
28/09/2025
๐ ๐๐, ๐ญ๐ฎ๐ฆ๐๐ฉ๐ฎ๐ฎ๐ณ๐ ๐ฆ๐๐ฅ๐๐ณ๐ข ๐ฒ๐ ๐ฆ๐๐๐๐ข๐ฅ๐ข ๐ง๐ ๐ฎ๐ญ๐ฎ, ๐ค๐ข๐๐ฌ๐ข ๐๐ก๐ ๐ค๐ฎ๐๐๐ก๐ ๐ฏ๐ข๐ฃ๐๐ง๐ ๐ฐ๐๐ญ๐ฎ ๐ค๐ฎ๐ฆ๐๐ณ๐ฐ๐ ๐ง๐ ๐ฆ๐ญ๐ข๐ง๐๐จ ๐ฐ๐ ๐ฆ๐๐ข๐ฌ๐ก๐ ๐ฎ๐ฌ๐ข๐จ ๐ฐ๐ ๐๐ข๐๐๐ซ๐ข๐ค๐?
Jamii yetu leo inajivunia elimu bora kwa watoto โ vyeti, ufaulu na nafasi za ajira.
Mitandao ya kijamii na mwingiliano wa tamaduni za kigeni umeleta changamoto kubwa. Vijana wanashawishiwa kuamini kwamba ushoga na usagaji ni haki ya kibinadamu na sehemu ya uhuru wa kibinafsi.
Lakini je, hii kweli ni haki, au ni kuharibika kwa misingi ya mila na desturi zetu?
Kwa Nini Vijana Wanavutwa?
Matumizi mabaya ya teknolojia: Video, filamu na mitandao inawafanya waamini kila kitu kilichopewa jina zuri ni sahihi.
Malezi dhaifu ya kifamilia: Wazazi wanakimbizana na uchumi, wanasahau kuzungumza na watoto.
Upweke wa shule za bweni: Watoto wanakaa muda mrefu bila usimamizi wa karibu wa wazazi, wakijifunza tabia kutoka kwa wenzao.
Jamii isiyo na mshik**ano: Zamani kijiji kizima kilimlea mtoto, leo hii kila mtu yupo bize na maisha yake binafsi.
Tunapaswa Kufanya Nini?
๐จโ๐ฉโ๐ง Wazazi: Zungumzeni kwa uwazi na watoto juu ya changamoto hizi, badala ya kuwaachia mitandao iwafundishe.
๐ Walimu: Msijikite tu kwenye ufaulu wa mitihani โ tengenezeni nafasi za malezi ya kimaadili shuleni.
๐ค Jamii: Tukubali kwamba mtoto si wa familia moja tu. Lazima tushirikiane kumlinda.
๐ฑ Vijana: Tambueni kwamba si kila kitu kinachoitwa โhakiโ ni chema. Uhuru bila maadili ni mtego unaobomoa utu na heshima.
Kumbuka:-
โ๏ธ Elimu ni msingi, lakini elimu bila maadili inazalisha kizazi kisicho na mwelekeo.
๐ Swali kwako wewe mzazi, mlezi, mwalimu na kijana:
Je, tuko tayari kushuhudia kizazi chetu kikimezwa na mtazamo wa ushoga na usagaji unaoingizwa kupitia mitandao na tamaduni za kigeni, au tutasimama kulinda heshima na utu wa mtoto wa Kitanzania na Mwafrika?