Dr.Joh Healthcare

Dr.Joh Healthcare Mfumo maarifa wa TEHAMA unaotoa habari, elimu na ushauri wa Afya kutoka kwa madaktari kulingana na sera, miongozo na viwango vya utoaji huduma za Afya.

https://imalilo.com/namna-gani-mwani-sea-moss-unapunguza-uzito-uliopita-kiasi/
06/09/2025

https://imalilo.com/namna-gani-mwani-sea-moss-unapunguza-uzito-uliopita-kiasi/

1️⃣ Virutubisho vya Mwani Vinavyosaidia Kupunguza Uzito 2️⃣ Namna mwani unavyofanya kazi kwenye Kupunguza Uzito πŸ₯£ Ushibishaji (Satiety effect) πŸ”₯ Kuongeza Metabolism πŸ’§ Kupunguza maji mwilini (diuretic effect) πŸ§ͺ Kuboresha usawa wa sukari kwenye damu 3️⃣ Tafiti za Kisayansi 4️...

*UMUHIMU WA MAZIWA YA SOYA KWA WANAWAKE WALIOFIKIA AU KUKARIBIA UKOMO WA HEDHI ( MENOPAUSE)*Menopause ni kipindi cha mai...
03/09/2025

*UMUHIMU WA MAZIWA YA SOYA KWA WANAWAKE WALIOFIKIA AU KUKARIBIA UKOMO WA HEDHI ( MENOPAUSE)*

Menopause ni kipindi cha maisha ya kila mwanamke, ambapo hedhi hukoma kabisa kutokana na kupungua kwa homoni za estrogen na progesterone. Hali hii mara nyingi hutokea kati ya umri wa miaka 45–55.

Kupungua kwa homoni hizi kunasababisha mabadiliko makubwa mwilini, yanayoweza kuathiri afya ya mwili na maisha ya kila siku. Ndiyo maana wanawake wengi katika menopause hukumbana na changamoto nyingi za kiafya na kihisia.

Kwenye somo hili Nitaeleza kwa kina changamoto za menopause, kwa nini maziwa ya soya ni muhimu, virutubisho vinavyopatikana ndani yake, namna yanavyofanya kazi (mechanism), na jinsi ya kuyatumia ili kupata faida kubwa kiafya.

πŸ“Œ *Changamoto za Menopause*

Baada ya homoni kushuka, mwanamke anaweza kupata dalili hizi:

🌑️ (hot flashes) na jasho la usiku

😴 Usingizi kuvurugika

πŸ˜” Mabadiliko ya hisia hasira, huzuni au msongo wa mawazo

🦴 Kupungua kwa nguvu za mifupa (osteoporosis)

❀️ Kuongezeka kwa hatari ya magonjwa ya moyo

🌿 Ukavu sehemu za siri na kupungua hamu ya tendo la ndoa

🧠 Kupungua kumbukumbu na umakini

Hizi changamoto hutokana zaidi na kukosekana kwa estrogen, homoni inayolinda mifupa, moyo, ngozi, ubongo na hata mfumo wa hisia.

πŸ“Œ *Kwa nini Maziwa ya Soya ni Muhimu kwa Menopause?*

Maziwa ya soya yana virutubisho vinavyoweza kusaidia mwili kujibu upungufu wa estrogen. Muhimu zaidi, yana isoflavones, ambazo ni phytoestrogens (estrogen asilia ya mimea).

Isoflavones hufanya kazi kwa kufunga kwenye vipokezi vya estrogen (estrogen receptors) ndani ya mwili, hivyo kusaidia kupunguza makali ya dalili za menopause.

πŸ“Œ *Virutubisho Muhimu Katika Maziwa ya Soya*

1. *Isoflavones (Phytoestrogens)*

Hufanya kazi sawa na estrogen ya mwili.

Hupunguza hot flashes na kutokwa jasho sana usiku.

Hulinda mifupa dhidi ya osteoporosis(kupungua kwa uimara wa mifupa)

*2. Calcium & Vitamin D*

Muhimu kwa uimara wa mifupa na meno.

Hupunguza hatari ya mifupa kudhoofika baada ya menopause.

*3. Protini ya Soya*

Hupunguza cholesterol mbaya (LDL).

Hukuza afya ya moyo.

Husaidia misuli kubaki na nguvu.

*4. Magnesium & Vitamin B6*

Hupunguza msongo wa mawazo.

Husaidia usingizi bora.

Huchochea utengenezaji wa serotonin (hormone ya furaha).

*5. Vitamin E & Antioxidants*

Huimarisha kinga ya mwili.

Hulinda ngozi isikauke wala kuzeeka haraka.

Husaidia macho na mishipa ya damu.

πŸ“Œ *Faida Kuu za Maziwa ya Soya kwa Wanawake Katika Menopause*

🌑️ Kupunguza dalili za hot flashes kwa 20–40% kulingana na tafiti.

🦴 Kuimarisha msongamano wa mifupa, kupunguza hatari ya osteoporosis.

❀️ Kulinda afya ya moyo, kupunguza cholesterol mbaya.

😌 Kusaidia usingizi na kupunguza msongo wa mawazo.

🌿 Kuhifadhi unyevunyevu wa ngozi na kuboresha afya ya nywele na ngozi.

🧠 Kulinda ubongo na kumbukumbu kwa kuongeza serotonin na neurotransmitters.

πŸ“Œ *Kiasi Sahihi cha Kunywa kwa siku*
Unaweza kuyatumia kwa njia tofauti:
βœ… Kwenye uji
βœ… Kutengeneza smoothie
βœ… Badala ya maziwa kwenye kahawa au chai
βœ… Kupikia supu au sauces

*Kiwango kinachopendekezwa kwa siku kwa watu wazima (ikiwemo wanawake wa menopause):*

20–50 mg za isoflavones kwa siku

Hii hupatikana kwenye takribani 25–30 g ya unga wa maziwa ya soya

*Tukivunja kwa vipimo vya nyumbani πŸ₯„*

Kijiko 1 cha chakula (tablespoon) cha unga wa soya β‰ˆ 8–10 g

Hivyo, vijiko 3 vya chakula (β‰ˆ 25–30 g) vya unga wa soya vinaweza kutoa kiwango cha isoflavones kinachopendekezwa kwa siku.

*Kwa urahisi* πŸ‘©β€πŸ‘©β€πŸ‘§β€πŸ‘¦

πŸ‘‰ Tumia vikombe 1–2 vya maziwa ya soya kwa siku, ambavyo vinatengenezwa kwa kuchanganya vijiko 2–3 vya unga wa maziwa ya soya kwenye kikombe cha maji (200 ml).

*Mwisho*

Menopause siyo mwisho wa afya njema ni mwanzo wa awamu mpya inayohitaji lishe bora na matunzo ya mwili.
Kwa kuingiza Clara Lishe Soy Milk kwenye lishe yako ya kila siku, unaweza kupunguza changamoto za menopause, kulinda mifupa, moyo, ngozi na akili yako, huku ukiendelea kuishi maisha yenye nguvu na afya bora.

K**a unahitaji :+255714880810

*Unachoka haraka? Unapata upungufu wa damu au kinga dhaifu? πŸ€”**Unajua kila kundi la watu  wajawazito, wanaonyonyesha, wa...
24/08/2025

*Unachoka haraka? Unapata upungufu wa damu au kinga dhaifu? πŸ€”*
*Unajua kila kundi la watu wajawazito, wanaonyonyesha, watoto, vijana na wazee lina mahitaji yake ya lishe?*

Changamoto ni kupata kinywaji kimoja cha asili kinachokidhi mahitaji yote.

🌿 Michelle Juice Powder ni mchanganyiko wa asili wa Beetroot, Rosella na Ubuyu superfoods tatu zinazojulikana kwa utafiti wa kisayansi.
βœ… Iron & Folate – kuongeza damu na kusaidia ukuaji wa mtoto
βœ… Vitamin C – kuimarisha kinga ya mwili kwa kila umri
βœ… Antioxidants – kulinda moyo na mishipa ya damu
βœ… Fiber – kuboresha mmeng’enyo na afya ya utumbo

Faida zake kwa kila mmoja:
🀰 *Wajawazito* – Huongeza damu na kupunguza uchovu
🀱 *Wanaonyonyesha* – Huimarisha kinga na kuongeza nguvu
πŸ‘Ά *Watoto* – Huchangia ukuaji na kinga imara
πŸ’ͺ *Vijana & Wanafunzi* – Huongeza stamina na uwezo wa kusoma
πŸ‘΄ *Wazee* – Hupunguza shinikizo la damu na kulinda moyo

πŸ“² Agiza sasa +255714880810

JIUNGE NA GROUP LETU UJIFUNZE BURE ELIMU YA LISHE KUTOKA KWA WATAALAMAfya njema huanza na lishe sahihi!Wajawazito, wanao...
23/08/2025

JIUNGE NA GROUP LETU UJIFUNZE BURE ELIMU YA LISHE KUTOKA KWA WATAALAM

Afya njema huanza na lishe sahihi!
Wajawazito, wanaonyonyesha, watoto, wazee na watu wanaotaka kupunguza au kuongeza uzito kila mmoja ana mahitaji yake ya lishe.

πŸ‘‰ Lakini je, unajua ni chakula gani kinakufaa zaidi?
πŸ‘‰ Unajua ni virutubisho vipi vinakosekana kwenye mlo wako?

✨ Clara Lishe inakuletea nafasi ya kipekee kujifunza kila kitu kuhusu lishe kupitia WhatsApp Group yetu ya bure!

βœ… Utapata elimu ya lishe ya kila siku
βœ… Utaelewa bidhaa sahihi za lishe kulingana na uhitaji wako
βœ… Utapata punguzo na ofa maalum kwa wanachama pekee
βœ… Utauliza maswali na kujibiwa na mtaalamu wa lishe

🌟 Usikose nafasi hii ya kuboresha afya yako na familia yako!
πŸ‘‰ Jiunge sasa kupitia link hii:

πŸ”— https://shorturl.at/pWzSs

Tupate kidogo elimu ya lishe kwa mama anaenyonyesha
06/02/2025

Tupate kidogo elimu ya lishe kwa mama anaenyonyesha

Lishe bora kwa mama anayenyonyesha ni muhimu sana kwa afya yake na ukuaji mzuri wa mtoto wake. Mama anayenyonyesha anahitaji virutubishi vya kutosha ili kuzalisha maziwa yenye lishe bora kwa mtoto na kudumisha afya yake mwenyewe.

https://imalilo.com/lishe-2/
03/02/2025

https://imalilo.com/lishe-2/

Lishe bora kwa mama anayenyonyesha ni muhimu sana kwa afya yake na ukuaji mzuri wa mtoto wake. Mama anayenyonyesha anahitaji virutubishi vya kutosha ili kuzalisha maziwa yenye lishe bora kwa mtoto na kudumisha afya yake mwenyewe.

https://imalilo.com/unga-wa-rosella-beetroot/
03/02/2025

https://imalilo.com/unga-wa-rosella-beetroot/

Unga wa Rosella (Hibiscus) na Beetroot ni mchanganyiko wenye nguvu wa mimea asilia unaotoa lishe bora kwa mwili wako. Unga huu unatokana na maua ya Rosella yaliyokaushwa na kusagwa pamoja na mizizi ya Beetroot, bila kemikali wala vihifadhi bandia. Rosella inajulikana kwa kuwa na vitamini C nyingi, i...

07/01/2025

DAWA ZA UZAZI WA MPANGO ZINAATHIRI VIPI MZUNGUKO WA HEDHI
Kwanza kabisa tuangalie udhibiti wa hormone katika mzunguko wa hedhi, yaani hormone zipi zinahusika na mzunguko wa hedhi na zinafanya vipi kazi.K**a inavyoonekana katika mchoro huu.

Katika ubongo kuna tezi ya hipothalmas inayozalisha hormone ya Gonadotropini hii hormone inachochea tezi ya pituitari ambayo nayo ipo kwenye ubongo kuzalisha hormone zifatazo

1.hormone chochezi ya mayai (FSH) ambayo huchochea kukua na kupevuka kwa mayai na kuchochea mfuko wa mayai (ovari) kuzalisha hormone za uzazi estrogen na progesterone.

2.Hormone ya lutea ambayo huchochea kuachiliwa kwa yai kutoka kwenye mfuko wa mayai (Ovulation).

Baadae estrogen na progesterone ambazo zinakazi kubwa katika mzunguko zinapokuwa zimezalishwa kwa kiasi cha kutosha zinafanya sasa tezi ya hipothalmus isizalishe tena Hormone ya gonadotropin na kuzuia mzunguko mzima.

Pindi unapokaribia hedhi estrogen na progesterone zinashuka kiwango ili kuruhusu Hipothalmus izalishe tena gonadotropin ili mzunguko uanze tena

JE DAWA ZA UZAZI WA MPANGO K**A MAJIRA ,P2 NA NYINGINEZO ZINAATHIRI VIPI MZUNGUKO?

Kwanza kabisa ile dhana kwamba zinaacha sumu si kweli,
Unapomeza mfano vidonge ndani ya masaa 24 hadi 36 zinakuwa zimeshatolewa kabisa mwilini kupitia ini.

Sasa kwa nini mtu anaweza kukosa hedhi baada ya kuacha kutumia hizi dawa.

Dawa hizi zinakuwa na kemikali ambazo zinafanana na hormone ya progesterone na nyingine zina dawa inayofanana na estrogen.

Zinapoingia mwilini zinafanya kazi k**a hormone hizo na kuziba vijishikizo (receptors) za hormone hizo, mwili huhisi kuwa kuna kiwango kikubwa cha hormone ya estrogen na progesterone matokeo yake hipothalmus inakuwa inactive na kuacha kuzalisha hormone ya gonadotropin na kuathiri uzalishwaji wa mayai na hedhi. Hadi mtu hapati ujauzito. Kwa hiyo znafanya kazi kwa kuvuruga huo mpangilio wa hormone.

Unapoacha kutumia tezi ya hipothalmus kurudia hali yake ya kawaida kuanza kuzalisha gonadotropin inatofautiana kati ya mtu na mtu wengine muda mfupi na wengine muda mrefu kwani mwili umekua tegemezi kwa hizo hormone zilizomo kwenye dawa kuliko zile unazozalisha wenyewe.

HIVO BASI DAWA HIZI HAZIACHI SUMU BALI ZINAVURUGA JINSI MFUMO WA HORMONE UNAVORATIBU MZUNGUKO WA HEDHI

SABABU ZA MAMA MJAMZITO KUTOKWA NA JASHO SANA.DR.JOHANESWanawake wengi katika kipindi cha ujauzito hutokwa sana na jasho...
07/01/2025

SABABU ZA MAMA MJAMZITO KUTOKWA NA JASHO SANA.
DR.JOHANES

Wanawake wengi katika kipindi cha ujauzito hutokwa sana na jasho hasa wakati wa usiku.

Je nini husababisha?

Mabadiliko ya viwango vya vichochezi vya mwili (homornes); kipindi cha ujauzito huambatana na mabadiliko ya viwango vya vichochezi, mabadiliko haya huuweka mwili katika hali ya kuweza kubeba ujauzito kwa kipindi cha miezi yote 9.

Kichochezi aina ya projesteroni huongezeka na kuwa katika kiwango kikubwa katika damu wakati wa ujauzito, mabadiliko haya hupelekea mishipa mingi ya damu iliyo karibu na ngozi kutanuka hivyo kuruhusu damu kupita kwa wingi hivyo kuongeza kiasi cha maji yanayopotea kwa njia ya jasho.

Kutokwa na jasho husaidia kuupoza mwili hivyo hii hutokea ili kuuweka mwili katika hali ya msawazo wa joto.

Kufanya kazi nzito: Mama mjamzito kwa kawaida huchoka haraka hata baada ya shughuli ndogo. Hivyo iwapo mama mjamzito anafanya shughuli nzito huweza kupelekea kuongezeka kwa kiwango cha jasho kinachotolewa.

Maambukizi ya magonjwa: Wakati mwingine kutokwa na jasho sana hasa wakati wa usiku huweza kuwa ni dalili ya mwanzo ya homa (fever) ambayo huashiria kuwepo kwa maambukizi ya magonjwa. Hivyo ni vyema k**a ukiona hali ya kutokwa na jasho si ya kawaida, basi wahi kituo cha afya kwa uchunguzi zaidi.

Je nifanye nini kupunguza kutokwa na jasho sana?

Pendelea kukaa maeneo ya wazi ambako kuna mzunguko mkubwa wa hewa safi.
Pia epuka kuvaa nguo nyingi au zinazobana mwili bali pendelea kuvaa nguo nyepesi kwani huruhusu mzunguko wa hewa.
Pendelea kufanya mazoezi mepesi
Ni vyema kuoga kabla ya kulala
Kwa sababu kutokwa na jasho kwa wingi husababisha mwili kupoteza maji sana hivyo basi ni vyema kunywa maji ya kutosha kila siku.

Karibu sana katika Whatsapp Community ya Afya! Hii ni mahali ambapo tunapenda kujifunza na kushirikishana mada mbalimbal...
02/04/2023

Karibu sana katika Whatsapp Community ya Afya! Hii ni mahali ambapo tunapenda kujifunza na kushirikishana mada mbalimbali kuhusu afya na lishe. Kupitia makundi yetu, tunakupa nafasi ya kujifunza kutoka kwa wataalamu wetu wa afya na lishe, na pia kushirikiana uzoefu na watu wengine kwenye jamii yetu.
Tunaelewa kuwa afya ni kitu cha msingi na ni muhimu kuhakikisha tunaimarisha afya zetu kwa kufuata maelekezo ya wataalamu. Kupitia makundi yetu, utapata elimu ya afya na lishe, na pia ushauri wa kitaalamu kuhusu matatizo ya afya.
Kwa hiyo, ikiwa wewe ni mpenzi wa afya na unataka kujifunza na kushirikishana na wengine kuhusu afya, basi hii ni jamii sahihi kwako. Karibu ujiunge nasi, tukajifunze na kuboresha afya zetu pamoja.
Tunayo makundi mbalimbali ambayo yatajikita kwenye masuala tofauti ya afya, ikiwa ni pamoja na:
Darasa la Afya: Kundi hili litakuwa na madaktari wetu wakitoa elimu ya afya kila siku. Tutajifunza kuhusu magonjwa mbalimbali na jinsi ya kuyatibu, pamoja na njia za kuzuia magonjwa haya.

Elimu ya Lishe: Kundi hili litakuwa maalumu kwa wataalamu wetu wa lishe watakao toa elimu ya lishe kwa wajawazito, watoto, mama wanaonyonyesha na watu wanaopungua uzito. Tutajifunza jinsi ya kula vyakula sahihi ili kuboresha afya zetu.

Hedhi Salama: Kundi hili litakuwa maalumu kwa watu wenye matatizo ya hedhi, k**a vile kutopata hedhi, kuvuja damu nyingi wakati wa hedhi na matatizo mengine ya hedhi. Tutapata mafunzo na ushauri kuhusu jinsi ya kutatua matatizo haya.

Hormones Class: Kundi hili litakuwa maalumu kwa watu wenye matatizo ya hormone imbalance. Tutajifunza jinsi ya kutambua na kutibu matatizo haya ya kiafya.

Rijali: Kundi hili litakuwa maalumu kwa wanaume tu, kwa ajili ya elimu ya afya ya uzazi kwa wanaume na matatizo yote ya wanaume, k**a vile tezi dume, nguvu za kiume na kadhalika.

Chat Room: Kundi hili litakuwa maalumu kwa ajili ya wana community kushirikiana mambo mbalimbali na experiences kuhusu afya. Pia kwa wenye bidhaa za afya kutangaza biashara zao.

Tunakukaribisha katika Whatsapp Community ya Afya, ambapo tutajifunza, kushirikiana na kuboresha afya zetu. bofya link hii kujiunga.
https://chat.whatsapp.com/K9TMlYdKMtLJbR1d58vAoj

Address

Bukoba
Bukoba
255

Telephone

+255762167811

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr.Joh Healthcare posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Dr.Joh Healthcare:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category