MOYO plus

MOYO plus Lengo letu kwako ni kuhakikisha unamaliza kabisa changamoto zako zote za Moyo na Mishipa ya damu.

____________________________________Cardiomegaly ni hali ambapo moyo wako unapanuka zaidi ya kawaida, maarufu k**a "enla...
13/11/2024

____________________________________

Cardiomegaly ni hali ambapo moyo wako unapanuka zaidi ya kawaida, maarufu k**a "enlarged heart."

Sio ugonjwa wa pekee bali ni dalili au athari ya matatizo mengine ya kiafya.

Kupanuka kwa moyo wako kunaweza kuathiri uwezo wake wa kusukuma damu kwa ufanisi, hali inayoweza kukusababishia magonjwa k**a vile heart failure, shinikizo la damu, na matatizo ya valve za moyo.

Sababu na Jinsi Cardiomegaly Inavyotokea

1. Shinikizo la Damu Juu (Hypertension)

Shinikizo la juu la damu huufanya moyo wako kufanya kazi kwa nguvu zaidi ili kusukuma damu kwenye mishipa.

Hii inasababisha misuli ya moyo kuongezeka ukubwa na mwishowe moyo wako kupanuka.

2. Magonjwa ya Valve za Moyo

Ikiwa valve za moyo wako hazifanyi kazi vizuri, moyo unalazimika kufanya kazi zaidi kusukuma damu kwa ufanisi, hali inayoweza kuleta upanuzi.

3. Cardiomyopathy

Huu ni ugonjwa unaoathiri misuli ya moyo wako na unaweza kuufanya moyo wako kupanuka.

Sababu zake zinaweza kuwa maumbile, matumizi mabaya ya pombe, au maambukizi.

4. Heart Failure

Wakati moyo wako hauwezi kusukuma damu vizuri, unaweza kupanuka k**a njia ya kujaribu kuongeza uwezo wa kusukuma damu.

5. Sababu Nyingine

Magonjwa k**a upungufu wa damu (anemia), shida za figo, na maambukizi makali ya virusi yanaweza pia kukusababishia cardiomegaly.

Athari za Cardiomegaly

Moyo ulio panuka unakuwa na uwezo mdogo wa kusukuma damu na kusababisha matatizo k**a:

🚫 Mkusanyiko wa maji kwenye mwili (edema).

🚫 Kuathiriwa kwa utendaji wa ogani k**a figo na mapafu.

🚫 Kuhatarisha maisha ikiwa hautatibiwa mapema.

Endapo wewe ni miongoni mwa wahanga wa tatizo hili na unahitaji msaada au ushauri wowote wa kitabibu basi usisite kuwasiliana nami

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1



_______________________

ZIJUE SABABU ZA TATIZO LAKO LA PRESHA YA KUPANDA___________________________Sababu za presha ya kupanda (hypertension) zi...
15/10/2024

ZIJUE SABABU ZA TATIZO LAKO LA PRESHA YA KUPANDA
___________________________

Sababu za presha ya kupanda (hypertension) zinaweza kugawanywa katika makundi mawili yafuatayo;

1.Hypertension isiyo na sababu maalum (Primary/Essential Hypertension):

Haina chanzo maalum kinachojulikana...

Lakini inahusishwa na mchanganyiko wa sababu mbalimbali za kijenetiki na kimazingira.

● Sababu za urithi

Historia ya familia ya ugonjwa wa presha inaongeza hatari.

● Umri

Shinikizo la damu huongezeka kadri unavyoongezeka umri.

● Mtindo wa maisha

Ulaji wa chumvi nyingi,sukari nyingi,mafuta mengi, uzito kupita kiasi, ukosefu wa mazoezi, na matumizi ya pombe na sigara huchangia sana.

2.Hypertension yenye sababu maalum (Secondary Hypertension)

Hutokana na magonjwa au hali nyingine za kiafya zinazojulikana k**a vile:

1.Magonjwa ya figo

Uharibifu wa figo huathiri usawa wa chumvi na maji mwilini, na kukuongezea presha.

2.Matatizo ya homoni

Magonjwa k**a Cushing's syndrome na hyperthyroidism husababisha uzalishaji wa homoni kupita kiasi ambazo hukuongezea presha.

3.Matumizi ya dawa fulani

Dawa k**a vile za uzazi wa mpango na dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs) zinaweza kukuongezea presha.

Kuelewa sababu hizi ni muhimu katika kudhibiti na kutibu shinikizo lako la damu.

Unaswali au unahitaji ushauri juu ya tatizo lako basi usisite wasiliana nami.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus

___________________________

HIZI HAPA DALILI ZA TATIZO LAKO LA PRESHA YA KUPANDA___________________________Dalili za shinikizo la damu la juu (presh...
15/10/2024

HIZI HAPA DALILI ZA TATIZO LAKO LA PRESHA YA KUPANDA
___________________________

Dalili za shinikizo la damu la juu (presha ya kupanda) zinaweza kuwa chache au hazipo kabisa kwa watu wengi.

Hata hivyo baadhi ya dalili zinazoweza kuashiria kwamba una presha ya kupanda ni pamoja na:

1.Maumivu ya kichwa hasa sehemu ya nyuma ya kichwa au paji la uso.

2.Kizunguzungu au kuhisi kupoteza usawa.

3.Kichefuchefu au kutapika.

4.Kutokwa na damu puani.

5.Uoni uliyopungua au wenye ukungu.

6.Mapigo ya moyo kwenda kwa kasi au kuhisi kugonga kifuani.

7.Maumivu ya kifua.

8.Kuchoka kupita kiasi au hali ya kutojisikia vizuri.

9.Kuvimba kwa miguu, mikono, uso au macho.

10.Kupumua kwa shida, hasa wakati wa shughuli za kimwili.

11.Kuhisi moto au joto usoni (flushing).

Dalili hizi zinaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu na mara nyingi hutokea pale shinikizo lako la damu linapokuwa juu sana au limeendelea kwa muda mrefu bila kutibiwa.

Ni muhimu kufanya vipimo vya mara kwa mara ili kugundua shinikizo lako la damu mapema.

Unaswali lolote au unahitaji ushauri juu ya tatizo lako, usisite kuwasiliana nami.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus

___________________________

JE, UNAJUA PRESHA YA KUPANDA NI NINI.?___________________________Kulingana na tafiti za kitaalam zinaeleza ya kwamba...P...
14/10/2024

JE, UNAJUA PRESHA YA KUPANDA NI NINI.?
___________________________

Kulingana na tafiti za kitaalam zinaeleza ya kwamba...

Presha ya kupanda (hypertension) ni hali ambayo shinikizo la damu kwenye mishipa yako huwa juu zaidi ya kiwango cha kawaida kwa muda mrefu.

Shinikizo la damu hupimwa kwa milimita ya zebaki (mmHg) na huwa na vipimo viwili:

1.Shinikizo la juu (systolic) linalopima nguvu ya damu wakati moyo unapoenda.

2.Shinikizo la chini (diastolic) linalopima nguvu ya damu wakati moyo unarelax.

Presha ya kupanda inaweza kukusababishia matatizo ya kiafya k**a vile ugonjwa wa moyo, kiharusi, na kushindwa kwa figo ikiwa haitadhibitiwa haraka.

K**a unaswali lolote au unahitaji ushauri wowote juu ya hali yako basi usisite kuwasiliana nami.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus
___________________________

HUU NDIO MUDA SAHIHI WA KUPIMA PRESHA YAKO___________________________Najua hata wewe ni miongoni mwa wasiojua muda sahih...
14/10/2024

HUU NDIO MUDA SAHIHI WA KUPIMA PRESHA YAKO
___________________________

Najua hata wewe ni miongoni mwa wasiojua muda sahihi wa kupima presha yao.

Hebu leo ngoja tujifunze kidogo kuhusu muda sahihi wa kupima presha yako.

Kitaalam muda sahihi wa kupima presha ni wakati mwili umepumzika ili kupata kipimo sahihi.

Inashauriwa kupima presha yako katika nyakati zifuatazo;

1.Asubuhi mapema

Kabla ya kula au kunywa chochote na kabla ya kufanya shughuli yoyote nzito, kwa sababu mwili unakuwa katika hali ya kupumzika.

2.Wakati wa Jioni

Kupima tena jioni inaweza kukusaidia kuona mabadiliko ya presha yako kwa siku nzima.

Ni muhimu kuhakikisha unakaa kimya kwa dakika tano kabla ya kipimo, na epuka kafeini, sigara, na mazoezi makali kwa angalau dakika 30 kabla ya kupima.

K**a unaswali lolote au unahitaji ushauri wowote juu ya hali yako basi usisite kuuliza.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus

___________________________

IJUE PRESHA YAKO_______________________Kuna umuhimu mkubwa sana wa kujua mambo ya msingi yaliyo katika mwili wako.Kwani ...
14/10/2024

IJUE PRESHA YAKO
_______________________

Kuna umuhimu mkubwa sana wa kujua mambo ya msingi yaliyo katika mwili wako.

Kwani hukusaidia kuelewa na kupata utatuzi wakitaalam sana bila kuathiri mwili wako na hali yako ya kiuchumi.

Presha mwilini inamaanisha nguvu inayosukuma damu dhidi ya kuta za mishipa yako ya damu wakati moyo unapopiga.

Kitaalamu hujulikana k**a shinikizo la damu (blood pressure) na inatokana na nguvu inayotumiwa na moyo wako kusukuma damu kupitia mfumo wa mzunguko wako wa damu.

Inapimwa kwa kipimo cha milimita za zebaki (mmHg) na ina vipimo viwili:

1.Shinikizo la juu (systolic pressure)

Ni presha wakati moyo unapoonyesha nguvu zaidi wakati wa kusukuma damu nje kwenye mishipa.

2.Shinikizo la chini (diastolic pressure)

Ni presha wakati moyo unarelax kati ya mapigo, ikiruhusu damu kujaza tena kwenye ventrikali.

Presha yako ya damu inategemea mambo k**a vile...

Kiasi cha damu inayosukumwa na moyo, upana na ulaini wa mishipa ya damu, na kiwango cha upinzani katika mtiririko wa damu yako.

K**a unaswali lolote kuhusu hili ambalo tumelizungumzia hapa.basi usisite kuuliza.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus

___________________________

HUU NDIO MOYO WAKO UJUE SASA___________________________Ni muhimu sana kuujua moyo wako na utendaji kazi wake itakusaidia...
13/10/2024

HUU NDIO MOYO WAKO UJUE SASA
___________________________

Ni muhimu sana kuujua moyo wako na utendaji kazi wake itakusaidia kujua vizuri matatizo ambayo yanaweza kuupata moyo wako.

Moyo ni kiungo cha misuli kilichoko kwenye kifua chako ambacho hufanya kazi k**a pampu ya kusukuma damu mwilini.

Unao uwezo wa kujibana na kupumzika, hivyo kusukuma damu kupitia mfumo wa mzunguko wako wa damu (circulatory system).

Kazi kuu ya moyo ni kuhakikisha kwamba oksijeni na virutubishi vinapatikana kwa viungo na tishu zote za mwili wako...
..na kusaidia kuondoa kaboni dioksidi na taka nyingine kutoka mwili wako.

Moyo una sehemu nne kuu:

1.Aurikoli ya kushoto na kulia (atria).

2.Ventrikali ya kushoto na kulia (ventricles), ambazo hufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha mzunguko sahihi wa damu.

K**a unaswali lolote karibu sana usisite kuuliza.

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

plus
___________________________

UNASUMBULIWA NA TATIZO LOLOTE LA MOYO AU PRESHA YA KUPANDA SOMA HAPA KWA MAKINI ___________________________Habari za wak...
13/10/2024

UNASUMBULIWA NA TATIZO LOLOTE LA MOYO AU PRESHA YA KUPANDA SOMA HAPA KWA MAKINI
___________________________

Habari za wakati huu.?

Ebwana mimi hapa sikupenda niwe msemaji sana katika hili ambalo lipo mbele yako.

Bila shaka wewe ni miongoni mwa wahanga wakubwa sana wa matatizo ya moyo na mishipa ya damu...
..na inawezekana kabisa kuwa kwa sasa umekata tamaa kabisa juu ya matatizo yako.!

Kwa sababu umejaribu kufanya kila namna ya kuweza kuondokana na matatizo hayo bila mafanikio si ndio.?

Ukienda hospital napo waambiwa mara presha haitibiki, hivyo unaishia tu kupewa dawa za kutuliza tatizo lako.

Daaaah.!

Kiukweli hali hiyo inatesa sana watu wengi na tayari asilimia kubwa wameshajijengea dhana hiyo hiyo...

Kwamba presha haitibiki.!

Kiufupi napenda tu nikwambie ya kwamba hakuna ugonjwa usiyokuwa na tiba.

Jambo la msingi ni lijue tatizo lako ni nini hasa na linasababishwa na nini kisha epukana nazo na baada ya hapo tafuta matibabu sahihi katika dalili za wali, presha au matatizo yote ya moyo yanatibika amini nakwambia.

Mimi naomba niishie hapa.!

Lakini k**a unaswali lolote au ungependa kupata ushauri zaidi, basi nitumie ujumbe wako whatsApp kupitia link hii 👇

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

Asante sana kwa kuwa pamoja nami.

plus
___________________________

MAAJABU YA ROSELLE (CHOYA) KWA MATATIZO YA MOYO NA MISHIPA YA DAMU____________________________________Choya jina la kiin...
11/10/2024

MAAJABU YA ROSELLE (CHOYA) KWA MATATIZO YA MOYO NA MISHIPA YA DAMU
____________________________________

Choya jina la kiingereza ni Rosella na jina la kisayansi ni "Hibiscus sabdariffa" ina phytonutrients muhimu k**a vile anthocyanins, flavonoids, na polyphenols.

Hizi phytonutrients zina uwezo wa kupambana na uchochezi (inflammation), kupunguza shinikizo la damu, na kuboresha afya ya mishipa ya damu.

Anthocyanins hasa zina uwezo wa kupunguza kiwango cha mafuta mabaya kwenye damu (LDL cholesterol), hali inayosaidia kuzuia magonjwa ya moyo.

Pia Rosella ina uwezo wa kushusha shinikizo la juu la damu (antihypertensive effect), jambo ambalo linachangia kudhibiti hatari za magonjwa ya moyo na mishipa.

Matumizi: tumia juice yake isiyo na sukari pia isiwe na maji mengi.

Kwa msaada zaidi usisite kuwasiliana nasi tuma ujumbe whatsApp kupitia link hii 👇

https://wa.me/message/PGIVY6D5OKDFG1

Asante sana

plus

__________________

Address

Pongwe Area
Tanga

Telephone

+255787278759

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MOYO plus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to MOYO plus:

Share