15/10/2020
KUTOKWA NA KIJINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA
( HEMORRHOIDS)
MIWASHO, MAUMIVU NA VIMBE KATIKA TUNDU LA HAJA KUBWA
Bawasiri ni ugonjwa ambao unatokana na kuathirika kwa mishipa ya sehemu ya ndani na nje ya tundu la haja kubwa na hupelekea wakati mwingine kutoa damu wakati wa kutoa haja kubwa.
Ugonjwa huu unasababisha muwasho na maumivu makali katika tundu la haja kubwa.
Ila kwasasa ugonjwa huu unawaathiri mpaka watoto wa umri wa chini kabisa:
CHANZO CHA UGONJWA WA BAWASIRI.
Bawasiri ni tatizo linaloanzia kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Huu mfumo ukishakua mbovu hupelekea kutokupata choo vizuri(Haja kubwa)
Mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula unasababisha chakula kisimeng'enywe vizuri kwenye utumbo mdogo na hivyo kupelekea chakula kupiliza kwenda moja kwa moja k**a kilivyo kwenda kwenye utumbo mkubwa ambapo maji maji kutoka kwenye chakula hufyonzwa na kuacha chakula kikiwa kikavu.Inapofikia wakati wa kupata choo; choo kinakua kikavu hivyo unatumia nguvu nyingi kukisukuma choo kitoke.
Hali hii hupelekea misuli ya haja kubwa kutanuka na kupelekea kukwanguliwa na choo kigumu na hivyo kinyama kuanza kujitengeneza, Hivyo husababisha kuanza kusikia maumivu na miwasho kwa ndani, na mara nyingine kupata choo chenye damu.
Hivyo basi kadri unavyoendelea kupata choo kigumu misuli ya tundu la haja kubwa huendelea kuathirika zaidi k mpaka kinatokeza.
Mtu mwenye afya nzuri anapata choo kulingana na milo aliopata kwa siku. K**a unauwezo wakupata milo mitatu kwa siku, unasitahili kupata choo mara tatu kwa siku, tena choo chako kitoke na urefu sawa wa ndizi mbivu, bila kujikatakata k**a kile cha mbuzi.
Bawasiri pia huweza kusababishwa na:
-Kufanya mapenzi kinyume na maumbile,
- Ujauzito
- kuhara kwa mda mrefu
-Kutopata choo kwa mda mrefu
DALILI ZA UGONJWA WA BAWASIRI
- Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa. Huu muasho unakuja kwa kujirudia mara kwa mara baada ya muda furani.
- Kukatishwa kwa haja kubwa na kurudi ndani wakati wa kujisaidia. Kitendo hiki huongeza msuguano katika mishipa ya ndani ya tundu la haja kubwa.
- Kujitokeza kwa uvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa. Uvimbe huu unaanza kuota k**a upele na huambatana na miwasho na maumivu makali.
- Kujitokezea kwa kijinyama katika tundu la haja kubwa. Kinyama hiki kinaanzia ndani ya tundu la haja kubwa na kutokea nje ya Tundu la haja kubwa. Hatua hii huashiria tatizo limesha kuwa kubwa na una hili tatizo la bawasili kwa muda mrefu, na linaweza kusababisha vifo vya gafla kwa sababu mishipa inayosafirisha damu ndio inakwanguliwa na mwishowe kuathirika.
Chukua tahadhari mapema kabla hujaathirika sana au upoteze maisha; kwasababu hiki ni chanzo cha kupatwa na magonjwa mengine mengi ya kiafya.
- Kujisaidia kinyesi chenye damu na kunuka kwa harufu mbaya sana
- Kupumua na kushindwa kuzuia kinyesi wakati ukipumua(kujamba na kutoa haja kubwa)
MADHARA YA UGONJWA WA BAWASIRI
Upungufu wa damu mwilini
Kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa na kusababisha mishipa ya sehemu ya haja kubwa kukwanguliwa.
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata saratani ya utumbo (Cancer) kwasababu kile kinyama kinakaa k**a kidonda
Kutopata hamu ya tendo la ndoa kwa jinsia zote. Yaani Mwanamke na Mwanaume.
Kuathirika kisaikolojia na hupelekea kuptojiamini katika hadhara ya watu hasa pale miwasho inapoanza.
Kuvuja damu, maumivu ya mda mrefu na hupelekea kushindwa kukaa.
Maumivu ya mgongo ya mara kwa mara na kiuno.
Kwa msaada, ushauri na tiba wasiliana nami moja kwa moja
WhatsApp
https://wa.me/255716497275
Call and text
255689606285
Prepared Dr Chaula
🔰Ijali afya yako.