Lubonji Wa Lubonji

Lubonji Wa Lubonji L.W.L MUSIC INTERNATIONAL

11/01/2026
JULES KIBENS QUITTE WENGE BCBG : UN PILIER S’EN VAJULES KIBENS AONDOKA WENGE BCBG : NGUZO IMEANGUKA1.  Kwa mujibu wa Bla...
11/01/2026

JULES KIBENS QUITTE WENGE BCBG : UN PILIER S’EN VA
JULES KIBENS AONDOKA WENGE BCBG : NGUZO IMEANGUKA

1. Kwa mujibu wa Blanchard Mosaka, Msemaji mashuhuri wa Wenge Musica BCBG, sakata la "Jules Kibens" halipaswi kuonekana k**a ukweli bali k**a mkakati wa kawaida wa binadamu: “Ukitaka kuondokana na mbwa wako, utasema ana kichaa.”
Kwa maneno haya makali, "Mosaka" anasisitiza kuwa "Profesa Kibens" wala si mchawi, bali ni Msanii mwadilifu ambae aligeuzwa kuwa mlengwa wa tuhuma zisizo na msingi katika mazingira yaliyotawaliwa na hofu na msongamano wa hisia.

2. Baada ya takribani miaka ishirini na saba ya uaminifu usiotetereka, "Kibens" alistahili kuaga "Wenge BCBG" kwa heshima, shukrani na taadhima.
Kwa sababu, k**a alivyoeleza "Mosaka", ndiye aliyekuwa “Nguzo ya uorodheshaji wa muziki”, Mtu alielipa kundi pumzi ya ubunifu na uthabiti.

3. Historia ya muziki wa Congo itakumbuka kwamba kati ya nyimbo mia moja zilizo Hit za Wenge BCBG, takribani themanini zilibebwa ubunifu na uchangiaji wa Kibens, hata pale ambapo jina lake halikuandikwa k**a mtunzi rasmi.
Unyenyekevu huu wa kimya unaonyesha Msanii aliyekuwa anaweka kazi mbele ya sifa binafsi.

4. Miongoni mwa kazi alizozitunga kimyakimya lakini zikahusishwa na wengine ni:

“Likala ya Moto” ya "Blaise Bula" mtunzi halisi ni "Kibens",

“48 Heures Gecoco” kazi yake,

“Libéré” iliyosainiwa na "Sunda Bass" lakini mtunzi ni Kibens,

“J’suis Là” utunzi wake kamili.
Haya yote yanathibitisha kuwa alichangia katika misingi ya muziki wa Group kwa kiwango kikubwa kuliko inavyo fahamika na wengi.

5. Hata hivyo, licha ya mchango huu mkubwa, mvutano wa ndani ulianza kuongezeka.
Migongano ya vizazi, tamaa za haraka za Wasanii chipukizi na msuguano wa muda mrefu viligeuza mamlaka ya "Kibens" kuwa shabaha rahisi ya lawama.

6. Hali ilizidi kuwa mbaya pale ambapo tuhuma za ushirikina zilianza kumzunguka.
Baada ya vifo vya mfululizo vya wanamuziki wa kundi :
Seguin Mignon (Drums), Zulema Strangaley (Mwimbaji), na Blaise Esabe Kamba (Drums), baadhi ya Watu walitafuta maelezo ya kishirikina, na Kibens akawa mhanga wa hofu hizo za kijamii.

7. Mambo yalichochewa zaidi na kusambaa kwa sauti inayodaiwa kurekodiwa na Mjane wa marehemu "Blaise Esabe", ikimtaja "Jules Kibens" kwa maneno yasiyopendeza kabisa.
Sauti hiyo, iliposambazwa bila uchambuzi, ilizidisha tuhuma na kuimarisha mazingira ya mashaka yasiyo na msingi.

8. Hofu ilifikia kiwango ambacho JB Mpiana, akiwa na Wanamuziki wote wa Group, walilazimika kwenda kwa "Mchungaji Mukuna" kwa ajili ya maombi maalum, wakiamini kuwa kifo kilikuwa kikiizunguka Wenge BCBG.
Hatua hii ya kiroho inaonyesha ukubwa wa taharuki iliyokuwa imetanda ndani ya Group.

9. Katika mazingira haya ya uvumi, hofu na tuhuma zisizo na ushahidi, "Jules Kibens" alichagua njia ya heshima: kujiuzulu kwa hiari.
Uamuzi wake haukuwa ishara ya hatia, bali kitendo cha busara cha kujilinda dhidi ya mazingira yaliyokuwa yamepoteza utulivu.

10. Kwa kuondoka kwake, Wenge BCBG haikumpoteza tu Mwanamuziki, bali mjenzi wa sauti, mshika mizani wa utamaduni wa kundi, na nguzo ya kimya iliyokuwa imebeba historia ya muziki wao.
Kwa mashabiki, ilikuwa pigo; kwa Group, ni mabadiliko makubwa; kwa "Jules Kibens" mwenyewe huenda ni mwanzo wa pumziko jipya mbali na kelele na kivuli cha tuhuma.

1. Selon "Blanchard Mosaka", porte‑parole emblématique de "Wenge Musica BCBG", l’affaire "Jules Kibens" révèle moins une vérité qu’un mécanisme bien connu : «Lorsque l’on veut se débarrasser de son chien, on l’accuse de rage.»
À travers cette formule incisive, "Mosaka" rappelle que "Kibens"n’a jamais été un sorcier, mais un Musicien d’une intégrité rare, injustement pris pour cible dans un climat de suspicion et de désordre émotionnel.

2. Après près de vingt‑sept années de loyauté, "Jules Kibens" aurait dû quitter "Wenge BCBG" sous les applaudissements, entouré de respect et de gratitude.
Car s’il existe un Homme qui a porté l’orchestre sur ses épaules, tant sur le plan de l’arrangement que de la cohésion interne, c’est bien lui.
Il fut, selon "Mosaka", «les poumons de l’orchestration», celui par qui le souffle musical circulait.

3. L’histoire retiendra que sur cent chansons à succès du groupe, près de quatre‑vingts portent en réalité la signature artistique de "Kibens", même lorsqu’il n’en apparaît pas comme auteur officiel.
Cette discrétion, presque ascétique, témoigne d’un homme qui privilégiait l’œuvre au prestige personnel.

4. Parmi ces compositions silencieusement offertes, on retrouve des titres devenus emblématiques :
«Likala ya Moto» de "Blaise Bula", dont le véritable compositeur est "Kibens" ;
«48 Heures Gecoco», écrite par lui ;
«Libéré», attribuée à "Sunda Bass" mais née de sa plume ;
ou encore «J’suis Là», dont il est l’auteur intégral.
Autant de preuves que son empreinte traverse l’histoire du groupe comme une trame invisible.

5. Pourtant, malgré cette contribution colossale, un climat de tensions internes s’est progressivement installé.
Les rivalités générationnelles, les ambitions mal contenues et les frustrations accumulées ont transformé l’autorité naturelle de "Kibens" en cible commode pour les mécontentements.

6. La situation s’est aggravée lorsque des accusations de pratiques occultes ont commencé à circuler autour de son nom.
Dans un contexte marqué par une série de décès successifs :
"Seguin Mignon" (Drums) ,"Zulema Strangaley" (Chanteur),"Blaise Esabe Kamba",(Drums) certains ont cherché des explications irrationnelles, et "Kibens" est devenu, à tort, le réceptacle de ces peurs collectives.

7. La diffusion d’un audio attribué à la v***e de "Blaise Esabe", évoquant des griefs contre lui, a servi de catalyseur à ces soupçons.
Relayé sans nuance, cet enregistrement a nourri une atmosphère de suspicion qui ne reposait sur aucune preuve, mais sur l’émotion brute et la rumeur.

8. L’inquiétude était telle que JB Mpiana, accompagné de l’ensemble de l’orchestre, s’est rendu chez "le pasteur Mukuna" pour une séance de prière destinée à conjurer l’idée que la mort planait sur "Wenge BCBG".
Ce geste, profondément symbolique, illustre l’état de fragilité psychologique dans lequel se trouvait le groupe.

9. Face à cette spirale de rumeurs, de tensions et d’accusations infondées, "Jules Kibens" a choisi la voie de la dignité : il s’est retiré volontairement, refusant de devenir l’otage d’un climat devenu toxique.
Sa démission n’est pas un aveu, mais un acte de lucidité et de préservation.

10. Avec son départ, "Wenge BCBG" perd non seulement un musicien, mais un Architecte du son, un passeur de tradition, un pilier silencieux dont l’œuvre dépasse largement les crédits officiels.
Pour les fans, c’est un choc ; pour l’histoire du groupe, un tournant ; pour Kibens, peut‑être enfin l’occasion de respirer loin des ombres et des malentendus.

Baba L.W.L

HATUTAKI UAMUZI WA UPENDELEO KWA MOROCCO!Dhidi ya Kameruni k**a ilivyokua dhidi ya Tanzania, Morocco imenufaika na maamu...
10/01/2026

HATUTAKI UAMUZI WA UPENDELEO KWA MOROCCO!

Dhidi ya Kameruni k**a ilivyokua dhidi ya Tanzania, Morocco imenufaika na maamuzi ya waamuzi yaliyoegemea upande mmoja, yakizidisha hisia za kutokuwepo kwa usawa na ukosefu wa haki katika mchezo.

Mwamuzi wa Misri, "Amin Mohamed Omar", ndie aliyeteuliwa kusimamia robo fainali kati ya Morocco na Cameroon.
Katika hali isio eleweka CAF ilimwondoa dakika za mwisho na kumweka Mmauritania "Dahane Beida" kutokana na shinikizo la Morocco.
jambo lililozua maswali mazito kuliko majibu...

Kwa hatua hii, bora tu Morocco wapewe ubingwa moja kwa moja na basi...

KOFFI OLOMIDE KUHUSU MICHEL KUKA Mboladinga "LUMUMBA"RDC imemwaga zaidi ya milioni 50 Barcelona, Monaco na AC Milan ikit...
10/01/2026

KOFFI OLOMIDE KUHUSU MICHEL KUKA Mboladinga "LUMUMBA"

RDC imemwaga zaidi ya milioni 50 Barcelona, Monaco na AC Milan ikitafuta kutangazwa Kimataifa.

Cha ajabu kijana mmoja asiekua na gari, nyumba, wala msafara "LUMUMBA VEA", ameipa Nchi mwanga ambao hata mabilioni hayakuweza kufaanikisha.

Cha kushangaza : Alikua akisimama imara pasipo kutmka chochote. Hakutoa kauli mbiu. Ukimya wake pekee ni zaidi ya diplomasia, ni zaidi ya Mabalozi.

USHUHUDA KUHUSU MAISHA YA “KANDA BONGO MAN” SEHEMU YA PILI1. Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kabisa maishani kumwona R...
06/01/2026

USHUHUDA KUHUSU MAISHA YA “KANDA BONGO MAN”
SEHEMU YA PILI

1. Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kabisa maishani kumwona Rais Bokassa kwa macho yangu mwenyewe, tukio lililoacha alama isiyofutika moyoni mwangu.
Nilikuwa pia nimeshirikiana na "Émile Soki" katika wimbo (Animave), ingawa kwenye YouTube waliuandika vibaya k**a (Alimate).
Tulifanya kazi pamoja pia kwenye Wimbo (Folie Rose), lakini "Émile Soki" hakuweza kuutoa kwa sababu aliamua kupatana na kaka yake "Maxime Soki Vangu" na kurejea kwenye kundi Bella Bella hivyo kuutoa Wimbo huo kwa Lebo ya BELLA BELLA.

2. Ndugu hao wawili walikuwa wakigombana mara kwa mara kiasi kwamba familia yao ililazimika kuingilia kati ili kupunguza mvutano.
"Émile Soki" aliondoka (Bella Mambo Rénové) pamoja na wanamuziki takriban wote na kujiunga na (Bella Bella).
Mimi binafsi sikuandamana nao, nikiwa na mashaka makubwa kuhusu mustakabali wangu wa baadae.

3. Siku moja, nikiwa nyumbani nikiangalia TV, nilimuona Bwana "Katalay", aliyewahi kuwa Meneja wa "Dokta Niko Kassanda", akitangaza kurejea kwake kutoka Ulaya akiwa na vifaa vipya vya muziki na akisema anatafuta vijana wa kuwaajiri.
Nilimfuata mara moja, na baada ya mazungumzo, alikubali kuwa Meneja wangu.

4. Hapo ndipo nilipoanzisha Group langu mwenyewe, (Bana Mambo).
Nilitaka kubakiza jina (Mambo) ili kuonyesha chimbuko langu kutoka (Bella Mambo Rénové).
Ndani ya Group langu, Mpiga Solo alikuwa si mwingine bali "Diblo Dibala".
"Bwana Katalay", Mtu wa uadilifu wa hali ya juu, alikuwa akishika wadhifa mkubwa katika kampuni ya Kiitaliano Franco Plast, ambako alikuwa Mkurugenzi Mkuu.

5. Alinichukulia k**a Mwanawe mwenyewe; wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 18 tu.
Alinilipia tiketi ya ndege kwenda Italy, na tulipofika huko akanipa fedha za kununua vifaa vipya vya muziki.
Baada ya kukaa Italy, nilitembelea pia Ubelgiji na Ufaransa kabla ya kurejea Kinshasa.
Kabla ya kujiunga na (Bella Mambo), nilikuwa nikifanya mazoezi na Bazou katika mtaa wa Kanda Kanda, pamoja na Papa Wemba na Groupe lake la Viva la Musica, Bisikita na Donnat Mobeti.

6. Niliporejea kutoka Ulaya, nilileta vifaa kamili vya muziki ambavyo hata "Papa Wemba" alikuwa akivikopa mara kwa mara kwa ajili ya mazoezi.
Urafiki wangu na mdogo wake "Papa Wemba" ajulikane kwa jina la "Dio" ulifanya jambo hilo kuwa la kawaida kabisa.
Hata hivyo, kwa kuwa (Bana Mambo) haikupata mafanikio tuliyotarajia, nilianza kufikiria kurudi Ulaya kuendelea na masomo.

7. Kabla sijasafiri, "Vieux Soki Vangu" alifika nyumbani kwangu akiniomba nimsaidie kuimba kwenye harusi kwa sababu "Émile Soki" alikuwa mgonjwa.
Nilikubali, na onyesho lilifanikiwa sana chini ya uongozi wa "Vieux Shaba Kahamba".

8. Tamasha letu la pili na Groupe (Bella Bella) lilifanyika katika Ukumbi wa Confidence Bar jijini Kinshasa.
Baada ya onyesho, nilimweleza "Soki Vangu" kuwa nilikusudia kuondoka kuelekea Ulaya.
Alijaribu kunizuia, lakini uamuzi wangu ulikuwa tayari umekamilika kwani nilikuwa nimeshanunua tiketi.
Mwaka 1978 nilisafiri kwenda Paris, ambako maisha yalikuwa magumu kupindukia.
Ningewezaje kuendelea na masomo nikiwa na changamoto za makazi, chakula na ada za chuo?

9. Wakati ule, Wazaire walikuwa wachache sana jijini Paris.
Nilifanya kazi kwa mwaka mzima ili kupata kibali cha kuishi na kufanya kazi.
Wakati huohuo, "Diblo Dibala" naye alikuwa akitafuta njia ya kuondoka Kinshasa kuja Ulaya.
Nilipowasili Paris, nyimbo zilizotikisa zilikuwa zikitia fora ni (Gergette Eckins) ya "Sam Mangwana", (Double Double) ya "Kanta Nyboma", na (Amio) ya "Bébé Manga".
"Diblo Dibala" alipopata viza ya Ubelgiji, alishukia kwenye Mjini wa (Mons), ambako nilimshauri ajiunge nami Paris.

10. Tukiwa Paris na "Diblo Dibala", tulirekodi wimbo (Iyole) kwenye kaseti.
Kisha nikaenda kumuona "Bwana Eddy Gustave", Producer wa "Sam Mangwana".
Baada ya kuusikiliza, alisema haukumvutia na akaniambia nijaribu mtindo wa rumba k**a aimbavyo "Sam Mangwana".
Laa sivyo usipime tena kurudia hapa kwangu.
Lakini sisi tulikuwa tumejikita kwenye mtindo wa (Ngwasuma Soukous).
Baadae nilimwona "Bi Lacoste", Producer wa "Mpongo Love", nae pia alikataa kunisaidia, akisema ningepaswa kuimba k**a "Mpongo Love" ili anisaidie.

11. Hatimaye, nilikutana na rafiki yangu "Narcisse", akiwa na Mtu wake wa karibu aitwaye "David Ouattara", mwenye duka la kuuza kanda za muziki.
Nilipo msikilizisha wimbo (Iyole), "David Ouattara" alivutiwa mara moja na mtindo wetu wa soukous na akakubali kufadhili kurekodi.
Akauliza utaratibu wa kuingia studio, nikamweleza, naye akaukubali.
Tuliingia studio Caroline jijini Paris na wanamuziki hawa:
— Solo : Diblo Dibala
— Rhythm : Aimé Kobo
— Bass : Miguel Yamba

Tukatoa diski yenye nyimbo nne:
Face A: 1. Iyole ; 2. N’Sambi-Carol
Face B: 1. Amini ; 2. Mazina

Ninakiri kwamba, hata nikitazama kazi zangu zote, sijawahi kutoa album iliyokamilika kiasi hicho: kwa siku mbili tu za studio tulizalisha kazi ya kiwango cha juu ajabu.

12. Sifa nyingi zinamwendea "Diblo Dibala", ambae alicheza gitaa kwa ustadi wa hali ya juu.
Changamoto iliyobaki ilikuwa jinsi ya kufanya matangazo.
Tulizungumza na "David Ouattara", ambae alipendekeza tushirikiane na Wanamuziki wa Ivory Coast, waliokuwa mashuhuri kwa uwezo wao wa kutangaza kazi za muziki.
Walikutana katika matukio yanayoitwa dédicaces, ambako walitathmini Wasanii jukwaani na, wakiridhika, walitangaza kazi zao kwa nguvu kubwa.

13. Tukaamua kuhudhuria mkutano wa dédicaces siku ya Jumamosi.
Baada ya Wasanii kadhaa kuonyesha kazi zao, nami niliitwa nijitambulishe.
Nilipopanda jukwaani, niliwasha moto hadi Umati wote ulisimama kwa shangwe.
Wakauliza mimi ni raia wa nchi gani, na "David Ouattara" akawaambia kuwa natoka Zaire.

14. Watu walitaka mara moja kujua jinsi ya kupata nakala za kanda zetu.
"David Ouattara" aliwaeleza kuwa duka lake hufungwa Jumapili na lingeweza kufunguliwa Jumatatu.
Walikataa kabisa: walitaka afungue kesho yake, bila kukosa.
Bila kusita, David alikubali.

15.
Jumapili asubuhi, David Ouattara alipofungua duka, alikuta foleni kubwa ya watu waliomiminika kununua nakala zote.
Muziki wetu ulipokelewa kwa shangwe kubwa, na kanda zote zikaisha papo hapo.
Habari zilipomfikia "Eddy Gustave" yuleyule aliyekataa kutusaidia hapo awali, alikuja kuniomba niwe chini ya uongozi wake k**a Producer.
Nikajibu kuwa jambo hilo halingewezekana kamwe, kwa sababu nilibaki mwaminifu kwa "David Ouattara" aliyenisaidia katika nyakati ngumu.
Alisisitiza, hata akapendekeza kuchukua mawakili iwapo ningekubali.
Nikamwambia aache kupoteza muda.

Itaendelea...

TÉMOIGNAGE SUR LA VIE DE « KANDA BONGO MAN
DEUXIEME PARTIE

1. Ce fut la toute première fois de ma vie que je vis le président "Bokassa" de mes propres yeux, un événement qui laissa en moi une empreinte indélébile.
J’avais également collaboré avec "Émile Soki" sur le titre (Animave), bien que celui-ci ait été mal orthographié (Alimate) sur YouTube.
Nous avions aussi travaillé ensemble sur (Folie Rose), mais Émile Soki ne put en assurer la sortie, ayant choisi de se réconcilier avec son frère Maxime Soki Vangu et de réintégrer le groupe Bella Bella.

2. Ces deux Frères se querellaient fréquemment, au point que leur famille devait régulièrement intervenir pour tenter d’apaiser les tensions.
Émile Soki quitta alors (Bella Mambo Rénové) avec l’ensemble des musiciens pour rejoindre (Bella Bella).
Pour ma part, je ne les suivis pas, hésitant profondément quant à mon avenir.

3. Un jour, alors que je regardais la télévision chez moi, j’aperçus "M. Katalay", ancien manager du "Docteur Niko Kassanda", annonçant son retour d’Europe avec de nouveaux instruments de musique et déclarant rechercher de jeunes artistes à engager.
Je me rendis aussitôt auprès de lui et, après un entretien, il accepta de devenir mon manager.

4. C’est ainsi que je fondai mon propre groupe, (Bana Mambo).
Je tenais à conserver le nom Mambo afin de rappeler mes origines au sein de (Bella Mambo Rénové).
Dans mon groupe, le guitariste solo n’était autre que Diblo Dibala.
M. Katalay, homme d’une grande probité, occupait alors un poste de haute responsabilité au sein de la société italienne Franco Plast, dont il était le directeur général.

5. Il me considérait comme son propre fils ; je n’avais alors que 18 ans.
Il finança mon billet d’avion pour l’Italie et, une fois sur place, me remit de l’argent afin que j’y achète des instruments neufs.
Après mon séjour en Italie, je visitai également la Belgique et la France, avant de regagner Kinshasa.
Avant d’intégrer (Bella Mambo), je m’exerçais avec Bazou dans le quartier de Kanda Kanda, aux côtés de "Papa Wemba" avec son "Viva la Musica", "Bisikita" et "Donnat Mobeti".

6. À mon retour d’Europe, j’apportai un équipement musical complet, que même "Papa Wemba" empruntait régulièrement pour ses répétitions.
Mon amitié avec son jeune Frère Dio rendait cela tout à fait naturel.
Cependant, (Bana Mambo) ne rencontrant pas le succès espéré, je commençai à envisager un retour en Europe afin de poursuivre mes études.

7. Avant mon départ, "Vieux Soki Vangu" vint me chercher chez moi : il souhaitait que je remplace au chant "Émile Soki" lors d’un mariage, car il était malade.
J’acceptai, et la prestation fut un véritable succès, sous la direction de "Vieux Shaba Kahamba".

8. Notre second concert avec (Bella Bella) eut lieu au Confidence Bar de Kinshasa.
À l’issue de la représentation, j’informai "Soki Vangu" de mon intention de repartir pour l’Europe.
Il tenta de me dissuader, mais ma décision était irrévocable, mon billet étant déjà acheté.
En 1978, je m’envolai pour Paris, où la vie se révéla extrêmement difficile.
Comment poursuivre mes études dans de telles conditions, entre logement précaire, manque de nourriture et frais universitaires ?

9. À cette époque, les Zaïrois étaient très peu nombreux à Paris.
Je travaillai une année entière afin d’obtenir un permis de séjour et de travail.
Pendant ce temps, "Diblo Dibala" cherchait lui aussi un moyen de quitter Kinshasa pour l’Europe.
À mon arrivée à Paris, les titres en vogue étaient (Gergette Eckins) de "Sam Mangwana", (Double Double) de "Kanta Nyboma", et (Amio) de "Bébé Manga".
Lorsque "Diblo Dibala" obtint un visa pour la Belgique, il atterrit à Mons, d’où je l’encourageai à me rejoindre à Paris.

10. À Paris, nous enregistrâmes le titre (Iyole) sur cassette.
Je me rendis ensuite chez "M. Eddy Gustave", Producteur de "Sam Mangwana".
Après écoute, il déclara ne pas apprécier le morceau et me suggéra d’adopter un style Rumba similaire à celui de "Sam Mangwana".
Pourtant, notre orientation musicale relevait clairement du (Ngwasuma Soukous).
Je rencontrai ensuite "Mme Lacoste", Productrice de "Mpongo Love", qui refusa elle aussi de me soutenir, estimant que je devrais chanter dans le style de "Mpongo Love" pour bénéficier de son appui.

11. Finalement, je rencontrai mon ami "Narcisse", accompagné d’un certain "David Ouattara", propriétaire d’une boutique de disques.
Lorsque je lui fis écouter (Iyole), "David Ouattara" fut immédiatement séduit par notre soukous et accepta de financer l’enregistrement.
Il me demanda l’organisation nécessaire pour entrer en studio, et je lui exposai le plan, qu’il approuva.
Nous enregistrâmes au studio Caroline à Paris, avec les musiciens suivants :
— Solo : Diblo Dibala
— Rythmique : Aimé Kobo
— Basse : Miguel Yamba

Nous produisîmes un disque de quatre titres :
Face A : 1. Iyole ; 2. N’Sambi-Carol
Face B : 1. Amini ; 2. Mazina

Je dois reconnaître que, même en considérant l’ensemble de ma carrière, je n’ai jamais sorti un album aussi abouti : en seulement deux jours de studio, nous avions créé une œuvre d’une qualité remarquable.

12. Une grande part du mérite revient à "Diblo Dibala", dont la virtuosité à la guitare fut exceptionnelle.
Restait la question de la promotion.
Nous en discutâmes avec David Ouattara, qui proposa de nous associer à des musiciens ivoiriens, réputés pour leur maîtrise de la publicité musicale.
Ils se réunissaient lors d’événements appelés dédicaces, où ils évaluaient les artistes sur scène et, s’ils étaient convaincus, assuraient la promotion de leurs œuvres.

13. Nous décidâmes donc d’assister à une séance de dédicaces un samedi.
Après les prestations de plusieurs artistes, je fus invité à me présenter.
Dès que je montai sur scène, je mis littéralement le feu : le public se leva, enthousiaste.
On demanda alors de quelle nationalité j’étais, et "David Ouattara" répondit que je venais du Zaïre.

14. Le public voulut immédiatement savoir comment se procurer nos cassettes.
"David Ouattara" leur expliqua que sa boutique était habituellement fermée le dimanche et qu’ils devraient attendre le lundi.
Ils refusèrent catégoriquement : il devait impérativement ouvrir dès le lendemain.
Sans hésiter, David accepta leur requête.

15. Le dimanche matin, lorsqu’il ouvrit sa boutique, David Ouattara découvrit une foule immense qui se précipita pour acheter toutes les copies disponibles.
Notre musique fut accueillie avec un enthousiasme extraordinaire, et les cassettes furent épuisées en un instant.
Lorsque la nouvelle parvint à "Eddy Gustave" le même producteur qui nous avait auparavant refusé tout soutien, il vint me solliciter pour devenir mon Producteur.
Je lui répondis que cela n’arriverait jamais, par fidélité envers "David Ouattara", qui m’avait aidé dans les moments les plus difficiles.
Il insista, allant jusqu’à proposer de prendre des avocats si j’acceptais son offre.
Je lui rétorquai qu’il perdait son temps.
A suivre

Baba L.W.L

USHUHUDA WA MAISHA YA "KANDA BONGO MAN" SEHEMU YA KWANZA. TUNAWATAKIENI HERI YA MWAKA MPYA 20261. Ninaitwa Kanda Bongo; ...
02/01/2026

USHUHUDA WA MAISHA YA "KANDA BONGO MAN" SEHEMU YA KWANZA. TUNAWATAKIENI HERI YA MWAKA MPYA 2026
1. Ninaitwa Kanda Bongo; neno Man ni jina la Aka lililoongezwa baadae.
Nilizaliwa Inongo, katika eneo la ziwa Mai‑Ndombe Inchini Congo, ambako nilikulia na kusoma.

2. Wakati wa likizo ndefu za shule, nilikua nafunga safiri mara kwa mara kwenda Kinshasa.
Nilipofika Mjini, shughuli yangu kuu ilikuwa muziki, ambao tayari ulikuwa shauku yangu kubwa.

3. Utotoni, nilikuwa Mpenzi mkubwa wa orkesta Bella Bella. Kadri nilipokua mkubwa, nilianza pia kuvutiwa na Afrisa International ya Tabu Ley pamoja na OK Jazz ya Franco Luambo Makiadi.
Hata hivyo, "BELLA BELLA" iliendelea kubaki ndani yangu k**a alama isiyofutika.

4. Nilianza rasmi muziki wakati wa likizo hizo, nikishiriki mazoezi ya orkesta "Tao Tao" katika Manispaa ya Bandalungwa (BANDAL). Wakati huo, wanamuziki kadhaa waliondoka "BELLA BELLA": ntawataja "BISIKITA" na "KAYEMBE" wakaanzisha Group lao nakulipa jina la "MAKOSO" huko Matonge.

5. Wakati huohuo, vijana wawili, "NZUBE" na "SOUZA" walikua wakifahamiana na Jamaa mmoja ambae alikua Sonara fundi wa dhahabu aitwaye "BAZOU", yeye aliyetamani sana kumiliki orkestra ili kusaidia vijana.

Ilikupata kukamilisha mahitaji ya "BAZOU", "NZUBE" na "SOUZA" Wakaja hadi "Bandal" sehemu yetu ya mazoezi na kutushawishi kuungana na "BAZOU", ndivyo tukaondoka Group nzima la "TAO TAO" nakuhamia kwenye Manispaa ya MATONGE, nyumbani kwao "SOUZA" ambako ikawa sehemu yetu ya mazoezi.

6. Sehemu yatu ya mazoezi nyumbani kwao "SOUZA" ilikua jirani sana na kwa Mwanamuziki "BISIKITA".
Sasa Kadri tulivyoendelea kufanya mazoezi, "BISIKITA" na "KAYEMBE" walisikia sauti yangu na kupendezwa sana na aina ya uimbaji wangu, wakadai kwamba unafanana sana na Uimbaji wa Orchestra "BELLA BELLA" huko waliko tokea wao.
Ndipo wakaanza kunishawishi niungane nao kwenye Group "MAKOSO", hata hivyo "SOUZA" akawa anapinga vikali wazo k**a hilo.

7. Kwa kuwa nilitamani sana kuendelea na kukua kimuziki, niliamua mwenyewe kuondoka "TAO TAO" na kwenda kujiunga na Group "MAKOSO" ilikua Mwaka 1972.
Mwaka 1973, nilijiunga na Group "BELLA MAMBO RENOVE" ikiwa chini ya uongozi wa "ÉMILE SOKI DIANZENZA", mdogo wake "SOKI VANGU".

8. Wakati najiunga "BELLA MAMBO RENOVE", niliwakuta wanamuziki hawa:

Waimbaji : Émile Soki Dianzenza, Milano Nzoyi

Gitaa la solo : Sebos

Gitaa Rhytm : Mazé

Drums : Ziatou

Bass : Samoy

9. Wimbo wa kwanza tuliouimba uliitwa "KALANDA", ambao hapo awali uliitwa "LOFESE".
Bali Kamati ya ukaguzi, iliyokuwa kali sana wakati wa utawala wa Mobutu, ilikataa jina hilo.
Tulipolibadirisha kuwa "KALANDA", jina hilo lilikubaliwa.
Tulirekodi wimbo huo katika studio ya mzee "BOKILO" huko manispaa ya Lemba, na ukawa maarufu sana yaani ulitokea kuwa TUBE.
Nilifaanikiwa kutunga pia wimbo "MAZINA", lakini Watu hawakujua kuwa mimi ndie mtunzi; walimhusisha nao "ÉMILE SOKI".
Ilikuja fahamika kuwa ni utunzi wangu nilipoonekana kwenye kipindi cha "KIN SHOW" kilichoendeshwa na Mtangazaji "KAYUMBI BEYA".

10. Nilifikaje kwenye televisheni? Kwa hapa ni hadithi ndefu.
Siku hiyo, Rais "BOKASSA" wa "CENTRAL AFRICAN REPUBLIC" alikuwa dhiarani Inchini "ZAIRE" kwa Rais "MOBUTU SESESEKO KUKUNGBENDU WAZABANGA" na alitamani sana kushuhudia live kipindi cha "KIN SHOW".
Ili apate kumridhisha mgeni wake rasmi, "Rais Mobutu" aliwatuma wanajeshi kuwaleta kwa nguvu Wanamuziki.

Gari la kijeshi lilifika nyumbani kwetu na nikaamriwa kupanda. Ndani kulikuwa na Mwanamuziki wa Group "EMPIRE BAKUBA" ambae nimesahau jina lake na BIMI OMBALE" wa Zaïko Langa Langa, yeye alik**atwa akiwa anatengeneza gari lake.

Tulipofika kwenye kituo cha TV "Télé Zaïre", tuliwakuta wachekeshaji "MANGOBO" na "MONZALI", pamoja na Group "KOSA KOSA" wakiwa tayar kwa burudani.

Rais "BOKASSA" alipoingia, niliimba wimbo "MAZINA" ikawa ndo kwa mara ya kwanza nauimba mbele ya Umma, na hapo ndipo Watu walipogundua kuwa nimimi ndiye mtunzi halisi.

TEMOIGNAGE DE KANDA BONGO MAN.
1. Je me nomme Kanda Bongo ; le terme Man n’est qu’un surnom ajouté ultérieurement.
Je suis né à Inongo, dans la région du lac Mai‑Ndombe, où j’ai grandi et poursuivi mes études.

2. Durant les grandes vacances scolaires, je me rendais régulièrement à Kinshasa.
Une fois dans la capitale, ma principale occupation était la musique, qui constituait déjà le centre de mes intérêts.

3. Dans ma jeunesse, j’étais un fervent admirateur de l’orchestre BELLA BELLA.

En mûrissant, je me suis progressivement intéressé à L'AFRISA INTERNATIONAL" de "TABU LEY", ainsi qu’à "l’OK JAZZ".
Toutefois, BELLA BELLA demeurait profondément ancré en moi.

4. J’ai véritablement commencé la musique au cours de ces séjours de vacances, en participant aux répétitions de l’orchestre "TAO TAO", basé dans la commune de Bandalungwa.
À cette époque, plusieurs musiciens quittèrent "BELLA BELLA" : "BISIKITA et KAYEMBE" partirent fonder leur propre formation, "MAKOSO" à Matonge.

5. Parallèlement, deux jeunes, "NZUBE" et "SOUZA", connaissaient un bijoutier nommé "BAZOU", désireux de devenir propriétaire d’un orchestre pour soutenir la jeunesse musicale.

Ils vinrent alors à Bandal recruter l’ensemble de "TAO TAO" et nous emmener à Matonge, où nous répétions dans la maison de "SOUZA", voisine de celle de "BISIKITA".

6. À force de répétitions, "BISIKITA" et "KAYEMBE" remarquèrent le timbre de ma voix, qu’ils jugeaient parfaitement adapté à "BELLA BELLA". "BISIKITA" me sollicita pour rejoindre "MAKOSO", mais "SOUZA" refusa catégoriquement cette proposition.

7. Désireux d’évoluer, je quittai finalement "TAO TAO" pour intégrer "MAKOSO" aux côtés de "BISIKITA" en 1972.
En 1973, je rejoignis l’orchestre "BELLA MAMBO RENOVE", dirigé par "ÉMILE SOKI DIANZENZA", Frère cadet de "SOKI VANGU".

8. Au sein de "BELLA MAMBO RENOVE", je trouvai les musiciens suivants :

Chanteurs : "ÉMILE SOKI DIANZENZA", "MILANO NZOYI"

Guitare solo : "SEBA SEBOS"

Guitare accompagnement : "MAZE"

Batterie : "ZIATOU"

Basse : "SAMOY"

9. La première chanson que nous interprétâmes s’intitulait "KALANDA", initialement nommée "LOFESE".
La commission de censure, très stricte sous "MOBUTU", refusa ce titre.
Après modification, "KALANDA" fut accepté.
Nous l’enregistrâmes au studio du vieux "BOKILO", à Lemba, et le morceau connut un immense succès.

J’avais également composé "MAZINA", dont le public ignorait que j’étais l’auteur, l’attribuant à "ÉMILE SOKI".
Ce n’est que lors de mon passage à la télévision, dans l’émission "KIK SHOW" animée par "KAYUMBI BEYA", que l’on découvrit ma paternité du titre.

10. Comment suis‑je passé à la télévision ?
Ce fut toute une histoire.
Le Président "BOKASSA" de Centrafrique était en visite officielle auprès du Président "MOBUTU" et souhaitait assister en direct à "KIN SHOW".

Pour satisfaire son hôte, "MOBUTU" envoya des militaires réquisitionner plusieurs musiciens.
Un jeep militaire arriva chez moi ; on m’ordonna de monter.
Dans le véhicule se trouvaient un musicien "d’EMPIRE BAKUBA" et "BIMI OMBALE" de Zaïko Langa Langa, embarqué alors qu’il réparait sa voiture.

Arrivés à Télé Zaïre, nous trouvâmes les humoristes "MANGOBO" et "MONZALI", ainsi que l’orchestre "KOSA KOSA" mis à notre disposition.
Lorsque tout fut prêt, Le Président "BOKASSA" fit son entrée.
Ce fut la première fois que j’interprétai "MAZINA" en public, révélant ainsi que j’en étais le véritable compositeur.

ITANDELEA...

BABA L.W.L

FALLY IPUPA Fally Ipupa, 🦅 atafanya historia kwa mara mbili mfululizo kwenye Uwanja wa Stade de France. Tarehe 2 Mei 202...
04/12/2025

FALLY IPUPA
Fally Ipupa, 🦅 atafanya historia kwa mara mbili mfululizo kwenye Uwanja wa Stade de France. Tarehe 2 Mei 2026 na tena tarehe 3 Mei 2026, Muziki wa rumba la Kongo utatawala uwanja mkubwa wa dunia.

Hii siyo tu sherehe ya miaka ishirini ya kazi yake ya Muziki, bali ni ushindi wa utamaduni wa Afrika, ushahidi kwamba sauti zetu zinaweza kufikia kilele cha heshima na hadhi ya kimataifa.

Fally Ipupa, figure emblématique de la rumba congolaise contemporaine, s’apprête à inscrire son nom dans les annales de la musique mondiale.

Le Stade de France, temple des grandes légendes, vibrera à ses accents le samedi 2 mai 2026, puis à nouveau le dimanche 3 mai 2026, pour célébrer deux décennies d’une carrière exceptionnelle.

Ce doublé, fruit d’un engouement populaire sans précédent, consacre non seulement l’artiste, mais aussi la puissance créatrice de la scène africaine, désormais hissée au rang des références universelles.

L.W.L

22/10/2025

Adresse

Avenue D'ORADOUR SUR GLANE
Bonneuil-sur-Marne
94380

Téléphone

33668312952

Site Web

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Lubonji Wa Lubonji publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Contacter La Pratique

Envoyer un message à Lubonji Wa Lubonji:

Partager

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram