katika familia

Dalili za ugonjwa wa kisukari

Kukojoa mara kwa mara
Kusikia kiu sana
Kusikia njaa sana
Kujisikia mchovu wa mwili na kukosa nguvu bila ya kufanya kazi
Kupungua kwa uzito na mwili kuwa mdhaifu
Kutoona vizuri
Kusikia kizunguzungu
Kuwa na vidonda visivyopona haraka
Kufa ganzi kwa vidole vya miguu na mikono

Ukiona dalili hizi nenda kituo cha huduma ya afya upate ushauri na kupimwa ili kudhibitisha.

Madhara ya ugonjwa wa kisukari

Madhara ya muda mfupi: Kushuka kwa kiwango cha sukari katika damu (damu sukatiti au hypoglaycaemia) : Hali hii hutokea wakati kiwango cha sukari kinaposhuka kuliko kawaida kwa sababu ya kutumia dawa kuzidi kipimo, kufanya mazoezi bila kula au kutokula kwa muda mrefu na kunywa pombe bila kula chakula. Dalili za kushuka kwa kiwango cha sukari katika damu hujitokeza k**a ifuatavyo:

Dalil za awali

Kusikia njaa sana
Kuwa na hasira
Mwili kukosa nguvu
Kupungua uwezo wa kufikiri na
Kuchoka sana

Dalili za kati

Kutokwa jasho kwa wingi
Mwili kutetemeka
Moyo kwenda mbio
Kichefuchefu
Kuumwa kichwa
Kusikia kizunguzungu
Kuona vitu viwili viwili (double vision) na
Kuchanganyikiwa

Dalili za baadae

Kukata kaul
Hali hii ikizidi unaweza kupoteza fahamu na hatimaye kifo k**a hutapata matibabu mapema. K**a ukipatwa ha hali hii kula au kunywa kitu chenye sukari k**a sukari, glukosi, soda au juisi

Tahadhari: Mgonjwa aliyepoteza fahamu asipewe kinywaji au chakula. Anaweza kuwekewa glukosi kidogo kati ya shavu na fizi. Awahishwe hospitali haraka iwezekanavyo.

Kupanda kwa kiwango cha sukari katika damu (damu suziada au hyperglycaemia): Hali hii hutokea wakati kiwango cha sukari kinapokuwa juu kuliko kawaida baada ya kuacha kutumia dawa au unapoacha kufuata masharti ya ulaji, unapopata maambukizo au magonjwa k**a malaria, mafua, nimonia.

Dalili za kupanda kwa kiwango cha sukari katika damu ni

Kupumua harakaharaka
Kukojoa mara kwa mara hasa wakati wa usiku
Kuwa na kiu au kukauka koo
Kunywa maji mengi
Kutoona vizuri
Kuchoka bila sababu
Kizunguzungu
Mapigo ya moyo kwenda mbio
Kuchanganyikiwa
Kupungukiwa na maji mwilini
Kupoteza fahamu. Mgonjwa asipewe kitu chochote

Madhara ya muda mrefu:

Kupata mtoto wa jicho na upofu
Magonjwa ya figo
Kupata magonjwa ya kinywa na kung’oka kwa meno
Shinikizo kubwa la damu
Magonjwa ya moyo
Kufa ganzi na kupoteza hisia hasa mikononi na miguuni
Miguu na mikono kuchomachoma
Vidonda kutopona upesi na hatari ya kukatwa miguu
Kiharusi na kupoteza kumbukumbu
Kupungua nguvu za kiume au kukosa nguvu kabisa
Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake na
Kupata fangasi ukeni.

Kumbuka: Madhara ya muda mrefu huweza kuzuilika. Fata masharti unayopewa na daktari.

Chakula kwa wagonjwa wa kisukari

Kula mlo kamili
Kula vyakula vya nafaka k**a ulezi, mtama, uwele na mtama, uwele na dona, ngano na shayiri

Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya ...
19/06/2023

Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus. Kemikali ambayo ni acidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, k**a ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.

Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine k**a kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito.

AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO

Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)

Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric ulcers) – Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa
Gastric_Ulcer-1200x720

2. Vidonda vya utumbo mdogo (Duodenal ulcers) – Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu)
duodenal-ulcer

CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni;

Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)
Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu k**a asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)
Kuwa na mawazo mengi
Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi
Kunywa pombe na vinywaji vikali
Uvutaji wa sigara
Kuto kula mlo kwa mpangilio

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia na endelea kukuza tatizo, vidonda vya tumbo vinadalili k**a;

gastrita

Kupata maumivu ya tumbo yanayokuwa k**a ya moto (kuunguza) baada na kabla ya kula
Kupatwa na kiungulia karibu na chembe ya moyo
Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa
Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu
Kupata haja kubwa ya rangi kahawia au nyeusi yenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu
Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito
Kushindwa kupumua vizuri.

By Dr Emmanuel Danson
0744130256📞

KIHARUSI ( STROKE ) STROKE : hii Ni Hali ya mwili kupoteza uwezo wake wa kufanya kaz upande mmoja wa mwili wako.  Eidher...
18/06/2023

KIHARUSI ( STROKE )

STROKE : hii Ni Hali ya mwili kupoteza uwezo wake wa kufanya kaz upande mmoja wa mwili wako. Eidher kulia au kushoto na kwa kiwango kidogo watu wanapooza kiunoni kushuka chini na udhaifu huu hutokea pale ubongo wako kichwani unapokosa damu ya kutosha na hewa Safi ya oxygen , pamoja na virutubisho muhimu ambapo hupelekea cell's za ubongo wako kufa kwa haraka kwa kukosa oxygen

* 1: SABABU ZA KUPATA STROKE

_ kuziba kwaishipa yako ya damu kichwani kwasababu. Mbali mbali ikiwemo kuganda kwa damu
_ kupasuka mishipa ya damu kichwani na kupelekea damu ishindwe kufika katika ubongo

MAMBO YANAYOPELEKEA KUTOKEA KWA STROKE

_ uzito uliopitiliza au kuzidi
_ _ tatizo la preasure ile ya kupanda
_ colestrol mbaya kwenye mishipa ya Damu ( mafuta yasiyo yeyuka )
_ unywaji wa pombe uliopitiliza
_ utumiaji madawa kwa kipindi kirefu
_ kukaa bila kufanya mazoezi au kutojishughulisha Ni vitu baadhi ambavyo hupelekea eidher kuziba au kupasuka kwa mishipa yako ya damu kichwani na kupata stroke na hi ya kuziba mishipa ya Damu ndo iko kwa kiasi kikubwa ndo maana watu hawana pressure lakini wanapata

* MADHARA YA STROKE :
Upande mmoja wa uso kuckia ganzi
_ kushindwa kuongea na kupata tabu ya kuongea
_ kushindwa kuelewa na kupata tabu ya kuelewa kwa urahisi
_ mdomo kwenda pembeni
_ mkono au mguu wa upande mmoja kuwa mzito au kushindwa kuunyanyua
_ maumivu makali ya kichwani pamoja na kizunguzungu pia hata kutapika
_ kushindwa kuona vizur
Call 0744130256

Kula matunda ili mzunguko wa damu uwe vizuri mwilini
15/06/2023

Kula matunda ili mzunguko wa damu uwe vizuri mwilini

09/06/2023
Maambukizi Katika Mfumo wa Uzazi wa Mwanamke (PID yaani Pelvic Inflamatory Disease)    Maambukizi katika mfumo wa uzazi ...
07/06/2023

Maambukizi Katika Mfumo wa Uzazi wa Mwanamke (PID yaani Pelvic Inflamatory Disease)

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake. Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.

PID husababishwa na nini?

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

Je mwanamke huambukizwaje PID?

Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na

Kufanya ngono isiyo salama
Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango, na
Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.

Dalili za PID ni zipi?
Zipo dalili kadhaa za ugonjwa huu wa PID. Miongoni mwa dalili hizi ni

- Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu
- Kupata maumivu ya mgongo
-Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za siri. Utoko huu huambatana na harufu mbaya.
-Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
-Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa
-Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi
-Kupata homa
-Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
-Pia kutapika

Vipimo vya PID
Ili kuweza kutambua k**a mwanamke ameambukizwa ugonjwa huu, tabibu anaweza kufanya vipimo kadhaa vikiwemo

Kuchunguza mkojo ili kufahamu k**a mgonjwa ana mimba. Kipimo hiki ni muhimu hasa kwa mwanamke aliye katika umri wa kuzaa au mwenye uwezo wa kubeba mimba
Uchunguzi wa mkojo kwenye darubini ili kutambua aina za vimelea vinavyomletea mgonjwa uambukizi. Aidha mkojo huweza kuoteshwa katika maabara kwa ajili ya kutambua aina nyingine za vimelea viletavyo uambukizi huo.
Kupima damu kwa ajili ya kuchunguza jinsi aina mbalimbali za chembe za damu zilivyoathiriwa na uambukizi huo au k**a kuna mwingiliano na magonjwa mengine yaliyojificha. Kipimo hiki kwa kitaalamu huitwa Full Blood Picture.
Kuchukua utando unaozunguka shingo ya uzazi na kuuotesha kwa ajili ya utambuzi wa aina za vimelea viletavyo maambukizi hayo. Kipimo hiki huitwa cervical culture
Aidha ni muhimu pia kufanya vipimo vingine kwa ajili ya utambuzi wa magonjwa yaambukizwayo kwa njia ya kujamiiana, k**a vile virusi vya ukimwi na kisonono.
Mgonjwa pia anaweza kufanyiwa ultrasound ya nyonga ili kuangalia k**a kuna athari yeyote katika mfumo wake wa uzazi.

Matibabu
Mara mgonjwa anapogunduliwa kuwa ameathiriwa na ugonjwa huu, dawa za jamii ya antibayotiki huweza kutumika kwa ajili ya kuua vimelea vya ugonjwa. Hata hivyo ieleweke kuwa matumizi ya dawa hizi hufuata miongozo mbalimbali ambayo imewekwa na wizara au mamlaka za afya zinazohusika. Miongozo hii hutofautiana kati ya sehemu na sehemu au nchi na nchi, ingawa kiujumla Shirika la Afya Duniani (WHO) nalo limeweka muongozo wake kwa ajili ya kufuatwa na nchi mbalimbali.

Miongoni mwa dawa hizo ni pamoja na Cefotetan na Doxycycline; Clindamycin pamoja na Gentamycin; Ampicillin na Sulbactam kwa pamoja na Doxycycline; na Ceftriaxone au Cefoxitin pamoja na Doxycycline.
Ieleweke pia haishauriwi kujinunulia na kutumia dawa hizi bila kupata ushauri ushauri wa mtaalamu wa afya. Aidha ili kuondoa maumivu na kushusha homa, dawa k**a Paracetamol (Panadol) yaweza kutumika.

Jinsi ya kuzuia maambukizi katika mfumo wa uzazi

Kuna njia kadhaa za kuzuia maambukizi katika mfumo wa uzazi. Njia hizi ni pamoja na

Kufanya ngono salama kwa kutumia kondomu au k**a ikiwezekana kujizuia kabisa kufanya ngono.
Kuwahi kuwaona wataalamu wa afya mara dalili za ugonjwa huu zinapoanza kujitokeza au pindi tu unapogundua kuwa mwenzi wako ana dalili za magonjwa ya zinaa
Kufanya vipimo mara kwa mara hasa vya mfumo wa uzazi, pamoja na vipimo vya maambukizi ya magonjwa yanayosambazwa kwa njia ya ngono (STI).
Kutofanya ngono mara baada ya kujifungua, mimba kutoka au mara baada ya kutoa mimba ili kuhakikisha njia ya shingo ya uzazi imefunga vema.

 # # # # #  WAJUA FAIDA ZA MAZOEZI??? # # # # # # #Soma hizi faida 17 za kufanya mazoezi uboreshe afya na maisha yako.1....
07/06/2023

# # # # # WAJUA FAIDA ZA MAZOEZI??? # # # # # # #

Soma hizi faida 17 za kufanya mazoezi uboreshe afya na maisha yako.

1. Mazoezi hukufanya uchangamke na kuwa shupavu.

2. Mazoezi huboresha ufahamu wako, uwezo wa kuelewa na kufikiri mambo katika mazingira yanayokuzunguka.

Kujua zaidi: Soma Namna ya kutunza afya ya akili na mwili wako

3. Mazoezi huboresha uwezo wa ubongo kuhifadhi kumbukumbu.

4. Mazoezi hupunguza msongo wa mawazo.

Soma pia: Namna ya kupunguza msongo wa mawazo

5. Mazoezi huimarisha moyo hivyo huepusha maradhi yatokanayo na mapigo mabaya ya moyo. (Body exercise prevents and reduces cadiovasicular diseases)

6. Mazoezi humfanya mtu ajiamini kwa kupunguza stress, tension, wasiwasi n.k

7. Mazoezi hupasha mwili joto hivyo husaidia kuzuia na kupunguza baridi.

8. Mazoezi husaidia kuweka sawa kiwango cha cholesterol na mafuta yaliyopo mwilini. (Physical exercise burn more calories)

9. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa kisukari.

Kujua zaidi: Soma hapa Ufahamu ugonjwa wa kisukari (diabetes)

10. Mazoezi hushusha kupanda kwa shinikizo la damu. (high blood pressure)

11. Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata baadhi ya maradhi ya saratani. (Reduces risk of getting breast cancer and colon cancer)

12. Mazoezi humsaidia mtu kuondokana na baadhi ya matatizo ya akili.

13. Mazoezi huongeza hamu ya mtu kutaka kula.

14. Mazoezi hupunguza uzito wa ziada wa mwili na kufanya mwili wako kuwa mwepesi.

Unaweza soma pia: Njia 5 za kupunguza uzito wa mwili

15. Mazoezi huimarisha mifupa hivyo hupunguza matatizo yatokanayo na kudhohofika kwa mifupa jina la kitaalamu (osteoporosis)

16. Mazoezi huboresha kinga ya mwili.

17. Mazoezi husaidia kuweka sawasawa mifumo mbalimbali ya mwili. Mfano: mfumo wa ufahamu, mzunguko wa damu, homoni na misuli.

Hizi ni baadhi ya faida za kufanya mazoezi, yote ya yote mazoezi hurefusha maisha kwa kukufanya uwe mwenye afya njema. Ni vyema ukajiuliza, hivi ni kweli kufanya mazoezi na kula vizuri (vyakula bora) ni kuboresha maisha yako? Jibu ni NDIYO mazoezi na vyakula ni dawa pekee ya kutibu au kukuepusha na magonjwa mengi yanayoweza kuzuilika. Fanya mazoezi kuimarisha afya yako!

Here’s what you can expect after drinking an ENERGY DRINK:=================================================After  : The ...
07/06/2023

Here’s what you can expect after drinking an ENERGY DRINK:
=================================================

After : The caffeine first enters your bloodstream. Your heart rate and blood pressure start to rise.

In : The caffeine level peaks in your bloodstream. The stimulant starts to affect you, improving not only concentration, but also how alert you are.

In : All of the caffeine is fully absorbed by your body. Your liver also responds by absorbing more sugar.

In : Your body starts to experience a sugar crash and the effects of the caffeine begin to die down. You’ll start to feel tired and low-energy.

In : This is the half-life of the caffeine. In other words, it takes this much time for your body to reduce the content of caffeine in your bloodstream by 50 percent. Women on birth control pills require double the length for their body to reduce it.

In : The time that it takes most people to fully remove caffeine from their bloodstream, depending on their age and activity level.

In : Withdrawal symptoms kick in, including headaches, irritability, and constipation.

: Studies have shown this to be the time frame for your body to become tolerant to regular caffeine intake, making you feel the effects less.

“Energy drinks are fine in moderation and as part of a balanced diet,” the infographic concludes.

But registered -nutritionist Karen Ansel, co-author of The Calendar Diet: A Month by Month Guide to Losing Weight While Living Your Life, tells Yahoo Health that final statement is “way off target.” “My concern about energy drinks is people don’t drink them in the same way that they would drink a cup of coffee or tea,” she says.

Here’s why: Coffee and tea are both naturally bitter, so a person is more likely to sip (rather than chug) them as they might with an energy drink. That natural bitterness also tells your body when you’ve have enough, so you’re unlikely to end up in the emergency room from drinking too much coffee as compared with energy drinks.

“That doesn’t even include concerns about all the sugar and calories in energy drinks,” Ansel says. A 12-ounce can of Red Bull contains 110 calories and 27 grams of sugar, while a 16-ounce can of Monster Energy has 200 calories and 50 grams of sugar

=============================================*********Tupate Elimu Juu ya Faida za PARACHICHI*********==================...
07/06/2023

=============================================
*********Tupate Elimu Juu ya Faida za PARACHICHI*********
=============================================
Parachichi ni tunda ambalo mti wake hujulikana kisayansi k**a Persea amerikana. Tunda hili lina aminika kuwa na asili kutoka jimbo la Puebla, bara Amerika ya kusini kunako nchi ya Mexico. Ushahidi wa kale kabisa, takribani miaka 10000 BC umeonyesha parachichi lilitumika katika jimbo la Puebla nchini Mexico. Lakini kutokana na faida nyingi kiafya zipatikanazo kwa ulaji wa tunda hili, tunda hili sasa hupatikana na kutumika kwa lishe sehemu nyingi duniani hususani barani Afrika.

Parachichi ni tunda la pekee ukilinganisha na matunda mengine, kimsingi matunda mengine huwa yana wanga(carbohydrate) kwa wingi, wakati parachichi lina aina ya mafuta ambayo yana faida kwa afya.

Parachichi katika tafiti nyingi limeonekana kuwa na faida katika afya ya moyo. Wagonjwa wa moyo wamekuwa katika makatazo ya kutumia aina ya mafuta ambayo yamekuwa yakichangia kuongezeka kwa lehemu katika damu(mafuta hayo kitaalam k**a polysaturated fat), na kuongeza matumizi ya mafuta yasiyoongeza lehemu katika damu (monosaturated fat). Parachichi ni chanzo kizuri cha mafuta yasiyoongeza lehemu katika damu. Utafiti unaonyesha kuwa matumizi ya mafuta haya katika parachi hupunguza lehemu iliyo hatari ( kitaalam k**a, Low density lipoprotein), na huchangia katika ongezeko la lehemu isiyo hatari( High density lipoprotein).
Madini ya Potasiamu ni aina ambayo huwa watu hawapati ya kutosha kutoka katika vyakula. Parachichi lina kiwango kikubwa cha madini ya potassium kuliko ndizi. Tafiti mbalimbali zimeonyesha kuwa matumizi ya madini haya huambatana na kupungua kwa shinikizo la damu, shinikizo la juu la damu laweza kupelekea mtu kupata kiharusi, shambulizi la moyo hata figo kushindwa kufanya kazi.

Parachichi lina kiwango kikubwa cha fiba. Fiba ni kirutubisho kutoka katika vyakula vya jamii ya mimea, fiba huwa hazimeng’enywi tumboni lakini huwa zina umuhimu mkubwa sana, k**a kusaidia kupunguza uzito wa mwili, kusaidia urekebishaji wa kiwango cha sukari mwilini na kupunguza hatari ya kupata magonjwa mengi mwilini. Kuna aina fulani ya fiba ambazo huwa ni virutubisho kwa ajili ya bakteria wenye faida tumboni, hii huimarisha kinga ya mwili na kusaidia mwili kufanya kazi katika kiwango kinachotakiwa. Kwa kuwa parachichi lina kiwango kikubwa cha fiba, husaidia kuboresha mmeng’enyo na kupata choo katika hali ya kawaida.

Aina ya mafuta na virutubisho tulivyoviona awali katika parachichi vinasaidia afya ya ngozi yako. Husaidia ngozi yako kutokuwa kavu na kuwa na unyevu unaotakiwa na kuifanya ngozi kuwa laini na yenye afya. Vitamini C husaidia katika kusaidia uponaji haraka wa ngozi na kujijenga upya kwa seli za ngozi zilizoharibika,husaidia kujenga elastini na collageni ambazo ni muhimu katika ngozi. Uwepo wa virutubisho viondoavyo sumu(antioxidants) katika parachichi k**a carotenoidi na vitamini E, hutusaidia kutukinga na mionzi mikali ya jua, kwa hiyo huzuia makunyanzi katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuwa na mwonekano mzuri wakati wote.

Tunda hili ni lishe bora kwa wale wenye kisukari. Parachichi lina kiwango kidogo cha sukari ukilinganisha na matunda mengine. Pia uwepo wa mafuta aina ya ‘monosaturated’ husaidia kuboresha ufanyaji kazi wa homoni ya insulini, katika urekebishaji wa kiwango cha sukari mwilini. Faida nyingine ni kuwa Vitamini C katika parachichi husaidia kuimarisha mishipa ya damu na kuboresha kinga ya mwili ambayo ni faida kubwa kwa wagonjwa wenye kisukari.

Faida katika afya ya uzazi ni dhahiri. Parachichi lina Vitamini E ambayo ni “antioxidant” Potasiamu, Vitamini B6,Vitamini C ambazo hutusaidia kutukinga na magonjwa ya moyo hata yale ya kisukari. Chochote kile kinachosaidia afya ya moyo pia husaidia afya ya uzazi. Wanaume wenye magonjwa ya moyo na kisukari huwa tatizo kubwa la upungufu wa nguvu za kiume.

Parachichi pia limeonekana kuwa na faida nyingi katika kuboresha afya ya macho, viungo vya mwili na nyinginezo nyingi. Katika utafiti mmoja uko Marekani, ulionyesha kuwa watu walao parachichi walionekana kuwa na afya bora ukilinganisha na wale wasiokula parachichi. Waliokula parachichi hawakupatwa na matatizo ya mmeng’enyo ukilinganisha na wale wasiokula. Matatizo ya mmeng’enyo huchangia watu kupatwa na magonjwa ya moyo na kisukari.

Hapo ni kwa mafupi tu, Ila kwa ushauri Tuwe tunapendelea kutumia matunda mara kwa mara ili kuweza kupata faida za kiafya na kuboresha miili yetu dhidi ya matatizo madogo madogo ambayo yakikua yanakua ni makubwa na yasiyokua rahisi kuyakabili.
Ukienda sokoni usisahau parachichi aka Avocado.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tehelled Afya Kwanza 04 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Tehelled Afya Kwanza 04:

Share