Jamii afya bora

Jamii afya bora Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jamii afya bora, Medical and health, Jamii afya bora na urembo, Dar es Salaam.

04/05/2022
FAHAMU KUUSU P.I.DP.I.D  inflammatory diseaseKwa kifupi P.I.D Ni maambukizi katika via vya uzazi. Wanawake wengi husumbu...
04/05/2022

FAHAMU KUUSU P.I.D

P.I.D
inflammatory disease
Kwa kifupi P.I.D Ni maambukizi katika via vya uzazi. Wanawake wengi husumbuliwa na tatizo hili kulingana na sababu zifuatazo:-
Matumizi ya antibiotics Kwa wingi, kimsingi matumizi haya huuwa bacteria wote, hivyo wanapokufa unakosa ulinzi wa bacteria wa kupambana na maambukizi.
ujauzito ikiwa ni pamoja na kujifungua. Pia sababu nyingine ni matumizi ya condoms na kufanya ngono zembe.
DALILI ZA UGONJWA WA PID
1️⃣Kutokwa na uchafu mzito sehemu za siri, yawezekana ukawa ni mweupe, njano, au maziwa
2️⃣Kuwashwa sehemu za siri
3️⃣Uke kutoa harufu mbaya
4️⃣Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
5️⃣Uke kuwa wa ulaini sana
6️⃣Maumivu wakati wa tendo la ndoa
7️⃣Kuvurugika Kwa hedhi
8️⃣Kutokwa majimaji ukeni kupita kiasi
9️⃣Maumivu wakati wa kukojoa na wakati wa choo kubwa
🔟Homa, uchovu,kizunguzungu na kukosa hamu ya kula

MADHARA YA PID
•Ugumba
•Kansa ya shingo ya kizazi
•Mirija ya uzazi kuziba
•Majeraha kwenye mirija ya uzazi

MATIBABU
inatibika na kupona Kwa haraka
Kwa ushauri au tiba ya tatizo hili waweza Fika ofisini kwetu piga simu 0672789066
# P.I.D

N.b - pia maradhi ya mfumo wa uzazi wa mwanamke yamekuwa Mengi ukiona unasumbuliwa na matatizo haya usisite kuwasiliana nasi
* Fungus sugu ukeni
* U.t.i mara kwa mara
* Tatizo la kutopata hedhi kwa wakati
* Maumivu wakati wa hedhi
* Vimbe kwenye kizazi
* Mirija ya uzazi kuziba
* Kutobeba ujauzito
* Kutokwa na uchafu na majimaji yenye harufu ukeni ..

Tiba ipo unapona kabisa bila kujirudia
Kwa mawasiliano zaid na ushari juu ya afya 0672789066

SULUHISHO LA MATATIZO YA MIGUU KUWAKA MOTO DALILI ZAKE NA TIBA SAHIHI.MIGUU KUWAKA MOTO,  ni ugonjwa unaotokea ambapo ka...
10/04/2022

SULUHISHO LA MATATIZO YA MIGUU KUWAKA MOTO DALILI ZAKE NA TIBA SAHIHI.

MIGUU KUWAKA MOTO, ni ugonjwa unaotokea ambapo katika mwili wa binadamu kutakuwa na matatizo k**a kudhoofika kwa neva za pembezoni mwa mwili yani za miguuni hivyo kupoteza uwezo wa utendaji kazi wa neva miguuni, sababu zingine ni k**a kutokuwa na mzunguko mzuri wa damu, kuwa na sumu nyingi mwilini,kurithi au mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.

DALILI ZA UGONJWA WA MIGUU KUWAKA MOTO.
Ugonjwa huu unadalili nyingi k**a,
•Kuhisi ganzi.
•Kuhisi kuchomwa na kitu chenye ncha Kali miguuni.
•Kuhisi miguu kuwa na majimaji kwa ndani.
•Joto Kali miguuni.
•Kuhisi k**a unaungua miguuni.
•Kushindwa kushika au kubeba vitu na maumivu makali.

SABABU/ MAMBO YANAYOWEZA KUPELEKEA MTU MIGUU YAKE KUWAKA MOTO
Kuna mambo mengi sana yakiwemo;
~UZITO MKUBWA WA MWILI(hii husababisha uti wa Mgongo kukaa tofauti na unavyostahili hivyo baadhi ya neva kukandamizwa na uzito wa mwili au misuli hivyo kusababisha miguu kupata maumivu na kufa ganzi.

~MATUMIZI YA BAADHI YA DAWA ZENYE KEMIKALI KWA MUDA MREFU/MARA KWA MARA mfano: DAWA ZA KUONDOA MAUMIVU NA TB.

~UPUNGUFU WA VIRUTUBISHO MWILINI HASA MKUSANYIKO WA VITAMINI B( VITAMINI B COMPLEX)

~MAGONJWA YA KISUKARI NA SHINIKIZO LA DAMU, MAGOTI ,MZIO NA FANGASI.

~MATATIZO YA MOYO.

~MATATIZO KATIKA MISHIPA YA DAMU.

~ULEVI WA KUPINDUKIA KWA MUDA MREFU.

YA KUEPUKA UGONJWA WA MIGUU KUWAKA MOTO.

~KUWA NA UZITO UNAOENDANA NA KIMOCHAKO.

~FANYA MAZOEZI YA MWILI.

~KULA CHAKULA KINACHOKUPATIA VIRUTUBISHO MWILINI HASA VITAMINI B COMPLEX.

~USAFI WA VIATU, SOX NA MIGUU.

~ ONDOA SUMU AU KEMIKALI MWILINI MARA KWA MARA.

MATIBABU;
Matibabu sahihi ya miguu kuwaka moto ni dawa ambazo hazina kemikali ambazo zina virutubisho vitakavyoweza kurudisha hali ya neva katika usalama na mzunguko wa damu kuwa sawa.

FIKA OFISINI KWETU MLIMANI CITY AU WASILIANA NASI KWA 0672789066 whatsap/inbox

Hii bidhaa ya watoto ni ya asili mchanganyiko( bidhaa hii itaenda kutatua changamoto yeyote ile aliyonayo mtoto wako)*Ma...
08/04/2022

Hii bidhaa ya watoto ni ya asili mchanganyiko( bidhaa hii itaenda kutatua changamoto yeyote ile aliyonayo mtoto wako)

*Mafuta ya samaki( omega three)
*Maziwa
*Matunda yenye vitamin C

Faida za dr cow kea watoto

*Kuongeza hamu ya kula
*Kuongeza ufanisi wa ubongo wa mtoto
*Inaongeza nguvu kwenye viungo vya watoto waliolegea ( watoto waliochelewa kutembea huwasaidia Sana kutembea haraka
*Inaongeza uzito wa mtoto

Kwa faida nyingi zaid za dr cow nicheki. 0672789066

*UGONJWA WA OSTEOARTHITIS NI NINIOsteoarthritis /Arthritis ni ugonjwa unaotokana na namna yo yote ya hitilafu katika mau...
04/04/2022

*UGONJWA WA OSTEOARTHITIS NI NINI

Osteoarthritis /Arthritis ni ugonjwa unaotokana na namna yo yote ya hitilafu katika maungio ya mifupa ya binadamu ambao husababisha maumivu na pengine kuvimba katika sehemu moja au zaidi ya maungio hayo. Neno arthritis halilengi ugonjwa mmoja bali jamii ya magonjwa ambayo kwa ujumla yapo zaidi ya 100.

Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa (joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo moja.

*CHANZO_CHA_ARTHRITIS_NI_NINI ?*

Kusudi kuelewa chanzo cha ugonjwa huu, hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana. Fikiria goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana: Ligaments: Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja. Hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje, ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi.
Cartilage: Huu ni utando unafunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja. Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu. Capsule: Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote. Ndani ya mfuko huu wa capsule kuna synovial fluid ambayo huzalishwa na synovial membrane. Synovial fluid ni ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule. Ugonjwa wa arthritis unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa. Inaweza kuwa cartilage inalika, upungufu wa synovial fluid, maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo.

*TIBA*
Tiba ya magonjwa haya ziko nyingi sana kulingana na aina ya tatizo, nyingi ni madawa ya kutuliza maumivu pamoja na kufanyiwa upasuaji na kuwekewa vitu vya bandia kulingana na tatizo taasisi ya Bright Future imetengeneza
tiba ya kipekee ya vidonge vya *ZAMINOCAL, ANTHROXTRA na GRUZOJOINT* Hivi ni virutubisho lishe maalum vinavyoweza kuondoa maumivu na kumaliza tatizo lako kuanzia kwenye chanzo chake bila kufanyiwa upasuaji wowote,Hizi Sio Dawa Za Kutuliza maumivu,Ni tiba Ya Moja Kwa Moja
Iwapo Unasumbuliwa na tatizo hili na mengineyo tafadhali wasiliana nasi upate tiba zisizo Na kemikali na madhara

Ukubwa Wa dose Unatokana Na Ukubwa Wa tatizo lenyewe,Nielezee tatizo lako Nikupe Dose Sahihi.
Kwa maelezo na msaada zaidi:0672789066

MAAMBUKIZI KWENYE VIA VYA UZAZI WA MWANAMKE(PID)   Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inf...
02/04/2022

MAAMBUKIZI KWENYE VIA VYA UZAZI WA MWANAMKE(PID)

Maambukizi katika mfumo wa uzazi wa mwanamke kwa kitaalamu Pelvic Inflamatory Diseases au kwa kifupi PID, ni moja ya matatizo ambayo huwaathiri sana wanawake.
Kwa kawaida maambukizi haya huusisha shingo ya uzazi (cervix) hali ambayo hujulikana k**a cervicitis, nyama ya mfuko wa uzazi (endometrium) ambayo kitaalamu huitwa endometritis, na mirija ya uzazi (fallopian tubes) hali ijulikanayo kitabibu k**a salpingitis.

?

Pamoja na aina kadhaa za vimelea kuhusishwa na PID, vimelea vya jamii ya Neisseria Gonorrhoeae pamoja na Chlamydia trachomatis ndivyo vinavyoongoza kwa umaarufu zaidi katika kusababisha PID kwa akina mama.

?

Kuna njia kadhaa ambazo mwanamke anaweza kuambukizwa PID. Njia hizo ni pamoja na
👉🏾Kufanya ngono isiyo salama
👉🏾Maambukizi ya njia ya uzazi hasa kipindi mara baada ya kujifungua (au postpartum period)
👉🏾Maambukizi ya njia ya uzazi mara baada ya kutoa mimba kwa njia zisizo salama (post abortion) au mara baada ya mimba kutoka (miscarriage)
👉🏾Kutumia vipandikizi vya ndani ya mfuko wa uzazi (IUCD) k**a njia mojawapo ya uzazi wa mpango, na
👉🏾Kuambukizwa kupitia damu iliyo na vimelea vya PID.
👉🏾Kuugua UTI au FANGUS Mara kwa Mara
👉🏾Kutumia dawa za kuzuia Mimba ndani ya msaa 72 maarufu K**a P2 Mara kwa mara.


kishakutana na tatizo hili Mara nyingi
👉🏾Hupoteza hamu ya tendo la ndoa
👉🏾Mwanamke kuhisi maumivu ya tumbo hasa maeneo ya chini ya kitovu
👉🏾Kupata maumivu ya mgongo
👉🏾Mwanamke kupata utoko mchafu sehemu za siri wenye harufu mbaya na miwasho
👉🏾Utoko huu huambatana na harufu mbaya.
👉🏾Kuhisi maumivu wakati wa kukojoa
👉🏾Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa ni maumv makali sana na yana umiza sana
👉🏾Kutoka damu bila mpangilio wakati wa hedhi na hedhi kuto eleweka
👉🏾Kupata homa
Wakati fulani kuhisi kichefuchefu na
Pia kutapika


👉🏾kukosa au kushindwa kubeba mimba
👉🏾hormones in balance,
👉🏾fibroid(Uvimbe katika KIZAZI)

Unaweza tumia antibiotics K**a metronidazole, doxycycline na ciproflaxin au unaweza kuchoma sindano K**a Ceftriaxone maarufu K**a powercelf kwa siku tano ukatapa nafuu.

Ila Mara nyingi imekuwa ikijirudia na kutengeneza usugu wa dawa na hvyo kuto kupona na na kupata madhara tajwa hapo juu.

Nitakupatia dawa dozi ni miezi 2 unapona kabisa kwasbb Dawa hii ina antioxidants nutrients hii ni kuondoa sumu manaake bacteria yyte hutolewa kwa njia ya maji maji ukeni na uke unakua mkavu kwasbb ndan ya ya hii dawa kuna phyto nutrients ndani ya siku 5 tu unaona matokeo kwasbb inanguvu sana

Ahsante kwa muda wako Najua umejifunza Kitu na utamshilikisha na mwenzako

Nitafute kupitia nambari
0672789066
WhatsApp +255672789066

UGONJWA WA KISUKARI: AINA YA KISUKARI, CHANZO, DALILI NA TIBA!Ugonjwa wa Kisukari au (jina la kitaalamu: diabetes mellit...
20/03/2022

UGONJWA WA KISUKARI: AINA YA KISUKARI, CHANZO, DALILI NA TIBA!

Ugonjwa wa Kisukari au (jina la kitaalamu: diabetes mellitus ) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza insulin ya kutosha au seli za mwili wake haziwezi kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote mawili kwa pamoja. Mgonjwa wa kisukari hupata haja ndogo mara kwa mara (polyuria), kusikia kiu kila wakati (polydipsia) na njaa (polyphagia).

AINA ZA KISUKARI

Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari:
▪Aina ya ugonjwa wa kisukari ya kwanza ni ugonjwa wa auto. Mfumo wa kinga unashambulia na huharibu seli katika kongosho, ambako insulini inafanywa. Haijulikani kinachosababisha mashambulizi haya. Kuhusu asilimia 10 ya watu wenye ugonjwa wa kisukari wana aina hii.

▪Aina 2 ya ugonjwa wa kisukari hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulini, na sukari hujenga katika damu yako.
Hutokea wakati sukari yako ya damu ni ya juu zaidi kuliko kawaida.
Homoni za kuzuia insulini zinazozalishwa na placenta husababisha aina hii ya ugonjwa wa kisukari. Ni hali tofauti ambayo figo yako huondoa maji mengi sana kutoka kwenye mwili wako.

Kila aina ya ugonjwa wa kisukari ina dalili za kipekee, sababu, na matibabu. Jifunze zaidi kuhusu jinsi aina hizi zinavyotofautiana.
Dalili za ugonjwa wa kisukari

CHANZO CHA UGONJWA WA KISUKARI

Viko vyanzo mbalimbali, navyo ni

1. Shinikizo la juu la damu (B.P)
2. Viwango vya juu vya triglyceride (Mafuta)
3. Lishe yenye Mafuta mengi na Wanga
4. Utumiaji mkubwa wa Pombe
5. Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6. Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7. Uzito na unene uliozidi
8. Kutoushughulisha mwili
9. Umri
10. Kurithi

DALILI ZA MTU MWENYE KISUKARI

Dalili ya ugonjwa wa kisukari husababishwa na sukari ya damu.
Dalili za jumla

Dalili za jumla za ugonjwa wa kisukari ni pamoja na:

1. Njaa iliyoongezeka
2. Kiu kikubwa
3. kupungua uzito
4. Kukojoa mara kwa mara
5. Maono machafu
6. Uchovu uliokithiri
7. Vidonda ambavyo haviponi
8. Inaweza pia kusababisha maambukizi ya mara kwa mara. Hii ni kwa sababu viwango vya juu vya glucose hufanya iwe vigumu kwa mwili kuponya na kinga ya mwili kushuka.

Dalili katika Wanaume.

Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa kisukari, wanaume wenye ugonjwa wa kisukari wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume au kushindwa kufanya tendo la ndoa (ngono), uume kushindwa kusima/ uharibifu wa erectile (ED), na nguvu za misuli duni.

Dalili kwa wanawake

Wanawake wenye ugonjwa wa kisukari wanaweza pia kuwa na dalili k**a vile maambukizi ya njia ya mkojo (U.T.I, Kichocho, n.k), maambukizi ya chachu, na ngozi kavu.

TIBA YA MAGONJWA YA KISUKARI

Ugonjwa wa Kisukari unatibika kwa hali tofauti, pia kufuatana na muda wa tatizo, mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakikata tamaa na kuwa wabishi, hii hufanya wagonjwa wengi kupata madhara makubwa au kufa kutokana na kuto kuwa makini na kile tunacho waeleza. Wakati huo wengi huendelea kutumia dawa pamoja na vitu vyenye kemikali na hii hufanya wengi kuendelea kuumwa zaidi. Tiba zinazotumika pamoja Kemikali kali (chemotherapy), mionzi (radiation), au upasuaji (surgery).

DAWA

Tuna dawa ya kutibu Ugonjwa wa Kisukari ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa.

Angalizo: Dawa hiyo hutibu kwa mda mrefu ni programme ya miezi 3; k**a ni tatizo la muda mrefu sana unatakiwa utumie kwa kipindi cha miezi 3 mfululizo, ukianza kutumia baada ya wiki mbili huonesha mabadiliko, pia mgonjwa anapewa mfumo wa maisha ambao anatakiwa autumie kwasababu kuna mitindo wa maisha inaendelea kuongeza tatizo pia kuna mitindo inapunguza hatari ya ugonjwa. Hizo dawa zinaondoa ugonjwa kabisa k**a ukifuata maelekezo yanayotolea.

Inajulikana kuwa watu wengi hawapendi dawa za muda mrefu wakati wana matatizo ya muda mrefu ambayo ni hatari, ni vigumu kupata dawa ya muda mfupi wakati una ugonjwa wa muda mrefu.

Tunamshukuru Mungu kwa uumbaji wake na kutupa dawa ambazo alizileta ili kutuimarisha na kutuponya, Mungu hakuumba dawa nyingine zaidi ya mimea na vitu vingine vya asili, japo wengi hudharau.

Mawasiliano:
Kupata ufafanuzi zaidi na tiba. Njoo whatsapp / tuma texts za kawaida 0672789066

UGONJWA WA KIHARUSI : MAMBO MUHIMU KUFAHAMU (STROKE) KIHARUSI (stroke) Kiharusi ni ugonjwa wa dharura na hatari ambao hu...
19/03/2022

UGONJWA WA KIHARUSI : MAMBO MUHIMU KUFAHAMU (STROKE)

KIHARUSI (stroke)
Kiharusi ni ugonjwa wa dharura na hatari ambao hutokea pale seli za ubongo zinapokufa kwa kukosa hewa ya oksijeni na chakula kutokana na kuziba au kupasuka kwa mishipa ya damu kwenye ubongo.

AINA ZA KIHARUSI
Kuna aina kuu mbili za Kiharusi
Kiharusi kinachotokana na kuziba kwa mishipa ya damu ya damu ya ubongo
2. Kiharusi kinachotokana na kupasuka kwa mishipa ya damu ya ubongo
Ukubwa wa tatizo la kiharusi

1. mwaka 2018 kulingana na ripoti maalumu ya Shirika la Afya duniani WHO kuhusu sababu za vifo ilionesha kiharusi kinashika nafasi ya pili kati ya magonjwa yote kwa kusababisha vifo VINGI.
2. Kiharusi husababisha ulemavu kwa wengi: Kiharusi kinashika nafasi ya tatu kati ya visabibishi vya ulemavu duniani. Waathirika wengi huishia kuwa walemavu

DALILI ZA KIHARUSI

1.GANZI
-Mtu anayepata kiharusi hupata ganzi inayoanza ghafla na mara nyingi huathiri upande mmoja wa mwili. Mfano: Upande mmoja wa uso kufa ganzi na kushindwa kuongea vizuri au kutabasamu

2.KUPATA SHIDA KUONGEA
Mgonjwa wa kiharusi hushindwa kuongea vizuri, utoaji wa maneno huwa sio wa kawaida
Mfano: Mgonjwa kushindwa kumaliza sentensi au kuongea k**a amelewa sana
-Pia hali hii huweza kuambatana na kutoka mate(udenda) kwa wingi mdomoni

3.KUSHINDWA KUONA
Mgonjwa wa kiharusi anaweza kushindwa kuona, hali hii hutokea ghafla. Inaweza kuhusisha jicho moja au macho yote mawili.

4.Pia mgonjwa anaweza kupoteza fahamu au kupata degedege

5. Mgonjwa anaweza kushindwa kuzuia haja kubwa au ndogo au vyote viwili

VITU VINAVYOCHANGIA MTU KUPATA KIHARUSI
1. Ugonjwa wa Shinikizo kubwa la damu (presha)
2. Uvutaji sigara
3. Ugonjwa wa kisukari
4. Magonjwa ya moyo hasa ugonjwa wa mtetemo wa moyo (atrial fibrillation)
5. Tatizo la mafuta mengi kwenye damu (Lehemu au cholesterol)
6. Uzito uliopitiliza
7. Unywaji wa pombe uliokithiri
8. Kutokufanya mazoezi

GUNDUA KIHARUSI HARAKA UOKOE MAISHA YA MPENDWA, NDUGU AU JAMAA
Kiharusi ni tatizo la dharura linaloweza kusababisha madhara makubwa ikiwemo kifo au ulemavu k**a mtu asipopata matibabu mapema. Hivyo ni vyema kila mtu akafahamu dalili za kiharusi ili iwe rahisi kuzitambua. na kuchukua hatua mapema.
Ili kurahisha kumbukumbu za dalili za kiharusi kifupisho FAST (Face Arm Speech Time) hutumika k**a ifuatavyo

A-FACE (Uso)
-Angalia k**a upande mmoja wa uso uko tofauti na mwingine. Mwambie mgonjwa. anyanyue kope au akunje ndita au atabasamu. Upande ulioathrika utashindwa kufanya hivyo.

B-HAND. (Mkono)
Mwambie mgonjwa anyanyue mikono juu kwa mbele au juu mara nyingi mkono wa upande ulioathirika hushindwa kunyanyuka au hudondoka unaporudishwa chini.

C-SPEECH (Uongeaji)
Mwambie mgonjwa atamke jina lake, mtu mwenye kiharusi hushindwa kuongea, au huongea k**a. mlevi au hupata shida kutafuta maneno k**a mtu aliyepoteza kumbukumbu

D-TIME (Muda)
Muda ni mali, chukua maamuzi ya kutafuta msaada wa kitabibu haraka maana kadri unavyochelewa ndio kiharusi kinaharibu sehemu muhimu za ubongo

KWA TIBA NASAHA NA USHAURI WASILIANA 0672789066 whatsap/inbox

ANATIC SOAP ni sabuni inayotokana na miti asilia,hutibu maradhi ya ngozi ikiwemo 1.chunusi sugu2.harara na upele 3.ngozi...
17/03/2022

ANATIC SOAP ni sabuni inayotokana na miti asilia,hutibu maradhi ya ngozi ikiwemo
1.chunusi sugu
2.harara na upele
3.ngozi kijikunjakunja
4.mabaka meusi katika ngozi
5.ngozi kuwasha
6.fangas wa ngozi
7.mashilingi,vibarango,na mpunye
8.na magonjwa mengine ya ngozi ambayo yametibiwa lakin hujirudia

Sabuni hii imewasaidia wengi na wamefanikiwa kutibu matatizo yao ya ngozi
BF SUMA wanayofuraha kukufikishia bidhaa hii kwaajili ya afya ya ngozi yako
Itunze afya yako,tunza muonekano wako hakika BF SUMA tunaijali afya yako kwa tiba asilia

Tunapatikana Tanzania nzima na duniani kote kwajina la BF SUMA popote ulipo utafikishiwa bidhaa hii
Kwa maelezo zaidi tuma ujumbe mfupi yani SMS au watsap 0672789066
Ahsanteni sana karibuni tuwahudumie

DALILI ZA UGONJWA WA FIGO.KUVIMBA USO:1)Kuvimba uso, miguu na tumbo, ni ishara za ugonjwa wa figo. Dalili za kuvimba kut...
14/03/2022

DALILI ZA UGONJWA WA FIGO.

KUVIMBA USO:

1)Kuvimba uso, miguu na tumbo, ni ishara za ugonjwa wa figo. Dalili za kuvimba kutokana na ugonjwa wa figo huwa inaanzia chini ya kibukio cha jicho (eye lids) na hutambulika sana asubuhi. Kushindwa kwa figo ni sababu ya kawaida na muhimu ya kuvimba. Lakini tunahitaji kuelewa kuwa kuvimba si lazima iwe ni figo kushindwa. Kuna ugonjwa mwingine wa figo licha ya figo hufanya kuvimba kutokea (mfano nephritic syndrome). Hoja nyingine ni vema kuwekwa akilini ni kuwa kuvimba huenda kusionekane kabisa kwa wagonjwa wachache wa ugonjwa dhahiri wa figo kushindwa kazi.

2)Kukosa hamu ya chakula, kusikia ladha isiyo ya kawaida mdomoni na kushindwa kula chakula vyema ni shida za kawaida zinazopatikana kwa watu wenye hitilafu ya figo. kushindwa kwa figo zaidi kwa sababu ya sumu nyingi mtu huwa na kichefuchefu, kutapika na kwikwi.

3)Kupanda kwa damu/ Shinikizzo la damu – hypertension
Kwa wagonjwa wa kushidwa kwa figo kufanya kazi, shinikizo la damu ni kawaida. Iwapo shinikizo la damu kunatokea katika umri mdogo (chini ya miaka 30) au shinikizo la damu liko juu wakati wa uchunguzi, sababu yaweza kuwa shida ya figo.

4)Kuvimba kwa uso chini ya macho mara kwa mara inaonyesha dalili ya ugonjwa wa figo.

5(Anemia (ukosefu wa damu) na kuwa dhaifu
Kuwa dhaifu, kuchoka mapema, kukosa kutulia sehemu ya kazi ni malalamishi ya mara kwa mara ya mtu mwenye anemia (low hemoglobin level). Wakati mwingine hizi ni dalili pekee za mtu mwenye hali za mwanzo za ugonjwa sugu wa figo kutofanya kazi. Iwapo anaemia haiponi baada ya matibabu kamili, ni vyema kufikiria kushindwa kwa figo k**a moja ya sababu ya anemia hiyo.

6)Malalamishi yasiyo kawaida
Kuumwa chini ya mgongo, kuumwa mwili, kujikuna na maumivu ya miguu (cramps) huwa ni malalamishi ya mara kwa mara ya ugonjwa wa figo. Kutoendelea kukuwa, mtu kuwa mfupi na kujikunja (bending) kwa mifupa ya miguu ni dalili nyingine kwa watoto wenye ugonjwa wa figo.

7)Kupata shida ya mkojo
Dalili za kawaida za kulalamikia mkojo :
1. Kiwango cha mkojo kilichopungua, ambacho husababisha kuvimba ni wazi kwa magonjwa mbalimbali ya figo.
2. Muwasho wa mkojo, kukojoa mara kwa mara na kukojoa damu au usaha ni dalili za maambukizo ya njia ya mkojo.
3. Ugumu wa kukojoa kunaweza kusababisha ugumu wa kusukumwa na kupitisha mkojo, mkojo hafifu au kudondokwa kwa mkojo. Katika hali mbaya kabisa kutopitisha/ kuziba kabisa mkojo ni hali ya kawaida kwa mgonjwa huyu,

Zingatia:
Ingawa mtu anaweza kuwa na dalili zilizotajwa hapo juu, hii haidhihirishi kuwa mtu huyu anaugua ugonjwa wa figo. Hata hivyo, kukiwa na dalili hizi, inahimizwa kumwona daktari na kuthibitisha k**a kuna dalili yoyote ya ugonjwa wa figo kwa kupima na kufanya uchunguzi.
Ni vyema kukumbuka kuwa, shida kubwa za ugonjwa wa figo zinaweza kuwepo chini chini kwa muda mrefu bila dalili au ishara zozote muhimu.

Nb:
Kwa shida ya FIGO na shida nyingine nyingi
K**a , TEZI DUME bila Upasuwaji, kuziba MKOJO, VIDONDA vya tumbo SUGU, bawasili KUTOKA kinyama njia ya haja kubwa, change limalozuia uzazi/ kutokunasa ujauzito, KUTOKWA UCHAFU MWEUPE UKENI, moyo, shida ya mapafu, SARATANI nk contact 0672789066

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA PUMU YA NGOZI ( ECZEMA )PUMU YA NGOZI ni Ugonjwa wa NGOZI unaosababisha kuvimba kwa NGOZI( Infl...
14/03/2022

FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA PUMU YA NGOZI ( ECZEMA )

PUMU YA NGOZI ni Ugonjwa wa NGOZI unaosababisha kuvimba kwa NGOZI( Inflammation ).
Hii huambatana na NGOZI Kuwasha, Kuwa Nyekundu, Vipele na Mabaka.

NINI KINASABABISHA PUMU YA NGOZI?
PUMU ya NGOZI husababishwa na Msh*tuko wa Kinga ya Mwili( hypersensitivity ) na Ngozi ya Mwili. Kuna Uhusiano wa PUMU ya NGOZI na Magonjwa k**a Asthma, Mafua, Msongo wa Mawazo pamoja Kurithi ( Vinasaba )

DALILI ZA PUMU YA NGOZI.
Dalili Kuu Tatu ni:-
1. Ngozi kuwa Nyekundu
2. Ngozi Kuvimba na Kupasuka
3. Ngozi Kukauka pamoja na Muwasho.
Mara nyingi UGONJWA huu huambatana na Magonjwa ya Njia ya hewa k**a Asthma( Atopic dermatitis ) au baada ya kukutana na kitu kinachosababisha Msh*tuko wa Kinga ya Mwili na Ngozi. Mfano Kipodozi, Kemikali nakadhalika.

