Afya ya Uzazi

Afya ya Uzazi Kiboko ya UTI sugu, Fangasi na PID sugu

JINSI YA KUTUMIA VIASHIRIA VYA HEDHI ILI KUTAMBUA UWIANO WA HOMONI ZAKO.Hapa chini nimeelezea uhusiano kati ya viashiria...
30/04/2022

JINSI YA KUTUMIA VIASHIRIA VYA HEDHI ILI KUTAMBUA UWIANO WA HOMONI ZAKO.

Hapa chini nimeelezea uhusiano kati ya viashiria hivi na homoni zako. Lengo langu ni kukuonesha namna ya kuusoma mwili na kuusikiliza pale unapoeda nje ya mstari. Mzunguko wa hedhi ni njia muhimu ya kuusoma mwili kuhusu uwezo wa kushika mimba.

1. Kukosa hedhi
Kukosa hedhi mara moja inaweza isiwe tatizo. Mpangilio wa homoni ni kitu sensitive sana na kinaweza kuathiriwa tu na msongo wa mawazo, lakini kwa kiasi kikubwa unaweza kujirekebisha wenyewe. Kukosa hedhi pekee siyo kiashiria kwamba hutaweza kushika mimba, manake yawezekana mayai yanatolewa(ovulation) lakini usipate hedhi. Kukosa hedhi kwa zaidi ya miezi 6 huitwa Amenorrhea na inaashiria kuna tatizo ambalo unahitaji kumwona Dactari haraka.

2. Period fupi
Mzunguko mfupi unaweza kuleta matatizo kwenye uwezo wa kushika mimba. Baadhi ya vihatarishi ambavyo hufupisha mzunguko wako ni k**a kukosa ovulation, upungufu wa virutubisho mwilini, uzito mdogo sana, upungufu wa damu .

3. Period ndefu
Mzunguko mrefu wa hedhi unaweza kuashiria kuvurugika kwa homoni na yai kutotolewa kwa yai kwenye kikonyo chake. Homoni ya progesterone ambayo hutolewa na mwili husaidia kuzuia bleed kuemdelea. K**a estrogen ni nyingi na progesterone ni kidogo bleed inaweza kuendelea kwa siku nyingi zaidi kuliko kawaida

4. Hedhi nzito na nyingi zaidi.
Kupata hedhi nzito na nyingi kupita kiasi husababishwa na ukuta wa uterus kusisimka zaidi kutokana na wingi wa estrogen, inapelekea ukuta kumomonyoka kupita kiasi. Tatizo hili linaweza kurekebishwa kwa kurekebisha lishe yako na kutumia tiba ya mimea kwa ajili ya kurekebisha homoni. Upungufu wa vitamin A na C inaelezwa kuchangia bleed nzito. unaweza kutumia Virutubisho k**a Multivitamin.

5. Hedhi kidogo inayoambatana na maumivu makali ya tumbo.
K**a unapata hedhi nyepesi, nyekundu inaweza kuashiria kwamba mzunguko kwenye mfuko wa mimba ni mdogo. Unaweza kupunguza hali hii kwa kufanya masaji kwenye eneo la tumbo ukitumia mafuta ya castor,ama kitambaa kilicholowekwa kwenye maji ya moto.

6. Hedhi ya damu nyekundu inayong’aa.
K**a hedhi yako inakuwa ni damu nyekundu inayong’aa basi hakuna tatizo endelea kufurahia hedhi yako.
Hedhi nzito yenye weusi ama brown
Hii inaonesha kwamba kuna masalia ya damu ya zamani kwa hedhi iliyopita. Kubaki kwa damu husababishwa na utokaji wa polepole sana na mzunguko mdogo ndani ya mfuko wa mimba. Unaweza kurekebisha tatizo hili kwa kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha, kufanya masaji eneo la tumbo.

7. Hedhi yenye damu mpauko na maji zaidi.
K**a unapata hedhi ya namna hii inaonesha kwamba damu yako kiujumla haina ubora na inakosa virutubishi muhimu. Kula lishe nzuri husaidia unaweza pia kutumia virutubishi vingine k**a Multivitamin na Spiriluna kuimarisha damu yako.

8. Kuganda kwa damu ya hedhi.
Kuganda kwa damu ya hedhi inaweza kuwa siyo jambo na kutisha ukilinganisha na kuganda kwa damu kwenye mishipa ya damu. Lakini yatakiwa kuendelea kufatitilia hedhi yako pia. K**a kuganda kwa hedhi yako kunatokea mara chache hasa mwanzoni mwa period, ni mabonge madogo madogo, yenye rangi nyekundu inayong’aa basi ni salama. Lakini k**a unapata mabonge mabubwa na inakuwa mfululizo basi yahitaji kumwona Daktari kupata ushauri. Unatakiwa kumwona Daktari haraka kwani kupata Damu nzito yenye mabongemabonge k**a unahisi unaweza kuwa na ujauzito yaweza kuashiria kwamba mimba imeharbika.Tumia maji ya kutosha na kufanya masaji eneo la tumbo kwa kutumia mafuta ya nyonyo (castor) ili kupunguza tatizo hili.

9. Kupata bleed kwenye kipindi kisichokuwa na hedhi.
Bleed katikati ya vipindi vya hedhi ni tatizo linalowachanganya sana wanawake. Yaweza kusababishwa na kuvurugika kwa mpangilio wa homoni (rejea maelezo yangu pale juu)Yai kutotolewa kwenye kikonyo chake(ovulation),
Uvimbe unaotokana na kukua kupita kiasi kwa tishu laini za ukuta wa uterus(endometriosis),Matumizi ya dawa za kupanga uzazi, Mazoezi magumu naLishe duni

10. Kukosa kabisa hedhi(Amenorrhea)
Inaweza kutatiza pale ambapo unashika ujauzito lakini hupati hedhi kabisa. Kuwa na mzunguko mzuri ni hatua ya kwanza katika kujua kwamba unaweza kushika ujauzito. Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kuchangia hedhi yako kuvurugika k**a msongo wa mawazo, lishe duni, uzito mdogo sana, kutumia vidonge vya kuzuia mimba, kuvurugika kwa homoni, umri kwenda (kukaribia menopause) na matatizo mengine ya kiafya.

▶️Sababu zinazoweza kusababisha ugumba kwa mwanamke:Karibu asilimia 10 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya mji wa uzazi...
14/01/2022

▶️Sababu zinazoweza kusababisha ugumba kwa mwanamke:

Karibu asilimia 10 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya mji wa uzazi usio wa kawaida (abnormal uterus).

➡️Hali zingine ni pamoja na uvimbe katika kizazi, kugandana au kunatana kwa mji wa uzazi na mirija ya uzazi.

Karibu asilimia 3 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya matatizo ya ute usio wa kawaida katika mlango wa kizazi (femaleís cervical mucus).

Ute ute huu unahitaji kuwa na hali fulani maalumu kwa mbegu za kiume kuweza kuogelea kirahisi katikati yake.

✔️Chanzo kikubwa cha tatizo hili ni usawa usio sawa wa homoni za k**e ambapo homoni ya uzazi ya k**e iitwayo ‘estrogen’ yaweza kuwa ni chache sana au homoni nyingine iitwayo ‘progesterone’ yaweza kuwa ni nyingi sana tofauti na inavyohitajika.

madini na vitamini zote mhimu kwa ajili ya kutungisha mimba k**a ifuatavyo;

1️⃣Vitamini B6

Kazi kubwa ya vitamini B6 ni kusaidia mimba kukaa sawa na salama wiki mbili za mwanzo tangu ujauzito utungwe (Luteal phase).

Hiki ni kipindi cha maandalizi cha kipindi kingine kijacho katika safari ya ujauzito na ni lazima mazingira yawe ya afya katika mji wa uzazi wa mwanamke ili kweli ujauzito uendelee kukua.

Hivyo siku hizi 14 za mwanzo vitamini B6 ni ya mhimu ili ujauzito ubaki na afya.

K**a huna hii vitamini vya kutosha basi hizi siku 14 hazitafika na ndani ya siku 7 au 10 ujauzito utakutoka.

2️⃣ Vitamini B12

Vitamini B12 ni vitamini mhimu sababu husaidia kuweka sawa homoni. K**a matokeo yake inakusaidia kupata siku zako vizuri na k**a siku zako zinaenda vizuri basi ni rahisi pia kwako kupata ujauzito wenye utulivu na afya bora ya mtoto.

Vitamini hii ni mhimu pia kwa baba kwani husaidia kumpa mwanaume mbegu nyingi na zenye ubora wa kutungisha mimba.

3️⃣ Vitamini C

Vitamini C imekuwa ikihusishwa na uzazi kwakuwa inasaidia kuweka sawa homoni na kukupa mzunguko mzuri wa hedhi vitu ambavyo ni mhimu ili uwe na afya ya kuweza kupata ujauzito.

Hii ni vitamini mhimu kwa kinamama ambao wamekuwa wakitumia dawa za uzazi wa mpango kwa kipindi kirefu. Husaidia mji wa uzazi uwe tayari na sawa kwa ajili ya kutunga ujauzito.

Vitamini hii inaisapoti homoni ya ujazi ijulikanayo k**a ‘progesterone’ katika mwili na kuimarisha kuta za mji wa uzazi baada ya mimba kutungwa.

4️⃣ Vitamini D

Upungufu wa Vitamini D umekuwa ukihusishwa na ugumba moja kwa moja.

Tafiti zinaonyesha upungufu wa vitamini D unaathiri tishu au ogani za uzazi za mwanamke kwamba ogani hizo haziwezi kufanya kazi kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya.

Vitamini D pia ina umhimu mkubwa katika kukua kwa seli na ufanyaji kazi wake. Tafiti zinaonyesha wanawake wenye vitamini D ya kutosha wanakuwa na mji wa uzazi mzuri na wenye afya.

5️⃣Vitamini E

Bila Vitamini E ni vigumu kupata ujauzito. Hii ni vitamini mhimu katika kulinda afya ya seli zetu na hufanya kazi ya kuondoa sumu mwilini na hivyo kuzilinda seli zisidhurike kirahisi.

Hii inajumuisha seli za mayai ya uzazi, kuta zinazozunguka yai zimetengenezwa kwa vitamini E.

Vitamini E pia husaidia kuweka sawa mbegu za mwanaume kwa kuongeza wingi na ubora wake kwa ajili ya uzazi.

6️⃣ Madini ya Folate

Kuwa na kiasi cha kutosha cha madini haya ni jambo la mhimu ikiwa unahangaika kupata ujauzito. Madini haya ni mhimu ili kuzuia ujauzito usitoke.

Ni mhimu mwili uwe na madini haya mapema wakati wowote unapojiandaa kushika ujauzito.

Ukisubiri mpaka upate ujauzito ndiyo uanze kutafuta haya madini tayari utakuwa umeshachelewa.

7️⃣ Madini ya chuma

Madini ya chuma yana uhusiano wa moja kwa moja na uzazi. Yanahitajika ili kuzizalisha homoni mbili mhimu za uzazi ambazo ni estrogen na progesterone, ambazo ni homoni mhimu kwa utungaji wa kawaida wa ujauzito.

Tafiti zinaonyesha wanawake wenye kiasi kidogo cha madini haya mwilini mwao wanapata wakati mgumu katika kushika ujauzito.

Mara tu upatapo ujauzito madini ya chuma ni ya mhimu sana ili kuwa na ujauzito wenye afya kipindi chote cha miezi 9.

8️⃣ Omega-3 na Omega-6

Haya hujulikana k**a mafuta mazuri (good fats). Kumbuka siyo kila mafuta ni mabaya kwa mwili wako, yapo mafuta mazuri na ambayo yanahitajika na mwili wako ili kuwa na afya bora.

Omega-3 na Omega-6 husaidia kuweka sawa homoni zako na kuzifanya zifanye kazi kwa usahihi jambo linalohamasisha uhakika wa kuwa na uwezo wa kutunga kwa mimba na kuwezesha damu kusambaa vizuri kwenye ogani za uzazi.

9️⃣Madini ya Selenium

Selenium ni madini madogo ambayo hufanya kazi k**a kiondoa sumu mwilini na hivyo kuimarisha ubora wa seli zetu.

Pia ni madini mhimu kwa ajili ya uundwaji wa mayai na hudhibiti kazi za tezi ya thyroid, tezi ambayo ni mhimu kwa uzalishwaji na uwekaji sawa wa homoni.

1️⃣0️⃣ Madini ya Zinki

Madini ya zinki ni mhimu kwa pande zote mbili kwa mwanamke na mwanaume. Kwa wanawake zinki husaidia uzalishwaji wa mayai na kuyaweka mayai yenye afya na kuweka sawa homoni.

Upungufu wa madini ya zinki pia unahusishwa na mimba kuharibika katika wiki za mwanzo mwanzo tangu kutungwa kwake.

Hivyo k**a umekuwa na bahati ya kupata ujauzito halafu haichukuwi muda zinatoka kuna uwezekano mkubwa una kiasi kidogo cha madini ya zinki kwenye mwili wako.

❌Vitu vya kuepuka kwa mtu mwenye tatizo la ugumba:

*Chipsi
*Vinywaji baridi
*Kaffeina
*Nyama nyekundu
*Vilevi

Feedback ya moto kabisa, watu wanaconcive, Je, umehangaika muda mrefu hupati mimba, suluhisho lipo🔥🔥🙏
15/10/2021

Feedback ya moto kabisa, watu wanaconcive,
Je, umehangaika muda mrefu hupati mimba, suluhisho lipo🔥🔥🙏

• KWA NINI HOMONI ZINAVURUGIKA?• MAMBO GANI TUKIYAFANYA HUWA TUNAVURUGA HOMONI ZA UZAZI....?•VITU GANI TUVIZINGATIE ILI ...
07/10/2021

• KWA NINI HOMONI ZINAVURUGIKA?

• MAMBO GANI TUKIYAFANYA HUWA TUNAVURUGA HOMONI ZA UZAZI....?

•VITU GANI TUVIZINGATIE ILI KUONDOA KERO ZA KUKOSA HEDHI KWA WAKATI ILI TUPATE UJAUZITO KWA MUDA TUNAOUTAKA...?

Karibu darasani....

Kwa bahati mbaya sana shule zetu za msingi hazina somo la endocrinology japo ni somo muhimu sana maana bila kuzifahamu vyema homoni, tunatumia pesa kubwa kutibu mambo ambayo unaweza kabisa kuyatatua ukiwa jikoni kwako.

👉🏾Sababu kubwa inayosababisha homoni kuvurugika ni Lishe Duni na ULAJI MBOVU (Mtindo Wa Maisha) usiofaa (hiki ndicho kiini kikubwa na ndio sababu ya kukualika katika kundi hili hili tupeane elimu kidogo kuhusu homoni)

Kile tunachokiingiza katika mwili wetu kwa kula na kunywa hicho ndicho kinajenga mwili au kuharibu mwili wetu iwe tunafahamu au hatufahamu.... (Sumu inaua tu iwe unajua ni sumu au umekunywa bahati mbaya itakuua tu) vivyo hivyo ulaji wetu ndivyo unafanya.

Katika Jamii na familia zetu tumeendekeza sana mtindo mbovu wa maisha ya kizungu katika ulaji na unywaji ila tumesahau kuiga mtindo wao wa mazoezi, kufanya vipimo mara kwa mara na kuzingatia kanuni bora za ulaji.

Unywaji soda, vyakula vya viwandani, vyakula vya wanga, vyakula vya kukaushwa kwa mafuta mengi, vyakula vya kisasa k**a mayai, nyama / samaki za kutunzwa kwenye makopo, uvutaji sisha na sigara, bia, pombe, vilevi n.k umekuwa utaratibu wetu wa mara kwa mara na kusahau kabisa ulaji wetu wa kawaida (Wa Kishamba) kitu ambacho kimefanya wadada wa kijijini wanaishi vizuri huku wadada mjini tunaishi kwa kutembelea hospital kila mwezi.

Umewahi kuambiwa na daktari wako kwamba punguza ulaji wa vyakula vya wanga na sukari nyingi?
👇🏿
KWA NINI TUNASEMA UPUNGUZE KULA WANGA NA SUKARI ILI KUWEKA HOMONI / UZAZI SAWA

Jamii haijui kwamba Vyakula vya Sukari na wanga Vinavuruga homoni, Vinakukosesha Hamu ya Tendo la ndoa, Vinakuletea Uvimbe kwenye Kizazi (Cyst na Pcos) mambo haya huwasababishia UGUMBA wanawake wengi sana:-

1. Mwili wa binadamu huwa unastahimili sukari kidogo sana. Inakadiliwa sukari tunaposema normal iwe Gram 5-10 kwenye Lita 5-7 za damu. Ambapo Inatakiwa isome 3-5mmol/L kwenye damu. Sasa Kwa lugha nyepesi ni sawa na kijiko 1-2 maana kijiko kidogo ni sawa na gram 5.

Jaribu kusoma kila kimiminika cha sukari unachokunywa. Mfano Soda 350mls inakisiwa kuwa na sukari gram 37 ukigawanya kwa 5 utapata vijiko 7.
Sasa Ukisuuza koo lako kwa soda baridi 2 utakuwa sawa na mtu aliyemba sukari vijiko 14. K**a kwa siku unakunywa soda 5 zidisha kwa 5 utakuwa umelamba vijiko 35 vya sukari. UPO HAPO...?

Mwili huwa unapata taabu sana Unapoupatia vijiko 35 kwa mkao mmoja angali sukari nyingine bado ipo na mwili unajiendesha vizuri. Hii inapelekea kongosho kuanza kupigana /kuishughulikia sukari hio kwa kumimina Insulin nyingi nyingi kadri unavyo mimina sukari.

2. Kadri unavyomimina sukari bila kujua, mwili wako haustahimili kiwango kikubwa cha sukari. Na kongosho linaendelea kupata shida kubwa kuisafisha kwenye damu haraka iwezekanavyo isilete uharibifu kwenye chembe nyekundu za damu (Ndio maana utakojoa sana baada ya kunywa vinywaji vyenye sukari). Itafikia hatua seli za mwili zinatengeneza njia ya kujikinga na sukari nyingi hali hio tunaita INSULIN RESISTANCE. Seli Za Mwili Zinaanza Kupuuza TAARIFA ZA INSULIN KUIAMURU SELI ITUMIE SUKARI. Hiyo ni Hatua za Awali za Kupatwa na Hormone Imbalances na Kisukari/Diabetes

3. Kiwango kingi cha Insulin kinachodumu muda mrefu (Hyperinsulinaemia) huenda kufubaisha Mishipa ya damu kwenye Moyo, Uume, Figo,Ubongo n.k. Lakini pia huenda kuathiri homoni za kiume na homoni za k**e pia.

4. Hali hiyo ikiendelea (Insulin resistance, Hyperinsulinaemia) huenda kufanya homoni za kiume testostorone zinashuka. Zikishuka mwanaume anakosa hamu na nguvu ya kushiriki tendo la ndoa. Mbali hivyo kwa mwanaume Homoni ya K**e (Estrogen) hupanda hii hupelekea mwanaume kuota matiti, hips zinakuwa k**a za mwanamke, na maumbile sehemu za siri yanapungua kabisa. (Kibamia)

K**a umejifunza, naomba Comment za kutosha Somo liendelee🙏❤️❤️

🌺 HOMON IMBALANCES🌺   Sasa mfumo wa uzazi huratibiwa nayafuatayo..Mzunguko wa hedhi ni mchakato tata unaohusisha mfumo w...
07/10/2021

🌺 HOMON IMBALANCES🌺
Sasa mfumo wa uzazi huratibiwa nayafuatayo..

Mzunguko wa hedhi ni mchakato tata unaohusisha mfumo wa uzazi na mfumo wa tezi. Tezi ndizo huratibu mzunguko huu.

Vichocheo viwili muhimu hutolewa na o***y ambavyo ni Oestrogen na progesterone.

OESTROGEN
Huwa na wajibu wa kuendeleza na kuimarisha ogani za uzazi za k**e na mabadiliko ya mwanamke yahusuyo uzazi, k**a vile :
• ukuaji wa matiti na
• mabadiliko ya mzunguko katika mfuko wa uzazi kwa kila mwezi.
Kuwepo kwa kichocheo hiki husababisha mwanamke kupata sifa za k**e k**a matiti, hedhi ama yai kupevuka, sauti na unawiri wa mwili, na kadhalika.

Endapo homon hii isipokuwa sawa basi huwezi kupata hedhi yako na ugumba ama hedhi kutoeleweka.

Kushuka kwa homoni ya 'estrogen' kabla ya kuingia kipindi cha hedhi kunaweza kuchangia uwepo wa maumivu ya kichwa, maumivu haya, mara nyingi hufuatana na kichefuchefu au bugdha kunako mwanga na sauti.

Baadhi ya wanawake hupatwa na maumivu ya kichwa kabla au wakati wa hedhi.

Maumivu haya yanayohusiana na hedhi huweza kutibiwa kwa njia za kawaida.

K**a huwa inakutokea Usishangae ni kawaida.

PROGESTERONE
Pia huratibu mabadiliko ambayo hutokea katika mfuko wa mimba wakati wa hedhi. Hutolewa na sehemu iliyobaki baada ya yai kutolewa (corpus luteum).

Hiki ni kichocheo muhimu katika kuuandaa mfuko wa mimba katika kubeba ujauzito, hivyo kukosekana kwa kichocheo cha progesterone huudhoofisha uandaaji wa mimba kutungwa, hivyo mimba hushindwa kutungwa kwa sababu ya kukosekana kwa maandalizi ya mfuko wa mimba.

Mwanamke anaweza akawa anapata hedhi vizuri lakini asibebe ujauzito kutokana na kukosekana kwa kichocheo kiitwacho progesterone.

K**a mimba itatungwa, placenta ndiyo hufanya kazi ya kutoa progesterone na kuendeleza mimba.

Pia progesterone hufanya kazi na estrogen katika kuandaa matiti(breasts) kutoa maziwa.

K**a matatizo ya mfumo wa hedhi yanakusumbua basi hakikisha unafika hospital na kupatiwa kipimo cha HOMON PROFILE ili kujua ni homon ipi iko juu sana au iko chini..

Niwatakie Asubuhi njema❤️❤️❤️

JINSI YA KUTUMIA VIASHIRIA VYA HEDHI ILI KUTAMBUA UWIANO WA HOMONI ZAKO.Hapa chini nimeelezea uhusiano kati ya viashiria...
06/10/2021

JINSI YA KUTUMIA VIASHIRIA VYA HEDHI ILI KUTAMBUA UWIANO WA HOMONI ZAKO.

Hapa chini nimeelezea uhusiano kati ya viashiria hivi na homoni zako. Lengo langu ni kukuonesha namna ya kuusoma mwili na kuusikiliza pale unapoeda nje ya mstari. Mzunguko wa hedhi ni njia muhimu ya kuusoma mwili kuhusu uwezo wa kushika mimba.

Kukosa hedhi

Kukosa hedhi mara moja inaweza isiwe tatizo. Mpangilio wa homoni ni kitu sinsitive sana na kinaweza kuathiriwa tu na msongo wa mawazo, lakini kwa kiasi kikubwa unaweza kujirekebisha wenyewe. Kukosa hedhi pekee siyo kiashiria kwamba hutaweza kushika mimba, manake yawezekana mayai yanatolewa(ovulation) lakini usipate hedhi. Kukosa hedhi kwa zaidi ya miezi 6 huitwa Amenorrhea na inaashiria kuna tatizo ambalo unahitaji kumwona Dactari haraka.

Period fupi

Mzunguko mfupi unaweza kuleta matatizo kwenye uwezo wa kushika mimba. Baadhi ya vihatarishi ambavyo hufupisha mzunguko wako ni k**a kukosa ovulation, upungufu wa virutubisho mwilini, uzito mdogo sana, upungufu wa damu .

Period ndefu

Mzunguko mrefu wa hedhi unaweza kuashiria kuvurugika kwa homoni na yai kutotolewa kwa yai kwenye kikonyo chake. Homoni ya progesterone ambayo hutolewa na mwili husaidia kuzuia bleed kuemdelea. K**a estrogen ni nyingi na progesterone ni kidogo bleed inaweza kuendelea kwa siku nyingi zaidi kuliko kawaida

Hedhi nzito na nyingi zaidi.

Kupata hedhi nzito na nyingi kupita kiasi husababishwa na ukuta wa uterus kusisimka zaidi kutokana na wingi wa estrogen, inapelekea ukuta kumomonyoka kupita kiasi. Tatizo hili linaweza kurekebishwa kwa kurekebisha lishe yako na kutumia tiba ya mimea kwa ajili ya kurekebisha homoni. Upungufu wa vitamin A na C inaelezwa kuchangia bleed nzito. unaweza kutumia Virutubisho k**a Multivitamin.

Hedhi kidogo inayoambatana na maumivu makali ya tumbo.

K**a unapata hedhi nyepesi, nyekundu inaweza kuashiria kwamba mzunguko kwenye mfuko wa mimba ni mdogo. Unaweza kupunguza hali hii kwa kufanya masaji kwenye eneo la tumbo ukitumia mafuta ya castor,ama kitambaa kilicholowekwa kwenye maji ya moto.

Hedhi ya damu nyekundu inayong’aa.

K**a hedhi yako inakuwa ni damu nyekundu inayong’aa basi hakuna tatizo endelea kufurahia hedhi yako.
Hedhi nzito yenye weusi ama brown
Hii inaonesha kwamba kuna masalia ya damu ya zamani kwa hedhi iliyopita. Kubaki kwa damu husababishwa na flow ya polepole sana na mzunguko mdogo ndani ya mfuko wa mimba. Unaweza kurekebisha tatizo hili kwa kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha, kufanya masaji eneo la tumbo na pia unaweza kujaribu fertility cleansing package yetu.
Hedhi yenye damu mpauko na maji zaidi.
K**a unapata hedhi ya namna hii inaonesha kwamba damu yako kiujumla haina ubora na inakosa virutubishi muhimu. Kula lishe nzuri husaidia unaweza pia kutumia virutubishi vingine k**a Multivitamin na Spiriluna kuimarisha damu yako.

Kuganda kwa damu ya hedhi.

Kuganda kwa damu ya hedhi inaweza kuwa siyo jambo na kutisha ukilinganisha na kuganda kwa damu kwenye mishipa ya damu. Lakini yatakiwa kuendelea kufatitilia hedhi yako pia. K**a kuganda kwa hedhi yako kunatokea mara chache hasa mwanzoni mwa period, ni mabonge madogo madogo, yenye rangi nyekundu inayong’aa basi ni salama. Lakini k**a unapata mabonge mabubwa na inakuwa mfululizo basi yahitaji kumwona Dactari kupata ushauri. Unatakiwa kumwona Dactari haraka kwani kupata Damu nzito yenye mabongemabonge k**a unahisi unaweza kuwa na ujauzito yaweza kuashiria kwamba mimba imeharbika.Tumia maji ya kutosha na kufanya masaji eneo la tumbo kwa kutumia mafuta ya nyonyo (castor) ili kupunguza tatizo hili.

Kupata bleed kwenye kipindi kisichokuwa na hedhi.

Bleed katikati ya vipindi vya hedhi ni tatizo linasowachanganya sana wanawake. Yaweza kusababishwa na kuvurugika kwa mpangilio wa homoni (rejea maelezo yangu pale juu)Yai kutotolewa kwenye kikonyo chake(ovulation),
Uvimbe unaotokana na kukua kupita kiasi kwa tishu laini za ukuta wa uterus(endometriosis),Matumizi ya dawa za kupanga uzazi, Mazoezi magumu naLishe duni

Kukosa kabisa hedhi(Amenorrhea)

Inaweza kutatiza pale ambapo unashika ujauzito lakini hupati hedhi kabisa. Kuwa na mzunguko mzuri ni hatua ya kwanza katika kujua kwamba unaweza kushika ujauzito. Kuna sababu nyingi ambazo zinaweza kuchangia hedhi yako kuvurugika k**a msongo wa mawazo, lishe duni, uzito mdogo sana, kutumia vidonge vya kuzuia mimba, kuvurugika kwa homoni, umri kwenda (kukaribia menopause) na matatizo mengine ya kiafya.

Mrejesho wa kibabe kabisa..., Wanaohangaika na homoni imbalance., Tiba ni rahisi sana na matokeo ni kwa muda mfupi
13/08/2021

Mrejesho wa kibabe kabisa..., Wanaohangaika na homoni imbalance., Tiba ni rahisi sana na matokeo ni kwa muda mfupi

Wanaofuatilia Masomo na Matokeo wanayaona Aseeh msichoke kujitibu na kuwa na imani Mungu atakupa kwa wakati sahihi, mire...
04/08/2021

Wanaofuatilia Masomo na Matokeo wanayaona Aseeh msichoke kujitibu na kuwa na imani Mungu atakupa kwa wakati sahihi, mirejesho yenu inanipa Nguvu sana, 🔥🔥🙏

02/08/2021

MAMBO YA KUZINGATIA UKITAKA KUSHIKA UJAUZITO;

1.hormone ziwe zimebalance

2. Usiwe na infection yoyote (UTI,FUNGUS & PID)

3.Mayai yako yawe na uwezo wa kupevuka na kuchevuka vizuri

4. Upate ute ute wa ovulation

5.Mirija iwe safi na wazi

6. Usiwe na uvimbe wa aina yoyote kwenye mfumo wa uzazi.

Kheri ya Mwezi wa Wakulima...❤️🙏

MVURUGIKO WA HOMONI (HORMONES IMBALANCE)Mvurugiko wa homoni kwa mwanamke huweza kuchangiwa kutokuwepo na usawa katika ho...
30/07/2021

MVURUGIKO WA HOMONI (HORMONES IMBALANCE)

Mvurugiko wa homoni kwa mwanamke huweza kuchangiwa kutokuwepo na usawa katika homoni zifuatazo Estrogen, Progesterone na Testosterone. Kupungua au kuzidi kwa homoni hizi kupelekea mvurugiko wa homoni kwa mwanamke.

DALILI ZA MVURUGIKO WA HOMONI

Mfumo wa homoni ni muhimu sana kwa afya ya ubongo na mili yetu. Husaidia kuzuia magonjwa yasiyo ambukizi kadri umri unavyo songa mbele. Baadhi ya dalili zinazoweza kuonekana kwa mtu mwenye changamoto ya mvurugiko wa homoni ni k**a vile:
• Ukavu ukeni
• Maumivu wakati wa tendo la ndoa
• Kutoa jasho usiku
• Maumivu chini ya kitovu wakati wa hedhi
• Upungufu wa hamu ya tendo la ndoa
• Mabadiliko ya siku za hedhi na kupata hedhi kwa muda mrefu unaozidi siku 7. (heavy bleeding, au kujaza pedi moja kwa saa moja)
• Kukosa hedhi kwa muda mrefu, na kutoa damu yenye mabonge mabonge wakati wa hedhi
• Uchovu wa mara kwa mara
• Hasira za mara kwa mara
• Kukosa usingizi
• Homa za usiku na Kizunguzungu cha mara kwa mara
• Mzio wa vyakula (Allergie), kuchagua chagua vyakula
• Ongezeko ya tumbo na nyama uzembe
• Kuharibika kwa ngozi (chunusi, vipele)
• Maumivu ya viungo
• Upungufu wa nywele kichwani.
• Kusahau sana (kukosa kumbukumbu)
• Kuwa na hamu ya kula vyakula au vinywaji vya wa ndani.
• Kupata hedhi wakati wa ujauzito (progesterone ikiwa imezidi)
• Kutokupata hedhi (balehe) adi umri wa miaka 20 na kuendelea
• Mwili kutokukua, kuonekana k**a binti mdogo, na kutokukua kwa via vya uzazi
• Msongo wa mawazo na kukosa kujiamini
• Kusinyaa na kupauka kwa
ngozi wakati wa siku za hedhi na wakati wa utumiaji wa njia za uzazi wa mpango
• Maumivu ya kichwa mara kwa mara
• Kuwa na tabia ya hamaki (kukosa utulivu)
• Kutokupata choo kwa wakati
• Misuli hudondoka

MADHARA
🌸 Mimba kuharibika mara kwa mara au Kukosa mtoto au Ugumba
🌸 Maumivu wakati wa tendo la ndoa
🌸 UTI (Urinary Tract Infection)
🌸 Kuziba kwa mirija ya uzazi
🌸 Uvimbe (Fibroids and Cysts)

Watu wanazidi kupona Fangasi Sugu kwa Formula Rahisi tu za Jikoni kwao
28/07/2021

Watu wanazidi kupona Fangasi Sugu kwa Formula Rahisi tu za Jikoni kwao

UDHAIFU WA MBEGU ZA KIUME: - K**a kila ukifanya tendo la ndoa, mwanamke anatoka shahawa/mbegu dakika chache mara baada y...
28/07/2021

UDHAIFU WA MBEGU ZA KIUME:
- K**a kila ukifanya tendo la ndoa, mwanamke anatoka shahawa/mbegu dakika chache mara baada ya kumaliza tendo la ndoa hata k**a hajasimama hiyo ni dalili mojawapo mbegu za kiume sio bora.

UBORA WA MBEGU ZA KIUME (S***M ANALYSIS).
- Kawaida kazi ya kuichunguzi wa UBORA WA MBEGU ZA KIUME hufanyika katika hospitali ambapo mbegu zako za kiume huchukuliwa na kisha kuchunguzwa na daktari mzoefu. Sote tunajua wazi ya kwamba unaweza fanya tendo la ndoa kila siku za hatari na bado usitungishe mimba. Tatizo linaweza kuwa kwa mama au baba au wote wawili. Tumesha yaelezea sana matatizo haya katika mada nyingi ziilizopita hapahapa. Kwa upande wa baba kuna wakati unaweza JITAMBUA K**A huna mbegu bora kutokana na muonekano wa manii/shahawa zako pamoja na kiasi cha shahawa kinachotoka katika kila tendo moja.

HAPA ILI UJIFUNZE MACHACHE
1- UWINGI WA MBEGU ZA KIUME: Mbegu za kiume katika kila tendo kamilifu moja linalofanywa zinatakiwa zisispungue milioni 40. Kiasi hiki sio rahisi kukijua kwa macho yako. Lakini ikiwa utatoa shahawa kidogo, kuna uwezekano wa kuwa na mbegu za kiume chache. Ingawa sio mara zote utoapo shahawa chache basi humaanisha una mbegu chache. Mshindo dhaifu au kufika kileleni kirahisi rahisi ni mojawapo ya dalili ya kwamba mbegu unazotoa sio nyingi, inaweza kuwa na maji mengi badala ya kuwa na mbegu nyingi.

2- UZITO WA MBEGU ZA KIUME NA UWEZO WA KUCHELEWA KUYEYUKA
– Shahawa/majimaji ya mbegu huwa na mbegu za kiume, na shahawa ni majimaji yanayobeba mbegu za kiume, kazi ya shahawa ni kusafirisha kwa usalama mbegu za kiume mpaka kulifikia yai. Sasa ikiwa shahawa zitakuwa nyepesi (zina yeyuka haraka) basi maana yake kwa haraka sana baada ya kutoka uumeni shahawa na mbegu za kiume zinatengana, na hivyo kuathiri uwezo wa mbegu kusafiri haraka na kulifikia yai. Mfano mdogo ni kwamba k**a ukishafanya tendo la ndoa na kisha muda huohuo mbegu za kiume kuanza kuchuruzika kutoka nje ya uke hata k**a mwanamke amelala basi hiyo ni dalili mojawapo ya mbegu kuwa nyepesi na hivyo kuweza kuathiri uwezo wa kutungisha mimba. Kunaweza kuwa na matatizo mengine ya uko kutoweza kushikilia vizuri mbegu za kiume pia, hiyo nayo inaweza kuwa sababu.

3- UWEZO WA KUOGELEA KWA KWENDA MBELE – Mbegu za kiume zenye afya bora zinakichwa kikubwa kilichochongoka na mkia mrefu unao anza mkubwa kichwana na kuishia mdogo kabisa mkiani, sifa hizi zinazipa mbegu uwezo wa wa kuogelea kwenda mbele katika mstari mnyoofu, ikiwa mbegu ya kiume itasafiri katika mstari wa zigzig au maumboumbo basi inapoteza uwezo wa kufika haraka kuliwahi yai. Hii ni kwa sababu zinachoka. Mbegu zinazoenda katika mstari mnyoofu zinawahi kufika kwa kuwa safari inakuwa fupi. Mfano mzuri ukisafiri na ndege toka Mwanza hadi Dar na Mwingine Asafiri na Train na mwingine na Basi utakuta wanafika muda tofauti na pia wanakuwa wamesafiri umbali tofauti kabisa. Ndivyo ilivyo kwa mbegu zinazoogelea kwa mwendo wa nyoka na zile zinazoogelea kwa kwenda mbele moja kwa moja

4- UWEZO WA KUISHI
– Mbegu bora inafaa iishi sio chini ya masaa 72 tangia itoke kwa mwanaume na kuingia kwa mwanamke, maisha mafupi ya mbegu yanaifanya mbegu kuwa na wakati mgumu wa kuliwahi yai ili kulitungisha mimba.

5- RANGI
– Kawaida shahawa zenye mbegu bora zina rangi nyeupe inayoelekea kwenye gray na kwa wazee inakuwa nyeupe inaelekea njano – Sasa huwezi ona rangi hii mara kwa mara kwa sababu mbalimbali za kiafya, chakula na hali ya hewa. Lakini kwa watu wazima miaka 40 kwenda juu ni kawaida sana mara nyingi kuonekana nyeupe/njano.

NINI CHA KUFANYA IKIWA UNAONA DALILI HIZI?
Ukiona dalili hizi au k**a umepima na kukutwa na dalili hizi, na ikiwa katika ndoa yako upatikanaji wa mimba imekuwa ngumu, na ikiwa pia mama mara kwa mara hujikuta na mbegu za kiume zinamtoka na kuchuruzika muda mchache mara baada ya tendo la ndoa basi tambua ya kwamba ubora wa mbegu zako ni mdogo na kwa iyo unahitaji utatuzi wake.

KWANZA BORESHA MBEGU ZAKO ZA KIUME kwa kula chakula chenye zinki kwa wingi mfano mbegu zote za matunda na maboga zinazolika, zina zinki na madini ya chuma kwa wingi. Hakikisha hukosi hizo mara kwa mara, ikiwa umeathirika zaidi au tuseme umetumia muda mrefu zaidi ya mwezi na huoni mabadiliko basi huna budi kupata dawa za hospitalini au kupata virutubisho na madini kutoka katika wasambazaji walio thibitishwa.

PILI ACHANA NA TABIA MBAYA ZINAZOWEZA KUWA SABABU YA MBEGU KUWA DHAIFU mfano ulevi wa kupingukia, sigara, madawa ya kulevya, punyeto, ngono kinyume na maumbile,kutokula chakula vizuri, madawa ya kulevya na kukosa kufanya mazoezi ya mara kwa mara.

HEDHI KUTOKA MABONGE MABONGE;    -Kuganda kwa damu wakati wa hedhi huonekana k**a jambo la kawaida kwakuwa ni hali tu il...
25/07/2021

HEDHI KUTOKA MABONGE MABONGE;
-Kuganda kwa damu wakati wa hedhi huonekana k**a jambo la kawaida kwakuwa ni hali tu iliyo katika sehemu ya mzunguko wa hedhi. Wanawake wengi, kwa mtazamo mwingine wakati wa mizunguko yao ya hedhi hushindwa kupitisha mabonge ya damu. Baadhi ya mabonge yanaweza kuwa makubwa yenye tishu nyeupe yakiambatana kwa pamoja katika mzunguko wa hedhi wa muda mrefu, yaani siku 8-14. Hali hii inaweza kujitokeza baada ya kuporomoka kwa mimba,
• lakini je, ni hali ya kawaida kwa mwanamke?



Mabonge ya damu hayakupaswa kumtokea mwanamke wakati wa hedhi. Hapo chini utaona mambo gani yanayosababisha damu kuganda wakati wa hedhi, na dalili gani zinazojitokeza, na je, unaweza kuzuiaje damu isigande wakati wa hedhi?



Je, Ni Kawaida Kuwa Na Mabonge Ya Damu Wakati Wa Hedhi?



Kwa asili, wanawake wengi huwa wanapatwa na hali hii ya mabonge wanapokuwa hedhini. Lakini hata hivyo, kuna mambo ambayo kwa kawaida huonyesha kuwa unaweza kuwa na mabonge wakati wa hedhi au la.
- Mambo yanayoweza kusaidia kubaini tatizo hili ni k**a yafuatayo:
• Uvimbe aina ya Fibroids
• Kizazi kuongezeka na kuwa kikubwa
• Uwezo wa misuli ya kizazi chako kusinyaa
• Uvimbe katika mlango wa kizazi


Vyanzo Vya Kuganda Kwa Damu Wakati Wa Hedhi;
- Kwanini mwanamke anatokwa na damu iliyoganda wakati wa hedhi?
• Na nini husababisha damu kuganda wakati wa hedhi?
🔴 Kwa ujumla, chanzo cha kuganda kwa damu wakati wa hedhi yako hutokana na kushindwa kwa kutoka kwa ute wenye kemikali unaozuia kugandanda kwa damu(anticoagulants) ili kuukinga ukuta wa kizazi usiharibike. Wakati wa hedhi, ute ute mzito unakuwa kwenye ukuta wa kizazi huanza kutoka. Ute huu unaokuwa na kemikali huanza kuachiliwa ili kuzuia damu isigande wakati wa hedhi. Wanawake wengi wanaotokwa na damu ya hedhi muda mrefu hutoka na damu yenye mabonge kwasababu damu inayotoka kwenye ukuta wa mfuko wa kizazi(uterus) hutoka kwa kasi kuliko ute wenye kemikali(anticoagulants) unazuia damu isigande. Hali hii ndio husababisha damu kuganda na hedhi kutoka na mabonge ya damu kwa muda mrefu.



1: Uvimbe Katika Kizazi(Uterine Fibroids)
- Uvimbe mmoja au zaidi ambao huwa sio salatani, kwa kawaida huota ndani ya kizazi cha mwanamke. Hata hivyo kwakuwa sio salatani, huwa havionyeshi kuwa vimetulia tu.
Dalili za kawaida anazozipata mwanamke mwenye uvimbe aina ya fibroids ni k**a ifuatavyo:
• Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
• Maumivu wakati wa tendo la ndoa
• Kutokwa na damu ya hedhi muda mrefu
• Tumbo kujaa gesi ama kukosa choo

Ikiwa k**a umewahi kuwa na dalili yoyote au zote nilizozitaja hapo juu, yafaa ukaenda hospitali haraka ili kufanya vipimo katika tumbo lako la kizazi. Daktari takuambia ikiwa k**a una tatizo la uvimbe kabla hujapata utaratibu wa matibabu.


2; Uzazi wa Mpango Pamoja Na Kutokwa Na Mabonge Ya Damu Wakati Wa Hedhi
- Mwili wa mwanamke umekuwa ukipokea vichochezi vya uzazi wa mpango kwa utofauti mkubwa sana, kwa mfano; vidonge vya uzazi wa mpango, nk. Kwa hali hiyo, wanawake hao wanapoingia hedhini hutokwa na damu kwa muda mrefu zaidi ya siku 8 na kuendelea.

Unaweza ukatambua kuwa unatokwa na damu ya hedhi nyingi kwa kuangalia idadi ya pedi unazobadirisha kwa siku. Ikiwa k**a unapaswa kubadirisha pedi zaidi ya mara moja kila baada ya masaa mawili au k**a mtiririko wa damu yako ya hedhi una mabonge makubwa ya damu yasiyokuwa ya kawaida, basi inamaanisha kwamba unatokwa na damu nyingi mno.

Endapo k**a utagundua kuwa mtiririko huo wa damu ulianza tu kipindi ulipoanza kutumia aina mpya ya vidonge vya mpango wa uzazi, basi unapaswa umweleze daktari wako akupe usahuri kuhusu jambo hilo.



3; Kuporomoka Kwa Mimba
- Kati ya asilimia 15-20 za ujauzito, mara nyingi huishia kuporomoka kabla haujafikisha wiki ya ishirini. Mabonge ya damu huwa ya kawaida sana wakati mwanamke mimba inapoporoka. Hata hivyo, k**a ukigundua kuwa ulitokwa na mabonge kwa kipindi cha mwezi mmoja, lakini yakaendelea mwezi uliofuata, basi usishangae kuona kuwa mimba iliporomoka, ikiwa pia k**a kuna mabadiriko badiriko kwenye mzunguko wako wa hedhi.



4; Kukaribia Kukoma Kwa Hedhi
- Hali ya kukoma kwa hedhi mara nyingi huambatana na kutokwa na mambonge mengi ya damu wakati wa kipindi cha hedhi. Hii ni hatua ambayo huonekana kabla ya kuanza kukoma hedhi(menopause). Mwanamke anapokuwa katika hatua hii, utagundua kuwa mwili wake utazarisha vichochezi(hormone) aina ya progesterone kwa viwango tofauti. Wakati uzazrishaji wa vichochezi(hormone) vya progesterone unapopanda na kushuka, viwango vya vichochezi(hormone) vya estrogen vitaanza kupanda na kufikia viwango ambavyo visingeweza kuchukuliwa taarifa hapo nyuma, na hali hii inaweza kusababisha kukua na kuvimba kwa tishu za ukuta wa kizazi.

Tishu za ukuta wa kizazi baadaye husababisha damu kuganda na kutokwa na damu nyingi muda mrefu wakati wa hedhi. Hivyo basi, naomba usishikwe na hofu kwakuwa umefikia hatua ya kukaribia kukoma hedhi. Endapo utaona hali ya mbonge ya damu sio ya kawaida, hakikisha kuwa unawahi hospitali kumuona daktari.



5; Mabonge Ya Damu Yasiyo Ya Kawaida
- Unapoona mabonge madogo ya damu iliyoganda wakati wa hedhi, chanzo chake kinaweza kuwa damu iliyoganda isiyokuwa ya kawaida. Magonjwa mbalimbali ya kuridhi yamekuwa yakifahamika kuwa yanaweza kumfanya mwanamke kupatwa na tatizo la kutokwa na damu muda mrefu. Kwa mfano, ugonjwa wa Von Willebrand, ni moja ya ugonjwa huo.

Unapokuwa na ugonjwa huo, siku zako za hedhi zinaweza kuwa nyingi
Siku zako za hedhi zinaweza kuambatana na vibonge vidogovidogo vya damu.
Mwanamke mwenye ugonjwa wa kurithi hujeruhiwa kwa urahisi sana. Kwa nyongeza, anaweza kupata tatizo la kutokwa na damu siku zote mara kwa mara, kwa mfano; damu kutoka kwenye fizi au puani, hali ambayo inaweza kuwa ya muda mrefu. Moja ya masomo ambayo wanawake wote wanahitaji kuyakumbuka ni kwamba, kadiri damu inavyozidi kuganda na kutengeneza mabonge ya damu mabaya, usiwe na hofu, yawezekana mabonge hayo yanakuonyesha jambo fulani kuhusiana na afya yako.



6; Maambukizi
• Aina ya kwanza ya maambukizi yanayoweza kusababisha hali hii ya kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi ni maambukizi katika via vya uzazi(PID). Maambukizi ya aina hii huathiri viungo vya uzazi kwa mwanamke, na k**a tatizo hili litaendelea bila kufahamika vizuri, basi linaweza kusababisha uharibifu mkubwa katika mfumo wa uzazi wa mwanamke

Address

Morogoro

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afya ya Uzazi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afya ya Uzazi:

Share