06/01/2026
USHUHUDA KUHUSU MAISHA YA “KANDA BONGO MAN”
SEHEMU YA PILI
1. Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kabisa maishani kumwona Rais Bokassa kwa macho yangu mwenyewe, tukio lililoacha alama isiyofutika moyoni mwangu.
Nilikuwa pia nimeshirikiana na "Émile Soki" katika wimbo (Animave), ingawa kwenye YouTube waliuandika vibaya k**a (Alimate).
Tulifanya kazi pamoja pia kwenye Wimbo (Folie Rose), lakini "Émile Soki" hakuweza kuutoa kwa sababu aliamua kupatana na kaka yake "Maxime Soki Vangu" na kurejea kwenye kundi Bella Bella hivyo kuutoa Wimbo huo kwa Lebo ya BELLA BELLA.
2. Ndugu hao wawili walikuwa wakigombana mara kwa mara kiasi kwamba familia yao ililazimika kuingilia kati ili kupunguza mvutano.
"Émile Soki" aliondoka (Bella Mambo Rénové) pamoja na wanamuziki takriban wote na kujiunga na (Bella Bella).
Mimi binafsi sikuandamana nao, nikiwa na mashaka makubwa kuhusu mustakabali wangu wa baadae.
3. Siku moja, nikiwa nyumbani nikiangalia TV, nilimuona Bwana "Katalay", aliyewahi kuwa Meneja wa "Dokta Niko Kassanda", akitangaza kurejea kwake kutoka Ulaya akiwa na vifaa vipya vya muziki na akisema anatafuta vijana wa kuwaajiri.
Nilimfuata mara moja, na baada ya mazungumzo, alikubali kuwa Meneja wangu.
4. Hapo ndipo nilipoanzisha Group langu mwenyewe, (Bana Mambo).
Nilitaka kubakiza jina (Mambo) ili kuonyesha chimbuko langu kutoka (Bella Mambo Rénové).
Ndani ya Group langu, Mpiga Solo alikuwa si mwingine bali "Diblo Dibala".
"Bwana Katalay", Mtu wa uadilifu wa hali ya juu, alikuwa akishika wadhifa mkubwa katika kampuni ya Kiitaliano Franco Plast, ambako alikuwa Mkurugenzi Mkuu.
5. Alinichukulia k**a Mwanawe mwenyewe; wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 18 tu.
Alinilipia tiketi ya ndege kwenda Italy, na tulipofika huko akanipa fedha za kununua vifaa vipya vya muziki.
Baada ya kukaa Italy, nilitembelea pia Ubelgiji na Ufaransa kabla ya kurejea Kinshasa.
Kabla ya kujiunga na (Bella Mambo), nilikuwa nikifanya mazoezi na Bazou katika mtaa wa Kanda Kanda, pamoja na Papa Wemba na Groupe lake la Viva la Musica, Bisikita na Donnat Mobeti.
6. Niliporejea kutoka Ulaya, nilileta vifaa kamili vya muziki ambavyo hata "Papa Wemba" alikuwa akivikopa mara kwa mara kwa ajili ya mazoezi.
Urafiki wangu na mdogo wake "Papa Wemba" ajulikane kwa jina la "Dio" ulifanya jambo hilo kuwa la kawaida kabisa.
Hata hivyo, kwa kuwa (Bana Mambo) haikupata mafanikio tuliyotarajia, nilianza kufikiria kurudi Ulaya kuendelea na masomo.
7. Kabla sijasafiri, "Vieux Soki Vangu" alifika nyumbani kwangu akiniomba nimsaidie kuimba kwenye harusi kwa sababu "Émile Soki" alikuwa mgonjwa.
Nilikubali, na onyesho lilifanikiwa sana chini ya uongozi wa "Vieux Shaba Kahamba".
8. Tamasha letu la pili na Groupe (Bella Bella) lilifanyika katika Ukumbi wa Confidence Bar jijini Kinshasa.
Baada ya onyesho, nilimweleza "Soki Vangu" kuwa nilikusudia kuondoka kuelekea Ulaya.
Alijaribu kunizuia, lakini uamuzi wangu ulikuwa tayari umekamilika kwani nilikuwa nimeshanunua tiketi.
Mwaka 1978 nilisafiri kwenda Paris, ambako maisha yalikuwa magumu kupindukia.
Ningewezaje kuendelea na masomo nikiwa na changamoto za makazi, chakula na ada za chuo?
9. Wakati ule, Wazaire walikuwa wachache sana jijini Paris.
Nilifanya kazi kwa mwaka mzima ili kupata kibali cha kuishi na kufanya kazi.
Wakati huohuo, "Diblo Dibala" naye alikuwa akitafuta njia ya kuondoka Kinshasa kuja Ulaya.
Nilipowasili Paris, nyimbo zilizotikisa zilikuwa zikitia fora ni (Gergette Eckins) ya "Sam Mangwana", (Double Double) ya "Kanta Nyboma", na (Amio) ya "Bébé Manga".
"Diblo Dibala" alipopata viza ya Ubelgiji, alishukia kwenye Mjini wa (Mons), ambako nilimshauri ajiunge nami Paris.
10. Tukiwa Paris na "Diblo Dibala", tulirekodi wimbo (Iyole) kwenye kaseti.
Kisha nikaenda kumuona "Bwana Eddy Gustave", Producer wa "Sam Mangwana".
Baada ya kuusikiliza, alisema haukumvutia na akaniambia nijaribu mtindo wa rumba k**a aimbavyo "Sam Mangwana".
Laa sivyo usipime tena kurudia hapa kwangu.
Lakini sisi tulikuwa tumejikita kwenye mtindo wa (Ngwasuma Soukous).
Baadae nilimwona "Bi Lacoste", Producer wa "Mpongo Love", nae pia alikataa kunisaidia, akisema ningepaswa kuimba k**a "Mpongo Love" ili anisaidie.
11. Hatimaye, nilikutana na rafiki yangu "Narcisse", akiwa na Mtu wake wa karibu aitwaye "David Ouattara", mwenye duka la kuuza kanda za muziki.
Nilipo msikilizisha wimbo (Iyole), "David Ouattara" alivutiwa mara moja na mtindo wetu wa soukous na akakubali kufadhili kurekodi.
Akauliza utaratibu wa kuingia studio, nikamweleza, naye akaukubali.
Tuliingia studio Caroline jijini Paris na wanamuziki hawa:
— Solo : Diblo Dibala
— Rhythm : Aimé Kobo
— Bass : Miguel Yamba
Tukatoa diski yenye nyimbo nne:
Face A: 1. Iyole ; 2. N’Sambi-Carol
Face B: 1. Amini ; 2. Mazina
Ninakiri kwamba, hata nikitazama kazi zangu zote, sijawahi kutoa album iliyokamilika kiasi hicho: kwa siku mbili tu za studio tulizalisha kazi ya kiwango cha juu ajabu.
12. Sifa nyingi zinamwendea "Diblo Dibala", ambae alicheza gitaa kwa ustadi wa hali ya juu.
Changamoto iliyobaki ilikuwa jinsi ya kufanya matangazo.
Tulizungumza na "David Ouattara", ambae alipendekeza tushirikiane na Wanamuziki wa Ivory Coast, waliokuwa mashuhuri kwa uwezo wao wa kutangaza kazi za muziki.
Walikutana katika matukio yanayoitwa dédicaces, ambako walitathmini Wasanii jukwaani na, wakiridhika, walitangaza kazi zao kwa nguvu kubwa.
13. Tukaamua kuhudhuria mkutano wa dédicaces siku ya Jumamosi.
Baada ya Wasanii kadhaa kuonyesha kazi zao, nami niliitwa nijitambulishe.
Nilipopanda jukwaani, niliwasha moto hadi Umati wote ulisimama kwa shangwe.
Wakauliza mimi ni raia wa nchi gani, na "David Ouattara" akawaambia kuwa natoka Zaire.
14. Watu walitaka mara moja kujua jinsi ya kupata nakala za kanda zetu.
"David Ouattara" aliwaeleza kuwa duka lake hufungwa Jumapili na lingeweza kufunguliwa Jumatatu.
Walikataa kabisa: walitaka afungue kesho yake, bila kukosa.
Bila kusita, David alikubali.
15.
Jumapili asubuhi, David Ouattara alipofungua duka, alikuta foleni kubwa ya watu waliomiminika kununua nakala zote.
Muziki wetu ulipokelewa kwa shangwe kubwa, na kanda zote zikaisha papo hapo.
Habari zilipomfikia "Eddy Gustave" yuleyule aliyekataa kutusaidia hapo awali, alikuja kuniomba niwe chini ya uongozi wake k**a Producer.
Nikajibu kuwa jambo hilo halingewezekana kamwe, kwa sababu nilibaki mwaminifu kwa "David Ouattara" aliyenisaidia katika nyakati ngumu.
Alisisitiza, hata akapendekeza kuchukua mawakili iwapo ningekubali.
Nikamwambia aache kupoteza muda.
Itaendelea...
TÉMOIGNAGE SUR LA VIE DE « KANDA BONGO MAN
DEUXIEME PARTIE
1. Ce fut la toute première fois de ma vie que je vis le président "Bokassa" de mes propres yeux, un événement qui laissa en moi une empreinte indélébile.
J’avais également collaboré avec "Émile Soki" sur le titre (Animave), bien que celui-ci ait été mal orthographié (Alimate) sur YouTube.
Nous avions aussi travaillé ensemble sur (Folie Rose), mais Émile Soki ne put en assurer la sortie, ayant choisi de se réconcilier avec son frère Maxime Soki Vangu et de réintégrer le groupe Bella Bella.
2. Ces deux Frères se querellaient fréquemment, au point que leur famille devait régulièrement intervenir pour tenter d’apaiser les tensions.
Émile Soki quitta alors (Bella Mambo Rénové) avec l’ensemble des musiciens pour rejoindre (Bella Bella).
Pour ma part, je ne les suivis pas, hésitant profondément quant à mon avenir.
3. Un jour, alors que je regardais la télévision chez moi, j’aperçus "M. Katalay", ancien manager du "Docteur Niko Kassanda", annonçant son retour d’Europe avec de nouveaux instruments de musique et déclarant rechercher de jeunes artistes à engager.
Je me rendis aussitôt auprès de lui et, après un entretien, il accepta de devenir mon manager.
4. C’est ainsi que je fondai mon propre groupe, (Bana Mambo).
Je tenais à conserver le nom Mambo afin de rappeler mes origines au sein de (Bella Mambo Rénové).
Dans mon groupe, le guitariste solo n’était autre que Diblo Dibala.
M. Katalay, homme d’une grande probité, occupait alors un poste de haute responsabilité au sein de la société italienne Franco Plast, dont il était le directeur général.
5. Il me considérait comme son propre fils ; je n’avais alors que 18 ans.
Il finança mon billet d’avion pour l’Italie et, une fois sur place, me remit de l’argent afin que j’y achète des instruments neufs.
Après mon séjour en Italie, je visitai également la Belgique et la France, avant de regagner Kinshasa.
Avant d’intégrer (Bella Mambo), je m’exerçais avec Bazou dans le quartier de Kanda Kanda, aux côtés de "Papa Wemba" avec son "Viva la Musica", "Bisikita" et "Donnat Mobeti".
6. À mon retour d’Europe, j’apportai un équipement musical complet, que même "Papa Wemba" empruntait régulièrement pour ses répétitions.
Mon amitié avec son jeune Frère Dio rendait cela tout à fait naturel.
Cependant, (Bana Mambo) ne rencontrant pas le succès espéré, je commençai à envisager un retour en Europe afin de poursuivre mes études.
7. Avant mon départ, "Vieux Soki Vangu" vint me chercher chez moi : il souhaitait que je remplace au chant "Émile Soki" lors d’un mariage, car il était malade.
J’acceptai, et la prestation fut un véritable succès, sous la direction de "Vieux Shaba Kahamba".
8. Notre second concert avec (Bella Bella) eut lieu au Confidence Bar de Kinshasa.
À l’issue de la représentation, j’informai "Soki Vangu" de mon intention de repartir pour l’Europe.
Il tenta de me dissuader, mais ma décision était irrévocable, mon billet étant déjà acheté.
En 1978, je m’envolai pour Paris, où la vie se révéla extrêmement difficile.
Comment poursuivre mes études dans de telles conditions, entre logement précaire, manque de nourriture et frais universitaires ?
9. À cette époque, les Zaïrois étaient très peu nombreux à Paris.
Je travaillai une année entière afin d’obtenir un permis de séjour et de travail.
Pendant ce temps, "Diblo Dibala" cherchait lui aussi un moyen de quitter Kinshasa pour l’Europe.
À mon arrivée à Paris, les titres en vogue étaient (Gergette Eckins) de "Sam Mangwana", (Double Double) de "Kanta Nyboma", et (Amio) de "Bébé Manga".
Lorsque "Diblo Dibala" obtint un visa pour la Belgique, il atterrit à Mons, d’où je l’encourageai à me rejoindre à Paris.
10. À Paris, nous enregistrâmes le titre (Iyole) sur cassette.
Je me rendis ensuite chez "M. Eddy Gustave", Producteur de "Sam Mangwana".
Après écoute, il déclara ne pas apprécier le morceau et me suggéra d’adopter un style Rumba similaire à celui de "Sam Mangwana".
Pourtant, notre orientation musicale relevait clairement du (Ngwasuma Soukous).
Je rencontrai ensuite "Mme Lacoste", Productrice de "Mpongo Love", qui refusa elle aussi de me soutenir, estimant que je devrais chanter dans le style de "Mpongo Love" pour bénéficier de son appui.
11. Finalement, je rencontrai mon ami "Narcisse", accompagné d’un certain "David Ouattara", propriétaire d’une boutique de disques.
Lorsque je lui fis écouter (Iyole), "David Ouattara" fut immédiatement séduit par notre soukous et accepta de financer l’enregistrement.
Il me demanda l’organisation nécessaire pour entrer en studio, et je lui exposai le plan, qu’il approuva.
Nous enregistrâmes au studio Caroline à Paris, avec les musiciens suivants :
— Solo : Diblo Dibala
— Rythmique : Aimé Kobo
— Basse : Miguel Yamba
Nous produisîmes un disque de quatre titres :
Face A : 1. Iyole ; 2. N’Sambi-Carol
Face B : 1. Amini ; 2. Mazina
Je dois reconnaître que, même en considérant l’ensemble de ma carrière, je n’ai jamais sorti un album aussi abouti : en seulement deux jours de studio, nous avions créé une œuvre d’une qualité remarquable.
12. Une grande part du mérite revient à "Diblo Dibala", dont la virtuosité à la guitare fut exceptionnelle.
Restait la question de la promotion.
Nous en discutâmes avec David Ouattara, qui proposa de nous associer à des musiciens ivoiriens, réputés pour leur maîtrise de la publicité musicale.
Ils se réunissaient lors d’événements appelés dédicaces, où ils évaluaient les artistes sur scène et, s’ils étaient convaincus, assuraient la promotion de leurs œuvres.
13. Nous décidâmes donc d’assister à une séance de dédicaces un samedi.
Après les prestations de plusieurs artistes, je fus invité à me présenter.
Dès que je montai sur scène, je mis littéralement le feu : le public se leva, enthousiaste.
On demanda alors de quelle nationalité j’étais, et "David Ouattara" répondit que je venais du Zaïre.
14. Le public voulut immédiatement savoir comment se procurer nos cassettes.
"David Ouattara" leur expliqua que sa boutique était habituellement fermée le dimanche et qu’ils devraient attendre le lundi.
Ils refusèrent catégoriquement : il devait impérativement ouvrir dès le lendemain.
Sans hésiter, David accepta leur requête.
15. Le dimanche matin, lorsqu’il ouvrit sa boutique, David Ouattara découvrit une foule immense qui se précipita pour acheter toutes les copies disponibles.
Notre musique fut accueillie avec un enthousiasme extraordinaire, et les cassettes furent épuisées en un instant.
Lorsque la nouvelle parvint à "Eddy Gustave" le même producteur qui nous avait auparavant refusé tout soutien, il vint me solliciter pour devenir mon Producteur.
Je lui répondis que cela n’arriverait jamais, par fidélité envers "David Ouattara", qui m’avait aidé dans les moments les plus difficiles.
Il insista, allant jusqu’à proposer de prendre des avocats si j’acceptais son offre.
Je lui rétorquai qu’il perdait son temps.
A suivre
Baba L.W.L