BIBI CARE Tanzania

BIBI CARE Tanzania BIBI CARE seeks to improve livelihoods of the marginalised rural communities in Tanzania.

21/10/2024

Watch, follow, and discover more trending content.

RC Kagera azindua Kampeni ya "Wasitiri."- BIBI CARE kuja na taulo za k**e za migombaMKUU wa mkoa wa Kagera, Bi Fatma Mwa...
20/10/2024

RC Kagera azindua Kampeni ya "Wasitiri."

- BIBI CARE kuja na taulo za k**e za migomba

MKUU wa mkoa wa Kagera, Bi Fatma Mwassa, amezindua kampeni ya Wasitiri inayolenga kutoa elimu ya hedhi salama na kuhamasisha upatikanaji wa taulo za hedhi kwa ajili ya kuwasitiri maelfu ya wanafunzi wasichana nchini, ikianzia mkoa wa Kagera.

Kampeni hiyo inayotekelezwa na Shirika la BIBI CARE kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ilizinduliwa jana Jumamosi katika ukumbi wa KCU, mjini Bukoba katika tamasha la Huruma ya Mungu lililosheheni burudani ya kwaya mbalimbali kutoka nchini na nchi jirani ya Uganda.

Akizindua kampeni hiyo, Bi Mwassa alisema uhitaji wa taulo za k**e ni mkubwa kuliko inavyofikiriwa, kwani yeye binafsi aliwahi kufanya kampeni iliyotoa misaada ya shuka, vyandarua, sare za shule, viatu vya ngozi, soksi, madaftari, kalamu na taulo za k**e kwa wasichana wa shule za bweni, lakini alipowarudia kuhoji wamefurahia nini zaidi, wanafunzi wengi walitaja taulo za k**e.

"Yaani umempa binti shuka mbili, chandarau, sare za shule, viatu vya ngozi, soksi, madaftari na kalamu, lakini anakwambia amefurahia zaidi taulo za k**e. Hii inaashiria kwamba uhitaji wa taulo za k**e ni mkubwa zaidi kuliko tunavyofikiria," alisema Bi Mwassa.

Awali, Mwenyekiti wa BIBI CARE, Edward Kinabo, alisema kuwa katika awamu ya kwanza ya kampeni ya "Wasitiri," shirika hilo pamoja na wadau wake, wamejipanga kutoa elimu na kusaidia taulo za k**e kwa wanafunzi ili kupunguza tatizo la baadhi yao kukosa masomo kwa sababu ya kushindwa kujisitiri wakati wa hedhi.

Alisema utafiti wa UNICEF uliofanyika kwenye wilaya 19 nchini ulithibitisha kuwa asilimia 16.8 ya wanafunzi wa k**e wanakosa masomo wakiwa katika siku zao za hedhi, huku akiweka angalizo kuwa k**a ukifanyika utafiti mpana zaidi wa ngazi ya taifa basi huenda tatizo hilo likaonekana kuwa kubwa zaidi kuliko lilivyoonekana kwenye wilaya 19 zilizofanyiwa tafiti.

Akigusia awamu ya pili ya kampeni hiyo, Kinabo amesema ili kuhakikisha upatikanaji endelevu na nafuu wa taulo za k**e, BIBI CARE imejipanga kuwezesha vikundi vya wanawake na vijana kumiliki na kuendesha viwanda vidogo vya kuzalisha taulo za k**e za kutengenezwa kwa kutumia nyuzi za mgomba.

"Kagera mnalima ndizi. Tunakwenda kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Taulo za k**e za mgomba zitaleta fursa ya kutengeneza vipato kwa wakulima wa zao la ndizi na wakati huo huo tutakuwa tumechangia upatikanaji endelevu na nafuu wa taulo za k**e. Tutahakikisha taulo hizo zinakidhi viwango vya ubora na kupata ithibati ya TBS," alisema Kinabo.

20/10/2024

Rev. Dr. Fr. Faustine Kamugisha atafakari NJIA TATU ZA HURUMA!

20/10/2024

Before the launch of the # campaign on Saturday, the Choristers of St Michael did some practice in preparation for the morning mass on Sunday

Today, the Choristers of St. Michael from Ntinda Parish, Kampala Archdiocese, animated at high mass celebrated at the Bu...
20/10/2024

Today, the Choristers of St. Michael from Ntinda Parish, Kampala Archdiocese, animated at high mass celebrated at the Bukoba Cathedral in Tanzania, echoing to the Holy Father’s message of evangelizing to the whole world in all our catholic vocations. After mass, the Choristers had a photo opportunity and conversations with Rt. Rev. Bishop Jovitus Mwijage of Bukoba Diocese. The Choristers of St. Michael were in Bukoba to take part in the launch of the campaign yesterday, hosted by BIBI CARE and graced by Hon. Fatma Mwasa, the Regional Commissioner for Kagera. The campaign seeks to support 80,000 schoolgirls in 313 schools within the region in a bid to help them access safe menstruation. Other choirs were St John Bosco (Bukoba Cathedral Parish), Mt. Theresia wa Mtoto Yesu (Maruku Parish) and KKKT-Kandegesho (Karagwe Diocese). Many thanks to the Choristers and other stakeholders for taking this initiative seriously as part of their corporal works of mercy for the needy schoolgirls.

20/10/2024

IPOSA ni washirika wa BIBI CARE katika kampeni ya kwa ajili ya kusaidia wanafunzi 80,000 mkoani Kagera wapate hedhi salama. Wadau wengine wanakaribishwa. Tukiwa washirika wengi, huduma inafika haraka. Tazama na sikiliza maelezo katika video hii. Halafu CHUKUA HATUA!

Kampeni ya  , yenye shabaha ya kusaidia wanafunzi 80,000 wa sekondari mkoani Kagera ili wapate hedhi salama, ilizinduliw...
20/10/2024

Kampeni ya , yenye shabaha ya kusaidia wanafunzi 80,000 wa sekondari mkoani Kagera ili wapate hedhi salama, ilizinduliwa jana Mjini Bukoba. Mgeni rasmi alikuwa Fatma Mwasa, Mkuu wa Mkoa Kagera. Wanakwaya kutoka Kampala, Maruku, Karagwe na Bukoba walishiriki. Wanafunzi kutoka shule za sekondari Bukoba na Omumwani walishiriki. Zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo. Kampeni imezinduliwa. Sasa tuwawezeshe watoto hawa wapate hedhi salama. Ni jukumu tukufu.

Katika ngwe ya kwanza, tunakusanya michango kwa ajili ya wanafunzi wa Omumwani na Bukoba Secondary schools.

Tumia ukurasa huu kufikisha mchango wako kwa BIBI CARE.

Akaunti: CRDB: 0150975278001.
MPESA LIPA NAMBA: 35661938.

PLEASE JOIN US IN LAUNCHING THE WASITIRI CAMPAIGN FOR SAFE MENSTRUATION IN 313 SECONDARY OF KAGERA REGION, TANZANIA.
02/10/2024

PLEASE JOIN US IN LAUNCHING THE WASITIRI CAMPAIGN FOR SAFE MENSTRUATION IN 313 SECONDARY OF KAGERA REGION, TANZANIA.

Check out SK Media’s video.

09/08/2024

Female student challenges government and stakeholders in Tanzania to facilitate access to sanitary pads

SERIKALI NA WADAU SAIDIENI WASICHANA SHULENI KUPATA TAULO ZA K**E
09/08/2024

SERIKALI NA WADAU SAIDIENI WASICHANA SHULENI KUPATA TAULO ZA K**E

Watch, follow, and discover more trending content.

Address

House No. 137, Mwanjale Street, Uyole
Mbeya

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255623003438

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BIBI CARE Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to BIBI CARE Tanzania:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram