11/05/2026
⚠️ MAMA MJAWAZITO, USIPUUZE MTOTO KUPUNGUZA KUCHEZA TUMBONI 😭💔
Moja ya mambo yanayoumiza sana hospitalini ni kusikia mama akisema:
🗣️ “Mtoto wangu alikuwa anacheza sana… lakini leo amecheza kidogo sana.”
Halafu akabaki nyumbani akitumaini kila kitu kiko sawa. 😢
Mama mjamzito, tafadhali sikiliza hili kwa umakini ❤️
Kucheza kwa mtoto tumboni ni moja ya ishara muhimu kwamba mtoto wako yupo salama ndani ya tumbo.
Ikiwa mtoto ambaye kawaida hucheza sana ghafla: ⚠️ Ameanza kucheza kidogo sana
⚠️ Anaonekana mnyonge
⚠️ Au hujamsikia kabisa kwa muda mrefu
🚨 USISUBIRI MPAKA KESHO.
Usiseme: ❌ “Labda amelala tu.”
Usiruhusu: ❌ Hofu
❌ Kukosa nauli
❌ Maneno ya watu
❌ Aibu ya kwenda hospitali
vikuzuie kwenda kupimwa.
Wakati mwingine inaweza isiwe tatizo kubwa… Lakini wakati mwingine hiyo kwenda hospitali mapema inaweza kuokoa maisha ya mtoto wako. 💔😭
Mtoto ambaye alikuwa anacheza vizuri hapaswi ghafla kuwa kimya sana bila kufuatiliwa.
Na mama mjamzito 🤰❤️
Usione k**a unawasumbua manesi au madaktari.
Ni bora kwenda ukakaguliwe na kuambiwa kila kitu kiko sawa… Kuliko kukaa kimya halafu ukaja kujuta baadaye. 🥺
Tafadhali, zingatia sana movement za mtoto wako tumboni. ❤️
Endelea kufuatilia post zangu kwa elimu muhimu ya ujauzito na uzazi ambayo wakati mwingine haifundishwi vizuri kliniki 🤱💛🔥
Nurse Presh Cares 🥰
Preshcute Utonwa 💕