
24/10/2021
MJUE JINNUL ZAWABIR NA TIBA YAKE
Asalam alaykum warahmatullahi wabarakatu Hawa ni majini wakorofi sana.Na pia wana madhara makubwa sana mwilini na pia miongoni mwa madhara yao humsababishia mgonjwa awe na saratani na maradhi ya mkanda wa jeshi.Huwaingia watu kwa haraka sana majini hususan wale ambao hupenda kukaa uchi baada ya kuoga.Na pia k**a atakuwa ni jinni mahaba wa kutoka ukoo huu huwa hapendi watu ambao wananuka jasho na akikaa karibu na mtu ambaye ana jasho atakuwa anatema tema mate ovyo ovyo.Siku za nyuma nilikuwa nimeelezea kwamba sio maradhi yote ambayo ukipimwa hospitalini tiba yake utaipata huko kwasababu maradhi yote hayo yanakuwaga yako sehemu mbili.ya kawaida na yale ya kusababishwa na majini wa kichawi.natumai kufikia hapo nimeeleweka.ijapokuwa kuna dalili ambazo zitakufahamisha ni jinni wa aina gani ambaye amekuvamia mwilini kwasababu kujua majini walioko ndani ya mwili kwa tabibu yeyote ni jambo la muhimu sana ili ajue anapambana na adui wa aina gani kwa dalilina kujua tiba yake kwasababu kila jinni ana tiba tofauti na mwingine.Na pia kuwajua majini kupitia ndoto ambazo mgonjwa anaota ni jambo ambalo ni la muhimu zaidi kwa tabibu
DALILI ZA KUMJUA JINNUL ZAWABIR AKIWA MWILINI
✔️Mwili kuwasha sana
✔️Mwili kuwa na vidonda vidonda vya upele
✔️ Mwili kupauka hata ukipaka mafuta
✔️Ngozi kumbambuka
✔️Mwili Kuvimba na kuwaka moto
✔️Ngozi kuvuka k**a gamba la nyoka
✔️Kuwa na majipu ya kila wakati
✔️ Rangi ya ngozi wakati mwingine kubadilika
✔️ Kukosa usingizi
✔️Kukosa utulivu wa moyo
TIBA YA KUMTOA JINNUL ZAWABIR
✔️ Mruturutu
✔️Kibiriti upele
✔️Shabu
✔️Karkam
✔️Mafuta ya ndimu
✔️Mafuta ya Thawm
✔️Mafuta ya nyonyo
MAANDALIZI NA MATUMIZI YA DAWA HIZO NI K**A YAFUATAYO
Hizi dawa zitatwangwa kisha zikilainika zichanganywe pamoja halafu mgonjwa atakuwa anafukiza mara mbili kwa siku.zoezi hilo atalifanya kwa siku 21 hadi 30 in sha Allah mgonjwa atapona
TIBA YA PILI NI DAWA ZA KULA
✔️Sanamaki
✔️Sidr
✔️Sufa nyekundu
✔️Haltit
✔️Pilipili manga
MAANDALIZI NA MATUMIZI YA DAWA HIZO
Dawa hizo zinatakiwa zikiwa ni za unga halafu zitachanganywa pamoja zote kisha ziwekwe kwenye asali lita moja.matumizi yake ni kijiko cha chakula kimoja kutwa mara 3 kwa siku 30 hadi 45 in sha Allah ni mujarab dawa hizo.Na mgonjwa afanyiwe Ruqya kwa ukamilifu wake siku 7.TUNATIBU NAYE ALLAH ANAPONYESHA.HII NI SABABU TU YA KUPONA KWAKO
Kwa wale ambao wanahitaji dawa hizo zikiwa tayari tunazo.unaweza ukaagiza na utafikiwa na mzigo wako popote ulipo
✔️+254756553838
✔️+254708995244