afya_point255

afya_point255 AFYA||TIBA||USHAURI
Suluhisho kwa changamoto ya uzazi kwa wanawake na wanume

SEHEMU YA PILI ๐Ÿ”จAina mojawapo ya endometriosis ni endometriosis inayopatikana ndani ya msuli wa mfuko wa  uzazi. Aina hi...
05/05/2024

SEHEMU YA PILI ๐Ÿ”จ

Aina mojawapo ya endometriosis ni endometriosis inayopatikana ndani ya msuli wa mfuko wa uzazi. Aina hii ya endometriosis huitwa Adenomyosis. Mara chache hutokea endometriosis kuwa sehemu zilozo mbali na viungo vya uzazi k**a vile kwenye mapafu, jambo ambalo husababisha kukohoa damu wakati wa hedhi (catamenial hemoptysis).

๐Ÿ’ฅ Dalili za Endometriosis ni zipi?

Dalili za uwepo wa endometriosis ni pamoja na;

Maumivu wakati wa hedhi kwa kitaalam (dysmenorrhoea)

Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi au siku za hedhi kuwa nyingi zaidi

Kushindwa kupata ujauzito (infertility),

Maumivu wakati wa kufanya tendo la ndoa (dyspareunia)

Maumivu wakati wa haja kubwa au ndogo.

๐ŸŒฟUtambuzi wa Endometriosis

Mwanamke mwenye dalili za endometriosis anatakiwa kupimwa na daktari ili aweze kupewa ushauri wa matibabu.
Zipo njia kuu tatu:

Njia ya uchunguzi wa pelvis inayofanywa na daktari

Kwa njia ya ultrasound

Kupimwa kwa njia ya upasuaji wa matundu madogo (laparoscopy). Njia ya upasuaji wa matundu madogo ndio inayotumika zaidi kwenye kugundua uwepo wa endometrisis na hapohapo ugonjwa huweza kuondolewa.
Daktari hupeleka sehemu ya ugonjwa aliyoitoa kwenye vipimo vya maabara (pathology) ambayo huthibitisha uwepo wa tishu aina ya endometriosis.

Kutokana na kutokuwepo kwa njia hii katika vituo vingi vya huduma nchini Tanzania, ugonjwa wa endometriosis hausikiki sana nchini, lakini upo na wanawake wengi wenye maumivu yasiyotibika kwa dawa wakipimwa wanauwezekano mkubwa wa kukutwa na ugonjwa huu

TUENDELEE...??๐Ÿ’‰






SEHEMU YA โœ๐Ÿพ๐Ÿ’ฅ Endometriosis ni ugonjwa gani?? Ukuta wa ndani wa mfuko wa  uzazi unaitwa endometrium. Ukuta huu hujengeka...
03/04/2024

SEHEMU YA โœ๐Ÿพ

๐Ÿ’ฅ Endometriosis ni ugonjwa gani??

Ukuta wa ndani wa mfuko wa uzazi unaitwa endometrium. Ukuta huu hujengeka na kubomoka kila mwezi na kusababisha hedhi kwa wanawake. Kujengeka na kubomoka kwa ukuta huu wa ndani wa kifuko cha uzazi kunasababishwa na mabadiliko ya kiasi cha homoni za uzazi mwilini.

Endometriosis ni ugonjwa unaosababishwa na uwepo wa tishu zinazofanana na ukuta wa ndani wa mfuko wa uzazi (endometrium) sehemu nyingine kwenye mwili. Mara nyingi tishu hizi huota kwenye sehemu ya chini ya tumbo (pelvis) karibu na ovari, kifuko cha uzazi, kibofu cha mkojo na njia ya haja kubwa. K**a ilivyo kwa ukuta wa ndani ya mfuko wa uzazi (endometrium), tishu hizi zinazopatikana nje ya mfuko wa uzazi pia hujengeka na kubomoka kutokana na mzunguko wa hedhi. Kwa sababu hii, hata dalili za uwepo wa ugonjwa wa endometriosis hufuatana na mzunguko wa hedhi.

๐Ÿ’ฅ Sababu za Endometriosis ni zipi??

Kitu kinachosababisha ugonjwa huu hakifahamiki kwa uhakika lakini zipo baadhi ya nadharia zinazohusishwa na ugonjwa huu

Endometriosis inahusishwa na damu ya hedhi yenye seli za ukuta wa mfuko wa uzazi yani endometrium kurudi nyuma kupitia mirija ya uzazi badala ya kutoka mwilini kupitia ukeni,hizi seli hushik**ana na kujua na hivyo kusababisha endometriosis,kwa kitaalam hali hii inaitwa retrogade menstruation.

Nadharia nyingine iliyopo kuhusu kisababishi cha endometriosis ni kuwa tishu za endometrium huenea sehemu nyingine za mwili kupitia damu au mfumo wa lymph

Kutokana na uwepo wa endometriosis ndani ya tumbo, damu inayotokana na kujengeka na kubomoka kwake kila mwezi hukosa njia ya kutokea. Kwa sababu hii, damu hii huganda na kusababisha makovu kwenye sehemu ya ndani ya tumbo (abdominal cavity). Ugonjwa ukiendelea muda mrefu makovu haya huweza kushambulia kiungo kilichokuwa na endometriosis na kukiharibu. Kwa mfano, endometriosis ikishambulia ovari inaweza kuziharibu na kusababisha mwanamke kushindwa kutoa mayai na kupata mtoto, ikishambulia njia ya mkojo inaweza kuiziba njia hiyo na kusababisha figo kuharibika

INAENDELEA......โœจโœจ

"KUIELEKEA SAFARI YA KUSHIKA UJAUZITO NA KUITWA MAMA "๐ŸŒฑ Safari ya kuwa wazazi inaweza kuwa ngumu, na kwa ulimwengu wa le...
24/02/2024

"KUIELEKEA SAFARI YA KUSHIKA UJAUZITO NA KUITWA MAMA "

๐ŸŒฑ Safari ya kuwa wazazi inaweza kuwa ngumu, na kwa ulimwengu wa leo, wapenzi wengi wanakabiliwa na ugumu wanapojaribu kupata ujauzito. ๐Ÿ’”๐Ÿ‘จโ€๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿ‘งโ€๐Ÿ‘ฆ Hebu tuangazie sababu zinazoweza kusababisha tatizo hili linaloongezeka๐Ÿ’ก

1๏ธโƒฃ Matatizo ya Ovulation: Ovulation isiyofuata mpangilio au kutokuwepo kwa ovulation inaweza kufanya iwe vigumu kwa wanawake kupata ujauzito. Hali k**a vile ugonjwa wa polycystic o***y syndrome (PCOS), usawa wa homoni usio sahihi, na upungufu wa mapema wa ovari unaweza kuharibu ovulation

2๏ธโƒฃ Mtindo wa maisha/Njia za maisha: Njia za maisha za kisasa zilizojaa msongo wa mawazo, tabia za kutokufanya mazoezi, na kuwa katika mazingira yenye sumu yanaweza kuathiri uzazi. Ni muhimu kuweka kipaumbele katika kujali afya yako, kusimamia msongo wa mawazo kwa ufanisi, na kuchukua mtindo wa maisha wenye afya. ๐ŸŒฟ๐Ÿ‹๏ธโ€โ™€๏ธ

3๏ธโƒฃ Kuvurugika kwa Homoni: Magonjwa ya homoni k**a s polycystic ovarian syndrome (PCOS) na kutokuwa kawaida kwa tezi yanaweza kuvuruga usawa wa homoni muhimu kwa ajili ya kutunga mimba. Kupata muongozo wa kitaalamu wa matibabu kunaweza kusaidia kutatua kuvurugika huku. ๐ŸŒธโš–๏ธ

4๏ธโƒฃ Matatizo ya Afya ya Uzazi:
Hapa ndipo penye changamoto nyingi za uzazi
Hali k**a endometriosis, fibroids, ovarian cysts,PID na mirija ya uzazi iliyoziba inaweza kuwa changamoto katika kutunga mimba. Kupata uchunguzi wa kitaalamu na kuchunguza njia za matibabu zilizopo kunaweza kuongeza nafasi za kupata ujauzito kwa mafanikio. ๐Ÿฉบ๐Ÿ’ช

UHALISIA WA HII HALI YA KUSHINDWA KUPATA UJAUZITO UKOJE???

Kiukweli wanawake wengi wanaopitia changamoto hii ya kushindwa kupata ujauzito hupitia wakati mgumu sana mpaka kupelekea kukosa furaha na amani katika ndoa zao na wengine hukata kabisa tamaa kutokana na kutafuta suluhisho la changamoto zao uzazi kwa muda mrefu bila mafanikio...

Habari njema ni kuwa suluhisho kwa changamoto za uzazi zinazopelekea kushindwa kushika ujauzito lipo,Tiba ipo na ni ya uhakika kabisa.Lengo letu ni kuwarejeshea furaha watu waliojaribu kushika ujauzito kwa muda mrefu bila mafanikio

Kwa tiba,ushauri kuhusu masuala ya kiafya,na elimu ya afya wasiliana nasi kupitia
WhatsApp/Calls:0753843505

"KUIELEKEA SAFARI YA KUSHIKA UJAUZITO NA KUITWA MAMA "๐ŸŒฑ Safari ya kuwa wazazi inaweza kuwa ngumu, na kwa ulimwengu wa le...
23/02/2024

"KUIELEKEA SAFARI YA KUSHIKA UJAUZITO NA KUITWA MAMA "

๐ŸŒฑ Safari ya kuwa wazazi inaweza kuwa ngumu, na kwa ulimwengu wa leo, wapenzi wengi wanakabiliwa na ugumu wanapojaribu kupata ujauzito. ๐Ÿ’”๐Ÿ‘จโ€๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿ‘งโ€๐Ÿ‘ฆ Hebu tuangazie sababu zinazoweza kusababisha tatizo hili linaloongezeka๐Ÿ’ก

1๏ธโƒฃ Matatizo ya Ovulation: Ovulation isiyofuata mpangilio au kutokuwepo kwa ovulation inaweza kufanya iwe vigumu kwa wanawake kupata ujauzito. Hali k**a vile ugonjwa wa polycystic o***y syndrome (PCOS) na usawa wa homoni usio sahihi.

2๏ธโƒฃ Mtindo wa maisha/Njia za maisha: Njia za maisha za kisasa zilizojaa msongo wa mawazo, tabia za kutokufanya mazoezi, na kuwa katika mazingira yenye sumu yanaweza kuathiri uzazi. Ni muhimu kuweka kipaumbele katika kujali afya yako, kusimamia msongo wa mawazo kwa ufanisi, na kuchukua mtindo wa maisha wenye afya. ๐ŸŒฟ๐Ÿ‹๏ธโ€โ™€๏ธ

3๏ธโƒฃ Kuvurugika kwa Homoni: Magonjwa ya homoni k**a s polycystic ovarian syndrome (PCOS) na kutokuwa kawaida kwa tezi yanaweza kuvuruga usawa wa homoni muhimu kwa ajili ya kutunga mimba. Kupata muongozo wa kitaalamu wa matibabu kunaweza kusaidia kutatua kuvurugika huku. ๐ŸŒธโš–๏ธ

4๏ธโƒฃ Matatizo ya Afya ya Uzazi:
Hapa ndipo penye changamoto nyingi za uzazi
Hali k**a endometriosis, fibroids, ovarian cysts,PID na mirija ya uzazi iliyoziba inaweza kuwa changamoto katika kutunga mimba. Kupata uchunguzi wa kitaalamu na kuchunguza njia za matibabu zilizopo kunaweza kuongeza nafasi za kupata ujauzito kwa mafanikio. ๐Ÿฉบ๐Ÿ’ช

UHALISIA WA HII HALI YA KUSHINDWA KUPATA UJAUZITO UKOJE???

Kiukweli wanawake wengi wanaopitia changamoto hii ya kushindwa kupata ujauzito hupitia wakati mgumu sana mpaka kupelekea kukosa furaha na amani katika ndoa zao na wengine hukata kabisa tamaa kutokana na kutafuta suluhisho la changamoto zao uzazi kwa muda mrefu bila mafanikio...

Habari njema ni kuwa suluhisho kwa changamoto za uzazi zinazopelekea kushindwa kushika ujauzito lipo,Tiba ipo na ni ya uhakika kabisa.Lengo letu ni kuwarejeshea furaha watu waliojaribu kushika ujauzito kwa muda mrefu bila mafanikio

Kwa tiba,ushauri kuhusu masuala ya kiafya,na elimu ya afya wasiliana nasi kupitia:

WhatsApp/Calls:0753 843 505

Unafahamu nini kuhusu ugonjwa wa Endometriosis?kaa tayari kwa somo weka notification onFollow afya_point255             ...
17/10/2023

Unafahamu nini kuhusu ugonjwa wa Endometriosis?kaa tayari kwa somo weka notification on





Follow afya_point255





๐Œ๐€๐”๐Œ๐ˆ๐•๐” ๐Œ๐€๐Š๐€๐‹๐ˆ ๐˜๐€ ๐Œ๐†๐Ž๐๐†๐Ž ๐๐€ ๐Š๐ˆ๐”๐๐Ž ( ๐๐š๐š๐๐š ๐ฒ๐š ๐Š๐ฎ๐ฃ๐ข๐Ÿ๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ๐š )Hili somo linawafaa wanawake wote, Mjulishe mwenzio aje ajifunz...
18/08/2023

๐Œ๐€๐”๐Œ๐ˆ๐•๐” ๐Œ๐€๐Š๐€๐‹๐ˆ ๐˜๐€ ๐Œ๐†๐Ž๐๐†๐Ž ๐๐€ ๐Š๐ˆ๐”๐๐Ž ( ๐๐š๐š๐๐š ๐ฒ๐š ๐Š๐ฎ๐ฃ๐ข๐Ÿ๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ๐š )
Hili somo linawafaa wanawake wote, Mjulishe mwenzio aje ajifunze,utapata ushauri na mambo ya kuzingatia

Somo litaendelea muda si mrefu

"JE WAYAJUA MAMBO MANNE(4) YANAYOWEZA KUKUZUIA KUPATA UJA UZITO KWA HARAKA??!!"Yafuatayo ni mambo yanayoweza kumpelekea ...
20/07/2023

"JE WAYAJUA MAMBO MANNE(4) YANAYOWEZA KUKUZUIA KUPATA UJA UZITO KWA HARAKA??!!"

Yafuatayo ni mambo yanayoweza kumpelekea mwanamke kushindwa kupata ujauzito haraka

๐Ÿ’ฅ PID(Pelvic inflammatory disease)
Haya ni maambukizi ya bakteria katika via vya uzazi,shingo ya kizazi,mirija ya uzazi,mayai na mfuko wa uzazi
PID huweza kupelekea kukosa ujauzito isipotibiwa mapema

๐Ÿ’ฅ Fibroids/Uvimbe
Fibroids ni uvimbe usio wa saratani ambao hujitokeza kwenye ukuta wa mfuko wa mimba.Fibroids zinaweza pia kusababisha kukosa ujauzito au ugumba

๐Ÿ’ฅ Kuziba Kwa mirija ya uzazi(Fallopian tubes)
Kuziba kwa mirija ya uzazi ni hali ya kujaa kwa maji kwenye mirija ya uzazi ambako kunazuia yai kusafiri kutoka kwenye mifuko ya mayai(ovaries) kwenda mji wa mimba(uterus)

๐Ÿ’ฅ Hormone imbalance(Kuvurugika kwa vichocheo)
Mvurugiko wa vichocheo ni sababu kubwa inayopeleka kuchelewa kupata ujauzito na kupelekea ugumba k**a hii hali isipotibiwa mapema

๐Ÿ‚Tatizo la kushindwa kupata ujauzito ni tatizo kubwa sana wanalopitia wanawake wengi na wengine wamekuwa wakihangaika kwa muda mrefu kupata suluhisho bila mafanikio na kupelekea hata kukata tamaa kwa baadhi yao na kufikiri hawawezi kupona,baada ya kujaribu tiba mbalimbali sababu kubwa ikiwa kutumia dawa mbali mbali bila kujua chanzo cha tatizo.

๐ŸŒฟHabari njema ni kwamba suluhisho kwa changamoto za uzazi zipo na ni za uhakika,unaweza kuwasiliana nasi kwa ajili ya ushauri,na elimu juu ya masuala ya afya,pamoja na tiba
Huduma ya ushauri au maswali yoyote kuhusu afya ni bure kabisa
Whatsapp/Calls:0753843505
Tuma sms Whatsapp/DM muda wowote ule 24/7

Asanteni๐Ÿค

SEHEMU YA 3 ๐Ÿ’ฅ Hatua 4 Zifuatazo Zitakusaidia  Kuzuia Kupata Maambukizi Kwenye Njia Ya Uzazi (PID) Na Magonjwa Ya Zinaa1....
20/07/2023

SEHEMU YA 3

๐Ÿ’ฅ Hatua 4 Zifuatazo Zitakusaidia Kuzuia Kupata Maambukizi Kwenye Njia Ya Uzazi (PID) Na Magonjwa Ya Zinaa

1.Fanya ngono salama kwa kutumia kinga na kuishi na mpenzi mmoja mwaminifu.
hii ni hatua muhimu ya kwanza na ya uhakika zaidi katika kuzuia kupata PID . K**a ukichagua kuwa na wapenzi wengi basi hakikisha unavaa condom kwa kila tendo.

2. K**a una mpenzi mmoja na kati yenu kuna ambaye kaugua basi hakikisheni mnaacha kufanya ngono mpaka pale mtakapotibiwa mkapona kabisa.

3. Hakikisha unafanya vipimo kwa magonjwa ya zinaa na kuyatibu haraka iwezekanavyo
wataalamu wa afya wanashauri kwamba watu walioko chini ya miaka ishirini na tano wafanye vipimo kila mwaka kwa magonjwa ya zinaa k**a chlamydia.

4. Wanawake wenye wapenzi wengi wanatakiwa kuonana na mtaalamu wa magonjwa ya wanawake(gynecologist) kwa vipimo kugundua uwepo wa vimelea vya magonjwa ya zinaa.ni muhimu kufanya vipimo mapema .

5. Jikinge na maradhi ya bacteria na maambukizi mengine

๐Ÿ’ฅ Baadhi ya njia unazoweza kutumika kuzuia kutokea kwa maambukizi ni

1.Tumia sabuni zisizo na harufu kali(mild soap) kujisafisha- kuosha uke kwa kutumia sabuni zenye harufu kali na kemikali hufanya tishu za uke kututumka, kuharibu uwiano wa bacteria kenye uke na pia kupunguza tindikali iliyopo mpaka kupelekea kuongezeka kwa uchafu unaotolewa

2.Ukiwa kwenye hedhi tumia pedi zisizo na kemikali, pedi za asili zisizo na harufu kali. Hii itasaidia kuzuia ukuaji wa bacteria kwenye uke.

3.Hakikisha unaimarisha kinga yako ya mwili : unapokuwa na kinga imara basi unajikinga dhidi ya kushambuliwa na magonjwa ya zinaa.

4. Epuka kujisafisha mara kwa mara ukeni. Kujisafisha kupita kiasi kunaharibu mpangilio wa kawaida wa bacteria kwenye uke(normal flora)

๐Ÿ’ฅ TIBA

๐ŸŒฟ Ukiwa na dalili hizo onana na Daktari na uwahi hospital, ufanyiwe vipimo kwanza (Mfano pelvic ultrasound) dawa zipo za kumaliza tatizo lako bila shida

JE, UMEFAIDIKA VIPI NA SOMO HILI?

ASANTENI ๐Ÿ™

SEHEMU YA 2 ๐Ÿ’ฅ Je, Dalili Za Pelvic Inflammatory Disease(PID) ni zipi?๐Ÿ’ฆ Dalili za PID zinatofautiana kwa mtu mmoja hadi m...
20/07/2023

SEHEMU YA 2

๐Ÿ’ฅ Je, Dalili Za Pelvic Inflammatory Disease(PID) ni zipi?

๐Ÿ’ฆ Dalili za PID zinatofautiana kwa mtu mmoja hadi mwingine. Kwa baadhi ya wanawake dalili huwa mbaya na kwa wengine dalili huwa za kawaida, wakati mwingine wanawake hukaa na ugonjwa kwa muda mrefu bila kujua kutokana na kuchanganya dalili na magonjwa mengine.

๐Ÿ’ฅ Zifuatazo ni dalili zinazojotokeza zaidi kwa wanawake wengi

1.Maumivu ya tumbo chini ya kitovu ambayo yanaweza kuwa upande mmmoja au pande zote kulia na kushoto

2.Sehemu za uke kuwa na ulaini sana

3.Kupata maumivu wakati watendo la ndoa wakati mwingine kupeleekea kuvuja damu wakati na baada ya tendo la ngono na hivo kukosa tena hamu ya tendo la ndoa

4.Kuvurugika kwa hedhi

5.Kutokwa na majimaji ukeni kusiko kawaida hasa yenye rangi ya njano na kijani

6.Maumivu wakati wa kukojoa

7.Kupata maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa

8.Kupata dalili za homa k**a kizunguzungu, mwili kukosa nguvu, kukosa hamu ya kula na uchovu mwingi.

๐Ÿ“ค Je, Madhara Yanayosababishwa Na (PID) ni yapi?

๐Ÿ“šMaambukizi kwenye njia ya uzazi husababisha athari kubwa sana kwa mwanamke,k**a tulivoona pale juu PID inaweza kusababisha ugumba na mimba kujishikiza mahali pasipo sahihi(ectopic pregnancy) tofauti na mfuko wa mimba. Kadiri unavoumwa zaidi PID ndivyo hatari ya kupata ugumba inavoongezeka.

Mimba kutokea nje ya mfuko wa mimba ni ishu kubwa ya kiafya na inahitaji uangalizi mkubwa wa kidaktari ili kuzuia kuvuja kwa damu na hatimae kupelekea kifo kwa mama, na hata mtoto pia

๐Ÿ“คMadhara mengine ya PID ni :

๐Ÿ‚ .Kupata majeraha kwenye mirija ya uzazi, majeraha yanaweza kutokea nje ama ndani, tatizo hili linaweza kuwa gumu kutibika na hutokea tu pale ambapo maambukizi hayakutibiwa kwa muda mrefu zaidi.

๐Ÿ‚ .Kuziba na kujaa maji kwa mrija ya uzazi(hydrosalpinx kutokana na majeraha ya tishu zake

๐Ÿ‚ .Maumivu ya tumbo ya muda mrefu husababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa na mwanamke kutofurahisa unyumba.

๐Ÿ‚. Kuongezeka kwa hatari ya kupata matatizo mengine wakati wa ujauzito

INAENDELEA.... ๐Ÿ’Š

SEHEMU YA 1 ๐Ÿ’ฅ Maambukizi kwenye njia ya uzazi au kwa kifupi PID, ni mambukizi ya bacteria yanayoathiri sana wanawake kwe...
12/07/2023

SEHEMU YA 1

๐Ÿ’ฅ Maambukizi kwenye njia ya uzazi au kwa kifupi PID, ni mambukizi ya bacteria yanayoathiri sana wanawake kwenye mfumo wa uzazi. Hata hivyo vijidudu vingine vyaweza pelekea PID japo bacteria ni wasababishi wakuu wa PID. Ugonjwa huu huweza kuleta athari katika sehemu zozote kwenye njia ya uzazi, moja ya athari za PIDย  ambayo wanawake hupata ni kutoweza kushika mimba yaani ugumba.

๐Ÿ’ฅ Tafiti zinasema kati ya wanawake nane walaiowahi kuugua PID basi mmoja wao atakutana na shida kupata mimba kwa siku za hapo baadae huku wale wanaofanikiwa kupata ujauzito basi hupata matatizo pia ikiwemo mimba kuharibika au kujifungua kabla ya wakati.

๐ŸŒฟ Nini kinasababisha PID?

๐ŸŒฟ Wataalamu wa afya wanaamini kwamba magonjwa ya zinaa ambayo hayakutibiwa ipasavyo hasahasa gonorrhea na chlamydia yanaongoza kwa kusababisha PID, japo kuna baadhi ya wanawake wanaugua PID kuna kwenye maambukizi ya kawaida ya bacteria(bacteria vagonosis)

๐ŸŒฟ Nini Maana Ya Pelvic Inflammatory Disease(PID)

๐Ÿ‚ Maana halisi ya PID ni hali ya kututumka au kucharuka kwa sehemu ya mfumo wa uzazi kwa mwanamke, sehemu hizi ni k**a mirija ya uzazi au o***y ambako kunasababishwa na magonjwa yanayosambazwa kwa njia ya ngono.

๐Ÿ‚ Maambukizi kwenye njia ya uzazi (PID) yana tabia ya kusambaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ndio maana kuna umuhimu wa kutibu tatizo hili mapema. Maambukizi haya yanaweza kusambaa kutoka kwenye uke mpaka sehemu zingine za uzazi wa mwanamke k**a mirija ya uzazi, mifuko ya mayai(ovari) na kwenye shingo ya kizazi(cervix).

๐Ÿ‚ Maambikizi haya yanaweza kusababisha makovu kwenye mirija ya uzazi na kupelekea kupata Ectopic pregnancy ambayo ni mimba iliyotungwa nje ya tumbo la uzazu kutokana na majeraha kwenye mirija.
INAENDELEA.... ๐Ÿ’‰

Address

Mikocheni
Dar Es Salaam

Telephone

+255753843505

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when afya_point255 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to afya_point255:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram