12/04/2026
HADITHI YA REBO TCHULO
L'HISTOIRE DE REBO TCHULO
Amezaliwa mwaka 1997 mjini Kinshasa, Rebo Tshulo, ambae jina lake halisi ni Déborah, ni miongoni mwa Wasanii wa kizazi kipya walioleta upekee mpya katika Muziki wa Congo.
Kalelewa katika mazingira yenye mchanganyiko wa ibada za kidini na harakati za kisanii za jiji, jambo lililomjengea msingi wa kipaji chake tokea utotoni.
Lwanzoni kaanza kufahamika kwa jina la Rebelle (Muasi) na hapo baadae akaja kuibuka na jina la Kisanii la "Rebo", ambalo likaja kuwa alama ya safari yake ya ubunifu.
Umaarufu wake uliongezeka mwishoni mwa miaka ya 2010, hasa baada ya kushirikiana na Ferré Gola mwaka 2019.
Aina yake ya Muziki inayochanganya Afrobeat, Rumba ya kisasa na ladha ya Pop ya mijini ulimfanya kuwa Msanii mwenye mvuto wa kipekee.
Nyimbo zake k**a “Pepele”, “Mboté”, “Contaminée”, “Mukaji Internationale”, pamoja na “Loketo Remix” iliyotamba sana kwenye TikTok mwaka 2023, zilimpa nafasi ya pekee katika Tasnia ya Muziki.
Mwaka 2024, alithibitisha umahiri wake kupitia “Choquer”, uliotazamwa zaidi ya mara milioni tatu.
Katika maisha yake binafsi, Rebo aliwahi kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na Msanii Innoss’B, na pamoja wakabarikiwa kupata mtoto.
Ingawa kwa sasa wametengana, hatua hiyo imebaki kuwa sehemu muhimu ya historia yake, bila kupunguza nguvu ya safari yake ya Kisanii.
Safari yake imeendelea kuimarika kupitia ushirikiano wake na wa Sanii wengine wenye majina yao k**a Innoss’B, Samarino, Awilo Longomba, Yemi Alade na Ferré Gola.
Akiwa amevutiwa na Wanamuziki k**a Fally Ipupa na Barbara Kanam, Rebo ameweza kuunganisha urithi wa Congo na mitindo ya kisasa kwa ustadi wa hali ya juu.
Mwaka 2023, ushiriki wake katika tamasha la kibinadamu Umoja huko Brussels ndo ukawa hatua muhimu katika kupanua upeo wake wa kimataifa.
Mwaka 2025, aliandika historia kwa kuwa Mwanamke wa kwanza wa Congo kusaini mkataba na Def Jam Africa, jambo lililothibitisha nafasi yake k**a Msanii mwenye ushawishi mkubwa na mwakilishi wa kizazi kipya cha Muziki wa Congo.
Version Française :
HISTOIRE DE REBO TCHULO
Née en 1997 à Kinshasa, Rebo Tshulo, dont le nom civil est Déborah, appartient à cette génération d’artistes congolaises qui ont introduit une singularité nouvelle dans le paysage musical de la RDC.
Elle a grandi dans un environnement où se mêlaient la ferveur des pratiques religieuses et l’effervescence artistique de la capitale, un contexte qui a façonné dès l’enfance les fondations de son talent.
À ses débuts, elle se fait connaître sous le nom de Rebelle (Muasi), avant d’adopter plus t**d le nom de scène «Rebo», qui deviendra l’emblème de son identité créative et de son parcours artistique.
Son ascension s’accélère à la fin des années 2010, notamment après sa collaboration avec Ferré Gola en 2019.
Son style musical, qui marie afrobeat, rumba contemporaine et esthétique pop urbaine, lui confère une aura singulière et un charme artistique distinctif.
Des titres tels que «Pepele», «Mboté», «Contaminée», «Mukaji Internationale», ainsi que «Loketo Remix», devenu viral sur TikTok en 2023, lui ouvrent une place privilégiée au sein de l’industrie musicale congolaise.
En 2024, elle confirme son talent avec le titre «Choquer», qui dépasse les trois millions de vues.
Sur le plan personnel, Rebo a vécu une relation amoureuse avec le chanteur Innoss’B, relation dont est né un enfant.
Bien qu’ils soient aujourd’hui séparés, cet épisode demeure une composante importante de son histoire, sans jamais diminuer la force ni l’autonomie de sa trajectoire artistique.
Sa carrière continue de s’enrichir grâce à des collaborations avec des artistes de renom tels qu’Innoss’B, Samarino, Awilo Longomba, Yemi Alade et Ferré Gola.
Inspirée par des figures majeures comme Fally Ipupa et Barbara Kanam, Rebo parvient à unir avec finesse l’héritage musical congolais et les tendances contemporaines, témoignant d’une maîtrise artistique remarquable.
En 2023, sa participation au concert humanitaire Umoja à Bruxelles marque une étape décisive dans l’élargissement de son rayonnement international.
Puis, en 2025, elle inscrit son nom dans l’histoire en devenant la première femme congolaise à signer avec Def Jam Africa, consacrant ainsi son statut d’artiste influente et de représentante emblématique du renouveau musical féminin en RDC.
BABA L.W.L