Kaakijanjatz

Kaakijanjatz We believe in the power of arts, creativity, and technology. https://www.kaakijanja.org/

KAA KIJANJA ARTS CARAVAN MBEYA – 2025Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya ...
21/10/2025

KAA KIJANJA ARTS CARAVAN MBEYA – 2025

Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya Mkoa wa Mbeya, waliadhimisha kwa upekee mkubwa Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025 yenye kaulimbiu “Nguvu Kazi ya Vijana kwa Maendeleo Endelevu.”

Kupitia Kaa Kijanja Arts Caravan iliyopita katika wilaya za Chunya, Rungwe, na Mbeya Mjini, wasanii Vinara wa Mradi wa REST zaidi ya 20 walishiriki kikamilifu kutumia sanaa kufikisha jumbe chanya kuhusu maendeleo ya vijana nchini na kuibua midahalo Chanya kuhusu Changamoto, fursa na maendeleo ya Kijana kwa ujumla.
Kwa heshima kubwa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Taasisi ya Kaa Kijanja kwa kushirikiana na DSW Tanzania walipata ridhaa ya kufanya uhamasishaji wa vijana kushiriki katika maadhimisho ya kitaifa katika Wilaya zote Caravan ilipotita

Katika siku ya ufunguzi wa maadhimisho hayo, yaliyofunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa tarehe 10 Oktoba 2025, vijana wasanii walipata nafasi ya kuonesha namna sanaa na ubunifu vinavyoweza kuwa daraja la elimu na mabadiliko chanya katika jamii kwa kutoa burudani zenye jumbe mbalimbali kuhusu Kijana mbele ya mgeni rasmi na maeflu ya wananchi waliohudhuria.

Aidha, Wasanii Vinara walishiriki kikamilifu katika Kongamano la Kitaifa la Wiki ya Vijana lililofanyika tarehe 12 Oktoba 2025, wakitoa burudani zenye ujumbe kuhusu vijana na maendeleo yao, mbele ya Mgeni Rasmi, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Kongamano hilo lilikutanisha zaidi ya vijana 1,500 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Kupitia maadhimisho haya, Taasisi ya Kaa Kijanja imeendelea kuonesha na kuhamasisha umuhimu wa kuwekeza katika mazingira wezeshi kwa vijana wasanaa na wabunifu nchini, ka kuwa kuwa sanaa ni fursa kubwa kwa vijana na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

20/10/2025

MAFUNZO YA SANAA KWA MAENDELEO YA VIJANA – MBEYA 2025

Katika kuadhimisha Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025, Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya Mkoa wa Mbeya, iliandaa mafunzo kwa vijana wasanii 20 mkoa wa Mbeya, kuwawezesha kutumia sanaa na ubunifu kuwasilisha jumbe chanya kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia (UWAKI), afya, na stadi za maisha kwa vijana.

Mafunzo yalifunguliwa rasmi tarehe 06 Oktoba 2025 na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mbeya, Bi. Elukaga Mwalukasa, ambaye aliongoza warsha kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia na kueleza namna wasanii na wabunifu wanavyoweza kuchangia katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II 2024/25–2028/29).

Dkt. Mariam Mhanjim kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya alitoa mafunzo kuhusu huduma rafiki kwa vijana, afya ya uzazi, na stadi za maisha, huku
Dkt. Reinfridy Chombo (Hospitali ya Rufaa ya Mbeya) akiongoza mafunzo kuhusu afya ya akili kwa vijana, hasa wasanii.

Dkt. Chombo alisisitiza umuhimu wa vijana kudhibiti changamoto za maisha, kufanya kazi kwa bidii, na kuchangia katika maendeleo ya familia, jamii, na uchumi wa taifa.
Mratibu wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Ndg. Francis Ngelela, aliwahimiza vijana kuendelea kuwa vielelezo vizuri kwenye jamii na kutumia sanaa zao kupinga mila kandamizi na tamaduni potofu zinazokwamisha maendeleo ya vijana.

Mafunzo yalifungwa rasmi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya (Mratibu Msaidizi wa Polisi), ASP Veronica Ponera, aliyesisitiza umuhimu wa sanaa k**a chombo cha mabadiliko chanya katika jamii, hasa katika kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji katika jamii.

Washiriki wote walipokea vyeti vya ushiriki na kutambuliwa rasmi k**a Vinara wa Mradi wa REST na Kampeni ya Kaa Kijanja 2025.

Mafunzo haya ni muendeleo wa utekelezaji wa mradi wa Reproductive Equity Strategic in Tanzania (REST II) wenye lengo la kujengea uwezo Vijana na taasisi za vijana kufikia malengo yao.

17/10/2025

MAFUNZO YA SANAA KWA MAENDELEO YA VIJANA – MBEYA 2025

Katika kuadhimisha Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025, Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya Mkoa wa Mbeya, iliandaa mafunzo kwa vijana wasanii 20 mkoa wa Mbeya, kuwawezesha kutumia sanaa na ubunifu kuwasilisha jumbe chanya kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia (UWAKI), afya, na stadi za maisha kwa vijana.

Mafunzo yalifunguliwa rasmi tarehe 06 Oktoba 2025 na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mbeya, Bi. Elukaga Mwalukasa, ambaye aliongoza warsha kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia na kueleza namna wasanii na wabunifu wanavyoweza kuchangia katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II 2024/25–2028/29).

Dkt. Mariam Mhanjim kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya alitoa mafunzo kuhusu huduma rafiki kwa vijana, afya ya uzazi, na stadi za maisha, huku
Dkt. Reinfridy Chombo (Hospitali ya Rufaa ya Mbeya) akiongoza mafunzo kuhusu afya ya akili kwa vijana, hasa wasanii.

Dkt. Chombo alisisitiza umuhimu wa vijana kudhibiti changamoto za maisha, kufanya kazi kwa bidii, na kuchangia katika maendeleo ya familia, jamii, na uchumi wa taifa.
Mratibu wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Ndg. Francis Ngelela, aliwahimiza vijana kuendelea kuwa vielelezo vizuri kwenye jamii na kutumia sanaa zao kupinga mila kandamizi na tamaduni potofu zinazokwamisha maendeleo ya vijana.

Mafunzo yalifungwa rasmi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya (Mratibu Msaidizi wa Polisi), ASP Veronica Ponera, aliyesisitiza umuhimu wa sanaa k**a chombo cha mabadiliko chanya katika jamii, hasa katika kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji katika jamii.

Washiriki wote walipokea vyeti vya ushiriki na kutambuliwa rasmi k**a Vinara wa Mradi wa REST na Kampeni ya Kaa Kijanja 2025.

Mafunzo haya ni muendeleo wa utekelezaji wa mradi wa Reproductive Equity Strategic in Tanzania (REST II) wenye lengo la kujengea uwezo Vijana na taasisi za vijana kufikia malengo yao.

MAFUNZO YA SANAA KWA MAENDELEO YA VIJANA – MBEYA 2025Katika kuadhimisha Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025, Taasisi ya...
16/10/2025

MAFUNZO YA SANAA KWA MAENDELEO YA VIJANA – MBEYA 2025

Katika kuadhimisha Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025, Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya Mkoa wa Mbeya, iliandaa mafunzo kwa vijana wasanii 20 mkoa wa Mbeya, kuwawezesha kutumia sanaa na ubunifu kuwasilisha jumbe chanya kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia (UWAKI), afya, na stadi za maisha kwa vijana.

Mafunzo yalifunguliwa rasmi tarehe 06 Oktoba 2025 na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mbeya, Bi. Elukaga Mwalukasa, ambaye aliongoza warsha kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia na kueleza namna wasanii na wabunifu wanavyoweza kuchangia katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II 2024/25–2028/29).

Dkt. Mariam Mhanjim kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya alitoa mafunzo kuhusu huduma rafiki kwa vijana, afya ya uzazi, na stadi za maisha, huku
Dkt. Reinfridy Chombo (Hospitali ya Rufaa ya Mbeya) akiongoza mafunzo kuhusu afya ya akili kwa vijana, hasa wasanii.

Dkt. Chombo alisisitiza umuhimu wa vijana kudhibiti changamoto za maisha, kufanya kazi kwa bidii, na kuchangia katika maendeleo ya familia, jamii, na uchumi wa taifa.
Mratibu wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Ndg. Francis Ngelela, aliwahimiza vijana kuendelea kuwa vielelezo vizuri kwenye jamii na kutumia sanaa zao kupinga mila kandamizi na tamaduni potofu zinazokwamisha maendeleo ya vijana.

Mafunzo yalifungwa rasmi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya (Mratibu Msaidizi wa Polisi), ASP Veronica Ponera, aliyesisitiza umuhimu wa sanaa k**a chombo cha mabadiliko chanya katika jamii, hasa katika kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji katika jamii.

Washiriki wote walipokea vyeti vya ushiriki na kutambuliwa rasmi k**a Vinara wa Mradi wa REST na Kampeni ya Kaa Kijanja 2025.

Mafunzo haya ni muendeleo wa utekelezaji wa mradi wa Reproductive Equity Strategic in Tanzania (REST II) wenye lengo la kujengea uwezo Vijana na taasisi za vijana kufikia malengo yao.

MAFUNZO YA SANAA KWA MAENDELEO YA VIJANA – MBEYA 2025

Katika kuadhimisha Wiki ya Vijana Kitaifa Tanzania 2025, Taasisi ya Kaa Kijanja, kwa kushirikiana na DSW Tanzania pamoja na Sekretarieti ya Mkoa wa Mbeya, iliandaa mafunzo kwa vijana wasanii 20 mkoa wa Mbeya, kuwawezesha kutumia sanaa na ubunifu kuwasilisha jumbe chanya kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia (UWAKI), afya, na stadi za maisha kwa vijana.

Mafunzo yalifunguliwa rasmi tarehe 06 Oktoba 2025 na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Mbeya, Bi. Elukaga Mwalukasa, ambaye aliongoza warsha kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia na kueleza namna wasanii na wabunifu wanavyoweza kuchangia katika utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II 2024/25–2028/29).

Dkt. Mariam Mhanjim kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya alitoa mafunzo kuhusu huduma rafiki kwa vijana, afya ya uzazi, na stadi za maisha, huku
Dkt. Reinfridy Chombo (Hospitali ya Rufaa ya Mbeya) akiongoza mafunzo kuhusu afya ya akili kwa vijana, hasa wasanii.

Dkt. Chombo alisisitiza umuhimu wa vijana kudhibiti changamoto za maisha, kufanya kazi kwa bidii, na kuchangia katika maendeleo ya familia, jamii, na uchumi wa taifa.
Mratibu wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Ndg. Francis Ngelela, aliwahimiza vijana kuendelea kuwa vielelezo vizuri kwenye jamii na kutumia sanaa zao kupinga mila kandamizi na tamaduni potofu zinazokwamisha maendeleo ya vijana.

Mafunzo yalifungwa rasmi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Mkoa wa Mbeya (Mratibu Msaidizi wa Polisi), ASP Veronica Ponera, aliyesisitiza umuhimu wa sanaa k**a chombo cha mabadiliko chanya katika jamii, hasa katika kutoa elimu na kukemea vitendo vya ukatili na unyanyasaji katika jamii.

Washiriki wote walipokea vyeti vya ushiriki na kutambuliwa rasmi k**a Vinara wa Mradi wa REST na Kampeni ya Kaa Kijanja 2025.

Mafunzo haya ni muendeleo wa utekelezaji wa mradi wa Reproductive Equity Strategic in Tanzania (REST II) wenye lengo la kujengea uwezo Vijana na taasisi za vijana kufikia malengo yao.

CHAI FM🙏🏿🫡
14/10/2025

CHAI FM🙏🏿🫡

jamii imetakiwa kujenga utaratibu wa kutoa taarifa kwenye vyombo ya kisheria kuhusu vitendo vya utatili MBEYA Na Lennox Mwamakula Vijana nchini wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika suala la kupinga vitendo vya ukatili kwani wao ndiyo nguvu kazi ya Taifa…

Thank you The Respondents 🫡Click the link to read more
11/10/2025

Thank you The Respondents 🫡

Click the link to read more

Respondent Online

Address

Arusha

Opening Hours

Monday 08:30 - 17:30
Tuesday 08:30 - 17:30
Wednesday 08:30 - 17:30
Thursday 08:30 - 17:30
Friday 08:30 - 17:30

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kaakijanjatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Kaakijanjatz:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram