10/05/2026
Heri ya Siku ya Wanawake/Wamama Duniani kwa wafanyakazi wote wamama wa LUHETI. Taasisi inatambua na kuthamini mchango wenu mkubwa katika familia, jamii, na taasisi kwa ujumla katika kuleta ustawi wa taifa, hususan katika sekta ya afya na maadili.
Tunawapongeza kwa juhudi, upendo, uvumilivu, na kujitoa kwenu kila siku katika kuwalea, kuelimisha, na kuhudumia jamii. Mungu awabariki na kuwaongezea afya, hekima, na mafanikio katika majukumu yenu yote.