PUMU YA NGOZI KWA WATOTO.
Asilimia 8 Mpaka Asilimia 18 ya WATOTO wote huathiriwa na Ugonjwa huu. Hii huambatana na mabadiliko ya Hewa na Magonjwa ya Mfumo wa Hewa mfano Mafua na Asthma .
Mara Nyingi Ugonjwa huu hupotea Ukubwani baada ya Matibabu.

TIBA YA PUMU YA NGOZI.
Kutokana na Utendaji Mzuri wa Bidhaa za BF SUMA katika Kukuongezea Kinga ya Mwili, Tunaweza Kukusaidia Uondokane na Chandamoto hii.
Ivyo Basi nikushauri anza sasa kutumia Bidhaa za BF SUMA Utapata Matokeo Mazuri kwa Haraka sana na kuacha Ngozi yako ikiwa Nyororo na ya Kuvutia.

Kupata tibalishe na maelezo zaidi
Inbox/whatsap
0672789066

PUMU(ASTHMA)=>Hii ni hali ya muda mrefu inayosababisha kuvimba na kuwa nyembamba njia ya hewa,kuzalishwa majimaji mengi ...
14/03/2022

PUMU(ASTHMA)
=>Hii ni hali ya muda mrefu inayosababisha kuvimba na kuwa nyembamba njia ya hewa,kuzalishwa majimaji mengi kwenye njia ya hewa na kuifanya misuli ibane,na hivyo kumfanya mtu apumue kwa shida.

VISABABISHI:
(1)Vinasaba:hali hii huweza kurithiwa kutoka kwa mwanafamilia/mwanaukoo mmoja hadi mwingine.
=>K**a kwenye familia/ukoo kuna ndugu mmoja ana pumu,basi kuna uwezekano wa ndugu mwingine kuwa na pumu.
(2)Maambukizi katika njia ya hewa;maambukizi ya vijidudu vya maradhi vinavyoshambulia njia ya hewa huweza kusababisha tatizo hili,kwani huweza kusababisha kuvimba kwa njia ya hewa na uzalishwaji wa majimaji yanayofanya kupumua kuwe kwa shida.
(3)Mazingira ya kazi
=>Watu wanaofanya kazi kwenye mazingira yenye kuzalisha vumbi au ungaunga wa vitu fulani huwa kwenye uwezekano mkubwa wa kupatwa na tatizo hili;mfano: viwanda vya unga,viwanda vya mbao,wahandisi barabarani,wajenzi,wanaofanya kazi kwenye karakana,wachimbaji wa madini,wanaofuga wanyama,na wakulima(haswaa wa pamba na sufi)
(4)uvutaji wa sigara
=>Uvutaji wa sigara upo ule wa moja kwa moja ambao mtu anavuta yeye K**a yeye,lakini kuna ule ambao mtu havuti sigara ila anavuta moshi kutoka kwa mtu aliyepo karibu(secondhand smoking),haijalishi unavuta kwa kupenda au umesimama karibu na mvutaji,bado utakua kwenye hatari ya kupatwa na tatizo hili.
=>Mama mjamzito anayevuta sigara huweza kujifungua mtoto mwenye tatizo Hilo.
(5)Mazingira yenye hewa chafu;
=>Mazingira yenye hewa chafu,karibu na viwanda,Moshi wa mahali na hata Moshi wa kuni jikoni huweza kusababisha tatizo hili,kwani moshi huu huumiza njia ya hewa ikavimba na kuzalisha majimaji na hivyo kumfanya mtu aheme kwa shida.
(6)unene kupitiliza:watu wenye unene wa kupitiliza huwa kwenye hatari hii,kutokana na uwezekano wa njia zao za hewa kuvimba na kuzalisha majimaji.
DALILI ZA PUMU;
=>Kifua kubana.
=>Kukohoa
=>Kukosa pumzi na kuhema kwa shida.
=>Kuhema kwa kutoa sauti.

TIBA LISHE:
= >Vyakula vingi vyenye vitamini C,E na beta carotene(antioxidants) huweza kusaidia tatizo hili,kwani hupunguza vimbe kwenye njia ya hewa na kumfanya mgonjwa aheme kawaida bila kutumia nguvu.Vyakula hivyo ni ;
=>Matunda na mbogamboga
=>Vitunguu swaumu
=>Tangawizi
=>Asali
=>Samaki.

Address

Jamii Afya Bora Na Urembo
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jamii afya bora posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram