Sobriety Forever Rehabilitation Centre

Sobriety Forever Rehabilitation Centre "Kagera Regional First De-addiction Centre"

SOBRIETY FOREVER REHABILITATION CENTRE - KAGERA is the treatment centre for
substance dependence and therefore the centre has a rich experience in handling alcoholics and drug addicts.

Homa ya ini inajulikana kitaalamu k**a *Hepatitis* . Ni hali ambapo ini  linavimba na kushindwa kufanya kazi zake vizuri...
25/03/2026

Homa ya ini inajulikana kitaalamu k**a *Hepatitis* . Ni hali ambapo ini linavimba na kushindwa kufanya kazi zake vizuri k**a kusafisha sumu mwilini na kusaidia mmeng’enyo wa chakula.
‎ *Chanzo cha homa ya ini*
‎Homa ya ini husababishwa zaidi na virusi vinavyoitwa:
▪️‎Hepatitis A
▪️‎Hepatitis B
▪️‎Hepatitis C
‎Lakini pia inaweza kusababishwa na:
▫️‎Matumizi makubwa ya pombe 🍺
▫️‎Dawa kali au sumu mwilini
▫️‎Magonjwa ya kinga kushambulia ini (autoimmune)
‎ *Njia za maambukizi*
‎Inategemea aina ya hepatitis
*‎1. Hepatitis A*
▫️‎Kula chakula au kunywa maji machafu
▫️‎Usafi duni wa mikono
▫️Lakini inaweza kuambukizwa kwa ngono ya mdomo (oral–anal contact)
*‎2. Hepatitis B & C*
▫️‎Ngono zembe bila kinga
▫️‎Kuchangia sindano au vifaa vyenye damu
▫️‎Kuongezewa damu isiyopimwa
▫️‎Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua
‎ *Dalili za homa ya ini*
▫️‎Uchovu sana
▫️‎Homa ndogo
▫️‎Kichefuchefu na kutapika
▫️‎Maumivu upande wa juu kulia wa tumbo
▫️‎Mkojo kuwa wa rangi ya giza
▫️‎Ngozi na macho kuwa ya njano (jaundice)
▫️‎Kupoteza hamu ya kula

U J U M B E
03/03/2026

U J U M B E

"HATA IWEJE, BADO NI WETU"Katika jamii au familia tunakuwa na waathirika wa pombe (walevi sugu) na dawa nyinginezo za ku...
10/02/2026

"HATA IWEJE, BADO NI WETU"

Katika jamii au familia tunakuwa na waathirika wa pombe (walevi sugu) na dawa nyinginezo za kulevya kulevya. Tunawatenga na kuwadharau waathirika na wakati huo huo tukiwaona k**a "HASARA" NA "LAANA" ndani ya jamii bila kujua kuwa hao ni WAGONJWA NA WANAHITAJI MSAADA WA TIBA K**A WAGONJWA WA MARADHI MENGINEYO.

Tukidhani kwa namna moja au nyingine "WARAIBU" hawana maana tena, tutakuwa tunakosea sana, cha msingi ni kushirikiana na taasisi, asasi, mbalimbali za kusaidia wagonjwa hawa.

Nasi k**a SOBRIETY FOREVER REHABILITATION CENTRE kazi yetu kubwa ni kutoa usaidizi kwa waathirika wa pombe na dawa nyinginezo za kulevya.

Tuwasiliane kwa namba hii:
+255 789 78 05 29. Ili tuweze kutoa usaidizi kwa wazazi, ndugu, jamaa, watoto, marafiki na hatimaye nao waweze kurudi katika utimamu na kuchukua MAJUKUMU YAO K**A ZAMANI na maisha yaleta MAANA. Asante. NB: USHAURI NI BURE.

K U J I K U B A L I (ACCEPTANCE):Wiz Khalifa, amethibitisha rasmi kuacha kunywa pombe kabisa. Kupitia ujumbe wake, rapa ...
30/09/2025

K U J I K U B A L I (ACCEPTANCE):

Wiz Khalifa, amethibitisha rasmi kuacha kunywa pombe kabisa. Kupitia ujumbe wake, rapa huyo alisema:

“Nilikwisha kuacha kunywa pombe kabla na sasa naweza kusema tena kwamba hakuna pombe yoyote itakayoweza kuingia mwilini mwangu kamwe.”

Wiz Khalifa ameeleza kuwa hata alipobakiza kunywa kinywaji kimoja tu kwa wiki, mwili wake haukushindwa kuhimili. Alisema:

“Nimepunguza hadi kinywaji kimoja kwa wiki lakini mwili wangu hauwezi hata kushughulikia hicho tena. Hangovers zinahisi k**a milango ya mbinguni inafunguka na hiyo haifai kwa starehe ya muda mfupi.”

Aidha, rapa huyo aliongeza kuwa kunywa pombe hakukuleta furaha ya kweli:

“Zaidi ya yote, si starehe hata kidogo. Yote ninayofanya ni kusema maneno yasiyo na maana na kulala kwenye kochi nikiwa nimevaa nguo zote. Niko sawa. Imatosha.”

Kwa mujbu wa maneno yake, sasa Wiz Khalifa anafurahia afya yake akiwa mbali na pombe.

*“Uraibu katika Muktadha wa Afya ya Akili na Kukatisha Uhai”* 🧠💔👉 Mada hii itaangazia namna uraibu wa dawa za kulevya un...
24/09/2025

*“Uraibu katika Muktadha wa Afya ya Akili na Kukatisha Uhai”* 🧠💔

👉 Mada hii itaangazia namna uraibu wa dawa za kulevya unavyohusiana na changamoto za afya ya akili na vitendo vya kukatisha uhai.

📌 Pia tutajikita kwenye Nafasi ya Mamlaka katika Kupambana na Kudhibiti Matumizi ya Dawa za Kulevya ili kupunguza athari zinazohusiana na afya ya akili kwa jamii.

🗣 Mzungumzaji:
SHABANI Miraji – Afisa Elimu Jamii, DCEA

🗓 Alhamisi, 25 Septemba 2025
⏰ Saa 2:00 – 3:00 Usiku (EAT)
👇🏽
https://us06web.zoom.us/j/87453481716?pwd=0MCWm9AHxza2gntlE83jO4Mlf6w0AD.1

Karibuni kwa mjadala wenye kuleta mwanga na matumaini! ✨

📞 Wasiliana nasi:
🌐 www.akilihuru.org | 📧 info@akilihuru.org | ☎ +255 746 802 135
📲 Instagram:

✝️ PUMZIKA KWA AMANI ✝️UONGOZI WA KITUO CHA Sobriety Forever Rehabilitation Centre.UNATOA POLE KWA FAMILIA KUFUATIA MSIB...
18/08/2025

✝️ PUMZIKA KWA AMANI ✝️

UONGOZI WA KITUO CHA Sobriety Forever Rehabilitation Centre.

UNATOA POLE KWA FAMILIA KUFUATIA MSIBA WA MMOJA WA WADAU WETU MA. DEMETRIA KOMUGISHA WALIKUWA WANAJITOLEA KWA HALI NA MALI KATIKA KUISAIDIA HUDUMA YETU.

PIA TUNATOA POLE SANA KWA KITUO CHA Radio Mbiu | Radio Maria Tanzania KWA KUMPOTEZA MTENDA KAZI NA KATIKA UHAMASISHAJI WA MATUKIO YA HUDUMA.

"RAHA YA MILELE UWAPE, EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UWAANGAZIE, MAREHEMU WOTE, WAPUMZIKE KWA AMANI". AMINA.

S O M O:Matumizi ya pombe kupitiliza (ulevi sugu) ni maradhi k**a yalivyo maradhi mengineyo. Maradhi haya hayana uhusian...
18/08/2025

S O M O:

Matumizi ya pombe kupitiliza (ulevi sugu) ni maradhi k**a yalivyo maradhi mengineyo.

Maradhi haya hayana uhusiano wowote na masuala ya USHIRIKINA / KUROGWA.

Zipo huduma mbalimbali za kudhibiti (to arrest) hali hiyo na mwathirika kuweza kurudi katika utimamu na kuchukua majukumu yake katika maisha.

KWA HUDUMA YA KUTOA USAIDIZI KWA WAATHIRIKA WA POMBE NA DAWA NYINGINE ZA KULEVYA WASILIANA NASI Sobriety Forever Rehabilitation Centre NAFUU INAPATIKANA NA MAISHA YANAENDELEA.

Kwa msaada zaidi tuwasiliane kwa namba hizi:
0789 78 05 29
0767 05 83 51
0620 17 62 48

Well, Another year of God's Grace in my life. 12 years of sober and clean living. We all have a choice each day, mine is...
30/07/2025

Well,

Another year of God's Grace in my life. 12 years of sober and clean living. We all have a choice each day, mine is to serve the plan God has for my life. Wish I could say it was always that way, but today is all that counts. Am only posting to let people know it is possible.

| HP | A.A | MEETINGS | STEP WORK | INTO ACTION | SPONSOR (SHIP) | KCB | ODAAT |

Love y'all.

S O M O:Wapendwa tujitahidi kulinda AFYA YA AKILI (MENTAL HEALTH ISSUES). Unakaribishwa SOBRIETY FOREVER REHABILITATION ...
20/05/2025

S O M O:

Wapendwa tujitahidi kulinda AFYA YA AKILI (MENTAL HEALTH ISSUES).

Unakaribishwa SOBRIETY FOREVER REHABILITATION CENTRE - KAGERA k**a una changamoto ya matumizi ya vileo kupita kiasi (ULEVI SUGU).

Usijaribu kukabiliana na msongo wa mawazo (depression) kwa kutumia vileo.

Tutembelea kituoni kwetu SOBRIETY FOREVER REHABILITATION CENTRE - BUKOBA MANISPAA - KATA YA KAGONDO - MTAA WA AMANI - JENGO NAMBA 104.

KWA MAWASILIANO ZAIDI:
0789 78 05 29
0620 17 62 48
0760 05 83 51

Email:
rnelsontz@gmail.com

SOMO: SEHEMU YA KWANZA.DALILI ZA ULEVI SUGU. Ni kwa hisani ya kituo cha kutoa usaidizi kwa waathirika wa matumizi ya pom...
17/05/2025

SOMO: SEHEMU YA KWANZA.

DALILI ZA ULEVI SUGU.

Ni kwa hisani ya kituo cha kutoa usaidizi kwa waathirika wa matumizi ya pombe kupita kiasi "ULEVI SUGU" na dawa nyinginezo za kulevya.

Sobriety Forever Rehabilitation Centre - KAGERA.

Mawasiliano:
+255 789 78 05 29
+255 620 17 62 48
+255 767 05 83 51

Email: sftanzania@gmail.com

06/05/2025

Address

Bukoba

Opening Hours

Monday 08:00 - 16:00
Tuesday 08:00 - 16:00
Wednesday 08:00 - 16:00
Thursday 08:00 - 16:00
Friday 08:00 - 16:00
Saturday 08:00 - 12:00

Telephone

+255789780529

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sobriety Forever Rehabilitation Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Sobriety Forever Rehabilitation Centre:

Share