RANIM SALIM.

RANIM SALIM. Kuelimishana, kukumbushana kuhusu mahusiano

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
05/10/2023

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Ikishindikana nyoka hata mjusi
04/02/2023

Ikishindikana nyoka hata mjusi

😨
04/02/2023

😨

07/10/2022
Habari yako mamy Naomba unipostie kwa wamama na wababa wanisaidie hii kitu Ina kazi gani kwa mwanaume na mwanamke naona ...
25/09/2022

Habari yako mamy Naomba unipostie kwa wamama na wababa wanisaidie hii kitu Ina kazi gani kwa mwanaume na mwanamke naona baadhi yao wanakula🀷

Watajua hawajui
20/08/2022

Watajua hawajui

Habari ndio hiyo wadau
10/05/2022

Habari ndio hiyo wadau

01/12/2021

Naomba unipostie kwa peji yako nipate maoni nipo na mahusiano yapata miez 8 na mme wamtu nanipo nae kwasababu alizoniolodheshea kutokana na mkewe ananipenda nampenda lakini nimekuja kwenu naombeni mawazo toa tumeanza mahusiano alinikuta Mimi ninabiashara zangu japo ndogondogo lakini zinaniweka mjini vitu nayeye anamishe zake lakini shida nihii yeye yuko bize mno kuonana kwetu nijion naikitokea tumeonana Mapema basi siku hiyo amemic shoo zakibabe ukimwomba elfu 20 anakupa elfu 10 ukiomba ela yakusukia atakwambia nyoa au nikutafutie naakiona umesuka kukusifia akuishi ukisimamishwa na mwanaume anaona wivu ukimwambia mamba niongezee mtaji anasema ntakutafutia Yani ajawahi to a Ella zaidi ya Elfu 10 naunakuta kwa wki Amekupa mala Moja au mala2 Nakazi anayofanya anaingiza hela yakutosha namambo yake yanaenda juzi nilimwomba ela yapedi kusudi akadai jion Naleta baht Maya akachelewa kulud akuleta nacku 2 akuleta nikampigia sm akupokea wiki ikakata akanipigia skupokea nikamsmc kuwa utakapomaliza ubize utanitafuta akujibu baada yacku 2 tukakutana seem Mona ivi tunaendaga kula akaanza kuniomba sm yang eti Nataka nione anaekupa kibulichakutopokea sm yang nikamnyima naapo Kuna SMS iliingia ya mwanaume mwingine akitema swaga skumpa cm akadai ninadharau lakini akaishia kuniomba msamaha sasa Jana nimekutana nae nimyonge mno kavaa nguo ovyo tu nakuusu wanawake sio mtu wamadem ata nywele ajachana niliumia kumwona ivo ila nikamchunia je nimludie au japo nampenda ila tunapishana kwenye matunzo

Nilimwambia nakaa kwetu Namimi nimepanga ila akisema anakuja kunisalimia natokea nyumbani manana nilipopanga simbali nakwamdogo

11/10/2021
KISASI CHA WACHAWISEHEMU YA ( 8 )ILIPOISHIA,,,,  Nusu kati yao walikuwa ni warefu  sana, wanakaribia kimo cha mnazi.  We...
11/10/2020

KISASI CHA WACHAWI
SEHEMU YA ( 8 )

ILIPOISHIA,,,,

Nusu kati yao walikuwa ni warefu sana, wanakaribia kimo cha mnazi. Wengine waliobakia walikuwa ni wafupi mfano wa mbilikimo waishio katika msitu wa nchi ya Kongo, ilikuwa pengine yapata saa nane hivi usiku.

INAENDELEA,,,

Kwa makisio ya haraka haraka watu hao wa ajabu walikuwa wanaelekea hapo kwenye mwembe ambako ndiko nilikojibanza ili kuwapisha wapite. "Mama yangu weee,, hee,! Wanakuja huku, hivi wakiniona hapa usiku huu si itakuwa balaa kubwa sana kwangu ?

Nikajiambia moyoni,,,.

Watu hao walikuwa wakiimba wimbo ambao hata mie niliusikia mtamu huku wakicheza na kuruka ruka, k**a vile ngoma ya kabila la kimasai. Wahenga walisema "tembea uone". Lakini mie sikutembea kwa hiari yangu, pamoja na kwamba ni kweli nimeyaona.

Nikasikiliza kwa makini wimbo waliokuwa wanaimba huku baadhi yao wakiitikia. "Tuwapeleke, tuwapeleke hao kwenye makao yetu. Chaaa chaaa chaaaa!! "Tuwapeleke, tuwapeleke hao kwenye makao yetu. Chaaa chaaa chaaa!!. Wengine walikuwa wanaimba. Tuwapeleke, tuwapeleke hao, baadhi yao walikuwa wakiitikia chaaa, chaaa, chaaaa!!!

Sasa pamoja na woga niliokuwa nao nikautafakari na kuuchambua huu wimbo ulioonekana dhahiri kuwakolea mno k**a vile wale waupendao muziki wa taarabu ama reggae au bongo fleva. Kwanza nikalitafakari hili neno "tuwapeleke", nikajiuliza ni akina nani kati yao wanapelekwa ?

Kisha nikalichambua neno "kwenye makao yetu". Nikajiuliza, jee, wanawapeleka wapi huko ambako ndiko kwenye maskani yao ? Pamoja na kuwaza nikashindwa kupata jibu. Watu hao walipoukaribia huu mti wa mwembe nami ndivyo nikazidi kuoatwa na mfadhaiko. Kuna wakati niliamua nitoke mbio, lakini nafsi ikanizuia.

Kwanza nikajiuliza nikimbie, nikimbilie wapi na wakati watu hao tayari wameshafika hapo nilipokuepo. Jambo lililonitia tashtit i zaidi kufanya nishindwe kuondoka hapo mtini haswa nikikumbuka maneno aliyoniambia bibi kizee kuwa watu wabaya hawatoweza kunidhuru kamwe, nikajipa ujasiri japo sio sana.

Nikahisi kuwa hao ndio watu wazuri, watu hao machoni mwangu niliwaona ni wa ajabu sana, walipofika kwenye huu mti wa mwembe ambao ndipo nilipokuwepo nikajibanza. Waliuzunguka mti huo ili hali wakiendelea kuimba, niliona ajabu mie nilipokuepo hapo, lakini sikuona wakunishtukia bali waliendelea na ngoma yao wakiicheza na kuuzunguka mti huo.

"Au yule bibi aliniambia kweli kwamba watu wabaya hawataniona ?" Kidogo nilianza kupatwa na imani. Ghafla k**a dakika tato hivi, nikaona wameisimamisha ngoma yao, na watu wanne kati yao wakaitana chemba.

Niliwasikia wakizungumza kwa sauti ya chini, "hapa leo hapafai kabisa tuondokeni", walinong'onezana. Nikahisi kuwa hao huenda ndio wakubwa wa kundi hilo. Mmoja kati yao nilimsikia akiuliza, jee, kwa nini anasema hapa hapafai ?

"Ndio nasikia harufu mbaya kwa vyovyote kuna kitu sio kizuri hapa chini ya mwembe au juu" akajibiwa. Nikashusha presha, nikagundua kuwa kwa vyovyote dawa ya kunywa na kupaka aliyonipa bibi imefanya kazi yake kiusahihi. Kwa sababu wao niliwaona laivu mambo yote waliyokuwa wakifanya , lakini inaonyesha kwamba wao hawakuniona kabisa.

Ila huenda walihisi kwamba mahala hapi siku hiyo palikuwa "pazito" sikuelewa ni kwa nini, lakini nikaona kwamba hiyo ndiyo heri yangu. Baada ya dakika chache tuu walipatana waote waondoke mahala hapo na kuendelea na safari yao.

Safari hii waliondoka kimya kimya bila wimbo waliokuwa wakiuimba walipokuwa wanakuja. Nikawashuhudia wakitokomea zao, hatimae wakatoweka machoni mwangu.

ITAENDELEA,,,

BY RANIM,,

KISASI CHA WACHAWISEHEMU YA ( 7 )ILIPOISHIAKwa swali hili nikamuona huyu bibi anakuna kichwa chake kilichozingirwa na mv...
06/10/2020

KISASI CHA WACHAWI
SEHEMU YA ( 7 )

ILIPOISHIA

Kwa swali hili nikamuona huyu bibi anakuna kichwa chake kilichozingirwa na mvi! "Ni swali zuri sana" ! Akatamka na kuendelea. "Utakapokaribia huko unakotaka kwenda, basi itakutokea ishara, akanijuza bibi.

INAENDELEA

"Ishara ipi hiyo ?"
"Kwanza utaona msitu umekwisha na umeingia katika maeneo ya mashamba yanayolimwa na watu, hiyo ni dalili ya kwanza ambayo ndio muhimu, zingatia utagundua tuu haina haja kukujulisha zaidi. "Akanieza."

Sikutaka kumuuliza maswali zaidi bali nikachukua zile shuka nyeupe na kuzitumbukiza ndani ya ule mfuko. " Basi mjukuu wangu" endelea na safari yako, na nnakutakia mafanikio mema. Sote tukanyanyuka na kupeana mkono wa kwa heri. "Nenda, ila hautoniona tena japokuwa unaweza kutokewa na mtihani kadhaa njiani, mengine ni ya kutisha zaidi. Akanifahamisha kisha akaondoka kutoweka msituni. Nikamwangalia hadi akatoweka kabisa machoni mwangu.

Mapigo ya moyo wangu yalinienda mbio kwa wasi wasi, hasa kila nilipokumbuka maneno yake ya mwisho aliyonieleza kuwa huko njiani naweza kukutana na mambo mengine na mengine ni ya kutisha zaidi. Swali ambalo nilihofia kumuuliza ni kwamba, jee safari hiyo isiyojulikana ninakokwenda itachukua siku ngapi na huko nifikiapo ni kwa nani ? Lakini nikaomba mungu niuvuke salama msitu huo mnene.

Haikunichukua muda mrefu baada ya kuagana na yule bibi kizee, nami nilianza tena "kukata mbuga" nikaenda hadi kijua kikazama na kuashiria kwamba usiku mwingine unaingia. Niljihisi kuchoka, hivyo nikaamua nijipumzishe tena. Kwa kukisia ilikuwa inakaribia saa moja hivi usiku.

Safari hii niliukata mti wa mzambarau hapo ndipo niliweka kambi ya muda, kwanza niangua zambarau zilizojazana mtini, kiasi cha kuweza kuchuma bila kupanda mtini. Nikazichuma kibao, nikazila sana na hadi nyingine nikazijaza ndani ya mfuko wangu.

Nikapumzika ndani ya masaa mawiili hivi, baadae nikala ule wali niliopewa na bibi kidogo mwingine nikaubakisha, nikanywa maji mengi tuu. Nikajiona niko sawa kwa hiyo nikaamua kutembea usiku, kwani sikuwa na usingizi hata lepe moja. Hivyo taratibu nikaendelea na safari yangu. Niliwasikia ndege warukao usiku wakipiga kelele njia nzima.

Njiani sikukutana na wanyama wakubwa, niliowaona wakipita ni k**a swala, kima n.k, japokuwa kwa mbali nilisikia miungurumo upande wa mashariki kwa hapo nilipokuwa. Lakini sikuogopa hata kidogo kwa vile bibi alinihakikishia kuwa sinto dhurika kwa jambo lolote katika safari yangu, nikajipa moyo.

Nikaendelea kuukata usiku njiani hadi nilipohisi kuchoka tena, kwa makisio ilikuwa yapata saa saba hivi za usiku. Niliamua nilale kidogo chini ya mti wa mwembe. Ni mwembe mkubwa sana uliokuwa katikati ya pori. Usiku huo mbalamwezi na nyota angani zilitoa nuru, kiasi kuonekana k**a mchana hata ikiwa umedondosha sindano basi ungeweza kuiona. Macho yangu yalitazama angani kuangalia mpangilio wa nyota, kisha nikaangalia juu ya huo mti wa mwembe.

Nikagundua kuwa mwembe ule haukua na maembe, moyoni nikajiambia kuwa huenda haukua msimu wa maembe. Lakini sikuwa na uhakika wakati nimeweka kirago changu nikijilaza kuusaka usingizi nikashtushwa na jambo nililokuwa nimeliona mbele yangu. Sikuamini macho yangu hata chembe mwili mzima nikawa natetemeka mithli ya mgonjwa wa homa kali.

Kila nilipoangalia kwa makini tukio hilo ambalo ndilo lililonishtua zaidi tokea nianze safari hiyo ya ajabu. Mwili wangu nikahisi unaishiwa nguvu, presha inapanda, presha inashuka, nikanyanyua mikono juu huku nikiwa nimepiga magoti kuomba mungu aniepushe na hili balaa.

Taratibu nikahisi kuwa kuna kitu kinachuruzika miguuni mwangu, nikajiangalia kwa makini kumbe ilikuwa ni haja ndogo inanitoka bila kujijua, yote hiyo ni kutokana na uoga uliokithiri ambao ulisababishwa na hayo niliyokuwa nikiyaona mbele yangu.

Nikajibanza kwenye huo mti wa mwembe kuhofia nisipatwe na madhara ya tukio hilo. Lakini yote nikaona k**a vile ni "mfamaji" haishi kutapa tapa, hata ukiona unyasi utauk**ata ukidhani waweza kumuokoa. "Maskini Rose mie", nani alie nizushia balaa hili na kunileta huku nisikokujua ambako ni hatari tupu ?

Nikajitamkia mwenyewe kwa sauti ya chini chini. Pamoja na kwamba nilikumbuka maneno aliyonieleza yule bibi kizee kwamba njiani naweza kukutana na vitu vibaya lakini nisingeweza kudhurika, lakini kwa hili imani ilinitoka. "Unajua nilichokiona ?" Sikiliza kwa makini. Katika kile kinjia kidogo kilichokuepo kwenye msitu huo ambacho ndicho kinjia nilichokua nikikifuata kutokana na maelekezo ya bibi , nikaona msururu wa watu k**a hamsini hivi kwa makisio ta haraka haraka.

Watu hao walionekana kuwa ni wa ajabu, kwani kwanza wote walikuwa wamevaa kaniki. Halafu mikononi mwao nusu yao walikuwa wameshika vitu vinavyowaka moto, mithli ya mwenge wa uhuru. Nusu kati yao walikuwa warefu sana wanakaribia kimo cha mnazi, wengine waliobaki walikuwa wafupi k**a mbilikimo waishio katika misitu ya nchi ya Kongo, ilikuwa pengine yapata saa nane hivi usiku.

ITAENDELEA,,,,

BY RANIM,,

KISASI CHA WACHAWISEHEMU YA ( 6 )ILIPOISHIA,,, Kilichonifanya hofu kuondoka ni kwa vile nilitambua kuwa yule anaekuja mb...
03/10/2020

KISASI CHA WACHAWI
SEHEMU YA ( 6 )

ILIPOISHIA,,,

Kilichonifanya hofu kuondoka ni kwa vile nilitambua kuwa yule anaekuja mbele yangu ni bibi yule yule nilieagana nae muda mchache tu uliopita. " Nikashangaa! Tusingeonana tena, mbona sasa amerudi ?

INAENDELEA,,,,

Moyoni nikajiuliza mapigo ya moyo yakienda mbio. Tulipokaribiana akaniamuru nisimame nami nikamkubalia, akanivuta pembeni kidogo ya kale kanjia, eneo hilo kulikuwa na nyasi.

Mikono yake ilikuwa na baridi sana, k**a vile nimeshika kipande cha barafu. "Rose hebu kaa hapo" , akanielekeza nikae kwenye nyasi, wasi wasi ulinijaa sikujua kwa nini alinirudia halafu ananiambia nikae chini, sio siri mwili wangu ukawa unatetemeka kwa woga.

" Mbona unatetemeka"? Akaniuliza. "Ah. Unajua bibi umenishtua sana, nikamjibu.

Kwa nini mjukuu wangu? Akaniuliza. " Ulisema kwamba hatutaonana tena, sasa huku kunitokea ghafla na kuniambia nikae kitako ndiko kulikonifanya nishtuke, nikamueleza.

"Basi mjukuu wangu ondoa shaka, si nimekwambia kuwa nitakuokoa kutoka katika janga hili ? Sasa iweje nibadilike ? Msimamo wangu uko pale pale ila kuna kitu cha muhimu nilisahau kukupatia ! Ndio maana nimekuletea ili kije kikusaidie baadae.

Bibi akanifahamisha kwa kirefu, " Kitu gani tena hicho ? "Nikamuuliza bibi nikiwa na hamu ya kuta kutambua alichosahau kunipa. "Unajua huku ni maporini, kwa hiyo kuna mambo mengi yanayoweza kukudhuru katika safari yako.

Kuna wanyama, kuna watu wabaya, wachawi, wengine mambo yao huja kufanyia porini hususan nyakati za usiku, na mengi tuu, usiku ni usiku mjukuu wangu.

Akaendelea kunieleza huku sote tukiwa tumekaa chini. "Sasa hebu chukua pumba hizi ubwie, kisha jipake mwilini". Akatoa unga unga flani hivi, kwa kiasi flani ulifanana na ugoro.

Nikaupaka unga unga huo nikafuatisha maagizo yake, nikabwia na kisha nikajipaka mwili mzima. " Tayari "? Bibi Akaniuliza. "Ndio bibi" nikamuitikia kwa unyenyekevu wa hali ya juu.

"Enheee, ngoja nikuelekeze faidaya hiyo "dawa" akanijuza, nami nikatega masikio kusikiliza atakaloniambia. "Mjukuu wangu dawa hii ina faida nyingi.

Kwa mfano k**a njiani utakutana na wanyama wakali, hawatoweza kukudhuru kwa nguvu ya dawa hii, kisha akanyamaza kidogo ilihali macho yake mekundu yakinitazama kwa makini.

Baada ya dakika mbili tatu akaendelea kunisimulia " unasikia mjukuu wangu'? " "ndio"! Nikamuitikia kwa maneno na kutikisa kichwa kuashiria kumuelewa. Faida nyingine ya dawa hii ni endapo ulikutana na watu wabaya watembea usiku, basi hawatoweza kukuona ila wewe utawaona, kwa wao kutokukuona kutawafanya washindwe kukudhuru.

Kwa kweli ni dawa yenye kusaidia katika mambo mengi sana. Hii sio tiba ni "dawa ya kichawi" akanieleza. Simulizi ilinishtua sana mpaka nikawa sina la kumuuliza tena. Baada ya dakika chache akatoa shuka nyeupe alizokuwa amezihifadhi mkobani. " Unaziona hizi shuka"? Akaniuliza. " Ndio" nikamjibu. "Hizi utakwenda nazo, ukiona umekaribia kufika unakokwenda hiyo shuka kubwa unajitanda mwilini, na hicho kipande utajifunika kichwa chako, akanijuza.

Alivyonieleza habari hizi pamoja na kupokea mzigo huo, lakini nikawa nina maswali kadhaa ya kumuuliza. "Bibi nashukuru kwa yote uliyonieleza, nina maswali kadhaa nitakayo kuuliza. " Umesema kwamba nitakapo karibia kufika ninako kwenda nijitande hizi shuka mwilini, niendako sikujui, jee, nitajuaje kuwa nakaribia kufika hali ya kuwa sijui mwisho wa safari ? Au ndio akili itakuwa imeshanikaa sawa na kurudiwa na kumbu kumbu njiani ? Nilimuuliza bibi.

Kwa swali hili nikamuona huyu bibi anakuna kichwa ambacho kilizingirwa na mvi tupu. "Ni swali zuri sana" akanijibu na kuendelea. "Utakapo karibia huko unapataka kwenda itakutokea ishara" bibi akanijibu.

ITAENDELEA

BY RANIM

KISASI CHA WACHAWISEHEMU YA ( 5 )ILIPOISHIA,,,    Kwanza nikamshukuru mungu kwa kuweza kuikubali sala yangu na kuniwezes...
03/10/2020

KISASI CHA WACHAWI
SEHEMU YA ( 5 )

ILIPOISHIA,,,

Kwanza nikamshukuru mungu kwa kuweza kuikubali sala yangu na kuniwezesha kupata kitu nilichokuwa nikikihitaji mno kwa wakati huo.

INAENDELEA,,,

Bibi nakushukuru sana kwa msaada wako, lakini samahani kwa swali nitakalokuuliza.
"Niulize tu mjukuu wangu, kwani mie nimeamua kukusaidia kwa moyo mmoja."

" Hivi umeniambia niongoze katika njia hii, hivi ninaelekea wapi na safari yenyewe itaisha lini ?"

Nikamuuliza bibi.

" Ahsante mjukuu wangu kwa swali lako zuri, mie sintokuambia lolote ila wewe ifuate tuu njia hii utaona mwisho wake". Na k**a nivyokueleza mwanzo kuwa baadae utapata kumbu kumbu ya kila jambo, hata mie utakuja kunikumbuka vizuri tulipoonana kwa mara ya kwanza na aidha utakuja kunijua.

" Mara ya kwanza si tumeonana pale msituni ? Nikamjulisha,. Akatikisa kichwa kuashiria kukataa, kisha akanieleza kuwa utakuja kukumbuka nilipokuona na uliponiona pale msituni tu. Unanifahamu ila kwa sasa huwezi kunitambua.

Maelezo hayo yalinishtua kiasi cha kufanya nimuulize tena swali lingine. "Unasema kuwa wewe tulishaonana tena zaidi ya kule porini, jee, mara ya kwanza tulionana wapi ?

Ha ha-ha-ha-ha ! Akacheka bibi huyu kiasi kwa mara ya kwanza nikaona mapengo yake yaliyokuwa kwenye meno ya mstari wa mbele ya mdomo wake.

" Kwa sababu akili haijakurudia sawa sawa najua utadhani kule porini ndio mara ya kwanza tulipokutana, lakini baadae utakapojiwa na kumbu kumbu kamili utayajua yote na mie utanikumbuka tulianza kuonana wapi zaidi ya pale msituni usiku ule.

Akanifahamisha bibi huyu.

Hapo mawazo yaliniteka na kujiambia huyu bibi ananifahamu vizuri, mbona mimi simjui kabisa na ndio mara ya kwanza kumuona ? Lakini sikutaka kudadisi zaidi mambo hayo aliyonieleza. Akili yangu sasa ikahamia kule ambako ninakoelekea sehemu nisiyoijua.

"Rose mie sasa naondoka" nadhani hatutaonana tena ila k**a nilivyokueleza fuatisha maagizo yangu ya kuifuata njia niliyokueleza.

Bibi akanifahamisha kwa msisitizo.

" Haya kwa heri bibi, ahsante kwa msaada wako". Nikamueleza. " Nashukuru, nawe nakutakia safari njema huko uendako" Akanitaatifu kisha akapotea machoni mwangu, akipitia njia ya kutokomea maporini.

Mara baada ya kuondoka bibi kizee, kitu cha kwanza nilichokifanya ni kunywa maji kwa sababu mapera niliyokula yalinitia kiu, nilipomaliza kunywa maji, nikajisikia unafuu kwa kiasi kikubwa.

Lakini niliamua niendelee kubaki hapo chini ya mti kujipumzisha zaidi huku nikijaribu kuirudisha kumbu kumbu irudi kichwani mwangu. Kwa vile niliamini kiasi maneno ya yule bibi kwamba kwa siku chache zijazo ningeweza kurudia hali ya kawaida ya utambuzi.

Huku nikiendelea kujipumzisha kwa masaa kadhaa, nikaamua nifungue hot pot za chakula nilizoletewa na bibi. Moja ilijaa wali na nyingine ya pili ilikuwa na mboga, mchuzi wa nyama na nyama nyingi, na ile ya tatu ambayo haikuwa kubwa sana ilijaa ndizi zilizochemshwa.

Nilifurahi kwa vile ndizi kwa nyama ndicho chakula ninachopenda kukila zaidi kuliko chakula kingine. Nikajuiiza sijui bibi yule alijuaje k**a mimi napenda chakula hicho. Nilianza kula ndizi na zile nyama taratibu nikajikuta nguvu zimenirejea, hivyo nikanyanyuka na kuanza kuendelea na safari
yangu huku nikiwa nimeshika "kapu" la chakula kichobaki.

K**a nivyoelekezwa nikaondoka hapo kwa kuifuata njia ile. Lakini nikiwa katika mwendo wa kasi niliyoipata baada ya kula chakula, ghafla nikamuona mtu akitokea mbele yangu niliogopa, lakini kadri tulivyokaribiana na mtu huyo ndivyo woga ulitoweka.

Kilichonifanya hofu kuondoka ni kwa vile nilimtambua kuwa yule anaekuja mbele yangu ni bibi yule yule nileagana nae muda mchache tu uliopita. " Nikashangaa! Tusingeonana tena, mbona sasa amerudi ?

ITAENDELEA

BY RANIM

KISASI CHA WACHAWISEHEMU YA ( 4 )ILIPOISHIA,,,   Kwa jinsi hali niliyokuwa nayo ya uchomvu uliochanganyika na njaa, na i...
03/10/2020

KISASI CHA WACHAWI
SEHEMU YA ( 4 )

ILIPOISHIA,,,

Kwa jinsi hali niliyokuwa nayo ya uchomvu uliochanganyika na njaa, na ile hali ya kuliogopa pori zito, nikazidi kuchanganyikiwa zaidi. Nikajiuliza maswali ambayo sikuweza kuyapatia majibu. Pamoja na yote hayo nikapiga moyo konde, nikapania kuendelea na safari japo kwa mwendo mdogo mdogo..,,

INAENDELEA,,,

Nikanyanyuka toka kwenye huo mti wa mbuyu niliokuwa nimelala nikajinyoosha nyoosha. Nikafikicha macho yangu vizuri baada ya muda nikaanza safari kuifuata ile njia. Nikatembea kiasi cha masaa mawili hivi, huku njaa ikiwa imenibana kweli kweli, hadi miguu ikawa haina nguvu.

Nikashindwa kuendelea na safari nikakaa chini ya mti wa mpera huku nikizidi kuumia kwa njaa iliyokuwa imenikabili. Kuna baadhi ya matunda ya mapera yalikuwa chini chini, nikayachuma na kuanza kuyala, nikasokomeza mdomoni kwa haraka haraka, mapera yapatayo kumi hivi.

Kwa kiasi flanj nikahisi ile njaa niliyokuwa nayo ya kupindukia angalau ilipungua. Jambo lingine likajitokeza sasa, nikabanwa na kiu ya maji kwa vile jua lilikuwa kali mno. Nadhani ilikuwa yapata saa sita mchana hivi, japo tumboni ilikuwa afadhali, lakini ile kiu ndio iliyonisumbua.

Nikajiuliza, "jamani Rose mie nimekosa nini mpaka kukutana na maswahibu k**a haya?" Nikajiuliza tena na tena, hivi huku maporini nitapata wapi maji ya kunywa ? Nikabaki chini ya huo mti wa mpera ilihali sina ufumbuzi juu ya tatizo hilo la kukidhi kiu yangu.

Machozi yakaanza kunitoka, nikalia sana. Lakini baadae nikaona hata k**a nikilia mchana kutwa ingenisaidia nini ? Kwa huko porini ni nani angeweza kusikia kilio changu na kuweza kunisaidia kunipa maji ? Nikapiga magoti na kumuomba mungu anisaidie niondoke na adha hii iliyonikumba.

Nikaamini ni mungu tuu awezae kuniokoa mie mja wake. Nikasali kwa nusu saa huku nikitamka maneno ya kumuomba mungu. Uchomvu na ile hali ya kiu hatimae vikanifanya nipate usingizi.

Nikiwa usingizini nikashtuka, kwani nilisikia mtu akiniamsha kwa kunitikisa mwili wangu.,, " Rose, "Rose," sauti ya mtu huyo ilikuwa nzito. Nilisikia nikashtuka, huku porini ni nani huyo anaeniita jina langu ? Nikajiuliza mwenyewe.

Nikageuza kichwa changu kumtazama mtu huyo aliekuwa akiniita. "Ala!!" kumbe ni bibi ?" nikatamka baada ya kumuona yule bibi niliekutana nae mara ya kwanza na kuninywesha ile dawa aliyodai kuwa ni "dawa" itakayoweza kunisaidia.

" Shikamoo bibi" nikamuamkia huku nikishusha pumzi taratibu, "Marahabaa mjukuu wangu, pole sana". Akanieleza, ndio hivyo hivyo tu bibi taabu napata, kiu pamoja na njaa.

Bibi akanijibu, jitahidi k**a nilivyokueleza, uifuate njia hii hii., nami nikamjibu, sawa bibi,, nikamuitikia...!

Najua njaa na kiu ya maji vinakusumbua katika safari yako, hivyo ndivyo maana nimekuletea chakula na maji ya kunywa. Yule bibi akanipa mfuko uliosukwa kwa ukindu, ndani ya mfuko huo kulikuwa na hot pot tatu za kuwekea chakula pamoja na chupa mbili kubwa za maji ya kunywa.

Mjukuu wangu hiki chakula na hayo maji yatakusaidia katika safari yako, akanieleza bibi. Lakini pamoja na chakula kwanza ahsante. Kwanza nikamshukuru mungu kwa kuweza kuikubali sala yangu na kuniwezesha kupata kitu nilichokuwa nikikihitaji mno kwa wakati huo.

ITAENDELEA

BY RANIM,,,,

Address

Tanga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when RANIM SALIM. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to RANIM SALIM.:

Share