Daktari Mwaka

Daktari Mwaka A Qualified Doctor,Starseed,life coach,an astrologer �

Kabla hujafikiria kukata tamaa kwenye haya maisha..Hebu angalia  nywele zinazoota sehemu ya haja kubwa.Licha ya mazingir...
30/09/2025

Kabla hujafikiria kukata tamaa kwenye haya maisha..

Hebu angalia nywele zinazoota sehemu ya haja kubwa.

Licha ya mazingira magumu, bado zinaendelea kukua.

TAFAKARI HAYA K**A CHACHU YA MAISHA YAKO.1. Ndege wote hukimbia mvua ila tai huruka juu ya mawingu. Changamoto ni kawaid...
29/09/2025

TAFAKARI HAYA K**A CHACHU YA MAISHA YAKO.

1. Ndege wote hukimbia mvua ila tai huruka juu ya mawingu. Changamoto ni kawaida kwenye maisha yako, mtazamo ndio huamua.

2. Meli huzama si kwa maji yaliyo nje yake, bali kwa maji yanayoingia ndani
yake. Linda amani yako ya ndani.

3. Haijawahi kuwa wimbo unaokufanya ubebe hisia, bali kumbukumbu na watu unaokumbushwa nao ndo wanaongoza Hisia zako.

4. U-perfect (Perfectionism) mara nyingi hupelekea msongo wa mawazo, kuchoka kupita kiasi, na hata msongo wa kiakili (depression). Usitake kilakitu kiwe Perfect ndipo uanze.
5. Takribani 80% ya mazungumzo ya makundi huwa ni malalamiko tu.
Pata mda wakukaa Mwenyewe na utafakari Maisha yako, Punguza muda wa kukaa kwenye makundi.

Usisahau ku share kwa uwapendao..✍️

Happy Moon Day

*MWANAUME* mmoja alimuuliza daktari:"Daktari, sielewi ... Mpenzi wangu ni mjamzito, lakini nimekuwa nikitumia kondomu, n...
22/09/2025

*MWANAUME* mmoja alimuuliza daktari:
"Daktari, sielewi ... Mpenzi wangu ni mjamzito, lakini nimekuwa nikitumia kondomu, na haijawahi kupasuka!"

Daktari alijibu kwa utulivu na hadithi:
"Hapo zamani za kale, kulikuwa na mwindaji ambaye kila mara aliingia msituni na bunduki yake.

Asubuhi moja akiwa amekengeushwa, alifanya makosa na kuchukua mwavuli badala ya silaha yake.

Akiwa katikati ya msitu, alikutana uso kwa uso na simba.

Kwa hasira, alinyoosha mwavuli wake na kujifanya anapiga risasi ... na simba akaanguka na kufa.

Kwa mshangao, mtu huyo akasema:
"Lakini huu ni upuuzi! Sio mwavuli ulioua simba.

🧏🏼👉 *kumbe mwanaume mwingine alimpiga risasi!"*

*Daktari alitabasamu na kuhitimisha: ```Hapo, umeipata*```

Mgonjwa anayefuata, tafadhali ingia."

I learned long ago, never to wrestle with a pig. You get dirty, and besides, the pig likes it.George Bernard Shaw
20/09/2025

I learned long ago, never to wrestle with a pig. You get dirty, and besides, the pig likes it.

George Bernard Shaw

Kuna wakati unajitahidi kutabasamu na kujifariji kwamba labda maumivu yako yatatulia siku moja…Lakini kila asubuhi, mial...
20/09/2025

Kuna wakati unajitahidi kutabasamu na kujifariji kwamba labda maumivu yako yatatulia siku moja…

Lakini kila asubuhi, miale ya moto inafukuta kifuani pako. Uvumilivu unakushinda. Dalili za kushindwa zinazidi kukaribia.

Ndani yako umeshakata tamaa, ila hofu ya kudhalilika mbele ya ndugu na jamaa inakulazimisha kuendelea kujipa moyo kwamba labda siku moja utanyamaza.

👉 Lakini je, unajua maumivu yako yamefika hatua ipi ya emotional instability?

Unapokwenda kuomba ushauri kumbuka:

Wapo wanaobeba trauma za utotoni kutokana na ndoa za wazazi.

Wapo waliobeba maumivu ya breakups kwa sababu ya usaliti.

Wapo waliogubikwa na betrayal & revenge, hawana amani kabisa.

Wapo wenye negatives kuhusu ndoa, hawana imani tena na upendo.

Na wapo walioamua moyoni mwao kwamba hawatadumu kwenye mapenzi, ambao hao ni hatari zaidi.

Kwa hiyo, kuomba ushauri ni jambo moja, lakini kumuomba mtu sahihi ni jambo lingine.

Be smart. Si kila kitu kitafanywa na Mungu moja kwa moja, vingine vinahitaji wewe utoe hatua, ndipo Mungu aingi.

Kindly follow me Daktari Mwaka

Kabla hujaenda out weekend natamani kukuambia hivi....Ukiona unataka ueleweke na kila mmoja ukubalike kila mahali na uki...
19/09/2025

Kabla hujaenda out weekend natamani kukuambia hivi....

Ukiona unataka ueleweke na kila mmoja ukubalike kila mahali na ukijiona wewe unajua kila kitu hata kwa usiyoyajua amini nakuambia wewe ni mgonjwa!

Hakuna anaejua kila kitu hakuna anaefiti kila mahali hayupo anaekubalika na watu wote.
Unaweza kuwa muhimu lkn sio mara zote na sio kwa watu wote.
Unaweza kupatia lkn hii haikufanyi usikosee
Kukosea ndio njia ya kwenda kwenye usahihi
kukosolewa ni sehemu ya ukuaji.

Nimewahi kusema mara kadhaa hasa kwa wafuasi wa Fb aina ya vitu tunachagua kusoma au watu tuliochagua kuwafuatilia wanachangia pakubwa mno kuongeza muyumbo wa Akili mkiamini kwamba mnapata nafuu kumbe mnakuwa mmejiunga kwenye kingenge cha watu wenye maumivu mbali mbali hivo mnakazi ya kusapotiana kupitia kila hatua itayomgusa mmoja wenu.

Unachosoma, unacho kula unaoambatana nao na kushirikiana nao wana nafasi kubwa ya kukujenga au kukubomoa usitegemee kupona k**a Mwl wako ni mgonjwa.

*TOFAUTI KATI YA KUONGEA NA KULALAMIKA*🍃🏓▫️Kuna tofauti nyingi kati ya kuongea na kulalamika, ila naomba nifafanue mbili...
18/09/2025

*TOFAUTI KATI YA KUONGEA NA KULALAMIKA*

🍃🏓▫️Kuna tofauti nyingi kati ya kuongea na kulalamika, ila naomba nifafanue mbili kubwa ambazo ukizingalia utajua k**a unaongea au unalalamika?

🍃🏓▫️(1) Unalalamika ukiwa na hasira, ukiwa umenuna, ukia umeudhiwa. Mtu anapokufanyia kitu, ukaongea wakati anakufanyia basi unakua unalalamika.

🍃🏓▫️Kwa mfano, mume wako amechelewa kurudi, una hasira umenuna, ukaanza kumuambia kwanini unaruidi saa anane, basi hapo utakua unalalamika.

🍃🏓▫️Lakini kuongea ni toafuti, unasubiri akili imepoa, huna hasira, kitu kilitokea jana au siku mbili nyuma, kichwa kimetulia, umepanga maneno kisha unamuambia kuwa siku hizi unachelewa sana, nini tatizo, anakaumbia wote mkiwa mmetulia, iwe ni uongo au kweli lakini kichwa chako kimetulia na chake kimetulia.

🍃🏓▫️(2) Kulalamika ni kurudia kitu kile kile kila siku.

🍃🏓▫️Inaweza kua hajakosea, lakini mtu anafanya kitu kile kile kila siku, na wewe unaongea kitu kilekile kila siku, hapo unalalamika.

🍃🏓▫️Mwenza wako ni mtu mzima, k**a umemuambia kitu mara moja au mbili basi kuna mawaili, moja ndiyo alivyo huwezi kumbadilisha na pili inawezekana anafanya makusudi ataacha akiamua.

🍃🏓▫️Kumuambia mtu kitu kile kile kila siku haisaidii yeye kukiacha kile kitu zaidi unakua unalalamika.

🍃🏓▫️Sasa kuongea hapa ni kumuambia mtu kitu mara moja, akirudia utamuamba tena na akirudia tena unanyamaza kwani ndivyo alivyo hata utembee uchi au uongee mishipa ya uso ipasuke hataacha au anakufanyia tu makusudi ili kukukomoa.

🍃🏓▫️ Mtu anayekufanyia makusudi ni k**a soda, ya koka, jinsi unavozidi kuitingisha ndivyo inazidi kutoa mapovu, hataacha mpaka nawe uache kuongea, atajiona k**a huudhiki basi ataacha asipoacha basi unapotezea maisha yanaenda.

Kwa wale wageni kuwakumbusha tu kabla ya kuwa mwalimu na Daktari wa kiroho nilifuzu pia kuwa Daktari au muuguzi ndio maa...
17/09/2025

Kwa wale wageni kuwakumbusha tu kabla ya kuwa mwalimu na Daktari wa kiroho nilifuzu pia kuwa Daktari au muuguzi ndio maana wengi wananijua k**a Dr.Mwaka haimaanishi ni jina tu la utani bali ni jina lenye hadhi kubwa sana kwangu hivyo leo tugusie maswala ya Afya ya mwili maana kuna mambo yanaendelea huku mitandaoni ukiskiza unaeza rukwa na akili, utasikia mara hoo mimi ni blood group O, siezi dumu kwa mahusiano, mimi ni blood group O nina hasira za kuua mtu😀😀 Sasa hawa blood group O ni nani haswaa mara Uskie “Mimi nina Group O Siugui Magonjwa Ovyo" JE..? Ukiwa na damu kundi O, Magonjwa hayawezi kukugusa...?

Au ni porojo tu za mtaani..?

Maana naona watu huwa mnatamba na Blood Groop O Kwamba hampati UKIMWI..Kirahisi..!☠️

Kundi la Damu O – La Kipekee au la Kawaida..?

Kabla ya kuchambua magonjwa na kinga ya kundi hili, hebu kwanza tulielewe vizuri....

Je, unajua kwamba kundi la damu O ndilo kundi la damu linalopatikana kwa wingi zaidi duniani..?

↳ Inakadiriwa kuwa karibu 45% ya watu duniani wana kundi la damu O

Hili ni kundi la damu linaloweza kutolewa kwa watu wa makundi yote mengine, lakini wenyewe wanaweza kupokea damu kutoka kwa kundi lao pekee...

Linaitwa *"Universal Donor"* kwa sababu wanaweza kumsaidia mtu yeyote anayehitaji damu...

K**a wewe ni kundi O, basi damu yako inaweza kuokoa maisha ya mtu yeyote bila kujali kundi lake.

*Lakini sasa swali kuu ni hili....*

Je, hii inamaanisha kinga yao ya mwili ni ya kipekee pia...?

Wenye Kundi la Damu O Hawashikwi na Magonjwa?

→Ebu tuweke rekodi sawa..!

Ukweli ni kwamba kuwa na kundi la damu O kunaweza kutoa faida fulani za kiafya, lakini si kwamba hauwezi kuugua !

Magonjwa Yaliyo na Hatari Ndogo kwa Wenye Damu O...

✔ Magonjwa ya Moyo...

Utafiti umeonyesha kuwa watu wenye kundi la damu O wana hatari ndogo ya kupatwa na magonjwa ya moyo k**a shinikizo la damu na mshtuko wa moyo (heart attack) ukilinganisha na makundi mengine ya damu.

Sababu ni kwamba damu yao ina chembe zinazosaidia kuzuia kuganda kwa damu haraka, hivyo kupunguza hatari ya kuziba kwa mishipa ya damu.

✔ Dengue...

Unasikia watu wakishikwa na homa ya dengue hadi hali zao zinakuwa mbaya sana..?

Wanasayansi wanasema kuwa wenye kundi la damu O wako katika hatari ndogo ya kupata madhara makali ya homa hii ikilinganishwa na makundi mengine..!

✔ Blood Clots (Damu Kuganda Kiholela)

Wenye kundi la damu O wana hatari ndogo ya kupata magonjwa yanayosababishwa na damu kuganda ovyo mwilini (deep vein thrombosis na pulmonary embolism).

Hii ni kwa sababu damu yao ina kiwango kidogo cha baadhi ya protini zinazohusika na mchakato wa kuganda kwa damu.

*Ps;* Kwa hiyo, k**a wewe ni O, unaweza kujivunia kuwa na kinga fulani dhidi ya magonjwa haya...! Lakini subiri… Si kila kitu ni kizuri kwa Kundi O

*Magonjwa Yanayowaathiri Zaidi Wenye Damu O..*

Sasa tusonge upande wa pili wa sarafu.

Watu wenye kundi la damu O si malaika wasioguswa na magonjwa..

Kuna hatari wanazokumbana nazo pia....

→Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)..

Utafiti unaonyesha kuwa watu wenye damu ya kundi O wana uwezekano mkubwa wa kupata vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na bakteria aitwaye Helicobacter pylori.

Bakteria huyu anapopata mazingira mazuri tumboni, husababisha vidonda ambavyo huleta maumivu makali na shida za mmeng’enyo wa chakula.

→ Matatizo ya Kupoteza Damu (Bleeding Disorders)...

Kwa sababu damu ya kundi O haishikani haraka, watu hawa wanaweza kuvuja damu kwa muda mrefu zaidi wakipata jeraha au kufanyiwa upasuaji...

Hii ni hatari hasa kwa wanawake wenye hedhi nzito au kwa watu wanaofanyiwa upasuaji mkubwa.

→ Maambukizi ya Bakteria na Virusi...

Ingawa wanapata kinga dhidi ya baadhi ya magonjwa, bado wako kwenye hatari ya kushambuliwa na maambukizi fulani ya bakteria na virusi.

Kwa hiyo, wale wanaosema “Mimi nina group O, magonjwa hayanipati” – Ujaribu tena kutamba na kauli hiyo!

*Lishe ya Wenye Kundi la Damu O Ukweli au Uzushi...?*

↳Kuna dhana kwamba kundi la damu linaweza kuathiri vyakula unavyopaswa kula.

Unakumbuka ile “BloodType Diet” inayosema wenye damu O wanapaswa kula nyama nyingi na kupunguza wanga?

*Ipo hivi...*

Hadi sasa, hakuna ushahidi wa kisayansi wa kuthibitisha kuwa chakula kinapaswa kutegemea kundi la damu.

Lakini kwa ujumla...

✔ Wenye kundi la damu O wanahimizwa kula lishe yenye protini nyingi k**a nyama, samaki, mayai, na mboga za majani kwa wingi....

❌ Wanga nyingi (mkate, wali, pasta) zinaweza kusababisha kuongeza uzito kwa haraka, hivyo ni vyema kupunguza kiasi.

Hii haimaanishi kuwa watu wa kundi O wasile vyakula vya wanga kabisa – inategemea mtu na mwili wake!

*Je, Huwezi Kuugua Ukiwa na Damu O?*

❌ HAPANA! Kuwa na kundi la damu O hakumaanishi huwezi kupata magonjwa!

Ni kweli kwamba una faida fulani za kiafya, lakini pia kuna magonjwa yanayoweza kuwa hatari zaidi kwako.

→Hakuna kundi la damu lisiloweza kuugua! Kinachoamua Kuwa na Afya bora ni..

✔ Kula chakula bora
✔ Kufanya mazoezi mara kwa mara
✔ Kupata usingizi wa kutosha
✔ Kupunguza msongo wa mawazo
✔ Kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara

Kwa hiyo, kwa wale wanaojiona kuwa “immune” kwa sababu wana kundi O, wajipange upya!...🫵🏾

Maisha ni mpangilio sio samani unaweza kuwa huna kitu kikubwa lakini kwa kuyapangalia maisha yako ukaishi vizuri tu kuli...
16/09/2025

Maisha ni mpangilio sio samani unaweza kuwa huna kitu kikubwa lakini kwa kuyapangalia maisha yako ukaishi vizuri tu kulingana na hali yako.

Kila mtu ana saa 24 za kuishi utakavyozitumia ndivyo utakavyoishi hakuna mabadiliko k**a ndani yako hakuna mabadiliko. Badilika ili ubadilike acha lawama simama nafasi yako hata k**a nafasi yako sio nzuri k**a za wengine simama hapo hapo.

Nisikilize mwananguMwanaume maskini hana kazi ya kukimbizana na wanawake. Kukimbizana na wanawake ni mchezo wa wanaume w...
15/09/2025

Nisikilize mwanangu

Mwanaume maskini hana kazi ya kukimbizana na wanawake. Kukimbizana na wanawake ni mchezo wa wanaume waliotulia kimaisha, siyo wavulana wasio na senti mfukoni.

Umaskini na umalaya havichanganyiki. Njaa itakudhalilisha. Kodi ya nyumba itakunyenyekeza. Mafuta ya usafiri yatakuangamiza. Ukifanya wanawake ndiyo shughuli yako huku huna kitu, tayari umekwisha. Unapoteza muda, nguvu na akili ambazo ulipaswa kutumia kujinasua kwenye umaskini; unazipoteza kwa sketi. Huo ni upumbavu.

Acha kushika matiti ilhali huwezi hata kushika pesa mkononi mwako. Acha kukimbizana na miadi ya kimapenzi ilhali huwezi kujilisha mwenyewe. Tafuta pesa kwanza; siyo utajiri mkubwa, bali angalau kujisimamia na kusimama imara. Jitengeneze kwanza kabla hujaanza kuwafuata wanawake.

Tambua hili: wanawake siyo wabaya, lakini kwa mwanaume maskini, wao ni kikwazo. Na kikwazo hicho kitakugeuka maangamizi. Hata wanaume wanaojitoa kwa nguvu za giza wanajua hili; wengi wao huacha ngono kwanza ili wapate pesa. Hilo linapaswa kukufundisha kitu.

Linda kesho yako. Waachane na wanawake kwa sasa. Wanawake bora zaidi wanakusubiri mbele. Unazeeka, na bado huna kitu? Jikaze!

Umeelewa?

Nishaona mapenzi ya dhati kwenye sura ya kahaba, na usaliti kwenye aibu ya mlokole.Nishashuhudia busara, kwenye meza ya ...
14/09/2025

Nishaona mapenzi ya dhati kwenye sura ya kahaba, na usaliti kwenye aibu ya mlokole.

Nishashuhudia busara, kwenye meza ya walevi mbwa.

Kisha nikaona ujinga kwa professor mwenye kila cheti kabatini mwake.

Nimeuona utu kwenye kinywa cha mwenye matusi, na roho mbaya kwa mstaarabu asiyependa kuchangamana na wenzie.

Nimesikia uongo kutoka kwa yule aliyehapa kwa Mungu wake kuwa anachosema hadanganyi.

Nikausikia ukweli kutoka kwa mtu ambaye amewahi kuachwa mara nyingi kwasababu za uaminifu.

Nimemuona dada anayekesha altare kwa maombi akiendelea kukosa mtoto.

Huku yule sister duu, kila siku akigundua mbinu mpya ya kutoa mimba..

Nimeona chafu tatu anayemkumbuka Mungu akiwa kwa sadari na muumini anayefikiria ngono akiwa msikitini..

Nimewaona wanandoa waliokutana baada ya wrong number, one night stand, na kuwasaliti wenzi wao wa zamani.

Kisha nimeona mauaji na ukatili kutoka kwa wapenzi waliojuana muda mrefu, vacation za kila mwaka na bado mahusiano yao yakaishia kwenye majeraha.

Kitu kimoja nilichojifunza, maisha sio hisabati na kanuni zake.. Si kila kin'gaacho ni dhahabu..

Katikati ya barabara ya maisha unaweza kufuata maelekezo yote na bado ukapotea njia..

Tusali mambo tunayoyapanga yaende k**a tunavyotaraji,

Kila element(kipengele) kina miungu wake Leo fahamu Moja WA miungu WA kipengele Cha moto,Ra ni mungu wa jua na mfalme au...
12/06/2024

Kila element(kipengele) kina miungu wake Leo fahamu Moja WA miungu WA kipengele Cha moto,
Ra ni mungu wa jua na mfalme au baba wa wotemiungu ya Misri. Mara nyingi anaonyeshwa kwa umbo la mwanadamu akiwa na kichwa cha mwewe, diski ya dhahabu na nyoka juu ya kichwa chake k**a taji, fimbo ya enzi katika mkono wake wa kushoto, na ankh katika mkono wake wa kulia . Ankh ilikuwa ishara ya kale ya Misri kwa maisha....

Dr.Mwaka

Address

Mombasa

Telephone

+254743889082

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Daktari Mwaka posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Daktari Mwaka:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram