Online_clinic

Online_clinic Tunawasaidia wanawake kuweza kupata ujauzito haraka kwa kutumia njia ya kalenda

Baraka za Mungu 🤲🤲
29/03/2022

Baraka za Mungu 🤲🤲

Kitu ndani ya box😁🤰
29/03/2022

Kitu ndani ya box😁🤰

Najiskia utamu sana Yani😍😁😁🏃💃
28/03/2022

Najiskia utamu sana Yani😍😁😁🏃💃

Usikate tamaa Unaweza kupona pata matibabu sahihi
06/01/2022

Usikate tamaa Unaweza kupona pata matibabu sahihi

PART 2*Ndoa ya pili*Baada ya ndoa ya kwanza kuvunjika, Salome hakukata tamaa kwamba ya kumpata mwanaume mwingine ambaye ...
15/10/2021

PART 2

*Ndoa ya pili*

Baada ya ndoa ya kwanza kuvunjika, Salome hakukata tamaa kwamba ya kumpata mwanaume mwingine ambaye angeelewa hali yake na kumkubali jinsi alivyo.
Miaka minne iliyopita alikutana na mumewe, lakini bado hajajaliwa kupata ujauzito japo anaendelea kuwa na matumaini.

Najda anaeleza kuwa baada ya mumewe kumchumbia, baadhi ya jamaa na marafiki walikuwa tayari wameanza kumweleza mume wake kuwa Salome alikuwa na matatizo ya kizazi na huenda wasifanikiwe kumpata mtoto.
"Baadhi ya watu walijitokeza kabla ya ndoa yangu ya pili , na walianza kumweleza mume wangu kuwa mimi nilikuwa tasa "Salome alieleza.

Salome anasema kuwa alifurahi kwa kuwa penzi kati yake na mumewe lilishinda vita vya maneno kutoka kwa watu ambao wamekuwa wakimkejeli kuwa hana uwezo wa kushika mimba.

Salome ana uzito wa mwili wa kati ya kilogramu 124 na 131 na anasema kuwa Daktari wanasema kuwa uzito huo ni moja ya sababu zinazosababisha yeye kutopata Mimba.

Anasema kuwa kutokana na hayo yeye na mumewe bado wanafikiria iwapo Salome atapitia operesheni za kumsaidia kupunguza uzito au la.

"Kwa kweli uzito wangu wa mwili ni kizuizi kikuu kwangu kupata mimba, lakini nimeshindwa kupunguza uzito na huenda nikahitaji upasuaji", anasema Salome.

*Je hali hii ya Polycystic Ovarian Sydrome ni hali gani?*

Kulingana na Daktari wa afya ya wanawake Bi Diana Ondieki, hali aliyonayo Salome kwa jina Polycystic o***y syndrome (PCOS) ni hali ambayo kwa kawaida ni hitilafu za homoni za wanawake ambao wamefikia wakati wanapotarajia kuwa wazazi.
Wanawake ambao wana hali hii ya PCOS wanaweza kuwa na hedhi ambazo hazipatikani kwa wakati fulani na wakati mwingine zikija pia zinachukua siku nyingi kabla hazijaisha.
Pia hali hii inaandamana na wanawake kuwa na homoni ambazo zinapatikana miongoni mwa wanaume zikijulikana k**a (androgen). Kwa hiyo mayai ya uzazi huenda yakaanza kuota maji na kwa kuwa na hivvyo kumsababishia mwanamke kutokua na uwezo wa kupata mimba.
Jinsi ya kuepukana na ugonjwa wa PCS ni kupitia lishe bora, kufanya mazoezi ya kila mara na pia kupata matibabu yanayofaa kutoka kwa madaktari bingwa wa afya ya uzazi.
clinic

WhatsApp 0699354523

PART 1*Salome jinsi mwanamke huyu alivyohangaika kupata ujauzito kwa miaka 8*. ''Sijafanikiwa bado lakini sijakata tamaa...
14/10/2021

PART 1

*Salome jinsi mwanamke huyu alivyohangaika kupata ujauzito kwa miaka 8*.
''Sijafanikiwa bado lakini sijakata tamaa nitaendelae kujaribu tena na tena'' anasema Bi Salome na kuongeza kuwa:

'' Kwa kweli k**a mwanamke saa nyingine unajisikia uko chini sana kutokana na shida hii ya kukosa mtoto , lakini najipa moyo kuwa siku moja nitafaulu" Alisema Salome

Bi Salome mwenye umri wa miaka 34 ni meneja mauzo katika kampuni moja mji mkuu Dodoma Tanzania.
Salome alikuwa ameolewa lakini ikawa vigumu kwake na mumewe kuendelea kuishi pamoja kutokana sababu nyingi mmojawapo ikiwa ni hali yake ya kutokua na uwezo wa kupata mtoto.
*Ndoa yake ya kwanza*

Salome alikuwa katika ndoa ya kwanza kwa mwaka mmoja hivi , japo anasema kuwa haikudumu sana lakini muda huo wa ndoa yake haukuwa mwepesi kwake kwani alitamani angelipata ujauzito kwa haraka.
"Katika ndoa yangu ya kwanza nilikuwa na imani kuwa ningepata ujauzito, japo tangu usichana wangu nimekuwa na tatizo la maumivu makali wakati wa hedhi, lakini sikudhani kuwa hilo lingekuwa sababu kuu ya mimi kukosa kupata uja uzito " Salome anasema.
Kadri siku zilivyosonga ndivyo Salome na mumewe walivyozidi kutoelewana na hivyo kushindwa kuishi pamoja k**a mke .
Salome anaeleza kuwa tangu akiwa na umri wa miaka 20, alikuwa na usumbufu wa hedhi zake na alipomtembelea Daktari wa afya ya uzazi katika kliniki, alielezwa kuwa alikuwa na ugonjwa ujulikanao k**a Polycystic Ovarian Sydrome, hali hii humsababishia Bi Salome kuwa na matatizo ya homoni na mojawapo ya athari za ugonjwa huo ni kuwa na uzito wa mwili usio wa kawaida na jambo ambalo hadi sasa anapigana nalo sana japo haijawa rahisi.
Alipewa dawa ya kutuliza hali hiyo, Salome amekuwa akipata hedhi zake kila mwezi lakini hajaweza kupata ujauzito.

"Licha ya kuwa mimi sio mlaji wa chakula kingi sana mwili wangu ni mnene kutokana na hitilafu za homoni mwilini, Dakitari hunishauri nipunguze uzito niwe na uwezekano wa kupata ujauzito" Salome anasema.
INAENDELEA......................

Mwanamke mjamzito huwa na uzuri wa kipekee
28/09/2021

Mwanamke mjamzito huwa na uzuri wa kipekee

*Njia 10 Bora Za Kupata Watoto Mapacha uhakika ni 90%*Hii ni special kwa wale ambao tayari wapo kwenye program ya usimam...
26/08/2021

*Njia 10 Bora Za Kupata Watoto Mapacha uhakika ni 90%*

Hii ni special kwa wale ambao tayari wapo kwenye program ya usimamizi wa Kupata Ujauzito ndani ya siku 90.

Tukutane inbox yako week hii upate Mapacha wako na wewe🤝🏿🤝🏿

26/08/2021
JINSI YA KUPATA MTOTO WA KIUME (PART 1)Kulingana na tamaduni zetu, wengi huwa tunamtanguliza Mungu una kumuomba atupatie...
15/08/2021

JINSI YA KUPATA MTOTO WA KIUME (PART 1)

Kulingana na tamaduni zetu, wengi huwa tunamtanguliza Mungu una kumuomba atupatie mtoto tunayemtaka.
.
Mwanamke huzalisha mbegu aina moja ‘XX’ (X-Chromosomes) Mwaanaume anazalishwa mbegu za aina mbili ‘X’ (k**e) na ‘Y’ (kiume) (XY-Chromosomes).
Wakati wa uchavushaji;
Mama akitoa X na baba X = XX (mtoto wa k**e)
Mama akitoa X na baba Y = XY (mtoto wa kiume)

Mbegu ‘X’ ni imara ukilinganisha na ‘Y’, pia ‘X’ zinatembea polepole kulinganisha na mbegu ‘Y’ ambazo zenyewe ni dhaifu (sio imara na hufa mapema), lakini zina mwendokasi mkubwa.

Kalenda

Lazima ujue mzunguko wa mwanamke husika ni wa aina gani… kwa maana kuna mizunguko ya wastani wa siku 28 ambayo hii yai lake hutoka siku ya 14, kuna mzunguko mfupi wa siku 21 na yai hutoka siku ya 10 na pia wale wa mzunguko mrefu wa siku 36 ambao yai hutoka katika siku ya 18.

Mfano unaweza pata HEDHI kuanzia tarehe 1-5 na wengine huchukua siku 7. Hiki ni kipindi ambacho uterus hutoa damu baada ya yai la mwanamke kukosa kurutubishwa na mbegu za kiume.


SALAMA, SIKU YA 6-10.

Hiki ni kipindi ambacho mwanamke hawezi kupata mimba japo kinaelekea kipindi cha hatari

HATARI, SIKU YA 11-18.

Hiki ni kipindi ambacho mwanamke akijamiiana anapata mimba.


K**a mfumo wake wa uzazi upo sawa. Yaani hana uvimbe sehemu yoyote, homoni zimebalance vizuri, mirija haijaziba, hana infections zozote km vile PID, fangasi na UTI, kizazi hakina mikwaruzo. Hapa atapata mimba bila shida.

SALAMA SIKU YA 19-28.

Hiki ni kipindi kingine baada ya Ovulation ambapo mwanamke hawezi kushika mimba. Anajiandaa kupata hedhi nyingine kwakuwa yai halikurutubishwa siku za hatari. Endapo limerutubishwa hawezi ona hedhi nyingine.

Imeandaliwa na

……………….INAENDELEA…………

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255699354523

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Online_clinic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram