AFYA NI MTAJI

  • Home
  • AFYA NI MTAJI

AFYA NI MTAJI Lengo kuu la ukurasa huu ni kuweza kusaidia watu mbalimbali na kukumbushana mambo muhimu katka kuimarisha afya zetu

UJUE UGONJWA WA KISUKARI ( DIABETES )HABARI ZENU WADAUWA WA MAKALA ZANGU ? LEO nimeona ni VYEMA nizungumzie UGONJWA wa K...
15/02/2021

UJUE UGONJWA WA KISUKARI ( DIABETES )

HABARI ZENU WADAUWA WA MAKALA ZANGU ?
LEO nimeona ni VYEMA nizungumzie UGONJWA wa KISUKARI ( diabetes ) ambao ni UGONJWA unaosumbua WATU wengi katika JAMII .

UGONJWA wa KISUKARI hutokea wakati SUKARI katika DAMU inapokuwa nyingi kupita KIWANGO cha kawaida kwa muda MREFU .

SUKARI hutumiwa na MWILI ili kupata NISHATI LISHE.Kwa kawaida Ili MWILI uweze kutumia SUKARI inayotokana na VYAKULA unahitaji KICHOCHEO cha INSULIN.

INSULIN husaidia SUKARI kuingia kwenye CHEMBECHEMBE HAI ili kutengeneza NISHATI LISHE.

UGONJWA wa KISUKARI unasababishwa na KICHOCHEO hiki KUPUNGUA au KUTOFANYA KAZI k**a inavyotakiwa.Hivyo KIWANGO cha SUKARI kinabaki KIKUBWA kwenye DAMU kwa sababu SUKARI haikuwezeshwa kuingia kwenye CHEMBECHEMBE HAI za MWILI .
INSULIN ni KICHOCHEO kinachotengenezwa kwenye KONGOSHO na kwamba hutumika kusaidia MWILI kutumia SUKARI inayotokana na VYAKULA tunavyokula.

AINA ZA KISUKARI :-
Kuna aina MBILI za KISUKARI nazo ni:-
(¡)AINA ya KWANZA ni KISUKARI kinachotegemea INSULIN. Hii INSULIN ni aina ya HOMONI inayozalishwa na KONGOSHO ambapo KAZI ya INSULIN ni kurekebisha HALI ya SUKARI kwenye DAMU.
Ikiwa NYINGI inapunguzwa kurudi kwenye HALI ya kawaida. Na ikiwa CHACHE huruhusu irejee kwenye HALI ya kawaida pia.

Kunapokuwa na HITILAFU kwenye KONGOSHO likazalisha HOMONI hii kwa wingi.SUKARI hupungua MWILINI .
Au ISIPOZALISHWA,SUKARI huongezeka MWILINI .
HOSPITALI aina hii ya SUKARI inatibiwa kwa kutumia SINDANO za INSULIN na kurekebisha ULAJI wa VYAKULA.

(¡¡) AINA ya PILI ni KISUKARI kisichotegemea INSULIN. Hiki HOSPITALI hutibiwa kwa kutumia VIDONGE pamoja na kurekebisha VYAKULA peke yake.
WATU wengi walio na aina ya KISUKARI kisichotegemea INSULIN ni WANENE kupita kiasi na ikiwa WATAPUNGUZA UZITO kasi ya UGONJWA hupungua au KUISHA kabisa.

SUKARI inaweza kuwa JUU au CHINI kupita kiasi cha KIWANGO kinachotakiwa kutokana na CHANGAMOTO ya UZITO.

HALI zote hizo MBILI si NZURI kwa BINADAMU kwasababu MGONJWA anaweza KUFA HARAKA .
SUKARI inaweza kuwa JUU bila DALILI zozote zile kujitokeza MWILINI mwa MGONJWA .

MADHARA YA KISUKARI :-

WATU wenye KISUKARI wapo katika HATARI zaidi ya kupatwa na MAGONJWA yafuatayo;

- MAGONJWA ya MOYO .
- KIHARUSI (Stroke)
- Matatizo ya KUHARIBIKA kwa KIBOFU cha MKOJO.
- SHINIKIZO la juu la DAMU .
- UPOFU
- Kufa MISHIPA ya FAHAMU.
- UHARIBIFU katika FIZI na UGONJWA wa FANGASI .

MTU anapokuwa na KISUKARI mzunguko wa DAMU MIGUUNI hupungua na hii ndiyo SABABU KUBWA ya KUFA kwa NEVA za FAHAMU na hivyo MTU kukosa HISIA katika eneo la MWILI .

DALILI ZA KISUKARI:-

Baadhi ya DALILI za KISUKARI ni zifuatazo;

- KIU ya MAJI isiyoisha.
- NJAA Kali
- Kwenda HAJA NDOGO mara kwa mara
- VIDONDA au MICHUBUKO kuchukua MUDA mrefu KUPONA .
- NGOZI kuwa KAVU na KUWASHA .
- Kupoteza UZITO bila sababu.
- Kuwa na UKUNGU MACHONI .
- KUCHOKA kusiko kwa KAWAIDA.
- HISIA kupungua katika VIDOLE na VIGANJA MIKONONI na MIGUUNI .
- Kuwa na UKUNGU katika FIZI,NGOZI na KIBOFU cha MKOJO.
- Kukosa HAMU ya TENDO la NDOA na UUME kutokusimama.

Sasa basi kupitia UTENDAJI MZURI wa BIDHAA zetu ZISIZO na MADHARA yeyote MWILINI na ambazo ZIMEDHIBITISHWA na SHIRIKA la VIWANGO NCHINI pamoja na MASHIRIKA mbalimbali ya VIWANGO DUNIANI napenda nikudhibitishie kwamba TUNATIBU kabisa UGONJWA huu hadi kupelekea MTU kurudi katika HALI ya KAWAIDA na kufurahia MAISHA k**a WATU wengine

Dar es salaam -mikocheni , Mikoani tunatuma tibalishe

Piga au Whatsap
0621595018

_Tunaendelea....._ Pharm_golden.💉 *SARATANI  YA SHINGO  YA  KIZAZI (Cervical Cancer)*SEHEMU  YA  2.🍀Na PHARM  HASHIM..🌴📌...
15/02/2021

_Tunaendelea....._

Pharm_golden.💉 *SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI (Cervical Cancer)*

SEHEMU YA 2.🍀
Na PHARM HASHIM..🌴

📌.BAADHI YA DALILI ZA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

1.Kutokwa na maji maji au uchafu wenye harufu kali ukeni

2.Kutokwa na damu ukeni mbali na siku za mwezi au baada ya tendo la ndoa

3.Maumivu makali ya sehemu ya chini ya tumbo ( pelvic area)

4.Kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiana

5.Kupungua kwa uzito wa mwili bila kukusudia pia mkojo wenye matone ya damu.

📌.JE SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI HUTIBIKA?

📤.Saratani ya shingo ya kizazi yaweza kutibika iwapo itagundulika mapema.

📚.PAP TEST (PAPANICOLAOUS TEST); Pap- smear ni test ambayo hutumika kuchunguza mabadiliko ya chembe zilizo katika mlango wa kizazi ili kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo na hivyo kuwahi kuyakabili mapema.

📌.UMRI WA KUFANYA PAP TEST

📚.Test hii hushauliwa kwa wanawake wa umri wa miaka 21 hadi 65 na chini ya um ri wa miaka 21 endapo umeingia katika tendo la ndoa au kujamiana kwa kipindi kisichopungua miaka 3.

📌.KUPUNGUZA HATARI YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

🌹.Pap test

📚.Waweza kupata Pap test mara moja kwa mwaka au mara 1 kwa miaka 2-3, hii inategemea ushauri wa daktari, umri, hali yako ya afya kwa ujumla, na majibu uliyoyapata katika test zilizotangulia na mfumo wako wa maisha

🌹.Pata HPV Vaccine (hii yashauliwa kati ya umri wa miaka 12 hadi 26 chini ya mwongozo wa daktari)

🌹.Kuwa na mpenzi mmoja. Mahusiano ya kimwili na mtu mmoja hupunguza hatari za maambukizi ya magonjwa ya zinaa.

🌹.Tumia kinga (Condoms). Hii husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa.

MWISHO NA AHSANTENI….🙏🙏

15/02/2021

*📎.MARUDIO...💉💉*

*SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI ( Cervical Cancher )*

Pharm_golden💉 *SARgATANI YASHINGO YA KIZAZI (Cervical Cancer)*

SEHEMU YA 1.🍀
Na PHARM HASHIM..🌴

📕.Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani ambayo hutokea kutokana na mabadiliko ya mfumo wa chembechembe au cells zilizoko katika shingo ya kizazi. Mabadiliko haya hupelekea chembe chmbe hizo kushamiri na kuzaliana kwa kasi kinyume na mpangilio wa maumbile.

📖.Saratani ya shingo ya kizazi yasemekana ni saratani inayoongoza kwankusababisha vifo vingi vya wanawake katika nchi zinazoendelea
Report ya mwaka 2012 ya shirika la afya duniani WHO imesema kati ya matukio 75,000 ya waathirika wa saratani ya shingo kizazi barani Afrika, 50,000 walifariki dunia.

*📌.NINI KINACHOSABABISHA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI.?*

📚.Ripoti za utafiti wa kisayansi zimeafiki kuwa asilimia 99% ya saratani ya shingo ya kizazi hutoakana na maambukizi ya virusi vya” Human Papilomavirus” au HPV vilivyoko katika jamii a Papilomma. Baadhi ya virusi hivi vyenye aina zaidi ya mia moja huambukizwa kwa njia ya kujamiana

📌.BAADHI YA MAMBO YANAYOONGEZA HATARI YA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI.

1.Kushiriki tendo la ndoa katika umri mdogo au chini ya miaka 18

2.Kuwa na wenzi tofauti au mwenzi aliye na wapenzi tofauti

3.Utumiaji wa sigara kwani hupunguza nguvu ya kinga mwilini (Impairs immune system)

4.Watu wenye kinga hafifu ya mwili au wagonjwa k**a wenye Ukimwi

5.Uzazi wa mara kwa mara

INAENDELEA….👇👇.

Address

Mwenge

Telephone

+255621595018

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA NI MTAJI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA NI MTAJI:

  • Want your practice to be the top-listed Clinic?

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram