Eliud Chamgeni

Eliud Chamgeni Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Eliud Chamgeni, Medical and health, Dar es Salasm, Dar es Salaam.

Jamii yetu ina maadui wakuu watatu yani Ujinga,Maradhi na Umaskini...ungana nami katika mapambano dhidi maadui hawa katika jamii yetu kupitia nafasi yako katika jami.Pata mawazo mbdala hapa.

29/07/2023
29/08/2022

▪️Tafakari nasi kisha andika kichwa cha habari kisichozidi maneno sita.

01/02/2022

FAHAMU DHANA YA UKATAJI KIMEO.
Habari tena.Jana niliishia kuelezea sababu ya kwanza kwa nini kimeo huvimba?...
sasa tuendelee ...
2.Allergies/mzio
Watoto wanapitia katika mazingira mengi ambayo hawajawahi kupitia,k**a vile baridi,joto,vyakula,mafuta,dawa,hewa n.k..kwa njia moja ama nyingine mazingira hayo yanawafanya wapate Allergy ambayo inapelekea kuvimba kwa kimeo.
3.Maambukizi.Hii inatokea pale mtoto anapopata maambukizi ya baktria/virus sehemu za karibu na kimeo k**a vile kooni,Masikio,tonsils,Adenoid ama mapafuni.

Mazingira ya ukataji Kimeo.
-Kazi hii hufanywa na waganga wa hadi wasio na utaalamu wowote wa maswala ya afya.
-Si Salama kiafya ,utakasaji wa vifaa vitumikavyo hauzingatii kanuni(IPC),udhibiti wa utokaji damu nyingi na maambukizi ya bakteria /virus hatari..
-Ni ujasiliamali hatari kwa jamii,wakataji wanajipatia fedha huku wakiwaacha watoto katika hatari kubwa ya kufa.

Nini madhara ya ukataji vimeo?
1.Kufubaza tatizo..haiondoi chanzo cha tatizo.
2.Upungufu wa Damu nyingi.
3.Maambukizi ya VVU,Homa ya ini na Tetanus.
4.Kushindwa kutamka baadhi ya maneno.
5.Kupata maambukizi ya koo Mara kwa Mara.
6.Ni ukatili wa kimwili(ukeketaji part 2).
7.Ongezeko gharama za matibabu..yani matokeo ya kukatwa hupelekea tatizo halisi kukomaa na kuhitaji matibabu zaidi.
8.Kifo..iwapo hayatatibiwa mapema.

Kwa nini wanaokatwa kuna wanaopona na wengine hawaponi???
Iko hivi..Mtoto a naweza pona baada ya kukatwa kwa sababu dalili alizonazo Mtoto kisababishi chake ni virus,allergy hivi vyote huwa havina dawa maalumu hivyo ni subira ya muda tu maana mwili mwenyewe hupambana hadi kujiponyesha ama wengine wanawakata kisha wanawambia wakaendelee kutumia dawa za Antibiotics ambazo zinasaidi baadhi ya visababishi vya tatizo...kwa upande mwingine Wengi wao hawawezi pona licha ya kukatwa kwa sababu bado chanzo cha tatizo kipo pale pale(kukatwa kwao ni sawa na kutaka kumuua nyoka kwa kumpiga mkiani).

Nini kifanyike??????
1.Elimu,Elimu..wataalamu tuzidi kutoa Elimu kwa njia zote ili jamii yetu iwe na afya tele.
2.Tuachane na mila potofu...wazazi vijana tunayoambiwa na wazee tuchuje ,ni Ujinga kufanya kila kitu unachoambiwa.
3.Wataalamu tuwachunguze kwa makini na kuwapima watoto vizuri ili kujua chanzo cha matatizo kwa watoto ili kuzuia wazazi kuwapeleka kwa sangoma.
4.Tupatapo mtoto aliyezidiwa tumtibu na tuombe walete PF3 kutoka polisi ili kuwabaini wanafanya kazi hiyo.

Endelea kufuatilia ukurasa wangu nitakuletea dhana ya kubemenda usiwe mbali.

FAHAMU DHANA YA UKATAJI KIMEO.Wengi wetu tumekuwa tukisikia dhana hii ndugu,jirani Rafiki wakihusisha ukataji wa kimeo n...
31/01/2022

FAHAMU DHANA YA UKATAJI KIMEO.
Wengi wetu tumekuwa tukisikia dhana hii ndugu,jirani Rafiki wakihusisha ukataji wa kimeo na baadhi ya dalili za magonjwa mbalimbali (Sio ugonjwa wenyewe)hasa kwa watoto.

Baadhi ya sababu za zinazohusishwa na ukataji wa kimeo kwa watoto ni:-
1.Kikohozi.
2.Kutokunyonya ama kukosa hamu ya kula.
3.Ukuaji hafifu.
4.Kuugua muda mrefu.
5.Kuvimba ama kurefuka kwa kimeo.

Nini kazi ya Kimeo???
Kimeo kina kazi kuu mbili.
1.Kina tezi nyingi zinazozalisha mate kwa ajili ya kulainisha koo,mdomo na kusaidia umeng'enyaji wa chakula.
2.Kimeo kinasaidia utamkaji wa maeno vizuri.

Nini ukweli wa dhana Hii ukataji vimeo????.
1.Sio kweli kuwa wataalamu hawajui kukata kimeo.zipo sababu chache sana za kukata kimeo kitaalamu k**a vile matatizo yanayosababisha kukosa usingizi kwa sababu ya kukoroma ama kuziba kwa njia ya hewa ya juu kwa sababu ya kimeo(k**a Daktari kajiridhiaha kuwa hakuna ugonjwa wowote zaidi unaosababisha tatizo la kuziba kwa njia ya hewa)
2.Wakata vimeo hawafanyi uchunguzi Kujua chanzo cha tatizo la Mtoto (wanaua nyoka kwa kumpiga nyoka mkiani).
3.Wakata kimeo wanatumia Ujinga wetu k**a fulsa wao kujipatia kipato(gharama kadiriwa kukata kimeo ni Tsh 10,000).
4.Mazingira ya ukataji kimeo Kienyeji ni hatarishi.
5.Idadi Kubwa ya wahanga wa kukatwa kimeo ni watoto kutoka katika jamii maskini wasio na Uwezo wa kumudu gharama za matibabu na wasio na Elimu.
6.Baadhi ya jamii imekuwa ni k**a mila na desturi yao,hivyo wanafanya hivyo kutimiza imani potofu kutoka kwa wazee wao.

Kwa nini Kimeo huvimba ??
Sababu kuu ya watoto kukatwa kimeo ni muonekano wa kimeo kuwa kimevimba ama kimerefuka.Zifuatazo ni sababu za kuvimba kwa kimeo.
1.Mkusanyiko wa Damu kwa sababu ya kikohozi cha mfululizo hupekea mahitaji makubwa ya nguvu katika misuli ya koo ambapo damu hupelekwa kwa wingi kwa ajili ya kukidhi mahitaji...hii inafanana sana na kusimama kwa Ume ama kisimi cha mwanamke pale wanapokuwa katika msisimko wa kimapenzi.Itaendelea kesho usikose

Tanzania tuna maadui watatu ..yaaani1.Ujinga2.Maradhi.3.Umaskini.Si  Maneno yangu..Nimemnukuu Baba wa Taifa Mwalimu J.Ny...
24/01/2022

Tanzania tuna maadui watatu ..yaaani
1.Ujinga
2.Maradhi.
3.Umaskini.
Si Maneno yangu..Nimemnukuu Baba wa Taifa Mwalimu J.Nyerere
Huu ni mfano halisi wa Ujinga.

Mjasiliamali Je  unaamini hili????...."Ukitaka ufanikiwe katika Biashara yoyote   basi moja ya zingatio  ni  kuanzisha b...
01/12/2021

Mjasiliamali Je unaamini hili????....
"Ukitaka ufanikiwe katika Biashara yoyote basi moja ya zingatio ni
kuanzisha biashara kwa malengo ya Kutatua changamoto/shida za Watu na pesa zitakuja tu zenyewe."

Nafasi uliyopo ni mpango wa MUNGU.kupitia changamoto tunazokutana nazo  Mara nyingine inakuwa ngumu kuwafanya wengine wa...
01/12/2021

Nafasi uliyopo ni mpango wa MUNGU.kupitia changamoto tunazokutana nazo Mara nyingine inakuwa ngumu kuwafanya wengine watabasamu..lakini usichoke jitafakari kila siku kwani Mungu ana mpango na wewe kuwa k**a ulivyo.

Address

Dar Es Salasm
Dar Es Salaam
POABOX45232

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Eliud Chamgeni posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram